Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Bw. Masha Mshomba, akipokea tuzo kutoka kwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Tuzo hiyo imetolewa kwa NSSF kwa kuwa miongoni mwa wadhamini wa sherehe za Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) zilizofanyika kitaifa mkoani Njombe.

Aidha, Dkt. Samia alisema: “Serikali imezindua skimu ya hifadhi ya jamii ili kuhakikisha wananchi waliojiajiri wanajumuishwa katika mfumo wa hifadhi ya jamii.”


 BY MOSES NTANDU, DAR ES SALAAM

Some villages and towns in Sudan particularly in the regions of West Darfur, South Darfur, South and North Kordofan, and Blue Nile State continue to be gripped by the sound of gunfire, which has increasingly become a common backdrop in these areas.

This harsh reality has shaken the hopes of innocent citizens striving to live normal lives and contribute to their nation’s future. Streets once filled with laughter and daily activity are now wrapped in silence, broken only by distant explosions, children’s cries, and the lingering smell of smoke after attacks.

Much of the violence has been linked to alleged actions by the Rapid Support Forces (RSF), widely accused of serious human rights violations. Reports from international organizations describe disturbing scenes civilians beaten, abused, and killed. Women and children have suffered the most, enduring unimaginable hardship and fear.

Entire villages have been burned to the ground, families torn apart, and thousands forced to flee their homes in search of safety that often remains uncertain.

In response, the Sudanese government has intensified efforts to contain the crisis. Military operations have been launched to regain control of affected areas and prevent further spread of violence. Leaders continue to express commitment to protecting civilians and restoring stability, despite the scale of the challenge.

Notable progress has been made, particularly in the capital, Khartoum, where the government has regained full control. Gradually, essential services are returning administrative activities have resumed, schools are reopening, and transport systems are being restored. Khartoum International Airport has also undergone major renovations and is now awaiting the return of international flights.

Beyond military action, the government has worked to secure vital infrastructure, including hospitals, water systems, and electricity services, to prevent further deterioration of living conditions.

At the same time, coordination with humanitarian organizations has aimed to deliver critical aid. Food, healthcare, and temporary shelter have reached many displaced people, although insecurity continues to limit access. Despite these challenges, efforts to reach vulnerable communities remain ongoing.

Diplomatically, Sudan has engaged with regional and international partners in search of a lasting solution. Calls for ceasefires and peace negotiations continue, alongside growing pressure on all parties to respect human rights and international law. The government has also pledged to investigate abuses and hold those responsible accountable.

Meanwhile, developments on the battlefield suggest a shift in momentum if availability of peace and restoring tranquility as it was before.

The Sudanese Armed Forces (SAF) are reportedly gaining ground, now controlling a significant portion of the country estimated at around 75%. Recent operations in the Kordofan region have led to the recapture of key cities previously held by the RSF.

In contrast, the RSF appears to be weakening.

Reports indicate rising internal divisions and declining leadership cohesion. A major setback came with the reported defection of senior commander Al-Nour Al-Qubba, who is said to have surrendered to the national army along with approximately 150 fully equipped combat vehicles. There are also indications that other commanders may follow.

These developments point to deeper fragmentation within the RSF. Analysts attribute this to several factors, including the structural imbalance between a formal national army and a force largely made up of irregular fighters and foreign mercenaries.

While such groups may sustain short-term operations, they often struggle in prolonged conflict against a more organized military.

Sustained pressure from the SAF has further weakened RSF positions. Continued military strikes, combined with reduced supplies and shifting regional support, have limited their operational capacity.

Additionally, the RSF appears to be losing one of its key recruitment incentives. As opportunities for looting decline, fewer fighters are drawn to the group, resulting in reduced manpower and effectiveness on the battlefield.

Taken together, these developments suggest a possible turning point in the conflict. The steady advance of the Sudanese Army, alongside the internal challenges facing the RSF, indicates a shift that may favor the restoration of central authority.

Regardlessof of the situation remains fluid and uncertain in some few areas of the few towns and villages in the country which continues to cause some suffering among civilians and communities being devastated, families displaced, and hopes for peace repeatedly shaken. Women and children remain the most affected by the ongoing humanitarian crisis cause by the RSF, but the SAF has never given up to play its role of restoring peace and tranquility.

Despite all those hardships, government efforts both military and humanitarian are showing signs of progress, particularly in strategic areas like Khartoum and other town. At the same time, the weakening of the RSF may signal a shift in the overall direction of the conflict.

Yet lasting peace will depend not only on military gains, but also on sustained humanitarian support, accountability for human rights violations, and meaningful diplomatic efforts aimed at long-term stability and reconciliation.



 


Na Mwandishi wetu- Dodoma

Mkurugenzi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Brigedia Jenerali Hosea Ndagala amewataka wataalamu ambao wamepatiwa mafunzo ya kukabiliana na maafa kuyatumia vyema katika  kuzuia, kujiandaa na kukabiliana na kurejesha hali baada ya maafa.
Ameyasema hayo jijini Dodoma wakati akifunga mafunzo ya siku nne  ya kujiandaa na kukabiliana na maafa  kwa  Kamati ya wataalamu , Timu ya kukabiliana na maafa na watumishi wa Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya dharura  (REOCC) Mkoa wa Dodoma.

Brigedia Jenerali Ndagala ameeleza kuwa Awamu ya kwanza ya utekelezaji ilianza katika Mkoa wa Mwanza na Arusha, ambapo hatua za kuanzisha Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura pamoja na kuimarisha Timu ya kukabiliana na Maafa ilianza kutekelezwa Mikoay a Mwanza na Arusha huku akiongeza kuwa mafunzo hayo yataendelea katika Mikoa yote Nchini.

Sambamba na hilo amebainisha kuwa mafunzo hayo ni  nyenzo muhimu katika kujenga na kuimarisha uwezo wa kitaalamu na kiutendaji kwa watumishi wanaohusika na uendeshaji wa kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura.
Pia ameeleza  kuwa Uanzishwaji wa kituo hicho katika Mkoa wa Dodoma ni hatua muhimu  kwani kitawezeshaufuatiliaji  wa matukio kwa ukaribu, ukusanyaji na uchambuzi wa taarifa kwa wakati, pamoja na kuimarisha mawasiliano kati ya wadau mbalimbali ndani na nje ya Mkoa wa Dodoma na Taifa kwa ujumla ili kuokoa maisha ya watu na mali zao.
Aidha Brigedia Jenerali Ndagala amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Bi. Rosemary Senyamule kwa kukubali mafunzo hayo kutolewa katika timu hizo na kuanzisha Kituo  cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura cha Mkoa ambacho kitaunganishwa na Kituo cha Taifa akisema uamuzi huo unaonyesha dhamira thabiti ya uongozi wa Mkoa wa  kuimarisha utayari, mwitikio wa haraka na uratibu madhubuti wakati wa dharura.

IDARA ya Utalii kwa kushirikiana na Kitengo cha Mawasiliano cha Wizara ya Maliasili na Utalii imesema inatarajia kuanza mchakato wa kupanga hadhi (Grading and regrading) kwa watoa huduma wa hoteli na chakula nchini.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Ijumaa Mei Mosi, 2026, na Mkurugenzi wa Idara ya Utalii Dkt. Thereza Mugobi, mchakato huo ambao ni wa kawaida ni hatua muhimu ya kujiandaa na ongezeko kubwa la wageni linalotarajiwa kuingia na kuhudumiwa nchini wakati wa michuano ya kuwania Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON-2027)

Pia amesema unalenga kuinua ubora wa huduma ili kuiwezesha Tanzania kujitangaza kimataifa kama kitovu cha utalii na ukarimu barani Afrika huku akidokeza kuwa zoezi hilo litaanza mwanzoni mwa mwezi Mei hadi Juni 2026 katika mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro na Kilimanjaro.

Zoezi hilo litahusisha ukaguzi wa kina wa miundombinu, usafi, ubora wa chakula, pamoja na huduma kwa wateja ili kuhakikisha zinakidhi viwango vya kimataifa.

Amewataka wamiliki na watoa huduma wa hoteli kutumia fursa hiyo kujipima kiwango cha ubora wa huduma huduma wanazotoa ili kuvutia na kuwahifadhi wageni kabla, wakati na baada ya AFCON-2027.

Kupitia zoezi hilo, hilo hadhi ya nyota kwa hoteli itatolewa huku likizingatia ubora wa hadhi ya nyota 5 ambapo zilizokidhi zitapandishwa hadhi na zile zisizokidhi zitashushwa hadi hiyo.




Wafanyakazi wa EWURA wakishiriki maandamano ya Mei Mosi mbele ya Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan.


...


Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) leo, Mei 1, 2026, imeungana na wafanyakazi wengine duniani kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi), maadhimisho yaliyofanyika kitaifa mkoani Njombe.

Sherehe hizo zilihudhuriwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ambaye alikuwa mgeni rasmi. Katika hotuba yake, Rais Samia amewahimiza waajiri na waajiriwa kote nchini kuendeleza ushirikiano, kuaminiana, na kutanguliza maslahi ya taifa katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuboresha mazingira na ustawi wa wafanyakazi, huku akiwataka kuongeza bidii na ufanisi kazini. Aidha, alibainisha wazi kuwa Serikali inathamini mchango wa wafanyakazi na itaendelea kuwaunga mkono katika juhudi za maendeleo ya nchi.

Katika maadhimisho hayo, EWURA imewakilishwa na wafanyakazi wake bora kutoka idara na vitengo mbalimbali. Wafanyakazi hao walichaguliwa kwa kura za wenzao kwa kuzingatia vigezo muhimu kama vile utendaji uliotukuka, nidhamu ya kazi, ubunifu pamoja na kujituma kazini.

Wawakilishi hao walishiriki katika maandamano rasmi yaliyopita mbele ya mgeni rasmi, wakibeba mabango yenye ujumbe wa kuhamasisha mshikamano na uwajibikaji kazini.

Ushiriki wao umeonesha dhamira ya EWURA kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi na kuchangia maendeleo ya taifa kwa ujumla.



Wafanyakazi wa EWURA wakishiriki maandamano ya Mei Mosi mbele ya Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwapungia mkono wafanyakazi wa EWURA, wakati wa maandamano ya Maadhimisho ya Sherehe za Meimosi leo.

Na Mwandishi Wetu.

WABUNGE wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  wameshiriki katika semina kuhusu Mpango Mkakati wa Gridi ya Maji ya Taifa.

Semina hiyo imefanyika katika ukumbi wa Bunge wa Msekwa,Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Mhandisi Mwajuma  Waziri katika mada yake amesema Gridi ya  Maji ya Taifa ni mfumo wa kimkakati wa usambazaji maji kutoka kwenye vyanzo vya uhakika na kuyapeleka katika maeneo yenye uhaba wa maji nchini.

Ameongeza hadi sasa  Wizara ya Maji imekamilisha vipande vya  mtandao wa Taifa wa maji ikiwamo kutoa maji ziwa Victoria kwenda mikoa ya Shinyanga, Tabora na Shelui katika mkoa wa Singida.

Kwa upande wake Waziri wa Maji  Jumaa Aweso akihitimisha mada amewaomba ushirikishwaji  wa jamii na  ushirikiano kwa wabunge wote ili kuhakikisha mpango mkakati wa Gridi ya Maji ya Taifa unafanikiwa ili kuhakikisha wananchi wote  wanapata huduma ya majisafi na salama na kuchochea ukuaji wa uchumi ili kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo (DIRA 2050).









Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila ameongoza mamia ya wafanyakazi Mkoani humo katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Duniani Mei Mosi yaliyofanyika kimkoa kwenye viwanja vya Mnazi mmoja na kuwataka wafanyakazi kufanya kazi kwa bidii na maarifa huku wakifanya tathmini ya matokeo ya mafanikio au tija ya utendaji wao kwenye taasisi wanazozifanyia kazi

Akizungumza kwenye maadhimisho hayo RC Chalamila amewataka wafanyakazi kutumia nguvu na maarifa yao vizuri kwenye kutekeleza wajibu wao wawapo kazini lakini pia kila mfanyakazi kutafakari mchango wake kwenye taasisi au mamlaka anayoifanyia kazi ili wanapopaza sauti zao kwa ajili ua stahiki zao utendaji wao pia uwe na tija kwenye taasisi zao

Aidha ametumia nafasi hiyo kuwapongeza waajiri wa sekta binafsi kwa kuisaidia Serikali kupunguza changamoto ya ukosefu wa ajira huku akiwataka kifuata taratibu, kanuni na sheria za kazi ili kupunguza malalamiko kutoka kwa wafanyakazi na ameweka msisitizo kwa wafanyakazi kutekeleza wajibu wao kwa ufanisi

Sanjari na hayo Mkuu wa Mkoa Mhe Albert Chalamila amewapongeza wafanyakazi Mkoani humo kwa kazi nzuri wanazozifanya huku akiendelea na msimamo wake wa kuzitaka taasisi kutoa zawadi ya pesa taslimu hadharani kwa watumishi waliofanya vyema kwenye utumishi wao

Akisoma risala ya wafanyakazi Mkoani humo kwa niaba ya katibu mkuu wa chama cha wafanyakazi Mkoa wa Dar es Salaam, Katibu wa Chama cha Walimu Mkoani humo Abraham Kamwela ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kuendelea kuboresha mazingira, haki na maslahi kwa wafanyakazi huku akiiomba serikali kuendelea kuboresha mazingira ya kazi ikiwemo kupunguza mfumuko wa bei, kupunguza msongamano wa magari, kuwezesha uwepp wa nyumba za gharama nafuu lwa wafanuakazina kuendelea kuboresha vipato vya wafanyakazi hasa ikizingatiwa changamoto ya ongezeko la gharama za maisha kwa kila nyanja

Maadhimosho hayo ya Mei Mosi yamebeba kaulimbiu isemayo "Kazi zenye Staha ni Nguzo Imara kwa Maendeleo Endelevu katika Utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050"










Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Zimbabwe umeadhimisha miaka 62 ya Muungano wa Tanzania katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Hyatt Regency Harare Zimbabwe.

Katika hafla hiyo, Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe, Kamishna wa Polisi (CP) Suzan Kaganda, alipata fursa ya kumkaribisha Fredrick Shava, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia wa Zimbabwe, aliyemwakilisha Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara za Kimataifa, Prof. Amon Murwira, aliye mwakilisha mgeni rasmi.

Akizungumza katika maadhimisho hayo yaliyobeba kauli mbiu isrmayo Miaka 62 Muungano amani umoja na Mshikamano ni Msingi wa Maendeleo endelevu, Balozi Kaganda alishukuru Serikali ya Zimbabwe, jumuiya za kidiplomasia na wadau mbalimbali kwa ushirikiano wao na Tanzania katika kukuza maendeleo huku akisisitiza kuwa Tanzania inaendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ambayo yameleta matokeo chanya.

Kwa upande wake, Waziri Shava aliipongeza Tanzania kwa kudumisha umoja na amani kwa miaka 62 ya Muungano, akieleza kuwa nchi hiyo imekuwa mfano bora katika ukanda wa SADC na Afrika kwa ujumla huku akibainisha kuwa Zimbabwe itaendelea kuthamini mchango wa Tanzania katika harakati za ukombozi na kudumisha ushirikiano wa maendeleo kati ya nchi hizo mbili.









Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Dodoma, Dkt. Neema Peter Majule, ameibua mjadala bungeni kuhusu uwazi na haki katika biashara ya kaboni, akitaka serikali kueleza mikakati iliyopo kuhakikisha wananchi wa chini, hususan wanawake na vijana, wananufaika ipasavyo.

Akizungumza Bungeni Jijini Dodoma, Dkt. Majule alitaka kujua ni viashiria gani na mfumo gani serikali imeweka kuhakikisha makisio ya mapato yanayotokana na misitu na ardhi ya wananchi yanazingatiwa kwa usahihi katika biashara hiyo inayohusisha wawekezaji.

Akijibu hoja hiyo, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Festo Dugange, alikiri kuwepo kwa changamoto za ukosefu wa uwazi katika vipimo na malipo ya biashara ya kaboni kutokana na ushirikiano kati ya wadau mbalimbali.

Dugange alieleza kuwa serikali imeanza hatua za makusudi za kuboresha mfumo huo kupitia uanzishwaji wa kituo maalum cha kuratibu biashara ya kaboni kilichopo Morogoro, ambacho kinatarajiwa kuhamishiwa Dodoma.

Alisema kituo hicho kitashirikiana na wadau na serikali kuhakikisha vipimo sahihi vya kaboni vinapatikana na wananchi wananufaika moja kwa moja kulingana na kiwango halisi cha kaboni kinachozalishwa katika maeneo yao. 




Top News