UCHAGUZI WA MARUDIO KATIKA KATA NNE ZA MANZASE (CHAMWINO), KIMAGAI (MPWAPWA), ISAMILO (MWANZA) NA MADANGA (PANGANI)
PAMOJA NA MAJIMBO YA SIHA (KILIMANJARO) NA KINONDONI (DAR ES SALAAM)
PAMOJA NA MAJIMBO YA SIHA (KILIMANJARO) NA KINONDONI (DAR ES SALAAM)
____________________
Chama
Cha Mapinduzi (CCM) kinapenda kuujulisha umma wa wanachama wa CCM kuwa
kimepokea taarifa kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuwa kutakuwa
na uchaguzi wa marudio katika Kata na Majimbo yaliyotajwa hapo juu.
Wanachama
wote wenye sifa za msingi kwa mujibu wa Katiba ya Nchi na waliokidhi
vigezo vya uanachama kwa mujibu wa Katiba ya CCM na Kanuni zake
wanahamasishwa kujitokeza ili kuomba ridhaa ya Chama kupeperusha bendera
ya CCM katika Uchaguzi huu wa marudio isipokuwa na kama
inakavyoelekezwa na taarifa hii.
Aidha Chama kimejipanga kufanya
kampeni za kistaarabu na kisayansi, na zilizosheheni siasa za hoja na
zinazojikita katika kushughulika na shida za wananchi na hatimaye
kushinda kwa kishindo katika uchaguzi huu wa marudio. Kwa maana hii,
msisitizo unawekwa kwa wanao omba ridhaa ya kugombea, vikao vya uchujaji
na mapendekezo, na vikao vya uteuzi kuzingatia Misingi ya Maadili na
kuhakikisha waombaji wana akisi uaminifu, uadilifu, uchapakazi, heshima
kwa watu, ukubalifu wa imani, siasa na itikadi ya CCM, nidhamu kwa chama
na wawe watu ambao umma wa wananchi unawatambua kwa nafasi yao katika
jamii inapokuja katika kushughulika na shida zao.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...