*Kamanda Mambosasa agusia upelelezi kifo cha Akwilina
Na Leandra Gabriel, Globu ya jamii
KAMANDA wa Kanda Maalumu ya Dar es salaam Lazaro Mambosasa amesema hali ya usalama wa Jiji kuelekea Sikukuu ya Pasaka na wamejiimarisha kulinda usalama wa raia na Mali zao.
Mambosasa ameeleza kuwa Jeshi limejipanga kwa kuimarisha ulinzi na kuhakikisha wakazi wa jiji la Dar es salaam wanasherekea vizuri sikukuu hii.
Akizungumza leo jijini Dar es Salaam,Mambosasa ameeleza hakuna mtu yeyote atakayepata fursa ya kufanya tukio lolote la kiharifu kwani jeshi limejipanga kwa doria ya miguu, mbwa, pikipiki, farasi na magari yote yaliyopo katika kuhakikisha usalama wa raia wote na pia wameongeza nguvu ya ulinzi katika fukwe zote.
Kuhusu disko toto Mambosasa amesema kuwa hakuna kibali kilichoombwa hivyo hategemei kuona kumbi yoyote itakayokusanya watoto.
Kuhusu mauaji ya Akwilina Akwilini kamanda Mambosasa ameeleza upelelezi bado unaendelea na maelezo waliyoyapata bado wanayafanyia kazi uchunguzi ukikamilika watatoa maelezo.
Ametoa rai kwa waendesha vyombo vya moto kuwa makini na kuepukana na ulevi ili kulinda usalama wao na wananchi kwa ujumla.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...