Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo hapo jana alifanya ziara kwenye machimbo ya Jasi (Gypsum) ya Mkoani Singida na kuzungumza na Wafanyabiashara na Wachimbaji wa Madini hayo ambapo aliwahakikishia ushirikiano wa dhati wa kufikia malengo waliyojiwekea.
Alitembelea maeneo ya machimbo ya Madini ya Jasi na Viwanda vidogo vya uongezaji thamani ya madini hayo ikiwemo viwanda vya kusaga madini ya Jasi ambayo unga wake unasafirishwa nje ya Mkoa huo, viwanda vya kutengeneza chaki vilivyopo Itigi na kiwanda cha utengenezaji wa mapambo ya majumbani kilichopo Singida Mjini.
Naibu Waziri Nyongo yupo Mkoani Singida kwenye ziara ya siku Tatu ya kutembelea maeneo mbalimbali ya uchimbaji wa madini Mkoani humo ili kujionea shughuli zinazofanywa kwenye maeneo hayo na kuzungumza na wachimbaji wa madini ili kubaini changamoto zinazowakabili kwa lengo la kutafuta ufumbuzi wake. 
Kwa mujibu wa wachimbaji wa madini hayo, Madini ya Jasi hutumika kwa matumizi mbalimbali ikiwemo kutengenezea chaki, hospitalini kwa watu waliovunjika na kutengeneza viungo bandia, kutumika kutengenezea saruji, urembo majumbani, hutumika kama insulation kwenye majengo makubwa kwa kuwa Jasi huzuia moto, kutengenezea midoli na masanamu, kutengeneza meno bandia na pia hutumika kama mbolea
 Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (kulia) akishuhudia upakiaji wa Madini ya Jasi katika kijiji cha Kihanju, Itigi yanayosafirishwa kuelekea kwenye Kiwanda cha Saruji cha Mbeya Cement ikiwa ni moja ya malighafi ya kutengenezea Saruji.
 Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (kushoto) akiwasikiliza wachimbaji na wafanyakazi wa machimbo ya Jasi, yaliyopo katika Kijiji cha Kihanju, Itigi, Mkoani Singida alipofanya ziara kwenye machimbo hayo.
 Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (wa pili kushoto) akitazama hatua ya uchomaji wa Madini ya Jasi kwenye kiwanda cha kampuni ya mzawa cha RSR kilichopo katika Kijiji cha Sanjaranda, Itigi kabla ya kusagwa kuwa unga na baadaye kusafirishwa hadi Dar es Salaam kwa ajili ya kuuzwa na mwingine kutumika katika Kiwanda cha kutengenezea mapambo ya Majumbani, katika kiwanda kilichopo Singida mjini.
 Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo akitazama Chaki zinazozalishwa na Kiwanda cha Dobercolor kilichopo katika Kijiji cha Majengo, Itigi ambazo huuzwa ndani na nje ya Mkoa huo huku lengo likiwa ni kuuza nje ya Tanzania.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...