Nteghenjwa Hosseah, Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo amesema mahitaji ya wataalam wa Maji kwa sasa katika Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Nchini ni kati ya elf nne – hadi elfu saba.

Jafo ameyasema hayo wakati alipokuwa mgeni rasmi katika Mahafali ya Tisa ya Chuo cha Mji yaliyofanyika Tar 11/01/2018 katika chuo hicho kilichopo Jijini Dar es salaam.

“Taalum hii ni muhimu sana katika ustawi na Afya ya wananchi wetu kote Nchini, uhakika wa kupata maji salama bado ni changamoto kubwa kutokana kutokuwa na miundombinu ya Uhakika na zaidi ni wataalamu wachache waliopo katika Mamlaka za Serikali za Mitaa” Alisema Jafo.

Aliongeza kuwa Nipongeze chuo hiki cha maji kwa kutoa Shahada kwa mara ya kwanza katika Historia ya Chuo hiki, hapo awali hapakuwa na Ngazi ya Shahada hivyo wataalamu wengi waliishia ngazi ya Stashahada ambapo mara nyingine ilihitajika Utaalamu zaidi kutokana na changamoto za kiutendaji katika maeneo mbali.

“Kwa sasa mmejibu changamoto hii katika Sekta ya Maji kwa kufanikisha kutoa wahitimu wa Ngazi ya Shahada haya ni mafanikio kwa Chuo, kwa Wahitimu na Taifa kwa Ujumla nawapongeza sana na nawakaribishe katika Kulitumikia Taifa hili kwa sababu ujuzi mlioupata unahitajika sana” Alisema Jafo.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe Selemani Jafo(Katikati) akiwasili kwenye Chuo cha Maji tayari kwa kutunuku Shahada na Stashahada katika mahafali ya Tisa ya Chuo hicho.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe Selemani Jafo akizungumza na wahitimu wa Chuo cha Maji, Wakufunzi na wageni waalikwa(hawapo pichani) wakati wa Mahafali ya Tisa ya Chuo hicho.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe Selemani Jafo akitoa Cheti kwa mwanafunzi wa kike aliyefanya vizuri Kitaaluma katika ngazi ya Astashahada.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe Selemani Jafo(Katikati aliyekaa) katika Picha ya Pamoja na wanafunzi waliohitimu Shaada ya Uhandisi na Rasilimali za Maji na Umwagiliaji katika Chuo cha Maji.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...