Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Doto James (kulia) akiwa pamoja na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika(AfDB) Alex Mubiru wakisaini mikataba ya makubaliano ya mkopo wa masharti nafuu wa jumla ya Shilingi bilioni 440.703 pamoja na msaada wa Shilingi bilioni 45 ambapo fedha hizo zote zitatumika katika Mradi mkubwa wa umeme mkoani Kigoma, Bajeti Kuu ya Serikali, Kilimo pamoja na mambo mengine ya kimaendeleo.
. Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Doto James (kulia) akizungumza na wanahabari (hawaonekani) pichani mara baada ya kusaini Mikataba hiyo ya mkopo wa masharti nafuu wa jumla ya Shilingi bilioni 440.703 pamoja na msaada wa Shilingi bilioni 45 kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) katika hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa wa Hazina jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika Alex Mubiru
Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika(AfDB) Alex Mubiru (kushoto) akizungumza na Wanahabari mara baada ya Benki hiyo kuikopesha Serikali ya Tanzania jumla ya Shilingi bilioni 440.703 pamoja na msaada wa Shilingi bilioni 45 ambapo fedha hizo zote zitatumika katika Mradi mkubwa wa umeme mkoani Kigoma, Bajeti Kuu ya Serikali, Kilimo pamoja na mambo mengine ya kimaendeleo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...