Na Victor Masangu,Bagamoyo

Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Shaibu Ndemanga amewahimiza viongozi na wananchi mbali mbali wakiwemo wadau, wanafunzi, walimu,kuhakikisha wanajenga tabia ya kushiriki kikamilifu katika michezo mbali mbali kwa lengo la kuweza kujenga afya zao ikiwa pamoja na kuondokana kabisa na changamoto ya kuwa na magonjwa yasiyoambukiza.

Hayo ameyabainisha wakati wa ufunguzi rasmi wa sherehe za maadhimisho ya miaka 20 ya Baobab tangu kuzaliwa kwake ambayo yameweza kushirikisha jumla ya washiriki zaidi ya ya elfu 1000 kutoka maeneo mbali mbali wakiwemo wadau wa michezo, wanafunzi, taasisis wezeshe pamoja na viongozi mbali mbali wa serikali.

Mkuu huyo wa Wilaya amebainisha kuwa kwa sasa jamii inapaswa kubadilika na kujikita zaidfi katika kufanya mazoezi ambayo yataweza kuwasaidia katika kujenga afya zao na kuondokana kabisa na magonjwa hivyo amewahimiza wananchi wa Wilaya ya Bagamoyo na maeneo mengine kuendelea kujitokeza kwa wingi pindi inapojitokeza michezo mbali mbali kama vile mbio za Marathon na michezo mingine.

"Niwapongeze kwa dhjati uongozi wa Baobab kw akuweza kunialika katika sherehe hizi za maadhimisho ya miaka 20 na mimi kama mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo nimewza kushiriki kikamilifu katika mbio za Marathon kwa hiyo kitu kikubwa ninachowaomba wananchi ni kuwa na tabia ya kushiriki katika michezo ili kuondokana na magonjwa mbali mbali,"amebainisha Mkuu huyo.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi za Shajar Shani Swai ambaye ndio inayoimiliki shule ya Sekondari Baobab amebainisha kwamba lengo kubwa katika Marathon hiyo ni kukusanya fedha kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 20 kwa lengo la kuweza kuwasaidia watoto wenye ulemavu na wanaoishi katika mazingira magumu.

"Tunashukuru sisi kama taasisi tumeweza kutimiza miaka 2o tangu kuanzishwa kwake na mimi napenda kusema lengo kubwa ya kufanya marathon hii ni kukusanya zaidi ya milioni 20 ambayo itaweza kusaidia katika kusaidia watoto yatima na wale amabo wanaoishi katika mazingira magumu na tunashukuru tueweza kutimiza malengo yetu,"amebainisha mkurugenzi.

Naye Mwanzilishi wa Taasisi hiyo ya Shajar Sophia Swai amebainisha kwamba wamemua kutumia maadjimisho hayo ya miaka 20 kukusanya fedha hizo ambazo zitaweza kuwasaidia watoto ambao wanaishi katika mazingira magumu pamoja na jamii mbali mbali ambazo zinauhitaji.

Katika maadhimisho hayo ya miaka 20 ya Baobab kumefanyika mbio za kuanzia kilometa 5 hadi kilometa 10 ambapo michezo mbali mbali imefanyika ikiwemo, soka,kikapu, pete,Riadha, kuvuta kamba ambapo washindi wameweza kuzawadiwa zawadi mbali mbali ya vikombe pamoja na medani.




Na Janeth Raphael - MichuziTv 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema Tamasha la Kizimkazi limekuwa kichocheo muhimu cha maendeleo ya kiuchumi na kijamii, huku eneo hilo likizidi kufunguka kwa fursa za biashara, uwekezaji na utalii kwa wananchi wa Kusini, Zanzibar na maeneo jirani.

Akizungumza leo, Ijumaa, Agosti 14, 2026, katika kilele cha Tamasha la Kizimkazi, Rais Samia amesema tangu kuanzishwa kwake mwaka 2016, tamasha hilo limeendelea kukua na kuacha alama katika maendeleo ya eneo hilo kupitia kuongezeka kwa shughuli za kiuchumi pamoja na uboreshaji wa miundombinu na huduma mbalimbali.

Rais Samia amesema mabadiliko yanayoendelea Kizimkazi yameifanya eneo hilo kuwa sehemu yenye mazingira yanayofaa zaidi kwa wafanyabiashara na wawekezaji, akiwataka kutumia fursa zilizopo kuanzisha na kuendeleza shughuli zitakazoongeza ajira na kuchochea uchumi wa eneo hilo.

“Tunawakaribisha kuja kuwekeza, mazingira mazuri ya uwekezaji yamekwishawekwa,” amesema Rais Samia, akisisitiza umuhimu wa sekta binafsi kutumia fursa zinazotokana na maendeleo yanayoendelea kufanyika Kizimkazi.

Amesema pia Serikali inaendelea na ujenzi wa uwanja wa michezo ambao ukikamilika utakuwa miongoni mwa miundombinu itakayotumika katika michuano ya AFCON 2027. Kwa kuzingatia idadi ya wageni, wanamichezo na washiriki watakaotarajiwa kufika, Rais Samia amewataka wawekezaji kuona fursa katika sekta za malazi, chakula, usafiri, burudani na huduma nyingine zitakazohitajika.



Na Mwandishi Wetu

BENKI ya DCB Commercial Bank Plc imemtangaza Dkt. Charles Stephen Kimei kuwa Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Wakurugenzi, akitarajiwa kutumia uzoefu wake wa zaidi ya miaka 40 katika sekta ya benki, sera za fedha, udhibiti, utafiti wa uchumi na utawala bora.

Dkt. Kimei ni miongoni mwa viongozi wenye uzoefu mkubwa katika sekta ya benki na fedha nchini Tanzania, ambapo alianza safari yake ya kitaaluma katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), akishika nyadhifa mbalimbali za juu ikiwamo Mkurugenzi wa Usimamizi wa Benki pamoja na Mkurugenzi wa Utafiti na Sera za Kiuchumi.

Baadaye aliteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji na Afisa Mtendaji Mkuu wa CRDB Bank Plc, nafasi aliyoitumikia katika kipindi ambacho taasisi hiyo ilifanya mabadiliko makubwa kutoka benki ya ushirika na kuwa benki ya biashara yenye ushindani mkubwa.

DCB Commercial Bank imesema uzoefu wa Dkt. Kimei katika mabadiliko ya taasisi, masoko ya fedha, usimamizi na utawala bora utakuwa muhimu katika hatua ambayo benki hiyo inaendelea kuimarisha shughuli zake na kuongeza thamani kwa wateja, wanahisa na wadau wengine.

Mbali na nafasi zake za kiutendaji, Dkt. Kimei amewahi kushika nyadhifa mbalimbali za uongozi na uwakilishi katika taasisi za ndani na nje ya sekta ya benki, zikiwamo Tanzania Bankers Association, Swissport Tanzania Plc, Economic and Social Research Foundation (ESRF), Baraza la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Tanzania Education Authority.

Kutokana na mchango wake katika sekta ya benki na fedha, Dkt. Kimei amewahi kutunukiwa tuzo mbalimbali, ikiwamo East Africa Banker Lifetime Achievement Award mwaka 2016.

DCB Commercial Bank imesema uteuzi huo unafungua ukurasa mpya wa uongozi wa benki hiyo, ukiwa na msukumo wa kuimarisha mabadiliko, ubunifu, ukuaji endelevu na uundaji wa thamani kwa benki, wateja, wanahisa na wadau wake.

Uteuzi wa Dkt. Kimei unatarajiwa kuongeza nguvu katika uongozi wa kimkakati wa DCB, kutokana na uzoefu wake mpana katika sekta ya fedha, udhibiti wa benki na usimamizi wa taasisi.




Na Mwandishi Wetu

BAADHI ya Wananchi wa Dar es Salaam hususani watumiaji wa usafiri wa Mabasi wametetea utaratibu wa Mabasi hayo kutoa huduma maeneo mengine tofauti na Kituo cha Mabasi cha Magufuli na kuutaka Uongozi wa Mkoa kulitafakari upya suala hilo.

Awali mapema wiki hii Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila alitoa muda wa wiki moja hadi Agosti 21 Mwaka huu kwa mabasi yote yanayotoa huduma tofauti na Kituo cha Mabasi cha Magufuli kuondoka katika maeneo hayo na kurejea kituoni hapo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti tangu kutolewa kwa agizo hilo, wananchi hao hususani watumiaji wa huduma hizo za Usafiri wamesema agizo hilo la Mkuu wa Mkoa lina lengo la kuwarejesha kwenye kadhia waliyokuwa wakiipata awali.

Wamesema kulingana na  jiografia ya Jiji la Dar es Salaam ni changamoto kubwa kwa abiria kutoka maeneo mbalimbali kupata 'urahisi' wa kwenda Mbezi kwa ajili ya kusafiri hususani nyakati za usiku ambapo mara nyingi usafiri huwa shida na wakati mwingine tatizo la foleni.

" Hakuna ubishi kuwa uwepo wa huduma hizi maeneo tofauti na Mbezi (Magufuli) umetusaidia kuondoa changamoto nyingi, mbali na usumbufu unaotokana na kero za wapiga debe, suala la umbali wa kukifikia kituo hicho ilikuwa ni tatizo jingine" amesema mmoja wa wananchi aliyejitambulisha kwa jina la Seif Juma

Amesema ni vyema uongozi wa Mkoa ukalitafakari upya suala hilo hasa Kipindi hiki ambapo pia safari nyingi za Mabasi zinafanyika usiku kwa madai kwamba uwepo wa 'vituo vidogo' hivyo mitaani vinasaidia kuepusha usumbufu kwa abiria ikiwemo kuepuka kuibiwa mizigo na mali zao.

Naye mwananchi Emmanuel Yesaya, abiria aliyekuwa safarini kuelekeza Mkoa wa Katavi, amesema imekuwa nafuu sana kwa wageni kutoka Mkoani kwa uwepo wa 'vituo vidogo' hivyo mitaani kwani imekuwa ikiwaondolea usumbufu Mkubwa kutokana na ugeni wao.

Amesema kwa mgeni ambaye mara ya kwanza anashuka Mbezi hukumbana na 'adha' kubwa ikiwemo usafiri kwenda eneo alilokusudia akisisitiza kuwa uwepo wa Mabasi hayo yanayopakia na kushusha mbali na Kituo cha Magufuli umeiondoa kabisa changamoto hiyo.

Wamesema tangia kuanza kwa huduma hizo, kwa kiasi kikubwa kumesaidia abiria wengi kuondokana kero zikiwemo za kupoteza mizigo yao sambamba na kero ya usafiri kutoka maeneo watokayo kwenda Kituo Cha Magufuli huku pia wakiitumia nafasi hiyo kuishukuru Serikali kwa kuruhusu uwepo wa 'vituo hivyo miaka michache iliyopita.

Hata hivyo Uongozi wa Chama Cha Wamiliki wa Mabasi Tanzania(TABOA)  haukupatikana kulizungumzia suala hilo huku ikielezwa kuwa Utaratibu wa uwepo wa vituo hivyo mitaani ulitokana na Baraka za Serikali huku Mamlaka ya Usimamizi wa Huduma za Usafiri nchini (LATRA) ikiweka utaratibu wa utoaji wa vibali vya Mabasi kutoa huduma hizo katika maeneo hayo.



Na Janeth Raphael -MichuziTv 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewataka Watanzania kulinda amani, usalama na utulivu wa nchi, akisisitiza kuwa misingi hiyo ndiyo nguzo kuu inayowezesha uwekezaji, ukuaji wa uchumi, utalii, biashara, ajira na maendeleo ya jamii.

Akihitimisha Tamasha la Kizimkazi Festival leo Ijumaa, Agosti 14, 2026, visiwani Zanzibar, Rais Samia amesema Tanzania imeendelea kupata mafanikio katika maeneo mbalimbali kutokana na kuwepo kwa mazingira ya amani na utulivu, hivyo wananchi wanapaswa kutambua thamani ya amani na kuilinda kwa nguvu zote.

Amesema maendeleo yanayoonekana nchini, ikiwemo kuongezeka kwa shughuli za uwekezaji, utalii, biashara na huduma za jamii, yanahitaji mazingira salama na yenye utulivu ili yaendelee kukua na kuwanufaisha wananchi. Kwa mujibu wa Rais Samia, juhudi za Serikali za kufungua fursa za kiuchumi na kijamii haziwezi kuzaa matokeo yaliyokusudiwa iwapo amani na usalama vitavurugwa.

Rais Samia amesisitiza kuwa Tanzania haiwezi kufikia malengo yake ya maendeleo endapo itaingia katika mazingira ya vurugu na machafuko, kwa kuwa hali hiyo inaweza kuvuruga shughuli za kiuchumi, kudhoofisha uwekezaji, kuathiri utalii na biashara, pamoja na kupunguza fursa za ajira zinazolengwa kuwafikia Watanzania, hususan vijana.

Kwa msisitizo, Rais Samia amewataka Watanzania kutolichukulia suala la amani kama jambo la kawaida au la kujihakikishia milele, bali kulitambua kama tunu muhimu inayohitaji kulindwa na kila mmoja. Amesema amani ndiyo mazingira yanayowezesha wananchi kufanya kazi, kufanya biashara, kuwekeza, kusoma na kushiriki katika shughuli mbalimbali za maendeleo bila hofu.

Aidha, amewataka vijana kuwa mstari wa mbele katika kulinda amani ya nchi na kutokubali kushawishiwa kufanya vitendo vinavyoweza kusababisha machafuko au kuvuruga utulivu wa taifa, akisisitiza kuwa kizazi cha sasa kina wajibu wa kuhakikisha Tanzania inaendelea kuwa nchi salama kwa ajili ya vizazi vijavyo.

“Uwekezaji, maendeleo tunayoyaona hapa; uwekezaji, utalii, biashara, ajira na huduma za jamii hayawezi kustawi katika mazingira ya vurugu na uvunjifu wa amani. Niwaombe Watanzania wenzangu hususan vijana msikubali kuharibu amani ya nchi yenu. Amani ndiyo kila kitu katika maisha yetu,” amesema Rais Samia.

Amesema kulinda amani ni zaidi ya kulinda utulivu wa nchi, kwani ni kulinda fursa za kiuchumi, ajira, uwekezaji, utalii, biashara na huduma zinazowezesha maisha ya wananchi kuendelea kuboreka. Kwa msingi huo, amewataka Watanzania wote kuendelea kushirikiana katika kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa nchi yenye amani, usalama na utulivu ili safari ya maendeleo iendelee kwa kasi.









 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amewataka wananchi wa Kizimkazi na maeneo ya Kusini Unguja kutunza na kudumisha miradi ya maendeleo, ikiwemo maji, afya na barabara, ili iendelee kutoa huduma bora kwa wananchi.

Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo, tarehe 14 Agosti 2026, katika kilele cha Tamasha la Kizimkazi 2026 kilichofanyika Uwanja wa Mwehe, Makunduchi, Mkoa wa Kusini Unguja.

Amesema miradi hiyo ni muhimu katika kuboresha maisha ya wananchi na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii, hivyo wananchi wanapaswa kushirikiana na Serikali katika kuitunza na kuhakikisha inatumika kwa malengo yaliyokusudiwa.

Aidha, Rais Dkt. Mwinyi amesema Tamasha la Kizimkazi limeendelea kuwa jukwaa muhimu la kutangaza utalii, utamaduni na fursa za uwekezaji, kukuza vipaji, pamoja na kuwaunganisha wafanyabiashara na wajasiriamali na masoko mapya.

Ameipongeza Kamati ya Maandalizi kwa kuendelea kulikuza tamasha hilo na kusisitiza kuwa Serikali itaendelea kuunga mkono matukio yanayochangia kukuza utalii, utamaduni, biashara, ajira na kipato kwa wananchi.

Tamasha la Kizimkazi 2026 lilifunguliwa tarehe 12 Agosti 2026 na Rais Dkt. Mwinyi na kuhitimishwa leo, tarehe 14 Agosti 2026, na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika Uwanja wa Mwehe, Makunduchi, Mkoa wa Kusini Unguja. 














NA: MWANDISHI WETU, ZANZIBAR 

Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Taifa, Mary Chatanda, ameungana na viongozi na wananchi katika Tamasha la Kizimkazi katika mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar.

Akizungumzia tamasha hilo,  Agosti 13, 2026, Chatanda amesema, linasaidia kukuza upendo, mshikamano na maendeleo miongoni mwa viongozi na wananchi, hivyo linapaswa kuendelezwa. 

"Tamasha la Kizimkazi linawaleta watu pamoja kutoka maeneo tofauti nchini, hili ni jambo kubwa sana, tunaongea na kubadilishana mawazo. Pia, miradi ya maendeleo kama ya elimu, afya, maji inazinduliwa katika kutatua kero za wananchi," amesema Chatanda

Aidha, amepongeza suala la utamaduni kuenziwa katika tamasha hilo, kwani utamaduni una umuhimu mkubwa katika kuliheshimisha taifa na kukuza maendeleo.

"Upekee mwingine wa tamasha hili ni kuenzi utamaduni wetu yaani mavazi, vyakula, ngoma za asili, lugha yetu ya Kiswahili, tukumbuke kuwa utamaduni unaibua fursa za kiuchumi katika kuongeza kasi ya maendeleo," amesisitiza.

Katika tamasha hilo, Chatanda ameshiriki uzinduzi na ukaguzi wa mradi wa Makaazi wa Amani (Amani Residency) na upandaji miti katika Kituo cha Afya Kizimkazi.

Viongozi mbalimbali wakiwemo Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, Dk. Hussein Mwinyi, mawaziri, wabunge, viongozi wa Chama, serikali na wananchi mbalimbali wameshiriki tamasha hilo ambalo linagusa nyanja zote za kijamii, kiuchumi na kisiasa katika kukuza maendeleo nchini.











Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akizungumza alipotembelea banda la Kampuni ya Mawasiliano Yas katika Maonesho ya Tamasha la Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, Agosti 12, 2026. Yas ni miongoni mwa wadau muhimu wa Uchumi wa Buluu na maendeleo ya utalii Zanzibar, kupitia uwekezaji wake katika miundombinu ya mawasiliano na huduma za kidijitali zinazochangia kuimarisha muunganisho na ukuaji wa sekta ya utalii visiwani humo.




 

MERIDIANBET imeongeza ladha mpya kwenye burudani za kasino kwa kuleta Expanse Epic Spins, Epic Rewards, mashindano maalum yanayowapa wachezaji nafasi ya kupanda kwenye leaderboard huku wakifukuzia sehemu ya zawadi nono yenye thamani ya jumla ya TSh milioni 6. Mashindano haya yanaendelea hadi Agosti 21, 2026, kupitia michezo ya sloti ya Expanse inayopatikana ndani ya Meridianbet.

Kwenye Expanse, kila raundi inaweza kuwa hatua nyingine kuelekea kilele cha msimamo. Ili kushiriki, dau la chini kwa kila mzunguko ni TSh 500, huku nafasi kwenye msimamo ikiamuliwa kwa kuzingatia jumla ya kiasi kilichowekwa kama dau kwenye michezo inayoshiriki. Hivyo, kadri mashindano yanavyozidi kupamba moto, wachezaji wanaweza kufuatilia nafasi zao na kuwania kupanda juu zaidi kabla ya muda wa mashindano kufikia ukingoni.

Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Mambo yanakuwa matamu zaidi kwenye Prize Pool ya TSh milioni 6, ambapo mshindi wa nafasi ya kwanza ataondoka na kitita kikubwa cha TSh 1,500,000, huku nafasi ya pili ikizawadiwa TSh 1,000,000 na mshindi wa tatu akipokea TSh 600,000. Lakini si nafasi tatu pekee zinazolipwa, kwani washindi wa nafasi ya nne na tano watapata TSh 450,000 kila mmoja, wakionyesha kuwa mbio za kwenye msimamo zina thamani hadi kwenye nafasi za juu.

Kwa wanaomaliza nafasi ya 6 hadi 10, kila mmoja atapata TSh 200,000, wakati nafasi ya 11 hadi 20 zikitoa TSh 100,000 kila mmoja. Hii ina maana kuwa mashindano yana zawadi kwa washindani wengi wanaofanikiwa kusalia ndani ya nafasi 20 za juu hadi mwisho, hivyo kila nafasi kwenye msimamo inaweza kuwa na maana kubwa wakati wa kufikia hesabu za mwisho.

Sasa ni wakati wa kuingia kwenye Expanse Epic Spins, Epic Rewards, na kujaribu kupanda nafasi za juu kabla ya Agosti 21, 2026. Kwa mashabiki wa kasino wanaopenda ushindani, msisimko na zawadi, Meridianbet inaleta jukwaa la kushindana kwa dau la kuanzia TSh 500 kwa raundi huku ukilenga sehemu ya zawadi hiyo ya TSh milioni 6.

MSIMU wa 2026/27 wa Ligi ya Championship ya Uingereza unaanza rasmi Ijumaa, Agosti 14, kwa mechi kubwa kati ya Wolverhampton Wanderers na Blackburn Rovers. Mechi hii itachezwa uwanjani Molineux, mji wa Wolverhampton, ikianza saa 21:00 usiku.

Wolves wanaingia msimu huu wakiwa wametoka kushuka daraja kutoka Premier League baada ya kumaliza msimu uliopita nafasi ya mwisho kabisa wakiwa na pointi 20 tu. Kushuka huko kuligharimu kazi ya kocha Rob Edwards, na sasa timu inaongozwa na kocha mpya, César Peixoto, aliyekuja kutoka klabu ya Gil Vicente nchini Ureno.

Peixoto ameshaanza kuiimarisha timu kwa wachezaji wapya akiwemo beki wa kimataifa Kieran Trippier na mshambuliaji Raul Jimenez, huku wachezaji kama Joao Gomes wakiondoka kwenda Aston Villa. Katika mechi yao ya maandalizi ya Kombe la Ligi (EFL Cup), Wolves walionyesha nguvu kwa kuwafunga Port Vale mabao 3-0, wakidhibiti mchezo kwa asilimia kubwa ya umiliki wa mpira.

Kwa upande wa Blackburn Rovers, timu hiyo ilimaliza msimu uliopita katika nafasi ya 20 ya Championship, ikiwa na pointi tano tu juu ya eneo la kushuka daraja. Msimu ulikuwa mgumu kwa Rovers, ambao walimaliza vibaya wakiwa hawajashinda katika mechi tano kati ya sita za mwisho.

Meridianbet inasema kuna michezo kama Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli. Ingia katika kasino ya mtandaoni ya Meridianbet na ujiokotee mkwanja mapema. Jiunge sasa au Tembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Klabu hiyo sasa inaongozwa na kocha mpya, Tony Mowbray, aliyeteuliwa Juni, na maandalizi yake ya awali yamekuwa ya mchanganyiko matokeo ya sare na hasara katika baadhi ya mechi za kirafiki. Hata hivyo, katika mechi yao ya kwanza rasmi ya msimu dhidi ya Burton Albion katika EFL Cup, Blackburn walionyesha ari nzuri wakishinda baada ya kuwa nyuma kwa bao, matokeo yaliyomridhisha kocha Mowbray.

Kihistoria, Wolves wana ubora dhidi ya Blackburn, wakiwa na ushindi 42 dhidi ya ushindi 40 wa Blackburn, huku mechi 25 zikiishia sare. Wolves pia wameshinda bila kufungwa katika mechi zao mbili za mwisho dhidi ya Blackburn, jambo linaloonyesha ugumu ambao Rovers watakutana nao katika ulinzi wao.

Kwa ujumla, mechi hii itakuwa kipimo cha awali cha uwezo wa makocha wapya wa pande zote mbili Peixoto kwa Wolves na Mowbray kwa Blackburn katika kuunda timu zenye ushindani kwa msimu mzima.

Wolves wana faida ya kuchezea nyumbani na msukumo wa kutaka kurejea haraka Premier League, huku Blackburn wakitafuta kuanza vizuri baada ya msimu mgumu uliopita. Matokeo ya mechi hii yataweka msingi wa hali ya kisaikolojia kwa timu zote mbili wanapoanza safari ndefu ya msimu wa Championship.

Serikali imevitaka vyama vya wafanyakazi nchini, ikiwemo Chama cha Walimu Tanzania (CWT), kutumia meza ya majadiliano (Social Dialogue) kutatua kero za wafanyakazi badala ya  migongano isiyo na tija inayodhoofisha mshikamano na kushusha morali ya kazi.

Rai hiyo imetolewa na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Ajira na Mahusiano Mheshimiwa Dr. Evaline Munisi wakati akifungua rasmi mafunzo ya siku mbili kwa watumishi wa Makao Makuu na Makatibu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) wa Mikoa na Wilaya kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi hiyo Deus Sangu leo Agosti 13, 2026 mjini Morogoro.

Amesema kuwa Vyama vya Wafanyakazi havikuundwa kwa ajili ya kusigana na Waajiri, bali viliundwa kama jukwaa la kisheria la kukaa meza moja na waajiri ili kujadiliana kwa hoja, ushahidi na kuheshimiana.

"Vyama vya wafanyakazi havikuundwa kwa ajili ya kusigana na waajiri, bali viliundwa kama jukwaa la kisheria la kukaa meza moja ili kupata suluhu ya pamoja. Katika miaka ya hivi karibuni tumeona kuibuka kwa makundi yanayojielekeza zaidi katika propaganda na migongano, jambo linalodhoofisha mshikamano wa walimu na kuathiri ubora wa elimu," alisema.

Akiangazia kaulimbiu ya CWT inayosema "Wajibu na Haki, Naibu Waziri amesema kuwa  mambo hayo mawili ni kama ndugu pacha wanaotembea pamoja, hivyo ni lazima walimu watimize wajibu wao wa kiutumishi kabla ya kudai haki zao.

Amesema ni wajibu wa chama hicho kutetea maslahi ya walimu kama mishahara, upandaji vyeo na malimbikizo, lakini pia ni wajibu wao kuwasimamia walimu wafundishe kwa juhudi na nidhamu.

"Mwalimu asiyetimiza wajibu wake, anayetoroka kazini au anayekiuka maadili anakosa halali ya kimaadili ya kudai haki zake na anakiharibia chama sifa njema. Utendaji bora darasani ndio unaoipa CWT nguvu ya kusimama mbele ya Serikali kudai haki," alisema.

Ameongeza kuwa ulimwengu wa leo unaendeshwa na mifumo ya kidijitali na sheria, hivyo mtazamo wa zamani wa kuendesha vyama kwa mazoea na mihemko hauna nafasi tena, Serikali inatarajia kuona mabadiliko makubwa katika kasi ya kutatua kero za walimu na uadilifu wa matumizi ya fedha baada ya mafunzo hayo.

Katika hatua nyingine, Naibu Waziri amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kufanya uwekezaji mkubwa katika sekta ya elimu kwa kujenga miundombinu na kuajiri walimu wapya ili kupunguza mzigo wa kazi.

Aidha Serikali itaendelea kuweka mazingira bora ya kazi na kushirikiana na CWT ili kulinda amani na utulivu mahali pa kazi. Mafunzo hayo ya siku mbili yamejumuisha washiriki takriban 240 yakilenga kuwajengea uwezo katika sheria za kazi, taratibu za Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), na utendaji wa Bodi ya Kitaaluma ya Walimu.

Aikizungumza awali mwakilishi wa Msajili wa Vyama vya Wafanyakazi na Waajiri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano Mussa Msami amesema kuwa kitengo cah Msajili wa Vyama vya Wafanyakazi na Waajiri milango iko wazi kwa ushauri ushirikiano wakati wote. 






Na Belinda Joseph-Dodoma.

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Mkoa wa Dodoma limefanya kikao kikao kazi na Maafisa wa Jeshi la Polisi ngazi ya kata, wilaya na Mkoa wa Dodoma, kwa lengo la kuimarisha ushirikiano katika ulinzi wa miundombinu ya umeme na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kulinda miundombinu hiyo.

Akizungumza katika kikao hicho, Kaimu Meneja wa TANESCO Mkoa wa Dodoma, Mhandisi Kurwa Mangara, amesema ushirikishwaji wa vyombo vya ulinzi ni muhimu kutokana na nafasi ya umeme katika maisha ya wananchi na shughuli za kiuchumi.

Amesema hatua hiyo imechukuliwa kutokana na changamoto za uhujumu na uharibifu wa miundombinu ya uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme, ikiwemo wizi wa vyuma na bolti pamoja na uvamizi wa maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya njia za kusafirisha umeme.

Mangara ameeleza kuwa baadhi ya maeneo hayo yamekuwa yakitumika kwa shughuli za kilimo na uchimbaji wa mchanga na kokoto, hali inayoweza kusababisha mmomonyoko wa udongo na kuhatarisha nguzo pamoja na miundombinu mingine ya umeme.

Aidha, ametaja changamoto ya kuibiwa nyaya zinazotumika kulinda transfoma na kuchomwa kwa nguzo za umeme wakati wa uandaaji wa mashamba vitendo ambavyo vinaweza kusababisha kukatika kwa umeme, hasara kwa TANESCO na usumbufu kwa wananchi.

Ametoa wito kwa wananchi kutambua thamani ya miundombinu ya umeme na kuacha vitendo vinavyoweza kuhatarisha upatikanaji wa nishati hiyo, akisisitiza kuwa ulinzi wa miundombinu ya umeme ni jukumu la pamoja kwa TANESCO, vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na wananchi.

Kwa upande wake, Kaimu Afisa wa Jeshi la  Polisi  ASP Regina Mtana, amewashukuru TANESCO kwa kutoa elimu hiyo na kuahidi kuwa Jeshi la Polisi litaendelea kushirikiana na shirika hilo katika kuimarisha ulinzi wa miundombinu ya umeme na kuchukua hatua dhidi ya vitendo vinavyoweza kuhatarisha usalama na upatikanaji wa nishati hiyo.






Top News