Mkuu wa Wilaya ya Magu Mkoani Mwanza Mhe. Philemon Sengati amesema kuwa Dhamira yake ni Kuhakikisha kuwa Ustawi wa Wananchi hasa Wanyonge Unafikiwa kwa Wakati kama ilivyo Dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano. Akizungumza wakati akifunga mafunzo ya kuwajengea uwezo wakulima 200 wa vijiji vya Shinembo na Kitongosima Wilayani humo yakilenga kuwawezesha kutumia rasilimali ardhi kujiletea maendeleo baada yakurasimisha maeneo yao na kupatiwa hati za kimila za kumiliki ardhi.
“Jukumu letu ni kuhakikisha kuwa tunaleta ustawi wa wananchi na hasa wale wanyonge kwa kuhakikisha kuwa wanapata haki zao katika maeneo yote ambayo yanalenga kuwawezesha wananchi kujikwamua ndio maana tunawasisitiza kufanya kazi kwa bidii”; Alisisitiza Mhe. Sengati Akifafanua amesema kuwa Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania umefanya kazi kubwa kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya hiyo kwa kufanikisha urasimishaji wa mashamba ya wakulima hao na kuandaa na kutoa jumla ya Hati Milki za kimila 1383 .
Akizungumzia umuhimu wa mafunzo hayo Mhe. Sengati amesema kuwa kati ya wakulima 2,690 waliopimiwa mashamba yao ni wakulima 200 waliobahatika kupata mafunzo hayo yakuwajengea uwezo ili waweze kushiriki katika kutekeleza dhana ya kilimo biashara hivyo jukumu lao ni kutumia vizuri mafunzo waliyopata na kuwashirikisha elimu hiyo wananchi wengine ambao hawakupata bahati ya kushiriki katika mafunzo hayo.
Mkuu wa Wilaya ya Magu Mkoani Mwanza akizungumza na wanachi walioshiriki katika mafunzo yakuwajengea uwezo ili waweze kutekeleza dhana ya kilimo biashara katika Wilaya hiyo, mafunzo hayo yameratibiwa na Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge (MKURABITA) kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya hiyo na kuwashirikisha wakulima 200, Kushoto ni mwenyekiti wa mafunzo hayo Bw. Benet Makongoro na kulia ni Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya hiyo Bi. Atupele Mwaikuju.
Meneja Urasimishaji Ardhi Vijijini kutoka MKURABITA Bw. Antony Temu akisisitiza faida za mafunzo kwa wakulima wa vijiji vya Shinembo na Kitongosima vya Wilayani Magu Mkoani Mwanza.
Sehemu ya Wananchi wa wakionesha hati ya kimila ya kumiliki ardhi wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo ili waweze kutekeleza dhana ya kilimo biashara kwa vitendo.
Sehemu ya wananchi walioshiriki katika mafunzo yakuwajengea uwezo ili watekeleze dhana ya kilimo biashara.
Meneja Urasimishaji Ardhi Vijijini kutoka MKURABITA Bw. Antony Temu akisisitiza jambo kwa wakulima 200 Wilayani humo ili waweze kushiriki kikamilifu katika kukuza uchumi wao kupitia sekta ya kilimo baada yakujengewa uwezo ili waweze kutekeleza miradi yakujiletea maendeleo ikiwemo kutekeleza kwa vitendo dhana ya kilimo biashara.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...