Diwani wa Chadema wa Kata Donyomurwak,
Wilaya ya Siha Mkoa wa Kilimanjaro, Ndg. Lwite Ndossi almaarufu “Nsonuu”, leo
tarehe 19 Disemba 2017 amejivua uanachama wa Chadema, na amejiuzuru Udiwani wa
Kata hiyo na ametangaza kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Ndugu Ndossi ameeleza sababu za
kujiunga kwake na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwa ni kujiunga na watu wanaofanya
siasa za kufanya kazi za maendeleo na si kulumbana na maneno matupu.
Imetolewa na,
IDARA YA ITIKADI NA UENEZI
CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...