Na Said Mwishehe,Michuzi TV
BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam limekutana katika kikao maalum kilichokuwa na lengo la kutekeleza maagizo ya Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kuhusu kutafuta ufumbuzi wa changamoto ya uchafu katika Jiji hilo.
Katika kutekeleza maagizo hayo pamoja na mambo mengine kikao hicho kilichoongozwa na Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Nurdin Bilal maarufu Shetta pamoja na Katibu wa kikao hicho ambaye ni Mkurugenzi wa Jiji hilo Elihuruma Mabelya wamekubaliana kushirikisha sekta binafsi kupitia mpango wa PPP kuendesha dampo la Pugu kinyamwezi ambalo kwa sasa limezidiwa.
Katika kikao hicho maalum kilichofanyika leo Septemba 4,2026 Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Elihuruma Mabelya amewasilisha mpango wa kushirikiaha sekta binafsi kusimamia dampo la Pugu Kinyamwezi ambalo ndilo linatumika kutupwa taka zote zinazozalishwa katika Jiji hilo.
“Kumekuwa na mpango mkakati wa Jiji la Dar es salaam unaotaka asilimia 80 ya taka zipelekwe dampo la Pugu na ukweli mpango huo umefeli.Kutokana na ongezeko la watu katika Jiji la Dar es Salaam umefika wakati wa kushirikisha sekta binafsi kupitia PPP ili kupata suluhu ya kudumu.”
Akifafanua zaidi katika kikao hicho Mabelya amesema maagizo yaliyotolewa na Rais Dk.Samia Suluhu Hassan yanapaswa kutekelezwa kwa haraka na jambo muhimu zaidi kuwa na suluhu ya kudumu.
“Tumepokea maagizo ya Rais Samia lakini pia Spika wa Bunge ameonesha kutoridhishwa n hali ya usafi katika Jiji la Dar es Salaam.Tumewasikia viongozi wetu na tumechukua hatua mbalimbali na leo tumekutana katika kikao maalum kujadili maagizo tuliyopewa.”
Kuhusu taka zinazozalishwa katika Jiji la Dar es Salaam amesema kwa siku zinazalishwa kiasi cha taka tani 1320 kwa siku na zinazopelekwa dampo la Pugu ni tani 792 pekee wakati taka zinaozalishwa katika halmashauri zote ni kati ya tani 2500 hadi 3000 kwa siku.”Taka nyingi bado zipo mtaani na zinaathiri wanannchi kiafya na mazingira.”
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Ilala Edward Mpogolo amepongeza kufanyika kikao hicho kutekeleza maagizo ya Rais na kusisitiza Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam linamshukuru Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kwa kusema ukweli kuhusu hali ya usafi katika Jiji hilo.
“Ni heshima kubwa kwa Kiongozi akishatoa maagizo kuona maagizo yanatekelezwa.Niwapongeze Baraza l madiwani kwa kikao hichi kilichokutana kutekeleza maagizo tuliyopewa.”
Pamoja na hayo amesema changamoto ya dampo la Pugu halmashauri imekuwa inatumia nguvu nyingi katika dampo hilo na mashine za kushusha taka zimekufa.
“Mtu anayekwambia ukweli anakupenda,hali ni mbaya.Heka 400 kabla ya kuingia dampo taka kila mahali na kwa miaka minne kumekuwa na siasa nyingi kuhusu dampo hilo..Nawapongeza kwa kutekeleza agizo la Rais Samia Suluhu Hassan.
“Spika amesema bungeni wapi ambapo wakandarasi wanakwamisha.Tunajua mpango huu mzuri wa kushirikisha sekta binafsi katika dampo letu kuna watu watanuna kwa maslahi yao binafsi. Hivyo kazi ambayo imebakia ni watalaam kukaa na kuona jinsi mikataba itakavyokuwa kwani kuingia PPP kuna mikataba ya kisheria .
“Rais amezungumza miaka yote tunakwenda tunarudi nyuma jambo halifiki mwisho kama tumekanyaga mdudu.Sasa twendeni tukatekeleze mpango huu wa dampo na dira ya 2050 inaeleza umuhimu wa kushirikisha sekta binafsi katika kutekeleza mipango ya Serikali.”
“Leo tunashuhudia maelfu ya wananchi wakirejeshewa matumaini ya kuona. Ushirikiano huu umeonesha kuwa tukifanya kazi pamoja tunaweza kusogeza huduma za kibingwa karibu na wananchi na kupunguza adha ya kusafiri kutafuta matibabu." amesema Mhe. Abdalla
Hati hiyo imesainiwa leo, Septemba 4, 2026, jijini Dodoma na Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA Anthony Kasore, pamoja na Meneja Mkuu wa Kampuni ya Van Mo, Fathi Ahmed.
Ushirikiano huo unalenga kuhakikisha mafunzo ya ufundi stadi yanaendana na mahitaji ya sekta ya viwanda na biashara, huku wahitimu wakijengewa umahiri, ubunifu, tija, maadili na uelewa wa usalama kazini, Van Mo pia itatoa fursa za mafunzo kwa vitendo na ajira kwa wahitimu wenye sifa zinazokidhi mahitaji yake.
Maeneo yatakayohusika katika makubaliano hayo ni pamoja na udereva wa magari makubwa, usimamizi wa vyombo vya usafiri, uchukuzi na uhifadhi wa mizigo, usimamizi wa mnyororo wa ugavi, ukaguzi na ukarabati wa magari pamoja na mifumo ya umeme na elektroniki ya magari.
Maeneo mengine ni uendeshaji wa maghala na usimamizi wa stoo, uendeshaji wa vituo vya mafuta, ujenzi na usimamizi wa majengo na miundombinu, shughuli za utalii na ukarimu, pamoja na kilimo na uhifadhi wa mazao.
Katika mashauriano ya awali yaliyofanyika Agosti 31, 2026, Mkuu wa Uzingatiaji wa Sheria, Kanuni na Taratibu wa Van Mo, Hamis Lugusha, alisema kampuni hiyo ina mahitaji makubwa ya madereva kutokana na ongezeko la magari, akieleza kuwa mwaka huu imepokea magari mapya 100 yanayohitaji madereva, huku magari mengine 150 yakitarajiwa kuongezwa mwakani.
Lugusha alisema pamoja na mahitaji hayo, kampuni imekuwa ikipata changamoto ya kupata madereva wanaokidhi viwango vinavyohitajika, hasa katika uadilifu, uaminifu, uwajibikaji na utamaduni wa kazi, hali hiyo imeifanya kampuni kuona umuhimu wa kushirikiana na VETA katika kuwaandaa madereva kuanzia misingi ya taaluma na maadili.
Kwa upande wake, CPA Kasore alisema programu hiyo inaweza kuwahusisha waombaji wenye mafunzo na wasio na mafunzo ya udereva, huku wenye uzoefu wakitakiwa kuchujwa kwa kuzingatia historia ya utendaji wao, alisema hatua hiyo itasaidia kupata waombaji ambao uzoefu wao unaendana na tabia na viwango vinavyohitajika na mwajiri.
Naye Mkurugenzi wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, Dkt. Abdallah Ngodu, alipendekeza ushirikiano huo utekelezwe kupitia mfumo wa uanagenzi, utakaowezesha Van Mo kushiriki katika kuwajenga wanafunzi kupitia mazingira halisi ya kazi, pamoja na kuwapa misingi ya nidhamu, uwajibikaji na utamaduni unaohitajika katika sekta ya usafirishaji.
Katika utekelezaji wa hati hiyo, VETA itatoa au kuwezesha programu za mafunzo, kushiriki katika uandaaji na mapitio ya mitaala, tathmini na utoaji wa vyeti vya umahiri, wakati Van Mo itatoa taarifa kuhusu mahitaji ya ujuzi, fursa za mafunzo kazini, mrejesho wa utendaji wa wanafunzi na wahitimu, pamoja na ajira kwa watakaokidhi vigezo vya kampuni.
.jpeg)


.jpeg)

Na Mwandishi Wetu
MKUU wa Shughuli za serikali (Chief of Staff) wa Ghana Dkt Julius Debras ametoa wito kwa nchi za Afrika kuangalia kwa namna gani rasilimali zilizopo zinaweza kujitosheleza kama bara hususani katika sekta ya nishati.
Dkt Debras ametoa wito huo katika wiki ya mafuta Afrika inayoendelea Accra Ghana wakati wa hotuba yake akimwakilisha Rais wa nchi hiyo John Dramani Mahama.
Amesema kuwa endapo bara la Afrika litakuwa na nishati ya uhakika itasaidia kuinua uchumi lakini swala la ajira pia halitakuwa wimbo kwani kutakuwa na maendeleo ya uhakika ya viwanda.
Ameweka bayana kuwa kwa upande wa Mkondo wa Juu wa Petroli wa Ghana, serikali imeweka mikakati mathubuti kuhakikisha kupitia sekta hiyo wanapata wawekezaji wenye uhakika.
Amesema ni lazima kama bara la Afrika kuangalia aina ya wawekezaji wanaokuja kuwekeza katika nishati ni lazima wawe na nguvu ya kiuchumi ili kuweza kuleta manufaa ya uhakika na haraka katika sekta hiyo.
Kwa upande wake Kamishna wa Miundombinu na Nishati kutoka Kamisheni ya Umoja wa Afrika Lerato Mataboge amesema vijana wa Afrika wapo tayari katika mabadiliko ya nishati yanayoendelea barani Afrika.
Amesema kinachotakiwa hivi sasa ni mshikamano wa Afrika kuweka njia madhubuti katika kuhakikisha kuwa katika kuelekea maendeleo hayo kuwe na mabadiliko makubwa katika matumizi ya teknolojia kwa kutoa vipaumbele katika bunifu zote zinazofanywa na vijana wa Afrika.
Ameweka bayana kuwa Umoja wa Afrika umeweka utengamano wa viwanda ili kuhakikisha kuwa kunakuwa na ushirikiano wa kikanda katika sekta ya nishati ambao baadaye utaleta tafsiri sahihi ya kuwa na nishati ya uhakika katika bara zima.
Wiki ya Mafuta barani Afrika imeanza Septemba 01 hadi 03 ambapo Tanzania imewakilishwa na wajumbe kutoka Wizara ya Nishati, wajumbe kutoka Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA), na wajumbe kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa Petroli Zanzibar (ZPRA).
Na Janeth Raphael – MichuziTv - Bungeni Dodoma
SERIKALI imesema maandalizi ya Tanzania kuwa mwenyeji wa Mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027 yanaendelea kwa kasi, huku ikihakikisha miundombinu muhimu ya michezo na huduma wezeshi inakamilishwa kwa wakati.
Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, amesema hayo leo, Ijumaa, Septemba 4, 2026, jijini Dodoma, wakati akiwasilisha hoja ya kuahirisha Bunge la 13, Mkutano wa Nne.
Amesema kazi zinazoendelea zinahusisha ujenzi na ukarabati wa viwanja vya mashindano na mazoezi, barabara zinazounganisha maeneo ya viwanja, pamoja na kuhakikisha upatikanaji wa huduma muhimu za afya, maji na umeme.
Kwa upande wa viwanja, Dkt. Mwigulu amesema ujenzi wa Uwanja wa Jiji la Arusha umefikia zaidi ya asilimia 91, huku ujenzi wa uwanja mwingine wenye uwezo wa kuchukua zaidi ya watazamaji 32,000 ukiendelea.
Amesema kwa upande wa Dar es Salaam, ukarabati wa Uwanja wa Benjamin Mkapa pamoja na viwanja vya mazoezi umekamilika, hatua inayoongeza utayari wa jiji hilo katika maandalizi ya mashindano hayo.
Kwa upande wa Zanzibar, Serikali imeeleza kuwa Uwanja wa Fumba unaendelea katika hali nzuri, huku miundombinu mingine ikiwemo New Amaan Complex, Amaan Annex One na Annex Two ikiwa imekamilika. Aidha, Uwanja wa Amaan umeelezwa kuwa katika hali nzuri kwa matumizi ya mashindano.
Dkt. Mwigulu amewataka wasimamizi wa miradi kuhakikisha fedha zinazowekezwa katika maandalizi ya AFCON 2027 zinazalisha thamani inayolingana na uwekezaji huo, akisisitiza kuwa Tanzania inapaswa kutumia nafasi ya kuwa mwenyeji wa mashindano hayo kupata manufaa ya kiuchumi.
Amesema wizara na taasisi zinazohusika zinapaswa kuendelea kuratibu mikakati itakayowezesha Tanzania kunufaika kikamilifu na fursa zitakazotokana na uenyeji wa mashindano hayo, huku akiwataka wadau wote kushiriki kikamilifu ili kuepusha vikwazo vinavyoweza kupunguza ufanisi na manufaa yanayotarajiwa.
Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesisitiza umuhimu wa Tanzania kuwa na timu ya taifa yenye ushindani wakati wa mashindano hayo, akisema mwenyeji hapaswi kuwa mshiriki wa kawaida au “msindikizaji”.
“Sisi ni wenyeji wa mashindano, hivyo tunapenda kuona timu ya taifa pia inakuwa na ubora na sio msindikizaji,” amesema Dkt. Mwigulu.
Amewataka makocha, Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na benchi la ufundi kuanza mapema kuweka mikakati maalumu itakayoiwezesha timu ya taifa kufanya vizuri katika AFCON 2027.
Tanzania itakuwa miongoni mwa wenyeji wa AFCON 2027 pamoja na Kenya na Uganda, hali inayoiweka nchi katika nafasi ya kutumia mashindano hayo kukuza sekta ya michezo, utalii, biashara na shughuli nyingine za kiuchumi.
WAZIRI Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, ameiagiza Wizara ya Madini kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu–TAMISEMI, kuchukua hatua za haraka kukabiliana na changamoto zinazokwamisha ufanisi wa sekta ya madini, ikiwemo tozo zinazotozwa zaidi ya viwango vilivyoainishwa kisheria.
Dkt. Mwigulu ametoa agizo hilo leo Septemba 4, 2026, wakati akilihutubia Bunge kabla ya kuahirishwa kwa shughuli zake hadi Oktoba 27, 2026, akisisitiza kuwa sekta ya madini imeendelea kuwa miongoni mwa sekta muhimu zinazochangia kwa kiasi kikubwa katika ukuaji wa uchumi na mapato ya Taifa.
Amesema mafanikio yaliyopatikana katika sekta hiyo yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na mageuzi yanayoendelea kufanywa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, pamoja na ushiriki wa wadau mbalimbali wa sekta ya madini.
“Sekta ya madini imekuwa moja ya sekta kinara inayochangia katika mapato ya Taifa,” amesema Dkt. Mwigulu.
Amesema pamoja na mchango wa wachimbaji wakubwa, wachimbaji wadogo wameendelea kuongeza uzalishaji wa madini siku hadi siku, hali ambayo imechangiwa na juhudi za Serikali katika kuweka mazingira wezeshi kwa Watanzania kushiriki na kunufaika na rasilimali hizo.
Hata hivyo, Dkt. Mwigulu amesema Serikali inatambua kuwa bado kuna changamoto zinazohitaji kushughulikiwa ili kuongeza ufanisi wa sekta hiyo, akitaja miongoni mwa changamoto hizo kuwa ni baadhi ya tozo zinazowatozwa wachimbaji wa madini katika maeneo mbalimbali.
Amesema baadhi ya tozo hizo zinahusisha malipo ya huduma yanayozidi kiwango kilichoainishwa katika Sheria ya Madini, hali ambayo imekuwa ikileta malalamiko miongoni mwa wachimbaji.
“Kwa mujibu wa sheria, kuna viwango vilivyowekwa. Hivyo, niwaelekeze Wizara ya Madini pamoja na Wizara ya Fedha na Ofisi ya Waziri Mkuu–TAMISEMI wakae kwa haraka kuziangalia changamoto hizo,” amesema.
Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ameitaka Wizara ya Madini kuchukua hatua kali kwa watu wanaoshikilia leseni za uchimbaji kwa muda mrefu bila kuendeleza maeneo waliyopewa, akisema hali hiyo inawanyima Watanzania wengine, hususan vijana na wachimbaji wadogo, fursa ya kushiriki katika shughuli za uchimbaji.
Amesema kushikilia leseni bila kuendeleza maeneo husika ni kinyume na matakwa ya sheria na kwamba Serikali haiwezi kuruhusu maeneo yenye rasilimali kubaki bila kuzalisha huku wananchi wengine wakikosa fursa za kuyatumia.
“Yeyote anayetaka leseni yake isifutwe, atimize masharti yaliyowekwa kwenye leseni, aiendeleze na awape nafasi vijana wengine wa Kitanzania kufanya shughuli za uchimbaji,” amesisitiza.
Dkt. Mwigulu amemwelekeza Waziri wa Madini kuchukua hatua za kisheria, ikiwemo kufuta vibali na leseni za wale watakaokiuka masharti na kugawa upya maeneo hayo kwa Watanzania wenye uwezo na nia ya kuyaendeleza.
Amesema hatua kama hizo tayari zimewahi kuchukuliwa na Rais Samia katika maeneo mbalimbali nchini, ambapo leseni zilizoshikiliwa bila kuendelezwa zilifutwa na maeneo hayo kupewa waombaji wengine.
Waziri Mkuu, amesema hatua hizo zimekuwa miongoni mwa sababu zilizochangia kuongezeka kwa uzalishaji, mapato na mchango wa sekta ya madini katika uchumi wa Taifa.
Amesema Serikali itaendelea kusimamia sekta hiyo kwa kuhakikisha rasilimali za madini zinatumika ipasavyo na kutoa manufaa kwa Taifa pamoja na kutoa fursa kwa Watanzania, hususan vijana na wachimbaji wadogo, kushiriki kikamilifu katika shughuli za uchimbaji.
Na Janeth Raphael - MichuziTv
MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imeendelea kuimarisha mafunzo yanayolenga kuwaandaa Watanzania wenye ujuzi unaoendana na mahitaji ya sekta ya madini, ikiwemo teknolojia za kisasa zinazotumika katika uchimbaji na uchakataji wa madini.
Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA Anthony Kasore, amesema sekta ya madini ni miongoni mwa sekta muhimu katika uchumi wa Tanzania kutokana na mchango wake katika pato la Taifa, uwekezaji, ajira pamoja na maendeleo ya viwanda vinavyoongeza thamani ya rasilimali za nchi.
Akizungumza na wanahabari jijini Dodoma Septemba 4, 2026, Kasore amesema maendeleo ya sekta ya madini hayawezi kutegemea uwepo wa rasilimali pekee, bali yanahitaji pia wataalamu wenye uwezo wa kutumia, kutengeneza na kusimamia teknolojia na mitambo inayotumika katika migodi ya kisasa.
Amesema kwa kutambua umuhimu wa kujenga nguvu kazi yenye ujuzi katika sekta hiyo, mwaka 2008 VETA kwa kushirikiana na Chemba ya Migodi Tanzania (TCM) ilianzisha Programu ya Mafunzo ya Ufundi kwa Shughuli za Uchimbaji Madini (Integrated Mining Technical Training - IMTT) katika Chuo cha VETA Moshi.
Kupitia programu hiyo, VETA imekuwa ikitoa mafunzo katika fani mbalimbali zinazohitajika kwenye sekta ya madini, zikiwemo Heavy Moving Equipment Mechanics, Fitting and Machining, Plater Welding, Auto Electrical na Industrial Electrical Installation.
Kasore,amesema tangu kuanzishwa kwa programu hiyo, zaidi ya vijana 1,688 wamepata mafunzo huku jumla ya kampuni 17 zikishiriki katika utekelezaji wa programu hiyo.
Hata hivyo, amesema mabadiliko ya teknolojia katika sekta ya madini yamelazimu VETA kuendelea kuboresha mafunzo yake ili kuhakikisha ujuzi unaotolewa unaendana na mahitaji halisi ya migodi ya kisasa, hususan matumizi ya mitambo ya uchimbaji chini ya ardhi.
Katika hatua hiyo, VETA kwa kushirikiana na TCM imeandaa mitaala sita mipya ya mafunzo ya uchimbaji madini chini ya ardhi, ambayo inalenga kuwaandaa vijana katika matumizi na uendeshaji wa vifaa na mitambo ya kisasa.
Mitaala hiyo inahusisha Bogger Equipment Operation, Jumbo Equipment Operation, Long Hole Drill Rig, Cubex (ITH) Equipment Operation, Underground Charge-Up Operation pamoja na Lifting and Rigging Operations.
Kasore amesema mafunzo hayo yanalenga kuhakikisha kuwa ukuaji wa sekta ya madini unatoa nafasi kubwa zaidi kwa Watanzania wenye ujuzi kushiriki katika shughuli mbalimbali za uchimbaji, huku wakinufaika na fursa za ajira zinazotokana na maendeleo ya sekta hiyo.
Aidha, VETA inaendelea kutekeleza Mradi wa Madini Muhimu (Critical Minerals Project) kwa kushirikiana na taasisi za GTK na REDU Edu kutoka Finland, pamoja na ASNL ya Tanzania inayowakilisha sekta binafsi.
Mradi huo unatarajiwa kuwafikia vijana wapatao 400 kupitia mafunzo yanayohusu uchimbaji, uchakataji pamoja na ukuzaji wa mnyororo wa thamani katika sekta ya madini muhimu.
Kasore amesema hatua za awali za mradi huo tayari zimeanza, ambapo wakufunzi 25 wa VETA wamepatiwa mafunzo ya wiki sita nchini Finland na kwa sasa wanaendelea kupata mafunzo katika migodi mbalimbali nchini Tanzania kwa lengo la kuongeza uelewa wa mazingira na mahitaji ya sekta hiyo nchini.
Amesema hatua hiyo ni muhimu katika kujenga uwezo wa VETA kutoa mafunzo yanayokidhi mahitaji mahsusi ya uchimbaji na uchakataji wa madini muhimu, sambamba na kuongeza ushiriki wa Watanzania katika mnyororo wa thamani wa sekta hiyo.
Mkurugenzi huyo amewataka wadau wa sekta ya madini, hususan kampuni za uchimbaji, watengenezaji na wasambazaji wa mitambo na vifaa vya migodini pamoja na taasisi nyingine zinazohusika katika mnyororo wa thamani, kuendelea kushirikiana na VETA katika kuandaa rasilimali watu yenye ujuzi unaohitajika.
Amesema ushirikiano huo utasaidia kuongeza ushiriki wa Watanzania katika sekta ya madini, kuimarisha matumizi ya teknolojia za kisasa na kuhakikisha ukuaji wa sekta hiyo unaendelea kuchangia katika ajira, uzalishaji na maendeleo ya Taifa.
Timu ya EASA ilieleza kuridhishwa kwake na maendeleo na juhudi zilizooneshwa na TCAA wakati wa ziara hiyo ya siku tatu. Aidha, timu hiyo ilitambua maendeleo yaliyofikiwa na kuhimiza TCAA kuendeleza kasi katika kushughulikia masuala yote muhimu ya usimamizi wa usalama wa anga.
Kwa upande wake Mkuu wa Ujumbe wa Umoja wa Ulaya alithibitisha dhamira ya EU ya kuendelea kuisaidia Tanzania kupitia msaada wa kitaalamu, mbinu za utekelezaji wa vitendo na kubadilishana ujuzi. Aidha, alieleza kuwa Umoja wa Ulaya umetenga Euro milioni 2 kwa ajili ya msaada unaohusiana na kuboresha zaidi Masuala ya usafiri wa anga nchini.
Ujumbe wa EASA uliongozwa na Bw. Jose Miguel Manso Angulo akiambatana na Bw. Gustavo Juan Roman Barba na Bw. Antonio Portales Pelaez.
Ujumbe huo, uliofika nchini kwa siku tatu kuanzia tarehe 1 hadi 3 Septemba 2026, ulifuatilia maendeleo ya Nchi (State) katika utekelezaji wa hatua za marekebisho pamoja na kuimarisha usimamizi wa usalama wa Usafiri wa anga.
Ujumbe huo ni sehemu ya juhudi zinazoendelea za Tanzania za kuimarisha usimamizi wa usalama wa Usafiri wa anga na kuonesha maendeleo endelevu kuelekea kutimiza matakwa ya kuondolewa kwenye Orodha ya Usalama wa Anga ya Umoja wa Ulaya (European Union Air Safety List).

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Dkt. Jabiri K. Bakari akizungumza wakati wa kikao cha kuhitimisha ujumbe wa timu wataalam kutoka Shirika la Usalama wa Anga la Umoja wa Ulaya (EASA).

Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki (Mb), amesema Tanzania inaendelea kuweka mazingira wezeshi ili wananchi wote wapate huduma za mawasiliano zilizo jumuishi, nafuu, salama na zenye uhakika, sambamba na kuimarisha ujuzi wa kidijitali na matumizi yenye tija ya teknolojia.
Waziri Kairuki ameyasema hayo wakati akishiriki Mkutano wa Saba wa Jukwaa la Sera za Mawasiliano na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (WTPF-26), unaofanyika Nassau, Bahamas, ambapo amesema hatua hizo zinalenga kutekeleza Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050 na Mkakati wa Taifa wa Uchumi wa Kidijitali 2024–2034.
Amesema Tanzania imekamilisha ujenzi wa minara 758 ya teknolojia ya 4G, hatua iliyowezesha zaidi ya vijiji 1,400 na takribani wananchi milioni 8.5 waliokuwa hawapati huduma za mawasiliano ya uhakika kuunganishwa na huduma hizo.
Aidha, kupitia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Serikali imeanzisha Vilabu vya Kidijitali 800 kwa ajili ya kujenga ujuzi wa TEHAMA, kuwezesha huduma za Wi-Fi katika maeneo 100 ya umma na kujenga maabara za kompyuta katika shule 250 za umma, zikiwemo huduma zinazozingatia mahitaji ya wanafunzi wenye ulemavu.
Akieleza vipaumbele vya Tanzania katika kuziba pengo la kidijitali, Waziri Kairuki amesema nchi inalenga kupanua huduma za mawasiliano kwa gharama nafuu, kuongeza ujuzi wa kidijitali na matumizi ya Akili Unde (AI), pamoja na kuendeleza miundombinu ya kidijitali iliyo salama, jumuishi na inayolinda taarifa binafsi za watumiaji.
Waziri Kairuki amesema Tanzania iko tayari kushirikiana na Umoja wa Kimataifa wa Mawasiliano (ITU) na wadau wengine wa maendeleo kuimarisha ujuzi wa kidijitali na matumizi ya Akili Unde barani Afrika. Amesisitiza kuwa mafanikio ya mageuzi ya kidijitali hayapaswi kupimwa kwa idadi ya minara pekee, bali kwa namna teknolojia inavyoboresha maisha, kuongeza fursa za kiuchumi na kijamii na kuhakikisha hakuna anayebaki nyuma katika uchumi wa kidijitali.











.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)








.jpeg)






.jpeg)








.jpg)