VICTOR MASANGU,KIBAHA .
Chama cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kibaha mjini imewapongeza kwa dhati wanachama wake na wananchi kwa ujumla kwa kuweza kukipa kura nyingi za kishindo wakati wa uchaguzi mkuu uliofanyika octoba 29 mwaka 2026.
Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa chama hicho Mwalimu Mwajuma Nyamka wakati wa ziara maalumu ambayo imeanza leo rasmi katika kata ya Mbwawa yenye lengo kubwa la kuwashukuru wanachama pamoja na wanannchi.
Katika ziara hiyo ambayo imehudhuliwa na viongozi mbali mbali wa chama hicho pamoja na baadhi ya viongozi wa jumuiya ya Wazazi,pamoja na jumuiya ya umoja wa wanawake wa (UWT) Kibaha mjini wameweza kuwatembelea na kuzungumza na baadhi ya mabalozi wa matawi Kata ya Mbwawa.
Mwenyekiti Nyamka amesema kwamba pamoja na ziara hiyo kulenga kutoa shukrani pia ameanbatana na baadhi ya wataalamu kutoka Ofisi ya vizazi na vifo Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha (Rita) kwa lengo la kuwasaidia wananchi wenye changamoto ya ukosefu wa vyeti vya kuzaliwa.
"Mimi kama mwenyekiti wa chama cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kibaha mjini pamoja na viongozi wenzangu tumeanza ziara rasmi ya kuwashukuru wanachama pamoja na wananchi kwa ajili ya kutoa pongezi na shukrani kwa kukipigania chama kushi da kwa kishindo katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2026,"amesema Mwenyekiti Nyamka.
Nyamka amebainisha kwamba amefarijika sana na kitendo cha wanachama wa ccm sambamba na wananchi wote kuweza kupambana na kuchagua mafiga matatu kwa kishindo katika nafasi ya udiwani,ubunge,pamoja na kiti cha Urais.
Kadhalika amewahimiza wanachama kuendelea kushikamana kwa kishindo kuanzia ngazi za chini lengo ikiwa ni kuweza kukiimarisha chama ikiwa pamoja na kutekeleza ilani kwa vitendo.
Nao baadhi ya viongozi mbali mbali wa mashina wakizungumza kwa nyakati tofauti wamempongeza kwa dhati Mwenyekiti wa CCM Mwalimu Mwajuma Nyamka kwa kuweza kufanya ziara hiyo na kwenda kuwatembelea na kuwajulia hali zao.
Mmoja wa balozi kutoka Mbwawa shule shina namba nne Ramadhani Chuma alikishukuru chama chake kwa kuweza kuona umuhimu mkubwa wa kwenda nyumbani kwake kumtembelea kitendo ambacho kimeweza kumfariji sana.
ZIara ya Mwenyekiti wa Chama cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kibaha mjini Mwalimu Mwajuma Nyamka imeanza leo rasmi katika kata ya Mbwawa ambapo imetembelea baadhi ya viongozi wakiwemo mabalozi pamoja na kufanya mkutano wa hadhara kwa lengo la kuwashukuru wanachama na wananchi.
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeelezea mafanikio yake katika maendeleo ya miji na sekta ya makazi wakati wa Kongamano la Pili la Miji Africa (2nd African Urban Forum) linalofanyika jijini Nairobi, huku ikitoa wito kwa wawekezaji wa ndani na kimataifa kuchangamkia fursa zilizopo nchini humo.
Hayo yameelezwa jijini Nairobi na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo wakati akitoa tamko la Tanzania likielezea jitihada za Serikali katika kuchochea maendeleo endelevu ya miji na makazi, ikiwa ni pamoja na sera, mipango na mikakati inayotekelezwa kuboresha makazi na upangaji wa miji.
Amesema, Tanzania imepiga hatua kubwa katika utekelezaji wa Ajenda 2063 ya Umoja wa Africa, hasa katika maeneo ya miundombinu, upatikanaji wa nishati, utoaji wa huduma za kijamii na kuimarisha ushirikiano wa kikanda.
‘’Juhudi hizo zinaendana na mkakati wa Bara la Africa wa kuimarisha muunganiko, biashara na maendeleo jumuishi’’. amesema
Aidha, Mhe. Dkt Akwilapo alielezea pia mikakati ya serikali ya Tanzania katika kukabiliana na changamoto za ukuaji wa kasi wa miji pamoja na upungufu wa makazi, ambapo kwa sasa makazi yasiyo rasmi yanakadiriwa kufikia asilimia 67.3.
Amesema, katika kukabiliana na hali hiyo, serikali ya Tanzania inaendelea kutekeleza mageuzi ya sera, kuanzisha mifumo bunifu ya fedha, kuboresha umiliki wa ardhi pamoja na kuhamasisha uwekezaji katika makazi nafuu kupitia ushirikiano kati ya sekta ya umma na binafsi.
Waziri huyo wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi amesisitiza kuwa, serikali ya Tanzania itaendelea kutumia rasilimali zake za asili pamoja na kudumisha amani na usalama ili kuharakisha utekelezaji wa Ajenda 2063.
Kupitia Kongamano hilo, Dkt Akwilapo alieleza salamu za dhati kutoka kwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyempongeza Mhe. William Ruto pamoja na wananchi wa Jamhuri ya Kenya kwa kuandaa Kongamano hilo muhimu.
Kongamano la Pili la Miji Africa limezinduliwa rasmi April 9, 2026 na Rais wa Kenya Mhe. William Ruto na linaongozwa na kauli mbiu isemayo “Adequate Housing for All: Advancing Socio-Economic and Environmental Transformation Towards the Realization of Agenda 2063,” ikilenga kuhamasisha mijadala inayotoa fursa kwa washiriki kutoka nchi mbalimbali za Africa kubadilishana uzoefu na suluhisho bunifu katika kukabiliana na changamoto za maendeleo ya miji na makazi.

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo akisoma tamko la Tanzania katika Kongamano la Pili la Miji Africa (2nd African Urban Forum) linalofanyika jijini Nairobi nchini Kenya.


Ujumbe wa Tanzania ukiwa katika Kongamano la Pili la Miji Africa (2nd African Urban Forum) linalofanyika jijini Nairobi nchini Kenya.


Sehemu ya washiriki wa Kongamano la Pili la Miji Africa (2nd African Urban Forum) wakiwa katika kongamano hilo linalofanyika jijini Nairobi nchini Kenya. ( PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI)
Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akichangia makadirio ya mapato na matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zake kwa mwaka wa fedha 2026/27 leo Aprili 9,2026 bungeni jijini Dodoma.
...
Mbunge wa Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo, amedhamiria kuwasilisha hoja binafsi bungeni itakayolenga kuishauri Serikali kuanzisha mpango maalum wa mikataba ya ajira za muda mfupi kwa vijana ili kupunguza changamoto ya ukosefu wa ajira nchini.
Akichangia makadirio ya mapato na matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zake kwa mwaka wa fedha 2026/27 bungeni, Jafo alisema mpango huo unaweza kuwa na mfumo wa Ajira za muda (part time employment) utakaodumu kwa kipindi cha miaka mitatu mitatu hadi ifikapo mwaka 2050 ambapo vijana watapata ajira za mikataba na kujipatia uzoefu wa kazi.
Alimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kwa juhudi kubwa za kuongeza fursa za ajira kwa vijana tangu aingie madarakani, akisema serikali imefanya kazi kubwa katika kuwawezesha wananchi, lakini bado kuna haja ya kuja na mikakati mipya ya kukabiliana na wimbi la vijana wasio na ajira.
Jafo alibainisha kuwa changamoto ya ajira bado ni kubwa, huku akitoa mfano wa vijana wengi waliopo kwenye shughuli zisizo rasmi kama bodaboda, baadhi yao wakiwa na elimu ya juu ikiwemo stashahada, shahada na kuendelea. Alipendekeza mpango maalum utakaolenga wahitimu hao ili kuwapa nafasi ya kupata ajira za muda na mikataba ya miaka mitatu.
Kwa mujibu wa mapendekezo yake, kila mwaka vijana 50,000 wanaweza kuingizwa kwenye mpango huo, ambapo asilimia 20 wawe wahitimu wa stashahada na asilimia 80 wawe wahitimu wa shahada na kuendelea. Aidha, alipendekeza malipo ya kujikimu ya Shilingi 500,000 kwa wenye stashahada na Shilingi 700,000 kwa wahitimu wa shahada.
Alisema gharama ya utekelezaji wa mpango huo inakadiriwa kufikia Shilingi bilioni 396, huku akisisitiza kuwa mpango huo utasaidia kukuza ujuzi wa vijana, kuongeza uzoefu wa kazi na kupunguza tatizo la ajira nchini.
Pia alipendekeza asilimia 10 zitoke katika mapato ya ndani ya kila Halmashauri, 10 ya gawio la Serikali kutoka kwenye mashirika ya umma, na fedha zingine zitokane na kubana maeneo mengine ya matumizi ya kawaida ya serikali(Recurrent Expenditure) ili zitumike kufadhili mpango huo. Aidha, alishauri mpango huo usimamie kupitia serikali za mitaa na Taasisi za Umma ili kurahisisha upatikanaji wa ajira katika halmashauri mbalimbali na Taasisi hizo za Umma.
Jafo alisisitiza kuwa mpango huo, kama utapitishwa, utaisaidia Serikali kuongeza wigo wa ajira na kuwawezesha vijana wengi zaidi kunufaika na fursa za kiuchumi nchini.
Na Leandra Gabriel, Michuzi TV
MSIMU wa mbio za Mac D Promotions ‘ Mac D Marathon’ kwa mwaka 2026 unatarajiwa kufanyika Julai 4 mwaka huu katika viwanja vya Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC,) Kwa kauli mbiu ya ‘Go Green With Gas’ yenye kulenga kuhamasisha matumizi ya nishati safi na kutunza misitu.
Akizungumza katika uzinduzi wa mbio hizo uliofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Mipango na Biashara wa Mac D Promotions Denzel Rweyunga amesema kuwa mbio hizo ambazo usajili wake umeanza rasmi leo zinatarajiwa kushirikisha wakimbiaji wa Kilomita 5, 10 na 21 pamoja na mbio za watoto za Kilomita 2.
Amesema kuwa licha ya kuhamasisha utunzaji wa afya kwa kukimbia mbio hizo pia zimelenga kuunga mkono juhudi za Serikali katika kutunza mazingira kwa kuhamasisha matumizi ya nishati safi.
“Tunategemea kuwa na washiriki 3500 katika mbio hizi na maandalizi yameanza mapema ili kuzipa hadhi na viwango vya juu, na tayari usajili umefunguliwa kupitia www.macdmarathon.com na baada ya kujisajili na kufanya malipo kupitia simu au benki washiriki wataweza kupata vifaa zikiwemo tisheti katika vituo mbalimbali vilivyoainishwa.” Amesema.
Akifafanua kuhusu huduma muhimu katika mbio hizo amesema; wamejipanga kwa kuwa na huduma ya kwanza, vituo vya maji safi na salama ya kunywa ya Kilimanjaro, matunda pamoja na ulinzi na washiriki wote watakaofanikiwa kumaliza mbio hizo watapatiwa medali.
“Mac D Marathon 2026 itarushwa mbashara siku hiyo kupitia vituo vya ITV pamoja na East Africa Televison na baada ya mbio kutakuwa na burudani katika FM Academia chini ya Patcho Mwamba, michezo ya watoto, chakula na vinywaji pamoja na mpira wa miguu kati ya IPP na Mac D promotions.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Riadha Mkoa wa Dar es Salaam Amani Ngoka amesema kupitia mbio hizo ambazo zimelenga kuhamasisha matumizi ya nishati safi, shirikisho litatumia fursa hiyo kusaka vipaji na wawakilishi wa kimataifa katika riadha.
Aidha amewasisitiza wazazi kushiriki mbio hizo na watoto ambao watakimbia Kilomita 2 ili waweze kutambua na kuendeleza vipaji vyao na kuwataka Mac D promotions kufanya mbio hizo kuwa za kimataifa kwa mwaka ujao.
Kwa taarifa zaidi za ushiriki wa mbio hizo pamoja na udhamini Mac D Promotions itapokea kupitia tovuti pamoja na mawasiliano ya simu 0791799848/0702562009 pamoja na barua pepe macdmarathon@gmail.com.
Mbio za Mac D kwa mwaka 2026 zimedhaminiwa na Shirika la Nyumba la Taifa ( NHC ) , Kilimanjaro Natural Mineral Water, Azania Bank, ITV, Eb Maritime Group, Mart Group Ltd kupitia vinywaji vyake pendwa Tanzanite RoyalGin na Tanzanite Crafted For Royalt, Kaluba, Radio One, EATV, Montage na Ayo Tv.
Mkurugenzi wa Mipango na Biashara wa Mac D Promotions Denzel Rweyunga akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mac D Marathon mwaka 2026 na kusema kuwa mbio hizo ambazo usajili wake umeanza rasmi leo zinatarajiwa kushirikisha wakimbiaji wa Kilomita 5, 10 na 21 pamoja na mbio za watoto za Kilomita 2. Leo jijini Dar es Salaam.Serikali imeeleza dhamira yake ya kuendelea kuimarisha sekta ya fedha nchini ili iwe chachu ya maendeleo ya haraka ya kiuchumi, huku ikisisitiza upatikanaji wa huduma za kifedha kwa wananchi wote kwa urahisi na gharama nafuu.
Kauli hiyo ilitolewa leo Aprili 9, 2026 jijini Dar es Salaam wakati wa ufunguzi wa jukwaa la wadau wa sekta ya fedha la mwaka 2026, lenye kauli mbiu isemayo “Sekta ya fedha bunifu na yenye uwajibikaji kwa maendeleo endelevu na jumuishi ya jamii na uchumi.”
Akizungumza katika hafla hiyo, Waziri wa Fedha, Khamis Mussa Omari, aliwataka wadau wa sekta hiyo kutumia jukwaa hilo kutoa mapendekezo yatakayosaidia kuboresha sera, sheria na mifumo ya kifedha, ili kufikia lengo la kuwa na uchumi imara unaotegemea sekta ya fedha ifikapo mwaka 2050.
“Sekta ya fedha ni mhimili muhimu wa maendeleo ya taifa. Tunahitaji kuhakikisha huduma za kifedha zinawafikia wananchi wote kwa urahisi na kwa gharama nafuu,” alisema Waziri Omari.
Ameeleza kuwa jukwaa hilo lina lengo la kuwakutanisha wadau mbalimbali ili kujadili utekelezaji wa Mpango Mkuu wa Maendeleo ya Sekta ya Fedha wa miaka kumi (2021–2029), huku akibainisha kuwa sekta hiyo ina mchango mkubwa katika kukuza uchumi na kuongeza upatikanaji wa huduma za kifedha kwa wananchi.
Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu Mwamba, amesema kuwa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, kumekuwa na mafanikio makubwa katika sekta hiyo, ikiwemo kuongezeka kwa upatikanaji wa huduma za fedha, ongezeko la matawi na mawakala wa benki pamoja na ukuaji wa huduma za fedha kidijitali.
Amebainisha kuwa asilimia 76 ya Watanzania sasa wanapata huduma rasmi za kifedha, hatua inayochangiwa kwa kiasi kikubwa na matumizi ya simu za mkononi na huduma za fedha mtandao.
Naye Naibu Waziri wa Fedha, Mhandisi Mshamu Munde, amesisitiza umuhimu wa kudhibiti hatari za kifedha ikiwemo biashara haramu na matumizi mabaya ya mifumo ya fedha, huku akihimiza usimamizi madhubuti wa teknolojia mpya za kifedha.
Washiriki wa jukwaa hilo walipata fursa ya kujadili changamoto na fursa zilizopo katika sekta ya fedha, hususan katika maeneo ya ubunifu wa teknolojia, ujumuishwaji wa kifedha na uwekezaji.
Jukwaa hilo linatarajiwa kutoa maazimio yatakayosaidia kuimarisha sekta ya fedha na kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini.
Wadau waliohudhuria ni pamoja na wawakilishi wa mabenki, taasisi za bima, vyama vya ushirika pamoja na sekta binafsi.
Na Oscar
Assenga, TANGA
Chama cha
Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tanga kimetoa maelekezo kwa Halmashauri ya Jiji la
Tanga kuhakikisha maeneo ya kukusanyia taka katika soko la Mgandini
yanaboreshwa kwa kujazwa kifusi ikiwemo kurekebisha barabara za ndani ili
kuimarisha usafi.
Agizo
hilo lilitolewa na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Tanga Rajab Abdurhaman wakati wa
ziara yake ambapo alisisitiza umuhimu wa kuhakikisha maji ya mvua yanaelekezwa
ipasavyo kwenye mifereji ili kuepusha mafuriko na uharibifu wa miundombinu.
Ziara hiyo
ilikuwa ni kufuatilia utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa awali kuhusu kuboresha
usafi wa soko hilo ambapo viongozi wa Jiji hilo walianza kuyafanyia kazi
ikiwemo kuondosha uchafuzi uliokuwepo awali.
Awali,
wakati wa ziara yake ya kukagua hali ya usafi, Mwenyekiti huyo hakuridhishwa na
mazingira ya soko hilo na kutoa muda wa mwezi mmoja kwa uongozi wa Jiji
kuhakikisha hali ya usafi inaboreshwa.
Akizungumza
baada ya kufanya ziara ya ufuatiliaji, Rajab aliwapongeza Mstahiki Meya pamoja
na viongozi wa Jiji kwa kuchukua hatua na kuanza kutekeleza maelekezo hayo ya
CCM.
“Hatuhitaji
viongozi wa kulalamika, tunahitaji viongozi wanaochukua hatua kutatua changamoto
za wananchi. Mlichokifanya ni kutimiza wajibu wenu,” alisema.
Alisema kuwa
hali ya uchafu iliyokuwepo awali haikuwafurahisha viongozi wala wafanyabiashara,
hivyo hatua zilizochukuliwa zinaonesha uwajibikaji wa uongozi.
Hata
hivyo Mwenyekiti Rajab alisisitiza kuwa atarejea kukagua maendeleo hayo baada
ya wiki mbili na kuonya kuwa hataki kusikia visingizio badala ya utekelezaji.
“Ndani ya
mwezi mmoja kuanzia Aprili 9 hadi Mei 9, tunatarajia kuona kazi imeanza. Hatutaki
hadithi, tunataka vitendo,” alisisitiza.
Aidha,
alieleza kuwa Jiji la Tanga ni taswira ya mkoa huo, hivyo linapaswa kuwa safi
na lenye mpangilio mzuri.
Alikumbusha
kuwa zamani Tanga ilikuwa mji unaojulikana kwa usafi na ustaarabu, hivyo ipo
haja ya kurejesha hali hiyo.
Kuhusu
huduma za vyoo katika soko hilo, Mwenyekiti alieleza kutoridhishwa na hali
iliyopo, akibainisha kuwa choo kilichopo hakitoshelezi mahitaji kutokana na
idadi kubwa ya watumiaji.
Alisema
kuwa hali hiyo inasababisha baadhi ya watu kulazimika kujisaidia katika maeneo
yasiyofaa, jambo linalohatarisha afya za wananchi na wafanyabiashara.
Alisisitiza
umuhimu wa Jiji kutafuta suluhisho la kudumu, ikiwemo kuboresha mfumo wa maji
taka ili kuendana na ongezeko la watumiaji.
Hata
hivyo, aliwapongeza viongozi kwa kuanza mpango wa kujenga choo kipya chenye
matundu 12 kitakachosaidia kupunguza changamoto hiyo, hasa katika kipindi hiki
ambacho soko linatarajiwa kujengwa upya.
Pia
alizungumzia changamoto ya msongamano wa magari yanayoleta bidhaa sokoni hapo,
akielekeza kuwepo kwa utaratibu maalum wa magari kuingia na kushusha mizigo kwa
mpangilio ili kupunguza msongamano na kuboresha usafi.
Alipendekeza
magari yapaki katika maeneo maalum yaliyo nje ya soko, kisha yaingie kwa zamu
kushusha bidhaa.
Katika
hatua nyengine alisisitiza umuhimu wa kujenga mifereji ya maji ili kuzuia maji
ya mvua kutuama au kuingia sokoni, hali inayochangia uchafu na uharibifu wa
mazingira.
Alimalizia
kwa kuwataka viongozi wa Jiji kuwa karibu na wananchi na kushughulikia
changamoto zao kwa vitendo, akibainisha kuwa wananchi hao ndio chanzo cha
mapato ya Jiji kupitia kodi.
Kwa
upande wake, Naibu Meya Khalid Rashid alisema kuwa Jiji lina mpango wa
kuboresha miundombinu ya ndani ya soko, ikiwemo njia za kupita ili kuondoa
changamoto ya matope wakati wa mvua. Alibainisha kuwa kazi hiyo inatarajiwa
kuanza ndani ya wiki moja.
Mwisho.
MAMLAKA ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) imewatangazia waingizaji wa mizigo mikubwa ya forodha ya bidhaa za Dawa, Vifaa Tiba na Vitendanishi nchini, kuwa mifumo ya TANCIS-TRA na RIMS-TMDA imeunganishwa ili kuongeza ufanisi katika kuingiza na kutoa shehena za bidhaa hizo nchini kwa njia ya kielektroniki.
Kwa mujibu wa taarifa kwa Umma iliyotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa TMDA, Dk. Adam Fimbo ameeleza kuwa, Lengo kuu la muunganiko huo ni kurahisisha michakato ya uombaji vibali kuwa na sehemu moja ya kuingiza taarifa, pamoja na kuboresha ufuatiliaji na shughuli za udhibiti wa maombi ya kuingiza na kutoa bidhaa nchini.
"Mnajulishwa rasmi kuwa kuanzia tarehe 1 Mei, 2026 maombi yote yaliyokuwa yanapitia TMDA-RIMS na TRA-Forodha kwa ajili ya kutolea taarifa (declaration) yatafanyika moja kwa moja katika mfumo wa TANCIS.
Ili kuepusha Hoja zisizo za lazima na kurahisisha huduma za upatikanaji wa vibali, mnakumbushwa kuzingatia; Usahihi wa taarifa za bidhaa zinazosimamiwa na TMDA (ikijuimuisha namba za usajili za bidhaa na majengo); na Wadau wote watatakiwa kushirikiana na Wakala wa Forodha kwa ukaribu ili kuthibitisha usahihi wa taarifa za kitaalam na nyaraka hitajika." Imeeleza taarifa hiyo kwa Umma.
Aidha, TMDA imewataka kuzingatia kuwa, tangazo hilo linawahusu waingizaji wa mizigo mikubwa ya forodha, na si waingizaji kwa matumizi binafsi (personal use).
Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA) imesema ujenzi wa moduli ya kupokea na kushughulikia malalamiko na rufaa katika mfumo wa NeST utachangia kuongeza uwajibikaji, uwazi na ufanisi kwenye mnyororo wa ugavi.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba (Mb), akizungumza na viongozi wa Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA), wakati alipotembelea banda ya maonesho katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, Jijini Dodoma, kabla ya kuzindua rasmi Sera Taifa ya Usimamizi wa Mnyororo wa Ugavi ya Mwaka 2025.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba (Mb), (Katikati Kulia), akiwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), na viongozi wengine wakisikiliza maelezo kutoka kwa Katibu Mtendaji wa Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA), Bw. James Sando (kushoto), kuhusu mchango wa PPAA katika Mnyororo wa Ugavi, wakati Mhe. Waziri Mkuu alipotembelea banda ya maonesho katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, Jijini Dodoma, kabla ya kuzindua rasmi Sera Taifa ya Usimamizi wa Mnyororo wa Ugavi ya Mwaka 2025.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba (Mb), akizindua rasmi Sera Taifa ya Usimamizi wa Mnyororo wa Ugavi ya Mwaka 2025 katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, Jijini Dodoma..jpeg)



















.jpeg)
