Serikali imeendelea kuweka nguvu katika kulinda haki na ustawi wa mnyama kazi punda kutokana na umuhimu wake kwa jamii katika kusaidia shughuli za kiuchumi na kuongeza kipato kwa wananchi.

Serikali imezitaka mamlaka zote kuhakikisha zinasimamia Sheria ya Wanyama, ikiwemo kulinda punda dhidi ya ukatili na kuwachukulia hatua za kisheria wanaovunja sheria hizo, aidha imehimiza wananchi kuhakikisha wanyama hao wanapatiwa chakula, matibabu pamoja na kutobughudhiwa.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Geita katika Maadhimisho ya Siku ya Punda Duniani yaliyofanyika kitaifa katika Mtaa wa Mgusu, Manispaa ya Geita, Mkuu wa Wilaya ya Geita, Hashimu Komba amesema baadhi ya wananchi wamekuwa wakipuuzia thamani ya punda huku wakimtendea ukatili mnyama huyo.

Maadhimisho hayo yameratibiwa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na Shirika la INADES-Formation Tanzania, ASPA pamoja na mashirika mengine kwa ufadhili wa Brooke East Africa.

Komba amesema kutoweka kwa punda kutasababisha athari kubwa katika shughuli za usafirishaji pamoja na maisha ya wananchi wanaomtegemea kwa shughuli mbalimbali za kiuchumi.

Akitoa taarifa ya shughuli zilizotekelezwa kuelekea maadhimisho hayo, Daktari wa Mifugo kutoka Taasisi ya INADES, Charles Bukula amesema zaidi ya wanyama kazi 200 wamefanyiwa matibabu huku wananchi zaidi ya 1,000 wakifikishiwa elimu kuhusu utunzaji na haki za wanyama kazi.

Kwa upande wake, Kaimu Mratibu wa Huduma za Mifugo Tanzania ambaye pia ni Mkurugenzi, Shabani Tuzzo amesisitiza umuhimu wa jamii kuendelea kushirikiana katika kuhakikisha wanyama kazi wanatunzwa na kuthaminiwa.

Naye Mkurugenzi wa Brooke East Africa amesema taasisi hiyo itaendelea kushirikiana na Serikali pamoja na wadau wengine ili kuhakikisha ustawi wa wanyama kazi unaimarishwa nchini.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Wanyama Kazi wa Kata ya Mgusu, eneo hilo lina zaidi ya wanyama kazi 800 wanaotumika katika shughuli mbalimbali za kijamii na kiuchumi huku wakazi wa maeneo hayo wakieleza namna wanavyomthamini mnyama huyo katika maisha yao ya kila siku.





 

Yahitimisha maadhimusho ya Wiki ya wazazi ngazi ya Wilaya katika kata ya Kwembe  kwa kutembelea  Wazee na kukabidhi baadhi ya mahitaji maalum. 

Viongozi na wanachama wote tunawashukuru kwa kufanikisha siku hii ki wilaya.

Malezi bora na Uzalendo ni Msingi wa Taifa
#WikiyaWazaziTanzania
#WazaziUbungo










 



Na Victor Masangu, Kibaha

Jumuiya ya wazazi ya chama cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kibaha mjini katika kusherekea miaka 48 ya maadhimisho ya wiki yao ya wazazi ngazi ya Wilaya imeamua kufanya shughulio mbali mbali za kijamii katika shule ya sekondari Bundikani ikiwemo kufanya zoezi laa upandaji wa miti ikiwa pamoja na kutoa zawadi na tuzo mbali mbali kwa walimu pamoja na wanafunzi wanaofanya vizuri katika masomo yao.

Katika sherehe za maadhinmisho hayo ambazo zilikwenda sambamba na matukio mbali mbali ya ugawaji wa zawadi kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu zilihudhuliwa na viongozi mbali mbali wa Chama pamoja na jumuiya zake ikiwemo viongozi wa serikali wakimwemo wanafunzi, walimu pamoja na wazazi na walezi.

Katibu wa Jumuiya hiyo ya wazazi Latifa Semweza amesema kwamba wameamua kutumia wiki hiyo kwa kwenda kutembelea shule ya sekondari Bundikani kwa lengo la kuweza kuwapa motisha zaidi walimu pamoja na wanafunzi kwani wamekuwa wakifanya vizuri sana katika sekta ya elimu katika Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha.

"Tupo katika sherehe za maadhimisho ya kuzaliwa kwa jumuiya yetu ya wazazi na tumetimiza miaka 48 tangu ilipozaliwa na leo hii tymeongozana na viongozi wenzangu mbali mbali n atumekuja katika shule ya Sekondari Bundikani na tumeweza kuendesha zoezi laa kupanda miti mbali mbali ikiwemo ya maatunda pamojaa na miti ya kivuli ikiwa sambamba na kutoa motisha ya zawadi kwa walimu na wanafunzi waliofanya vizuri katika masoma," amebainisha Katibu Latifa.

Kadhalika Katibu huyo amebainisha kuwa katika wiki yao ya wazazi kata zote 14 zilizopo katika Wilaya ya Kibaha mjini tayari zimeshafanya maadhimisho yao na kwamba katika ngazi ya Wilaya wao wameamua kufanya sherehe hizo katika shule ya sekondari Bundikani na lengo kubwa ni kuweza kuboresha sektya ya elimu pamoja na suala zima la upandaji wa miti ambayo itasaidia kuboresha utunzaji wa mazingira.

Katika hatua nhyingine Katibu huyo amesema kwamba katika jumuiya yao wamepewa malengo mbali mbali kwa ajili ya kuyatekeleza ikiwemo suala la kusimamia elimu kuanzia ngazi ya msingi, sekondari,pamoja na vyuo,ikiwa pamoja na kusimamia sekta ya afya, elimu pamoja na malezi.

Naye Mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi Wilaya ya Kibaha mjini Yahaya Mtonda amesema kwamba waatendelea kushirikiana bega kwa bega na walimu na wanafunzi wa shule mbali mbali za msingi na sekondari lengo kubwa ikiwa ni kuweza kuleta mabadiliko chanya ya kimaeneleo katika kuongeza kasi ya ufaulu kwa wanafunzi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi (CCM) Mwalimu Mwajuma Nyamka aliwahimiza wanafunzi wa shule hiyo ya bundikani kuweka misingi imara katika kuingeza juhudi ya kufanya vizuri katika masomo yao ikiwemo kusoma kwa bidii kwa lengo la kufanya vizurii katika mitihani yao.

Nao baadhi ya wanafunzi wanaosoma kaatika shule hiyo ya sekondari Bundikani pamoja naa walimu wao hawakusita kutoa shukrani zao za kipekee kwa Jumuiya hiyo ya wazazi kwa kuona umuhimu mkubwa wa kwenda kutimia wiki ya sherehe za maadhimisho yao kwa kuwatembelea na kuwapa motisha ya zawadi mbali mbali hali amabyo wamesema imewapa molali zaidi katika kufanya vizuri katika elimu.

Jumuiya ya wazazi inasherekea maadhimisho ya miaka 48 tangu ilipozaliwa rasmi na kauli mbiu ya mwaka huu wa 2026 ikiwa inasema kwamba malezi bora na uzalendo ni msingi wa Taifa.






 














Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi wa maeneo mbalimbali ya Jiji la Dodoma pembezoni mwa Uwanja wa Ndege wa Dodoma kabla ya kuelekea Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Mei, 2026.



MAHAKAMA ya Wilaya ya Ilala imewahukumu raia wa China XU Fuyu (39) na mfanyakazi wake wa mgahawa wa Kibonge, Blandina Mwalutola (24) wamehukumiwa kulipa faini ya Sh milioni  sita kwa kushindwa kutoa risiti ya kielektroniki, baada ya kutoa huduma ya chipsi kuku, sahani ya baga, sahani ya wali na vinywaji.

Washtakiwa hao walishtakiwa Kinyume na Kifungu cha 97(1)(b) cha Sheria ya Usimamizi wa Kodi [Sura ya 438 Toleo la 2023], kikisomwa pamoja na Vifungu vya 96 na 97 vya Sheria ya Fedha Na. 6 ya mwaka 2024.

Pia imedaiwa walikamatwa, wakati maofisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), wakiwa katika utafiti na upelelezi kuhusiana na utoaji wa risiti za kielektroniki. Ambapo imedaiwa waliagiza chakula na vinywaji ila walipewa risiti za mkono.

Hukumu hiyo, imetolewa leo Mei 8, 2026 na Hakimu Mwandamizi Mohamed Burhani, baada ya washtakiwa kukiri mashtaka mawili kushindwa kutoa risiti za kielektroniki kinyume na sheria za kodi.

Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Burhani amesema kesi kama hizo lazima adhabu zitolewe ili kuzuia makosa hayo yasitendwe na watu wengine. 

"Kwa mujibu wa sheria sitawapa adhabu ya Magereza nitawaacha huru kwa sababu mmekiri mashtaka yenu, shtaka la kwanza kila mmoja atalipa faini ya Sh milioni mbili na shtaka la pili ambalo linamkabili Fuyu peke yake atalipa Sh milioni mbili." amesema Hakimu Burhani 

Hata hivyo, Hakimu Burhani amewaeleza washtakiwa kuwa wakishindwa kulipa faini hiyo kila mmoja atatumikia kifungo cha miaka mitatu gerezani. 

Hata hivyo washtakiwa waliweza kulipa faini hiyo na kuachiwa huru.

Mapema akisoma hati ya mashtaka Wakili wa Serikali Salome Assey amedai kuwa Machi 24, 2026 katika Mtaa wa Gerezani, eneo la Kariakoo, Wilaya ya Ilala, Mkoa wa Dar es Salaam, wakiwa walitoa huduma za chakula na vinywaji katika Kampuni ya Dicos (Mgahawa wa Kibonge) na kushindwa kutoa risiti ya kielektroniki walipotoa huduma ya chakula ambayo ni sahani moja ya baga yenye thamani ya Sh.13,000.

Katika shtaka la pili, inadaiwa kuwa tarehe hiyo na mahali hapo mshtakiwa Fuyu alishindwa kutoa risiti ya kielektroniki alipotoa huduma ya chakula na vinywaji ambayo ni sahani mbili za chipsi kuku, sahani moja ya wali uliochanganywa na mayai, chupa mbili za plastiki za Coca-Cola na chupa moja ya maji ya kunywa ya Kilimanjaro, vyote vikiwa na thamani ya Shilingi 35,000.

Baada ya washtakiwa kusomewa mashtaka hayo, walikiri kutenda makosa hayo ambayo Hakimu Burhani aliutaka upande wa mashtaka kuwasomea washtakiwa maelezo ya awali (PH).

Alidai kuwa Machi 24,2026 Fuyu akiwa Meneja wa Kampuni hiyo na Mwalutola akiwa mhudumu walikuwa wanatoa huduma ya chakula na vinywaji kwa wateja na tarehe maofisa wa TRA walipewa kazi kwa ajili ya kufanya utafiti na upelelezi katika mgawaha huo kama wanatoa risiti za kielektroniki.

Ilidaiwa kuwa Ofisa wa TRA, Cecilia Lussa aliagiza sahani ya baga ambayo ilikuwa ni Sh. 13,000 na baada ya kulipa fedha alipewa risiti ya mkono, alipouliza kwa nini hajapewa risiti ya kielektroniki aliambiwa mashine haifanyi kazi ni mbovu.

"Na maofisa wengine wawili Hosea Kasiba na Kisabo Focus walifika katika mgawaha huo, wakaagiza sahani mbili za chipsi kuku, sahani moja ya wali iliyochanganywa na mayai, chupa mbili za Coca-Cola na maji ya Kilimanjaro chupa mbili jumla ilikuwa Sh 35,000, baada ya kulipa walipewa risiti ya mkono, walipouliza walielezwa kuwa mashine ni mbovu,"alidai 

Baada ya hapo walijitangaza kama wao ni maofisa wa TRA, watuhumiwa walikwenda kuripoti Idara ya Kodi kwa kosa la kushindwa kutoa risiti za kielektroniki , ambapo walikiri kutenda kosa hilo.

Hata hivyo, washtakiwa walikili maelezo hayo kuwa ni ya kweli, Mahakama ilipokea vielelezo mbalimbali vya Jamhuri ikiwemo risiti walizozitoa kwa wateja kama kielelezo namba moja.

"Baada ya kusomewa mashtaka yenu mmekiri kosa hilo na PH pia mmekiri kutokana na kukiri kwenu Mahakama inawatia hatiani kwa makosa yote. Je! Jamhuri washtakiwa wanamakosa ya nyuma?,"alisema Hakimu Burhani 

Hata hivyo, Wakili Assey alidai hawana taarifa za nyuma za washtakiwa, kwa hiyo hakimu aliwapa nafasi ya washtakiwa kujitetea kabla adhabu haijatolewa.

Fuyu ambaye ni Meneja Kampuni ya Decos Catering Ltd na Mkazi wa GSM Plaza -Gerezani amedai kuwa yeye ni bosi na pia ni mpishi kwa wakati mmoja, kwa hiyo hawezi kuona kinachoendelea kama risiti za kielektroniki zinatolewa au, ila anakubali kutenda kosa hilo.

Mshtakiwa wa pili,  Mwalutola ambaye ni Mkazi wa Temeke Mwembe Yanga alidai kuwa siku hiyo kweli mashine ilikuwa inasumbua ilikuwa ikiandika 'Illegal', lakini ilipotengemaa waliendelea kutoa risiti za kielektroniki kwa sababu ndiyo utaratibu wao ni siku hiyo tu ndiyo kulitokea changamoto. 

Wakati kesi hiyo inaendelea, Mkalimani Maria Katambo alikuwa akitafsiri kutoka lugha ya kiswahili kwenda Kichina na kichina kwenda Kiswahili kwa ajili ya mshtakiwa Fuyu.

Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), leo tarehe 7 Mei, 2026 limefanya kikao na wadau wa ujenzi wa meli jijini Mwanza kwa lengo la kuhamasisha uwekezaji katika ujenzi wa meli na vyombo vingine vya majini nchini ili kusaidia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Akizungumza wakati alipokutana na ujumbe huo, uliongozwa na Wakili Leticia Mutaki, Mkurugenzi wa Udhibiti, Ulinzi, Usalama na Utunzaji wa Mazingira ya Usafiri Majini, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Saidi Mtanda, aliipongeza TASAC kwa kuitisha kikao hicho akisema kuwa kimekuja wakati muafaka kutokana na umuhimu wa sekta ya usafiri majini katika maendeleo ya Mkoa wa Mwanza na Taifa kwa ujumla.

Mhe. Mtanda alisema Mkoa wa Mwanza upo tayari kushirikiana na TASAC katika kuhamasisha uwekezaji kwenye sekta ya ujenzi wa meli kwa kuwa Mwanza ni lango kuu la usafiri majini katika Ukanda wa Ziwa Victoria na kuwa na meli bora kutasaidia kuimarisha usalama wa usafiri majini.

Aliongeza kuwa zaidi ya asilimia 53 ya eneo la Mkoa wa Mwanza ni maji, hali inayodhihirisha umuhimu wa sekta hiyo kwa uchumi wa mkoa.

Kwa upande wake, Wakili Mutaki akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TASAC alisema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imeendelea kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji na kuhimiza maendeleo ya uchumi wa buluu pamoja na viwanda vya ndani kupitia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Wakili Mutaki aliongeza kuwa TASAC itaendelea kuhamasisha sekta binafsi kuwekeza katika ujenzi wa meli na vyombo vya majini nchini ili kupunguza utegemezi wa kuagiza vyombo hivyo kutoka nje ya nchi, hatua ambayo pia itasaidia kupunguza matumizi ya fedha za kigeni.

Wadau waliohudhuria kikao hicho ikiwemo kampuni za Songoro Marine, Ankola Shipyard Co. Ltd, na Mkombozi Marine waliishukuru TASAC kwa kuandaa kikao hicho na kueleza kuwa kimewapa fursa ya kutambua maeneo mbalimbali ya uwekezaji katika ujenzi wa meli  pamoja na umuhimu wa kushiriki katika maendeleo ya uchumi wa buluu nchini.













📌Bodi ya Nishati Vijijini (REB)  yafanya kikao na Wakandarasi wa miradi Umeme Vijijini Mkoa wa K'manjaro, Arusha

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) ikiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu, Jacob Kingu, leo tarehe 8 Mei, 2026 imefanya kikao na Wakandarasi wanaotekeleza miradi ya kupeleka umeme vijijini katika Mikoa ya Kilimanjaro na Arusha wanaosimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ili kupata taarifa ya utekelezani wa miradi hiyo.

Mwenyekiti Kingu ambaye alikuwa ameongozana na Wajumbe wa Bodi hiyo, Mhe. Balozi Radhia Msuya na Mhandisi Sophia Mgonja walikutana na Kampuni ya Ceylex Engineering Limited na Derm Group Limited na ambao wanatekeleza miradi kwa Mkoa wa Kilimanjaro na pia walikutana na Kampuni ya Ceylex Engineering Limited na Nakuroi Investment Company Limited ambazo zinatekeleza miradi kwa Mkoa wa Arusha.

Mwenyekiti Balozi Meja Jenerali Mstaafu Kingu, amewatata wakandarasi hao kutekelezea miradi hiyo ndani ya muda wa mkataba waliosaini na kuhakikisha wanazingatia ubora unaotakiwa.

Kikao hicho ambacho kilihudhuriwa pia na Mkurugenzi wa Umeme Vijijini kutoka REA, Mhandisi Jones Olotu, Meneja Msimamizi wa Miradi kutoka REA, Mhandisi Deogratius Nagu, Meneja wa Teknolojia za Nishati kutoka REA, Mhandisi Michael Kyessi, Mhandisi Miradi kutoka REA, Isaac Sanga pamoja na Mameneja wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) wa Mikoa ya Kilimanjaro na Arusha.









Top News