Na Mwamvua Mwinyi, Rufiji April 19


Jeshi la Wananchi wa Tanzania limetoa magari kumi kwa ajili ya kusaidia kusafirisha vyakula kwenda kwenye makambi ya waathirika wa mafuriko walioko kwenye Wilaya za Rufiji na Kibiti Mkoa wa Pwani.

Akipokea Magari hayo April 18, 2024 Wilayani Rufiji, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amempongeza Amiri Jeshi Mkuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mkuu wa Majeshi kwa magari hayo.

Ameeleza kuwa wamepata misaada ya vyakula lakini kulikuwa na changamoto ya usafiri na Barabara katika kufikia walengwa.

Amesema magari hayo yatasaidia kufika kirahisi maeneo hayo yenye changamoto.

Vilevile Kunenge amepongeza Jeshi kwa kuendelea kulinda mipaka ya nchi na Amani kuendelea kuhudumia Jamii.

Kadhalika Kunenge,amekabidhi magari hayo kwa Wakuu wa Wilaya za Kibiti na Rufiji.



 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...