Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Hemedi Mgaza (kulia)amefanya mazungumzo na Balozi wa Tanzania nchini Kuwait, Mhe. Said Shaibu Mussa alipokuja kuaga uongozi wa Wizara tarehe 14 Januari 2022 jijini Dodoma.

Viongozi hao walijadili hali halisi ya utekelezaji wa majukumu ndani ya Idara ya Mashariki ya Kati na kuweka mikakati madhubuti ya usimamizi wa majukumu katika dawati la Kuwait linaloratibiwa na idara hiyo.
Kwa pamoja wameazimia kufanya kazi kwa ushirikiano, kusimamia miradi ya ushirikiano inayoendela katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu inayofadhiliwa na Mfumo wa Kuwait hususani miradi ya kilimo, maji, ujenzi wa miundombinu, afya, elimu na ajira za kitaalamu.

Balozi Mgaza akimkaribisha Mhe. Said Shaibu Mussa katika ofisi za Wizara jijini Dodoma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...