Mwenyekiti wa Baraza la Watoto wa Wilaya Temeke Mkoa wa Dar es Salaam Yusra Mohamed pamoja na Katibu wa Baraza la Watoto Mkoa wa Arusha Raphael Denis wamechaguliwa na wajumbe wa Baraza la Watoto Taifa kuiwakilisha Tanzania katika Mkutano wa kimataifa wa kuzuia ukatili dhidi ya watoto utakaofanyika Nchini Swedeni Februari 2018.

Watotao hao wamechaguliwa baada ya kupita katika Mchujo mkali uliowakutanisha wagombea kutoka Mikoa ya Bara na Visiwani na wataiwakilisha Tanzania katika Mkutano huo ambao Tanzania ni moja ya Nchi chache Barani Afrika kupewa kipaumbele cha ushiriki kufuatia hatua kubwa iliyofikia katika juhudi zake za kupambana na ukatili dhidi ya watoto.

Kwasasa Tanzania inatekeleza mkakati wake wa miaka mitano wa kutokomeza kabisa ukatili dhidi ya wanawaka na watoto unaotekelezwa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto pamoja na wadau mbalimbali wa wanaopambanakuhakikisha Tanzania inakomesha kabisa vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto.
Mwenyekiti wa Baraza la Watoto wa Wilaya Temeke Mkoa wa Dar es Salaam Yusra Mohamed kulia pamoja na Katibu wa Baraza la Watoto Mkoa wa Arusha Raphael Denis kushoto mara baada ya kuchaguliwa na wajumbe wa Baraza la Watoto Taifa kuiwakilisha Tanzania katika Mkutano wa kimataifa wa kuzuia ukatili dhidi ya watoto utakaofanyika Nchini Swedeni Februari 2018.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...