Kutokana na mvua zilizonyesha usiku wa kuamkia leo katika baadhi ya maeneo ya jiji la Dar es salaam, kumepelekea Barabara ya Mbezi kwa Msuguli kuelekea Bwaloni-Masaki mpaka Malamba Mawili kupitika kwa shida kutokana na utelezi wa tope. hali iliyoleta adha kubwa kwa watumiaji wa njia hiyo, kwani si gari wala pikipiki zinazoweza kupita kwa sasa.
Mmoja wa waendesha bodaboda akijaribu kumuelekeza dereva wa gari iliyokuwa mbele yake kutembea katika sehemu yenye unafuu kidogo wa kupitika.
Ni nadra sana kuona waendesha bodaboda wakiwa kwenye msururu namna hii, lakini kutokana na hali ya barabara hiyo imewalazimu na wao kufuata utaratibu na kukubali matokeo.
Baadhi ya watembea kwa miguu.
Moja ya gari ikiwa imekwama katika barabara hiyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...