JUBILEE Health Insurance imetoa elimu kuhusu afya ya akili kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mzizima jijini Dar es Salaam lengo likiwa kuijengea uelewa jamii kuhusu afya ya akili huku ikieleza mpango huo utafanyika kwa wanafunzi wa shule mbalimbali nchini.
Akizungumza katika Shule ya Sekondari Mzizima jijini Dar es Salaam wakati wa kutolewa elimu kuhusu afya ya akili kwa wanafunzi 100 wa shule hiyo , Dk.Milembe Makoye ambaye ni Senior wellness officer kutoka Jubilee Health Insurance amesema wanaamini elimu ni ufunguo wa maisha hivyo wakielewa watajitambua.
“Tuko hapa kwa ajili ya kutoa elimu kuhusiana na afya ya akili lakini afya kwa ujumla.Kwanini tumeamua kutoa elimu hii ? Tunaamini wakielewa watajitambua.
“Kwanini afya ya akili ? Afya ya akili ni jambo ambalo ni changamoto kwa watu wengi sio kwa watu wazima pekee, lakini hata kwa watoto ambao wamekuwa wanasahaulika.
“Sasa kama Jubilee Health Insurance tunaamua kuingia kwenye jamii kuwagusa watoto wapate elimu sahihi waweze kujitambua ili hata wanapokua waweze kudhibiti changamoto ya matatizo ya afya ya akili lakini na afya ya mwili kwa ujumla,”amesema Dk.Makoye.
Aidha amesema Sekondari ya Mzizima ni ya kwanza kufikiwa lakini watakwenda shule nyingi zaidi kadri watakavyoweza huku akifafanua sababu za kuja na programu hiyo inatokana na ukweli Jubilee Health Insurance wanatoa huduma za bima ya afya.
“Lakini tukaona tusiishie kutoa tu bima basi tuguse jamii kwa kutoa elimu ya ustawi wa Afya, maana wakielewa maana ya afya ya akili watachukua njia sahihi ya kutunza afya zao na hapo tutakuwa tumefuzu.
Kwa upande wake Dkt.Isaac Marro akizungumza baada ya kutoa elimu ya afya ya akili kwa wanafunzi hao amesema kuna kila sababu ya Jamii kuwa na uelewa na afya ya akili mapema kwani kwa muda mrefu elimu kuhusu changamoto ya akili inatolewa kwa watu wazima.
“Kwa kifupi afya ya akili duniani kote imekuwa changamoto kubwa lakini tofauti na wenzetu ambao wao mapema waliwahi kubaini sisi tukachelewa.Kwahiyo changamoto zilipoanza kuwa kubwa na mapokeo yameendelea kuwa hasi.
Amesisitiza umuhimu kuzungumza kuhusu afya ya akili kuanzia umri mdogo wakiwemo watoto na vijana ili wajue, kwani hiyo inasaidia kutengeneza sio tu mbinu za kujilinda lakini pia kujilinda wenyewe kwa wenyewe.
Wakati huo huo Mshauri wa wanafunzi katika Sekondari ya Mzizima Theresia Mwaijala ametoa pongezi kwa Jubilee Health Insurance kwa kuona umuhimu wa kutoa elimu ya afya ya akili kwa wanafunzi.
“Juhudi zinazofanywa na Jubilee Health Insurance ni nzuri, wamekuja shuleni kwetu kuzungumza na wanafunzi kuhusu afya ya akili kitu ambacho ni muhimu kwasababu tunafahamu changamoto ya afya ya akili zinaanza mapema kuanzia miaka 14.
Hivyo amesema vizuri watoto wakapewa uelewa ,wafundishwe ili waweze kujilinda lakini wakiona kama kuna dalili ambazo zinaweza kusababisha afya ya akili wachukue hatua
Amesisitiza mafunzo ya Jubilee Health Insurance kuhusu afya ya akili kwa ujumla yanafaida kubwa ikiwemo kupata uelewa, na ukiwa na uelewa utachukua hatua sahihi.”


.jpeg)























.jpg)





.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)

