Mkali wa miondoko ya Dance hall kutoka nchini Marekani Beenie Man (kulia) akila pozi na Michuzi Jnr. katika hoteli ya collesium mara baada ya kutua jana Dar na kufanya onesho lake moja tu usiku wa kuamkia leo katika viwanja vya chuo cha posta maeneo ya kijitonyama. onyesho hilo liliandaliwa na kampuni ya Entertainment Masters na kudhaminiwa na kampuni ya sigara ya TCC kupitia chapa yake ya muziki ya Str8 Muzik.
Kwa picha zaidi za ujio wa Beenie Man
Duuuuh Jamaa kwa Pombe sio mchezo yaani nakumbuka mwaka 2000 alikuja Tanzania alifikia katika Hotel ya Sheraton yaani kila muda alikuwa na chupa au Glass ya pombe mkononi kuanzia asubuhi mpaka jioni! Nadhani muda pekee ambapo hanywi ni wakati wa kulala tu tembelea hiyo link uone vimbwanga
ReplyDeletehttp://michuzijr.blogspot.com/2009/06/beenie-man-atua-bongo-jioni-hii-na.html
Mzee Michuzi correction ndogo ni kwamba Beenie Man siyo Mmarekani,yeye ni true-born Jamaican na anaishi jamaica ila amefanya collaboration nyingi na wamarekani.
ReplyDeleteoyaa inaonekana mr ben hatosahau kama atavuta msuba mkali kama alioupata bongo yaani mpaka macho hayafunguki
ReplyDelete