Na Mwandishi Wetu, Dodoma
NIC Insurance imewahimiza wakulima nchini kutumia fursa ya Bima ya Kilimo ili kujikinga dhidi ya hasara zinazoweza kusababishwa na majanga mbalimbali ya asili na kulinda uwekezaji wao katika sekta ya kilimo.

Akizungumza katika Maonesho ya Kilimo ya Nane Nane yanayoendelea katika Viwanja vya Dkt. John Samwel Malecela jijini Dodoma, Afisa Bima wa NIC Insurance, Aman Mollel, amesema bima hiyo inalenga kuwakinga wakulima dhidi ya madhara yanayosababishwa na ukame, mafuriko, magonjwa na wadudu wa mimea, pamoja na majanga mengine yanayoweza kuathiri uzalishaji na kipato.

Mollel amesema mazao yanayoweza kukatiwa bima ni pamoja na pamba, korosho, kahawa, tumbaku, maharage, mahindi, mpunga, shayiri, alizeti na chai.

Amesema bima hiyo pia inamlinda mkulima dhidi ya majanga kama vimbunga na mvua ya mawe, ambayo yanaweza kusababisha uharibifu wa mazao, kupunguza uzalishaji na kuathiri kipato cha mkulima.

Kwa mujibu wa Mollel, ili mkulima aweze kupata huduma hiyo anatakiwa kuwa na fomu ya maombi iliyojazwa na kusainiwa, taarifa za gharama za uzalishaji kwa hekta, makisio ya gharama au bei kwa kilogramu pamoja na taarifa za kihistoria za uzalishaji wa mkulima.

Amesema matumizi ya Bima ya Kilimo ni muhimu katika kuwawezesha wakulima kuendelea na shughuli zao za uzalishaji bila kukumbwa na athari kubwa za kifedha pale majanga yanapotokea.

“Bima ya Kilimo ni kinga ya mkulima dhidi ya majanga, hasara na changamoto zinazoweza kujitokeza katika uzalishaji wa mazao,” amesema Mollel.

Amesema NIC Insurance pia inatoa Bima ya Mifugo katika kumkinga mfugaji dhidi ya hasara inayoweza kujitokeza kutokana na vifo vya mifugo vitokanavyo na ajali ,Wizi wa Mifugo ,Magonjwa ,Uchinjwaji wa lazima kutokana na ushauri wa daktari.

Amesema Bima ya Mifugo iko katika mifugo ya Ng'ombe wa Maziwa ,Ng'ombe wa Nyama ,Kuku pamoja na Mbuzi katika vigezo kuwa na fomu ya maombi iliyosainiwa,ripoti ya ukaguzi wa mnyama kutoka kwa afisa mifugo pamoja na ratiba ya chanjo ya mifugo.

Mollel amesema gharama za Bima hizo kwa Ng'ombe wa Maziwa asilimia Tano kwa Makato ya ulinganifu wa asilimi a 10,Ng'ombe wa nyama asilimia Nne kwa Makato ya ulinganifu wa asilimi a 10,Kuku asilimia Tano kwa Makato ya ulinganifu wa asilimi a 15,Mbuzi asilimia Tano kwa Makato ya ulinganifu wa asilimi a 10

Amesema Ada ya Bima inapatikana kwa kuchukua kiwango cha asilimia kinachotolewa na Kampuni ya Bima kuzidisha na thamani ya mfugo au mnyama.

Ameongeza kuwa faida ya Bima ni kukuza uwekezaji ,kumrudisha mfigaji kwenye hali aliyokuwa nayo kabla ya mifigo kufa pamoja na kupata mkopo kutoka taasisi za kifedha kwa masharti nafuu.


Na Mwandishi Wetu, Dodoma
MBUNIFU wa Mashine ya Kuchanganya Chakula cha Mifugo kutoka Chuo cha Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) Songea, Mwalimu Sussack Mbulu, amesema mashine hiyo ni mkombozi kwa wafugaji katika kuandaa chakula bora cha mifugo na kuongeza thamani ya mifugo yao sokoni.

Mwalimu Mbulu ameyasema hayo katika Viwanja vya Dkt. John Samwel Malecela jijini Dodoma, ambako yanaendelea Maonesho ya Wakulima na Wafugaji Kitaifa.

Amesema mashine hiyo ni miongoni mwa ubunifu unaolenga kurahisisha shughuli za ufugaji, ambapo inaweza kuchanganya chakula cha mifugo kwa uwezo wa kilogramu 480 kwa saa.

“Mashine hii itamsaidia mfugaji kurahisisha maandalizi ya chakula cha mifugo na kuhakikisha anapata chakula kilichochanganywa vizuri, hivyo kuongeza ufanisi katika ufugaji,” amesema.

Mwalimu Mbulu amesema mashine hiyo inauzwa kwa Shilingi 400,000, huku wananchi wakihitaji ya wanaweza kufikiwa popote walipo.

Amewataka wafugaji kutumia teknolojia na ubunifu huo ili kurahisisha kazi, kuongeza uzalishaji na kuwawezesha kufuga mifugo kwa wingi yenye tija na inayoweza kuingia katika masoko.

Mbali na mashine hiyo, amesema VETA Songea imebuni pia kifaa cha kumwagilia mashamba (Sprinkler) ambacho kina uwezo wa kumwagilia eneo la robo ekari ndani ya dakika 15.

Aidha, amewataka wananchi na wafugaji kutembelea Banda la VETA katika maonesho hayo ili kupata elimu kuhusu teknolojia za kilimo na ufugaji, pamoja na kupata taarifa kuhusu fursa za kujiunga na masomo katika vyuo vya VETA vilivyopo nchi nzima.

Na Mwandishi Wetu, Dodoma
MAMLAKA ya Serikali Mtandao (e-GA) inaendelea kushirikiana na Wizara ya Kilimo katika kuimarisha matumizi ya mifumo ya kidijitali inayolenga kurahisisha utoaji wa huduma, kuongeza uwazi na kuboresha usimamizi wa shughuli za kilimo nchini.

Akizungumza jana katika Maonesho ya Wakulima ya Kitaifa yanayoendelea katika Viwanja vya Dkt. John Samwel Malecela jijini Dodoma, Meneja wa Mawasiliano wa e-GA, Subira Kaswaga, alisema mamlaka hiyo imeshiriki katika ujenzi wa mifumo mbalimbali inayotumika katika sekta ya kilimo.

Alisema mifumo hiyo inaiwezesha Wizara ya Kilimo kupata taarifa za wakulima nchini, kufuatilia shughuli za taasisi zilizo chini ya wizara hiyo pamoja na kutoa taarifa muhimu za kilimo kwa wadau.

Kaswaga alisema e-GA pia imeshirikiana na Tume ya Maendeleo ya Ushirika kutengeneza Mfumo wa Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (MUVU), unaolenga kuongeza uwazi na uwajibikaji katika uendeshaji wa vyama vya ushirika.

Alisema mfumo huo pia unawawezesha wakulima kufuatilia mauzo ya mazao yao, bei pamoja na malipo wanayostahili kupata.

“Hadi sasa, zaidi ya vyama 6,000 vya ushirika vinatumia mfumo huo, jambo ambalo limesaidia kuboresha usimamizi wa mapato na kuongeza uwajibikaji katika sekta ya ushirika,” alisema.

Alieleza kuwa e-GA ina jukumu la kuandaa na kusimamia mifumo mbalimbali ya TEHAMA inayotumika serikalini kwa lengo la kuboresha utendaji kazi wa taasisi za umma na kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi.

Aidha, alisema e-GA imeshirikiana na Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) kuanzisha Fertilizer Information System (FIS), mfumo unaosaidia kusimamia wazalishaji na waingizaji wa mbolea, kufuatilia mwenendo wa soko na kuhakikisha wauzaji wanazingatia bei elekezi zinazotolewa na Serikali.

Kwa mujibu wa Kaswaga, mfumo huo unaisaidia Serikali kudhibiti soko la mbolea na kuhakikisha wakulima wanapata pembejeo hizo kwa bei stahiki, hatua inayolenga kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao.

Mbali na mifumo hiyo, alisema taasisi za sekta ya kilimo zinaendelea kutumia mifumo mingine ya Serikali, ikiwemo Government Email System na Mfumo wa Ofisi Mtandao, ambayo imechangia kuboresha mawasiliano na utendaji kazi ndani ya taasisi za umma.

Mamlaka hiyo imewataka wananchi kutembelea banda la e-GA katika maonesho yanayoendelea jijini Dodoma ili kupata elimu zaidi kuhusu mifumo ya kidijitali inayotumika kuboresha utoaji wa huduma za Serikali na mchango wake katika maendeleo ya sekta ya kilimo.


SHIRIKISHO la Viwanda Tanzania (CTI) limetangaza kuwa Tuzo za Rais za Wazalishaji Bora wa Mwaka (PMAYA) kwa mara ya 19, jukwaa kubwa nchini Tanzania la kutambua mafanikio ya viwanda, litafanyika Agosti 24 mwaka huu.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa CTI, Hussein Sufian, alisema kaulimbiu ya mwaka huu, “Green Elegance — Celebrating Sustainable Manufacturing Practices,” inaonesha mabadiliko katika kile ambacho PMAYA inatambua; si tu uzalishaji wa viwanda, bali pia uendelevu, uwajibikaji na ustahimilivu unaosimamia uzalishaji huo.

Alisema jioni hiyo itashuhudia zulia la kwanza la kijani (Green Carpet) nchini Tanzania, likichukua nafasi ya zulia la kawaida jekundu, ikiwa ni ishara ya dhamira ya pamoja ya sekta kuelekea ukuaji endelevu wa viwanda.

“Kwa miaka kumi na tisa, PMAYA imekuwa ikieleza hadithi ya viwanda vya Tanzania katika hali yake bora zaidi. Mwaka huu, tunaeleza hadithi kamili zaidi, inayotambua si tu kile wazalishaji wetu wanachozalisha, bali pia jinsi wanavyozalisha kwa uwajibikaji. Green Elegance si kaulimbiu tuliyoikopa; ni mwelekeo ambao sekta hii tayari inaufuata, na PMAYA ipo kutambua uongozi huo,” alisema.

Pia kwa mara ya kwanza katika historia ya miaka 19 ya PMAYA, mbali na washindi wa kategoria za tuzo, PMAYA itatangaza Mabalozi sita wa ESG (ESG Ambassadors), ambao wameainishwa kupitia tathmini ya CTI kama viongozi katika utekelezaji wa masuala ya Mazingira, Jamii na Utawala Bora.

Alisema mabalozi hao wameainishwa kupitia tathmini ya moja kwa moja ya utendaji wao viwandani na watatumika kama mabalozi wa sekta kwa muda wa miezi 12. Kundi hilo litakuwa msingi wa kuanzishwa kwa tuzo mpya ya kudumu ya Mzalishaji Bora wa Mazingira wa Mwaka (Green Manufacturer of the Year), itakayoanza kutolewa katika PMAYA ya 20.

Mkurugenzi Mtendaji wa CTI, Mhandisi Leodegar Tenga, alisema kupitia mradi wa ESG, timu ya CTI ilitembelea viwanda mbalimbali nchini na kushuhudia utekelezaji wa masuala hayo kwa vitendo.

“Balozi sita wa ESG tutakaowatangaza waliainishwa kupitia mchakato huo. Huu ni mwanzo wa njia ya kudumu ya kutambua uzalishaji endelevu viwandani hapa Tanzania, na tunatarajia kushiriki hadithi zao tarehe 24 Agosti,” alisema.

Alisema PMAYA ya 19 inaungwa mkono na wazalishaji na kampuni mashuhuri za Tanzania, ikiwemo Tanzania Cigarette Company (TCC), Tanzania Breweries Limited (TBL), Chemi Cotex Limited na Africab Group (Kilimanjaro Cables).

CTI imezihimiza kampuni nyingine zenye nia ya kushirikiana katika PMAYA ya 19 kuwasiliana na Sekretarieti ya CTI kwa maelezo zaidi kuhusu udhamini.

Tenga alisema tuzo hizo zilitokana na mashindano kati ya wazalishaji yaliyoanzishwa mwaka 2005 na kuandaliwa na CTI kwa lengo la kutambua, kutathmini na kuenzi umuhimu na mchango wa sekta ya viwanda katika maendeleo ya nchi.

“Siku hii ni ya muhimu sana kwetu kwa sababu ni fursa ya pekee tunayoipata mara moja kwa mwaka, kwa pamoja, ili kutambua, kutathmini na kuenzi umuhimu na mchango wa Sekta ya Viwanda katika maendeleo ya uchumi wa Taifa letu,” alisema.

Alisema katika miaka 19 tangu kuanzishwa kwa utaratibu huo, maboresho mbalimbali yamefanyika, ikiwemo kuongeza wigo wa washiriki kwa kuhusisha sekta za uzalishaji 26, ili kujumuisha viwanda vidogo, vya kati na vikubwa.

Aidha, alisema washindi wa tuzo hizo hupatikana kwa kuzingatia mchango wa mzalishaji katika uchumi, maendeleo na uwekezaji katika teknolojia ya kisasa inayojali na kutunza mazingira, mauzo ya nje, afya na usalama wa mazingira ya kazi, pamoja na mchango katika kuendeleza jamii inayowazunguka (Corporate Social Responsibility) na vigezo vingine.

Tuzo hizo zinaendelea kuwa jukwaa kuu la Tanzania katika utambuzi wa viwanda, uhamasishaji wa uwekezaji na majadiliano baina ya sekta binafsi na Serikali.

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar, akizungumza na waandishi wa habari kuelekea mkutano mkuu wa wanahisa wa Afrika50 na jukwaa la miundombinu Afrika, Agosti 03, 2026, Ofisi za Wizara ya Fedha, jijini Dar es salaam.

Na Avila Kakingo
TANZANIA itakuwa mwenyeji wa Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa Taasisi ya Africa50 (Africa50 General Shareholders' Meeting - GSM) pamoja na Jukwaa la Miundombinu Afrika (Infra for Africa Forum), yatakayofanyika Agosti 5 na 6, 2026 katika Ukumbi wa Julius Nyerere International Convention Centre (JNICC), Dar es Salaam.

Na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kuwa mwenyeji na mwenyekiti wa hafla ya ufunguzi wa mkutano huo, ambao pia utahusisha taasisi mbalimbali za umma na sekta binafsi nchini, benki za biashara na maendeleo, taasisi za hifadhi ya jamii, masoko ya mitaji na wadau wa sekta za nishati, uchukuzi, reli, bandari, usafiri wa anga, maji, afya, madini, mafuta na gesi.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, leo Septemba 03, 2026  Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omar, amesema mkutano huo wa kimataifa unafanyika wakati Africa50 inatimiza miaka 10 tangu kuanza shughuli zake mwaka 2016, huku ukitarajiwa kukutanisha washiriki zaidi ya 1,200 kutoka Afrika na maeneo mbalimbali duniani.

Balozi Omar amesema Africa50 ilianzishwa mwaka 2013 kwa ushirikiano wa Serikali za Afrika na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), ikiwa na lengo la kuharakisha maandalizi, uendelezaji na ufadhili wa miradi mikubwa ya kimkakati ya miundombinu kupitia ubia kati ya Serikali na sekta binafsi katika sekta za nishati, uchukuzi, afya, elimu, TEHAMA na huduma za kifedha.

Amesema Tanzania ilijiunga rasmi na Africa50 Februari 14, 2023 kama mwanahisa wa kundi la “A” (African Sovereign States), hatua iliyopanua fursa za nchi kushiriki kikamilifu katika maandalizi na ufadhili wa miradi mikubwa ya miundombinu.

Kwa mujibu wa Waziri huyo, tangu kujiunga na taasisi hiyo, Tanzania imeanza kunufaika kupitia maandalizi ya miradi ya kimkakati ikiwemo maendeleo ya Bandari ya Mangapwani Zanzibar, Mradi wa Mini Liquefied Natural Gas (Mini LNG), miundombinu ya usafirishaji wa umeme na upanuzi wa huduma za usafishaji wa figo (dialysis) kupitia ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi (PPP).

Mkutano wa mwaka 2026 unafanyika chini ya kaulimbiu isemayo “A Decade of Economic Impact: From Ambition to Delivery.”

Balozi Omar amesema katika kipindi cha siku mbili za mkutano kutakuwa na Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa Africa50, Jukwaa la Miundombinu Afrika na hafla za kusaini makubaliano mbalimbali ya maandalizi na utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya miundombinu.

Amesema kwa kuwa mwenyeji wa mkutano huo, Tanzania itapata fursa ya kuendelea kujitangaza kama kitovu cha uwekezaji na maendeleo ya miundombinu Afrika Mashariki, kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali, sekta binafsi na taasisi za fedha za kimataifa, pamoja na kuhamasisha uwekezaji katika miradi ya kimkakati yenye tija kwa maendeleo ya taifa.

“Serikali inawahakikishia wananchi kuwa maandalizi yote yanaendelea vizuri kwa ushirikiano na Africa50 pamoja na taasisi mbalimbali za Serikali ili kuhakikisha mkutano huo unafanyika kwa mafanikio makubwa,” amesema Balozi Omar.

Ameongeza kuwa Serikali inawakaribisha wananchi kuendelea kutoa ushirikiano na kuwapokea wageni watakaofika nchini kwa ajili ya mkutano huo, ambao unatarajiwa kuwa miongoni mwa mikutano mikubwa ya kimataifa itakayofanyika nchini mwaka 2026.




AFISA Kumbukumbu za Wanachama wa Mfuko wa PSSSF Bw.Alex Bwanakunu (kulia) akimsikiliza mwananchi aliyetembelea Banda la PSSSF kwenye Maonesho ya Nanenane Kanda ya Ziwa Magharibi yanayofanyika uwanja wa Nyamhongolo Jijini Mwanza Agosi 2,2026


Dodoma, Agosti 2, 2026

Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) unashiriki katika Maonesho ya Nanenane 2026 kwa kutoa huduma mbalimbali na elimu kuhusu Hifadhi ya Jamii kwa wanachama wake na wananchi kupitia mabanda yake yaliyopo katika kanda tano nchini, ikiwemo Zanzibar.

Msanii maarufu nchini ,Mrisho Mpoto (wa pili kushoto) akiwa ameshika mkanda ,moja ya bidhaa zinazozalishwa katika kiwanda cha KLICL,Kinachomilikiwa na PSSSF kwa ushirikiano na Jeshi la Magereza ,alipotembelea Banda la Mfuko wa PSSSF kwenye maonesho ya Nanenane yanayofanyika Kitaifa kwenye viwanja vya Nzunguni Jijini Dodoma Agosti 2,2026,kushoto ni Afisa Mkuu wa Uhusiano wa Mfuko wa PSSSF Bw.Abdul Njaidi na kulia ni Afisa Mauzo kiwanda cha KLICL ,Bi,Mary Muna

Kwa mujibu wa Afisa Uhusiano Mkuu wa Mfuko wa PSSSF, Bw. Abdul Njaidi, PSSSF imeshiriki maonesho hayo katika Kanda ya Kati viwanja vya Nanenane mkoani Dodoma, ambako Maonesho ya Nanenane 2026 yanafanyika kitaifa na tayari yamezinduliwa na Waziri Mkuu, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, Agosti 1, 2026. Kaulimbiu ya mwaka huu ni ‘Tambua Soko; Ongeza Tija na Thamani ya Kuelekea Dira 2025’.

Wanachama wa Mfuko wa PSSSF wakihudumiwa kwenye Banda la Mfuko huo kwenye Maonesho ya Nanenane yanayofanyika Kitaifa kwenye viwanja vya Nzunguni Jijini Dodoma Agosti2,2026

Katika maonesho ya mwaka huu, PSSSF inashiriki; Zanzibar katika viwanja vya Dole, Kanda ya Magharibi mkoani Tabora katika viwanja vya Ipuli Mnadani, Kanda ya Ziwa jijini Mwanza katika viwanja vya Nyamhungolo, Kanda ya Kusini mkoani Lindi katika viwanja vya Ngongo na Kanda ya Nyanda za Juu Kusini jijini Mbeya, viwanja vya Nanenane.


Afisa Matekelezo wa Mfuko wa PSSSF Bi.Esther Mpemba (kulia ) akimuunganisha Mwanachama wa PSSSF ,Bi.Maliasa Sajoho na Mfumo wa PSSSF Member Portal ambao unamuwezesha kupata huduma za mfuko Kidijitali,kwenye maonesho ya Nanenane Viwanja vya Nzunguni Jijini Dodoma Agosti 2,2026

"Tunawakaribisha wanachama wetu na wananchi wote kutembelea mabanda ya PSSSF katika kanda hizo ili kupata huduma mbalimbali ikiwa ni pamoja na elimu kuhusu mafao, kuhakiki taarifa zao na michango, pamoja na kuwaunganisha katika huduma zetu za kidijitali, huku tukiwahakikisha kesho ya uhakika wanachama wetu’" alisema Bw. Njaidi

Afisa Huduma kwa Wateja wa Mfuko wa PSSSF ,Bi .Saluna Ally (kushoto) akimuhudumia Mstaafu anayepokea Pensheni PSSSF ,Bw.Mwakibete G.Kasilati,kwenye banda la mfuko huu katika maonesho ya Nanenane Kanda ya Nyanda za Juu Kusini kwenye viwanja vya Nanenane Jijini Mbeya,Agosti 2,2026

Aidha, watakaotembelea kwenye mabanda ya PSSSF watapata nafasi ya kuona fursa za uwekezaji wa Mfuko ambazo ni pamoja na bidhaa za ngozi zinazotengenezwa na Kiwanda cha KLICL na nyama kutoka machinjio ya Kimataifa ya Nguru.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt Mwigulu Nchemba akitoa hotuba ya ufunguzi wa Maonesho ya Nanenane Kitaifa katika viwanja vya Nzunguni Jijini Dodoma Agosti 1,2026



Meneja wa PSSSF Kanda ya Magharibi Bw.Eliadi Mndeme akitoa elimu kwa mwanachama wa PSSSF wakati wa Maonesho ya Nanenane Kanda ya Magharibi ambayo yanafanyika viwanja vya Ipuli mkoani Tabora Agosti 2,2026
Benki ya Exim Tanzania na Taasisi ya Wanasayansi Chipukizi Tanzania (YST) leo wamezindua rasmi ushirikiano wao wa mwaka 2026 kupitia Programu ya YST 2026, wakithibitisha dhamira yao ya pamoja ya kuendelea kuandaa kizazi kijacho cha wabunifu, watafiti na watatuzi wa changamoto kupitia sayansi, teknolojia, ubunifu na utafiti.

Ushirikiano huu unafikisha mwaka wa sita mfululizo tangu Benki ya Exim Tanzania ilipoanza kuunga mkono Taasisi ya Wanasayansi Chipukizi Tanzania (YST), jambo linalodhihirisha dhamira ya Benki ya kuwekeza katika elimu, ubunifu na maendeleo ya vijana, huku ikichangia maendeleo ya muda mrefu ya kijamii na kiuchumi nchini Tanzania.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo uliofanyika katika Makao Makuu ya Benki ya Exim Tanzania (Exim Tower) jijini Dar es Salaam, Meneja Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Exim Tanzania, Kauthar D’souza, alisema ushirikiano huo unaakisi imani ya Benki kuwa kuwawezesha vijana ni msingi muhimu wa kujenga taifa lenye ubunifu, ushindani na maendeleo endelevu kupitia falsafa yao ya “Ubunifu ni maisha”.

"Exim Bank Tanzania tunaamini kuwa ubunifu huanza kwa kuwawezesha vijana. Ushirikiano wetu na Taasisi ya Wanasayansi Chipukizi Tanzania (YST) unaonesha dhamira yetu ya kuwaunga mkono wanafunzi wenye udadisi, ubunifu na ari ya kutafuta suluhisho zinazoweza kubadilisha jamii na kuchangia maendeleo ya taifa”. alisema D'Souza.

"Kwa miaka sita sasa, YST imekuwa mshirika wetu muhimu katika kuwaibua na kuwawezesha vijana wenye fikra bunifu kutumia sayansi, utafiti na ubunifu kutatua changamoto zinazoikabili jamii. Tunaamini kuwa kwa kuwekeza katika elimu, ubunifu na maendeleo ya vipaji vya vijana leo, tunajenga msingi imara wa maendeleo endelevu ya Tanzania”. Aliongeza D’Souza

Programu ya mwaka huu imeweka rekodi mpya kwa kupokea jumla ya mawasilisho 1,330 ya miradi kutoka shule 287 za sekondari zilizopo katika mikoa yote ya Tanzania. Baada ya mchakato wa tathmini na ulezi wa kitaalamu uliofanywa na washauri wa sayansi wa YST, miradi 162 imechaguliwa kuingia hatua inayofuata, huku miradi 45 bora ikitarajiwa kushiriki Maonesho ya Kitaifa ya Sayansi na Teknolojia ya taasisi ya wanasayansi chipukizi yatakayofanyika tarehe 17 Septemba 2026 katika Ukumbi wa maktaba mpya, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Akizungumzia ushirikiano huo, Mwanzilishi Mwenza wa taasisi ya wanasayansi chipukizi Tanzania, Dkt. Gozbert Kamugisha, aliishukuru Benki ya Exim Tanzania kwa kuendelea kuwa mshirika muhimu katika kuwawezesha vijana wabunifu nchini.

"Tunatoa shukrani zetu za dhati kwa Benki ya Exim Tanzania kwa msaada wake endelevu katika kipindi cha miaka sita iliyopita.Kilichoifanya programu ya mwaka huu kuwa ya kipekee ni kwamba Benki ya Exim Tanzania haijajikita tu katika kutoa udhamini wa kifedha, bali pia imekuwa sehemu ya utekelezaji wa programu. Kupitia wataalamu wake, Benki imeungana nasi kutembelea shule mbalimbali, kukutana na walimu na wanafunzi, pamoja na kutoa ushauri wa kitaalamu unaowasaidia kuboresha tafiti na ubunifu wao ili kupata suluhisho zenye tija kwa jamii," aliongeza Dkt. Kamugisha

Katika hatua nyingine, Dkt. Gozibert Kamugisha alibainisha baadhi ya changamoto zinazoikabili YST, ikiwemo uhaba wa rasilimali fedha unaozuia kuwafikia vijana wote wenye vipaji na mawazo bunifu, pamoja na uelewa mdogo wa jamii kuhusu umuhimu wa kuwekeza katika maendeleo ya vijana wabunifu.

“Bado jamii haijaelewa vya kutosha kwamba kama taifa hatuwezi kufikia maendeleo tunayoyataka bila kuwekeza kwa dhati katika vijana wetu, hususan katika sayansi, teknolojia na ubunifu. Tukitazama mataifa yaliyopiga hatua, yamewekeza kwa kiwango kikubwa katika kuwawezesha vijana kufanya utafiti, ubunifu na ugunduzi. Serikali imeweka sera na mazingira mazuri ya kuhamasisha ubunifu, sasa ni wajibu wetu kuungana na kuhakikisha vijana wetu wanapata fursa za kutimiza ndoto zao na kuchangia maendeleo ya Taifa.” Aliongeza Kamugisha

Kwa zaidi ya miaka 16, taasisi ya wanasayansi chipukizi Tanzania (YST) imekuwa ikiwajengea uwezo wanafunzi wa shule za sekondari katika utafiti wa kisayansi na ubunifu kupitia programu za mafunzo na uhamasishaji, zikiwawezesha kutambua changamoto zinazozikabili jamii na kubuni suluhisho zinazotekelezeka na zenye kuendana na mazingira ya Tanzania.

Ushirikiano wa Exim Bank unaimarisha dhamira hiyo kwa kuwaunga mkono vijana wanaobuni suluhisho katika maeneo mbalimbali, ikiwemo akili unde (Artificial Intelligence), kilimo na mifugo, uhifadhi wa mazingira, afya, usalama wa chakula, mawasiliano na ubunifu wa kijamii.

Ikiongozwa na falsafa yake ya "Ubunifu ni maisha", benki ya Exim Tanzania inaendelea kuunga mkono mipango inayofungua fursa kwa vijana wa Kitanzania na kuhamasisha ubunifu wa ndani. Kupitia ushirikiano wa kimkakati na YST, kwa zaidi ya miaka sita sasa toka mwaka 2021, Benki hiyo inaendelea kuwasaidia vijana kutumia elimu na maarifa wanayopata darasani kubuni suluhisho za changamoto halisi zinazoikabili jamii, huku ikikuza utamaduni wa utafiti, ubunifu, ujasiriamali na maendeleo ya teknolojia.

Wakati maandalizi ya Maonesho ya Kitaifa ya Sayansi na Teknolojia ya mwaka 2026 yakiendelea, Benki ya Exim Tanzania na Taasisi ya Wanasayansi Chipukizi Tanzania (YST) wanaendelea kushirikiana kuwawezesha vijana wabunifu ambao mawazo, tafiti na ugunduzi wao vitachangia kujenga Tanzania yenye ubunifu zaidi, ushirikishwaji na ustawi endelevu.
Meneja Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Exim Tanzania, Kauthar D’souza (kushoto), akisalimiana na Mwanzilishi Mwenza wa Taasisi ya Wanasayansi Chipukizi Tanzania (YST), Dkt. Gozibert Kamugisha (kulia), muda mfupi baada ya Benki ya Exim Tanzania na YST kuzindua ushirikiano wa mwaka 2026 kupitia Programu ya YST 2026 jijini Dar es Salaam.

 Ushirikiano huo unaofikisha mwaka wa sita unaendelea kuwawezesha vijana wa Kitanzania kutumia sayansi, utafiti na ubunifu kubuni suluhisho za changamoto za jamii. Kwa mwaka huu, miradi 1,330 kutoka shule 287 za sekondari imewasilishwa, huku miradi 45 bora ikitarajiwa kushiriki Maonesho ya Kitaifa ya Sayansi na Teknolojia ya YST yatakayofanyika tarehe 17 Septemba 2026 katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ambapo kupitia wataalamu wake, Benki ya Exim Tanzania imeshiriki kutoa ulezi na ushauri wa kitaalamu kwa wanafunzi na walimu ili kuboresha tafiti na ubunifu wao. Uzinduzi wa ushirikiano huo umefanyika tarehe 31 Julai 2026 katika Makao Makuu ya Benki ya Exim Tanzania (Ex



WAPENZI wa michezo ya kubashiri na burudani za kasino sasa wana sababu mpya ya kutabasamu baada ya Meridianbet kuleta mchezo mpya kabisa unaovutia hisia za ushindi, Jungle Temple kutoka Expanse. Mchezo huu uliotambulishwa rasmi, umeingia ukiwa na dhamira moja kubwa ya kuwapeleka wachezaji kwenye safari ya kipekee ya msituni iliyojaa siri, mahekalu ya kale na hazina zinazoweza kubadilisha siku yako kwa mzunguko mmoja tu.

Kama wewe ni miongoni mwa wanaopenda michezo yenye mandhari ya kusisimua, michoro ya kisasa na nafasi nyingi za kushinda, basi Jungle Temple ndiyo mchezo ambao hutakiwi kuukosa katika Meridianbet kasino. Ni zaidi ya sloti ya kawaida ikikupa nafasi kusaka utajiri ambapo kila raundi inaweza kuwa mwanzo wa ushindi mkubwa.

Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Mchezo huu umebuniwa kuwafanya wachezaji wajisikie kama wagunduzi wanaopenya ndani ya misitu yenye historia ndefu na mahekalu yaliyofichwa kwa karne nyingi. Kila unapocheza, unafungua ukurasa mpya wa safari iliyojaa alama za siri na zawadi zinazoweza kujitokeza wakati wowote. Mbali na mwonekano wake wa kuvutia, Jungle Temple imebeba vipengele maalum vya bonasi vinavyoongeza msisimko na kukupa nafasi zaidi za kuibuka mshindi.

Kwa Meridianbet, ujio wa Jungle Temple unaongeza chaguo jipya kwenye maktaba ya michezo ya kasino inayozidi kukua kila siku. Wachezaji sasa wana nafasi ya kuwa miongoni mwa watu wa kwanza kuonja ladha ya mchezo huu mpya na kufungua siri zilizojificha ndani ya msitu huu wa ajabu.

Mchezo umeundwa kwa teknolojia ya kisasa inayohakikisha uchezaji laini, michoro yenye ubora wa hali ya juu na sauti zinazokuingiza moja kwa moja kwenye mazingira ya safari ya kutafuta hazina. Hali hiyo huifanya kila raundi kuwa tukio lenye hisia tofauti, huku ukisubiri kuona kama bahati yako itafungua mlango wa bonasi kubwa au ushindi utakaoacha tabasamu usoni. Kwa wapenda michezo yenye mchanganyiko wa burudani na fursa za kushinda, Jungle Temple ni uzoefu unaostahili kujaribiwa.

Kinachoufanya Jungle Temple kuwa wa kipekee si tu mandhari yake ya kuvutia, bali pia uwezo wake wa kuleta msisimko katika kila hatua ya mchezo. Bonasi mbalimbali, nafasi za ushindi zenye nguvu na safari ya kusaka hazina huifanya kila dakika mbele ya skrini kuwa ya kusisimua zaidi. Kwa wale wanaopenda kujaribu bahati yao kwenye michezo mipya, huu ni wakati sahihi wa kuingia ndani ya msitu huu wenye mafumbo na kuona ni zawadi gani zimefichwa kwa ajili yako.

Safari imeanza rasmi, na Meridianbet inakualika uwe sehemu ya uzinduzi huu mkubwa wa Jungle Temple. Ingia Meridianbet leo, chagua mchezo huu mpya wa Expanse na uanze safari yako kuelekea kwenye mahekalu ya kale yanayoficha utajiri mkubwa.

MERIDIANBET wakiwa kama wakali wa ubashiri Tanzania wamekuja na Jackpot ya kibabe haswa ya Bilioni 2 ambayo kwa dau la shilingi 500 tuuh unajiweka kwenye nafasi ya washindi.

Ukiwa na akaunti ya Meridianbet ni rahisi sana kuota ndoto kubwa zaidi na safari hii ni ile Jackpot kubwa kabisa ya Bilioni 2 ambayo ukipatia kwenye mechi zako 14 unajiweka kwenye nafasi kubwa ya kuondoka na mpunga huo.

Wazo la kushinda Bilioni 2 linaweza kuonekana kama ndoto kwa wengi, lakini hapa linakuwa karibu zaidi na uhalisia. Hii siyo fursa inayohitaji uwekezaji mkubwa au maandalizi magumu. Jero moja tu inakuwa tiketi yako ya kuingia kwenye safari ya matumaini, msisimko na uwezekano wa ushindi mkubwa.

Bila intanenti au kwa kubonyeza *149*10# Meridianbet imehakikisha kuwa kila mchezaji anaweza kushiriki bila kikwazo cha intaneti au kifaa cha kisasa. Hii ina maana kwamba popote ulipo, ukiwa na simu yako ya kawaida tu, unaweza kuingia kwenye jackpot na kuanza safari yako ya kuelekea ushindi mkubwa. Jisajili hapa.

Kwa kiasi kidogo sana ambacho karibu kila mtu anaweza kumudu, unaweza kuingia kwenye mashindano ya kutabiri matokeo ya mechi mbalimbali na kujikuta ukiwa kwenye njia ya ushindi mkubwa usiotarajiwa. Jero moja linakuwa tiketi ya matumaini, nafasi ya kujaribu, na mwanzo wa safari ya kuelekea mabadiliko makubwa ya maisha.

Ukiachana na Jackpot hiyo, Meridianbet inakwambia tengeneza mkwanja kupitia michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Hii siyo nafasi ya wachache, bali ni jukwaa la kila mmoja kujaribu bahati yake. Jero moja linaweza kuonekana kuwa dogo, lakini ndani yake linaweza kubeba uwezo wa kubadilisha maisha yako kabisa.

Kubashiri kunapaswa kubaki kuwa burudani, na wachezaji wanahimizwa kuweka mipaka yao ili kuhakikisha wanapata uzoefu chanya bila kuathiri maisha yao ya kila siku.

 

Meneja wa EWURA Kanda ya Magaharibi, Mha. Karim Ally(kushoto) akitoa maelezo ya majukumu yanayotekelezwa na Mamlaka kwa Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, Mh. Dkt. Rashid Chuachua(kulia) ikiwemo utoaji wa leseni na vibali vya ujenzi wa vituo vya mafuta, vituo vya CNG, utatuzi wa migogoro na malalamiko na nafasi ya EWURA katika kuweka mazingira wezeshi ya kupata wasambazaji wakubwa wa gesi ya mitungi ( LPG) katika eneo la Kanda ya Magharibi linalohudumia mikoa ya Tabora, Shinyanga, Katavi na Kigoma, wakati kuongozi huyo alipotembelea banda la EWURA katika maonesho ya NaneNane yanayoendelea viwanja vya Ipuli, Tabora, leo 02/08/2026.

Na.Mwandishi Wetu-Tabora

Wakuu wa Wilaya za Tabora, Mh. Upendo Wella, na Kigoma, Mh. Dkt. Rashid Chuachua, wameipongeza EWURA kwa usimamizi mzuri wa huduma za nishati na maji nchini. Wametoa pongezi hizo walipotembelea banda la EWURA, katika maonesho ya NaneNane yanayoendelea viwanja vya Ipuli, Tabora, leo, 02.08.2026.

Viongozi hao wameitaka EWURA kuongeza hamasa kwa wananchi ili kubadili mtazamo na kuhamia katika matumizi ya nishati safi ya kupikia ili azma ya kufikia 80% ya watumiaji ifikapo 2034 itimie.

Aidha, wameisisitiza EWURA kuendelea kuhamasisha uwekezaji wa vituo vya mafuta maeneo ya vijijini, wakieleza kuwa huduma hiyo inahitajika kutokana na kushamiri shughuli za kilimo, ufugaji na uvuvi.

Meneja wa EWURA Kanda ya Magharibi, Mha. Karim Ally, alitumia fursa hiyo kueleza nafasi ya EWURA ya kuweka mazingira wezeshi ya kupata wasambazaji wakubwa wa gesi ya mitungi (LPG) katika eneo la Kanda ya Magharibi linalohudumia mikoa ya Tabora, Shinyanga, Katavi na Kigoma, ambapo kwa sasa ni 19 pekee.

Meneja wa EWURA Kanda ya Magaharibi, Mha. Karim Ally(kushoto) akitoa maelezo ya majukumu yanayotekelezwa na Mamlaka kwa Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, Mh. Dkt. Rashid Chuachua(kulia) ikiwemo utoaji wa leseni na vibali vya ujenzi wa vituo vya mafuta, vituo vya CNG, utatuzi wa migogoro na malalamiko na nafasi ya EWURA katika kuweka mazingira wezeshi ya kupata wasambazaji wakubwa wa gesi ya mitungi ( LPG) katika eneo la Kanda ya Magharibi linalohudumia mikoa ya Tabora, Shinyanga, Katavi na Kigoma, wakati kuongozi huyo alipotembelea banda la EWURA katika maonesho ya NaneNane yanayoendelea viwanja vya Ipuli, Tabora, leo 02/08/2026.

Meneja wa EWURA Kanda ya Magahribi, Mha. Karim Ally(kulia) akimweleza Mkuu wa Wilaya ya Tabora, Mh. Upendo Wella (kushoto), Mamlaka inavyoendelea kutoa elimu na kuhamasisha ujenzi wa vituo maeneo ya vijijini ambapo uhitaji bado ni mkubwa hususan katika maeneo ya pembezoni na hivyo kuendelea kuwepo uuzaji holela wa bidhaa za petroli, ambao ni hatari kwa afya, mazingira na maisha ya watu, wakati kiongozi huyo alipotembelea banda la EWURA, katika maonesho ya NaneNane, viwanja vya Ipuli, Tabora, leo, 02/08/2026.




Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Needpeace Wambuya, amepongeza kasi ya utekelezaji wa majukumu ya Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB), hususan hatua ya kuanzisha mpango wa kuuza mifugo kupitia Mfumo wa Stakabadhi za Ghala.

Akizungumza alipotembelea banda la WRRB katika Maonesho ya Nanenane yanayoendelea viwanja vya John Malecela jijini Dodoma leo Agosti 2, 2026, Wambuya amesema "Niwapongeze sana, kwa kazi nzuri mnayofanya, nimeona mpango wenu kuingiza mifugo kwenye Mfumo wa Stakabadhi za Ghala, natumai mpo hatua nzuri kwasasa."

Kwa upande wake, Ofisa Leseni wa WRRB, Nasri Khea, amesema maandalizi ya mnada wa kwanza wa mifugo kupitia Mfumo huu yamefikia hatua za mwisho, huku mnada huo ukitarajiwa kufanyika hivi karibuni katika Wilaya ya Mvomero.

Amesema pia mfumo huo unakwenda kuingiza kuwezesha biashara za bidhaa mbalimbali ikiwamo Mwani na mahindi.
*Wananchi wakumbushwa kuchukua Amana zao zilizokuwa Benki ya FBME

Na Mwandishi Wetu, Dodoma
BODI ya Bima ya Amana (DIB) imewataka wananchi kutembelea Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima ya Nane Nane ili kupata elimu kuhusu ulinzi wa amana zao na taratibu za kufidiwa fedha wanazoweka katika benki na taasisi za fedha zilizopewa leseni na Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Akizungumza katika maonesho hayo yanayoendelea katika Viwanja vya Dkt. John Samwel Malecela jijini Dodoma, Mkurugenzi Mkuu wa DIB, Isack Kihwili, amesema wananchi wanapaswa kuhakikisha wanaweka fedha zao katika benki na taasisi za fedha zilizosajiliwa na kupewa leseni na Benki Kuu ya Tanzania.

Amesema kufanya hivyo ni muhimu kwa kuwa kuweka fedha katika taasisi zisizo rasmi kunaweza kuwanyima wananchi haki ya kupata fidia endapo taasisi hizo zitashindwa kutekeleza majukumu yake au kushindwa kurejesha fedha za wenye amana.

Kihwili pia amewataka wenye amana katika iliyokuwa Benki ya FBME ambao bado hawajachukua fedha zao kujitokeza haraka ili kukamilisha mchakato wa malipo, akisema fedha zao bado zinawasubiri.

Amesema DIB imefikia hatua kubwa katika kulipa madai ya wenye amana wa benki hiyo, huku akibainisha kuwa ni asilimia ndogo tu ya walengwa ambao bado hawajajitokeza kuchukua fedha zao.

Kwa mujibu wa Kihwili, madai ya wenye amana wa FBME kwa upande wa Tanzania yalifikia takribani Sh bilioni 35, ambapo hadi sasa zaidi ya asilimia 85 ya fedha hizo tayari zimelipwa kwa walengwa.

Amesema bado kuna takribani watu 428 ambao hawajajitokeza kuchukua fedha zao zenye thamani ya karibu Sh bilioni nne, licha ya fedha hizo kuwa tayari zimetengwa kwa ajili yao.

“Tunawasihi wale ambao bado hawajajitokeza kuchukua fedha zao wafanye hivyo haraka, kwa sababu fedha hizo zimetengwa na zipo tayari kwa ajili ya malipo,” amesema.

Amefafanua kuwa baada ya kundi hilo kujitokeza na kulipwa fedha zilizotengwa kwa ajili yao, hatua inayofuata itakuwa ni kulipa asilimia 15 iliyobaki ili kuhakikisha kila mwenye amana anayestahili fidia analipwa madai yake kwa asilimia 100, kwa kuzingatia taratibu zinazotumika.


Aidha, Kihwili amesema bado kuna kundi la wadai wengine, wakiwemo baadhi ya wafanyakazi waliokuwa na madai yaliyofikishwa mahakamani, ambao malipo yao hayajahusishwa katika awamu inayoendelea kutokana na mchakato wa kufuatilia na kuhakiki mali za benki hiyo.

Amesema DIB inaendelea kufuatilia mali zilizobaki za benki hiyo ili kuhakikisha fedha za kutosha zinapatikana na kuwezesha kukamilishwa kwa malipo ya wadai hao kwa kuzingatia taratibu za kisheria.

Na Mwandishi Wetu, Dodoma
MAMLAKA ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) imesema Maonesho ya Kilimo na Mifugo ya Nane Nane ni fursa muhimu kwa wakulima kupata elimu na taarifa zitakazowasaidia kujiandaa kwa msimu wa kilimo wa mwaka 2026/2027.

Akizungumza katika Maonesho ya Kilimo na Mifugo ya Nane Nane yanayoendelea katika Viwanja vya Dkt. John Malecela jijini Dodoma, Mkurugenzi wa Huduma za Udhibiti Ubora wa TFRA, Happiness Mbelle, amesema wakulima wanapaswa kuhakikisha taarifa zao zimesajiliwa na kuhuishwa kwa wakati ili kuepuka changamoto wakati wa usambazaji wa mbolea.

Amesema mbolea inapatikana kwa kiasi cha kutosha, huku akiwataka wakulima kushirikiana na maafisa ugani katika kupima udongo ili kubaini mahitaji sahihi ya mbolea kulingana na aina ya mazao na hali ya udongo.

“Mkulima anapaswa kushirikiana na maafisa ugani kupima udongo ili kubaini mahitaji ya mbolea. Hii itasaidia kutumia mbolea kwa usahihi na kuongeza tija katika uzalishaji,” amesema Mbelle.

Aidha, amesema maonesho hayo ni fursa kwa wananchi kutoka maeneo mbalimbali nchini kupata elimu kuhusu matumizi sahihi ya mbolea, pamoja na huduma na majukumu ya TFRA.

Amesema TFRA itaendelea kutoa elimu kwa wananchi katika maeneo mbalimbali nchini ili kuwawezesha kuelewa majukumu ya mamlaka hiyo na kuhakikisha wanapata huduma bora zenye viwango.

Mbelle amewataka wakulima kutumia fursa ya maonesho hayo kupata elimu na ushauri kutoka kwa wataalamu ili kuongeza ufanisi na tija katika shughuli za kilimo.

Na Mwandishi Wetu, Dodoma
BARAZA la Taifa la Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) limesema Maonesho ya Kilimo na Mifugo ya Nane Nane ni fursa muhimu ya kutoa elimu kwa wanafunzi na wahitimu wa vyuo vya kati vinavyotoa mafunzo katika fani za kilimo na mifugo kuhusu fursa za kujiajiri katika sekta hizo.

Akizungumza katika Maonesho ya Kilimo na Mifugo ya Nane Nane yanayoendelea katika Viwanja vya Dkt. John Malecela, jijini Dodoma, Afisa Udhibiti Ubora wa NACTVET, Doris Chiwambo, amesema sekta ya kilimo ina fursa kubwa za ajira na kujiajiri, hivyo wahitimu wa fani za kilimo na mifugo wanapaswa kutumia ujuzi walioupata kuanzisha shughuli za uzalishaji.

Amesema wahitimu hao wanaweza kujiajiri kupitia shughuli mbalimbali ikiwemo kilimo, ufugaji na utoaji wa elimu na huduma za kitaalamu katika sekta hizo.

“Sekta ya kilimo ina fursa nyingi za ajira na kujiajiri. Wahitimu wa fani za kilimo na mifugo wanaweza kutumia elimu na ujuzi walioupata kujiajiri katika kilimo, ufugaji na hata kutoa elimu kwa jamii,” amesema Chiwambo.

Aidha, amesema maonesho hayo ni fursa pia kwa wananchi wanaopanga kuanzisha vyuo vinavyotoa mafunzo ya kilimo, mifugo na uvuvi kupata elimu na maelekezo kuhusu taratibu na vigezo vya kuanzisha na kuendesha vyuo hivyo.

Chiwambo amesema NACTVET itaendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu majukumu yake, pamoja na kuhakikisha jamii inaelewa huduma zinazotolewa na baraza hilo ili kufanikisha lengo la kutoa elimu na mafunzo yenye viwango vinavyokidhi mahitaji ya soko la ajira.

Ameongeza kuwa ushiriki wa NACTVET katika maonesho hayo unalenga kuongeza uelewa kwa wananchi kuhusu umuhimu wa elimu na mafunzo ya ufundi stadi, pamoja na fursa zinazopatikana kupitia taaluma za kilimo, mifugo na uvuvi.

 

MKUU wa Kampasi ya Dodoma wa Chuo cha Uhasibu Arusha,Prof. Epaphra Manamba,akizungumza na waandishi wa habari leo Agosti 2,2026 kwenye banda la chuo hicho akimwakilisha Mkuu wa Chuo, Profesa Eliamani Sedoyeka,wakati wa Maonesho ya 49 ya Kilimo ya Nane Nane yanayoendelea katika viwanja vya Dkt. John Samuel Malecela Nzuguni jijini Dodoma kwa niaba ya 

.....

MKUU wa Kampasi ya Dodoma wa Chuo cha Uhasibu Arusha,Prof. Epaphra Manamba,amesema wanaendelea kuandaa wataalamu wenye ujuzi na uwezo wa kutumia teknolojia za kisasa katika uzalishaji, usimamizi na biashara ya mazao, hatua itakayochangia kuongeza tija, ushindani na thamani ya sekta ya kilimo nchini.

Akizungumza katika Maonesho ya 49 ya Kilimo ya Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Dkt.John Malecela Nzunguni jijini Dodoma, Mkuu wa Kampasi ya Dodoma wa Chuo cha Uhasibu Arusha, Prof.Epaphra Manamba, akimwakilisha Mkuu wa Chuo, Profesa Eliamani Sedoyeka, amesema IAA imeamua kushiriki maonesho hayo ili kuwa karibu na wakulima, kutoa elimu na kuonesha mchango wa taaluma katika kuimarisha uzalishaji wa kilimo nchini.

Amesema sekta ya kilimo ndiyo uti wa mgongo wa uchumi wa Tanzania kwa kuwa inategemewa na takribani asilimia 65 ya nguvu kazi ya Taifa, lakini bado mchango wake katika Pato la Taifa ni takribani asilimia 26 pekee, hali inayoonesha kuwa kuna nafasi kubwa ya kuongeza tija kupitia matumizi ya maarifa, teknolojia na usimamizi bora wa biashara.

"Kilimo kinahitaji nguvu kazi yenye ujuzi, ubunifu na maarifa ya kisasa. Ndiyo maana Chuo cha Uhasibu Arusha kinaendelea kutoa programu mbalimbali za biashara, uchumi, fedha na teknolojia ili kuwajengea uwezo wataalamu watakaosaidia kuifanya sekta ya kilimo iwe yenye ushindani na yenye mchango mkubwa zaidi katika uchumi wa Taifa," amesema Prof.Manamba.

Ameeleza kuwa pamoja na changamoto za mitaji zinazowakabili wakulima wengi pamoja na utegemezi wa zana duni za kilimo, bado kuna fursa kubwa ya kuongeza uzalishaji endapo wakulima wataunganishwa na taasisi za kifedha pamoja na huduma za kitaalamu zitakazowezesha upatikanaji wa mitaji na uwekezaji katika teknolojia za kisasa.

Prof.Manamba amesema IAA imejikita pia katika kufundisha teknolojia zinazoibukia ikiwemo Akili Unde (Artificial Intelligence - AI), ambapo wanafunzi wa chuo hicho tayari wamebuni mifumo inayotumia AI kuboresha uzalishaji wa mazao kama vitunguu kwa lengo la kuongeza tija, kupunguza gharama za uzalishaji na kuifanya kilimo kuwa biashara yenye faida zaidi.

"Hatutaki kuona kilimo kinabaki kwa ajili ya kujikimu pekee. Tunataka wakulima walime kwa mtazamo wa biashara, waongeze thamani ya mazao yao na kuongeza kipato cha familia zao pamoja na kuchangia zaidi katika uchumi wa Taifa," amsisitiza.

Akizungumzia kaulimbiu ya Nanenane ya mwaka huu isemayo "Tambua Soko, Ongeza Tija, Tekeleza Dira ya Taifa 2050," Prof.Epaphra Manamba amesema dira hiyo inalenga kujenga nguvu kazi yenye ujuzi na maarifa inayoweza kuleta mapinduzi katika sekta mbalimbali za uchumi, hususan kilimo.

Amebainisha kuwa taasisi za elimu zina jukumu la kuhakikisha zinatoa wahitimu wenye ujuzi unaoendana na mahitaji ya soko la ajira na mabadiliko ya teknolojia ili kuongeza ufanisi katika uzalishaji na kuifanya Tanzania kufikia malengo ya maendeleo ya Dira ya Taifa 2050.

Amesema kupitia ushiriki wa Maonesho ya Nanenane, Chuo cha Uhasibu Arusha kinaendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu programu zake mbalimbali na namna zinavyoweza kuwaandaa vijana kuwa wataalamu watakaochangia maendeleo ya kilimo, biashara na uchumi wa kidijitali nchini.


Top News