Filbert Bayi Sanka ni mwanariadha aliyeiandikia Tanzania historia isiyoweza kusahaulika. Filbert Bayi ndie mwanariadha wa Pili ambae anakamilisha medali ya pili ya Tanzania kwenye Mashindano ya Olympic.
Tanzania Imewahi kupata Medali mbili tu katika Mashindano ya Olympic mpaka sasa. Filbert Bayi alipata Medali ya Silver katika mbio za mita 3000 katika mashindano ya Olympic yaliyofanyika mwaka 1980 MOSCOW Mwaka 1978(mita 1500) na Mwaka 1973 (mita 1500) katika mashindano ya All African Games Fibert Bayi alishinda Medali za Dhahabu kwa kuibuka namba moja katika mashindano yote mawili.
Ushindi huu ulitengeneza historia kubwa Tanzania. Mwaka 1974 katika mashindano ya Commonwealth Games yaliyofanyika Christchurch “New Zealand” Filbert Bayi aliweka rekodi ya kukimbia mita 1500 kwa dakika 3 na sekunde 32.2 mbele ya mwanariadha kutoka New Zealand John Walker na Mkenya Ben Jipcho, hivyo kuiwezesha Tanzania kupata medali ya Dhahabu katika mashindano hayo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...