Na Mwandishi Maalumu, Dar es Salaam

Tanzania imesisitiza umuhimu wa zao la tumbaku kwa uchumi wa nchi kubwa zinazolizalisha barani Afrika, ikitoa wito wa kuimarishwa kwa ushirikiano wa kikanda ili kulinda maisha ya mamilioni ya wakulima na kuhakikisha sera za kimataifa kuhusu tumbaku zinazingatia hali halisi ya nchi zinazozalisha zao hilo.

Akifungua mkutano wa nchi zinazolima tumbaku uliofanyika jijini Dar es Salaam
mwishoni mwa wiki, Waziri wa Kilimo, Daniel Chongolo, alisema tumbaku inaendelea kuwa zao muhimu la kimkakati kutokana na mchango wake mkubwa katika upatikanaji wa fedha za kigeni, ajira, mapato ya Serikali, maendeleo ya viwanda na kupunguza umaskini.

"Kwa nchi zetu, tumbaku si zao la kawaida bali ni bidhaa ya kimkakati inayochangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya uchumi," alisema Chongolo, akisisitiza kuwa sera za kimataifa zinazoihusu sekta hiyo zinapaswa kuzingatia ushahidi wa kisayansi na tathmini halisi ya athari zake kiuchumi na kijamii kwa nchi zinazozalisha.

Alisema tumbaku ni miongoni mwa mazao makuu ya biashara nchini Tanzania, likiwa chanzo cha kipato kwa maelfu ya familia za wakulima, kichocheo cha maendeleo ya maeneo ya vijijini na msingi wa ukuaji wa viwanda vinavyoongeza thamani ya mazao.

Chongolo alisema kupitia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, sekta ya kilimo itaendelea kuwa nguzo ya mageuzi ya uchumi, huku mazao ya kimkakati kama tumbaku yakitarajiwa kuongeza mapato ya mauzo ya nje, ajira na ukuaji wa viwanda.

Aliongeza kuwa zaidi ya wakulima 120,000 waliosajiliwa nchini wanategemea tumbaku moja kwa moja, huku mamia ya maelfu ya wananchi wengine wakinufaika kupitia shughuli za usafirishaji, uchakataji na biashara ya zao hilo.

Katika msimu wa mauzo wa 2024/25, alisema wakulima waliuza kilo milioni 160.9 za tumbaku na kujipatia zaidi ya dola za Marekani milioni 411, jambo linalodhihirisha mchango mkubwa wa zao hilo katika kuongeza kipato cha wakulima na mapato ya fedha za kigeni.

Chongolo alisema umuhimu wa tumbaku hauishii Tanzania pekee, akitolea mfano Malawi ambako zao hilo huchangia takribani asilimia 50 ya mapato yote ya fedha za kigeni, hali inayoonyesha nafasi yake muhimu katika uchumi na maisha ya wananchi wa nchi kadhaa za Afrika.

Alizitaka nchi zinazozalisha tumbaku kuimarisha ushirikiano katika tafiti, matumizi ya teknolojia, kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi, kuongeza thamani ya mazao na kuendeleza uzalishaji endelevu ili kuongeza ushindani katika soko la dunia.

Aidha, alisisitiza umuhimu wa kuwawezesha wakulima wadogo kupitia upatikanaji wa mitaji, huduma za ugani na masoko, huku akizitaka nchi wanachama kuunganisha nguvu katika kutetea maslahi yao ya pamoja kimataifa.

Mwenyekiti wa Bodi ya Tumbaku Tanzania (TTB), Victor Mwambalaswa, alisema mafanikio ya sekta hiyo yanategemea ustawi wa wakulima wa tumbaku.

"Kiini cha juhudi zetu zote ni mkulima wa tumbaku. Maendeleo na uendelevu wa sekta hii yanategemea ustawi wa wakulima wetu," alisema.

Mwambalaswa alisema mkutano huo ni fursa muhimu ya kubadilishana uzoefu, kutafuta suluhisho la changamoto zinazokabili sekta hiyo na kuimarisha ushirikiano katika mnyororo mzima wa thamani wa tumbaku.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Idara ya Uchambuzi wa Sera, Uratibu, Ugatuzi na Mipango ya Maendeleo katika Ofisi ya Rais na Baraza la Mawaziri la Zimbabwe, Dk. Willard Manungo, alisema tumbaku ni moja ya nguzo kuu za uchumi wa nchi yake.

Alisema Zimbabwe inalenga kuvuna kilo milioni 400 za tumbaku mwaka 2026 kutoka kilo milioni 355 zilizovunwa mwaka 2025, huku sekta hiyo ikiwaingizia wakulima zaidi ya dola za Marekani bilioni 1.2 mwaka uliopita.

Aliongeza kuwa zaidi ya kaya 135,000 nchini humo zinategemea kilimo cha tumbaku kwa maisha yao, huku Serikali ikitekeleza awamu ya pili ya Mpango wa Maboresho wa Mnyororo wa Thamani wa Tumbaku (2026–2030), unaolenga kuongeza uzalishaji hadi kilo milioni 500, kukuza uchakataji wa ndani, kuongeza thamani ya zao na kuimarisha ushindani katika soko la kimataifa.

Dk. Manungo alisema Zimbabwe pia inawekeza katika uhifadhi wa mazingira kupitia upandaji miti, matumizi ya teknolojia za ukaushaji zinazookoa nishati, kilimo himilivu dhidi ya mabadiliko ya tabianchi na kuimarisha viwango vya kimazingira, kijamii na utawala bora.

Pamoja na changamoto za ziada ya uzalishaji duniani na kushuka kwa bei, alisema ushirikiano wa karibu kati ya nchi zinazozalisha tumbaku ni muhimu ili kuhakikisha sekta hiyo inabaki kuwa endelevu, yenye ushindani na yenye manufaa kwa wakulima.
Waziri wa Kilimo Mheshimiwa Daniel Chongolo akipokelewa na Mwenyekiti wa Bodi ya Tumbaku Victor Mwambalaswa alipowasili kufungua mkutano wa wadau wa tumbaku kutoka kwenye nchi tano za Afrika uliofanyika Dar es Salaam mwishoni mwa juma.
Waziri wa Kilimo Daniel Chongolo ma wadau wa tumbaku akielekea ukumbini kufungua mkutano wa wadau wa tumbaku mara baada ya kuwasili.Katikati ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Prof.Peter Msofe na kushoto ni Mkurugenzi wa Bodi ya Tumbaku Stanley Mnozya.
Waziri wa Kilimo Daniel Chongolo akiwa katika picha ya pamoja na wadau wa zao la tumbaku kutoka nchi 5 za Afrika mara baada ya kufungua mkutano wao mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam
Wadau wa zao la tumbaku kutoka nchi tano za Africa wakimsikiliza Waziri wa Kilimo Daniel Chongolo wakati akifungua mkutano wao uliofanyika mwishoni mwa wiki Jijini Dar ea Salaam

 



MERIDIANBET, kupitia programu yake ya Uwajibikaji kwa Jamii (CSR), imeendelea kuthibitisha kuwa mafanikio ya biashara yana maana zaidi yanapoweza kugusa maisha ya watu moja kwa moja. Safari hii, kampuni hiyo imefika katika kata ya Kasekese, Manispaa ya Wilaya ya Tanganyika mkoani Katavi na kutoa msaada wa taulo za kike katika kampeni ya Hedhi Salama, hatua ambayo imepokelewa kwa furaha kubwa na viongozi pamoja na wananchi wa eneo hilo. Msaada huo umebeba ujumbe mkubwa wa matumaini, heshima na uwekezaji katika kizazi cha kesho.

Kwa miaka mingi, changamoto ya upatikanaji wa bidhaa za msingi za usafi imekuwa ikiwakabili wasichana wengi, hasa katika maeneo ya vijijini. Kutokana na hali hiyo, baadhi yao hulazimika kukosa vipindi vya masomo au hata kuathiriwa kisaikolojia kutokana na mazingira yanayowazunguka. Meridianbet imeona umuhimu wa kushiriki katika kampeni hii ya Hedhi Salama hili kuhakikisha kuwa wasichana wanapata mahitaji muhimu yanayowasaidia kuendelea na masomo yao kwa kujiamini zaidi.

Meridianbet haikuachi nyuma, kuna michezo mbalimbali ya kasino mtandaoni pamoja na mechi za kimataifa za kubashiri zenye odds bomba na nafasi ya kuongeza kipato chako kila siku. Kujiunga ni rahisi! Tembelea tovuti ya MERIDIANBET au piga *149*10#.

Akizungumza baada ya kupokea msaada huo, Afisa Mtendaji wa Kata ya Kasekese Bi. Bahati Kasanga alieleza kuwa mchango huo umefika kwa wakati muafaka na utaongeza nguvu katika jitihada za kuhakikisha wasichana wanabaki shuleni na kufikia malengo yao ya kielimu. Alisisitiza kuwa msaada wa Meridianbet sio tu umetoa suluhisho la muda mfupi, bali pia umeleta hamasa mpya kwa jamii kuzungumza kwa uwazi kuhusu afya ya hedhi na haki za mtoto wa kike. Kauli hiyo imeungwa mkono na wadau mbalimbali ambao wamepongeza hatua ya kampuni hiyo kuwekeza katika maisha ya vijana.

Kwa upande wake, Meridianbet imeendelea kusisitiza kuwa dhamira yake ni kuwa zaidi ya kampuni ya burudani, ni kuwa mshirika wa maendeleo ya jamii. Kupitia miradi yake ya kijamii inayotekelezwa katika maeneo mbalimbali nchini, kampuni hiyo imekuwa ikilenga kugusa maisha ya wananchi kwa njia zinazozalisha matokeo chanya ya muda mrefu. Msaada huu wa taulo za kike ni sehemu ya maono mapana ya kuhakikisha kuwa kila msichana anapata nafasi sawa ya kufanikiwa bila kuzuiwa na changamoto zinazoweza kutatulika.

Katika kipindi ambacho vijana ndio nguvu kazi na tumaini la taifa, Meridianbet inaamini kuwa kila hatua inayochukuliwa leo inaweza kubadilisha maisha ya kesho. Kupitia msaada huu kwa wasichana wa Wilaya ya Tanganyika, kampuni hiyo imeonyesha kuwa uwajibikaji kwa jamii sio kauli mbiu pekee, bali ni ahadi ya kweli ya kushiriki katika kujenga Tanzania yenye usawa, afya bora na fursa kwa kila kijana.

Msajili wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu akizungumza kwenye hafla ya kupokea Gawio na Michango kutoka kwa Taasisi na Mashirika ya Umma, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 30 Juni, 2026.




















Viongozi na wageni mbalimbali wakiwa kwenye hafla ya kupokea Gawio na Michango kutoka kwa Taasisi na Mashirika ya Umma, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 30 Juni, 2026.

 Julai 1, 2026 Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan , Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atatoa Ramsi Tuzo ya Mlipakodi bora kwa walipakodi waliokidhi vigezo ili kuleta Hamasa ya ulipaji kodi nchini na kuwashukuru kwa mchango wao mkubwa katika maendeleo ya nchi yetu. 

Sambamba na hilo TRA itaadhimisha miaka 30 tangu kuanzishwa kwake Julai 1 1996 ikisherehekea mahusiano mazuri yaliyo jengwa kati ya TRA na walipakodi kwa miongo mitatu na kuchangia maendeleo ya kila sekta katika nchi yetu. TRA inawashukuru sana walipakodi wote kwa kuendelea kulipa kodi kwa hiyari na kwa wakati kwa kipindi chote cha miaka thelathini. Miaka 30 ya TRA kulipa kodi ni Uzalendi na Ushujaa kwa maendeleo na kujitegemea kwa Taifa letu. 



Arusha, Tanzania, Juni 27, 2026 – Maadhimisho ya Siku ya Bima yamehitimishwa kwa mafanikio kupitia mashindano ya gofu ya ICEA LION King of the Course, yaliyowakutanisha wataalamu wa sekta ya bima, viongozi wa biashara na wadau mbalimbali kwa siku ya ushindani, kujenga mahusiano na kubadilishana uzoefu.

Mashindano hayo, yaliyodhaminiwa na ICEA LION General Insurance, yalidhihirisha dhamira ya kampuni hiyo ya kuendelea kuunga mkono mipango inayokuza ushirikiano ndani ya sekta ya bima huku yakihamasisha ushindani wenye tija na kuimarisha mahusiano ya kitaaluma.

Karim Jamal aliibuka mshindi wa jumla na kutwaa taji la King of the Course (Mfalme wa Uwanja). Kutokana na ushindi huo, amejishindia safari yenye udhamini kamili ya kuiwakilisha Tanzania katika fainali za King of the Course, zitakazofanyika Mombasa, Kenya, mwezi Oktoba mwaka huu. Aidha, alikabidhiwa zawadi mbalimbali wakati wa hafla ya utoaji wa tuzo.

Mashindano hayo yalihudhuriwa na viongozi wa ICEA LION Group, viongozi wa Taasisi ya Bima Tanzania (Insurance Institute of Tanzania – IIT) pamoja na wadau wengine kutoka sekta ya bima, wakionesha mshikamano na dhamira ya pamoja ya kuendeleza sekta hiyo nchini.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Jared Awando, Mtendaji Mkuu wa ICEA LION General Insurance Tanzania, alisema kampuni hiyo itaendelea kuunga mkono mipango inayojenga ushirikiano na kuimarisha maendeleo ya sekta ya bima.

"Katika ICEA LION tunaamini kuwa mahusiano imara ni msingi wa kujenga sekta ya bima yenye uimara na uwezo wa kukidhi mahitaji ya wateja. Tunajivunia kuunga mkono mipango inayowaleta pamoja wataalamu wa sekta hii huku tukisherehekea ubora ndani na nje ya uwanja wa gofu," alisema.

Mashindano hayo yalihitimisha rasmi maadhimisho ya Siku ya Bima mwaka huu, yakionesha dhamira ya wadau wa sekta hiyo ya kuimarisha ushirikiano, taaluma na kuongeza uelewa wa umma kuhusu umuhimu wa bima katika kukuza ustahimilivu wa kiuchumi.




Kuhusu ICEA LION General Insurance

ICEA LION General Insurance imekuwa ikitoa huduma za bima nchini Tanzania tangu mwaka 1999. Kampuni hiyo hutoa huduma mbalimbali za bima, ikiwemo bima za magari, afya, mali na biashara, kwa lengo la kuwasaidia watu binafsi na taasisi kulinda mali na shughuli zao dhidi ya hatari mbalimbali.

Ikiendeshwa chini ya ahadi yake ya chapa ya Simba wa Bima, ICEA LION imejizatiti kutoa huduma za bima zenye ubunifu na zinazotegemewa, zinazowapa wateja ujasiri wa kusonga mbele kwa kujiamini. Kama sehemu ya ICEA LION Group, mojawapo ya makundi yanayoongoza kwa huduma za kifedha Afrika Mashariki, kampuni hiyo inaendelea kuhamasisha matumizi ya bima na kuimarisha ustahimilivu wa kifedha nchini Tanzania.
Bw. Jared Awando (wa tatu kutoka kushoto), Mtendaji Mkuu wa ICEA LION General Insurance Tanzania, akiwa pamoja na washindi wa mashindano ya gofu ya ICEA LION King of the Course na viongozi wa ICEA LION Group mara baada ya hafla ya utoaji wa tuzo iliyofanyika jijini Arusha. Mashindano hayo, yaliyofanyika ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Bima, yalimshuhudia Karim Jamal akitwaa ubingwa wa jumla na kujishindia safari yenye udhamini kamili ya kuiwakilisha Tanzania katika fainali za King of the Course zitakazofanyika Mombasa, Kenya, mwezi Oktoba mwaka huu, pamoja na zawadi nyingine mbalimbali.

Na Janeth Raphael MichuziTv

Bodi ya Kitaaluma ya Ununuzi na Ugavi (PSPTB) imetangaza matokeo ya mitihani ya 33 ya taaluma ya Mnyororo wa Ugavi iliyofanyika nchini kuanzia Mei 11 hadi 15, 2026, huku jumla ya watahiniwa 682 sawa na asilimia 43.7 wakifaulu.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dodoma, Mkurugenzi Mtendaji wa PSPTB, Godfrey Mbanyi, amesema jumla ya watahiniwa 1,632 walikuwa wamesajiliwa kufanya mitihani hiyo, lakini watahiniwa 1,559 ndio walioifanya, huku watahiniwa 73 wakishindwa kushiriki kutokana na sababu mbalimbali.

Amesema kati ya watahiniwa waliofanya mitihani hiyo, watahiniwa 682 (asilimia 43.7) wamefaulu, watahiniwa 773 (asilimia 49.6) wamepata hadhi ya referral na watarudia baadhi ya masomo yao, huku watahiniwa 104 (asilimia 6.7) wakifeli na kulazimika kuanza upya masomo katika ngazi husika.

Mbanyi amesema bodi inawahimiza watahiniwa waliopata referral na wale waliofeli kujisajili kwa ajili ya mitihani ya kati (Mid-Session Examinations) itakayofanyika Agosti 24 hadi 28, 2026, au kushiriki mitihani ya Novemba 2026 ili kuboresha matokeo yao.

Ameongeza kuwa dirisha la usajili kwa ajili ya mitihani ya kati litafunguliwa kuanzia Julai 1 hadi Agosti 7, 2026.

Aidha, aliwataka watahiniwa wenye hadhi ya Last Chance Referral kutumia ipasavyo fursa ya mitihani ya kati au ya Novemba 2026, kwani ndiyo nafasi yao ya mwisho ya kukamilisha ngazi za mitihani wanazosomea.

Katika hatua nyingine, PSPTB imewaalika watahiniwa wote wa ngazi ya CPSP II waliofaulu kushiriki warsha ya utafiti itakayofanyika mwishoni mwa Julai 2026, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya hatua zinazofuata katika taaluma yao.

Mbanyi pia ametoa wito kwa wahitimu wa vyuo vikuu vya ndani na nje ya Tanzania kujisajili kufanya mitihani ya kitaaluma ya PSPTB ili kupata sifa zinazotambulika kitaaluma katika fani ya Ununuzi na Ugavi.

Vilevile, amewataka wazazi, wadhamini na waajiri kuendelea kuwawezesha watahiniwa kwa kulipia ada za maandalizi na mitihani, akisema hatua hiyo itasaidia kuongeza idadi ya wataalamu wenye ujuzi na maarifa katika sekta ya ununuzi na ugavi.

Hata hivyo, PSPTB imesisitiza kuwa haitavumilia vitendo vya ukiukwaji wa kanuni na taratibu za mitihani. Mbanyi alisema bodi itaendelea kuchukua hatua kali za kinidhamu dhidi ya watakaobainika kufanya udanganyifu au kukiuka maadili ya mitihani.

Alieleza kuwa adhabu zinazoweza kutolewa kwa mujibu wa kanuni ni pamoja na kufutwa kwa matokeo ya mitihani, kusimamishwa kushiriki mitihani kwa kipindi cha hadi miaka mitatu, pamoja na adhabu nyingine za kisheria ikiwemo faini au kifungo cha jela kulingana na uzito wa kosa.

Kwa mujibu wa PSPTB, hatua hizo zinalenga kulinda uadilifu wa mitihani na kuhakikisha taaluma ya Ununuzi na Ugavi inaendelea kujengwa katika misingi ya maadili, weledi na uwajibikaji.


Serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), kwa ufadhili wa Green Climate Fund (GCF), kwa kushirikiana na Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP) na Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania (TAFORI), imefikia hatua muhimu katika utekelezaji wa Mradi wa Kujenga Uhimilivu dhidi ya Athari za Mabadiliko ya Tabianchi katika Mkoa wa Kigoma kwa kuanza uthibitishaji wa matokeo ya tathmini ya awali (Baseline Survey) ya mradi huo kabla ya kuanza kwa zoezi muhimu la Mpango wa Matumizi Bora ya Ardhi kwa vijiji 22 vilivyopo katika wilaya za Kasulu, Kakonko na Kibondo.

Uthibitishaji huo unafanyika kupitia warsha inayofanyika katika Wilaya ya Kibondo, Mkoa wa Kigoma, na unalenga kuhakiki hali halisi ya kijamii, kiuchumi na kimazingira katika maeneo ya mradi kabla ya utekelezaji wa shughuli mbalimbali za kuimarisha uhimilivu wa jamii dhidi ya mabadiliko ya tabianchi.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa warsha hiyo, Meneja wa Mradi kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira, Mhandisi Onesphory Kamukuru, alisema mradi unatekelezwa katika wilaya za Kasulu, Kibondo na Kakonko kutokana na maeneo hayo kuathiriwa kwa kiwango kikubwa na uharibifu wa mazingira, mmomonyoko wa ardhi na athari nyingine za mabadiliko ya tabianchi.

Alieleza kuwa mojawapo ya sababu zilizochangia uharibifu huo ni historia ya maeneo hayo kupokea idadi kubwa ya wakimbizi, hali iliyosababisha ongezeko la matumizi ya rasilimali za misitu, ikiwemo ukataji wa miti kwa ajili ya kuni na mkaa.

“Mradi huu ni wa wananchi na unatekelezwa katika maeneo matatu makuu ambayo ni kilimo mseto, usimamizi wa hifadhi za misitu ya vijiji na za TFS pamoja na kurejesha maeneo yaliyoharibiwa na mmomonyoko wa ardhi,” alisema Mhandisi Kamukuru.

Mradi huo unatekelezwa katika vijiji 22 vya wilaya za Kasulu, Kibondo na Kakonko, ambavyo vimeathiriwa kwa kiwango kikubwa na mabadiliko ya tabianchi na uharibifu wa mazingira, hususan vijiji vilivyo karibu na maeneo yaliyowahi kuhifadhi wakimbizi.

Katika mradi huu, TAFORI imepewa jukumu la kukusanya na kuchambua taarifa za awali zitakazotumika kama msingi wa ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa mradi. Aidha, taasisi hiyo inasimamia utekelezaji wa shughuli za kitaalamu katika maeneo matatu ya kipaumbele ambayo ni Usimamizi Shirikishi wa Misitu ya Jamii (CBFM), Kilimo Mseto (Agroforestry) na Upandaji Miti (Afforestation).

Akizungumza kwa niaba ya timu ya wataalamu wa TAFORI, Mtafiti Mwandamizi na Msimamizi wa Ushauri wa Kitaalamu wa Mradi, Dkt. Numan Amanzi, alisema matokeo ya tathmini ya awali yaliyowasilishwa kwa wadau yameridhisha na yanaakisi hali halisi iliyopo katika vijiji vinavyotekeleza mradi.

“Matokeo haya yatatumika kama msingi wa kupima mafanikio ya mradi baada ya kukamilika ili kubaini kwa kiwango gani umechangia kuboresha hali za kiuchumi, kijamii na kimazingira katika jamii husika,” alisema Dkt. Amanzi.

Hatua ya uthibitishaji wa matokeo ya tathmini ya awali ni awamu ya tatu ya utekelezaji wa mradi. Awamu ya kwanza ilihusisha utambulisho wa mradi kwa mamlaka za Mkoa wa Kigoma na wilaya husika, huku awamu ya pili ikihusisha uthibitishaji wa vigezo vya uteuzi wa vijiji, maeneo ya utekelezaji na aina za miti zitakazotumika katika shughuli za usimamizi shirikishi wa misitu, kilimo mseto na upandaji miti.

Warsha hiyo imewakutanisha wadau mbalimbali wakiwemo wawakilishi kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Maafisa Mazingira,  Maafisa Mkoa, Wilaya na Wakala wa Huduma za Misitu (TFS)  na Wawakilishi wa vijiji 22 vya wilaya za Kasulu, kibondo na Kakonko.




KILA mbashiri mwenye mapenzi ya soka anaweka dau lake kupitia Meridianbet akiamini timu yake pendwa itaibuka na ushindi. Dakika zinaposogea, timu yake ikafanikiwa kufunga mabao mawili ya haraka na kuongoza mchezo kwa tofauti ya mabao mawili basi kabla hata mwamuzi hajapuliza filimbi ya mwisho, Meridianbet inakuwa tayari imemtangaza kuwa mshindi kupitia huduma mpya kabisa ya Early Payout.

Meridianbet, kampuni inayoendelea kuongoza katika ubunifu wa michezo ya kubashiri, imezindua rasmi huduma ya Early Payout ukiwa ni ubunifu mkubwa unaolenga kuwapa wateja uzoefu wa kipekee, wa haraka na wenye msisimko zaidi. Kupitia huduma hii mpya, mchezaji aliyebashiri timu kushinda atatangazwa mshindi mara tu timu yake inapopata uongozi wa mabao mawili, bila kulazimika kusubiri mechi kumalizika.

Meridianbet haikuachi nyuma, kuna michezo mbalimbali ya kasino mtandaoni pamoja na mechi za kimataifa za kubashiri zenye odds bomba na nafasi ya kuongeza kipato chako kila siku. Kujiunga ni rahisi! Tembelea tovuti ya MERIDIANBET au piga *149*10#.

Kwa vijana wengi ambao hujumuika kutazama mechi katika vibanda vya mpira, migahawa au kupitia simu zao, huduma ya Early Payout inaleta msisimko mpya kabisa. Fikiria umeweka dau kwenye timu yako unayoiamini, halafu ndani ya dakika chache tayari unapata taarifa kuwa wewe ni mshindi kabla mchezo haujaisha. Hiyo ndiyo nguvu ya ubunifu huu mpya kutoka Meridianbet. Huduma hii inapatikana kwenye mechi za soka, ambazo ndizo zinazovutia mamilioni ya mashabiki duniani kote.

Ili kuhakikisha kila mchezaji anatambua kwa urahisi mechi zinazohusika na huduma hii maalum, Meridianbet imeweka alama maalum ya kijani kwenye matukio yote yenye Early Payout. Alama hiyo itaonekana kwenye orodha ya mechi, kwenye tiketi ya dau lako pamoja na sehemu ya beti zako, hivyo hakuna nafasi ya kukosa fursa hii ya kipekee. Mfumo huu umeundwa kwa kuzingatia urahisi wa matumizi na kuhakikisha kila mteja anapata uzoefu bora, wa kisasa na unaoendana na kasi ya maisha ya leo yanayotaka teknolojia, burudani na ushindi wa haraka.

Kuletwa kwa Early Payout kunathibitisha tena dhamira ya Meridianbet ya kuendelea kuwa kinara wa ubunifu katika sekta ya michezo ya kubashiri. Kwa mashabiki wa soka na wapenzi wa burudani, huu ni wakati wa kufurahia kiwango kipya cha msisimko, ambapo ushindi hauhitaji tena kusubiri dakika ya mwisho. Sasa unaweza kushangilia ushindi wako mapema, kufurahia mchezo kwa utulivu zaidi na kupata uzoefu wa kipekee ambao unapatikana Meridianbet pekee.



Na Mwandishi Wetu, Kondoa

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dkt. Leonard Akwilapo, amesema Serikali itaendelea kushirikiana kwa karibu na taasisi za kidini katika kuboresha huduma za jamii, hususan sekta za elimu, afya na malezi, kwa kutambua mchango mkubwa wa taasisi hizo katika maendeleo ya taifa.

Dkt. Akwilapo ameyasema hayo Juni 28, 2026, mkoani Dodoma aliposhiriki Harambee ya Ujenzi wa Nyumba za Walimu katika Shule ya St. Peters and St. Paul Secondary School iliyopo Wilaya ya Kondoa. Hafla hiyo ilihudhuriwa pia na Baba Askofu wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Kondoa, Askofu Given Gaula, pamoja na viongozi na waumini wa kanisa hilo.

Katika hafla hiyo, Waziri huyo alishiriki pia ibada maalumu ya kumsimika mfadhili kutoka Uingereza, Bw. Peter Ruxton, kuwa Lay Canon wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Kondoa kutokana na mchango wake mkubwa katika maendeleo ya elimu na shughuli za kanisa.

Akizungumza katika hafla hiyo, Dkt. Akwilapo alisema Serikali inaendelea kutekeleza maelekezo ya Rais ya kuimarisha ushirikiano na madhehebu mbalimbali ya dini kwa lengo la kuboresha huduma za jamii zinazowagusa wananchi moja kwa moja.

"Rais amekuwa akituambia kuwa ataendelea kushirikiana na madhehebu ya dini, na azma yake ni kuboresha huduma za jamii," alisema Dkt. Akwilapo.

Alisema Serikali inatambua mchango mkubwa wa Kanisa la Anglikana katika sekta ya elimu, akibainisha kuwa kwa mujibu wa takwimu za Wizara ya Elimu, kanisa hilo linaendesha shule za awali 39, shule za msingi 40, shule za sekondari 17, vyuo vya kati 17 pamoja na chuo kikuu kimoja.

Alieleza kuwa taasisi hizo zimeendelea kutoa mchango muhimu katika kuwajengea vijana maarifa, maadili, uzalendo na hofu ya Mungu, mambo ambayo ni msingi wa maendeleo endelevu ya taifa.

Aidha, Dkt. Akwilapo aliipongeza Dayosisi ya Kondoa kwa juhudi zake za kupanua huduma za elimu kwa kuongeza idadi ya shule, akieleza kuwa hivi karibuni shule nyingine itazinduliwa katika wilaya hiyo.

Kwa upande wake, Askofu wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Kondoa, Dkt Given Gaula, amesema ili kumtia moyo mfadhili anayesaidia maendeleo ya kanisa ikiwemo ujenzi wa shule waumini wa kanisa hilo wanapaswa kuchanga fedha kwa ajili ya maendeleo ya ujenzi wa nyumba za walimu.

‘’Shule zinazoendeshwa na kanisa la Angilikana hapa Kondoa zimeleta mabadiliko makubwa katika maisha ya watoto kwa kutoa elimu bora bila ubaguzi wa dini au itikadi’’. amesema

Jumla ya shilingi milioni tano zilichangwa katika hafla hiyo ikiwa ni jitihada za kumuunga mkono mfadhili anayejenga nyumba za walimu katika Shule za St. Peters and St. Paul Secondary School iliyopo Wilaya ya Kondoa

Katika hatua nyingine, Dkt. Akwilapo alimpongeza Bw. Peter Ruxton baada ya kusimikwa kuwa Lay Canon, akisema ametoa mchango wa kipekee katika maendeleo ya elimu na shughuli za kanisa kwa miaka mingi.

Alisema Serikali inathamini mchango wa mfadhili huyo, ambaye amesaidia kujenga na kuendeleza shule mbalimbali pamoja na kuchangia maendeleo ya taasisi za kidini zinazotoa huduma kwa jamii bila ubaguzi.

Naye Askofu Dkt Given Gaula alisema Bw. Ruxton amekuwa mshirika muhimu wa Dayosisi ya Kondoa, akibainisha kuwa karibu asilimia 97 ya shule zinazomilikiwa na dayosisi hiyo zimejengwa kwa msaada wake. 

Aidha, amesema mfadhili huyo amechangia ununuzi wa mabati kwa makanisa mengi yaliyopo vijijini na kusaidia miradi mingine ya maendeleo inayowanufaisha wananchi.

Alisisitiza kuwa ushirikiano kati ya Serikali, taasisi za kidini na wadau wa maendeleo unaendelea kuwa chachu muhimu katika kuimarisha elimu, kuboresha ustawi wa jamii na kuharakisha maendeleo ya taifa.Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dkt. Leonard Akwilapo akizungumza wakati wa Harambee ya Ujenzi wa Nyumba za Walimu katika Shule ya St. Peters and St. Paul Secondary School iliyopo Wilaya ya Kondoa jana.

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dkt. Leonard Akwilapo akiendesha Harambee ya Ujenzi wa Nyumba za Walimu katika Shule ya St. Peters and St. Paul Secondary School iliyopo Wilaya ya Kondoa.Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dkt. Leonard Akwilapo akishiriki ibada wakati wa Harambee ya Ujenzi wa Nyumba za Walimu katika Shule ya St. Peters and St. Paul Secondary School iliyopo Wilaya ya Kondoa tarehe 28 Julai 2026.Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dkt. Leonard Akwilapo akipongezwa alipopatiwa zawadi mara baada ya kuendesha Harambee ya Ujenzi wa Nyumba za Walimu katika Shule ya St. Peters and St. Paul Secondary School iliyopo Wilaya ya Kondoa.

 Mfadhili kutoka Uingereza Bw. Bw. Peter Ruxton akisimikwa kuwa Lay Canon wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Kondoa kutokana na mchango wake mkubwa katika kanisa hilo jana.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dkt. Leonard Akwilapo akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Kanisa la Anglikana mara baada ya kuendesha Harambee ya Ujenzi wa Nyumba za Walimu katika Shule ya St. Peters and St. Paul Secondary School iliyopo Wilaya ya Kondoa.
Given Gaula wa Kanisa la Anglikana akiwa katika picha na viongozi wa kanisa hilo mara baada ya kumsimika Bw. Peter Bw. Peter Ruxton kuwa Lay Canon wa kanisa la Anglikana Dayosisi ya Kondoa.


Sehemu ya waumini wakiwa katika Harambee ya Ujenzi wa Nyumba za Walimu katika Shule ya St. Peters and St. Paul Secondary School iliyopo Wilaya ya Kondoa.




Top News