Watumishi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), wamepongezwa kwa kuendelea kufanya Baraza la Wafanyakazi lenye tija lililofanya mamuzi makubwa yenye tija kwa kutuoa huduma bora na kukuza sekta ya usafiri wa anga nchini.

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi Mkuu wa TCAA Bw. Hamza Johari wakati wa ufunguzi wa Baraza la wafanyakazi la TCAA uliofanyika Novemba 23, 2023 makao makuu ya Mamlaka Banana jijini Dar es salaam.

Bw. Johari amewasifu wajumbe wa baraza kwa kufanya kuweka mbele maslahi ya taasisi na kuwasilisha hoja zinazoichochea menejimenti kutekeleza majukumu yake vyema. Pia ameongeza kuwa vikao hivyo vya Baraza ni njia bora ya kuimarisha demokrasia mahala pa kazi,na kuwataka wajumbe wa Baraza hilo kurudisha mrejesho kwa watumishi wenzao.

”Kama tunavyofahamu Mamlaka imetekeleza na inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya kimkakati ukiwemo wa Ununuzi wa Rada nne za kuongozea ndege, kuboresha Mfumo wa Masafa ya Mawasiliano wa Sauti baina ya rubani na waongozaji ndege katika vituo vyote vya kuongozea ndege nchini na Mradi wa kuimarisha na kuboresha utoaji taarifa za anga kuwa dijitali na yote hii ni mazao ya mawazo na hoja muhimu mnazoleta hapa na kwa pamoja tunapata ufumbuzi” alisema Bw. Johari.

Awali akiwasilisha salamu kwa niaba ya Chama cha Wafanyakazi Mkoa wa Dar es Salaam (TUGHE) Katibu wa TUGHE Mkoa wa Dar es Salaam Bi. Sara Rwezaula ameupongeza uongozi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania kwa kuteleza majukumu yake kwa namna shirikishi kwani inafanya kila mtumishi kujisikia sehemu ya Mamlaka na hivyo kuongeza ari ya utendaji kazi.

Akitoa maelezo ya jumla, Katibu wa Baraza hilo Bw. Mweya Dedacus amesema hichi ni kikao cha sita cha Baraza ambacho dhima kuu ni kuwasilisha mrejesho wa yale yaliyokuwa yamejadiliwa na kuazimiwa wakati wa kikao kilichopita cha Baraza kilichofanyika mwezi Aprili.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Hamza S. Johari (katikati) akizungumza na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la TCAA wakati wa kufungua kikao hicho. Kulia ni Bi. Massa K. Mumburi Katibu Msaidizi wa Baraza, Kushoto ni Katibu wa Baraza Bw. Dedacus Mweya


Katibu wa TUGHE Mkoa wa Dar es Salaam Bi. Sara Rwezaula akitoa pongezi wakati wa kikao cha Baraza

Katibu wa Baraza Bw. Mweya Dedacus akiwasilisha mrejesho wakati wa Baraza

Afisa Uchunguzi, Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma. Bw. Silvanus Njenga akiwasilisha mada kuhusu Maadili ya Utumishi wa Umma

Menejimenti ya TCAA ikifuatia wasilisho la maadili.




Wajumbe wa Baraza wakiendelea kufuatilia mada hiyo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...