Ukaguzi wa mradi wa maji wa kisima kirefu katika Kijiji cha Matela, Kata ya Isangijo wilayani Magu.
Ukaguzi wa mradi wa uzalishaji mali wa kikundi cha ESM Kangara ambapo kinajihusisha na ufugaji wa kuku, bata, njiwa, mbwa na paka.
Ukaguzi wa Zahanati ya Bundilya wilayani Magu.
Jiwe la Msingi la Kituo cha Afya cha kwanza kujengwa wilayani Magu.
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella kwenye ukaguzi wa Kituo cha Afya Nyerere kilichopo Kata ya Kangara wilayani Magu.
Mkuu
wa Mkoa Mwanza, John Mongella akiwa ameambatana na Kamati ya Ulinzi na
Usalama Mkoa pamoja na viongozi mbalimbali ngazi ya Wilaya anaendelea na
ziara ya kutembelea na kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo
mkoani Mwanza. Hapa Mongella akiwasili kukagua maendeleo ya ujenzi wa
Shule ya Sekondari Lumnve iliyopo Kata ya Bujora wilayani Magu.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Mkuu
wa Mkoa Mwanza, John Mongella kwenye ukaguzi wa kisima kirefu cha maji
Isangijo ikiwa ni moja ya visima 16 vinavyochimbwa wilayani Magu ili
kuondoa adha ya maji kwa wananchi.
Ukaguzi
wa shamba la miti la Bahati Kwangu ambaye ni mkazi wa Kijiji cha
Busekwa, Kata ya Bujashi wilayani Magu lenye miti zaidi ya elfu 10
likiwa na ukubwa wa Hekali saba, lengo likiwa ni kuhifadhi mazingira
pamoja na kitega uchumi kwa baadae.
Ukaguzi wa Zahanati ya Isangijo wilayani Magu.
Ukaguzi wa shughuli za kikundi cha wazalishaji mali cha "Meremeta Leather Group" wilayani Magu kinachojihusisha na utengenezaji wa bidhaa za ngozi ikiwemo viatu.
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella alitembelea Shule ya Musabi wilayani Magu ambapo kuna klabu ya TAKUKURU kwa wanafunzi wa shule ya msingi.
Wanafunzi wakafurahi kukutana na viongozi wao.
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akaweka jiwe la msingi la ujenzi wa madarasa katika Shule ya Sekondari Maligisu wilayani Kwimba.
Wananchi wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella alipotembelea Shule ya Sekondari Maligisu wilayani Kwimba.
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella aligoma kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa maji Kadashi wilayani Kwimba ambao ulianza mwaka 2013 ambapo aliagiza mradi huo ukamilike na kutoa maji katika magati yote 21 ifikapo Juni Mosi 2019.
Tazama BMG Online TV hapa chini
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...