Na Victor Masangu, Kibaha

Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha katika kumuunga mkono Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuleta chachu ya maendeleo imeamua kutumia fursa ya makusanyo ya fedha za mapato yake ya ndani katika kuhakikisha inakabiliana na changamoto mbali mbali zinazowakabili wananchi ikiwemo suala la kuboresha  miundombinu ya  barabara za mitaa zilizopo katika kata zote 14.

Hayo yamebainishwa na Mstahiki meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dr. Nicas Mawazo wakati wa kikao cha kikanuni cha  baraza la madiwani robo ya tatu  ya kuanzia mwezi januari mwaka huu wa 2026 hadi kufikia Machi ambapo amebaini lengo kubwa ni kuhakikisha wanawaletea mabadiliko chanya ya kimaenndeleo katika nyanja mbali mbali kupitia mapato ya ndani.

Mstahiki Meya amebainisha kwamba katika kikao hicho wamemeweza kupata fursa ya kupokea taarifa mbali mbali kutoka katika baadhi ya taasisi ikiwemo Dawasa, Tanesco, Bima ya afya, Tarura, pamoja na nyinginezo kwa lengo la kujadili mambo mbali mbali ambayo yataweza kuletaa tija zaidi katika kutatua changamoto mbali mbali za wananchi katika maeneo ambayo wanaishi.

"Tumefanya  kikao chetu cha kikanuni cha baraza letu la  madiwani   na kwamba tumejadili mambo mbali mbali ikiwemo suala la  upatikanaj  wa huduma ya maji safi na salama, kuboresha miooundombinu ya barabara za mitaa ambapo tumeweza kutenga kiasi cha shilingi milioni 50 kwa kila mtaa na hii itaweza kusaidia kwa kiais kikubwa katika kuboresha miundombinu ya barabara sekta ya elimu na afya ,"amebainisha  Dr. Nicas

Kwa upande  Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dkt. Rogers Shemwelekwa amesema kwamba lengo kubwa niu kuzidi kuendelea kuongeza kasi zaidi katika suala zima  ukusanyaji wa mapato ya ndani ambayo pia yataweza  kusaidia  katika  kutekeleza  baadhi ya miradi mbali mbali ya maendeleo.

Shemwelekwa  ameahidi kuendelea kushirikiana bega kwa bega na viongozi pamoja na  madiwani kwa lengo la kuweza   kuleta dhana pana ya ushirikishwaji  ambayo   itaweza  kuleta matokeo chanya kataika suala zima la maendeleo.

Nao baadhi ya madiwani wa viti maalumu akiwemo Selina Wilson katika kupambana naa maambukizi mapya ya virusi vya ukimvi (VVU) hakusita kuwahimiza wakinababa kutumia kinga kwa lengo la kuweza kuepukana na maambukizi mapya na kwamba ni vema sasa kuwahimiza umuhimu wa kutumia kondomu katika tendo la ndoa na kuacha na ngono zembe.

Naye Diwani wa viti maalumu Shufaa Mshana pamoja na Sara  Uledi wamesema wameomba juhudi za makusudi zifanyika katika kuboresha sekta ya afya hasa kwa upande wa wakinamama wajawazito ambao wamekuwa wakitembea umbari mrefu katika baadhi ya maeneo kwa ajili ya kwenda  kupata huduma ya kujifungua.

Kikao cha kikanuni  cha baraza la madiwani robo ya tatu ya kuanzia Januari hadi machi mwaka huu kimeweza kujadili mambo mbali mbali ikiwemo suala la kuimarisha miundombinu ya barabara za mitaa, kuboresha huduma ya maji safi na salama, upatikanaji wa bima ya afya kwa wote, suala la afya, elimu  pamoja na mambo  mengine yaa msingi kwa ajili ya maslahi ya wananchi kwa ujumla.








Na Munir Shemweta, WANMM MOROGORO
Katika kukabiliana na changamoto zinazoikabili sekta ya ardhi nchini, Serikali imelenga kutekeleza mikakati ya kuongeza kasi ya uandaaji wa mipango ya matumizi ya ardhi vijijini pamoja na kutumia mbinu jumuishi na shirikishi zinazowahusisha wananchi na wadau katika hatua za upangaji wa ardhi.

Mikakati hiyo inalenga kutekelezwa kwa kupanua programu za kitaifa za upangaji ardhi vijijini kwa kushirikiana na wadau wa maeneo husika, kutumia teknolojia za kisasa na ramani za kidigitali ili kuongeza ufanisi, pamoja na kuharakisha upimaji na utoaji wa hati za kimila, kwa lengo la kupunguza migogoro ya ardhi.

Akizungumza wakati wa kuzindua jukwaa la siku tatu la wadau wanaohusika na uandaaji, usimamizi na utekelezaji wa mipango ya matumizi ya ardhi mkoani Morogoro tarehe 12 Mei 2026, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo, alisema mikakati hiyo pia inahusisha kuimarisha ushirikiano kati ya wizara, halmashauri, wadau na jamii kwa ujumla katika utekelezaji wa majukumu ya sekta hiyo.

Amesema serikali inahamasisha matumizi endelevu ya ardhi, ikiwemo kilimo hifadhi na ufugaji unaozingatia uwezo wa ardhi, ili kuhakikisha rasilimali hiyo inatumika kwa tija na kwa njia inayopunguza migogoro.

Kwa ujumla, Mhe. Dkt. Akwilapo ameeleza kuwa mikakati hiyo inalenga kuleta mabadiliko kutoka katika hatua ya kupanga mipango kwenda katika utekelezaji wake kwa vitendo, ili kuhakikisha ardhi inatumika kwa njia jumuishi inayozingatia maendeleo endelevu.

Ametoa rai kwa jamii kushiriki kuchangia gharama za uandaaji wa hati za hatimilki za kimila, kama ambavyo tayari imeanza kutekelezwa katika baadhi ya maeneo na kusisitiza kuwa, utaratibu huo utasaidia kuongeza kasi ya umilikishaji wa ardhi na kuwafanya wananchi kuwa na milki salama.

“Bila shaka, uchangiaji huu wa gharama utaongeza kasi ya umilikishwaji na hivyo kuwafanya wananchi kuwa na milki salama,” alisema.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Adam Malima, alisema mkoa wake umechukua hatua madhubuti katika kukabiliana na migogoro ya ardhi, hususan kati ya wakulima na wafugaji, kwa kufanya tathmini na utafiti wa kina kubaini chanzo cha changamoto hizo.

Amesema mkoa wa Morogoro umeweka utaratibu wa kujadili migogoro ya wakulima na wafugaji kama ajenda ya kudumu katika vikao vya Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa vinavyofanyika kila mwezi.

“Tumefanya maamuzi ya makusudi ya kuhakikisha tunabaini tumetokea wapi. Katika Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa, kila mwezi tumeweka ajenda ya migogoro ya wakulima na wafugaji,” alisema Mhe. Malima.

Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Matumizi ya Ardhi, Bw. Joseph Mafuru, alisema takwimu zinaonesha kuwa kati ya vijiji 12,333 nchini, ni vijiji 4,925 pekee, sawa na asilimia 39.9, ndivyo vilivyo na mipango ya matumizi ya ardhi, huku vijiji 7,408 bado havijapata mipango hiyo.

Bw. Mafuru alisema changamoto kuu zinazosababisha kasi ndogo ya uandaaji wa mipango ya matumizi ya ardhi ni ufinyu wa rasilimali fedha na matumizi hafifu ya teknolojia stahiki.

Ameeleza kuwa, licha ya kuongezewa bajeti kila mwaka, bado kuna haja ya wadau mbalimbali kukutana na kuweka mikakati ya pamoja itakayowezesha kukamilisha hatua zote za upangaji wa matumizi ya ardhi.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo akizungumza wakati wa kuzindua jukwaa la wadau wanaohusika na uandaaji, usimamizi na utekelezaji wa mipango ya matumizi ya ardhi lililofanyika mkoani Morogoro tarehe 12 Mei 2026.

Sehemu ya washiriki wa jukwaa la wadau wanaohusika na uandaaji, usimamizi na utekelezaji wa mipango ya matumizi ya ardhi.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo (Wa pili kushoto) na Mkuu wa mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima (kushoto) wakipata maelezo ya vitabu vinavyoelezea mipango ya matumizi ya ardhi kutoka kwa Afisa Mipango Miji Mkuu wa Tume ya Taifa ya Matumizi ya Ardhi Bw, John Chua wakati wa Jukwaa la wadau lililofanyika mkoani Morogoro tarehe 12 Mei 2026.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe Adam Malima akizungumza katika Jukwaa la wadau wanaohusika na uandaaji, usimamizi na utekelezaji wa mipango ya matumizi ya ardhi linaloendelea mkoani Morogoro.
Mkurugenzi wa Tume ya Matumizi bora ya Ardhi Bw. Joseph Mafuru akizungumza wakati wa uzinduzi wa jukwaa la wadau wanaohusika na uandaaji, usimamizi na utekelezaji wa mipango ya matumizi ya ardhi lililofanyika mkoani Morogoro.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo (Wa pili kulia), Mkuu wa mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima (kulia) na Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Matumizi ya Ardhi Bw. Joseph Mafuru (kulia) wakifuatilia michango ya wadau wakati wa uzinduzi wa jukwaa la wadau wanaohusika na uandaaji, usimamizi na utekelezaji wa mipango ya matumizi ya ardhi uliofanyika mkoani Morogoro.
( PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI).

Na Mwandishi Wetu
* Matumizi sahihi ya tiba asili na ulinzi wa mazingira.
SHIRIKA la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira Tanzania (TRAMEPRO)limesema linatambua nafasi ya wanawake na akina mama katika: uhifadhi wa mimea dawa,malezi ya maadili ya jamii,

TRAMEPRO imeyasema hayo kupitia Katibu Mkuu wake Boniventura Mwalongo wakati wakitoa salamu katika Maadhimisho ya Siku ya Mama Duniani.

Mwalongo amesema Shirika hilo linatoa salamu za heshima, upendo na pongezi kwa akina mama wote duniani katika maadhimisho hayo ambayo huadhimishwa duniani kote kila Jumapili ya pili ya mwezi Mei.

Ameongeza lengo ni kuthamini mchango mkubwa wa mama katika malezi, ustawi wa familia, maadili ya jamii na maendeleo ya Taifa. Historia inaonyesha kuwa maadhimisho haya yalianzishwa kupitia juhudi za Anna Jarvis nchini Marekani mwanzoni mwa karne ya 20, kama njia ya kutambua upendo, kujitoa na nafasi ya mama katika maisha ya mwanadamu.

"Katika maadhimisho haya ya mwaka 2026, tunawakumbusha wananchi kuendelea kuwaheshimu, kuwathamini na kuwaenzi akina mama kwa mchango wao mkubwa katika jamii, afya, malezi, elimu, kilimo, mazingira na maendeleo ya kizazi cha sasa na kijacho."

Pia amesema TRAMEPRO inaamini kuwa jamii yenye kuwathamini wanawake na akina mama ndiyo msingi wa Taifa lenye maadili, afya njema na maendeleo endelevu.

Kauli ya kutafakari mwaka 2026: “Upendo wa Mama ni msingi wa familia imara na jamii yenye utu.”

" Mungu awabariki akina mama wote duniani.

Mungu ailaze roho ya marehemu mama yangu mzazi Ostela Sanga mahali pema peponi. Amina."

Airtel Tanzania imezindua mnara mpya wa mawasiliano wenye kasi ya 4G katika kata ya Kayenze, hatua inayolenga kuimarisha ubora wa mtandao na kuondoa changamoto ya mawasiliano hafifu iliyokuwa ikiwakabili wananchi kwa muda mrefu.

Uzinduzi huu ni sehemu ya mkakati wa Airtel Tanzania kusogeza karibu huduma bora za mawasiliano na kifedha kwa wananchi, hususan maeneo yanayokua kwa kasi kiuchumi na kijamii.

Akizungumza May 9, 2026 wakati wa uzinduzi huo, Meneja wa Biashara wa Kanda ya Mwanza Mlaki Mchala alisema Airtel inatambua changamoto ya kipato kwa Watanzania wengi, hivyo inaendelea kuhakikisha huduma zinapatikana kwa gharama nafuu zaidi.

Alisema Airtel imeendelea kuimarisha ushindani katika huduma za Airtel Money kwa lengo la kupunguza gharama kwa wananchi katika matumizi ya kila siku, huku akieleza kuwa kampuni hiyo kwa sasa ni miongoni mwa zenye viwango vya chini vya makato nchini.

“Katika huduma za Lipa, awali wananchi walikuwa wakilalamikia makato makubwa, lakini sasa tumeondoa kabisa makato hayo kwa wateja. Tutaendelea kuboresha huduma hizi kadri mahitaji yanavyoendelea kuongezeka,” alisema.

Mchala alisisitiza kuwa kipaumbele cha Airtel ni kuboresha ubora wa mtandao, kurahisisha upatikanaji wa huduma na kuhakikisha zinamudu gharama kwa wananchi wengi zaidi.

Kwa upande wake, Mektirida Jacob, makzi wa Kayenze alisema ujio wa mnara huo ni faraja kubwa kwa wakazi wa eneo hilo waliokuwa wakikumbana na changamoto ya kukatika kwa mawasiliano.

“Kwa sasa tutafaidika vizuri kwa sababu mnara upo karibu nasi. Zamani mtandao ulikuwa unakatika mara kwa mara, lakini sasa hali itakuwa bora zaidi,” alisema.

Aliongeza kuwa wananchi wanatarajia kuendelea kunufaika na maboresho ya huduma pamoja na ofa mbalimbali za mawasiliano kama vile muda wa maongezi, SMS na data.

Naye Mwenyekiti wa Mtaa wa Kayenze, Yasin Haruna alisema wananchi wa Kayenze wanatoa pongezi kwa Serikali na Airtel kwa kuwaletea huduma hiyo muhimu.

“Tunafurahi sana kuona wamefika hapa kwetu na kutujengea mnara wa mawasiliano. Tunaahidi kuulinda ili uendelee kutoa huduma kwa muda mrefu,” alisema.

Kayenze ni miongoni mwa kata zinazokua kwa kasi ndani ya Ilemela, ikiwa chini ya Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela. Kata hiyo ina mitaa mitano, kaya 4,187 na wakazi 17,201.

Eneo hilo lina shughuli mbalimbali za kiuchumi zikiwemo uvuvi kutokana na ukaribu na Ziwa Victoria, kilimo cha mbogamboga na biashara ndogondogo, ambazo zote zinategemea kwa kiasi kikubwa upatikanaji wa mawasiliano ya uhakika.

Katika uzinduzi wa mnara huo, Diwani wa kata ya Kayenze, James Katoro aliwataka wananchi kushiriki katika kulinda miundombinu hiyo muhimu kwa maendeleo ya jamii.

“Miundombinu hii inagharimu fedha nyingi, hivyo kila mwananchi ana wajibu wa kuilinda ili iendelee kutoa huduma kwa muda mrefu,” alisema.

Aliongeza kuwa Serikali chini ya uongozi wa Samia Suluhu Hassan imeendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo yenye lengo la kuboresha maisha ya wananchi nchini.

KILA kona ni stori za ushindi, watu wakibishana nani alipiga pesa nyingi zaidi na nani bado anasubiri bahati imuangukie. Ni kupitia mchezo wa Magic Wheel kutoka Meridianbet ukiwa na burudani yenye msisimko wa kila sekunde.

Magic Wheel imekuja na mtindo wake tofauti kabisa. Mbele yako kuna gurudumu lenye nafasi 56 zinazozunguka kwa kasi huku kila mmoja akisubiri kuona litakaposimama. Ndani yake kuna namba 53 na nafasi 3 maalumu zinazoweza kubadilisha kila kitu kwa muda mfupi sana. Kila mzunguko ni nafasi mpya ya kushinda.

Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya MERIDIANBET au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Kuicheza ni rahisi sana. Unachagua namba zako kati ya 1, 2, 6 au 11, unaweka dau lako halafu unasubiri bahati yako iamue. Gurudumu likianza kuzunguka ndipo presha na msisimko vinaanza kupanda. Hapo ndipo utajua kwa nini vijana wengi wameukubali mchezo huu.

Na kama unataka moto zaidi, Box Bonus ipo kukupa nafasi nyingine ya kutoboa. Mabox matatu yanakuja na uchaguzi wa low, medium au high odds. Hakuna anayejua kilichojificha ndani mpaka uchague box lako mwenyewe. Ukipatia, unaweza kusepa na ushindi mkubwa bila kutarajia.

Meridianbet wameleta burudani inayochanganya bahati, msisimko na nafasi ya kushinda kwa pamoja. Kama unapenda changamoto na unataka kuonja ladha ya ushindi, huu ndio muda wako wa kuingia kwenye Magic Wheel. Zungusha gurudumu na uone kama leo bahati itasimama upande wako.

NA MWANDISHIWI WETU – MASVINGO – ZIMBABWE

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Kaspar Mmuya (Mb), amewasili nchini Zimbabwe kushiriki Mkutano wa Sita (6) wa Kawaida wa Kamati ya Mawaziri Wanaohusika na Usimamizi wa Maafa kwa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu Mheshimiwa Profesa Palamagamba Kabudi unaofanyika Masvingo, Zimbabwe kuanzia tarehe 11 haadi 14 Mei, 2026.

Mara baada ya kuwasili, Mhe. Mmuya amepokelewa na Balozi wa Tanzania nchini humo, Mhe. Balozi Suzan S. Kaganda na kuipongeza Tanzania kushiriki katika mkutano huo unaolenga kujadili maendeleo yaliyopatikana katika utekelezaji wa programu za kikanda na masuala ya kimkakati katika utekelezaji wa afua mbalimbali katika Usimamizi wa maafa kwa nchi za SADC.

Masuala mengine yaliyoelezwa na Mheshimiwa Balozi Suzani ni  pamoja na Tanzania kuendelea kuzitangaza fursa zilizopo ikiwemo sekta ya utalii, uchukuzi pamoja na kilimo  huku akiahidi kuendelea kuimarisha ushirikiano uliopo baina ya Tanzania na Zimbabwe.

Sambamba na hayo, mkutano huo utahudhuriwa na wadau mbalimbali wa masuala ya Usimamizi wa Maafa kutoka Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ambapo ni fursa kwa Tanzania kuendelea kujitangaza Kimataifa kwa kuwa na mifumo thabiti ya Usimamizi wa Maafa pamoja na  kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya Menejimenti ya maafa.

Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizoshiriki katika Mkutano huo wa siku Nne ambapo umekutanisha wadau wa  masuala ya maafa kutoka nchi kumi na sita wakiwemo wataalamu kutoka  katika ngazi za Kimataifa pamoja na Mashirika ya Umoja wa Kimataifa.








Na Janeth Raphael MichuziTv

Serikali imeendelea kuimarisha sekta ya afya nchini kwa kuongeza ajira za watumishi wa kada mbalimbali, hatua inayolenga kupunguza uhaba wa wataalamu katika hospitali, vituo vya afya na zahanati, hususan katika maeneo yenye upungufu mkubwa wa watumishi.

Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Dkt. Jafar Seif, amesema katika kipindi cha mwaka wa fedha 2020/21 hadi 2025/26 Serikali imeajiri jumla ya watumishi 37,921 wa kada za afya na kuwapangia vituo vya kazi katika Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini.

Dkt. Seif ametoa kauli hiyo bungeni leo wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Christina Solomon Mndeme, aliyetaka kufahamu mkakati wa Serikali wa kuongeza watumishi wa afya katika Mkoa wa Tabora ili kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Akizungumzia hali ya Mkoa wa Tabora, Dkt. Seif amesema mahitaji halisi ya wataalamu wa afya ni watumishi 8,121, lakini waliopo sasa ni 3,467 pekee, sawa na asilimia 43 ya mahitaji yote. Hivyo, mkoa huo bado unakabiliwa na upungufu wa watumishi 4,654, sawa na asilimia 57.

Amesema licha ya changamoto hiyo, Serikali imeendelea kuchukua hatua za kupunguza pengo hilo ambapo kati ya mwaka wa fedha 2024/25 hadi 2025/26, jumla ya watumishi 856 wa kada mbalimbali za afya wameajiriwa na kupangiwa vituo vya kazi katika halmashauri zote za Mkoa wa Tabora.

Aidha, Dkt. Seif amesema halmashauri nane za Mkoa wa Tabora zimeandaa mkakati maalum wa kuongeza nguvu kazi katika sekta ya afya kupitia mapato ya ndani. Kwa mwaka wa fedha 2026/27, halmashauri hizo zimetenga jumla ya shilingi milioni 413.8 kwa ajili ya kuajiri watumishi 87 wa afya kwa mfumo wa mikataba.

Kwa mujibu wa Serikali, hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya karibu na maeneo yao pamoja na kupunguza mzigo wa kazi kwa watumishi waliopo sasa katika vituo vya kutolea huduma.

Serikali imeendelea kusisitiza kuwa itaendelea kuboresha mazingira ya utoaji huduma za afya nchini kwa kuongeza ajira, kuimarisha miundombinu ya afya na kuhakikisha wataalamu wa kutosha wanapatikana katika maeneo yenye uhitaji mkubwa.





Viongozi mbalimbali wa Chama cha mapinduzi Mkoa na Wilayani wakiambatana na Viongozi wa Serikali mkoa wa Dodoma wameanza safari ya Kikazi kuelekea mkoani Mtwara kwenye Vyama Vikuu na Vyama vya Ushirika vya Msingi.

Viongozi hao wakingozana na Mrajis Msaidizi wa mkoa wa Dodoma Ndg Joseph Chitinka na Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Ushirika mkoa wa Dodoma Bibi Theresia Nyoka wameanza ziara hiyo leo Mei 12, 2026 kutokea mkoani Dodoma kuelekea mkoani humo.

Mrajis Msaidizi wa mkoa wa Dodoma ameeleza lengo la ziara hiyo ni kuwajengea uwezo, kujifunza utekelezaji wa Mfumo wa stakabadhi za ghala na kujionea utekelezaji wa miradi mbalimbali kwenye Vyama Vikuu na Vyama vya Msingi Ushirika vya mkoa wa Mtwara na hivyo kurahisisha utekelezaji wa majukumu ya kiushirika ndani ya Mkoa wa Dodoma.

Ziara hiyo inafanyika kwa muda wa siku mbili kuanzia Mei 13 hadi 14, 2026 na kuwahusisha Wajumbe wa Kamati ya Siasa Mkoa, Wenyeviti wa CCM Wilaya Mkoani Dodoma, Sekretariti ya Mkoa CCM, Baadhi ya Makatibu wa Chama wilaya na Wenezi,, Makatibu, Makatibu Tawala Uchumi na Uzalishaji Viwanda na Biashara na Kilimo.

Na Munir Shemweta, MASASI

Mbunge wa Jimbo la Mtwara Mjini ambaye pia ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo ameahidi kukiunga mkono kikundi cha vijana cha UBINAKI kinachojishughulisha na mradi wa utengemezaji samani za majumbani na ofisini.

Mradi wa vijana wa UBINAKI unatokana na mkopo wa asilimia 10 unaotolewa na Halmashauri kwa makundi ya vijana, wanawake pamoja na watu wenye walemavu ambapo vijana hao wa Masasi wameonesha ubunifu mkubwa pamoja na matumizi sahihi ya fedha walizopatiwa kwa kuanzisha shughuli yenye tija kwao na kwa jamii inayowazunguka.

Akizungumza wakati wa ukaguzi wa mradi wa vijana wa UBINAKI wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa jana katika halmashauri ya Mji Masasi Dkt Akwilapo amewapongeza vijana hao kwa kuungana, kufanya kazi pamoja sambamba na kujitegemea katika kuendesha shughuli za kujitafutia kipato.

‘’Hawa ni mfano wa kuigwa na ningependa vijana wengine wote waige mfano wa vijana hawa na mimi hawa nitawaunga mkono’’ amesema Mhe. Dkt Akwilapo

Katika kuonesha dhamira ya kuwawezesha vijana hao, Mhe. Dkt Akwilapo aliahidi kununua kitanda kimoja kati ya vile vilivyotengenezwa na vijana hao ikiwa ni ishara ya kuwaunga mkono.

Aidha, aliwaambia vijana hao wa UBINAKI kuwa, katika ile pesa wanaorejesha mkopo wa asilimia 10 wa halmashauri ya Mji Masasi atawachangia kiasi cha shilingi laki nne katika kipindi cha miezi sita ya marejesho.

Amesema, uamuzi wa kuwasaidia vijana hao ni kuongeza hamasa kwa vijana wengine kuanzisha vikundi kama hivyo na yeye atawaunga mkono kwa sababu uanzishwaji vikundi vya aina hiyo utawafanya vijana kujitegemea, kuwa na kazi na kuacha kutumia muda mwingi katika michezo ya pool table na mambo mengine yasiyo na faida.

Kwa mujibu wa taarifa ya kikundi cha UBINAKI, mafanikio makubwa yaliyopatikana ndani ya kikundi hicho ni pamoja na vijana kujiajiri kupitia shughuli za utengenezaji na uuzaji wa samani, kupata soko la bidhaa za ndani ya mkoa wa Mtwara na nje ya Mkoa pamoja na kutoa ajira kwa vijana 8.

Kikundi cha Vijana cha UBINAKI kilianzishwa tarehe 21.03.2023 kikiwa na mtaji wa shilingi 3,380,000 ikijumuisha na mashine za mkono ambazo zilitokana na michango toka kwa wanakikundi. Kikundi kilipata usajili kwa namba MTW/MAS/VIJ/2023/0044 kikiwa na wanachama 5(1Ke na 4 Me).

Halmashauri ya Mji Masasi ilikipatia mkopo wa Shilingi 30,972,000/= kikundi cha UBINAKI kupitia fedha za asilimia 10% ya mapato ya ndani. Mkopo huo umekisaidia kikundi cha vijana hao kuboresha mazingira ya kiwanda, ununuzi wa Malighafi, vitendea kazi ikiwemo Kununua mashine za kisasa mbili (2).

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo akizungumza wakati wa ukaguzi wa mradi wa Kikundi cha Vijana cha UBINAKI uliofanywa wakati wa Mbio za Mwenge kitaifa katika halmashauri ya Mji Masasi mkoani Mtwara jana.

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo akiangalia sehemu ya Samani zilizotengenezwa na kikundi cha vijana cha UBINAKI wakati wa ukaguzi wa mradi wa Kikundi hicho uliofanywa wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru katika halmashauri ya Mji Masasi mkoani Mtwara jana.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2026 Bw. Michael Mwang’onda akipata maelezo ya mradi wa utengenezaji Samani unaofanywa na Kikundi cha Vijana cha UBINAKI wakati wa ukaguzi wa mradi wa Kikundi katika halmashauri ya Mji Masasi mkoani Mtwara jana. Wa tatu kulia ni Mbunge wa jimbo la Masasi Mjini na Waziri wa Ardhi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2026 Bw. Michael Mwang’onda akizungumza wakati wa ukaguzi wa mradi wa utengenezaji Samani unaofanywa na Kikundi cha Vijana cha UBINAKI katika halmashauri ya Mji Masasi mkoani Mtwara jana.

Na. Aron Msigwa - Nairobi, Kenya.

Mkurugenzi wa Mafunzo na Elimu ya Jumla ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Kanali Beno Mathias Nzowa amesema Tanzania imejipanga kikamilifu kushiriki zoezi la pamoja la 14 la Vituo vya Uamrishaji vya Kijeshi vya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) - Ushirikiano Imara 2026, litakalofunguliwa rasmi Mei 14, 2026 katika viwanja vya Ulinzi Sports Complex jijini Nairobi, Kenya.

Kanali Nzowa amesema hayo baada ya kutembelea kikundi cha Tanzania kinachoshiriki zoezi hilo katika Kituo cha Mafunzo cha Masuala ya Usalama na Haki za Binadamu (HPSS) jijini Nairobi kwa lengo la kukagua maandalizi na utayari wa washiriki kuelekea uzinduzi rasmi wa zoezi hilo la kikanda lililowajumuisha Maofisa  wa Jeshi, Polisi, Magereza, Uhamiaji, Zimamoto,Wizara na taasisi za kiraia  .

“Nimekuja hapa kuangalia maandalizi kuelekea ufunguzi wa zoezi ambalo litafanyika kwa siku 14. Maandalizi ni mazuri na Kikosi chetu kutoka Tanzania kina utayari mkubwa pamoja na morali ya hali ya juu kutokana na maandalizi na mafunzo ya awali yaliyoelekezwa na Mkuu wa Majeshi kufanyika jijini Arusha,” amesema Kanali Nzowa.

Zoezi la Ushirikiano Imara 2026 linawakutanisha washiriki kutoka Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa lengo la kuimarisha ushirikiano wa kijeshi, usalama wa kikanda pamoja na uwezo wa kukabiliana na changamoto mbalimbali za kiusalama.








JUMATANO ya leo mechi za ligi mbalimbali zinaendelea kuanzia kule EPL na kwingine huku kuelekea mwishoni mwa ligi pointi 3 zikiwa ni muhimu sana. Je nani kuondoka na ushindi?

Ligi pendwa Duniani, yaani EPL kutakuwa na mechi moja kali sana kati ya Manchester City dhidi ya Crystal Palace ambao wapo nafasi ya 15 kwenye msimamo wa ligi wakiwa pia na uhitaji wa ushindi kwenye mechi hii. Vijana wa Pep Guardiola wanahitaji ushindi kwenye mechi hii kujiweka vyema kwenye mbio za ubingwa.

Kwenye mechi ya mkondo wa kwanza walipokutana hawa wawili, City aliondoka na ushindi mnono. Hii ni mechi nyingine ambayo wanakutana na inaweza ikawa inabeba hatma ya ubingwa wa wenyeji kwani presha ya kuchukua taji hilo inazidi kupamba moto baada ya kutoa sare dhidi ya The Toffees.

Nafasi ya kuondoka na ushindi pale kwa wakali wa ubashiri wamepewa City kutokana na kiwango chao kwenye ligi msimu huu. Je Palace wanaweza kuwazuia wenyeji kupata ushindi siku ya leo?. Jisajili hapa.

Piga pesa leo kwenye michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile Keno, Aviator, Poker, Roullette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Pia kule Ufaransa LIGUE 1 itaendelea huku nafasi ya wewe kutengeneza mkwanja ikiwa nje nje kabisa vinara wa ligi PSG watakuwa ugenini kumenyana dhidi ya RC Lens ambapo timu hizi zote mbili zipo kwenye mbio za ubingwa.

Tofauti ya pointi kati yao hadi sasa ni 6 pekee, bingwa mtetezi anahitaji kushinda mechi hii ili ajiweke vyema kileleni na kwenye mbio za ubingwa huku zikiwa zimesalia mechi chache sana. Mechi ya kwanza walipokutana kwenye ligi Lens alipasuka kule Parc des Princes hivyo hii ni nafasi ya wao kulipa kisasi.

Ikumbukwe kuwa PSG mpaka sasa wapo kwenye nafasi ya kushinda matatu baada ya kuingia kwenye Fainali za UEFA msimu huu. Kushinda mechi hii ni muhimu sana kwao kwani kutawasogeza kwenye kuchukua mataji mengi na kuwafanya kuwa timu bora tena kwenye bara la Ulaya. ODDS KUBWA zipo hapa.

Vilevile kutoka Hispania mechi zipo nyingi lakini kuna mtanange huu hapa wa Villarreal dhidi ya Sevilla ambapo wote wawili wanagombania nafasi tofauti kwenye ligi. Nyambizi wa njano wao wanapambania nafasi ya kucheza michuano ya UEFA msimu ujao huku wageni wao wakihitaji ushindi kujiondoa kwenye nafasi ya kushuka daraja msimu huu.

Villarreal wao wapo nafasi ya 3 kwenye msimamo wa ligi ambapo mpaka sasa tayari nafasi ya wao kushiriki UEFA ipo, hivyo anayehitaji nafasi hii ni Sevilla ambao wapo nafasi ya 17 kwenye msimamo wa ligi.

Meridianbet wameipa mechi hii Odds kubwa na machaguo zaidi ya 1000. Hivyo ingia kwenye akaunti yako na usuke jamvi lako la ushindi na wakali hawa wa ubashiri siku ya leo.

 


UBORA wa rasilima watu( Afya na Maarifa) ndio sarafu ya dunia kwa sasa na hivyo kete muhimu kwa Tanzania kujiunga na Mataifa tajiri mwaka 2050( Trilioni dola Club).

Wauguzi ndio Nguzo ya Rasilimali Watu na Mhimili wa Uchumi wa Dola Trilioni 1 (2050)

Katika Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani, tunatambua kuwa uuguzi si kazi tu, bali ni wito wa kitume unaohitaji upendo, subira, na utu wa hali ya juu. Wauguzi ni daraja kati ya wagonjwa na kupona, wakiwa mstari wa mbele kuokoa maisha.

Bila afya bora, hakuna tija kazini; wauguzi wanahakikisha jamii ina afya, na hivyo kuwa kiungo muhimu kimkakati katika kujenga uchumi mkubwa.

Tanzania inalenga kujiunga na "Club" ya nchi zenye uchumi wa kuanzia dola trilioni moja ifikapo 2050. Hata hivyo, ili kufika huko, tunahitaji rasilimali watu yenye afya bora.

Pamoja na uwekezaji mkubwa wa kibajeti kuboresha miundomibinu ya huduma, vifaa tiba, dawa, wauguzi na madaktari uliofanywa na Serikali, Bado kuna changamoto kubwa ya uwiano idadi ya wauguzi kwa idadi ya watu.Wakati WHO inapendekeza uwiano wauguzi kwa idadi ya watu kuwa wauguzi 45 kwa watu 10,000, Afrika kwa wastani bado ipo chini sana ikiwa na wastani wa wauguzi 18 kwa watu 10,000. Huku nchi tajiri duniani, zimefika uwiano wa wauguzi100 kwa watu 10,000.

Hii inamaanisha uwekezaji wetu katika uuguzi lazima uongezeke mara dufu kuelekea kujiunga na nchi hizo kama tulivyokubaliana kwenye Dira2050, Na kufikia hilo hatuwezi kutegemea serikali pekee.

Mchango wa sekta binafsi ni muhimu sana:Takwimu zinaonesha Sekta binafsi nchini Tanzania inatarajiwa kuchangia asilimia 70 (Tsh Trilioni 334) ya gharama za Mpango wa Maendeleo wa Taifa ifikapo 2026/27- 2030/31.

Zaidi ya asilimia 50 ya matumizi ya afya yanachangiwa na sekta binafsi, na takriban 40% ya vituo vya afya vinamilikiwa au kuendeshwa na sekta binafsi nchini.

Changamoto ya sekta hii ni mtambukwa, Na ina wajibu wa pande zote. Kwa upande wa Serikali ni kuendelea kuimarisha Ubia kati yake na Sekta Binafsi na dhana nzima ya uwekezaji kama inavyosisitizwa na Rais wetu Dr SSH, lakin kwa upande wa wananchi ni kutekeleza uzazi wa Mpango kwani kuna uhusiano mkubwa kati ya umasikini na kasi ya ongezeko la watu hasa katika nchi masikini ambazo uwezo wa serikali kutoa afya na elimu bora kwa kaya masikini bado changamoto kubwa.

Nikatika juhudi za kuongeza uwezo wa kugharimia sekta muhimu kama Afya na Elimu kwa masikini, tunaendelea kusisitiza PPP ili Serikali iendelee kuachana na kuwekeza maeneo yenye mvuto wa sekta binafsi na inachokiokoa kisaidie maeneo kama afya kwa masikini ambayo hayana mvuto kwa Sekta Binafsi kwakuwa hayalipi kibiashara lakin ni muhimu kwa uchumi na ustawi wa Taifa.

Wauguzi ndio uhai wa sekta ya afya. Uwekezaji katika wauguzi ni uwekezaji katika uchumi wetu.

Kazi ya kipekee ya muuguzi ni kumsaidia mtu, mgonjwa au mzima, katika kufanya shughuli zile zinazochangia afya au kupona (au kifo cha amani), ambazo angeweza kufanya bila kusaidiwa kama angekuwa na nguvu, utashi, au maarifa ya kutosha. Heri ya Siku ya Wauguzi. Changamoto ni nyingi lakini lipo tumaini kadiri tunavyojenga na kufungua uchumi! Upo uhusiano mkubwa kati ya ukubwa wa uchumi na ubora wa maisha ya wauguzi
Na Mwandishi Wetu
KUELEKEA msimu mwingine wa Tamasha la Kyela Ibhasa Festival linalofanyika kila mwisho wa mwaka wilayani Kyela mkoani Mbeya, kikundi cha wazawa wa Kyela kiitwacho Bhalondo kimeweka rekodi mpya ya uchangiaji baada ya kufanikisha kukusanya shilingi milioni 2.85 kwa ajili ya maandalizi ya tamasha hilo.

Rekodi hiyo imekuwa ya kipekee tangu kuanzishwa kwa umoja huo, huku kikundi hicho chenye wanachama 19 kikionekana kuwa mfano wa kujitolea na mshikamano katika kuendeleza shughuli za kijamii na maendeleo ya nyumbani kwao.

Kwa mujibu wa wanakikundi hao, mafanikio hayo yametokana na utaratibu waliouweka wa kuchanga fedha kila mwisho wa mwezi kwa lengo la kuhakikisha kabla ya mwezi Juni tayari wanakuwa wamemaliza mchango wao, ili muda unaobaki uwe wa kujipanga zaidi kwa ajili ya kufanikisha tamasha hilo litakalofanyika mwezi Desemba mwaka huu.

Mtunza Hazina wa kikundi hicho, Janeth Mophaty, amesema siri ya mafanikio yao ni moyo wa uzalendo na dhamira ya dhati ya kuipenda Kyela pamoja na kutambua kuwa maendeleo ya tamasha hilo yanahitaji watu kujitoa kwa hali na mali.

“Tumekuwa na ushirikiano mkubwa ndani ya kikundi chetu. Kila mmoja ameonyesha dhamira ya kuona Kyela Ibhasa Festival inakuwa kubwa zaidi mwaka hadi mwaka. Ndiyo maana tumeweza kuvunja rekodi na kumaliza mchango wetu mapema,” amesema Janeth.

Amesema tamasha hilo limeendelea kuwa chachu ya kuwakutanisha wana Kyela waliopo ndani na nje ya nchi, sambamba na kutangaza utamaduni, utalii na fursa mbalimbali za kiuchumi zilizopo wilayani humo.

Ikumbukwe kuwa , Umoja wa Kyela Ibhasa Festival umeweka utaratibu wa kila mwana Kyela kuchangia kuanzia shilingi 150,000 na kuendelea, kwa ajili ya kuhakikisha maandalizi ya tamasha hilo yanafanikiwa kama ilivyokusudiwa.


Na Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma 

Wakati Tanzania ikiendelea kukabiliwa na changamoto ya ongezeko la taka ngumu mijini na vijijini, Serikali imezitaka halmashauri zote nchini kuhakikisha mapato yatokanayo na shughuli za usafi na udhibiti wa taka yanatumika moja kwa moja kuboresha huduma hizo pamoja na kuimarisha mazingira.

Hatua hiyo inalenga kuongeza ufanisi wa ukusanyaji na usimamizi wa taka huku Serikali ikihimiza jamii kuanza kuzitazama taka kama rasilimali yenye thamani ya kiuchumi badala ya mzigo wa mazingira.

Akizungumza leo Mei 12, 2026 jijini Dodoma wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Mwaka wa Tathmini ya Utekelezaji wa Afua za Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Miji, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Profesa Riziki Shemdoe amesema halmashauri zote zinapaswa kutenga na kurejesha asilimia 10 ya mapato yanayotokana na shughuli za udhibiti wa taka ili kuviwezesha vitengo vya usafi wa mazingira kufanya kazi kwa ufanisi zaidi.

Mkutano huo umebeba kaulimbiu isemayo “Taka Ngumu ni Mali; Tumia, Rejeleza na Weka Miji Safi.”

Profesa Shemdoe amesema bado hali ya usimamizi wa taka nchini si ya kuridhisha kutokana na baadhi ya halmashauri kushindwa kuwa na maeneo rasmi ya kutupia taka.

Amesema kati ya halmashauri 184 zilizopo nchini, ni halmashauri 43 pekee zenye madampo rasmi, jambo ambalo linaathiri juhudi za usafi wa mazingira na kuongeza hatari ya uchafuzi wa mazingira pamoja na magonjwa ya mlipuko.

“Ni muhimu kuhakikisha taka zinakusanywa na kuhifadhiwa katika maeneo maalum ili kulinda afya za wananchi na kuweka mazingira safi katika miji na makazi yetu,” amesema.

Aidha, ameonya kuhusu tabia ya utupaji holela wa taka kwenye mitaro ya maji, akisema hali hiyo imekuwa chanzo kikubwa cha mafuriko wakati wa mvua kutokana na kuziba kwa mifumo ya maji.

Kwa mujibu wa Profesa Shemdoe, viongozi wa mikoa, wilaya pamoja na serikali za mitaa wanapaswa kuhakikisha suala la usafi wa mazingira linakuwa agenda ya kudumu katika vikao vya maamuzi ili kuongeza uwajibikaji katika jamii.

Katika hatua nyingine, Serikali imehimiza wananchi kuanza kutenganisha taka kuanzia zinakozalishwa ili kurahisisha shughuli za urejelezaji wa plastiki, vyuma, karatasi na taka nyingine zinazoweza kutumika tena.

Amesema mfumo huo utasaidia kuongeza thamani ya taka na kufungua fursa mpya za ajira na biashara kwa wananchi, hususan vijana na wanawake.

“Tunapaswa kubadili mtazamo kuhusu taka. Zinaweza kuwa chanzo kikubwa cha kipato kupitia shughuli za ukusanyaji, uchakataji na urejelezaji,” amesema.

Profesa Shemdoe pia amewataka vijana na wanawake kutumia mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri kuanzisha miradi ya ukusanyaji na uchakataji wa taka ngumu ili kujiongezea kipato huku wakichangia uhifadhi wa mazingira.

Amesema Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan inaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo ikiwemo Japan kutafuta teknolojia za kisasa za uteketezaji na urejelezaji wa taka kwa lengo la kupata suluhisho la kudumu la usimamizi wa taka nchini.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule amesema Mkoa wa Dodoma umeongeza bajeti ya usafi wa mazingira kutoka Shilingi milioni 750 hadi Shilingi bilioni 3 kwa mwaka wa fedha 2026/27.

Amesema fedha hizo zitatumika kununua vifaa vya usafi, kuboresha ukusanyaji wa taka pamoja na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu utunzaji wa mazingira.

Naye Mkurugenzi Msaidizi wa Sehemu ya Mabadiliko ya Tabianchi na Tathmini kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Dk. Kanizio Manyika amesema Tanzania huzalisha zaidi ya tani milioni 17 za taka ngumu kila mwaka huku asilimia 60 hadi 75 ya taka hizo zikibaki kwenye mazingira kutokana na kutokusanywa ipasavyo.

Ameonya kuwa hali hiyo ni tishio kwa afya za wananchi na mazingira na kusisitiza umuhimu wa kuwa na mifumo endelevu ya usimamizi wa taka.

Kwa upande wake, mwakilishi kutoka Wizara ya Afya, Joseph Birango amesema takwimu zinaonyesha magonjwa sita kati ya 10 yanayoisumbua jamii yanachangiwa na uchafuzi wa mazingira pamoja na mifumo duni ya usimamizi wa taka.

Awali, Mwenyekiti wa Wakuu wa Vitengo vya Udhibiti wa Taka na Usafi wa Mazingira Tanzania Bara, William Mpangala aliitaka Serikali kutoa maelekezo madhubuti zaidi kwa halmashauri ili kuhakikisha fedha zinazotokana na shughuli za udhibiti wa taka zinarejeshwa kikamilifu katika kuboresha huduma za usafi wa mazingira.







*Rais Macron atangaza uwekezaji wa dola bilioni 27 Barani Afrika

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Mei 11, 2026 ameshiriki katika ufunguzi wa Mkutano wa Ushirikiano kati ya Afrika na Ufaransa (Africa Forward: Africa–France Partnership for Innovation and Growth Summit) unaofanyika jijini Nairobi, Kenya.

Mkutano huo umewakutanisha Wakuu wa Nchi na Serikali, viongozi wa sekta binafsi, wadau wa maendeleo pamoja na wawekezaji kwa lengo la kuimarisha ushirikiano kati ya Afrika na Ufaransa katika sekta mbalimbali ikiwemo biashara, teknolojia, nishati, afya, Akili Unde (AI), kilimo, uchumi wa buluu pamoja na viwanda.

Akizungumza baada ya mkutano huo, Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba amesema mkutano huo umekuwa wa manufaa kwa Bara la Afrika na Ufaransa kwa pamoja kwani majadiliano yamegusa namna ya kuzifanya pande hizo mbili ziweze kunufaika na ushirikiano huo.

Amesema rasilimali zinazopatikana barani Afrika zinatosheleza ikiwa zitatumika vizuri katika kujenga uchumi wa Afrika.

“Lengo kubwa la jitihada hizi ni kupambana na umasikini lakini pia na kutengeneza ajira kwa makundi makubwa ikiwemo la vijana pamoja na wanawake,” amesema.

Aidha, Waziri Mkuu amesema maeneo mengi yaliyojadiliwa ni maeneo ambayo yamepewa umuhimu katika Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050.

“Nguzo zote zilizoongelewa kwenye dira lakini pia na maeneo ya kipaumbele yameguswa katika mijadala ya leo,” amesema.

Akizungumza katika mkutano huo, Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mheshimiwa Dkt. William Samoei Ruto, alizitaka nchi za Afrika kutafakari upya mifumo ya kiuchumi kwa kuimarisha ukusanyaji wa rasilimali za ndani, uwekezaji pamoja na ushirikiano wa kikanda ili kuhakikisha kunakuwa na maendeleo ya muda mrefu.

Aidha, Rais Ruto amesema ni wakati wa Afrika kujiweka kama mdau katika uchumi wa kimataifa badala ya kuwa mnufaika wa misaada ya nje pekee.

“Afrika haiwezi tena kubaki kama mshiriki asiyekuwa na sauti katika mifumo ya kimataifa ambapo baadhi ya maamuzi muhimu hufanywa bila sauti ya usawa,” alisema.

Kwa upande wake, Rais wa Jamhuri ya Ufaransa, Mheshimiwa Emmanuel Macron, alisema Bara la Afrika linapiga hatua kubwa za maendeleo na ni bara ambalo halisubiri majawabu ya changamoto bali linatoa majawabu ya changamoto mbalimbali lilazokabiliana nazo.

Katika hatua nyingine, Rais Macron alitangaza uwekezaji wa thamani ya dola za Marekani bilioni 27 barani Afrika katika sekta za nishati, Akili Unde, uchumi wa bahari pamoja na kilimo.

“Mpango huu utasaidia kutengeneza takriban ajira 250,000 barani Afrika na nchini Ufaransa,” alisema.

Aidha, Rais Macron aliwataka wafanyabiashara wa Afrika kuona fursa zilizopo nchini Ufaransa na kwenda kuwekeza.

“Hatuko hapa tu kuja kuwekeza katika Bara la Afrika pamoja nanyi, tunawahitaji viongozi wakubwa wa biashara wa Afrika kuja kuwekeza nchini Ufaransa,” alisema.

Kwa Upande wake Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres alisema watu wa Bara la Afrika wanapaswa kuwa wa kwanza kunufaika na rasilimali za bara hilo.

“Bara hili limebarikiwa rasilimali nyingi, hapa wenyewe ndio wanapaswa wawe wa kwanza kunufaika,” alisema.

Dkt. Mwigulu amemuwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mkutano.


Top News