▪️Waziri Mavunde na Waziri Kabamba wakubaliana msingi wa ushirikiano,
▪️Ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais Samia na Rais Tshisekedi ya ushirikiano baina ya nchi hizo mbili,
▪️Ushirikiano walenga kurahisisha usafirishaji na biashara ya madini,
▪️Wakubaliana kuweka mikakati ya pamoja kuimarisha ufuatiliaji wa uzalishaji wa madini (traceability),
TIANJIN, CHINA
Pembezoni mwa Mkutano wa Madini wa China uliofanyika Jijini Tianjin, Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Madini wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Mheshimiwa Louis Watum Kabamba yaliyolenga kufungua ukurasa mpya wa ushirikiano kwenye sekta ya madini.
Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika tarehe 11 Septemba, 2026 Waziri Mavunde na mwenzake Mhe. Kabamba walijadiliana kwa kina namna ya kuendeleza sekta ya madini baina ya Nchi zao na hatimaye kuweka msingi ambao utakuwa ni mwanzo wa kuimarisha ushirikiano utakaoleta tija kwa pande zote mbili.
"Leo tumekutana hapa si kwa bahati mbaya, haya ni matokeo ya maelekezo ya viongozi wetu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na Mhe. Felix Tshekedi ya kwamba Nchi zetu ni muda muafaka wa kuimarisha ushirikiano kwenye sekta ya madini kwani tunahitajiana na kutegemeana hususan katika masuala ya usafirishaji wa madini"
"Viongozi wetu wameshatuwekea msingi, sisi kazi yetu ni kuhakikisha tunayaishi maono yao na kuimarisha ushirikiano ambao utakwenda kuongeza tija na kuboresha sekta zetu za madini kuanzia uzalishaji mpaka biashara na uongezaji thamani madini" alisisitiza Waziri Mavunde.
Aidha, Waziri Mavunde alibainisha kuwa ushirikiano baina ya Kongo DRC na Serikali ya Jamhuri ya Tanzania umelenga kwa kiasi kikubwa kurahisisha ufanyaji wa biashara na usafirishaji wa madini kwa maslahi mapana ya Nchi zetu.
Vilevile, Mavunde alieleza kuwa kwa sasa ni vyema Tanzania na DRC wakaweka mikakati ya pamoja na kuisimamia kwa lengo la kuimarisha ufuatiliaji wa mnyonyoro wa uzalishaji wa madini kuanzia yanapochimbwa mpaka yanapouzwa au kusafirishwa kwenda nje (traceability).
Naye, Waziri wa Madini wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC), Mhe. Louis Kabamba alishukuru kwa kukutana na mwenzake na kuahidi kuwa, kwa namna yeyote ni vyema kuyaishi maono ya Viongozi wakuu wa Mataifa haya ili kuleta manufaa yanayotarajiwa kwa wananchi na Taifa kwa ujumla.
Aliendelea kusisitiza kuwa ushirikiano baina ya Tanzania na DRC pia utasaidia kubadilishana uzoefu wa namna ya kuendeleza sekta ya madini hususani katika kuwezesha uchimbaji mdogo na kuongeza mapato ya Serikali, hatua ambayo kwa DRC bado wachimbaji wadogo wanachangia kiasi kidogo. Pia, Mhe. Kabamba alisifu maendeleo ya STAMICO na kuomba uzoefu wao usaidie kuimarisha Shirika la Madini la Kongo ili liweze kuzalisha na kujiendesha kwa faida.




.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)



.jpeg)

.jpeg)



.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)


.jpeg)






.jpeg)


.jpeg)





.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

