Usajili Vitambulisho vya Taifa katika mkoa wa Mwanza na wilaya zake umepamba moto, ambapo wananchi kutoka Wilaya za Kwimba, Ukerewe, Ilemela, Misungwi na Sengerema wamejitokeza kwa wingi kusajili. Kwa wananchi wa Wilaya Nyamagana, taratibu za kuanza kwa Usajili zinaendelea ambapo wataanza usajili rasmi wiki hii. 
Katika kufanikisha zoezi hilo Mkuu wa Mkoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri na Manispaa pamoja na Watendaji wa mitaa/Vijiji wamejizatiti kwa dhati kuhakikisha zoezi hili linafanyika na kukamilika kwa wakati uliopangwa. Aidha; Wamewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kusajiliwa kutokana na manufaa mapana ya zoezi hilo kwa mwananchi mmoja mmoja na kwa Taifa kwa ujumla.
Zoezi la Usajili wa Vitambulisho vya Taifa kwa wananchi wa Wilayani ya Ukerewe likiendelea, pichani ni baadhi ya wananchi wa kata ya Kakelege wakisubiri zoezi la kupigwa picha na kuchukuliwa alama za Kibaiolojia.
Afisa Usajili Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa Ndg. Zabron Rusohoka akiwaelekeza baadhi ya wananchi taratibu wanazopaswa kuzifuata wakati wa ujazaji fomu za maombi ya Wilayani Ukerewe.
Umati wa wananchi wa Kata ya Ukerewe kijiji cha Nakatunguru wakisubiri huduma ya Usajili wakati zoezi la Usajili likiendelea Wilayani humo. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...