

SERIKALI imedhamiria kuendelea kuimarisha afua za masuala ya UKIMWI nchini kwa kuboresha mazingira ya utekelezaji wa shughuli hizo, huku ikihimiza ushirikiano na wadau mbalimbali katika kuendeleza mapambano dhidi ya UKIMWI.
Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Dkt. Jim Yonazi, alipotembelea na kujionea utekelezaji wa shughuli zinazotekelezwa na vikundi vya watu wanaoishi na Maambukuzi ya Virusi vya UKIMWI katika Wilaya ya Nyamagana, Jijini Mwanza.
Akiwa katika ziara hiyo, Dkt. Yonazi amesema Serikali imeendelea kuboresha mazingira na kutenga bajeti inayosaidia kuratibu na kutekeleza afua za masuala ya UKIMWI nchini, huku ikishirikiana na wadau mbalimbali
“Ushirikiano ni muhimu sana kwani, tunaamini unauwezo wa kutuvusha katika mapambano dhidi ya VVU, ambapo tumeendelea kuunganisha nguvu pamoja katika mapambano hayo,” alisema Dkt. Yonazi.
Aliongeza kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu, yenye dhamana ya kuratibu shughuli zote za Serikali, ikiwemo masuala ya UKIMWI, itaendelea kuhakikisha vifaa na huduma zinatolewa kwa wakati na ubora kwa WAVIU, huku kanuni na taratibu za afya zikizingatiwa.
Dkt. Yonazi Ametumia jukwaa hilo kuiasa jamii kuendelea kupima afya ili kujitambua na kuchukua hatua za mapema endapo mtu atabainika kuwa na maambukizi ya VVU, ili aweze kuishi kwa tahadhari na kuwalinda wengine.
Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza, Ndugu Balandya Elikana, amesema kuwa mkoa umechukuwa hatua madhubuti kuimarisha mapambano dhidi ya UKIMWI kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa sekta ya afya na kamati za utekelezaji wa mikakati ya kuzuia maambukizi, huku wakihimiza upatikanaji wa huduma bora na elimu kwa jamii.
“Jamii inaendelea kuhamasishwa kuhusu upimaji wa afya kwa hiari na matumizi sahihi ya njia za kujikinga na maambukizi ya Virusi vya UKIMWI pamoja na kuendelea kushirikiana kwa karibu na mashirika na wadau wa afya ili kuboresha huduma za kinga na tiba,” alisema Elikana
Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dkt. Kheri Kagya, akiwasilisha taarifa ya hali ya UKIMWI mkoani humo, amesema Mkoa wa Mwanza una kiwango cha maambukizi ya VVU cha asilimia 4.7, ikilinganishwa na kiwango cha kitaifa cha asilimia 4.4, kwa mujibu wa matokeo ya Utafiti wa Kitaifa wa THIS 2022/2023.
Alisema kwa mujibu wa taarifa ya DHIS2 Annual Report ya mwaka 2025/2026, Mkoa wa Mwanza unakadiriwa kuwa na idadi ya watu wanaoishi na VVU (WAVIU) 112,685.
“Mkoa, kwa kushirikiana na wadau, umeendelea kutoa elimu ya kujikinga dhidi ya maambukizi ya VVU kwa kuhamasisha matumizi sahihi ya kondomu. Katika kipindi cha mwaka 2025/2026, Mkoa ulisambaza jumla ya kondomu 2,265,772 katika jamii, hususani sehemu za kulala wageni, sehemu za kuuzia vileo (baa), kumbi za starehe na kwenye mikusanyiko mbalimbali,” alisema.
Harambee ya kuchangisha fedha na vifaa kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kaskazini, Jimbo la Kilimanjaro, kupitia Usharika wa Msitu wa Tembo, Mtaa wa Israel, imefanyika kwa mafanikio huku viongozi na wadau mbalimbali wakijitokeza kuunga mkono ujenzi huo.
Katika harambee hiyo, Mdau wa maendeleo wilayani Simanjiro, Taiko Ole Kulunju, ameendelea kuonesha mshikamano wake katika kusaidia shughuli za maendeleo kwa kuchangia kiasi cha shilingi milioni 4 pamoja na mifuko 100 ya saruji, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuhakikisha ujenzi wa jengo hilo unakamilika.
Taiko Ole Kulunju amesema mchango wake ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za waumini na uongozi wa kanisa katika kuhakikisha wanapata jengo lenye mazingira bora kwa ajili ya ibada pamoja na shughuli mbalimbali za kijamii.
Amesisitiza kuwa maendeleo hayawezi kufikiwa na mtu mmoja pekee, bali yanahitaji ushirikiano wa viongozi, taasisi za dini, wafanyabiashara, wadau wa maendeleo na wananchi kwa ujumla, bila kujali tofauti zao.
Harambee hiyo pia imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, akiwemo Frank Ole Leshwa, mwakilishi wa Mbunge wa Jimbo la Simanjiro, Mhe. James Ole Milya, pamoja na madiwani mbalimbali kutoka Wilaya ya Simanjiro. Kwa pamoja, viongozi hao wamechangia zaidi ya shilingi milioni 21, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za waumini katika kukamilisha ujenzi wa kanisa hilo.
Kwa upande wake, Diwani mwenyeji na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro, Mh Kaleya Mollel, ambaye alikuwa mgeni rasmi katika harambee hiyo, amewashukuru viongozi, waumini na wadau wote waliojitokeza kuchangia ujenzi huo kwa fedha, vifaa na namna nyingine mbalimbali.
Mhe. Kaleya amesema ushirikiano na moyo wa kujitolea uliooneshwa na washiriki wa harambee hiyo ni mfano mzuri wa mshikamano unaopaswa kuendelezwa katika jamii, hususan katika kusaidia miradi yenye manufaa kwa wananchi.
Lengo la harambee hiyo ni kuchangisha fedha na vifaa kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa jengo la kanisa, ikiwemo kukamilisha hatua mbalimbali za ujenzi kutoka kwenye lenta ya kwanza na ya pili hadi hatua ya upauaji, pamoja na mahitaji mengine muhimu.
Mchango wa Taiko Ole Kulunju na viongozi wengine katika harambee hii unaonesha kuwa maendeleo ya jamii hayapaswi kubaki kuwa jukumu la taasisi au kundi moja pekee.
Pale viongozi, taasisi za dini, wafanyabiashara na wananchi wanapoweka tofauti zao pembeni na kuungana kwa lengo moja, miradi ya kijamii hupata nguvu na kasi ya kukamilika.
Harambee hii ni mfano unaothibitisha kuwa mshikamano, kujitolea na uwajibikaji wa pamoja vinaweza kuwa chachu ya maendeleo endelevu katika jamii.
Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba Nchini (TMDA), imeingia mashirikiano na Mamlaka ya Udhibiti wa Dawa ya Denmark, (Danish Medicines Agency
-DKMA) katika nyanja ya udhibiti wa bidhaa tiba Nchini.
Hayo yamebainishwa wakati wa kikao maalum kilichofanyika Jijini Arusha hivi karibuni, ambapo ujumbe wa DKMA umekutana na uongozi wa TMDA ulioongozwa na Mkurugenzi Mkuu wake Dkt. Adam Fimbo.
Katika kikao hicho, maeneo ya ushirikiano yaliyojadiliwa ni pamoja na matumizi ya Teknolojia ya Akili Unde 'AI' katika udhibiti wa vifaa tiba, ufuatiliaji wa ubora na usalama wa bidhaa tiba pamoja na usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa.
Wakizungumza baada ya kikao hicho, pande zote mbili zimesema ushirikiano huo utasaidia kubadilishana uzoefu, taarifa za kisayansi na kuimarisha mifumo ya udhibiti ili kuhakikisha bidhaa tiba zinazopatikana ni salama, zenye ubora na zinafaa.
Aidha, TMDA ni miongoni mwa mamlaka bora barani Afrika katika ubora wa maabara. Maabara yake imepata hadhi ya WHO Prequalified na ipo katika orodha ya maabara 57 duniani zilizothibitishwa na WHO.
Kwa upande wa DKMA ina dhamira ya kuwa kinara katika ushirikiano wa kitaifa na kimataifa na mamlaka za dawa duniani kote.
Na Oscar Assenga, Tanga
WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu 2026, inayofanyika katika Viwanja vya Usagara, jijini Tanga.
Maonyesho hayo yaliyoanza Agosti 15 na yanatarajiwa kuendelea hadi Agosti 24, mwaka huu, yanalenga kuonyesha mchango wa elimu, ujuzi, sayansi, teknolojia na ubunifu katika kufikia malengo ya maendeleo ya Taifa kupitia Dira ya Taifa 2050.
Akizungumza kuhusu maandalizi ya maonyesho hayo, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dk Batilda Burian, alisema mkoa huo umejiandaa kikamilifu kumpokea Profesa Mkenda pamoja na washiriki wengine watakaohudhuria tukio hilo.
Dk Batilda alisema Serikali ya Mkoa imeimarisha maandalizi, ikiwemo ulinzi na usalama, ili kuhakikisha washiriki na wananchi wanaotembelea maonyesho hayo wanapata mazingira salama na rafiki.
“Tanga inajivunia kuwa mwenyeji wa maonyesho haya. Tunawahakikishia Wizara ya Elimu na wananchi kuwa Serikali ya Mkoa imejipanga kuhakikisha ulinzi na usalama unaimarishwa wakati wote wa maonyesho,” alisema.
Alisema maonyesho hayo ni fursa muhimu kwa wananchi kujionea kwa vitendo namna Serikali, taasisi za elimu, watafiti na wabunifu wanavyoshiriki katika kuleta maendeleo ya Taifa.
Kaulimbiu ya maonyesho hayo ni “Elimu, Ujuzi na Ubunifu: Njia ya Kufikia Dira ya Taifa 2050,” ambayo, kwa mujibu wa Dk Batilda, inaendana na hatua ambayo Taifa limefikia katika utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050.
Alisema kila sekta, taasisi, wizara, mkoa na halmashauri ina wajibu wa kuwaelimisha wananchi kuhusu Dira ya Taifa 2050 na nafasi yao katika kuifikia.
“Maonyesho haya yataonyesha Tanzania tunayotaka kuifikia ifikapo mwaka 2050. Taasisi za elimu, vyuo vya ufundi, taasisi za utafiti na shule zitaonyesha mchango wao katika kufikia dira hiyo,” alisema.
Washiriki zaidi ya 300
Dk Batilda alisema zaidi ya washiriki 300 kutoka maeneo mbalimbali wanashiriki katika maonyesho hayo, wakiwemo wawakilishi kutoka vyuo vikuu, taasisi za utafiti na maendeleo, vyuo vya mafunzo na ufundi stadi pamoja na taasisi binafsi zinazohusiana na sayansi na teknolojia.
Alisema washiriki hao watapata fursa ya kuonyesha bunifu, teknolojia, ujuzi na shughuli mbalimbali zinazohusiana na elimu na maendeleo ya Taifa.
Aidha, alisema maonyesho hayo yanatoa fursa muhimu kwa vijana wanaotarajia kujiunga na vyuo vikuu na taasisi nyingine za elimu kupata taarifa sahihi kuhusu fursa za elimu na namna ya kufanya maombi ya kujiunga na vyuo.
“Vijana wanaoanza mchakato wa kujiunga na vyuo vikuu Mtapata fursa ya kuelekezwa namna sahihi ya kujaza maombi na kupata taarifa nyingine muhimu kuhusu elimu ya juu,” alisema.
Sh156 bilioni elimu Tanga
Katika hatua nyingine, Dk Batilda alimshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji mkubwa unaofanywa katika sekta ya elimu, akisema Mkoa wa Tanga umepokea zaidi ya Sh156 bilioni kwa ajili ya kuboresha mazingira ya kujifunza na kufundishia.
Alisema uwekezaji huo ni sehemu ya juhudi za Serikali kuhakikisha wanafunzi wanapata mazingira bora ya elimu na kuongeza ubora wa huduma za elimu nchini.
Pia alimpongeza Profesa Mkenda na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa kuendelea kuunga mkono maonyesho hayo, akisema tukio hilo limeendelea kukua na kuboreshwa.
Kwa upande mwingine, Mkuu huyo wa Mkoa aliwataka wananchi wa Tanga na mikoa jirani kujitokeza kwa wingi katika Viwanja vya Usagara kushuhudia maonyesho hayo na kupata elimu kuhusu fursa mbalimbali zinazopatikana katika sekta ya elimu, ujuzi, sayansi na ubunifu.
Alisema maonyesho hayo pia yatawapa wananchi nafasi ya kujionea hatua ambazo Tanzania imepiga katika matumizi ya teknolojia, utafiti na ubunifu katika kutatua changamoto mbalimbali za jamii.
Uzinduzi rasmi wa maonyesho hayo unatarajiwa kufanyika Agosti 18, 2026, ukiongozwa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda, huku Waziri Mkuu, Mwigulu Nchemba, akitarajiwa kuwa mgeni rasmi katika hafla ya kufunga maonyesho hayo Agosti 24.

SportPesa World Cup promotion crowns 10 winners with TZS 5 million each
Ten SportPesa Tanzania customers each won TZS 5 million in the final draw of the Twenzetu Duniani na SportPesa campaign. These ten winners shared a total prize of TZS 50 million, bringing to a conclusion to the campaign after weeks of World Cup-themed draws. Their wins highlighted how the campaign combined prize rewards with shared football moments across Dar es Salaam.
The campaign offered a total prize of TZS 100 million. SportPesa allocated half of this amount to weekly draws, while the remaining TZS 50 million was split evenly among the ten final winners. During the SportPesa World Cup promotion, eligible bettors who placed qualifying bets were automatically entered into the draw. This structure made the final draw the exciting climax of a month-long event, rather than just a single prize announcement.
Ten final-draw winners each won TZS 5 million
SportPesa held the final draw on July 20th, following the promotion’s close on July 19th. Then ten winners were confirmed, each receiving TZS 5 million, totaling TZS 50 million. This result followed the promotion’s awarding structure, which set aside half of the TZS 100 million prize pool for the final draw.
According to the promotion rules, all customers with qualifying entries were eligible for the final draw. SportPesa Tanzania managed the computerized draw and contacted winners through the phone numbers linked to their accounts. Before payment, each winner’s identity was verified, ensuring a clear and organized process from entry to prize award.
Weekly rewards built momentum before the final
The ten grand-draw winners received the largest individual prizes in a broader reward program. SportPesa set aside another TZS 50 million for weekly draws, planning to select 100 winners each week. Early draws showed that over 200 people won prizes in the first two weeks, as the weekly prize pool increased from TZS 5 million in the first week to TZS 10 million in the second.Before the final draw, weekly rewards had already built momentum, with more than 200 winners recorded in the first two weeks of the campaign.
Twenzetu Duniani na SportPesa was designed to make the World Cup more rewarding for our customers. The 10 final winners show how the campaign created real reward moments, while the weekly draws and match screenings helped fans stay connected throughout the tournament,” said SportPesa Tanzania Head of Marketing Tracy Humplick.
Three Dar screenings took the campaign into fan spaces
By hosting screenings at Mlimani City, Mwinjuma and Tips Bar, SportPesa moved the campaign from the betting platform into real fan spaces where supporters could watch, react and celebrate together. These events provided fans with shared spaces to watch World Cup games and linked the online promotion to live football experiences across the city.
SportPesa director Abbas Tarimba attended the Mwinjuma screening to represent the company and engage with supporters during the match. His presence was welcomed by fans at the event. These three screenings also showcased SportPesa’s larger program of football match events, which gives live match watching to community and hospitality venues and helps bring fans together for major games.
Digital rewards met Dar es Salaam’s football culture
The campaign connected two key areas. SportPesa handled qualifying entries and prize draws on its platform, while the screenings brought the brand into the shared social experience of watching football. Mlimani City provided a major commercial venue, Mwinjuma brought the events to Mwananyamala, and Tips Bar extended them to Mikocheni.
This approach helped SportPesa Tanzania keep the spotlight on the winners while staying engaged throughout the tournament. The TZS 5 million prizes gave the campaign a clear and measurable end, while the screenings allowed fans to enjoy important matches together. The campaign showed how digital access and live events can work together without overshadowing the people who won.
Conclusion
The ten winners who each received TZS 5 million became the highlight of the Twenzetu Duniani na SportPesa campaign. They shared a total of TZS 50 million, completing the TZS 100 million promotion that also rewarded weekly winners. By hosting screenings at Mlimani City, Mwinjuma, and Tips Bar, SportPesa linked the World Cup’s biggest moments to both individual winners and shared fan experiences across Dar es Salaam.

.jpeg)
















.jpeg)

.jpeg)



.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)














.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)
