Na. Vero Ignatus Dodoma.
Taasisi
ya mabalozi wa usalama barabarani nchini wamefanya kongamano la siku
Mkoani Dodoma dhima kuu ikiwa '' Mabadiliko ya sheria ni muhimu katika
kuimarisha usalama nchini''
Kongamano
hilo limefanyika kwasababu ya mkono mabadiliko ya sheria za usalama
barabarani kushirikiana /kuwahusisha viongozi wanaohusika na mambo ya
kisera na waunge mkono mabadiliko ya sheria hiyo.
Mkurugenzi wa habari na mawasiliano RSA, ambae pia ni mjumbe wa Baraza la Taifa usalama barabarani Augustus Fungo amesema
kuwa wanahitaji mabadiliko ya sheria ya usalama barabarani kwani
iliyopo haikidhi na imepitwa na wakati kwani ilitungwa mwaka 1983.
''
Wakati sheria hii ikitungwa sayansi na teknolojia ilikuwa haijashika
kasi kama ilivyo sasa, barabara zetu, vyombo vya moto vilikuwa vichache
tofauti na miaka ya leo'' alisemaFungo.
Kwa upande wake Kamanda wa kikosi cha usalama barabarani Tanzania Fortunatus Musilim
amewapongeza RSA kwa ushirikiano wao na jeshi la polisi kwa kutoa
taarifa mbalimbali pale ajali inapotokea na hata pale sheria
zinapovunjwa hata uhalifu unapotokea.
Mkuu wa wilaya ya Dodoma Mjini Patrobas Katambi ambae pia alimuwakilisha mkuu wa mkoa wa Dodoma Dkt Binilith Mahengeakizungumza katika kongamano la Usalama. Barrabarani lililoandaliwa na Mabalozi wa usalama barabarani( RSA) na kufanyika katika Ukumbi wa Pius Msekwa Bungeni Dodoma jana. Picha na Vero Ignatus
Mwalimu wa Elimu ya Usalama barabrani ambae pia ni mmoja wa Baraza la Usalama. Barabarani Nchini. Picha na Vero Ignatus
Mkuu wa wilaya ya Gairo Siriel Mchembe akizungumza katika kongamano hilo Jijini Dodoma. Picha na Vero Ignatus
Mkurugenzi wa Huduma ya Sheria Nchini Marlin Komba Akiwa na Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama barabarani Nchini Fortunatus Musilim. Picha na Vero Ignatus.
Wa kwanza kushoto ni mwenyekiti wa Mabalozi wa Usalama Barabarani Nchini (RSA) John Seka akifuatiwa na Kamanda wa Polisi Kikosi chq Usalama Barabarani SACP Fortunatus Musilim, Mkuu wa wilaya ya Gairo Siriel Mchembe, Mkuu wa wilaya ya Dodoma mjini Patrobas Katambi, Mkuu wa Polisi kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Iringa Kamotta, na Mkurugenzi wa Huduma ya sheria Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Marlin Komba. Picha na Vero Ignatus.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...