*Ni la kusaka Wazo bora la kiuchumi ili kuibua ubunifu wa vijana,washindi kuvuna mamilioni
Na said Mwishehe,Michuzi TV
VIJANA wenye umri kuanzia miaka 15 hadi 35 wameshauriwa kujitokeza kwa wingi kushiriki Shindano la vijana uchumi challenge lenye kauli mbiu inayosema kwamba ‘Wana tunafikiri, Taifa linasonga’.
Akizungumza leo Aprili 13,2026 jijini Dar es Salaam ,Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya Vijana Uchumi Chalenji’, Joseph Malekela, ametangaza rasmi kuanza kwa shindano hilo la kupata wazo bora la kiuchumi linalolenga kuibua ubunifu wa vijana katika kukuza uchumi wa Taifa.
“Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Maendeleo ya Vijana, Dk.Joel Nanauka aliutangazia umma kuwa kutakuwa nashindano maalum na kwamba ameunda kamati ya kusimamiashindano hilo. Siku ya leo tunakuja kwenu tukiwa na maelezo ya kina kuhusu shindano la vijana uchumi challenge.”
Amesema kwa kutambua ongezeko la changamoto mbalimbali duniani ikiwemo vita, majanga ya kimataifa na ushindani wa kiuchumi, na kwa kuzingatia kwamba nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania zinaweza kuathirika moja kwa moja kutokana na madhara ya changamoto za kimataifa, Ofisi ya Rais - Maendeleo ya Vijana imeamua kuja na Shindano la Vijana Uchumi Challenge.
“Shindano hili linalenga kukuza Mawazo ya vijana, yenye ubunifu, yanayotekelezeka na endelevu katika kulinda na KukuzaUchumi wa Taifa letu dhidi ya athari za misukosuko yakimataifa.
“Ni shindano ambalo linakaribisha ushiriki wa kijana yeyote wa kitanzania mwenye umri kati ya miaka 15 – 35. Ili kushiriki, kijana mmoja mmoja anakaribishwa kuwasilisha wazo lake, kwanjia ya maandishi yasiyozidi maneno 300 au kwa njia ya video isiyozidi dakika 3 kupitia kiunganishi: bit.ly/VijanaUchumiChallenge2026\ kabla ya Aprili 30,2026.
Malekela amesema wazo linalowasilishwa ni sharti likidhi vigezo ambavyo vitatumika kupata washindi ambavyo ni Ubunifu: Kiwango cha fikra mpya na upekee wa wazo,Uelewa wa Changamoto za Kiuchumi: Kiwango cha uelewa wa mshiriki kuhusu changamoto za kiuchumi za sasa na muktadha wa kimataifa, Uhalisia: Utekelezekaji wa wazo na uwezekano wake kutekelezwa kwa vitendo.
Pia Athari kwa Uchumi: Mchango unaotarajiwa wa wazokatika kukuza uchumi wa taifa,Uwezo wa Kuleta fursa: Uwezo wa wazo kuzalisha nakuongeza fursa za ajira kwa vijana, Uendelevu: Uwezo wa wazo kudumu na kuleta matokeochanya ya muda mrefu pamoja na Ubora wa Uwasilishaji: Mpangilio, uwazi na urahisi wakuelewa pendekezo.
Kuhusu utaratibu utakaotumika kupata mshindi wa shindano hilo amesema kutakuwa na mchujo wa awali ambayo ni hatua ya mwanzo kabisa ambapo mawazo yote yatachambuliwa na wataalamu wa Kamati ya kitaifa ya Vijana, kisha watachagua mawazo 100 bora yawashiriki wote nchi nzima, na washiriki hao watepewataarifa moja kwa moja kupitia mawasiliano yaoyaliyowasilishwa.
Hatua ya pili ni robo fainali ambapo washiriki wote 100 kutoka nchi nzima watapata nafasi ya kukutanishwa pamoja, ili kutoa fursa ya kukutana ana kwa ana na timu ya majaji, kupata mafunzo ya kuboresha mawazo yao na kushiriki mchujo wa robo fainali utakaotoa dakika 10 kwa kila mshiriki kuwasilisha wazo lake, ambapo mawazo 30 bora yatachaguliwa kwenda hatua inayofuata.
Wakati mchujo wa nusu fainali ni kwamba washiriki waliofanikiwa kufikiahatua hii watapata nafasi ya kuboresha mawazo yao, kupata mafunzo zaidi na kushiriki mashindano ya nusu fainali, ambayo yatawapa nafasi ya dakika 10 kuwasilishakwa kina, ukubwa wa mawazo yao na kwanini yanafaakushinda. Mawazo 10 bora yatachaguliwa kuingia fainali.
“Vijana Platform ya fainali - Kitaifa: Washirika walioingia fainali watapata fursa ya kupata mafunzo ya muda mfupi ya namna bora ya kuwasilishaji wa Mawazo yao kwa umma na kuweza kuyapangilia kitaalamu.
“Washiriki wote 10 watapata nafasi ya dakika 10 kuwasilisha Mawazo yaokatika fainali ya shindano hili, litakalofanyika Mwishonimwa mezi mei, tarehe na mahali mtajulishwa. Tukio la fainali litatoa fursa kwa umma kushiriki na kujioneaubunifu wa Mawazo ya vijana wa Tanzania. “
Kuhusu zawadi za washindi amesema Mshindi wa Kwanza atapa fedha Sh. milioni 30, wa pili Sh. milioni 15 na watu Sh.milioni 5 pamoja na utambuzi wa vyeti rasmi kwawashiriki 100 bora.
Aidha, washindi 10 bora watanufaika na mentorship ili kukuza uwezo wao katika ubunifu na kuwapa fursa yakutekeleza kwa vitendo mawazo yao. Wakati washiriki 30 watakaoingia nusu fainali wataunganishwa na wadau mbalimbali wa umma na binafsi iki kutoa fursa ya kukuza uwezo wao na kuendelea kuyafanya mawazo yao yatekelezeke.
Ameongeza kuwa washiriki 100 bora wote watapata nafasi ya kutambuliwa(exposure) na jamii kwa kuwa watatambulishwa rasmi katika kurasa za shindano hilal na za wizara ili wadau wengi zaidi waweze kuona vipaji vya vijana na namna bora ya kuendeleakuwaunga mkono.
“Shindano hili ni kwa kila kijana wa Tanzania, hivyo tunawakaribisha vijana wote kushiriki kikamilifu. Pia tunawakaribisha wadau wa maendeleo ambao wangependa kuunga mkonoji tihada hizi ili kufanikisha kwa ukubwa zaidi shindano hili.”





Na said Mwishehe,Michuzi TV
VIJANA wenye umri kuanzia miaka 15 hadi 35 wameshauriwa kujitokeza kwa wingi kushiriki Shindano la vijana uchumi challenge lenye kauli mbiu inayosema kwamba ‘Wana tunafikiri, Taifa linasonga’.
Akizungumza leo Aprili 13,2026 jijini Dar es Salaam ,Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya Vijana Uchumi Chalenji’, Joseph Malekela, ametangaza rasmi kuanza kwa shindano hilo la kupata wazo bora la kiuchumi linalolenga kuibua ubunifu wa vijana katika kukuza uchumi wa Taifa.
“Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Maendeleo ya Vijana, Dk.Joel Nanauka aliutangazia umma kuwa kutakuwa nashindano maalum na kwamba ameunda kamati ya kusimamiashindano hilo. Siku ya leo tunakuja kwenu tukiwa na maelezo ya kina kuhusu shindano la vijana uchumi challenge.”
Amesema kwa kutambua ongezeko la changamoto mbalimbali duniani ikiwemo vita, majanga ya kimataifa na ushindani wa kiuchumi, na kwa kuzingatia kwamba nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania zinaweza kuathirika moja kwa moja kutokana na madhara ya changamoto za kimataifa, Ofisi ya Rais - Maendeleo ya Vijana imeamua kuja na Shindano la Vijana Uchumi Challenge.
“Shindano hili linalenga kukuza Mawazo ya vijana, yenye ubunifu, yanayotekelezeka na endelevu katika kulinda na KukuzaUchumi wa Taifa letu dhidi ya athari za misukosuko yakimataifa.
“Ni shindano ambalo linakaribisha ushiriki wa kijana yeyote wa kitanzania mwenye umri kati ya miaka 15 – 35. Ili kushiriki, kijana mmoja mmoja anakaribishwa kuwasilisha wazo lake, kwanjia ya maandishi yasiyozidi maneno 300 au kwa njia ya video isiyozidi dakika 3 kupitia kiunganishi: bit.ly/VijanaUchumiChallenge2026\ kabla ya Aprili 30,2026.
Malekela amesema wazo linalowasilishwa ni sharti likidhi vigezo ambavyo vitatumika kupata washindi ambavyo ni Ubunifu: Kiwango cha fikra mpya na upekee wa wazo,Uelewa wa Changamoto za Kiuchumi: Kiwango cha uelewa wa mshiriki kuhusu changamoto za kiuchumi za sasa na muktadha wa kimataifa, Uhalisia: Utekelezekaji wa wazo na uwezekano wake kutekelezwa kwa vitendo.
Pia Athari kwa Uchumi: Mchango unaotarajiwa wa wazokatika kukuza uchumi wa taifa,Uwezo wa Kuleta fursa: Uwezo wa wazo kuzalisha nakuongeza fursa za ajira kwa vijana, Uendelevu: Uwezo wa wazo kudumu na kuleta matokeochanya ya muda mrefu pamoja na Ubora wa Uwasilishaji: Mpangilio, uwazi na urahisi wakuelewa pendekezo.
Kuhusu utaratibu utakaotumika kupata mshindi wa shindano hilo amesema kutakuwa na mchujo wa awali ambayo ni hatua ya mwanzo kabisa ambapo mawazo yote yatachambuliwa na wataalamu wa Kamati ya kitaifa ya Vijana, kisha watachagua mawazo 100 bora yawashiriki wote nchi nzima, na washiriki hao watepewataarifa moja kwa moja kupitia mawasiliano yaoyaliyowasilishwa.
Hatua ya pili ni robo fainali ambapo washiriki wote 100 kutoka nchi nzima watapata nafasi ya kukutanishwa pamoja, ili kutoa fursa ya kukutana ana kwa ana na timu ya majaji, kupata mafunzo ya kuboresha mawazo yao na kushiriki mchujo wa robo fainali utakaotoa dakika 10 kwa kila mshiriki kuwasilisha wazo lake, ambapo mawazo 30 bora yatachaguliwa kwenda hatua inayofuata.
Wakati mchujo wa nusu fainali ni kwamba washiriki waliofanikiwa kufikiahatua hii watapata nafasi ya kuboresha mawazo yao, kupata mafunzo zaidi na kushiriki mashindano ya nusu fainali, ambayo yatawapa nafasi ya dakika 10 kuwasilishakwa kina, ukubwa wa mawazo yao na kwanini yanafaakushinda. Mawazo 10 bora yatachaguliwa kuingia fainali.
“Vijana Platform ya fainali - Kitaifa: Washirika walioingia fainali watapata fursa ya kupata mafunzo ya muda mfupi ya namna bora ya kuwasilishaji wa Mawazo yao kwa umma na kuweza kuyapangilia kitaalamu.
“Washiriki wote 10 watapata nafasi ya dakika 10 kuwasilisha Mawazo yaokatika fainali ya shindano hili, litakalofanyika Mwishonimwa mezi mei, tarehe na mahali mtajulishwa. Tukio la fainali litatoa fursa kwa umma kushiriki na kujioneaubunifu wa Mawazo ya vijana wa Tanzania. “
Kuhusu zawadi za washindi amesema Mshindi wa Kwanza atapa fedha Sh. milioni 30, wa pili Sh. milioni 15 na watu Sh.milioni 5 pamoja na utambuzi wa vyeti rasmi kwawashiriki 100 bora.
Aidha, washindi 10 bora watanufaika na mentorship ili kukuza uwezo wao katika ubunifu na kuwapa fursa yakutekeleza kwa vitendo mawazo yao. Wakati washiriki 30 watakaoingia nusu fainali wataunganishwa na wadau mbalimbali wa umma na binafsi iki kutoa fursa ya kukuza uwezo wao na kuendelea kuyafanya mawazo yao yatekelezeke.
Ameongeza kuwa washiriki 100 bora wote watapata nafasi ya kutambuliwa(exposure) na jamii kwa kuwa watatambulishwa rasmi katika kurasa za shindano hilal na za wizara ili wadau wengi zaidi waweze kuona vipaji vya vijana na namna bora ya kuendeleakuwaunga mkono.
“Shindano hili ni kwa kila kijana wa Tanzania, hivyo tunawakaribisha vijana wote kushiriki kikamilifu. Pia tunawakaribisha wadau wa maendeleo ambao wangependa kuunga mkonoji tihada hizi ili kufanikisha kwa ukubwa zaidi shindano hili.”












































.jpeg)










