Matokeo mazuri ya kila jambo yanahitaji maandalizi timamu na ndivyo tunavyofanya kuelekea msimu mpya wa ligi daraja la kwanza.
Wakati maandalizi yakiwa yamenoga jana tumetangaza tarehe rasmi ya utambulisho wa timu kwa wakazi wa Temeke na mkoa wa Dar es salaam kwa ujumla.w
Mtendaji mkuu wa klabu Abubakar Jafo amewaambia wanahabari kwamba kuanzia leo ni wiki ya REHA FC ambapo kilele chake itakua siku ya jumapili kwenye uwanja wa Bandari Tandika.
Wakati maandalizi yakiwa yamenoga jana tumetangaza tarehe rasmi ya utambulisho wa timu kwa wakazi wa Temeke na mkoa wa Dar es salaam kwa ujumla.w
Mtendaji mkuu wa klabu Abubakar Jafo amewaambia wanahabari kwamba kuanzia leo ni wiki ya REHA FC ambapo kilele chake itakua siku ya jumapili kwenye uwanja wa Bandari Tandika.
"Wiki
ya Reha itahusisha shughuli mbalimbali za kijamii ikiwemo kufungua
matawi yetu na kuhitimishwa kwa michezo maalum itakayohusisha timu nne
ambazo ni Mtibwa, KMC na Transit Camp na wenyeji Reha fc" amesema Jafo.
Jafo amesema michezo hiyo itaanza jumamosi kwa mchezo wa mapema saa 8 mchana kati ya Reha dhidi ya Transit Camp na saa 10 jioni Mtibwa itacheza na KMC kisha washindi watacheza fainal siku ya jumapili jioni huku waliofungwa wakicheza mchana. "Siku hiyo tutaitumia kuwatambulisha wachezaji wetu pamoja na benchi la ufundi".
Jafo amesema michezo hiyo itaanza jumamosi kwa mchezo wa mapema saa 8 mchana kati ya Reha dhidi ya Transit Camp na saa 10 jioni Mtibwa itacheza na KMC kisha washindi watacheza fainal siku ya jumapili jioni huku waliofungwa wakicheza mchana. "Siku hiyo tutaitumia kuwatambulisha wachezaji wetu pamoja na benchi la ufundi".
Mtendaji Mkuu wa timu ya Reha Fc Abubakar Jafo
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...