Kwa
mara ya tatu mfululizo, CITI Foundation ikishirikiana na Shirikisho la
Asasi zinazotoa huduma ndogo za fedha (TAMFI), jana wamezindua awamu ya
tatu ya tuzo za wajasiriamali za CITI (CITI Micro entrepreneurship
Awards – CMA).Tuzo hizi zinalenga kutambua mchango mkubwa wa
wajasiriamali kwenye kuinua uchumi wa familia zao na jamii
zinazowazunguka.
Kwa mujibu wa Mtendaji Mkuu wa Citibank Tanzania, Bw. Joseph Carasso, tuzo za CITI zimeshamiri na katika kipindi cha miaka miwili iliyopita kumekuwa na mafanikio makubwa kwa wajasiriamali wadogo na walio wabunifu.
Kwa mujibu wa Mtendaji Mkuu wa Citibank Tanzania, Bw. Joseph Carasso, tuzo za CITI zimeshamiri na katika kipindi cha miaka miwili iliyopita kumekuwa na mafanikio makubwa kwa wajasiriamali wadogo na walio wabunifu.
Mtendaji huyo alisema CITI inaamini kuwa wajasiriamali wadogo wenye ubunifu ndio wajasiriamali wakubwa wa kesho. Tunawathamini sana.Tuzo za wajasiriamali za CITI (CMA) zimekuwa alama kubwa ya utendaji wa kazi za Citi Foundation kwa zaidi ya muongo mmoja.
Tangu mwaka 2005, wakati zilipoanzishwa nchini Marekani tuzo za CITI, zimelenga kuleta mageuzi ya kiuchumi na fursa kwa wajasiriamali katika nchi zaidi ya nchi thelatini duniani kote.Hapa nchini katika awam,u ya tatu , CITI itatoa zaidi ya shilingi milioni 70 kwa washindi kumi na sita. Na tuzo hizi zitaweka alama na kutoa motisha kwa wajasiriamali na asasi zinazotoa huduma ndogo za fedha.
Mtendaji mkuu Citi bank Tanzania joseph Carasso akizungumza. Mwingine ni wmenyekiti wa bodi ya Tamsi Joel Mwakitalu .
Mtendaji wa TAMFI Terry akielezea hafla ya uzinduzi wa tuzo
Washiriki katika uzinduzi
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...