Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya Oryx Energies Tanzania imezindua kituo kipya cha mafuta eneo la Wazo jijini Dar es Salaam huku mkakati wake wake ukiwa ni kuendelea kusogeza huduma za nishati za mafuta na gesi karibu na wananchi.
Akizungumza leo Juni 15,2026 jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa kituo hicho,Mkurugenzi Mkuu wa Oryx Energies Tanzania Iman Mtafya amesema mazingira bora ya uwekezaji yanayofanywa na Serikali katika sekta ya nishati ya mafuta na gesi imewezesha Oryx kuendelea kusogeza upatikanaji wa nishati hizo.
“Oryx ndio tunaongoza kwenye mtandao wa vituo vya mafuta na usambazaji wa gesi na tutaendelea kuiunga mkono serikali katika kuhamasisha matumizi ya nishati na uzinduzi wa kituo hiki ni mkakati wetu wa kuendelea kusogeza huduma zetu.
“Kwahiyo tunaendelea kuwekeza maeneo mbalimbali na tumeanza hapa Wazo na hivi karibuni tutafungua kituo kingine Dodoma ambacho kitakuwa umbali wa kilometa 40 kutoka Dodoma Mjini.Lengo ni kuonesha kama kampuni tunaendelea kuwafikia wateja kokote walipo, hata vijijini.”
Akieleza zaidi kampuni ya Oryx inajali usalama na katika kituo hicho wametumia teknolojia ya juu huku akisisitiza pia wanazingatia ubora wa bidhaa zao na Oryx ndio kampuni pekee yenye maabara ya kupima ubora wa bidhaa zao ili kuhakikishia wateja wanapoweka mafuta katika vyombo vya moto yanakuwa yamezingatia ubora.
Mtafya amesema pia kama Serikali inavyoendelea kuweka mazingira bora ya uwekezaji ndio maana unaona na wao wanaendelea kukua kwa panua huduma na sio Dar es Salaam tu bali na mikoani.
“Mazingira yaliyowekwa na Serikali kupitia Wizara ya Nishati wawekezaji tunapata msaada mkubwa wa kupanua wigo wa kusogeza huduma karibu na wananchi, katika sekta ya nishati tunaona Waziri wa Nishati anavyoendelea kuhamasisha uwekezaji katika sekta ya nishati .
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa CDT Oil na CDT Energies Boniphace Nasibu ambaye ndio msimamizi wa kituo hicho katika biashara ya mafuta,vilainishi pamoja na gesi amesema wameangalia jamii inayozunguka eneo hilo na kuona kuna kila sababu ya kusogeza huduma.
“Kituo chetu kipo karibu Madale ambako kuna mashamba ya jeshi,kiwanda cha saruji cha Wazo pamoja na watu wa eneo la Wazo na kwa ujumla tumejiridhisha hapa ni sehemu sahihi ya kuwahakikishia wananchi kupata mafuta na gesi ya kupikia.”
Amewahakikishia wateja wao watapata huduma zote zinazostahili ili wafurahie huduma za Oryx zinazopatikana huku akiishukuru oryx kwa kufanikisha uwepo wa kituo hicho.
Wakati huo huo akizungumza kwa niaba ya wananchi wa eneo la Wazo Sheikh Amani Hamis amesema kufunguliwa kwa kituo hicho mbali ya kusogeza huduma za nishati ya mafuta pamoja na gesi pia imewezesha vijana wa eneo hilo kupata ajira kupitia kituo hicho.
Amesema pia anaishukuru Serikali kwa kutoa fursa kwa wawekezaji kuja kuwekeza nchini na hivyo wawekezaji hao kuwezesha wananchi wa Watanzania kunufaika na uwekezaji huo.
Aidha, amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi wakuu wa shule za Biashara, Sayansi na Uhandisi na kuahidi kuendeleza ushirikiano wa kitaaluma kati ya Chuo cha Hong kong polytechnic na Chuo Kikuu cha Sayansi cha Nelson Mandela (NM-AIST) cha jijini Arusha nchini Tanzania.
Balozi Dkt. Haji amesema kupitia ushirikiano huo, HKPU imeonesha utayari wa kusaidia wanafunzi wa Tanzania kupata maarifa na uzoefu wa kimataifa katika maeneo ya Akili Unde (Artificial Intelligence - AI), Sayansi, Utafiti, Teknolojia na Uhandisi ambayo ndiyo nguzo muhimu za maendeleo katika dunia ya sasa pamoja na kutoa mafunzo kwa vitendo (Internship) kwa kipindi cha miezi sita hadi mwaka mmoja.
"Pamoja na mambo mengine, ushirikiano huu wa Tanzania na China katika Sekta ya Elimu, utahusisha programu maalumu za kukuza vipaji vya wanafunzi katika nyanja za Sayansi na Teknolojia, Uhandisi na Hisabati, hatua ambayo itasaidia kuandaa kizazi chenye uwezo wa kushindana katika uchumi wa maarifa na ajira za kimataifa," amesema.
Na Janeth Raphael MichuziTv - Bungeni Dodoma
Serikali imeagiza Jeshi la Polisi pamoja na Madawati ya Jinsia nchini kuchukua hatua kali dhidi ya vitendo vinavyokiuka sheria, ikiwa ni pamoja na ushoga, ukahaba na uendeshaji wa madanguro.
Agizo hilo limetolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi, alipokuwa akizungumza Bungeni, ambapo amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kusimamia utekelezaji wa Sheria ya Kanuni za Adhabu Sura ya 16, inayobainisha makosa mbalimbali ya jinai yanayohusiana na makosa ya kijinsia na uendeshaji wa biashara haramu za ngono.
Amesema vifungu vya 139 hadi 147 vya sheria hiyo vinaeleza wazi makosa yanayohusiana na vitendo hivyo, na kwamba mamlaka husika zitaendelea kuchukua hatua mara pale ushahidi wa kutosha utakapopatikana.
Aidha, Waziri Katambi ametoa onyo kwa watu wanaojihusisha na uendeshaji wa madanguro na shughuli za ukahaba, akibainisha kuwa sheria inakataza kumiliki au kunufaika na mapato yatokanayo na biashara hiyo pamoja na kushiriki kwa namna yoyote ile.
Kwa upande wake, Mbunge wa Katavi, Thomas Maganga, alihoji kauli ya Serikali kuhusu kuongezeka kwa matukio ya vitendo vya ushoga katika baadhi ya maeneo ya makazi, akidai kuwa hali hiyo imeanza kujitokeza katika baadhi ya kata na mitaa licha ya uwepo wa vyombo vya ulinzi na usalama.
Akijibu hoja hiyo, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Ayoub Mohammed Mahmoud, alieleza kuwa vitendo vya ushoga ni kosa la jinai kwa mujibu wa sheria za Tanzania, na wahusika wanapaswa kuchukuliwa hatua stahiki za kisheria.
Amesema mchakato wa kushughulikia makosa hayo unahusisha uthibitishaji wa tuhuma, uchunguzi wa kina, upelelezi wa kina wa vyombo vya dola, na hatimaye kufikishwa mahakamani kwa mujibu wa taratibu za sheria.
KATAMBI amesitiza kuwa Serikali itaendelea kuhakikisha kuwa wahalifu wote wanaobainika kutenda makosa ya jinai wanachukuliwa hatua sawa na wengine wote bila upendeleo, kwa mujibu wa sheria za nchi.
Serikali ya Tanzania imeeleza mkakati wake wa kuendeleza na kutenga Maeneo Maalum ya Uwekezaji (Special Economic Zones – SEZs) kwa lengo la kuvutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi, kupitia uboreshaji wa mazingira ya uwekezaji na miundombinu wezeshi.
Hayo yameelezwa Bungeni na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Dkt.Pius Chaya
alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Itigi, Yohana Stephen Msita, aliyehoji kuhusu hatua za Serikali katika kutenga ardhi na kulipa fidia kwa ajili ya maeneo hayo ya uwekezaji.
Dkt. Chaya amebainisha kuwa Serikali, kupitia Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA), inaendelea kutekeleza mkakati wa kitaifa wa kutambua, kutenga na kuendeleza maeneo ya kimkakati ya uwekezaji kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali za Serikali.
Taasisi hizo ni pamoja na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI pamoja na Ofisi ya Msajili wa Hazina. Ushirikiano huo unalenga kuhakikisha ardhi inapatikana kwa wakati, fidia inalipwa ipasavyo, na maeneo yanakuwa tayari kwa matumizi ya uwekezaji.
Mkakati huo unahusisha hatua muhimu zikiwemo utambuzi wa maeneo yenye fursa za kimkakati, uandaaji wa mipango kabambe ya matumizi ya ardhi, kufanya upembuzi yakinifu (feasibility studies), pamoja na kushirikisha sekta binafsi katika uendelezaji wa maeneo hayo kwa kujenga miundombinu muhimu kama barabara, maji na umeme.
Kwa mujibu wa Serikali, hadi kufikia Mei 2026, jumla ya Maeneo Maalum ya Kiuchumi 34 yamekwisha tangazwa katika maeneo mbalimbali nchini. Kati ya hayo, maeneo 16 yako chini ya usimamizi wa TISEZA, 12 yanamilikiwa na sekta binafsi, 4 yanasimamiwa na Halmashauri za Serikali za Mitaa (LGAs), na 2 yanamilikiwa na taasisi za umma.
Serikali pia imeeleza kuwa inaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha maeneo hayo yanaendelezwa na kuvutia wawekezaji, ili kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi na ajira nchini.
Aidha, imezitaka Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhakikisha zinayalinda maeneo yote yaliyotengwa kwa uwekezaji—ikiwemo yale yaliyolipiwa fidia na yale yanayosubiri malipo—ili kuzuia uvamizi na kupunguza migogoro ya ardhi.
Serikali imesisitiza kuwa ulinzi na usimamizi madhubuti wa maeneo hayo ni msingi muhimu wa mafanikio ya mkakati wa Maeneo Maalum ya Uwekezaji nchini.
SERIKALI YAFUNGUA MLANGO WA MABORESHO YA MIKOPO YA ASILIMIA 10, YAAHIDI KUONDOA VIKWAZO KWA WANANCHI
Serikali imesema itaendelea kuboresha mfumo wa utoaji wa mikopo ya asilimia 10 inayotolewa kupitia halmashauri ili kuondoa changamoto za kisheria na kiutendaji zinazowakabili wananchi wanaonufaika na mikopo hiyo.
Kauli hiyo imetolewa bungeni na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Dkt. festo Ndugange wakati akijibu swali la Mbunge wa Kinondoni, Tarimba Gulam Abbas, aliyetaka kujua kama Serikali iko tayari kutoa waraka maalumu wa kurahisisha utoaji wa mikopo kwa wananchi kutokana na changamoto zilizopo.
Dkt Ndugange amesema Serikali imeendelea kusimamia utoaji wa mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kupitia asilimia 10 ya mapato ya ndani ya halmashauri, kwa kuzingatia Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa Sura ya 290 pamoja na Kanuni zake za mwaka 2024.
Ameeleza kuwa kanuni hizo zimeweka bayana taratibu zote za usimamizi, utoaji, ukopaji na urejeshaji wa mikopo hiyo, jambo ambalo limeongeza uwazi na ufanisi katika utekelezaji wake.
Aidha, Dkt Ndugange amesema mwaka 2025 Serikali ilitoa mwongozo maalumu wa utoaji wa mikopo ya asilimia 10 kwa lengo la kuimarisha uwajibikaji, uwazi na usimamizi wa vikundi vinavyonufaika na mikopo hiyo.
Kwa mujibu wa mwongozo huo, majukumu ya kamati mbalimbali zinazoshughulikia mikopo katika ngazi za mikoa na serikali za mitaa yameainishwa wazi, ikiwemo jukumu la kuhakikisha maombi ya mikopo yanachakatwa kwa wakati na walengwa wanapata huduma kwa haraka zaidi.
Katika hatua nyingine ya kuboresha huduma, Serikali imeanzisha mfumo wa kielektroniki wa WEZESHA Portal unaolenga kurahisisha usimamizi na utoaji wa mikopo hiyo pamoja na kuongeza uwazi katika mchakato mzima.
Dkt. Ndugange amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kupokea maoni kutoka kwa wadau mbalimbali ili kufanya maboresho zaidi yatakayorahisisha upatikanaji wa mikopo na kuongeza tija kwa makundi maalumu yanayolengwa.
Hatua hizo zinatarajiwa kuongeza ufanisi wa utoaji wa mikopo, kupunguza urasimu na kuwezesha wananchi wengi zaidi kunufaika na fursa za kiuchumi zinazotolewa kupitia mikopo ya asilimia 10 ya halmashauri.

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dennis Londo, amesema wazalishaji, wafanyabiashara na watoa huduma nchini ni nguzo muhimu katika maendeleo ya uchumi kutokana na mchango wao katika uzalishaji, biashara na utoaji wa huduma mbalimbali na jitihada zao zinapaswa kutambuliwa ili kuhamasisha utendaji bora na kuongeza ushindani wenye tija.
Londo amesema hayo mwishoni mwa wiki wakati wa utambuzi wa kampuni bora 100 za chapa za Afrika zinazotengeneza bidhaa zilizoko barani humo, jijini Dar es Salaam.
Amesema serikali inatambua mchango wa Wafanyabiashara na wazalishaji, na ni njia mojawapo ya kuwapa hamasa ya kuendelea kufanya vizuri zaidi katika shughuli zao za kiuchumi.
"Mwaka huu ni wa kihistoria kutokana na kupitishwa kwa bajeti itakayoweka msingi wa utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2050, ambapo sekta binafsi inatarajiwa kuwa mhimili mkubwa wa ukuaji wa uchumi,hivyo Serikali inaitambua sekta binafsi kama mdau muhimu katika kufanikisha maendeleo ya Taifa",amesema Londo.
Katika hatua nyingine Mhe. Londo amesema Serikali ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, inaendelea kuweka mazingira rafiki kwa wawekezaji na wafanyabiashara ili kuongeza ushiriki wa Watanzania katika shughuli za uzalishaji, biashara na uchumi wa viwanda, ameeleza kuwa hatua hizo zitasaidia kuimarisha uchumi wa wananchi na kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha biashara katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika.
Kwa upande wake Mratibu wa tuzo hizo, Deogratius Kilawe, amesema kwamba lengo la kuandaliwa kwa tuzo hizo ni kutengeneza ushindani wa soko kwa bidhaa za Afrika, na kuongeza huduma bora kwa wananchi.
“Mwaka wa nne tunawatambua wazalishaji hao sasa, watu walioshiriki kuwania ni takribani 5,000 hadi kufikia mchakato wa kampuni 500, kutoka katika nchi zaidi ya saba,” amesema Kilawe.
.jpeg)



.jpeg)

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema mkataba wa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa Barabara ya Kitusha–Kinampanda–Kisana–Kisiriri umeshasainiwa, hatua inayofungua njia ya kuanza kwa utekelezaji wa mradi huo unaotarajiwa kubadilisha shughuli za usafiri na uchumi katika maeneo ya Wilaya ya Iramba.
Dkt. Mwigulu amesema hayo leo, Jumapili Juni 14, 2026, wakati akizungumza, kusikiliza na kutatua changamoto za wananchi wa Tarafa ya Kinampanda katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Chuo cha Ualimu Kinampanda, Wilaya ya Iramba mkoani Singida.
Amesema Serikali imekamilisha hatua muhimu ya upatikanaji wa fedha za mradi huo na kwamba changamoto iliyobaki sasa ni kukamilisha taratibu za kumpata mkandarasi atakayetekeleza ujenzi huo.
“Leo tunavyoongea, mkataba wa upatikanaji wa fedha umeshasainiwa. Kwa hiyo fedha si tatizo tena. Tunamshukuru sana Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa na Mwenyekiti wa Halmashauri ambao walishuhudia kusainiwa kwa mkataba huo,” amesema Dkt. Mwigulu.
Amesema barabara hiyo itaanzia Kitusha, kupita Kinampanda, Galangala, Kisana na kuunganishwa na Kisiriri kabla ya kuelekea Sibiti, hatua itakayorahisisha mawasiliano na usafirishaji wa watu na bidhaa katika ukanda huo.
Waziri Mkuu amesema mradi huo utatekelezwa kwa kiwango cha kisasa na unatarajiwa kuwa miongoni mwa barabara bora zaidi mkoani Singida.
“Barabara hii huenda ikawa moja ya barabara bora kuliko zote hapa mkoani Singida. Itakuwa ni barabara ya kisasa kweli kweli,” amesema.
Akitoa ufafanuzi wa hatua za utekelezaji wa mradi huo, Meneja wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mkoa wa Singida, Mhandisi Claver Mwinuka amesema tayari mchakato wa kumpata mshauri elekezi unaendelea na unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Juni mwaka huu.
Amesema baada ya kukamilika kwa michoro na nyaraka za zabuni, Serikali itaanza mchakato wa kumpata mkandarasi huku matarajio yakiwa ni mkandarasi huyo kupatikana ifikapo mwezi Septemba mwaka huu.
Mhandisi Mwinuka amesema barabara hiyo ina urefu wa kilometa 38.5 na itajengwa kwa upana wa mita 9.5, tofauti na barabara nyingi za TARURA ambazo hujengwa kwa upana wa mita 8.5.
Aidha, amesema barabara hiyo itakuwa na taa zaidi ya 400 pamoja na vituo vya mabasi vya kisasa vitakavyoboresha huduma za usafiri kwa wananchi.
Wakati huohuo, Dkt. Mwigulu amesema Serikali itaendelea kuimarisha huduma za afya katika Tarafa ya Kinampanda kwa kupeleka gari jipya la wagonjwa (ambulance) katika Kituo cha Afya Kinampanda ndani ya wiki moja hadi mbili.
Amesema hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za Serikali za kuboresha huduma za afya kwa wananchi kufuatia kukamilika kwa ujenzi wa Kituo cha Afya Kinampanda kupitia mpango wa Serikali wa kujenga vituo vya afya katika kila tarafa.
“Leo kama sehemu ya shukrani, nawaletea ambulance mpya. Itakuwepo hapa kituoni ili iweze kuwasaidia wananchi wa Kinampanda,” amesema.
Aidha, Dkt. Mwigulu ambaye pia ni Mbunge wa Iramba Magharibi amesema Serikali inaendelea na maandalizi ya utekelezaji wa miradi mingine ya barabara katika Wilaya ya Iramba ikiwemo Shelui–Nkongilangi–Tulya–Kidaru, Mtoa–Mtekente–Urugu–Mlandala–Sepuka pamoja na Iguguno–Nduguti–Gumanga–Sibiti ambayo ipo katika hatua mbalimbali za usanifu na maandalizi ya utekelezaji.
Dkt. Mwigulu ametoa maelekezo hayo leo, Jumapili Juni 14, 2026, wakati akizungumza, kusikiliza na kutatua changamoto za wananchi wa Tarafa ya Kiomboi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Shule ya Msingi Lulumba, Wilaya ya Iramba mkoani Singida.
Amesema amepokea taarifa kuhusu changamoto ya maji katika Mkoa wa Mwanza na tayari amemuelekeza Waziri mwenye dhamana ya maji kwenda eneo husika kusimamia upatikanaji wa suluhisho la haraka.
“Nimemtuma Waziri aende haraka Mwanza akasimamie jambo lile mpaka maji yapatikane. Sisi watu wa Singida tunataka tupate maji toka Mwanza. Simiyu tunataka tupate maji toka Mwanza. Dodoma tunataka tupate maji toka Mwanza. Tabora, wengine wameshaanza kupata maji toka Mwanza. Leo kuja kuambiwa Mwanza, pale pale lilipo Ziwa Victoria, pana shida ya maji. Hili ni jambo ambalo haliwezi kueleweka, na wala hatuwezi kulielewa,” amesema Dkt. Mwigulu.
Amesema hakuna sababu ya wananchi kuendelea kukosa huduma hiyo wakati chanzo cha maji kinajulikana na miundombinu ya mradi ipo.
“Hatutaki ngonjera za maneno. Hawa wanasema si bomba limekuwaje, hawa wanasema si umeme umekuwaje. Chanzo sisi tunajua kiko pale, hatuna shida ya chanzo cha maji, na mradi upo, na maji yapo. Haya mambo mengine ni ya ngonjera, mimi sitaki kuyasikia,” amesema.
Waziri Mkuu amewataka wataalamu wa sekta ya maji pamoja na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kufanya kazi kwa pamoja na kuhakikisha wananchi wanapata huduma hiyo kwa haraka.
“Mkuu wa Mkoa awatafute wataalamu wake, awatafute TANESCO na wataalamu wa maji. Wachimbe kiini cha tatizo na wakeshe mpaka wananchi wapate maji. Kunapopambazuka kesho nipate majawabu kwamba maji yamepatikana,” amesema.
Juni 9, 2026, Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mwanza (MWAUWASA) ilitoa taarifa kwa umma kuhusu upungufu wa huduma ya maji uliosababishwa na hitilafu za umeme zilizokuwa zikijitokeza mara kwa mara.
Wakati huohuo, Dkt. Mwigulu amesema Serikali imejipanga kuhakikisha changamoto ya upatikanaji wa maji katika Tarafa ya Kiomboi na maeneo mengine ya Wilaya ya Iramba inapata ufumbuzi wa kudumu kupitia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maji pamoja na uwekezaji mkubwa unaoendelea kufanywa katika sekta hiyo nchini.
Amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeweka kipaumbele maalum katika sekta ya maji kwa kutekeleza miradi ya kimkakati inayolenga kuongeza upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi.
“Niwahakikishie kwamba hili ni eneo ambalo Mheshimiwa Rais ameliwekea kipaumbele cha hali ya juu kwa sababu maji ni uhai, maji ni maisha. Tulihangaika kupata chanzo cha uhakika cha maji na sasa kimepatikana, hatua mbalimbali zinaendelea ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma hiyo kwa uhakika,” amesema.
Aidha, amesema Serikali inaendelea na utekelezaji wa mpango wa Gridi ya Taifa ya Maji pamoja na kuimarisha uwezo wa uchimbaji wa visima, ujenzi wa mabwawa na upimaji wa vyanzo vya maji ili kukabiliana na changamoto ya maji katika maeneo mbalimbali nchini.
Dkt. Mwigulu ambaye pia ni Mbunge wa Iramba Magharibi amesema Serikali inaendelea na usanifu wa barabara ya Kiomboi–Kisiriri–Sibiti kwa lengo la kuijenga kwa kiwango cha lami na kuboresha mawasiliano kati ya wananchi wa maeneo hayo na maeneo jirani.
Aidha, amesema usanifu wa barabara ya Kitusha–Galangala–Kisana–Kinampanda–Kisiriri umekamilika, huku Serikali ikiendelea na maandalizi ya utekelezaji wa miradi mingine ya barabara katika Wilaya ya Iramba ili kurahisisha shughuli za kijamii na kiuchumi.
Pia amesema usanifu wa daraja la kuunganisha eneo la Hospitali ya Kiomboi na maeneo ya Meli pamoja na Iguguno umekamilika na hatua zinazofuata ni kumpata mkandarasi kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa mradi huo.
Sambamba na hilo, Dkt. Mwigulu amesema Serikali inaendelea na maandalizi ya kuanzisha Chuo Kikuu katika eneo la Kiomboi baada ya eneo lililotengwa kuridhiwa na wataalamu husika.
“Hapa Kiomboi tutakuwa na Chuo Kikuu. Eneo limekaguliwa na kuridhiwa na hatua za utekelezaji zinaanza,” amesema.
Amesema pindi ujenzi wake utakapokamilika, Chuo Kikuu hicho kinatarajiwa kuanza kwa awamu ya kwanza kwa uwezo wa kuhudumia wanafunzi takribani 10,000.
Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Utawala na Rasilimali Watu Ofisi ya Waziri Mkuu,Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu Vedastina Kagombora amesema kuwa Suala la ujumuishaji sio jukumu la Sekta moja bali ni la kila Wizara kushirikiana ili kuweka mazingira rafiki katika upatikanaji wa huduma muhimu ikiwemo afya,Elimu na Miundombinu rafiki kwa watu wenye ulemavu.
Vedastina ameyasema hayo Jijini Dodoma katika kikao kilichoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu,Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu na Wawakilishi wa Madawati ya wenye ulemavu wa Wizara zote na baadhi ya Taasisi za Serikali.
Ambapo amesema kuwa umuhimu wa madawati haya ya kuleta haki,ushiriki wa watu wenye ulemavu yanayojumuisha katika mipango na Sera,Bajeti,Programu na shughuli zote za maendeleo ni za Wizara husika na sio kuyaacha yashughulikiwe na Ofisi inayoratibu masuala ya watu wenye ulemavu pekee.
"Ni muhimu kutambua kuwa ujumuishaji sio jukumu la Sekta au Wizara moja pekee bali ni wajibu na jukumu la kila Wizara na sisi wote kuendelea kushirikiana katika kuweka mazingira rafiki yanayowezesha upatikanaji wa huduma zote muhimu ikiwemo Elimu jumuishi,Huduma za Afya,Ajira,Teknolojia Saidizi,Huduma za Kijamii,Miundombinu Fikivu pamoja na ushiriki wa watu wenye ulemavu katika kutoa maamuzi yanayoweza kuwafikia watu weny Ulemavu".
Aidha Vedastina amebainisha mafanikio makubwa waliyoyapata katika kuratibu masuala ya watu wenye ulemavu kuwa pamoja na mapitio ya Sera ya watu wenye ulemavu,kuunda madawati ya watu wenye ulemavu katika Wizara mbalimbali,kupata mikopo ya Serikali na pia kutengeneza mfumo wa taarifa za watu wenye ulemavu ambapo wanasajiliwa na kupata namba ya usajili ili kuwatambua kwa urahisi mahali walipo.
Kwa upande wake Mdoka Omary ambaye ni Mtakwimu Mwandamizi kutoka Ofisi wa Taifa ya Takwimu ameeleza kuwa Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 iliendelea kutumia maswali sita kulingana na Mwongozo wa Kimataifa wa Washington Group pamoja na nyongeza ya maswali mengine ya ulemavu kutoka SHIVYAWATA ambapo Maswali yaliyoulizwa kwenye sehemu ya hali ya ulemavu, ni Ualbino, Kuona, Kusikia, Kutembea/kupanda ngazi, Kukumbuka/kufanya vitu kwa umakini, Kujihudumia, Kuwasiliana na “Aina Nyingine ya Ulemavu” ambapo Aina nyingine ya ulemavu ilijumuisha maswali ya ulemavu wa Mdomo Sungura, Kichwa Kikubwa, Mgongo Wazi; Kuumia Uti wa Mgongo; Kifafa; Mabakamabaka ya Ngozi, Mbalanga (Storiasis); Usonji (Autism); Matatizo ya Afya ya Akili; Ulemavu wa Akili; Mtu Mwenye Kimo Kifupi; Ukoma na mtu Mwenye Kibiongo.
Aidha, kwa mara ya kwanza waliuliza maswali yanayohusu chanzo cha ulemavu na iwapo mtu mwenye ulemavu anatumia kifaa saidizi, na Kwa mujibu wa Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka huo wa 2022, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilikuwa na watu wenye ulemavu 5,347,397,na kiwango cha ulemavu nchini kiliongezeka kutoka asilimia 9.3 mwaka 2012 hadi asilimia 11.2 mwaka 2022.
Naye Harun Harun ambaye ni Afisa Ustawi wa Jamii kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI,amesema kuwa Ofisi hiyo kupitia sektretarieti za Mikoa na Halmashauri kuna Mikakati ambayo inafanyika ya kuwabaini watu wenye ulemavu wa kila aina na pia kutenga bajeti kwa makundi haya ambapo bajeti imekuwa ikiongezeka mwaka hadi mwaka.
Ambapo pia Ofisi hiyo imekuwa na kamati katika ngazi za Halmashauri za watu wenye ulemavu ambazo zimeundwa kwenye Mikoa yote 26 Halmashauri 184 na kata zaidi ya 3,400 ili kubaini na kutambua changamoto wanazokutana nazo watu hawa wenye ulemavu ili Maafisa Ustawi waweze kuwafikia kwa urahisi.
Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu ilikondoisha huduma za watu wenye ulemavu katika ngazi za Wizara kwa kuunda madawati ya watu wenye ulemavu mnamo mwaka 2018
Imewakutanisha Wawakilishi hao ili kuwajengea uelewa na kuwakumbusha juu majukumu yao kwa madawati hayo.
RABIA: CCM INATHAMINI JASHO LA KILA MTANZANIA.
Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Ndg. Rabia Abdalla Hamid amesema Chama cha Mapinduzi kinathamini sana jasho la kila Mtanzania.
Amesema CCM kupitia Serikali yake imejipanga kuhakikisha makundi yote ya kijamii yanagusa na kufikiwa kwa namna moja ama nyingine, ili yaweze kushirikishwa kikamilifu katika shughuli za kujiletea maendeleo.
Akizungumza Juni 14, 2026 mkoani Lindi alipokutana na makundi mbalimbali ya kijamii wakiwemo wakulima, wavuvi, wafugaji, vyama vya ushirika, baba lishe na mama lishe, maafisa usafirishaji, wajane, watu wenye mahitaji maalum, viongozi wa serikali za mitaa, viongozi wastaafu pamoja na vikundi mbalimbali vya ujasiriamali.
“Ndugu zangu Wanalindi, CCM inatambua jasho lenu katika kujitafutia mali kupitia shughuli zenu mbalimbali kama kilimo, biashara na ujasiriamali, Serikali ya CCM itaendelea kuweka mazingira wezeshi ili mnufaike na shughuli zenu”.
Aidha, ameyaomba makundi hayo kuendelea kushirikiana na CCM kwa ukaribu zaidi, kutoa ushauri na mawazo yatakayojenga umoja na mshikamano, ili kuendelea kuisimamia Serikali kwa ukaribu zaidi.
Amesema Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amedhamiria kuacha tabasamu la kweli kwa kila Mtanzania na kwa makundi yote ya kijamii.
Amesema anahitaji kuungwa mkono na kutiwa moyo katika kuhakikisha anaendelea kuliongoza Taifa kwa kuliletea maendeleo yatakayogusa makundi yote, pia katika mapendekezo ya bajeti kuu ya serikali 2026/2027, Serikali imekusudia kutenga asilimia 15 ya mapato ya halmashauri kutoka asilimia 10 ya awali ili kuongeza wigo katika upatikanaji wa mikopo.
Katika hatua nyingine, Ndg. Rabia ameisihi Serikali ya Mkoa wa Lindi na uongozi wa Chama kutenga muda na kufanya mikutano maalum ya kuyasikiliza makundi ya kijamii.






.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)





.jpeg)


.jpeg)



.jpeg)










.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)