Na Gift Thadey, Simanjiro

Mkuu wa Wilaya mstaafu wa Simanjiro, mhandisi Zephania Adrian Chaula na Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga, RAS Zuwena Omary Jiri wameagwa rasmi na chama cha wachimbaji wa madini Mkoa wa Manyara (MAREMA) Tawi la Mirerani na kukabidhiwa tuzo na Mkuu wa Mkoa huo, Charles Makongoro Nyerere.

DC mstaafu mhandisi Chaula na Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga (RAS Shinyanga Zuwena ambaye awali alikuwa Katibu Tawala wa Wilaya DAS wa Simanjiro, waliagwa rasmi na MAREMA Tawi la Mirerani kwa kukabidhiwa tuzo na RC Makongoro kwenye tukio la kuwapa tuzo 19 za aina tatu, wamiliki tisa wa migodi ya madini ya Tanzanite katika Mji mdogo wa Mirerani.   

Hata hivyo, katika tukio hilo RAS Shinyanga Zuwena alikabidhiwa tuzo hiyo ila DC mstaafu Simanjiro Chaula hakuwepo na tuzo yake ikakabidhiwa kwa Kaimu Katibu Tawala wa wilaya hiyo Mussa Waziri.

Akizungumza baada ya kukabidhiwa tuzo hiyo RAS Zuwena amewashukuru wadau wote, wachimbaji madini, viongozi na wananchi wa Simanjiro kwa ujumla kwa namna walivyofanikisha utendaji kazi wake kipindi akiwa DAS.  

Amesema alipata wepesi wa kutekeleza wajibu wake kutokana na umoja, mshikamano na upendo uliokuwepo kwa wananchi na viongozi wa Simanjiro hivyo anawaaga kwa upendo mkubwa na kuwashukuru.

“Nawashukuru wote ila Katibu wa MAREMA Tawi la Mirerani Rachel Njau na Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Simanjiro Yefred Myenzi, kwa nafasi ya kipekee nawashukuru sana kwa namna mlivyokuwa mnanisaidia kutekeleza maelekezo ya Mkuu wetu wa wilaya,” amesema Zuwena.

Amewaahidi kuendeleza mazuri yote kwenye nafasi mpya aliyoipata ya RAS Shinyanga na akamshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa namna alivyomuamini na kumteua katika kushika nafasi hiyo.

Hata hivyo, Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Charles Makongoro Nyerere, amempongeza RAS Zuwena kwa kuteuliwa na Rais Mama Samia kushika nafasi hiyo hivyo awakilishe vyema huko Shinyanga kwa heshima ya alipotoka.

“Utakapofanya kazi zako vizuri ukiwa Shinyanga sifa zitakuja Simanjiro na Manyara kwa ujumla ila ukiharibu utasababisha sisi sote tuonekane kuwa tumeharibu nakusihi usije kutuangusha huko Shinyanga,” amesema Makongoro


Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga, RAS Zuwena Omary Jiri akiwa na mumewe baada ya kukabidhiwa tuzo na Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Charles Makongoro Nyerere, kama ishara ya zawadi ya utumishi uliotukuka kwenye nafasi ya Katibu Tawala wa Wilaya DAS Simanjiro iliyotolewa na Chama cha wachimbaji madini Mkoa wa Manyara, (MAREMA) Tawi la Mirerani.
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Charles Makongoro Nyerere, akimkabidhi tuzo Katibu Tawala wa Mkoa RAS Shinyanga, Zuwena Omary Jiri kama ishara ya zawadi ya utumishi uliotukuka kwenye nafasi ya Katibu Tawala wa Wilaya DAS Simanjiro iliyotolewa na Chama cha wachimbaji madini Mkoa wa Manyara, (MAREMA) Tawi la Mirerani.

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...