Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe akizungumza na Wadau wa Sanaa (hawapo pichani) kuhusu nini kifanyike kwa mavazi ya wasanii sababu ya kuwepo kwa wasanii wengi wanaovaa mavazi yanayokiuka na maadili ya kitanzania katika kikao chake na wadau mbalimbali wa Sekta ya Saana nchini kilichofanyika leo jijini Dar es Salaam, kutoka kushoto ni Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Tanzania Bibi. Joyce Fissoo na Katibu Mtendaji Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Godfrey Mngereza (kulia).
Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Tanzania Bibi. Joyce Fissoo (kushoto) akitoa ufafanuzi kwa wadau wa Sanaa (hawapo pichani) kuhusu Sheria ya Filamu nchini inayosema lolote linalotoka nje ya nchi,Michezo ya kuigiza na kazi yoyote ya kisanii inayotengenezwa hapa nchini kusawili hali halisi ya kitanganyika, katika kikao kilichofanyika leo jijini Dar es Salaam na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe (Kulia) kujadili nini kifanyike kutokana na kuwepo na mmomonyoko wa maadili katika mavazi kwa wasanii.

Katibu wa Shirikisho la Muziki Tanzania ambaye ni Mwanamuziki Mkongwe John Kitime akisisitiza kuwepo kwa Kampeni ya Kitaifa kusisitiza suala la mavazi yenye kulinda utamaduni wetu katika kikao kilichofanyika leo jijini Dar es Salaam na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe (hayupo pichani) kujadili suala la mavazi kwa wasanii na taifa kwa ujumla.
Mwanamuziki wa Bongo Fleva nchini Stara Thomas akichangia mada ya kuhusu mavazi ya heshima kwa wasanii nchini katika kikao kilichofanyika leo jijini Dar es Salaam na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe (hayupo pichani).Na Anitha Jonas – WHUSM

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...