Mwenyekiti wa Bodi wa Stamico , Elexender Muganda akizungumza na waandishi habari juu shirika la Taifa la Madini (Stamico) kupata mtambo wa kisasa wa uchorongaji kwa kutumia upepo , jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi wa Utafiti na Uchorongaji wa Stamico, Alex Rutagwelela akitoa ufafanuzi juu ya mtambo wa kisasa wa uchorongaji miamba jijini Dar es Salaam, kushoto ni Meneja Masoko na Uhusiano, Koleta Njelekela.
Kaimu Mkurugenzi wa Utafiti na Uchorongaji, Alex Rutagwelela akiangalia mtambo wa uchorongaji wa miamba Bandarini , jijini Dar es Salaam.

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.

SHIRIKA la Taifa la Madini (Stamico) limepata mtambo wa uchorongaji kwa kutumia upepo (Air Rotary Drill Rig) wenye thamani dola za Kimarekani milioni 1.3 utakaotumika kupata taarifa za kijiolojia na mashapo kwa wachimbaji wadogo .

Kunufaika kwa wachimbaji wadogo kunatokana na stamico kupata mtambo wa kisasa wa uchorongaji miamba. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Bodi wa Stamico, Elexender Muganda amesema kuwa mtambo umetengenezwa nchini Canada ambapo  mtambo huo utasaidia wachimbaji wadogo kupata taarifa za kjiolojia na mashapo katika maeneo yao kwa gharama nafuu.

Amesema mtambo huo umetolewa na serikali kupitia Wizara ya Madini chiini ya ufadhili wa Benki ya Dunia chini ya mradi wa usimamizi endelevu wa rasilimali ya madini Tanzania (SMMRP).
Muganda amesema huo una uwezo wa kuchoronga miamba kwa kutumia upepo na kwa haraka zaidi kati ya kina mita 30 hadi 200 na kwa gharama ambazo mchimbaji mdogo anamudu na kuchana uchimbaji wa kubahatisha pamoja kuwezesha kupata mikopo katika taasisi za fedha.

Aidha amesema kuwa wachimbaji wadogo wanaohitaji huduma za uchorongaji kwa kutumia upepo wafike katika ofisi za Stamico ili kupata taarifa zaidi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...