*Ni la kusaka Wazo bora la kiuchumi ili kuibua ubunifu wa vijana,washindi kuvuna mamilioni

Na said Mwishehe,Michuzi TV

VIJANA wenye umri kuanzia miaka 15 hadi 35 wameshauriwa kujitokeza kwa wingi kushiriki Shindano la vijana uchumi challenge lenye kauli mbiu inayosema kwamba ‘Wana tunafikiri, Taifa linasonga’.

Akizungumza leo Aprili 13,2026 jijini Dar es Salaam ,Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya Vijana Uchumi Chalenji’, Joseph Malekela, ametangaza rasmi kuanza kwa shindano hilo la kupata wazo bora la kiuchumi linalolenga kuibua ubunifu wa vijana katika kukuza uchumi wa Taifa.

“Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Maendeleo ya Vijana, Dk.Joel Nanauka aliutangazia umma kuwa kutakuwa nashindano maalum na kwamba ameunda kamati ya kusimamiashindano hilo. Siku ya leo tunakuja kwenu tukiwa na maelezo ya kina kuhusu shindano la vijana uchumi challenge.”

Amesema kwa kutambua ongezeko la changamoto mbalimbali duniani ikiwemo vita, majanga ya kimataifa na ushindani wa kiuchumi, na kwa kuzingatia kwamba nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania zinaweza kuathirika moja kwa moja kutokana na madhara ya changamoto za kimataifa, Ofisi ya Rais - Maendeleo ya Vijana imeamua kuja na Shindano la Vijana Uchumi Challenge.

“Shindano hili linalenga kukuza Mawazo ya vijana, yenye ubunifu, yanayotekelezeka na endelevu katika kulinda na KukuzaUchumi wa Taifa letu dhidi ya athari za misukosuko yakimataifa.

“Ni shindano ambalo linakaribisha ushiriki wa kijana yeyote wa kitanzania mwenye umri kati ya miaka 15 – 35. Ili kushiriki, kijana mmoja mmoja anakaribishwa kuwasilisha wazo lake, kwanjia ya maandishi yasiyozidi maneno 300 au kwa njia ya video isiyozidi dakika 3 kupitia kiunganishi: bit.ly/VijanaUchumiChallenge2026\ kabla ya Aprili 30,2026.

Malekela amesema wazo linalowasilishwa ni sharti likidhi vigezo ambavyo vitatumika kupata washindi ambavyo ni Ubunifu: Kiwango cha fikra mpya na upekee wa wazo,Uelewa wa Changamoto za Kiuchumi: Kiwango cha uelewa wa mshiriki kuhusu changamoto za kiuchumi za sasa na muktadha wa kimataifa, Uhalisia: Utekelezekaji wa wazo na uwezekano wake kutekelezwa kwa vitendo.

Pia Athari kwa Uchumi: Mchango unaotarajiwa wa wazokatika kukuza uchumi wa taifa,Uwezo wa Kuleta fursa: Uwezo wa wazo kuzalisha nakuongeza fursa za ajira kwa vijana, Uendelevu: Uwezo wa wazo kudumu na kuleta matokeochanya ya muda mrefu pamoja na Ubora wa Uwasilishaji: Mpangilio, uwazi na urahisi wakuelewa pendekezo.

Kuhusu utaratibu utakaotumika kupata mshindi wa shindano hilo amesema kutakuwa na mchujo wa awali ambayo ni hatua ya mwanzo kabisa ambapo mawazo yote yatachambuliwa na wataalamu wa Kamati ya kitaifa ya Vijana, kisha watachagua mawazo 100 bora yawashiriki wote nchi nzima, na washiriki hao watepewataarifa moja kwa moja kupitia mawasiliano yaoyaliyowasilishwa.

Hatua ya pili ni robo fainali ambapo washiriki wote 100 kutoka nchi nzima watapata nafasi ya kukutanishwa pamoja, ili kutoa fursa ya kukutana ana kwa ana na timu ya majaji, kupata mafunzo ya kuboresha mawazo yao na kushiriki mchujo wa robo fainali utakaotoa dakika 10 kwa kila mshiriki kuwasilisha wazo lake, ambapo mawazo 30 bora yatachaguliwa kwenda hatua inayofuata.

Wakati mchujo wa nusu fainali ni kwamba washiriki waliofanikiwa kufikiahatua hii watapata nafasi ya kuboresha mawazo yao, kupata mafunzo zaidi na kushiriki mashindano ya nusu fainali, ambayo yatawapa nafasi ya dakika 10 kuwasilishakwa kina, ukubwa wa mawazo yao na kwanini yanafaakushinda. Mawazo 10 bora yatachaguliwa kuingia fainali.

“Vijana Platform ya fainali - Kitaifa: Washirika walioingia fainali watapata fursa ya kupata mafunzo ya muda mfupi ya namna bora ya kuwasilishaji wa Mawazo yao kwa umma na kuweza kuyapangilia kitaalamu.

“Washiriki wote 10 watapata nafasi ya dakika 10 kuwasilisha Mawazo yaokatika fainali ya shindano hili, litakalofanyika Mwishonimwa mezi mei, tarehe na mahali mtajulishwa. Tukio la fainali litatoa fursa kwa umma kushiriki na kujioneaubunifu wa Mawazo ya vijana wa Tanzania. “

Kuhusu zawadi za washindi amesema Mshindi wa Kwanza atapa fedha Sh. milioni 30, wa pili Sh. milioni 15 na watu Sh.milioni 5 pamoja na utambuzi wa vyeti rasmi kwawashiriki 100 bora.

Aidha, washindi 10 bora watanufaika na mentorship ili kukuza uwezo wao katika ubunifu na kuwapa fursa yakutekeleza kwa vitendo mawazo yao. Wakati washiriki 30 watakaoingia nusu fainali wataunganishwa na wadau mbalimbali wa umma na binafsi iki kutoa fursa ya kukuza uwezo wao na kuendelea kuyafanya mawazo yao yatekelezeke.

Ameongeza kuwa washiriki 100 bora wote watapata nafasi ya kutambuliwa(exposure) na jamii kwa kuwa watatambulishwa rasmi katika kurasa za shindano hilal na za wizara ili wadau wengi zaidi waweze kuona vipaji vya vijana na namna bora ya kuendeleakuwaunga mkono.

“Shindano hili ni kwa kila kijana wa Tanzania, hivyo tunawakaribisha vijana wote kushiriki kikamilifu. Pia tunawakaribisha wadau wa maendeleo ambao wangependa kuunga mkonoji tihada hizi ili kufanikisha kwa ukubwa zaidi shindano hili.”




Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo, amesema kuwa mkutano wa taasisi za ushindani barani Afrika umeleta pamoja wadau muhimu kutoka nchi mbalimbali kwa lengo la kujadili changamoto zinazoikumba sekta ya biashara. 

Amesema mkutano huo unahusisha zaidi ya nchi 37 na unalenga kuimarisha ushirikiano miongoni mwa taasisi hizo.

Akizungumza katika mkutano huo, Londo alieleza kuwa moja ya malengo makuu ni kubadilishana uzoefu na kujengeana uwezo katika kusimamia ushindani wa kibiashara.

 Aidha, amesisitiza umuhimu wa kubadilishana mbinu na mikakati ya kukabiliana na changamoto zinazofanana katika mataifa mbalimbali.

"Dunia ya sasa imekuwa kama kijiji, ambapo changamoto zinazotokea katika nchi moja huweza kuathiri nchi nyingine. Hivyo, mkutano huo ni fursa ya kujifunza na kupata suluhisho la pamoja kwa matatizo yanayoathiri biashara barani Afrika,"amesema
.
Londo amebainisha kuwa mabadiliko ya kiuchumi duniani, yakiwemo vita na kupanda kwa bei ya nishati, yameleta athari kubwa katika uzalishaji na usafirishaji wa bidhaa. Hali hiyo imeongeza gharama za uzalishaji na kuathiri upatikanaji wa bidhaa na huduma.

Kutokana na hali hiyo, amesema kuwa kuna hatari ya kuongezeka kwa biashara zisizo halali, ambapo baadhi ya wafanyabiashara wanaweza kupunguza gharama kwa njia zisizozingatia ubora na usalama wa bidhaa.Hiyo inaleta changamoto kubwa kwa taasisi zinazosimamia ushindani.

Amesema taasisi hizo zina jukumu la kuhakikisha walaji wanalindwa na wanapata bidhaa bora kwa bei halali. Hata hivyo, amekiri kuwa changamoto za sasa zinahitaji mbinu mpya na ushirikiano wa karibu zaidi kati ya nchi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC),Khadija  Ngasongwa amesema kuwa mkutano huo unahusisha pia wanachama binafsi zaidi ya 53 na taasisi za kikanda kama zile za Afrika Mashariki na COMESA. Lengo ni kuimarisha ushirikiano na kujenga uwezo wa pamoja.

Ameeleza kuwa kupitia jukwaa hilo, wataalamu wanapata nafasi ya kushirikiana katika masuala yenye athari za kuvuka mipaka (cross-border effects), ambapo changamoto ya nchi moja inaweza kuathiri nchi nyingine. Hivyo, ushirikiano ni muhimu katika kutatua matatizo hayo.

Kuna vikundi kazi vinavyoshughulikia maeneo mbalimbali ikiwemo utoaji wa elimu kwa walaji na uchunguzi wa vitendo vya ukiukwaji wa ushindani sokoni. Vikundi hivyI vina mchango mkubwa katika kuhakikisha soko linakuwa la haki,"amesema.

Akizungumzia kuhusu kupanda kwa bei, ameeleza kuwa si kila ongezeko husababishwa na udanganyifu wa wafanyabiashara, bali wakati mwingine hutokana na majanga ya asili au hali ya kimataifa. 

Amesema ni muhimu kufanya uchunguzi wa kina kabla ya kuchukua hatua, huku elimu kwa walaji ikiendelea kutolewa ili waweze kufanya maamuzi sahihi.

Naye Mwenyekiti wa AFC na Mkurugenzi Mtendaji wa Kamisheni ya Ushindani Mauritius,Vipin Naugah amesema

























Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Songea (SOUWASA) imekutana na Madiwani wa Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma, na kuwaeleza hali ya upatikanaji wa huduma ya maji, kutembelea na kujionea maendeleo ya mradi wa maji wa miji 28, pamoja na mikakati inayotekelezwa kuboresha huduma hiyo kwa wananchi.

SOUWASA imekutana na Madiwani hao leo Aprili 13, 2026 katika kikao kilichoandaliwa na Mamlaka hiyo, kilicholenga kuwajengea uelewa viongozi hao kuhusu utekelezaji wa majukumu ya mamlaka pamoja na mipango ya muda mfupi na mrefu ya kuimarisha upatikanaji wa maji safi na salama.

Akizungumza Mkurugenzi Mtendaji wa SOUWASA, Mhandisi Patrick Kibasa, amesema wanaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuboresha huduma ya maji, ikiwemo kuimarisha miundombinu ya uzalishaji na usambazaji pamoja na kupunguza upotevu wa maji.

Ameeleza kuwa pamoja na mafanikio yaliyopatikana, bado kuna changamoto katika baadhi ya maeneo, na juhudi zinaendelea kufanyika ili kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma ya maji safi na salama kwa uhakika.

Mhandisi Kibasa ameeleza lengo la kuwashirikisha madiwani katika ziara hiyo ni kuongeza uelewa wao kuhusu miradi ya maji ili waweze kusimamia kwa karibu na kuwasilisha kwa usahihi mahitaji na changamoto za wananchi wanaowawakilisha.

Ameongeza kuwa ushirikiano kati ya SOUWASA na viongozi wa wananchi ni muhimu katika kuhakikisha mipango na miradi ya maji inatekelezwa kwa ufanisi na kuleta matokeo chanya kwa jamii.

Kwa upande wake, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea, Abraham Egno Mbunda, amesisitiza umuhimu wa kudumisha ushirikiano na mawasiliano ya karibu kati ya madiwani na menejimenti ya SOUWASA ili kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Amesema ziara za viongozi kwenye miradi ya maendeleo ni muhimu kwa kuwa zinawapa uelewa wa moja kwa moja kuhusu utekelezaji wake na kusaidia kufanya maamuzi sahihi.

Baadhi ya madiwani wameeleza kuwa ziara hiyo imewapa uelewa mpana kuhusu mradi wa Miji 28, na matarajio, ni kuona mradi unakamilika na kuondoa changamoto ya upatikanaji wa maji, hususan katika maeneo ya pembezoni.

Kwa ujumla, Mradi wa maji wa miji 28 ni miongoni mwa miradi ya kimkakati inayotekelezwa na Serikali kwa lengo la kuboresha huduma ya maji katika maeneo ya mijini, na unatarajiwa kuchangia kuboresha hali ya upatikanaji wa huduma hiyo kwa wakazi wa Manispaa ya Songea.



Ushirikiano kati ya VETA, Enabel na kiwanda cha Kasulu Sugar umeanza kuzaa matunda baada ya vijana 36 waliokuwa wakifanya kazi bila vyeti kutathminiwa na kupatiwa vyeti kupitia mfumo wa urasimishaji wa ujuzi (RPL).

Meneja Rasilimali Watu wa Kasulu Sugar, Samweli George Aoram, amesema hayo wakati Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA Anthony Kasore, alipotembelea kiwanda hicho Aprili 9 hadi 10, 2026.

Amesema hatua hiyo imechangiwa na ushirikiano thabiti baina ya taasisi hizo, akibainisha kuwa pia wanafunzi 20 kutoka VETA Kasulu wanaendelea na mafunzo kwa vitendo kiwandani hapo huku wakichangia uzalishaji.

Aoram amesema kampuni iko tayari kuendeleza ushirikiano huo ili kupata wataalamu wenye ujuzi unaoendana na mahitaji ya kazi.

Naye Meneja wa Mradi wa Wezesha Binti kutoka taasisi ya Enabel, Christine Karungi, amesema lengo ni kuelewa mahitaji ya waajiri ili kuhakikisha mafunzo yanayotolewa yanatatua changamoto za ajira kwa vijana.

Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA Anthony Kasore, amesema ushirikiano kati ya taasisi za mafunzo na viwanda ni nguzo muhimu katika kuzalisha wahitimu wenye ujuzi unaokidhi mahitaji halisi ya soko la ajira.

Amesema ziara hiyo imelenga kujionea mahitaji ya ujuzi viwandani na kuimarisha ushirikiano utakaosaidia kuboresha mitaala ya mafunzo ili iendane na mazingira ya kazi.

Amefafanua kuwa kupitia ushirikiano huo, VETA inalenga kuandaa mitaala inayozingatia mahitaji ya waajiri pamoja na kuongeza fursa za mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi.

“Ushirikiano wa karibu na viwanda utatusaidia kuandaa wahitimu watakaoanza kazi moja kwa moja bila kuhitaji mafunzo ya ziada,” amesema.

Aidha, amesema hatua hiyo inawajengea uwezo wakufunzi kwa kuwapatia uzoefu wa teknolojia za kisasa viwandani, hali inayoongeza ufanisi wao wanaporejea kufundisha.










Top News