NA MWAMVUA MWINYI, PWANI
MWENYEKITI wa kamati ya ulinzi na usalama mkoani Pwani, Mhandisi
Evarist Ndikilo, ameridhishwa na ujenzi wa nyumba 42 za askari ambazo
zipo kwenye hatua ya umaliziaji kwa kanda maalum ya kipolisi Rufiji na
jeshi la polisi mkoani Pwani ambazo zitagharimu sh. bilioni moja.
Aidha amewaasa wadau kushiriki kusaidia ujenzi wa makazi ya askari ili
kutatua changamoto ya upungufu wa makazi ya askari ilihali kuimarisha
ulinzi wa mali ,raia na miradi mikubwa ya kimkakati.
Akizungumza wakati alipokwenda kutembelea ujenzi wa nyumba za askari huko Rufiji, Ndikilo alitaka ujenzi huo ,ukamilike ifikapo Juni 30 mwaka huu, kama amiri jeshi wa majeshi ya ulinzi na usalama ,dkt. John Magufuli alivyoelekeza.
Alisema, baadhi ya askari wanakabiliwa na tatizo la upungufu wa makazi ya kuishi, hali inayosababisha kushindwa kuwahi wakati wakihitajika haraka katika dharula za majukumu yao ya kikazi.
"Kutokana na hali hiyo, kwasasa jeshi hilo linajenga nyumba 22 kanda ya kipolisi Rufiji na nyumba 20 za makazi ya askari polisi hao Kibaha mjini ,ambapo kwa mkoa wetu makamanda wa polisi wapo wawili hivyo kila mmoja amekabidhiwa milioni 500 "
"Uzuri wa kuanza kuimarisha makazi haya ,mjue mkoa upo karibu pia na mradi mkubwa wa ujenzi wa kuzalisha umeme stigo wilayani Rufiji,kwa maana nyingine maandalizi haya vijana wetu askari tunawaweka tayari na karibu kulinda miradi ya aina hii"alifafanua Ndikilo
Hata hivyo Ndikilo alielezea,milango ya kushirikiana kutatua
changamoto hiyo ipo wazi.
Awali akitoa taarifa fupi juu ya ujenzi unavyoendelea, Mwenyekiti wa
kamati ya ujenzi ambae pia ni kaimu kamanda wa kanda maalum ya
kipolisi Rufiji ,Taraja Gibe alibainisha, walipokea milioni 500
,ujenzi ulianza January mwaka huu ,na wamehusisha wadau mbalimbali
ambao wamechangia vifaa na milioni 19.
Wakati huo huo kamanda wa polisi mkoani Pwani ,Wankyo Nyigesa amesema,
wamepokea michango mbalimbali kutoka kwa wadau na wawekezaji ambapo
jana wamekabidhiwa pia vigae (tiles) kutoka kiwanda cha KEDA kilichopo
Chalinze ,zilizogharimu milioni tano.
Mkoa wa Pwani ni moja ya mikoa ambayo , Amiri Jeshi wa Majeshi dk.
Magufuli akiwa anazindua nyumba za askari polisi mkoani Arusha ,april
7 mwaka 2018, alitoa maelekezo kwa mkuu wa jeshi la polisi nchini
(IGP) kwamba atapatiwa fedha kwa ajili ya makazi ya askari ,ambapo
mkoa huo umeanza utekelezaji baada ya kupokea fungu hilo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...