Ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Majule ameendelea kuwa sauti ya wale wanaotazama matumaini yao kupitia viongozi wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, Kwa hoja zenye mwelekeo wa maendeleo, alihoji ni lini Serikali itawekeza kikamilifu katika ujenzi wa viwanda vitakavyofungua milango ya ajira, akisisitiza kuwa mikopo midogo midogo, ingawa ni muhimu, haiwezi peke yake kubadili kwa kiwango kikubwa maisha ya watu.
Majibu ya Serikali yalieleza mwelekeo wa hatua kwa hatua kuwa baadhi ya wanufaika wa mikopo hiyo wameweza kukuza biashara zao, kurejesha mikopo na hatimaye kufikia hatua ya kupata mitaji mikubwa iliyowezesha kuanzishwa kwa viwanda vidogo, hii ni picha ya mafanikio yanayokua taratibu, lakini pia inaacha nafasi ya kujiuliza: je, kasi inaweza kuongezwa zaidi?
Katika kuonesha kuwa uongozi si kauli pekee bali ni matokeo yanayoonekana, tarehe 14 Aprili 2026, Dkt. Majule aliratibu utoaji wa mikopo ya shilingi bilioni moja kwa wanawake na vijana wajasiriamali wa Mkoa wa Dodoma kwa kushirikiana na Benki ya CRDB, Hapa ndipo nadharia inakutana na uhalisia ndoto za wajasiriamali zikipewa mtaji, na juhudi zao kupewa mwelekeo mpya wa ukuaji.
Kwenye sekta ya miundombinu, alielekeza mjadala kwenye changamoto ya mvua zinazosababisha uharibifu wa barabara Dodoma, kwa mtazamo wa mbele, aliitaka Serikali kuweka mifumo ya kudumu ya mifereji ili kulinda uwekezaji huo muhimu.
Serikali ilijibu kwa kueleza kuwa inaboresha usanifu wa barabara zote mpya ili ziwe na mifereji ya kudumu ya maji, hatua inayolenga kuongeza uimara na maisha ya miundombinu hiyo, hii inaonesha jinsi hoja zinavyoweza kuwa chachu ya maboresho ya sera na utekelezaji.
Aidha, alifuatilia kwa karibu ujenzi wa barabara ya Kongwa Junction hadi Mpwapwa na Kibakwe ni barabara ambayo kwa muda mrefu imekuwa kilio cha wananchi, swali lake lilikuwa la moja kwa moja ni lini barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami?
Majibu ya Serikali yalieleza kuwa utekelezaji wake utategemea vipaumbele vilivyopo, huku miradi yenye mikataba tayari ikipewa kipaumbele. Ni jibu linaloonesha uhalisia wa upangaji wa miradi ya kitaifa, lakini pia linatoa mwanga wa matarajio ya utekelezaji wake hapo baadaye.
Katika eneo la haki na ustawi wa jamii, tarehe 24 Aprili 2026, Dkt. Majule aligusa moyo wa wengi kwa kuzungumzia ucheleweshaji wa vyeti vya vifo kutoka RITA, Hapa hakuzungumza kwa takwimu pekee bali kwa uhalisia wa maisha ya yatima wanaokwama kielimu na wajane wanaochelewa kupata haki zao za msingi.
Alisisitiza kuwa huduma hizi hazipaswi kucheleweshwa, na akaishauri Serikali kuongeza ufanisi katika taasisi hiyo, Ingawa majibu ya kina hayakuainishwa wazi, hoja yake ilibeba uzito wa kuamsha mjadala mpana juu ya uwajibikaji wa taasisi za umma.
Katika upande wa mafanikio, aliipongeza Serikali kwa kampeni ya Mama Samia Legal Aid Campaign, akibainisha mchango wake katika kusogeza huduma za kisheria kwa wananchi wa kawaida. Lakini kama ilivyo hulka ya uongozi makini, hakusimama kwenye pongezi alipendekeza kuanzishwa kwa mfuko maalum wa kusaidia gharama za usafiri na mahitaji ya msingi kwa wananchi wanaofuatilia kesi zao, pamoja na kuhimiza kasi ya usikilizwaji wa kesi mahakamani.
Nje ya ukumbi wa Bunge, Dkt. Majule aliendelea kuishi kile anachokiamini ushiriki wake katika matukio kama Bunge Marathon umeonesha kuwa uongozi hauishii kwenye hotuba, bali unahusisha uwepo wa karibu na jamii, kuhamasisha afya, mshikamano na umoja.
Kwa ujumla, Aprili 2026 si tu mwezi wa matukio, bali ni kioo kinachoonesha aina ya uongozi unaohitajika, uongozi unaounganisha sauti za wananchi na mifumo ya maamuzi, unaosukuma majibu kutoka kwa mamlaka, na unaoweka mbele maslahi ya watu.
Dkt. Neema Peter Majule anajitokeza kama kiongozi wa aina hiyo anayesikiliza kwa makini, anauliza kwa ujasiri, na anafuatilia kwa uthabiti hadi majibu yageuke kuwa matendo ni uongozi unaoleta matumaini unaojenga kesho iliyo bora.
















.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)






.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)






.jpg)



.jpeg)
