Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge amezitaka Halmashauri za Wilaya, Mji na Manispaa Mkoani Dodoma kuhakikisha zinatenga asilimia kumi (10%) ya makusanyo yao ya ndani kwa ajili ya vijana, wanawake na Walemavu kuanzisha miradi ya viwanda vidogo na vya kati.

Lengo ni kuitikia kampeni ya Serikali inayoitaka Mikoa kuanzisha viwanda kama ilivyozinduliwa hivi karibuni na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mheshimiwa Seleman Jafo.

Akizungumzia hilo, ameonya tabia ya baadhi ya Halmashauri kutotoa asilimia kumi (10%) ya makusanyo yake ya ndani au kutoa kiasi kidogo kwa ajili ya vijana, wanawake na walemavu na kuwa utaratibu unaotumika sasa wa Halmashauri kukopesha fedha hizo wakati mwingine sio muafaka sana badala yake Halmashauri zitumie fedha hizo kuwafungulia vijana, wanawake na walemavu viwanda vidogovidogo na kuwakabidhi waendeleze uzalishaji na kuviendesha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...