NA JOHN MAPEPELE, MWANZA
WAKUU wa mikoa inayozunguka Ziwa Victoria wamekosoa vikali tabia ya
baadhi ya wanasiasa kuipaka matope dhamira njema ya Serikali ya
kupambana na uvuvi haramu ulioshamiri katika ziwa hilo na kutaka
viongozi wa aina hiyo kutangaza masilahi yao kwenye eneo la uvuvi kabla
ya kuwashambulia viongozi wanaosimamia zoezi hilo kwa misingi ya
kisheria.
Wakizungumza kwenye kikao cha tathmini ya operesheni sangara awamu ya
pili iliyowahusisha Wakuu wa Mikoa,Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala wa
Mikoa, Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya, Makamanda wa Polisi wa
mikoa na Wakuu wa Idara ya Usalama wa Taifa wa mikoa yote inayozunguka
Ziwa Victoria jijini Mwanza jana viongozi hao wametaka hatua zaidi
zichukuliwe ili kunusuru rasilimali hizo muhimu kwa maendeleo ya Taifa.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Antony Mtaka alielezea kuchukizwa na tabia
inayoanza kuota mizizi ya baadhi ya viongozi wa kisiasa kuipaka matope
dhamira nzuri ya Serikali ya kukabiliana na uvuvi haramu na kutaka
viongozi wa aina hiyo watangaze masilahi yao kabla ya kuanza
kuwashambulia viongozi wanaosimamia operesheni hiyo inayotekelezwa kwa
mujibu wa sheria .
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina akihutubia hadhara ya kikosi kazi cha watu 260 alichokiunda kwa ajili ya operesheni Sangara 2018 na Wakuu wa Mikoa mitano inayozunguka Ziwa vicktoria wakati wa mkutano wa kufanya tathimini ya Operesheni hiyo. Picha na John Mapepele
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina akihutubia hadhara ya kikosi kazi cha watu 260 alichokiunda kwa ajili ya operesheni Sangara 2018 na Wakuu wa Mikoa mitano inayozunguka Ziwa vicktoria wakati wa mkutano wa kufanya tathimini ya Operesheni hiyo. Picha na John Mapepele
Viongozi wakuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi waliokaa wakiwa katika picha ya pamoja na makamanda wakuu wa Operesheni Sangara 2018 (waliosimama) wakati wa mkutano wa kufanya tathimini ya Operesheni hiyo.
Viongozi wakuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi waliokaa wakiwa katika picha ya pamoja na sekretarieti ya Operesheni Sangara 2018 (waliosimama) wakati wa mkutano wa kufanya tathimini ya Operesheni hiyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...