Viongozi wa Serikali wameshauriwa kuongeza Elimu ya utoaji na urejeshaji wa mikopo ya asilimia 10, ambayo katika bajeti ya mwaka 2026/2027 itakuwa asilimia 15.

Hayo yameelezwa leo Julai 12,2026 na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Idara ya Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Ndg Rabia Abdalla Hamid katika muendelezo wa ziara yake ya Kusikiliza na kutatua changamoto za Makundi mbalimbali ya kijamii mkoani Rukwa.

“Nitoe rai kwa Viongozi wa serikali kuhakikisha Elimu ya utoaji na urejeshaji wa mikopo ya asilimia 10,ambayo katika bajeti ya mwaka 2026/2027 itakuwa asilimia 15 inatolewa kwa kasi  ili wananchi wawe na uelewa mpana katika masuala ya fedha na walengwa waendelee kunufaika ”,amesema Ndugu Rabia.
















- Apokelewa na Mkuu wa Mkoa, Mhe. Makongoro Nyerere pamoja na Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Jacqueline Mzindakaya


Na OWM–TAMISEMI, Sumbawanga

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Silas Shemdoe, amewasili mjini Sumbawanga kwa ajili ya kumuwakilisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, katika ufunguzi wa mafunzo ya utoaji elimu kuhusu fursa za mitaji na huduma za uwezeshaji wa wananchi kiuchumi.

Mafunzo hayo yatafanyika kuanzia Julai 13 hadi 16, 2026 katika Manispaa ya Sumbawanga, yakiwa yameratibiwa na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Rukwa, Mhe. Jacqueline Mzindakaya, kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC).

Prof. Shemdoe alipokelewa katika Kiwanja cha Ndege cha Sumbawanga na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Makongoro Nyerere akiambatana na Mhe. Mhe. Jacqueline Mzindakaya pamoja na viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali.

Kesho, Julai 13, 2026, Prof. Shemdoe atafungua rasmi mafunzo hayo katika Ukumbi wa Country Hotel, ambapo yanatarajiwa kuwakutanisha wananchi, wajasiriamali, vikundi vya wanawake na vijana, makundi yenye mahitaji maalum pamoja na wadau mbalimbali wa maendeleo.

Lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea wananchi uelewa kuhusu fursa za mitaji, mikopo na huduma mbalimbali za uwezeshaji zinazotolewa na Serikali na taasisi zake, ili kuongeza ushiriki wao katika shughuli za uzalishaji, kukuza biashara, kuongeza ajira na kuinua kipato cha familia.

Mafunzo hayo pia yanatarajiwa kuwapa washiriki taarifa sahihi kuhusu namna ya kufikia huduma za kifedha na programu za uwezeshaji wa kiuchumi, hatua itakayochochea ukuaji wa uchumi wa wananchi na kuharakisha maendeleo ya mkoa wa Rukwa kwa ujumla.











Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba, amesema thamani ya fedha itaendelea kuwa imara kuelekea kipindi cha mavuno ili kuwawezesha wakulima kupata thamani stahiki ya mazao yao kulingana na shughuli za kiuchumi wanazozifanya.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) Julai 10, 2026, Tutuba amesema kiwango cha riba ya Benki Kuu cha asilimia 6.25 kinalenga kuhakikisha kunakuwa na utulivu wa bei na mfumuko wa bei unaendelea kubaki kati ya asilimia 3 hadi 5.

Amesema kiwango hicho pia kitawezesha Mabenki  kuwa na ukwasi wa kutosha kwa ajili ya utoaji wa mikopo kwa wananchi na wafanyabiashara, hivyo kusaidia shughuli mbalimbali za uzalishaji na biashara nchini.

Tutuba amesema wakulima wanapoanza kuvuna mazao yao, thamani imara ya fedha itasaidia kuhakikisha wanapata malipo yanayolingana na thamani halisi ya mazao yao sokoni.

Ameongeza kuwa wafanyabiashara wanaouza bidhaa nje ya nchi pia watanufaika kwa kupata fedha za kigeni kulingana na thamani ya fedha walizotumia katika uzalishaji, huku tathmini ikionyesha kiwango cha riba cha asilimia 6.25 kinatosha kuendelea kuimarisha shughuli za kiuchumi.

Aidha, amesema BoT hutumia Maonesho ya Sabasaba kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kiwango cha riba ya Benki Kuu katika kudhibiti mfumuko wa bei, kuongeza ukwasi katika mzunguko wa uchumi na kuwezesha upatikanaji wa fedha kwenye mabenki ya biashara.

Tutuba amesema maonesho hayo pia ni fursa kwa Watanzania kujifunza, kupata bidhaa na huduma mbalimbali pamoja na mbinu mpya za kufanya shughuli za kiuchumi zinazochangia ukuaji wa uchumi wa nchi.




Kituo cha Uzalishaji na Ukuzaji wa Viumbe Maji cha Lubambangwe kilichopo Chato Mkoa wa Geita, kimefikia asilimia 80 ya utekelezaji. Kituo hicho kiko chini ya Wizara ya Uvuvi na kinatarajiwa kuhudumia wafugaji wa samaki kutoka mikoa yote ya Kanda ya Ziwa.

Hayo yamebainishwa na Kamati ya Siasa na Utekelezaji ya CCM Mkoa wa Geita wakati wa ziara yake ya kutembelea miradi ya maendeleo wilayani hapa.

Akitoa taarifa, Kaimu Ofisa Mfawidhi wa Kituo hicho Bilali Banali amesema kituo hicho kina uwezo wa kuzalisha zaidi ya samaki laki tatu kwa mwezi pamoja na kuzalisha vyakula vya samaki.

Amesema lengo la kituo hicho ni pia kukusanya zaidi ya shilingi milioni 180 kwa mwaka kupitia utoaji wa vibali vya viranga na vizimba kwa wafugaji.

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita Waridi Mngumi amewataka wananchi kulinda kituo hicho ili kiweze kuwanufaisha kiuchumi.

Amesema kituo hicho kimejengwa kwa kuzingatia Falsafa ya Uchumi wa Buluu kwani kitatoa pia mafunzo mafupi kwa wananchi kuhusu ufugaji wa samaki na uzalishaji wake.

















Halmashauri ya Wilaya ya Geita imetoa mifuko 50 ya saruji kuwezesha ujenzi wa ghala la kisasa la kuhifadhi mazao Kata ya Bukoli.

Msaada huo umetolewa Julai 11, 2026 na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Karia Rajab Magaro wakati wa harambee iliyoongozwa na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu  TAMISEMI Dkt. Jafar Rajab Seif ukumbi wa Gwila.

Akizungumza katika harambee hiyo, Magaro amesema Halmashauri itaendelea kutoa ushauri wa kitaalamu kupitia wahandisi na maafisa kilimo ili ujenzi wa ghala hilo ufanyike kwa viwango. 

"Tutahakikisha kikundi kinasajiliwa kwa wakati. Tunawasihi msishirikishe wahandisi wa Halmashauri katika kila hatua ili mradi huu uwe na tija kwa wakulima," amesema Magaro.

Kwa upande wake Dkt. Seif ameipongeza Halmashauri ya Geita kwa kuweka mazingira wezeshi kwa vikundi vya wananchi. Amesisitiza umuhimu wa vikundi hivyo kuwa mfano wa kuigwa na vingine nchini.

"Serikali itaendelea kuwezesha vikundi kupitia mikopo iliyoidhinishwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa lengo la kuongeza ajira na kuimarisha uchumi wa wananchi," amesema Dkt. Seif.

Mwenyekiti wa Kikundi cha Amani Group Bukoli Issa Masanzu ameishukuru Serikali kwa sera na mipango inayowawezesha wananchi kushiriki katika shughuli za maendeleo.

Ghala hilo la kisasa lenye ukubwa wa mita 48 kwa 38 linatarajiwa kugharimu shilingi milioni 200. Mradi huo unalenga kuongeza uwezo wa kuhifadhi mazao, kupunguza upotevu baada ya mavuno na kuongeza kipato cha wakulima wa Bukoli na maeneo jirani.










Katika kuonesha ujirani mwema Mbunge wa Kiteto Edward Ole Lekaita na Mbunge wa Kilindi Salehe Mhando wameamua kushirikiana kuhakikisha barabara ya Lengatei- Songe inatengenezwa kwa kiwango cha changarawe na kupitika kwa mwaka mzima.

Mbali ya kushirikiana kusimamia Ujenzi wa barabara hiyo pia Wabunge hao wameshiriki shughuli ya uzinduzi wa shule ya awali na msingi Kijiji cha Lesiot Kata ya Lengatei Kiteto.
Aliyekuwa Mkuu wa Polisi Wilaya ya Ngara (OCD), William Solla, amewataka askari wanaoendelea na utumishi katika Wilaya ya Ngara, Mkoani Kagera, kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi na kujenga mahusiano mazuri na jamii wanayoihudumia.

Solla alitoa rai hiyo wakati wa sherehe ya kumuaga baada ya kumaliza rasmi utumishi wake katika Jeshi la Polisi Tanzania, Katika hafla hiyo, alitumia fursa hiyo kutoa nasaha mbalimbali kwa askari pamoja na wananchi waliohudhuria sherehe hiyo.

Aidha, aliwashukuru wananchi wa Wilaya ya Ngara kwa ushirikiano waliouonyesha kwa Jeshi la Polisi katika kipindi chote cha utumishi wake, huku akiwaomba kuendelea kutoa ushirikiano huo kwa askari wanaoendelea na majukumu ya kulinda usalama na amani Wilayani humo.

Vilevile, aliwasisitiza askari kutumia mitandao ya kijamii kwa busara na kwa kuzingatia maadili ya kazi, ili iwaletee ufanisi na majibu katika kupambana na uhalifu huku akieleza kuwa maendeleo ya sayansi na teknolojia yameifanya mitandao kuwa sehemu muhimu ya maisha ya kila siku ya wananchi.

Sambamba na hayo, aliwakumbusha askari umuhimu wa kutenga muda wao ili kufanya ibada na kumwomba Mwenyezi Mungu awaongoze, awalinde na kuwapa afya njema ili nao wafikie hatua ya kustaafu wakiwa salama na wenye afya, kama ilivyokuwa kwake.

Akihitimisha hotuba yake, Solla aliwashukuru viongozi wa Jeshi la Polisi Tanzania kwa ushirikiano waliompatia katika kipindi chote cha utumishi wake, akiwemo Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Camillus Wambura, pamoja na viongozi wa Polisi Mkoa wa Kagera.






Top News