Kampuni ya Mawasiliano ya ZANTEL, leo imezindua kampeni yake kabambe inayoitwa 'JERO YAKO TU', promosheni ambayo imelenga kuwashukuru wateja kwa kuwapa zawadi mbalimbali mara wanapoongeza salio la kiasi cha shilingi 500 tu.

Kampeni hiyo ambayo imeanza rasmi siku ya leo, itadumu kwa muda wa miezi mitatu huku takribani washindi 235 wakitarajiwa kuibuka na zawadi kabambe kutoka Zantel.

Zawadi kubwa katika promosheni hii itakuwa ni pamoja na magari matatu aina ya Suzuki Carry kwa washindi watatu, ambazo zitakabidhiwa mwishoni mwa kampeni hii mwezi Machi.Zawadi za kila wiki ni pamoja na pikipiki 1, na baiskeli 4 huku zawadi za kila siku zikiwa ni simu aina ya smartphone 4G pamoja na fedha taslimu kiasi cha Sh. 50,000/= kila siku.

Kwa mujibu wa Zantel, Promosheni ya ‘JERO YAKO TU' ni mahususi kwa ajili ya kuwazawadia wateja na kuthamini uvumilivu wao wakati ambapo mtandao huo ulikuwa kwenye hatua za maboresho na hatimaye kuzindua mfumo wa 4G katika mikoa 22 nchini Tanzania.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo mjini Zanzibar, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Zantel, Sherrif El- Barbary alisema, "Sisi Zantel tunathamini mchango wa wateja wetu ambao wametuonyesha kwa miaka mingi, na wanastahili kupongezwa kwa kuendelea kuwa nasi hususani kutufanya kuendeliea kuwa mtandao wa simu unaoongoza Zanzibar pamoja na kuongoza kwenye utoaji wa huduma ya data nchini Tanzania.

Mkuu wa Zantel Zanzibar, Mohammed Khamis Mussa (Baucha) akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa Kampeni ya ‘JERO YAKO TU’ iliyozinduliwa na Zantel jana mjini Zanzibar. Kampeni hiyo kabambe ya miezi mitatu imelenga kuwashukuru wateja wa Zantel kwa kuwapa zawadi mbalimbali mara wanapoongeza salio la kiasi cha shilingi 500 tu. Katikati ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Zantel, Sherif El-Barbary na kushoto ni Mkurugenzi wa kitengo cha Biashara Zantel, Wane Ngambi.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Zantel, Sherif El Barbary akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa Kampeni ya ‘JERO YAKO TU’ iliyozinduliwa na Zantel jana mjini Zanzibar. Kampeni hiyo kabambe ya miezi mitatu imelenga kuwashukuru wateja wa Zantel kwa kuwapa zawadi mbalimbali mara wanapoongeza salio la kiasi cha shilingi 500 tu. Pamoja nae ni Mkurugenzi wa kitengo cha Biashara Zantel, Wane Ngambi (kushoto) na Mkuu wa Zantel Zanzibar, Mohammed Khamis Mussa (Baucha) (kulia).
Afisa Mtendaji Mkuu wa Zantel, Sherif El-Barbary akijaribu moja ya Pikipiki ambazo zitakazoshindaniwa kila wiki kwenye Kampeni ya ‘JERO YAKO TU’ iliyozinduliwa na Zantel jana mjini Zanzibar. Kampeni hiyo kabambe ya miezi mitatu imelenga kuwashukuru wateja wa Zantel kwa kuwapa zawadi mbalimbali mara wanapoongeza salio la kiasi cha shilingi 500 tu. Pamoja nae ni Mkuu wa Zantel, Zanzibar, Mohammed Khamis Mussa (Baucha). 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...