Na Agness Francis Globu Ya jamii

MCHEZO uliokuwa uchezwe na timu Lipuli dhidi ya Ndanda katika dimba la Samora mkoani Iringa Wasogezwa mbele kwa maandalizi zaidi. 

Bodi ya Ligi (TPLB), imefanya mabadiliko ya mchezo huo namba 153 kati ya timu hizo mbili uliokuwa uchezwe Ijumaa ya Machi 2 mwaka huu.

Taarifa iliyotolewa leo, imeeleza kuwa sababu za kusogezwa mbele mchezo huo ni kutaka kuipa nafasi na muda zaidi Ndanda FC kusafiri kutoka Mtwara baada ya kumaliza mchezo wao wakiwa wenyeji dhidi ya Mabingwa watetezi Ligi Kuu Tanzania Bara Yanga.

Ambapo sasa umepangwa kuchezwa Jumatano ya Februari 28 mwaka huu kwenye Uwanja wa Nangwana Sijaona. Bodi ya Ligi (TPLB) imeamua mchezo huo wa Lipuli na Ndanda sasa umesogezwa mpaka siku ya Jumapili.Mchezo utachezwa kwenye Uwanja ule ule wa Samora mkoani Iringa. 

Ambapo mzunguko uliopita Lipuli alilazwa chali kwa bao 2-1 na Ndanda wakiwa ugenini katika Dimba la Nangwanda Sijaona Mkoani Mtwara. "Kupelekea mbele kwa mchezo huu sisi wachezaji umetupa muda zaidi wa kuendelea kufanya mazoezi,"amesema Beki namba 4 wa kikosi cha Lipuli, Martin Kazira.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...