Hakuna hadithi nyingine zaidi ya Wewe kupata haki yako, Muhimu Njoo na Nyaraka zako zote na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda yupo tayari kukuhudumia na kupambana kwaajili yako dhidi ya wanaozuia haki yako kwa muda mrefu.

Mkuu wa Mkoa Mhe. Paul Christian Makonda anakualika na kukusihi usiwe mnyonge kwasababu haki yao inakwenda kupatikana kupitia Mawakili na Wanasheria wabobezi walioandaliwa kukusikiliza na kuhakikisha unaipata haki yako kikamilifu.

Ni fahari na Heshima kwa Mkuu wa Mkoa wetu Mhe. Paul Christian Makonda kukuhudumia na kupambana kuhakikisha unaipata Haki yakl na kuyafuta Machozi yako.Ni Kheri pia kukuhudumia wewe Mkazi wa Arusha Popote Pale Ulipo.

Karibu Kwenye Ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Arusha kuanzia majira ya saa Mbili asubuhi ili uhudumiwe na kufutwa Machozi kutokana na Haki unayoistahili na kwa bahati mbaya ilifichwa, kukandamizwa na kupokwa na watu wasiokutakia mema.

Kazi ni Moja tu kwa siku tatu mfululizo, kukusikiliza na kurejesha Haki yako iliyopotea.


  Picha ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha Paul Christian Makonda

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...