Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa wenyeviti wa bodi sita za taasisi za Serikali baada ya wenyeviti waliokuwepo kumaliza muda wao.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo tarehe 06 Desemba, 2017 na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi, Kwanza Mhe. Rais Magufuli amemteua Bi. Monica Ngenzi Mbega kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mazao Mchanganyiko kuanzia tarehe 30 Novemba, 2017.

Pili, Mhe. Rais Magufuli amemteua Prof. Egid Beatus Mubofu kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya Mbolea Tanzania (TFC) kuanzia tarehe 01 Desemba, 2017.

Tatu, Mhe. Rais Magufuli amemteua Prof. Abiud Kaswamila kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro kuanzia tarehe 01 Desemba, 2017.

Nne, Mhe. Rais Magufuli amemteua Prof. Esther Hellen Jason kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kuanzia tarehe 01 Desemba, 2017.

Tano, Mhe. Rais Magufuli amemteua Dkt. Kenneth Mdadila kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya taasisi ya kifedha ya Self Microfinance Fund Limited kuanzia tarehe 01 Desemba, 2017. 

Sita, Mhe. Rais Magufuli amemteua Dkt. Titus Mlengeya Dismas Kamani kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania kuanzia tarehe 06 Desemba, 2017.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
06 Desemba, 2017

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...