Na Ripota Wetu, Globu ya jamii
KAMPUNI ya Puma Energy Tanzania imezindua kampeni maalumu ya mafunzo ya usalama barabarani kwa wanafunzi wa shule za msingi kwa lengo la kueneza elimu hiyo kuanzia ngazi ya chini.
Kampeni hiyo inayokwenda sambamba na mashindano ya uchoraji michoro ya usalama barabarani imezinduliwa Dar es Salaam jana na ofisa wa Polisi, ASP Mbuya Matibu, kutoka Makao Makuu ya Kikosi cha Usala,ma Barabarani.
AKizungumza kwenye uzinduzi wa kampeni hiyo, ASP Matibu, alisema Puma Energy Tanzania, wana mchango mkubwa katika utoaji elimu ya usalama barabarani, hivyo kuwataka wadau wengine kuiga mfano huo.
Pia, aliwataka madereva nchini wasiendeshe magari kwa kukariri sheria, bali wazitambue ili waweze kuzitumia vizuri kupunguza ajali.
Kwa upande wake Meneja Mkuu wa Puma Energy Tanzania, Philippe Corsaletti, alisema elimu ya usalama kwa wanafunzi ni muhimu, kwani inawapa uelewa wa matumizi ya barabara kwa usalama.
"Tunawaangalia sana watoto wa shule za msingi kwani wao wanakabiliwa na hatari nyingi za barabarani," alisema Corsaletti na kuongeza;
Meneja Mkuu wa Puma Tanzania, Philippe Corsaletti, Trafki kutoka makao makuu, ASP Mbuja Matibu wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali mara baada ya kumalizika kwa uzinduzi rasmi wa mafunzo hayo uliofanyika Makao makuu ya Kampuni ya Puma leo jijini Dar es Saaam.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KAMPUNI ya Puma Energy Tanzania imezindua kampeni maalumu ya mafunzo ya usalama barabarani kwa wanafunzi wa shule za msingi kwa lengo la kueneza elimu hiyo kuanzia ngazi ya chini.
Kampeni hiyo inayokwenda sambamba na mashindano ya uchoraji michoro ya usalama barabarani imezinduliwa Dar es Salaam jana na ofisa wa Polisi, ASP Mbuya Matibu, kutoka Makao Makuu ya Kikosi cha Usala,ma Barabarani.
AKizungumza kwenye uzinduzi wa kampeni hiyo, ASP Matibu, alisema Puma Energy Tanzania, wana mchango mkubwa katika utoaji elimu ya usalama barabarani, hivyo kuwataka wadau wengine kuiga mfano huo.
Pia, aliwataka madereva nchini wasiendeshe magari kwa kukariri sheria, bali wazitambue ili waweze kuzitumia vizuri kupunguza ajali.
Kwa upande wake Meneja Mkuu wa Puma Energy Tanzania, Philippe Corsaletti, alisema elimu ya usalama kwa wanafunzi ni muhimu, kwani inawapa uelewa wa matumizi ya barabara kwa usalama.
"Tunawaangalia sana watoto wa shule za msingi kwani wao wanakabiliwa na hatari nyingi za barabarani," alisema Corsaletti na kuongeza;
Meneja
Mkuu wa Puma Tanzania, Philippe Corsaletti akizungumza kuhusu
wanavoshiriki na kufanikisha mafunzo ya usalama barabarani kwa wanafunzi
wa shule za msingi hapa nchini ambapo kwa mwaka huu watatoa mafunzo kwa
shule 22 kwa mkoa wa Ruvuma na Dar es Salaam.
Trafki
kutoka makao makuu, ASP Mbuja Matibu akinzumgumza na waandishi wa
habari katika uzinduzi wa mafunzo ya Usalama barabarani kwa wanafunzi wa
shule za msingi mkoa ya Dar es Salaam.
Meneja
Miradi wa taasisi isiyo ya kiserikali ya Amend, Simon Kalolo
akizungumzia mafunzo ya usalama barabarani wanayoyatoa kwa wanafunzi wa
shule za msingi wakati wa uzinduzi rasmi wa mafunzo hayo uliofanyika
Makao makuu ya Kampuni ya Puma leo jijini Dar es Saaam.
Mshindi
wa mchoro 2017, mwanafunzi wa darasa la sita shule ya Msingi Mbande,
Nasri Mustafa akiwaonyesha mchoro wake wa usalama barabarani
alioshindawakati wa uzinduzi wa mafunzo ya Usalama barabarani kwa
wanafunzi wa shule za msingi jijini Dar es Salaam, kutoka kulia, Meneja
Miradi wa taasisi isiyo ya kiserikali ya Amend, Simon Kalolo, meneja
Mkuu wa Puma Tanzania, Philippe Corsaletti, trafki kutoka makao makuu,
ASP Mbuja Matibu na Sajent Hussein Ramadhani. Picha na Emmanuele
Massaka,Globu ya jamii
Meneja Mkuu wa Puma Tanzania, Philippe Corsaletti, Trafki kutoka makao makuu, ASP Mbuja Matibu wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali mara baada ya kumalizika kwa uzinduzi rasmi wa mafunzo hayo uliofanyika Makao makuu ya Kampuni ya Puma leo jijini Dar es Saaam.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...