Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. George Masaju akiwa katika picha ya pamoja na Baadhi ya Mawakili wapya muda mfupi baada ya kukubaliwa na kusajiliwa. Pichani pia yupo Jaji Mkuu Mhe. Profesa Ibrahim Hamis Juma na Majaji.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. George Masaju akizungumza na Mawakili wapya waliokubaliwa na kusajiliwa ambapo katika nasaha zake kwao alisema atawashangaa sana mawakili hao kama watakuwa wazururaji mitaani wakisubiri ajira badala ya kuitumia taaluma yao kujiajiri wenyewe. Hafla ya kuwakubali na kuwasajili Mawakili hao imefanyika leo katika Viwanja vya Karimjee
Sehemu ya Mawakili wapya 296 ambao wamekubaliwa na kusajiliwa kuwa Mawakili wakimsikiliza Mwanasheria Mkuu wa Serikali na wakashindwa kujizuia kushangilia pale alipowapa changamoto ya kuzitumia fursa zilizopo kujiajiri wenyewe kwa kwenda Mikoani na Wilayani badala ya kung'ang'ania kukaa Dar es Salaam.
Mhe. George Masaju, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, akibadilishana mawazo na Mkurugezi wa Mashtaka ( DPP) Bw. Biswalo Maganga muda mfupi kabla ya hafla ya kuwakubali na kuwasajili Mawakili 296 wapya katika hafla iliyofanyika leo Ijumaa katika Viwanja vya Karimjee.
Na Mwandhishi maalum.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. George Masaju, amewataka
Mawakili wapya kuzitumia fursa nilizopo kujiajiri badala ya kusubiri
kuajiriwa.
Ametoa ushauri huo leo ( Ijumaa) wakati wa hafla ya kuwakubali na
kuwasajili Mawakili wapya 296. Hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya
Karimjee.
“Niwashauri Mawakili wapya, anzeni kufanya kazi. Itashangaza
sana, na nitawashangaa sana kama na nyie mtakaa mtaani mkisubiri
kuajiriwa badala ya kutumia taaluma na ujuzi milioupata kujiajiri wenyewe”
Mhe. Masaju amewataka mawakili hao wa kike na wakiume, na
ambao wengi wao ni vijana wa umri wa kati ya miaka 30 na 40, kwenda
mikoani na wilayani ambako amesema, kuna fursa nyingi za kujiajiri na
pia kuna wateja wengi wenyeuhitaji mkubwa wa kupata huduma ya za
kisheria.
“Nendeni mikoani na wilayani badala ya kung’ang’nia kukaa hapa
Dar es Salaam na katika majiji na miji mingine mikubwa hapa nchini. Huko
mtapata soko kubwa la wananchi wanaohitaji huduma zenu na wenye
uwezo wa kulipia huduma hizo kutokana na shughuli zao mbalimbali
zikiwamo za kilimo” amesisitiza Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Kwa wale Mawakili ambao wataajiriwa na Ofisi ya Mwanasheria
Mkuu wa Serikali na katika Utumishi wa Umma. Mwanasheria Mkuu
amesema watatakiwa kuzingatia ipasavyo Maadili ya Msingi
yanayosimamia utekelezaji wa majukumu ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu
wa Serikali.
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...