Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
SERIKALI imesema kuwa inatambua na kuthamini mchango unaotolewa na Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA)katika kuandaa watalaam wa Tasnia ya Uhasibu, Ununuzi na Ugavi Biashara pamoja na uongozi wa Rasilimali Watu.
Hayo ameyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Doto James wakati alipomwakilisha Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango katika mahafali ya 16 ya Taasisi Uhasibu Tanzania kwa Kampasi za Dar es Salaam pamoja na Mtwara yaliyofanyika katika viwanja vya Taasisi hio jijini Dar es Salaam.
James amesema kuwa serikali itaendelea kuunga mkono pamoja na taasisi kutekeleza majukumu kwa weledi katika kubuni mbinu mpya za kuimarisha mapambano ya kupata mafanikio makubwa.
Amesema Taasisi hiyo iendelee kubuni mbinu kujitangaza zaidi na kujiuza kwa bidhaa wanazozitoa kwa ndani na nje nchi katika ili kuongeza wanachuo zaidi.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Doto James akizungumza katika mahafali ya 16 ya Taasisi Uhasibu Tanzania (TIA) kwa Kampasi za Dar es Salaam pamoja na Mtwara yaliyofanyika katika viwanja vya Taasisi hio jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri wa TIA, Wakili Said Chiguma akizungumza kuhusiana na hali ya uendeshaji wa Taasisi hiyo katika mahafali ya 16 ya Taasisi Uhasibu Tanzania (TIA) kwa Kampasi za Dar es Salaam pamoja na Mtwara yaliyofanyika katika viwanja vya Taasisi hio jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA)Dkt. Joseph Kihanda akizungumza historia ya taasisi hiyo mahafali ya 16 ya Taasisi Uhasibu Tanzania (TIA) kwa Kampasi za Dar es Salaam pamoja na Mtwara yaliyofanyika katika viwanja vya Taasisi hio jijini Dar es Salaam
Wahitimu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) katika mahafali ya 16 ya Taasisi hiyo kwa Kampasi za Dar es Salaam pamoja na Mtwara yaliyofanyika katika viwanja vya Taasisi hio jijini Dar es Salaam.
Wahitimu wakicheza muziki baada ya kutunukiwa shahada mbalimbali zinazotolewa na Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA)katika katika mahafali ya 16 ya Taasisi hiyo kwa Kampasi za Dar es Salaam pamoja na Mtwara yaliyofanyika katika viwanja vya Taasisi hio jijini Dar es Salaam.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...