📌 Asema wajibu wa kila Mtanzania ni kuhakikisha mafanikio yanakuwa endelevu

KIZIMKAZI, ZANZIBAR

Naibu Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Bukombe, Mhe. Dkt. Doto Biteko, amesema Tanzania imepiga hatua kubwa katika utekelezaji wa Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia, huku akisisitiza kuwa ni wajibu wa kila Mtanzania kuhakikisha mafanikio yaliyopatikana yanaendelea kuwa endelevu.

Dkt. Biteko amesema hayo wakati akishiriki mjadala kuhusu “Uongozi wa Kimkakati wa Tanzania katika Kuharakisha Mabadiliko ya Nishati Endelevu na Jumuishi”, uliofanyika katika Mdahalo wa Nishati Safi ulioandaliwa na Taasisi ya Mwanamke Initiative Foundation (MIF), Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar.

Amesema uwepo wa Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia ni sehemu ya jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye ameendelea kuipa msukumo ajenda hiyo katika ngazi mbalimbali za uongozi wake na kuifikisha hadi katika majukwaa ya kimataifa.

Dkt. Biteko amesema umuhimu wa kuendelea kuipa kipaumbele ajenda hiyo unatokana na ukubwa wa athari za matumizi ya nishati isiyo safi ya kupikia, ikiwemo uharibifu wa mazingira unaosababishwa na matumizi ya kuni na mkaa, ambapo takribani hekta 470,000 za misitu hupotea kila mwaka nchini.

Aidha, amesema zaidi ya watu 33,000 hupoteza maisha kila mwaka kutokana na magonjwa yanayohusishwa na uchafuzi wa hewa wakati wa kupika, hali inayoonesha umuhimu wa kuongeza kasi ya mpito kuelekea matumizi ya nishati safi.

Ameongeza kuwa matumizi ya nishati isiyo safi yana athari za kijinsia, hususan kwa wanawake ambao hutumia muda mwingi kutafuta kuni badala ya kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji na maendeleo ya kiuchumi.

Amesema athari hizo pia zinawagusa watoto, ambapo baadhi yao hukosa muda wa kutosha wa kuhudhuria masomo kutokana na kulazimika kusaidia familia zao kutafuta kuni kwa ajili ya kupikia.

Katika mjadala huo, Dkt. Biteko amesisitiza umuhimu wa kufanya tathmini za mara kwa mara ili kubaini kiwango cha uendelevu wa matumizi ya nishati safi ya kupikia, hususan baada ya wananchi kuwezeshwa kupata teknolojia na miundombinu husika.

Amesema tathmini hizo zitasaidia Serikali na wadau kubaini changamoto zilizopo, kupima matokeo yaliyofikiwa na kuweka mikakati madhubuti zaidi ya kuendeleza matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini.

Pia, Dkt. Biteko ameipongeza Taasisi ya Mwanamke Initiative Foundation (MIF) kwa kuwa miongoni mwa taasisi zinazochangia utekelezaji wa Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia kupitia shughuli mbalimbali, ikiwemo kusaidia upatikanaji wa miundombinu pamoja na kuendesha midahalo inayowakutanisha wadau kujadili namna bora ya kuharakisha matumizi ya nishati safi, salama na endelevu nchini.


NA: MWANDISHI WETU

Kodi ni chanzo muhimu cha mapato kinachoiwezesha serikali kufanikisha mipango na mikakati yake ya kimaendeleo kwa wananchi wake.

Wananchi wanahitaji huduma nzuri za kijamii kama elimu, afya, maji, umeme, barabara na masoko. Aidha, wanahitaji pia kuwezeshwa kiuchumi kwa kupatiwa mikopo nafuu ya kuwawezesha kujikwamua kiuchumi kwa kuanzisha shughuli za kibiashara na za kiujasiriamali.

Ni kwamba, mambo haya mazuri na mengine mengi, hayawezi kufanikiwa endapo serikali haitakuwa na fedha za kutekeleza miradi ya maendeleo kwa manufaa ya wananchi wao. Hapa ndipo umuhimu wa ulipaji kodi unapoonekana.

Kimsingi, pamoja na umuhimu wa ulipaji kodi kwa maendeleo, walipakodi wanazo changamoto ambazo wanahitaji kuziwasilisha serikalini kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ili ziweze kufanyiwa kazi.

Iko hivi: Ulipaji kodi unahusisha wadau wawili yaani TRA na walipakodi. Kutokana na hili, haitawezekana ulipaji kodi ukawa na ufanisi endapo walipakodi hawatatatuliwa changamoto zao kwa wakati. 

Pia, kwa upande wa TRA, hawataweza kukusanya kodi kwa uendelevu mzuri ikiwa walipakodi wao wamesongwa na changamoto lukuki.

Ndiyo maana, kwa kutambua umuhimu wa pande zote kuwa na uhusiano mzuri na kufanikisha ulipaji kodi, TRA wameamua kuitenga siku ya Alhamisi ya kila wiki, nchi nzima, katika ofisi za wilaya na mikoa, kusikiliza kero za wafanyabiashara na walipakodi kwa ujumla.

Na hapa, Meneja Elimu Kwa Mlipakodi TRA, CPA Paul Walalaze, anasema, kutokana na umuhimu wa ulipaji kodi unaozingatia utu, siku ya Alhamisi imetengwa kwa upekee kabisa, kuhakikisha walipakodi wanawasilisha changamoto zao kwa uwazi ili kupata ufafanuzi na ufumbuzi wake.

"Hatuwezi kufanikiwa ukusanyaji kodi kama walipakodi wetu wamesongwa na changamoto. TRA imetenga siku hii ya Alhamisi, wafanyabiashara watoe changamoto zao, maoni na ushauri ili azma ya kukuza maendeleo nchini kwetu ifanikiwe," amesema.

Ameongeza kuwa, "Sasa, siku ya Alhamisi imekuwa jukwaa muhimu kwa walipakodi nchini. Ni siku ambayo walipakodi wanaonana na maofisa mapato kueleza changamoto zao, kupata ufafanuzi wa masuala mbalimbali ya kikodi na kibiashara ili kuweza kufanya shughuli zao katika mazingira mazuri zaidi".

Ikumbukwe kuwa, mwelekeo wa serikali ni kujitegemea kibajeti kwa asilimia kubwa. Mwelekeo huu umejengwa katika misingi kuwa, nchi inajengwa na wananchi wenyewe. 

Pamoja na ukweli kuwa, serikali haitaacha kupokea misaada kutoka kwa wadau na wabia wa maendeleo, lakini misaada hiyo itukute tukiwa katika safari yetu ya kujisimamia na kujitegemea kibajeti kufanikisha miradi ya maendeleo na ya kimkakati.

Ukweli ni kwamba, hatutaweza kufikia dhamira hii njema, endapo walipakodi hawatatatuliwa changamoto zao, ikizingatiwa kuwa walipakodi ndiyo waliobeba hatma ya maendeleo ya nchi kupitia ulipaji kodi.

Kwa kusisitiza hili, CPA Walalaze amesema, "Ewe mlipakodi mwenye changamoto, itumie siku ya Alhamisi kuwasilisha changamoto yako ili ipatiwe ufumbuzi. Utatuzi wa kero za kikodi utawezesha ulipaji kodi kufanyika vizuri na kujenga uhusiano mzuri baina ya Mamlaka na walipakodi wao".

Kwahiyo, mlipakodi hana sababu ya kulalamika, analo jukwaa rasmi la kuwasilisha changamoto zake kwa ufumbuzi zaidi. Utatuzi wa changamoto za walipakodi, utarahisisha ulipaji kodi wa hiari na kuharakisha maendeleo ya wananchi.



Na Pamela Mollel,Arusha

Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kwa kushirikiana na Serikali ya Ujerumani kupitia GIZ imezindua awamu ya pili ya mpango wa Akili Bandia unaolenga kuwajengea uwezo wananchi kutumia teknolojia ya AI katika kutatua changamoto mbalimbali na kushiriki kikamilifu katika uchumi wa kidijitali

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Naibu Katibu Mkuu wa EAC anayesimamia Miundombinu, Uzalishaji, Jamii na Siasa, Mhe. Aguer Ariik Malueth, amesema mpango huo ni sehemu ya juhudi za Jumuiya kuwaandaa vijana, watafiti na wajasiriamali kutumia fursa zinazotokana na maendeleo ya teknolojia ya Akili Bandia

Amesema awamu hiyo inalenga kuwafikia zaidi ya wananchi 20,000 kutoka nchi wanachama wa EAC kupitia mafunzo ya AI, huku ikiweka mkazo katika kukuza vipaji, ubunifu na utafiti ili Afrika Mashariki iweze kujenga uwezo wa ndani na kushindana katika uchumi wa kidijitali duniani

Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Afrika Mashariki na Kati katika BMZ, Joachim Schmitt, amesema Ujerumani inaona umuhimu wa nchi za EAC kuwa na mwelekeo wa pamoja katika maendeleo ya teknolojia ya AI, akibainisha kuwa uwekezaji mkubwa uliofanyika barani Afrika bado haujasambaa kwa usawa katika nchi zote

Naye Mkurugenzi wa Uvumbuzi na Teknolojia wa Kundi la Equity, Winnie Mangeni, amesema ushirikiano huo utatoa nafasi kwa wanafunzi, watafiti na wabunifu kutengeneza suluhisho zinazotumia AI katika sekta ya fedha na maeneo mengine yenye umuhimu kwa maisha ya wananchi wa Afrika Mashariki

Katika hatua nyingine, waandaaji wametenga Dola za Marekani 50,000 kwa ajili ya kuzisaidia timu zitakazofanya vizuri katika shindano hilo, huku mwaka huu kukiwa na kipengele maalum kinachowaalika wabunifu kutumia AI katika kusaidia kugundua, kuzuia na kukabiliana na milipuko ya magonjwa, ikiwemo Ebola

Mpango huo pia unalenga kuimarisha ufundishaji na utafiti katika vyuo vikuu, kuongeza ujuzi wa kidijitali na kusaidia nchi wanachama kujenga sera zinazofanana kuhusu matumizi ya Akili Bandia, huku ukizingatia usawa wa kijinsia na kuhakikisha teknolojia hiyo inawanufaisha wananchi kwa upana zaidi.











Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wanachama wa Chama hicho katika Maskani Kaka Kisonge, Michenzani Zanzibar, tarehe 11 Agosti, 2026.

Shamra shamra za Mapokezi ya Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, baada ya kuwasili Maskani Kaka Kisonge, Michenzani Zanzibar, tarehe 11 Agosti, 2026.






Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema Serikali itaendelea kutenga rasilimali za kutosha ili kuhakikisha skuli zote zinakuwa na miundombinu ya kisasa, walimu wenye sifa, na vifaa stahiki vya kufundishia na kujifunzia.

Makamu wa Rais amesema hayo, wakati wa hafla ya Ufunguzi wa Jengo la Dakhalia katika Skuli ya Sekondari ya Hasnuu Makame iliyopo Kibuteni Unguja, Zanzibar, ikiwa ni shamrashamra ya Tamasha la Kizimkazi (Kizimkazi Festival 2026). Amesema jitihada za Serikali katika kuimarisha miundombinu ya elimu ni endelevu ambazo zinajumuisha upatikanaji wa vifaa vya kufundishia, samani na upatikanaji wa walimu wenye sifa.

Makamu wa Rais amesema lengo la uwekezaji huo, ni kuandaa vijana wenye maarifa, ubunifu na ujuzi utakao wawezesha kujitegemea na kuchangia kikamilifu katika ujenzi wa Taifa. Amewasihi kutunza Dakhali hiyo na miundombinu mingine ya elimu kwa umakini mkubwa. Ametoa rai kwa Wananchi, Wazazi na walezi wa eneo hilo kuunga mkono jitihada za Serikali kwa kuwahimiza vijana kusoma kwa bidi na kulinda miundombinu ya elimu ya eneo hilo.

Aidha, Makamu wa Rais amesema mageuzi makubwa yaliyofanyika katika sekta ya elimu Zanzibar na Tanzania kwa ujumla yamekuwa na matokeo mengi chanya, ikiwemo kuongezeka kwa idadi ya wanafunzi wanaoandikishwa katika ngazi mbalimbali za elimu, kuimarika kwa miundombinu ya ufundishaji na ujifunzaji, ambako kumesababisha kuongezeka kwa ufaulu wa wanafunzi katika mitihani ya kitaifa.

Amesema Dakhalia hiyo iliyofunguliwa ni sehemu ya miradi lukuki inayotekelezwa Zanzibar yenye lengo la kukuza na kuendeleza sekta ya elimu na kuifanya kuwa ya mfano wa kuigwa kupitia uwekezaji mkubwa katika sekta ya elimu, na miundombinu ya kisasa kote visiwani.

Vilevile, Makamu wa Rais amesema ufunguzi wa dakhalia hiyo unakwenda kutatua moja ya changamoto kubwa iliyokuwa inawakabili wanafunzi ya kutembea umbali mrefu na kutumia muda mwingi kwenda na kurudi skuli. Pia mazingira mazuri yanayotokana na kuwepo kwa dakhalia hiyo yataongeza umakini, nidhamu, na ushirikiano wa karibu miongoni mwa wanafunzi, ambapo pia ni fursa nzuri kwa walimu kuwasimamia, kuwalea, na kuwasaidia kikamilifu katika masomo yao ya kila siku. 

Kwa upande wake Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Serikali ya Mapinduzi, Zanzibar Mhe. Lela Mussa amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, imeendelea juhudi za kuboresha elimu ikiwemo kusudio la kuondoa utaratibu wa wanafunzi kusoma katika awamu mbili yaani mchana na jioni ambao umekuwa ukiwaathiri katika elimu zingine ikiwemo masuala ya kidini.

 Amesema uwekezaji wa Serikali ya Awamu ya Nane katika elimu unajidhihirisha wazi ambapo bajeti ya elimu imetoka bilioni 256 hadi kufikia trilioni 1.1 ikiwa ni uwekezaji mkubwa wa serikali kuhakikisha inaweka mazingira wezeshi ya kutekeleza malengo endelevu ya dunia katika nyanja ya elimu.







  

Na Pamela Mollel, Arusha

Ujerumani kupitia Shirika lake la Maendeleo (GIZ) imeahidi kutoa jumla ya Euro milioni 39.8 kwa ajili ya kuimarisha biashara ya kikanda na ushirikiano wa kiuchumi katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), baada ya kukamilika kwa mazungumzo ya ushirikiano wa maendeleo kati ya pande hizo mbili

Akizungumza katika kikao na ujumbe wa Ujerumani, Katibu Mkuu wa EAC, Balozi Stephen P. Mbundi, ameipongeza Serikali ya Ujerumani kwa kuendelea kuwa mshirika muhimu wa Jumuiya hiyo, akisema mchango wake umekuwa na nafasi kubwa katika kuimarisha mchakato wa ushirikiano na maendeleo ya kikanda

Naibu Katibu Mkuu wa EAC anayesimamia Masuala ya Forodha, Biashara na Fedha, Annette Ssemuwemba, amesema msaada huo umefika wakati muhimu kwa Jumuiya hiyo ikiwa katika hatua za utekelezaji wa Mkakati wake wa Saba wa Maendeleo, unaolenga kuongeza biashara, uwekezaji na fursa za kiuchumi kwa nchi wanachama

Kwa mujibu wa Mkuu wa Kitengo cha Afrika Mashariki na Kati katika Wizara ya Shirikisho ya Ushirikiano wa Kiuchumi na Maendeleo ya Ujerumani (BMZ), Joachim Schmitt, Afrika Mashariki ni miongoni mwa maeneo yenye kasi kubwa ya ukuaji wa biashara, hali inayolifanya kuwa eneo lenye mvuto kwa wawekezaji kutoka Ujerumani na Ulaya

Schmitt amesema sehemu ya fedha hizo italenga kuongeza upatikanaji wa huduma za kifedha kwa biashara ndogo na za kati katika EAC, kupitia ushirikiano wa benki ya maendeleo ya Ujerumani na Benki ya Maendeleo ya Afrika Mashariki, huku hatua nyingine zikilenga kukuza ushiriki wa sekta binafsi na maendeleo ya mnyororo wa thamani

Aidha, washirika hao wamekubaliana kuendeleza ushirikiano katika maeneo mbalimbali yakiwemo biashara, teknolojia na mabadiliko ya kidijitali, afya, usimamizi wa maji ya mipakani, asasi za kiraia na maendeleo endelevu ya kiuchumi, kwa kushirikisha nchi wanachama, Umoja wa Ulaya, sekta binafsi na washirika wengine wa maendeleo

Katika fedha hizo, Euro milioni 4.8 zimetengwa kwa ajili ya kuimarisha maandalizi na mwitikio dhidi ya mlipuko wa Ebola kupitia mradi wa EAC/GIZ wa Support to Pandemic Preparedness in the EAC Region (PanPrep). Fedha hizo zitatumika katika mafunzo ya wahudumu wa afya, vifaa vya kujikinga, maandalizi ya upatikanaji wa chanjo na dawa, pamoja na uhamasishaji wa jamii kuhusu kinga na chanjo, kwa ushirikiano na Sekretarieti ya EAC, nchi wanachama, Africa CDC na WHO. 





Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Rhimo Nyansaho (Mb), amefanya ziara ya kikazi ya siku moja katika Shirika la Tanzania Automotive Technology Centre (TATC), maarufu kama NYUMBU, lililopo Kibaha, Mkoa wa Pwani, kwa lengo la kujionea utendaji na utekelezaji wa majukumu yake.

Katika ziara hiyo, alitembelea maeneo mbalimbali ya shirika hilo linalomilikiwa na JWTZ na kuzungumza na uongozi wake ukiongozwa na Mwenyekiti, Luteni Jenerali na Balozi mstaafu Paul Meela. Dkt. Nyansaho aliupongeza uongozi wa NYUMBU kwa kazi zinazofanyika na kusisitiza shirika hilo liendelee kuongeza mchango wake katika uchumi, maendeleo ya teknolojia na ustawi wa Taifa.

TATC (NYUMBU) ni shirika la umma chini ya Wizara ya Ulinzi na JKT linalojihusisha na utengenezaji, ukarabati na ubunifu wa teknolojia katika eneo la vyombo vya moto, vipuri na vifaa vya uhandisi.






Yanga Day at Uhuru Stadium shows how SportPesa backs football beyond matchday
Yanga Day at Uhuru Stadium shows how SportPesa backs football beyond matchday

Yanga Day at Uhuru Stadium shows how SportPesa backs football beyond matchday

On Sunday, August 9, 2026 thousands of Young Africans SC supporters filled Uhuru Stadium as the club marked its 91st anniversary and introduced its squad and technical team for the 2026/27 season. The celebration combined player presentations, speeches, music and fan activities before Yanga faced Les Aigles du Congo in an international friendly. For SportPesa Tanzania, Yanga’s main sponsor since 2017, the event provided a live demonstration of how long-term football support can extend beyond branding on a match shirt.

Tickets had been offered at TZS 20,000 for Mzunguko, TZS 100,000 for VIP and TZS 300,000 for Royal seating. Outside the stadium, SportPesa set up a truck and provided a free live screening of the match. Dancers entertained supporters, while free merchandise was distributed during the match. SportPesa director Abbas Tarimba also attended to represent the sponsor and support the club, making Yanga Day a direct meeting point between the brand, the team and its supporters.

Yanga Day as a season launch

Green and yellow colours covered the stadium and surrounding areas as supporters welcomed the new squad under the theme “Mwakani Tena”. One of the most anticipated introductions was Namibia international Peter Shalulile, whose arrival has increased expectations around Yanga’s attack. The pre-match programme also gave the occasion its festival atmosphere, with DJ Ally B and artists including Chid Benz, T.I.D, Madee, Chege, Q Chilla, Mr Blue, Dogo Paten and Click Master entertaining the crowd.

Yanga Day, also known as Mwananchi Day, has evolved into a major football and entertainment event in Tanzania’s sporting calendar. The previous edition marked the club’s 90th anniversary at Benjamin Mkapa Stadium and featured a friendly against Kenya’s Bandari FC. This year’s move to Uhuru Stadium preserved the event’s central purpose: bringing the team and its supporters together before the new campaign.

The result provided an early test for the new squad

Yanga began the friendly strongly and took the lead in the 27th minute when Shalulile converted a penalty on his debut. Les Aigles responded nine minutes later through Tonny Talasi after the hosts failed to clear the danger inside their penalty area. Talasi struck again in the second half to complete the visitors’ comeback and give the Congolese side a 2–1 victory.

Coach Manqoba Mngqithi made several changes after the interval as he assessed different combinations across the squad. Although the result disappointed the home crowd, it gave the technical team an immediate view of the defensive work required before competitive football begins. The match showed why a season launch must balance celebration with an honest test of readiness.

Five consecutive titles raise expectations

Yanga entered the event as five-time consecutive league champions after a 3–0 win over JKT Tanzania secured the latest title. The club finished with 75 points, only two ahead of Simba SC, underlining how narrow the margin for another championship could be. New players must now meet the standards behind that run, while the technical team must turn the energy of the season launch into results.

The SportPesa Yanga partnership adds further significance to that challenge. The new signings must uphold the standards that produced five consecutive titles, while the technical staff must demonstrate that the club’s hunger remains strong. For supporters who closely follow Yanga’s fixtures and results, the event offered the first collective view of the team preparing to carry that pressure into the new season.

A sponsorship beyond the shirt

The partnership between Yanga SC and SportPesa began in 2017 and entered a new phase through a three-year renewal valued at TZS 21.7 billion. The agreement supports the men’s first team, the women’s team and grassroots football within the club. SportPesa also awarded a TZS 262.5 million bonus after Yanga secured its fourth consecutive league title.

These details show why sustainable sponsorship is about more than visibility. Reliable resources, technical planning and clear development pathways allow a club competing domestically and across Africa to plan effectively and invest at multiple levels. At Uhuru Stadium, the truck screening, dancers, merchandise distribution and Tarimba’s attendance made that relationship tangible for supporters, including those who followed the match from outside the venue.

“Yanga Day is more than a seasonal launch. It is a celebration of the supporters, the players and the football structure that keeps the club moving forward. Our partnership with Yanga goes beyond matchday visibility because it supports the men’s team, women’s football, grassroots development and the wider growth of Tanzanian football,” said SportPesa Tanzania Head of Marketing Tracy Humplick.

Beyond Tanzanian football opportunities

Yanga’s recent achievements show why the occasion matters beyond domestic success. The club reached the CAF Confederation Cup final and narrowly lost the title to USM Alger on the away-goals rule after a 2–2 aggregate score. That run demonstrated the continental reach Tanzanian clubs can achieve when strong performance, passionate support and stable management work together.

Yanga Day gave SportPesa Tanzania a live platform to show that football sponsorship is not only about shirt branding. It is about supporters, visibility, development and long-term club ambition. The partnership gives Yanga a foundation stretching from the men’s first team to women’s football and grassroots programmes, turning the event into a bridge between past success and the demands of a new season.

Conclusion

Yanga Day at Uhuru Stadium brought together celebration, supporter engagement and an early sporting test. The 2–1 defeat offered Yanga lessons before the new campaign, while the entertainment, free screening and merchandise distribution showed how SportPesa’s role can extend beyond shirt visibility. By supporting the senior team, women’s football, grassroots development and fan experiences, SportPesa continues to connect Yanga’s recent success with the demands of its next season.


Dodoma
JARIBIO la kwanza la Mbegu ya viazi mviringo lililotafitiwa na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) limeonesha mafanikio makubwa mkoani Dodoma katika shamba la Makamu wa Rais Mstaafu Mhe. Dkt Philip Mpango lililopo Kijiji cha Mayamaya, Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma.

Jaribio hilo lililochukua siku 104 za majaribio shambani hadi kuvuna limedhihirisha kuwa zao la viazi mviringo linaweza kustawi katika mazingira ya Mkoa wa Dodoma na kuufanya Mkoa huo kuwa na fursa mpya ya zao la chakula na biashara ambalo linaweza kuwasaidia wananchi wa mkoa huo kuondokana na umasikini.

Akiongelea kuhusu jaribio hilo na matokeo yake, Makamu wa Rais Mstaafu Mhe. Dkt. Philip Mpango, ameishukuru TARI kwa kusimamia jaribio hilo ambalo kwa mara ya kwanza limeonyesha mafanikio katika Kijiji cha Mayamaya na kuwataka wakazi wa Mkoa wa Dodoma kuchangamkia fursa ya kulima zao hilo pindi utafiti utakapokamilika.

“ Wakazi wa Dodoma sasa tuanze kuchangamkia hii fursa na TARI wako tayari kutusaidia kwa kutupatia mbegu bora zinazofaa zaidi na hii itatusaidia chakula na kipato kwa ajili ya kusaidia watoto wetu kwenda shule. Dodoma sio nusu jangwa, ni maarifa tu ya kupata na kuvuna maji kwa ajili ya kuendeleza kilimo chetu, hatuwezi kuendelea kwa kutegemea mtama, mahindi, zabibu au alizeti pekee lazima tuongeze na mazao mengine” alisema Mhe. Dkt. Mpango.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TARI, Dkt. Thomas Bwana amemshukuru Mhe. Dkt. Mpango kwa kukubali TARI kuweka jaribio la viazi mviringo katika shamba lake lililopo katika Kijiji cha Mayamaya na kueleza kuwa kwa sasa TARI imepanga kuweka majaribio ya zao hilo kwa wakulima wadogo wanaolima kwa kutegemea mvua.

Katika hatua nyingine Dkt. Bwane ameongeza kuwa TARI itaendelea na majaribio ya utafiti wa mazao katika maeneo mbalimbali nchini ili kuondoa dhana iliyojengeka ya ikolojia hii ni ya mazao Fulani pekee na kuwaomba wananchi hususan wakulima kuwakaribisha TARI kuweka majaribio ya utafiti katika mashamba yao.

Kwa mujibu wa Mtafiti Kiongozi wa zao la viazi mviringo kutoka kituo cha TARI - Uyole Dkt. Owekisha Kwigizila, mbegu hiyo mpya ya TARI ina sifa ya kukomaa kwa muda mfupi wa takribani siku 90, kustahimili ukame na baadhi ya magonjwa pamoja na kuwa na uwezo wa kuzalisha tani 35 hadi 40 kwa hekta moja.

Baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Mayamaya walioshiriki katika zoezi la uvunaji wa viazi hivyo wameonesha kustaajabishwa na kustawi kwa zao hilo katika Kijiji hicho cha Mayamaya na kueleza kuwa hiyo ni mara yao ya kwanza kuona zao hilo la viazi likilimwa na kustawi Mkoani Dodoma na kuonyesha shauku kubwa ya kujaribu kulima zao hilo katika mashamba yao,

Utafiti huo wa zao la viazi Mkoani Dodoma bado unaendelea ili kukamilisha hatua zote muhimu kabla ya mbegu hiyo kuingizwa rasmi sokoni. Mafanikio hayo yanaendelea kuthibitisha kuwa Dodoma inaweza kuzalisha mazao mbalimbali ya chakula na biashara kupitia nguvu ya utafiti, ubunifu na teknolojia za kilimo na kubadilisha maisha ya wakulima wa Mkoa wa Dodoma.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
JUMUIYA ya Khoja Shia Ithna-Asheri Mkoa wa Dar es Salaam imeandaa Kambi ya Afya na Macho pamoja na Mafunzo ya Imam Hussein (a.s), yatakayofanyika kwa Agasti 14 hadi Agasti 16 katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

Kambi hiyo inayotolewa bure inalenga kuwafikishia wananchi huduma muhimu za afya, hususan wale ambao hawana uwezo wa kuzipata kwa urahisi.

Akizungumza kuhusu kambi hiyo, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Khoja Shia Ithna-Asheri Mkoa wa Dar es Salaam, Alhaj Mohamedraza Dewji, amesema shughuli hiyo ni sehemu ya jitihada za jumuiya hiyo za kutoa huduma kwa jamii bila kujali dini, kabila wala hali ya maisha.

Amesema kambi hiyo, ambayo mwaka jana ilihudumia maelfu ya wananchi, itawakutanisha wataalamu wa afya, taasisi mbalimbali pamoja na mashirika ya tiba kutoka ndani ya Tanzania kwa lengo la kuwafikia wananchi wengi zaidi.

“Huduma hizi zitatolewa bila gharama yoyote na zinalenga kuwahudumia wananchi wote bila kujali dini, kabila au hali ya maisha,” amesema Mohamedraza.

Amesema katika kambi hiyo wananchi watapata huduma mbalimbali, zikiwemo uchunguzi wa macho, vipimo vya sukari, shinikizo la damu, uzito na urefu (BMI) pamoja na uchunguzi wa ugonjwa wa mtoto wa jicho (cataract).

Aidha, amesema wananchi wenye uhitaji watapatiwa miwani na dawa bure, huku wanawake wakipata huduma za uchunguzi wa saratani ya matiti na shingo ya kizazi kwa kushirikiana na Taasisi ya Saratani Ocean Road.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti huyo, pia kutakuwa na elimu kuhusu afya ya akili pamoja na zoezi la uchangiaji damu litakalofanyika kwa kushirikiana na Taasisi ya Damu Salama.

KUMBUKUMBU YA IMAM HUSSEIN
Mohamedraza amesema jina la kambi hiyo limechukuliwa kutoka katika historia ya Imam Hussein (a.s), mjukuu wa Mtume Muhammad (s.a.w), ambaye alifariki katika tukio la Karbala lililotokea mwaka 61 Hijria (A.H).

Amesema tukio la Karbala limeendelea kuwa kumbukumbu muhimu kwa wafuasi wa Ahlulbayt na watu wengine, likisisitiza misingi ya haki, huruma, utu na kujitolea kwa ajili ya wengine.

“Lengo ni kugeuza mafunzo ya Karbala kuwa vitendo vya huruma vinavyogusa maisha ya watu, hasa walioko pembezoni,” amesema.

Amesema utoaji wa huduma za afya bila malipo ni miongoni mwa njia zinazotumiwa na jumuiya hiyo kuhuisha mafunzo na urithi wa Imam Hussein (a.s) kwa vitendo vinavyomnufaisha mwanadamu.

Kwa mujibu wa baadhi ya washiriki wa kambi hiyo katika miaka iliyopita, shughuli hiyo imekuwa zaidi ya utoaji wa huduma za afya, kwa kuwa imekuwa pia sehemu ya kuwakutanisha watu kutoka makundi mbalimbali kwa msingi wa utu, huruma na kusaidiana.

Jumuiya ya Khoja Shia Ithna-Asheri Jamaat Mkoa wa Dar es Salaam, ikiwa miongoni mwa jamii za Waislamu wa Shia na wafuasi wa Ahlulbayt, imekuwa ikifanya shughuli mbalimbali za kijamii kwa kusaidia wagonjwa, wahitaji na makundi yenye uhitaji.

Kwa mujibu wa jumuiya hiyo, kambi hiyo ni sehemu ya kuendeleza dhamira ya kusaidia jamii kupitia matendo ya huruma na huduma za kibinadamu, huku ikisisitiza kuwa huduma hizo zinapaswa kupatikana kwa heshima na bila ubaguzi.

 


Shirika la Madini la Taifa ( STAMICO) katika muendelezo  wa kuhakikisha linaendelea kuwa kinara  katika kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi Tanzania nzima, leo tarehe 11/8/2026  imeingia mkataba mnono  wa pande tatu kati ya  STAMICO, Chuo cha Mafunzo  na taasisi ya FDH  ya kuhakikisha magereza yote ya Zanzibar  yanaanza kutumia Nishati ya Rafiki  Briquettes.

Makubaliano hayo yamefanyika katika ukumbi wa Chuo cha Mafunzo Zanzibar  na kushuhudiwa  na Kamishna  wa Magereza  Zanzibar Khamis Abdalah Khamis pamoja na  Mkurugenzi  Mtendaji  wa STAMICO  Dkt Venance  Mwasse na  Mkurugenzi  wa FDH  Bwn Michael Salali.

Akiongea katika hafla hiyo, Dkt Mwasse ameipongeza  taasisi ya FDH kwa kufanikisha kuingia makubaliano  haya ambayo yatawezesha Magereza  zote za Zanzibar  kupata Nishati hii ya Rafiki Briquettes  ambayo  inaenda kuleta afueni kwenye  gharama za Nishati kwa Magereza   lakini pia kuanza kutekeleza agenda ya Nishati Safi kwa taasisi zote zinazohudumia watu zaidi ya 100.

"Suala la Nishati Safi ni  Agenda ya Kitaifa na sisi STAMICO  tumeibeba kwa mikono miwili kuhakikisha tunatumia Nishati yetu ya Rafiki Briquettes  kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi" amesema Dkt Mwasse 

Dkt Mwasse  pia ameahidi kusaidia kuleta mafunzo na Kongamano  la  kuhamasisha  matumizi  ya Nishati Nzima kwa Watumishi wa Magereza na Wananchi wote wa Zanzibar.

Awali akiongea na kutoa salamu kutoka FDH, Bwn Salali ameahidi kuhakikisha  taasisi yake kwa kushirikiana  na STAMICO  itahakikisha Nishati hii inafika kwenye  Magereza  yote kwa wingi na inafika katika ubora unaostahili.

Naye, Kamishna Khamis ameishukuru na kuipongeza STAMICO  kwa kuhakikisha Nishati hii inafika  Zanzibar.

Ameomba pia STAMICO  iangalie kuwapa fursa hii  ya kusambaza  Nishati hii kwa wale  wafungwa ambao wamemaliza vifungo vyao ili iwe njia ya kujitengenezea Kipato  baada ya kumaliza vifungo vyao.

Kamishna ametoa rai kwa taasisi nyingine kuhakikisha ziznaanza kutumia Nishati Safi kuendana na agenda ya kitaifa ya Nishati Safi ili kulinda mazingira.

Naye, Mwenyekiti  wa Wanawake na Samia Bi Fatuma Madidi ameipongeza STAMICO  kwa juhudi za kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi na akapigia msumari kwenye suala la kuhakikisha na  taasisi yake hiyo inashiriki kikamilifu kuisambaza Nishati ya Rafiki Briquettes  katika kona zote za Tanzania.

STAMICO  imejipanga  kuhakikisha inaendelea  kuwa kinara katika kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi Tanzania Nzima.





Na Farida Saidi Morogoro

Wanafunzi 6,800 kutoka nchi tano za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) wamewasili mkoani Morogoro kushiriki Mashindano ya Michezo ya Wanafunzi wa Shule za Msingi na Sekondari ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (FEASSA) 2026, yanayotarajiwa kuanza rasmi kesho, Agosti 12, hadi Agosti 23, mwaka huu.

Mashindano hayo, yanayofanyika kwa mara ya 23 katika Jumuiya ya Afrika Mashariki na mara ya tano nchini Tanzania, yatawakutanisha wanafunzi kutoka Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Morogoro, Mkuu wa Mkoa huo, Adam Kighoma Malima, amesema Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), imejipanga kuhakikisha mkoa huo unakuwa mwenyeji bora wa mashindano hayo.

Amesema jumla ya viwanja 21 pamoja na maeneo manane ya malazi vimetengwa kwa ajili ya washiriki wa mashindano hayo.

Malima amewahakikishia washiriki kuwa ulinzi na usalama umeimarishwa vya kutosha, huku akiwataka wananchi wa Morogoro kuchangamkia fursa za kiuchumi zitakazotokana na ujio wa maelfu ya wageni.

Aidha, amewataka wakazi wa mkoa huo kuwakaribisha wageni kwa ukarimu na kutumia mashindano hayo kujenga mahusiano mazuri kati ya Tanzania na nchi nyingine wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Amesema Tanzania itawakilishwa na wanafunzi 1,510 kutoka mikoa 26 ya Tanzania Bara, ikiwa ni idadi kubwa zaidi ya washiriki kutoka nchini humo katika historia ya mashindano hayo.

Kwa upande wa Morogoro, Malima amesema mkoa huo utashiriki katika michezo 13 baada ya kufanya vizuri katika mashindano ya UMISSETA na UMITASHUMTA yaliyofanyika mkoani Iringa Juni mwaka huu.

Kwa ujumla, FEASSA 2026 itahusisha michezo 20 kwa wanafunzi wa shule za sekondari, michezo sita kwa shule za msingi na michezo minne kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum.

Malima amesema ujio wa maelfu ya washiriki na wageni unatoa fursa kubwa kwa wananchi kunufaika kiuchumi kupitia biashara, usafiri, chakula, malazi na huduma mbalimbali.

Ameongeza kuwa mashindano hayo pia yatatoa fursa ya kutangaza vivutio vya utalii vya Morogoro na Tanzania kwa ujumla kwa wageni kutoka nchi mbalimbali za Afrika Mashariki.

Ufunguzi rasmi wa mashindano hayo unatarajiwa kufanyika Agosti 16, ambapo Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi.

Mkuu huyo wa Mkoa amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kushuhudia mashindano hayo na kuwakaribisha wageni kwa ukarimu, huku akivitaka vyombo vya habari kutumia fursa hiyo kuitangaza Morogoro na Tanzania kwa ujumla.

Madaktari bingwa wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) leo, Agosti 6, 2026, wamefanikiwa kufanya upasuaji wa kwanza wa kutenganisha mapacha walioungana aina ya parasitic conjoined twins, ambapo mmoja wa mapacha hakukua kikamilifu na alikuwa akimtegemea mwenzake kwa ukuaji na uhai.

Akizungumza mara baada ya upasuaji huo, Dkt. Victor Ngotta, Bingwa wa Upasuaji wa Watoto wa MNH, amesema mafanikio hayo yanaonyesha uwezo wa hospitali kushughulikia kesi ngumu na adimu zinazohitaji utaalamu wa hali ya juu, na ni hatua muhimu katika kuendelea kuimarisha huduma za upasuaji wa kibingwa nchini.

Dkt. Ngotta amesema upasuaji huo ulihitaji maandalizi ya kina na ushirikiano wa wataalamu kutoka fani mbalimbali kutokana na hali ya kipekee ya mtoto huyo, ambaye alikuwa na pacha aliyekuwa na mikono, miguu na sehemu ya kiuno pekee huku akimtegemea mwili wa mwenzake kwa ukuaji na uhai.

Mafanikio ya upasuaji huo yanaendelea kuimarisha nafasi ya Hospitali ya Taifa Muhimbili kama kituo kinachoongoza nchini katika utoaji wa huduma za kibingwa na ubingwa bobezi.

Mtoto anaendelea vizuri na yupo chini ya uangalizi wa karibu wa madaktari









Na Mwandishi Wetu
MAMLAKA ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) na Vodacom Tanzania PLC zimesaini makubaliano ya ushirikiano yenye lengo la kuharakisha mageuzi ya kidijitali katika mfumo wa uwekezaji nchini na kuboresha huduma kwa wawekezaji wa ndani na nje ya Tanzania.

Ushirikiano huo wa miaka miwili umewekwa rasmi kupitia Mkataba wa Makubaliano (MoU) uliosainiwa jijini Dar es Salaam jana, ukilenga kutumia teknolojia katika kurahisisha huduma za uwekezaji, kuboresha mazingira ya kufanya biashara na kuimarisha Tanzania kama eneo linalovutia uwekezaji endelevu na wenye thamani kubwa.

Kupitia makubaliano hayo, Vodacom Tanzania itatoa huduma mbalimbali za teknolojia kwa TISEZA, zikiwemo mawasiliano ya kibiashara, huduma za intaneti, teknolojia ya Internet of Things (IoT) pamoja na huduma za fixed internet.

Huduma hizo zinatarajiwa kusaidia TISEZA katika utekelezaji wa jukumu lake la kukuza, kuratibu na kuwezesha uwekezaji nchini, huku zikiboresha uzoefu wa wawekezaji katika hatua mbalimbali za uwekezaji.

Mbali na huduma za kiteknolojia, taasisi hizo zitashirikiana katika kuandaa shughuli za kutangaza fursa za uwekezaji nchini, ikiwemo mikutano ya wafanyabiashara, roadshows na majukwaa ya kuwafikia na kuwahudumia wawekezaji.

Akizungumza wakati wa hafla ya kusaini makubaliano hayo leo Agosti 11, 2026, Mkurugenzi wa Biashara wa Vodacom Tanzania, Nguvu Kamando, amesema teknolojia imekuwa nyenzo muhimu katika kukuza uwekezaji, ubunifu na ushindani wa kiuchumi.

Amesema ushirikiano huo utaunganisha uwezo wa Vodacom katika teknolojia na jukumu la TISEZA la kukuza uwekezaji, kwa lengo la kujenga mazingira yaliyounganishwa zaidi, yenye ufanisi na rafiki kwa wawekezaji.

“Teknolojia imekuwa kichocheo muhimu cha uwekezaji, ubunifu na ushindani wa kiuchumi. Kupitia ushirikiano huu na TISEZA, tunaunganisha uwezo wa Vodacom katika teknolojia na dhamira ya Mamlaka ya kukuza uwekezaji,” amesema Kamando.

Amesema lengo ni kuhakikisha teknolojia inakuwa kichocheo cha uwekezaji kwa kuwezesha wafanyabiashara kupata mawasiliano na suluhisho za kidijitali zitakazowasaidia kuanzisha shughuli zao kwa haraka, kufanya kazi kwa ufanisi na kuchangia katika ukuaji wa uchumi wa Tanzania.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa TISEZA, Gilead J. Teri, amesema ushirikiano huo unaonyesha dhamira ya pamoja ya taasisi hizo katika kuboresha huduma kwa wawekezaji na kuendana na mwelekeo wa Tanzania wa kujenga uchumi unaotegemea ubunifu na teknolojia.

Amesema Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2050 inasisitiza umuhimu wa kuwa na uchumi wenye ushindani, unaoongozwa na ubunifu na unaoungwa mkono na miundombinu ya kisasa ya kidijitali pamoja na huduma bora za umma.

“Ushirikiano huu unaonyesha dhamira yetu ya pamoja ya kutumia teknolojia kuboresha uzoefu wa wawekezaji, kuimarisha uwezeshaji wa uwekezaji na kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma,” amesema Teri.

Ameongeza kuwa kadiri Tanzania inavyoendelea kuvutia uwekezaji wa kimkakati katika sekta mbalimbali, ushirikiano na Vodacom utasaidia kuiweka nchi katika nafasi nzuri zaidi ya kuwa eneo linalopendelewa kwa uwekezaji endelevu na wenye thamani kubwa.

Ushirikiano huo pia unaendana na vipaumbele vya maendeleo ya taifa vya kuimarisha ushirikiano kati ya sekta ya umma na binafsi, pamoja na kutumia teknolojia za kidijitali kuboresha mfumo wa uwekezaji nchini.

Kupitia kuboresha mawasiliano, kuchochea ubunifu wa kidijitali na kuimarisha huduma zinazolenga wawekezaji, ushirikiano huo unatarajiwa kujenga mazingira ya uwekezaji yenye ufanisi, ushindani na yanayotumia teknolojia.

Vodacom Tanzania, ambayo ni miongoni mwa kampuni zinazoongoza katika teknolojia na mawasiliano nchini, imeendelea kuwekeza katika miundombinu ya kidijitali na suluhisho za kiteknolojia kwa ajili ya biashara, taasisi na jamii.

Ushirikiano huo na TISEZA unaelezwa kuwa sehemu ya jitihada za kampuni hiyo kuunga mkono ajenda ya Tanzania ya mageuzi ya kidijitali na kujenga mazingira yanayowezesha ubunifu, uwekezaji na ukuaji endelevu wa uchumi.



Na Mwandishi Wetu.
GLOBAL Education Link (GEL) imewakabidhi nyaraka rasmi za safari wanafunzi 387 wa Kitanzania wanaotarajia kwenda kuendelea na masomo ya elimu ya juu nchini China na India, huku wakihimizwa kutumia fursa hiyo kujenga maarifa, ujuzi, teknolojia, mitandao ya kimataifa na uwezo wa kujitengenezea fursa za maisha, badala ya kulenga shahada pekee.

Ukabidhi huo umefanyika kupitia mikutano miwili maalumu iliyofanyika Agosti 10 na 11, 2026 katika Ukumbi Mkuu wa Makao Makuu ya Global Education Link, Dar es Salaam, na kuhudhuriwa na wazazi pamoja na walezi wa wanafunzi hao.

Kati ya wanafunzi hao, 198 wanaelekea China na 189 India kwa ajili ya kuanza masomo katika vyuo mbalimbali vya elimu ya juu.

Lengo la mikutano hiyo lilikuwa kuwakabidhi wanafunzi nyaraka muhimu za safari zilizokamilishwa na GEL, zikiwemo pasipoti, visa, tiketi za ndege, NOC (No Objection Certificate), cheti au kijitabu cha chanjo ya homa ya manjano (Yellow Fever Certificate) pamoja na nyaraka nyingine zinazohitajika na mamlaka husika kulingana na nchi, chuo na masharti ya safari.

Mbali na kukabidhiwa nyaraka hizo, wanafunzi pamoja na wazazi na walezi wao walipata maelekezo ya mwisho kuhusu taratibu za safari, uhamiaji, mazingira ya vyuo, makazi, bima ya afya, usalama, matumizi ya fedha, nidhamu na namna ya kukabiliana na mazingira mapya watakapofika katika nchi wanazokwenda.

Mtoa mada mkuu katika mikutano hiyo alikuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Global Education Link, Abdulmalik Mollel, akishirikiana na wawakilishi wa vyuo kutoka China na India waliotoa ufafanuzi kuhusu masomo, huduma za vyuo na maisha ya mwanafunzi wa kimataifa.

Akizungumza katika mikutano hiyo, Mollel aliwataka wanafunzi kutokwenda China na India kwa lengo la kupata cheti au shahada pekee, bali kutumia mazingira ya vyuo watakakosoma kujenga uwezo mpana utakaowasaidia baada ya kuhitimu.

Alisema kwenda kusoma nje ya nchi kunamfungulia mwanafunzi mazingira mapya yenye teknolojia, maabara, warsha, vituo vya ubunifu, wataalamu pamoja na wanafunzi kutoka mataifa mbalimbali, hivyo ni jukumu la mwanafunzi kutumia fursa hizo kwa manufaa yake na Taifa.

Aliwataka vijana hao kwenda zaidi ya masomo ya darasani kwa kutembelea maabara, warsha na vituo vya ubunifu na kujifunza kwa vitendo namna teknolojia na bidhaa mbalimbali zinavyozalishwa na kutumika katika kutatua changamoto za jamii.

Akitolea mfano mwanafunzi anayesomea Business Administration, alisema haipaswi kutosha kujifunza nadharia za usimamizi wa biashara pekee, bali anapaswa kutafuta maarifa kuhusu bidhaa, teknolojia, uzalishaji na mifumo mbalimbali ya viwanda ili aweze kuelewa kile anachoweza kukisimamia au kukigeuza kuwa biashara.




Top News