TAASISI ya kuzuia na kupambana na rushwa mkoani Tanga(Takukuru) imewafikisha mahakamani wahasibu wawili wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Tanga Josiah Mwaipela na Julius Idana kwa mashtaka matatu ya rushwa. 

Washtakiwa hao wamefikishwa mahakamani kwa makosa ya
uchepushaji,ubadhirifu na matumizi mabaya ya madaraka kuhusiana na shilingi milioni 276,095,106.9 za mishahara ya watumishi ambaowalikoma utumishi wao wa umma kati ya Machi 3 ,2012 na Novemba 2013. 

Hayo yalisemwa na Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Tanga, Christopher Mariba wakati akitoa taarifa yake kwa vyombo vya habari ambapo alisema washtakiwa hao walifikishwa mahakamani jana Desemba 18 mwaka huu. Alisema washtakiwa hao walifikishwa mbele ya hakimu mfawidhi wa mahakama ya hakimu mkazi Tanga,Crisencia Kisongo na kusomewa mashtaka na waendesha mashitaka wa Takukuru Noel Gabba na Neema Kazoka. 

Alisema washtakiwa hao wanadaiwa kutenda makosa ya uchepushaji,ubadhirifu na matumizi mabaya ya madaraka kuhusiana na shilingi milioni 276,095,106.9 za mishahara ya watumishi ambao walikoma utumishi wao wa umma kati ya Machi 3 ,2012 na Novemba 2013. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...