Agness francis,Blogu ya jamii
LIGI ya Wanawake ya Serengeti Premium Lite inatarajia kuendelea wikiendi hii katika hatua ya nane bora huku wadhamini wa ligi hiyo wamekabidhi jezi rasmi kwa timi hizo kwa lengo la kuhakikisha wanafanya vizuri ndani ya nje.
Ratiba ya ligi hiyo inaonesha Aprili 21 zitachezwa mechi tatu na mchezo mmoja utachezwa Jumapili ya Aprili 22 mwaka huu .Pia siku hiyo hiyo katika Uwanja wa Karume Evergreen watakuwa nyumbani dhidi ya Alliance.
Wakati kwenye uwanja wa Mbweni JKT Quenns watakuwa wenyeji wa Simba Queens na Kigoma Sisters ikiwa katika dimba la Tanganyika wakiavaana na Baobab.
Pia mechi nyingine itakuwa kati ya Panama na Mlandizi Queens itakayochezwa Jumapili kwenye Uwanja wa Samora Iringa.
Akizungumza leo, Meneja Masoko wa Serengeti Anitha Msangi amesema wanaami kuidhamini Ligi Kuu ya Wanawake kwao inadhihirisha namna ambavyo wanachangia kuleta mafanikio katika mpira wa Wanawake nchini.
"Mashabiki wanayo nafasi kubwa katika maendeleo ya mpira wa Wanawake na niwaombe wajitokeze kuunga mkono Ligi Kuu ya Wanawake" amesema Msangi.
Hata hivyo ligi hiyo ilikuwa imesimama ili kupisha maandalazi ya timu ya Taifa ya Wanawake iliyokuwa na mchezo wa kufuzu fainali za Afrika kwa Wanawake dhidi ya Zambia.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...