Mkuu wa Wilaya ya Temeke
Felix Lyaniva azindua jukwaa la wanawake Kiwilaya katika viwanja vya Mwembe Yanga. Katika uzinduzi huo DC Lyaniva asisitiza wanawake kupendana,kuwa na umoja ili kujiletea maendeleo ya kweli,hata kufikia uchumi wa kati.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke Felix Lyaniva akiwa akishuhudia wakina mama wakipiga na mabanho yenye ujumbe tofauti katika uzinduzi wa jukwaa la wanawake Wilaya ya Temeke.

Wanawake hao ambao wamejitokeza kwa wingi katika uzinduzi huo, huku sherehe hizo zikipambwa na shamrashamra za maandamano ya vikundi mbalimbali vya wanawake wajasiriamali.
Pia wanawake wajasiriamali walionesha kazi za mikono na ubunifu ufanywao na vikundi vyao.
Katika uzinduzi huo ulifanyika uchaguzi wa mwenyekiti wa jukwaa la wanawake Kiwilaya ambapo Johari Maulid Mkonde alichaguliwa rasmi kuwa mwenyekiti wa jukwaa la wanawake wilayani Temeke.
Hata hivyo wanawake wa Temeke wamepewa fursa kushiriki uchumi wa viwanda ili waweze kufika malengo ya maendeleo endelevu ya 50/50 ya dunia kufikia mwaka 2030.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...