Meneja wa chapa wa Vodacom Tanzania,Yvonne Maruma(kushoto)akimkabidhi
hundi yenye thamani ya Tsh.Milioni 1/=mchezaji bora wa mwezi
septemba,Shafik Batambuze wa timu ya Singida United inayoshiriki ligi
kuu ya Vodacom Tanzania bara,Katikati ni Afisa Udhamini na Matukio wa
kampuni hiyo,Ibrahim Kaude.
Mchezaji bora wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara mwezi Septemba wa Singida United, Shafik Batambuze akiwa ameshikilia hundi yake yenye thamani ya shilingi Milioni 1/- baada ya kukabidhiwa rasmi na wadhamini wakuu wa ligi kwa kuibuka mchezaji bora wa mwezi huo.
KAMPUNI ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania PLC,Ambao ndiyo wadhamini wa ligi kuu Tanzania bara,Jana wamemkabidhi mchezaji bora wa ligi kwa mwezi septemba wa Singida United,Shafik Batambuze hundi yenye thamani ya shilingi Milioni 1/- kwa kuibuka mchezaji bora wa mwezi huo.
Akimkabidhi hundi hiyo Meneja wa Chapa wa kampuni hiyo,Yvonne Maruma alisema kwa mjibu wa taratibu unaofanywa na kamati ya Tuzo ya VPL iliyopo chini ya shirikisho la mpira wa miguu nchini Vodacom ikiwa kama mdhamini mkuu haina budi kutekeleza matakwa yote yale yaliyopo katika mkataba na kuweza kutoa kitita cha shilingi milioni 1/-kwa mchezaji bora wa kila mwezi ikiwa na lengo la kuwapa motisha wachezaji wote wanaoshiriki ligi kikuu,Alisema Maruma.
“Kwa mjibu wa wa kikao cha kamati ya Tuzo ya VPL imeonesha kwamba mchezaji huyu alitoa mchango mkubwa kwa singida united kupata pointi 10 katika michezo mine,ambayo timu yake ilicheza kwa mwezi huo,matokeo ambayo yaliiwezesha Singida United kutoka nafasi ya 10 katika msimamo na kupanda hadi nafasi ya nne kwa mwezi huo wa Septemba,Singida United ndiyo timu iliyokusanya alama nyingi kwa mwezi huo ukilinganisha na timu nyingine 15 zinazoshiriki ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara”,Alisema Maruma
Kwa upande wake Sharif Batambuze,aliishukuru kamati ya tuzo ya ligi na wadhamini wakuu kwa kumpatia fedha hizo na kusema atazitumia vizuri ili iwe kumbukumbu nzuri katika maisha yake kwa msimu wa 2017 Batambuze.
KAMPUNI ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania PLC,Ambao ndiyo wadhamini wa ligi kuu Tanzania bara,Jana wamemkabidhi mchezaji bora wa ligi kwa mwezi septemba wa Singida United,Shafik Batambuze hundi yenye thamani ya shilingi Milioni 1/- kwa kuibuka mchezaji bora wa mwezi huo.
Akimkabidhi hundi hiyo Meneja wa Chapa wa kampuni hiyo,Yvonne Maruma alisema kwa mjibu wa taratibu unaofanywa na kamati ya Tuzo ya VPL iliyopo chini ya shirikisho la mpira wa miguu nchini Vodacom ikiwa kama mdhamini mkuu haina budi kutekeleza matakwa yote yale yaliyopo katika mkataba na kuweza kutoa kitita cha shilingi milioni 1/-kwa mchezaji bora wa kila mwezi ikiwa na lengo la kuwapa motisha wachezaji wote wanaoshiriki ligi kikuu,Alisema Maruma.
“Kwa mjibu wa wa kikao cha kamati ya Tuzo ya VPL imeonesha kwamba mchezaji huyu alitoa mchango mkubwa kwa singida united kupata pointi 10 katika michezo mine,ambayo timu yake ilicheza kwa mwezi huo,matokeo ambayo yaliiwezesha Singida United kutoka nafasi ya 10 katika msimamo na kupanda hadi nafasi ya nne kwa mwezi huo wa Septemba,Singida United ndiyo timu iliyokusanya alama nyingi kwa mwezi huo ukilinganisha na timu nyingine 15 zinazoshiriki ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara”,Alisema Maruma
Kwa upande wake Sharif Batambuze,aliishukuru kamati ya tuzo ya ligi na wadhamini wakuu kwa kumpatia fedha hizo na kusema atazitumia vizuri ili iwe kumbukumbu nzuri katika maisha yake kwa msimu wa 2017 Batambuze.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...