Na. Vero Ignatus, Arusha

Waziri wa Maliasili na Utalii Angela Kairuki amesema kuwa katika takwimu na tafiti za Shirika la Utalii duniani Tanzania imewekwa katila nchi ya kuigwa ambayo imekuza uchumi wake kwa kupitia mapato ya utalii na kuingia kwenye kumi Bora, kwani kwa mwaka 2022 imeweza kupokea watalii 1,456,920 mwaka 2023 1,808,205 hii ikiwa ni kwa mwaka mmoja sawa na ongezeko la asilimia 24.28.

Kairuki amesema hayo katika mikutano mkuu wa mwaka wa Taasisi ya waongoza watalii nchini mei 4,2024 Jijini Arusha, kuwa mapato ya utalii kwa mwaka 2022 waliweza kuwa dola za kimarekani bil 2.5 ambapo mwaka 2023 waliweza kufunga mwaka kwa dola za kimarekani bil. 3.3
Malengo ya serikali ifikapo 2025 unapaswa kuwa na mapato ya utalio yasiyopungua bil 6

" Rais Dkt Samia amekuwa ni mwongoza watalii namba moja kwenye kutangaza utalii haswa kupitia program yake ya Royal tour ambapo wameweza kuona matokeo makubwa,ya kuongezeka kwa watalii nchini,sambamba na juhudi nyingine za kuboresha miundombinu ya utalii ambapo aliweza kutoa mafunzo kwa waongoza utalii zaidi ya 1000 kipindi cha covid 19. "

Aidha amewapongeza waongoza watalii Hao kwa kusema kuwa eneo hilo ni nyeti ambalo ni la kukuza Utalii ni la muhimu na kuwa taka kuendelea kuwa mabalozi wazuri katika ulinzi wa mazingira katika hifadhi , sambamba na kulinda utamaduni na Mila za Mtanzania.

Akijibu changamoto za waongoza utalii amesema kuwa suala la bima ya Afya siyo kwamba iliyokuwa awali ya kicurishi vha 100,000 imefutwa la hasha badala yake ni kwamba taarifa za awali alizonazo kupitia kwamba imeongezeka na kufikia 192000 kwa mwaka amewataka wao wenyewe kijuridhisha na kiwango hicho

"Kwa upande wa barabara ya londware kupitia karate kwa sasa inaendelea kufanyia kazi kwani serikali imeweza.kupitia Baheti yetu ya 2023-24 Kutenga shilingi Bil 16 , pia serikali kwa Baheti ya mwaka 2024-25 serikali imetenga shilingi Bil. 40 ambazo zitatumiks. Line. Ga barabara za londware kwa aina ya tabaka gumu".

"Changamoto ya leseni za waongoza utalii na tozo zake maslahi mbalimbali, gharama za malazi kwa waongoza watalii tauari tumeshaanza kufanyia kazi Malalamiko yote ili kuyapatia suluhu kwsajili ya kuboresha na kukuza biashara ya utalii, ni Bornora mokajiwekea viwango vya ubora, hivyo 2024 -2025 serikali itatoa tena mafunzo ya utalii kwenu kwani ninyi ndio taswira ya nchi yetu.'alisema

"Suala la mikataba ya Ajira 6 april nilishamueleza Afisa kazi mkoa wa Arushana tayari alishaitisha kikao 25 April 2024 ambacho kilihudhiriwa na wadau kutoka TTGA, Wizaara ya kazi na niliwaambia lazima wataalam kutoka Wizara ya maliasili na utalii wawepo maana ndio walezi wenu na washauri wenu na waliweza kupeana eliminate juu ya mikataba ya Ajira.

Awali akisoma risala Katibu Mkuu wa Taasisi ya waongoza watalii Tanzania Robert Max Asilimia 70% ya waongoza utalii nchini hawana mikataba ya ajira 30% tu ndiyo wameajiriwa wengi mbali na sekta hiyo kuliingizia Taifa 25℅ya pesa za kigeni na inachangia Pato la Taifa 15% ambapo muda mwingi wanakaa na wageni kwa muda mrefu Hadi wanaondoka nchini

Max ameeleza kuwa zipo changamoto wanazokutana nazo ni pamoja na kutokuwa na mikataba na mishahara kutoka kwa waajiri wao , bima ya Afya imekuwa changamoto kubwa kwao kwani hapo awali wali kuwa wanaipata kwa kifurushi kwa tsh 100,000 Ila kwa sasa kimefutwa

Tunakuomba utusaidie kwani hadi tunapozungumza wakati huu waongoza watalii wengi wamelala Vitandani hawana matibabu ,tunaomba suala la miundombinu ndani ya hifadhi kutoka Lodware getini hadi Karatu kuelekea Serengeti barabara hiyo imekuwa changamoto,pia hakuna huduma ya (picnic site)kwaajili ya huduma ya choo kwa wageni Jambo ambalo tunalazimika kuwashusha wageni porini kwani ni hatari kwajili ya wanyama na nyoka.

Dkt. Christopher Nzella Red Cross MKT wa Bodi ya TTGA:nimefika kilele cha mlima Kilimanjaro Mara 43 hawa waongoza watalii mhe.Waziri wanachangamoto nyingi haswa za kimaslahi, wanaweza kuharibi nchi au kuijenga nchi kutoka na na kile wanachokifanya, tunaomba uyaunganishe MAKUNDI haha wanashida wanapunjwa maslahi yao, na waajiri wao.

Vilevile Dkt. Nzella aliweza kuwasihi waongoza utalii Hao kuwa na Tania ya kujiwekea akiba akiba kwani uzee una kuja kesho kutwa huku akimsihi mhe. Waziri was Kara hiyoasiwasahau Bali awe anawatvelea Mara kwa Mara kwa Mara ili watoe changamoto zao.

Kwa upande wake mwenyekiti mstaafu wa TTGA 2012-2018 ndugu Alifa Msangi alisema kuwa mkutano huo umewela Historia kwenye taasisi hiyo tangia kimeanzishwa kwa Waziri kuwa morning rasmi na yupo tayari kufanyabkazi na waongoza watalii nchini kwa karibu zaidi.

"Yupo tayari kupokea changamoto zetu Sisi waongoza watalii ambao tunaonekana watu wa chini Sana Ila yeye ameonyesha anamaono kwenye sekta hiyo" Alisema Msangi

Nae Mwenyekiti wa TTGA Lembrice Loipuko mkutano huo ni mkutano wa kawaida wa mwaka ambao unalenga kuwasomea maps to na matumizi pamoja na kuangalia malengo mikakati waliyokuwa wamejiwekea kama imetekelezwa na kutaka kuwa na mbinu mbadala kwaajili ya kuendeleza ukuaji wa Utalii nchini kwa kupitia waongoza watalii
Katikati ni Mwenyekiti wa TTGA Tanzania Lebrice Loipoku kushoto kwake ni Karibu wa TTGA Tanzania Robert Max wakiteta jambo kabla ya kuanza kikao cha mkutano mkuu wa mwaka uliofanyika katika ukumbi wa chuo cha Sauti Jijini Arusha




Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Angela Kairuki akisalimiana na baadhi ya viongozi wa Taasisi ya waongoza Utalii Jijini Arusha alipowasili kwaajili ya mkutano mkuu wa mwaka


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...