Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi
(CCM) Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein leo Februari 4, 2018 ameongoza
Kikao cha kawaida cha siku moja cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya
Taifa Zanzibar.
Hiki ni
Kikao cha kwanza tangu Wajumbe wa Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya
Taifa (NEC) walipochaguliwa kupitia Mikutano Mikuu ya Mikoa, Jumuiya na
Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi uliofanyika mwaka jana katika
Uchaguzi wa Chama.
MAKAMU Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akiwa katika ukumbi wa mkutano baada ya kuwasili na kupokelewa na Wajumbe wa Kamati Maalum ya CCM Zanzibar, kulia Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Makamu wa Rais wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi na kushoto Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk. Abdallah Juma Mabodi.(Picha na Ikulu)
MAKAMU Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akiongoza Kikao cha kwanza cha Kamati Maalum ya CCM kilichofanyika katika Ukumbi wa Afisi Kuu ya CCM kisiwandui Zanzibar, baada ya kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu wa CCM uliofanyika mwaka jana Dodoma.(Picha na Ikulu).
MAKAMU Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza wakati wa Mkutano wa Kamati Maalum ya CCM Zanzibar mkutano uliofanyika katika Ukumbi wa Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Zanzibar kushoto Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk. Abdallah Juma Mabodi.(Picha na Ikulu)
WAJUMBE wa Mkutano wa Kamati Maalum ya CCM Zanzibar wakiwa katika ukumbi wa mkutano wakimsikiliza Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein, akifungua mkutano huo wa kwanza wa Kamati Maalum ya CCM Zanzibar, uliofanyika katika ukumbi wa Afisi Kuu ya CCM kisiwandui Zanzibar.(Picha na Ikulu) .
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...