Na Bashir Yakub.

Umenunua kiwanja au nyumba. Aliyekuuzia amekuhahakikishia kuwa kiwanja/nyumba hiyo iko salama na haina mgogoro wowote. Mbali na mgogoro pia amekuhakikishia kuwa kiwanja/nyumba hiyo hajaiweka rehani popote ili kuchukua mkopo. 

Amekuhakikishia kuwa mpaka wakati unanunua kiwanja/nyumba hiyo, ni kuwa iko salama na haijashikiliwa na benki au taasisi yoyote ya fedha kwa ajili ya mkopo.

Au pengine hukuuliza kabisa kama kuna deni lolote, umejikuta tu umenunua bila kuuliza swali kama hilo. Baadae sasa ndio unagundua kuwa kiwanja/nyumba uliyonunua kuna taasisi moja ya fedha ambapo aliyekuuuzia alichukua mkopo na kuiweka dhamana/rehani na bado hajamalizia mkopo huo. 

Taasisi hiyo inakuonesha nyaraka halali za kushikilia kiwanja/nyumba hiyo kama dhamana muda mrefu hata kabla wewe hujanunua. Na kwa bahati mbaya aliyekuuzia hujui tena alipo au bahati nzuri unajua alipo.

Lakini hata ukijua alipo, tayari umeishanunua na hela ulishampa na kila kitu kilikwishakamilika. Nini kinakusaidia kukutoa katika hali hii ambayo sasa unaelekea kuingia katika mgogoro mkubwa wenye sura ya hasara. 

Sheria namba 4 ya 199, Sheria ya ardhi itatupatia majibu ya jambo hili.

1.UNUNUZI WA AINA HIYO UNAVYOTAMBULIKA KISHERIA.

Ununuzi wa aina hiyo unatambulika kama aina ya ununuzi ambao unaingilia haki ya mtoa mkopo. Kifungu cha 69(1) cha sheria hiyo kinauita ununuzi huo kama ununuzi unaolenga kupora/kuharibu(defeat) haki ya mtoa mkopo. 
Mtoa mkopo hapa ni benki au taasisi nyingine ya fedha iliyotoa mkopo. 
Kwahiyo kujikuta umenunua eneo lenye mazingira ya namna hiyo hadhi yake ni kama ilivyoelezwa hapa juu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...