Na Rhoda Ezekiel Kigoama.

WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina, ameagiza Viongozi wote waliohusika kupokea mifugo Pamoja na wafugaji kutoka Nje ya nchi kuchukuliwa hatua za kisheria  baada ya uchunguzi kukamilika, ikiwa ni pamoja na kuwafukuza kazi baadhi ya watendaji watakao gundulika walijihusisha na suala hilo ambalo ni kinyume na maadili ya utumishi wa umma.

Hata hivyo Waziri huyo alisema kuwa zoezi la ukamataji wa Ng'ombe zilizo ingizwa nchini kinyume na utaratibu, jumla yake ni Ng'ombe 1580 ambao wanashikiliwa, na akaagiza kuwa Ng'ombe hizo zitaifishwe na kupigwa mnada baada ya uchunguzi kukamilika na kuhakikisha ifikapo Novemba 10 mwaka huu Mifugo yote iliyoingia kinyume na utaratibu iwe zimeondolewa kabisa.

Akizungumza juzi mara baada ya ukamataji wa Ng'ombe Wilayani kasulu Mkoani Kigoma, Mpina alisema viongozi walioshiriki kupokea mifugo kutoka Nje ya Nchi,  viongozi wa aina hiyo washughulikiwe kisheria, anaejihusisha na suala la kuingiza mifugo hiyo kama itathibitika hawawezi kuwa na viongozi wanowahifadhi wahalifu wanaoingia Nchini bila kujali masilahi ya nchi na Ng'ombe zimekuwa kero kwa kuharibu Mashamba ya wananchi na Katika maeneo mengi ya hifadhi yameharibiwa sana na Wavamizi hao.

Alisema mpaka sasa mifugo yote iliyokamatwa kwa Nchi nzima ni mifugo 9500, na mifugo hiyo itatakiwa kutaifishwa baada ya Wanasheria na maafisa uhamiaji kuthibitisha kuwa iliingia kinyume cha sheria ili kuifanyia mnada na kukomesha wavamizi wote wanaoingia kinyume na utaratibu na kuharibu misitu na kuwa kichocheo cha migogoro ya wakulima na Wafugaji katika Maeneo ya vijijini.
 WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina akizungumza jambo na
kaimu Mkuu wa Wilaya ya kasulu ambae pia ni Mkuu wa wilaya ya Buhigwe, kanali Marco Gaguti mara baada ya ukamataji wa Ng'ombe Wilayani kasulu Mkoani Kigoma
WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina akizungumza jambo na
kaimu Mkuu wa Wilaya ya kasulu ambae pia ni Mkuu wa wilaya ya Buhigwe wakitafakari jambo kwa pamoja.


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...