Na Said Mwishehe, Globu ya jamii
MKURUGENZI Mtendaji wa Elimu Solutions (T) Limited Neithan Suedy amesema ni vema Watanzania hasa wanafunzi nchini kuwa makini na matapeli wanaochukua fedha za wanafunzi kwa kigezo cha kuwatafutia vyuo vikuu nje ya nchi.
Amesema wanaungana na Balozi wa Tanzania nchini China kuonya tabia ya baadhi ya mawakala kuchukua fedha za wanafunzi na kisha kushindwa kuwapeleka Kwenye vyuo ambavyo wanaahidi kuwapeleka au kuwapeleka na kusababisha wanafunzi wakifika huko kukosa malazi na makazi.
Akizungumza Dar es Salaam leo, Sissy amesema wenye tabia hiyo wanasababisha matatizo kwa wanafunzi na wanaokwenda huko nchini China wanasababisha mzigo kwa vyuo husika.
"Wanafunzi wanatapeliwa sana na watu hao ambao wanajiita mawakala wa kutafutia ufadhili wanafunzi wa Tanzania kwa vyuo vikuu vya nchini China.
"Ni vema Serikali yetu ikasaidia kudhibiti utapeli huu ambao unafanywa kwa wanafunzi wanaotaka kusoma nchini China, "amesema Suedy.
Akizungumzia kwa upande wao amesema wamekuwa wakitafuta ufadhili kwa wanafunzi wanaohitaji kujiendeleza kielimu nchini China na wanachozingatia wao ni kufuata taratibu ambazo zinatambulika kisheria.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Taasisi ya Elimu Solutions Tanzania Ltd, Neithan Swedy
akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kuanza kwa zoezi la kutuma
maombi ya udahili wa masomo kwa wanafunzi wa nje ya nchi (China, Japan
na Korea Kusini) pamoja na taratibu mbalimbali zinazopaswa kuzingatiwa
na waombaji. Kushoto ni Afisa Tawala wa Taasisi hiyo, Irene Kigwangwa leo Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Taasisi ya Elimu Solutions Ltd, Neithan Swedy akionyesha
kwa waandishi wa habari nyaraka ya Namba ya Utambulisho Mlipa Kodi (TIN)
inayotolewa na Mamlaka ya Mapato Tanzania ( TRA) na kupaswa kuwa nayo
kila kampuni ya uwakala wa utafutaji wa nafasi za masomo katika vyuo vya
nchi za nje ya Tanzania. Wengine ni Afisa Tawala Irene Kigwanga na
Meneja mwendeshaji wa Elimu Solutions, Ibrahim Swedy leo Jijini Dar es
Salaam.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...