Na, Editha Edward-Tabora.
Uhaba wa Miundombinu ya madarasa,viti,meza katika shule za msingi, Halmashauri ya manispaa ya Wilaya ya Tabora, unatajwa kurudisha nyuma jitahada za ufaulu wa wanafunzi wilayani humo.
Hayo yamebainishwa mapema hii leo na mkuu wa Wilaya ya Tabora Manispaa,Erick Komanya wakati akipokea mifuko 200 ya Saruji kutoka shirika la Reli Tanzania Mkoa wa Tabora (TRC).
Komanya amesema tatizo hili la uhaba wa madarasa linayumbisha jitihada za ufaulu kwa vijana walioko mashuleni huku akiwahakikishia wadau wote wanaotoa michango yao ili kuinua Elimu katika Halimashauri ya Wilaya ya Tabora Manispaa kuwa michango hiyo itafanya kazi iliyokusudiwa.
"Madarasa 128 ambayo tumekusudia kuyajenga kwa mwaka huu, kila kata katika Halimashauri ya Manispaa ya Tabora inatakiwa kuhakikisha inajenga vyumba vinne (4)vya Madarasa" amesema Komanya.
Akizungumza na Michuzi Blog Kwaniaba ya Mkurugenzi wa Shirika la Reli nchini Bwn Kadogosa Masanja,mkuu wa chuo cha Reli mkoani Tabora ndugu John Kaberege,huku akikabidhi mifuko 200 ya saruji amesema shirika limeamua kufanya hivi ikiwa ni moja ya kufanya kazi ya jamii Coorparate Social Responsibility(CSR).
"Shirika la Reli mkoani Tabora tumeamua kuchangia mifuko hii ya saruji ili kutengeneza mazingira mazuri ya Elimu kwa watoto wetu ambao ni viongozi wa kesho" amesema Kaberege.
Hatahivyo Halimashauri ya Manispaa ya Wilaya ya Tabora bado inakabiliwa na uhaba wa vyumba vya Madarasa zaidi ya 230 ikiwa mahitaji ni vyumba 360 na tayari vyumba 128 vimeshaingizwa kwenye mpango wa Ujenzi, hali hii inapelekea baadhi ya wanafunzi kukaa kwa kubanana na kushusha kiwango cha Ufaulu wao.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...