Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Algeria, Mhe. Iman Njalikai, alikutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Chama cha Kamati za Kitaifa za Olimpiki za Afrika (ANOCA), Bwa. Mustapha Berraf, tarehe 01 Machi, 2026, katika Ofisi za Michezo ya Vijana Afrika, jijini Algiers.

Kupitia mazungumzo hayo, wawili hao walijadili kuhusu namna ya kuimarisha ushirikiano kwenye masuala ya olimpiki. Kadhalika, waliangazia namna ya kuimarisha ushirikiano wa michezo kwa ujumla kati ya Tanzania na Algeria kupitia Wizara za Michezo za nchi hizo mbili.

Viongozi hao, walisisitiza kwamba kukamilisha na kusaini Hati ya Makubaliano (MoU) kwenye eneo la michezo, kutaimarisha ushirikiano huo. Mhe. Balozi Njalikai alisisitiza umuhimu wa kutoa kipaumbele kwenye eneo la mafunzo sambamba na kuandaa programu maalumu za mafunzo ya olimpiki kwa ajili ya vijana ili kuwajengea uwezo wa kushiriki na kufanya vizuri katika mashindano mbalimbali ya kimataifa.

Kwa upande wake Bw. Berraf alionesha utayari wa kutoa kipaumbele maalumu kwa Tanzania kwenye eneo la mafunzo na kuahidi pia kuchagiza ukamilishwaji wa MoU kwenye eneo la michezo kati ya Tanzania na Algeria.

Mhe. Balozi Njalikai, alihitimisha mazungumzo yake kwa kumshukuru Bw. Berraf kwa kuonesha nia thabiti ya kuimarisha ushirikiano pamoja na juhudi anazofanya za kukuza vipaji vya vijana wa kitanzania kimichezo.




Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Profesa Riziki Shemdoe ameziagiza halmashauri zote kwenye mikoa ya Geita, Tabora na Iringa kuendelea kutenga kiasi cha sh 1,000 kwenye bajeti zao kwa kila mtoto wa chini ya miaka mitano ili kuboresha miradi ya lishe katika halmashauri hizo.

Ametoa maagizo hayo wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kuimarisha Huduma za Lishe katika mikoa ya Geita, Iringa na Tabora ili kusaidia kupunguza changamoto za udumavu, ukondefu na utapiamulo wa watoto.

Profesa Shemdoe ameitaka mikoa ya Geita, Iringa na Tabora kuimarisha ufuatiliaji wa mradi jumuishi wa lishe na shughuli zote zinazotekelezwa katika jamii kwa ajili ya kukabiliana na matatizo ya lishe

Mradi wa Kuimarisha Huduma za Lishe  unatekelezwa chini ya ufadhili wa taasisi ya BWP ya nchini Uingereza kwa thamani ya dola za kimarekani milioni 2 malengo makuu yakiwa ni kuimarisha lishe na maendeleo ya watoto.

Halmashuri zote zimetakiwa kuhakikisha zinatoa takwimu sahihi na kwa wakati ili kuzingatia utoaji huduma sahihi kwa kuzingatia ushahidi unaotokana na takwimu.

Naibu Katibu Mkuu wa TAMISEMI, Profesa Tumaini Nagu amesema kuwa kupitia  mradi huu serikali itaongeza kasi ya ufuatiliaji wa huduma bora za malezi na makuzi ya awali ya mtoto hususani katika vituo ya kulelea watoto mchana,

Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Lishe Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI, Luitfrid Nnally amesema kuwa pamoja na nchi kuwa na kiwango kikubwa cha vyakula lakini bado watoto wanapata utapiamlo katika mikoa hii mitatatu kutokana na kukosa matunzo kutokana na shughuli nyingi za wazazi hususani kilimo

Mwakilishi wa taasisi ya BWP, Dr Taye Balcha alisisitiza kuwa mradi huo umezingatia tathimini ya serikali na hivo na kutambua kuwa wahanga wakubwa wa udumavu ni watoto.

Mkuu wa mkoa wa Geita, Martine Shigella aliahidi kuwa mkoa wa Geita kwa kushirikiana na mikoa inayonufaika na mradi huo watatumia fursa hiyo kupunguza kiwango cha lishe kilichopo.






 

 Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, Mhe. Subira Mgalu leo Machi 03, 2026 amekabidhi magari mapya kwa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani kwa lengo la kuimarisha huduma kwa wateja na kuongeza ufanisi wa utendaji kazi katika kuwahudumia Wateja wilayani Bagamoyo.

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika Ofisi ya TANESCO Bagamoyo, Mhe. Mgalu amesema kuwa hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za Serikali kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya umeme kwa wakati, kwa ubora na kwa uhakika zaidi.

“Magari haya yatawezesha mafundi na wahandisi wa TANESCO kuwafikia wananchi kwa haraka pale panapotokea hitilafu au changamoto za umeme. Tunataka kuona muda wa kushughulikia matatizo unapungua na huduma inaboreshwa,” amesema Mhe. Mgalu.

Amesisitiza kuwa, hivi sasa TANESCO imeimarika katika utoaji wa huduma ikiwa ni pamoja na kutoka katika kutengeneza hasara na linajiendesha bila kupata ruzuku kutoka Serikalini.

Aidha, amesema baada ya kukamilika bwawa la Julius Nyerere linalozalisha megawati 2115 na kupelekea Nchi kuwa na uwezo wa takribani wa megawati 4,000 huku mahitaji yakiwa takribani megawati 2,000 hivyo kuitaka TANESCO kuongeza kasi ya kuwaunganishia wateja.

Mkurugenzi wa TANESCO Kanda ya Mashariki,Mha. Kenneth Boymanda amesema  TANESCO inatekeleza miradi mingi ya maendeleo Wilaya ya Bagamoyo ikiwemo ya umeme Vijijini hivyo upatikanaji wa magari hayo kutarahisisha utekelezaji wa miradi hiyo.

“Bagamoyo tunao mpango mkubwa wa kuhakikisha kila nyumba inafikishiwa nishati ya  umeme nak ama Nchi mpaka mwaka 2030 kuunganisha nyumba milioni nane na laki tatu na nyumba Milioni Moja na Laki Saba kwa mwaka”, amesema Mha. Boymanda

Ameongeza kuwa, majukumu hayo yanahitaji uwepo wa vitendea kazi na kusisitiza kuwa TANESCO itafanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha malengo yaliyowekwa na Serikali kupitia mpango wa mission 300.

Serikali imeendelea kuweka mkazo katika kuboresha miundombinu ya umemme kama msingi wa maendeleo ya viwanda, biashara na ustawi wa jamii.

 Hatua ya TANESCO kununua magari hayo ni sehemu ya juhudi za kuimarisha huduma kwa wateja  na kuongeza ubora wa huduma kwa wananchi.


Serikali imesema itaendelea kuratibu na kuimarisha Sera, Sheria na Miongozo inayosimamia programu za Mafunzo ya Uanagenzi na kuhamasisha sekta binafsi kushiriki kikamilifu katika kutoa nafasi za mafunzo kwa vitendo kwa wanagenzi nchini.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano Deus Sangu amesema hayo  leo Machi 03,2026 katika chuo cha ufundi stadi Daon Bosco jijini Dodoma wakati akifungua  Awamu ya Nane ya Mafunzo ya Stadi za Kazi kwa Njia ya Uanagenzi kwa Vijana 5,746 waliodahiliwa katika Vyuo 46 nchini kwa mwaka 2025/26 ambapo utekelezaji wa programu umewezesha jumla ya wanufaika 93,495 hadi kufikia Februari, 2026.

Waziri Sangu amesema mafunzo hayo yanachangia kwa kiasi kikubwa katika kuwapa vijana uzoefu wa kazi kwa nadharia na vitendo, kupunguza pengo la ujuzi kati ya mafunzo ya kitaaluma na mahitaji ya waajiri na kuongezeka kwa ajira kwa vijana kuajiriwa au kujiajiri.

“Hii ni dhamira ya dhati ya Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kujenga nguvukazi yenye ushindani na tija kwa maendeleo endelevu ya Taifa.” amesema.

Aidha, amesisitiza kuwa kuelekea Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, Tanzania inahitaji nguvukazi yenye ujuzi, weledi na uwezo wa kutumia teknolojia ili kuhimili ushindani wa kikanda na kimataifa, huku Serikali ikiendelea kuboresha sera, sheria na mifumo ya mafunzo kuongeza fursa za ajira kwa vijana.

Awali akitoa salamu za wananchi wa Dodoma, Mkuu wa Mkoa huo Rosemary Senyamule ameipongeza serikali kwa kuendelea kutenga bajeti maalum kwa ajili ya mafunzo ya uanagenzi hatua ambayo inaonyesha wazi kuwa serikali inawekeza katika rasilimali muhimu za taifa hususani Vijana.

Kwa upande wake Naibu Katibu, Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano Zuhura Yunus amesema Serikali kupitia Ofisi hiyo, inatekeleza Mafunzo ya Uanagenzi kupitia Programu ya Taifa ya Kukuza Ujuzi Nchini kuanzia mwaka 2016/17 na dhumuni la programu hiyo ni kukuza ujuzi wa nguvukazi iliyopo katika soko la ajira ili kuongeza tija kwenye uzalishaji wa bidhaa na utoaji wa huduma.

Naye, Mkuu wa Chuo cha Don Bosco Dodoma, Mhandisi Dkt. Justine Mulebya, ameshukuru Serikali kwa kukipatia chuo hicho wanafunzi 650 na ameiomba kuwawezesha vifaa wahitimu wa mafunzo ya uanagenzi ili kuwawezesha kujiajiri na kuajiri vijana wengine wakihitimu mafunzo yao.






Naibu Waziri wa Kilimo Mhe David Silinde amesema kuwa Serikali imeweka dhamira ya kuleta mabadiliko katika sekta ya kilimo ili kupunguza umaskini na kuongeza ajira hasa kwa vijana na wanawake na kufikia asilimia 10 ya ukuaji wa kilimo ifikapo mwaka 2030.


Mhe Silinde ameyasema hayo leo Jijini Dodoma Machi 3,2026 wakati akifungua Mkutano wa nne wa Kitaifa wa Kilimo ikolojia hai, akimuwakilisha Waziri wa Kilimo Mhe Daniel Chongolo. 

Ambapo amesema Serikali imechukua hatua za kuleta mabadiliko hayo katika sekta ya kilimo ikiwa ni pamoja na kuongeza bajeti ya Wizara kufikia trilioni 1.24 kwa 2025/2026.

"Ndugu Washiriki, nipende kuwajulisha kwamba Serikali imedhamiria kwa dhati kabisa kuleta mabadiliko makubwa katika sekta ya Kilimo ili kuchangia katika kupunguza umaskini, kuongeza ajira hususani kwa vijana na wanawake na kufikia asilimia 10 ya ukuaji wa kilimo ifikapo mwaka 2030. Katika jitihada za kuleta mabadiliko hayo, Serikali imechukua hatua mahsusi katika sekta ya kilimo ikiwa ni pamoja kuongeza bajeti ya kilimo kufikia trilioni 1.24 mwaka 2025/2026".

Aidha ameeleza kuwa Mkutano huu uliohudhuriwa na wadau kutoka ndani na nje ya Tanzania, unalenga kutafakari kwa kina namna ya kuendeleza jitihada mbalimbali za Kilimo Ikolojia Hai ikiwemo utekelezaji wa Mkakati wa Kilimo Ikolojia Hai wa 2023-2030 lengo ikiwa ni kuhakikisha kuwa viashiria vya mipango ya maendeleo ikiwemo Mpango Kabambe wa Kilimo (Agriculture Master Plan), Mpango Jumuishi wa Maendeleo ya Kilimo Afrika (CAADP), Dira ya Maendeleo na Malengo Endelevu ya Maendeleo (SDGs) vinatekelezwa kufikia utoshelevu wa chakula nchini kwa kuzingatia lishe bora na utunzaji wa mazingira.

Na kuongeza kuwa katika kutekeleza maazimio ya mkutano wa Tatu wa Kilimo Ikolojia Hai uliofanyika mwaka 2023, Serikali imetenga fedha kwenye bajeti ya Wizara ya mwaka 2025/26 kwa ajili ya utekelezaji wa Mkakati wa vyuo kuanza kufundisha Kilimo Ikolojia, mfano Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA). na Wizara kufanya jitihada mbalimbali za kutunza mbegu za asili kupitia Taasisi ya Utafiti wa Kilimo kwa kukusanya, kusafisha na kuhifadhi jumla ya mbegu za asili 770 za mazao ya ulezi, mpunga, mtama, uwele, migomba, maharage na papai,  

Ambapo Wizara kupitia TOSCI tayari imekamilisha utambuzi wa aina 13 za mbegu za asili za mahindi, mpunga, maharage na papai ambazo zimeingizwa kwenye mfumo rasmi wa mbegu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Mwamvuli wa kilimo hai(TOAM) Dkt Mwatima Juma amesema kuwa huu ni Mkutano wa wadau kukumbushana, kuwapa nafasi za kuwa na maudhui mbalimbali ya kisayansi,ya kijamii na ya maendeleo ambayo yatazungumzwa na watu kupata nafasi ya kujadiliana.

Na kusema kuwa kilimo hai kinakwenda mbio sana duniani hivyo nao wanatakiwa kukaza kamba kukisukuma kiende mbio zaidi kutokana na mujibu wa masoko.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa  mwamvuli wa Kilimo hai (TOAM) Bwana Bakari Mongo ameeleza kuwa Mkutano huu huwa ni jukwaa muhimu sana kwa wadau mbalimbali wakiwemo wakulima,watafiti,wanazuoni,Wana Habari,Sekta binafsi na pia wabia wa Maendeleo kubadilishana maarifa na uzoefu ambao utasaidia kuendeleza kilimo Ikolojia Hai katila Taifa la Tanzania. 

Kwani katika Mkutano wao huu wa nne wanategemea kuwa na maazimio lakini pia kujipima walipofikia juu ya yale ambayo walikubaliana katika mikutano iliyopita na kuweka maazimio tena yanayolenga zaidi kusukuma gurudumu la kilimo Ikolojia hai katika Taifa.

Awali wakitoa ushuhuda wa mafanikio ya kilimo hai Bwana Manase Noeki kutoka Halmashauri ya Arusha DC amesema kilimo cha Ikolojia hai kimempa manufaa makubwa ikwemo kuendana na mabadiliko ya Tabia nchi na pia namna ya kutunza mazingira kama vile kuweka kingo,kuotesha miti,kuotesha majani na kutumia mbolea za mifugo kwaajili ya kutunza afya ya udongo.

Naye Bi Mercy Meena mkulima kutoka Morogoro amesema kilimo hiki kimemsaidia kulima mazao mbalimbali ambayo yalisemwa hayatostawi katika maeneo yao lakini kwa kufuatilia kilimo Ikolojia hai alikuta yote yakistawi na akitumia mbegu za asili.

Mkutano huu ni wa siku tatu na unaongozwa na kauli mbiu inayosema “Kilimo Ikolojia Hai: Kuimarisha Usalama wa Chakula na Lishe, Uhimilivu na Ustahimilivu wa Kiuchumi”.





 

Mwakilishi wa Jimbo la Kiwani ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amewashauri viongozi kujenga utamaduni wa kuwasaidia wananchi hasa katika kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani ili kuweka uwiano sawa wa mahitaji.

Ametoa wito huo mara baada ya zoezi la kuwagawa Iftar kwa  wananchi wa jimbo la kiwani shehia ya kendwa yenye nyumba zaidi ya 1156 hafla iliyofanyika kwenye uwanja wa mpira wa Mauuwani Jimbo la Kiwani.

Amesema ataendeleza utamaduni wake wa  kugawa Iftari kwa wananchi wote hasa wenye mahitaji Maalum ili kupunguza ukali wa maisha na kupata chakula katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Amefahamisha kuwa  mwezi Mtukufu wa Ramadhan ni Maalum kwa waumini wa Dini ya kiislamu kufanya matendo mema  yanayompendeza Mwenyezi Mungu,hivyo ni vyema kwa kila mwenye uwezo kutoa na kuwapa wahitaji ili kupata fadhila zilizomo ndani ya mwezi huu.

Aidha, Mhe. Hemed amesema anatarajia kuzifikia shehia zote saba ( 7 )  zilizomo ndani ya Jimbo hilo na kuzipatia Iftari jambo ambalo litaongezea umoja na mshikamano kwa wannachi wa jimbo hilo.

Sambamba na hayo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amewaomba wafanya biashara kuwasaidia watu wenye mahitaji maalumu wakiweo Masikini, Wajane, Mayatima na watu wasiojiweza hasa katika mwezi mtukufu wa ramadhani ili kuzidi kuzitakada biashara zao na kupata fadhila zilizomo ndani ya mwezi wa ramadhani.

Kwa upande wake mfanya biashara SAID NASSIR NASOR ( BOBAR ) ameishukuru serikali ya mapinduzi ya Zanzibar kwa kuendelea kumpatia ushirikiano ambapo kwa mwezi huu wa ramadhani amepatiwa  usafiri wa kusafirisha bidhaa mbali mbali  ambazo atawakabidhi wananchi wa kisiwani Pemba wakiwemo waannchi wa jimbo la kiwani.

Amesema kuwa lengo lake ni kuwafikia  wananchi mbali mbali wasio na uwezo kwa Unguja na Pemba ili kila mwananchi apate sadaka  itakayowasaidia kwa Iftari lakini pia aweze kupata fadhila hapa duniani na kesho akhera.

Nao wananchi waliopatiwa sadaka hizo wamemshukuru mwakilishi wao kwa kuendelea kuwatumikia kwa  moyo wa upendo,  huruma na usawa kwa wananchi wote jimboni humo jambo ambalo linawapa faraja na imani kubwa juu yake.

Wamesema hawana shaka na utendaji kazi wa Mhe. Hemed na matumaini yao makubwa ni kuzidi kuwaletea maendeleo jimbo humo kama vile alivyoanza kuzitekeleza ahadi mbali mbali alizoziahidi wakati akiomba ridhaa ya kuwa mwakilishi wa Jimbo la Kiwani.












Katika kuelekea maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Haki za Mlaji Duniani, Tume ya Ushindani (FCC) imetangaza mkakati wa kuendelea kutoa elimu kwa umma ili kuhakikisha walaji wanapata bidhaa na huduma salama zinazokidhi viwango vinavyotakiwa.

Akizungumza tarehe 3 Machi 2026 jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Khadija Ngasongwa, amesema tume hiyo itaendelea kuchukua hatua madhubuti kulinda maslahi ya walaji pamoja na kuimarisha ushindani wa haki sokoni.

Maadhimisho na Kaulimbiu ya Mwaka
Kwa mujibu wa Ngasongwa, Siku ya Mlaji huadhimishwa kila mwaka Machi 15, huku kilele chake kikiwa Machi 31. Mwaka huu maadhimisho hayo yanaongozwa na kaulimbiu isemayo: “Bidhaa Salama, Imani kwa Mlaji.”

Kaulimbiu hiyo inalenga kusisitiza umuhimu wa kuhakikisha bidhaa na huduma zinazotolewa sokoni ni salama, zinakidhi viwango vya kitaifa na kimataifa, na hazihatarishi afya, usalama wala maslahi ya mlaji.

Umuhimu wa Kujenga Imani Sokoni

Ngasongwa ameeleza kuwa maadhimisho ya Siku ya Mlaji ni fursa ya kujenga imani ya walaji katika soko kwa kuhakikisha kunakuwepo uwazi, ubora na uwajibikaji miongoni mwa wafanyabiashara.

Amesema mlaji anayezingatia ubora huchangia ukuaji wa uchumi imara. Aidha, wafanyabiashara wanaozalisha na kusambaza bidhaa bora hunufaika na mazingira ya ushindani wa haki, jambo linalochochea ubunifu, ufanisi na hatimaye kukuza uchumi.

Elimu kwa Umma Kupewa Kipaumbele

Katika kuadhimisha siku hiyo, FCC imepanga kutoa elimu kwa wadau mbalimbali ili kuimarisha uelewa wa masuala ya ushindani na ulinzi wa mlaji. Lengo ni kuhakikisha wananchi wanafahamu haki zao na wanapata bidhaa pamoja na huduma zilizo bora na salama.

Kwa ujumla, maadhimisho ya mwaka huu yanatoa wito kwa wazalishaji, wasambazaji na watumiaji kushirikiana katika kujenga soko lenye ushindani wa haki na linaloweka mbele maslahi ya mlaji.


Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC), Khadija Ngasongwa, akizungumza na waandishi wa habari wakati akitangaza maadhimisho ya Siku ya Mlaji Duniani leo tarehe 3 Machi 2026 jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikali wa FCC, Bi. Roberta Feruzi,
akitoa maelezo wakati akimkaribisha Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, tarehe 3 Machi 2026, jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya Watumishi  wa FCC katika Mkutano na Waandishi wa Habari  katika Mkutano  wa Kaimu Mkurugenzi  Mkuu wa FCC.
Baadhi ya Waandishi wa Habari wakifatilia  Mkutano  wa Kaimu Mkurugenzi  Mkuu wa FCC jijini Dar wa Dar es Salaam.

 

TUME ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyojitokeza wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, leo Machi 2, 2026 imekutana na mwanasiasa mkongwe wa Chama cha Mapinduzi (CCM) nchini Tanzania, Abdulrahman Kinana.

Mkutano huo wa Tume na Kinana umefanyika katika ukumbi wa Tanganyika uliopo jengo la Benki Kuu ya Tanzania (BoT) mkoani hapa, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Tume kukusanya taarifa, maoni na ushauri kutoka kwa watu mbalimbali wakiwemo wataalamu, watu wa kawaida, viongozi wa sasa na wastaafu.

Katika mkutano huo hoja zilizojadiliwa zilihusu maeneo ya tathmini ya athari za matukio hayo ndani ya nchi na kimataifa na ushauri wa hatua za kijamii na kisheria zinazochukuliwa ili kuimarisha amani, mshikamano wa kitaifa.

Tume inaendelea na mahojiano na waathirika wa Matukio hayo baada ya hivi karibuni Mamlaka ya Uteuzi kuiongezea Tume muda wa siku arobaini na mbili (42) kuanzia tarehe 20 Februari, 2026 ili Tume iweze kukamilisha uchunguzi wa matukio ya uvunjifu wa amani ya wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa tarehe 29 Oktoba, 2025 na kuitaka ikamilishe kazi na kuwasilisha Taarifa yake kabla au ifikapo tarehe 3 Aprili, 2026.








Top News