

Na Janeth Raphael- MichuziTv -Dodoma.
Serikali imesema inaendelea kuchukua hatua mahsusi za kupunguza gharama za uzalishaji wa zao la tumbaku ili kuongeza faida kwa wakulima na kuimarisha mchango wa zao hilo katika uchumi wa nchi.
Kauli hiyo imetolewa leo Mei 12, 2026 bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Kilimo, David Silinde, wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Jacqueline Kainja Andrew, aliyetaka kujua ni lini Serikali itaangalia upya gharama za uzalishaji wa tumbaku ili wakulima waweze kunufaika zaidi na kilimo hicho.
Akijibu swali hilo, Silinde amesema Serikali inatambua changamoto mbalimbali zinazowakabili wakulima wa tumbaku, ikiwemo ongezeko la bei za pembejeo, gharama kubwa za nishati inayotumika katika ukaushaji wa tumbaku kama kuni na makaa, pamoja na riba kubwa za mikopo kutoka taasisi za kifedha.
Amesema kupitia Bodi ya Tumbaku kwa kushirikiana na wadau wa sekta hiyo, tayari Serikali imeanza kufanya tathmini ya kina ya muundo wa gharama za uzalishaji ili kubaini maeneo yanayochangia mzigo mkubwa kwa wakulima na namna ya kupunguza gharama hizo.
“Serikali inaangalia maeneo mbalimbali ikiwemo tozo za vyama vya ushirika, gharama za pembejeo pamoja na masharti ya mikopo inayotolewa kwa wakulima wa tumbaku,” amesema Silinde.
Aidha, amesema Serikali tayari imeanza mazungumzo na benki pamoja na taasisi za kifedha zinazotoa mikopo kwa wakulima wa tumbaku ili kujadili uwezekano wa kupunguza riba na gharama nyingine zinazohusiana na huduma za kifedha.
Kwa mujibu wa Silinde, hatua hizo ni sehemu ya mkakati wa Serikali wa kuhakikisha wakulima wa tumbaku wanapata faida stahiki kutokana na jasho lao, huku zikilenga kuongeza tija na kuimarisha uzalishaji wa zao hilo muhimu la biashara nchini.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na viongozi mbalimbali kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam kabla ya kuondoka nchini, kuelekea Uganda kuhudhuria Sherehe za Uapisho wa Rais wa nchi hiyo Mhe. Yoweri Kaguta Museveni tarehe 12 Mei, 2026.


NA: MWANDISHI WETU, PANGANI.
Utekelezaji wa mtaala mpya wa elimu unaozingatia umahiri kwa wanafunzi unaendelea kutekelezwa nchi nzima katika kuhakikisha nchi inazalisha wahitimu wenye uwezo wa kujiajiri badala ya kutegemea kuajiriwa.
Katika Shule ya Sekondari Funguni ya wilayani Pangani mkoani Tanga, Mei 8, 2026, wanafunzi wa kidato cha pili wa shule hiyo, katika somo la Biashara (Business Studies), wameweza kupika vitafunwa mbalimbali kama chapati, maandazi, sambusa na vitumbua ikiwa ni sehemu ya ujifunzaji kwa vitendo wa uzalishaji wa bidhaa mbalimbali zilizo katika mazingira yao (local production).
Mwalimu wa somo la Biashara wa shule hiyo, Shija Clement amesema baada ya ujifunzaji wa nadharia wa Mada ya Uzalishaji (Production), wanafunzi wanapaswa kuweka ujifunzaji huo kwa vitendo ili kuwajenga katika umahiri na kujitegemea hata baada ya kuhitimu masomo yao ili pia waweze kujiajiri wenyewe na kuanzisha biashara zao.
"Wanafunzi wanapaswa kuwa na ujuzi fulani wanapohitimu masomo, wanafunzi hawa wamefanya kwa vitendo utengenezaji wa sambusa, chapati, maandazi na vitumbua lakini pia wamewauzia wanafunzi wenzao ili kuangalia kama uzalishaji wao umewapatia faida au hasara," amesema Shija.
Sambamba na hilo, Shija amesema somo la Biashara linahitaji kufanya vitendo zaidi kwa sababu elimu ya biashara inapaswa kuwekwa katika vitendo ili tija ya kupata faida ionekane badala ya kubaki na maarifa ya biashara kichwani pekee.
Katika hatua nyingine, mwanafunzi ambaye ameshiriki kupika vitafunwa hivyo, Fatuma Madaba amesema amefurahia mapishi na ameongeza uelewa wa namna ya kupika vitafunwa hivyo, ujuzi ambao anaweza kutumia hata akimaliza shule katika kujiingizia kipato.
"Nimeongeza kitu kikubwa katika mapishi ya leo, elimu hii ya ujasiriamali tunayofundishwa imenisaidia kunijenga hata baada ya kuhitimu masomo yangu naweza kuingiza kipato," amesema Madaba.
Kwa upande wa Mkuu wa Shule hiyo, Nassoro Gamba, amepongeza ubunifu huo ambao umejikita kuimarisha stadi za umahiri katika ujenzi wa vizazi vyenye kujitegemea katika maisha. Pia, ameahidi kuwa mteja wa kudumu wa bidhaa zao watakazoendelea kuzizalisha shuleni hapo.
Ikumbukwe kuwa somo la Biashara ni miongoni mwa masomo ya lazima kwa wanafunzi wa shule za sekondari nchini, ikiwa ni mkakati wa serikali wa kuzalisha wahitimu wenye maarifa na ujuzi fulani katika kujipatia kipato ili kuepuka kusubiri kuajiriwa.
📍Lwamgasa, Geita
Bodi mpya ya Wakurugenzi ya Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) leo 11 Mei, 2026 imefanya ziara ya kutembelea miradi mbalimbali ya Shirika hilo iliyoko kanda ya Ziwa. Lengo la ziara hiyo ni kujionea utekelezaji na kuhakikisha miradi inatekelezwa kama ilivyopangwa na kukidhi malengo yaliyowekwa na Shirika.
Wajumbe wa bodi hiyo wametembelea kwanza kituo bora cha mfano kwa wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu uliopo katika Kata ya Lwamgasa, Wilaya ya Geita. Mradi huo hutumika kama darasa la kutoa elimu kwa wachimbaji wadogo wa madini kutoka sehemu mbalimbali nchini.
Akizungumza moja ya wajumbe hao Bw. Leonard Chacha, amesema mgodi wa Lwamgasa ni mgodi wa mfano nchini. Amesisitiza kuwa kupitia mgodi huo, wachimbaji wanafundishwa namna bora ya kuchimba kisasa ili kuongeza tija na kuhakikisha usalama wao wakati wa kazi na utunzaji wa mazingira.
Chacha aliongeza kuwa pamoja na mafunzo ya uchimbaji, wachimbaji hao pia huwezeshwa kutumia mashine za kisasa katika uchenjuaji wa madini ya dhahabu. Alisema kuwa hatua hiyo inalenga kuwaondoa wachimbaji wadogo kwenye teknolojia duni inayowapotezea madini mengi na kuharibu mazingira.
Katika hatua nyingine ya ziara hiyo, wajumbe wa bodi walitembelea Mgodi wa Dhahabu wa Buckreef ambao STAMICO inauendesha kwa ubia na kampuni ya TRX Gold Corporation. Wajumbe hao walipata wasaa wa kupata taarifa ya mradi na kukagua shughuli mbalimbali za uzalishaji kuanzia uchimbaji hadi uchenjuaji.
Aidha, Wajumbe wa bodi wameridhishwa na hali ya utunzaji wa mazingira katika mgodi wa Buckreef. Wamesema uongozi wa mgodi umeweka mikakati mizuri ya kuhakikisha shughuli za uchimbaji hazileti madhara kwa mazingira yanayozunguka eneo la mradi.
Wilson Mutagwaba, Mjumbe wa Bodi ya STAMICO, amekiri kuridhishwa na hatua zinazochukuliwa katika mgodi wa Buckreef. Amesema pamoja na utunzaji wa mazingira, suala la usalama mahali pa kazi limepewa kipaumbele kikubwa na wafanyakazi wote wanafuata taratibu za usalama.
Bodi ya Wakurugenzi imeahidi kutoa ushirikiano wa dhati katika kufanikisha shughuli za Shirika na kuendelea kufanya ziara za mara kwa mara katika miradi yote ya STAMICO nchini. Lengo ni kuhakikisha miradi hiyo inakuwa na tija kwa Taifa, inalipa kodi stahiki na inawanufaisha wananchi wanaozunguka maeneo ya miradi hiyo.
Stylish women. Beautiful moments. Premium vibes. #ToastToMoms by Serengeti Apple ilikuwa full elegance all weekend.#SerengetiApple #SophisticationBottled #ToastToMoms @serengeti.apple
Wanawake wa kisasa walitokelezea kwa fashion, confidence na classy vibes kusherehekea #ToastToMoms.#SerengetiApple #SophisticationBottled #ToastToMoms @serengeti.apple
Mother’s Day lakini kwa elegance, style na unforgettable vibes.#SerengetiApple #SophisticationBottled #ToastToMoms @serengeti.apple
Wanawake walipendeza. Vibes zilikuwa premium. Serengeti Apple delivered the moment.#SerengetiApple #SophisticationBottled #ToastToMoms @serengeti.apple
Fashion, laughter, beautiful toasts na premium moments — hivyo ndivyo #ToastToMoms ilivyokuwa.#SerengetiApple #SophisticationBottled #ToastToMoms @serengeti.apple
Soft life, stylish moments na celebration za kweli Siku ya Mama Duniani.#SerengetiApple #SophisticationBottled #ToastToMoms @serengeti.apple
Classy looks. Beautiful smiles. Mother’s Day vibes done right.#SerengetiApple #SophisticationBottled #ToastToMoms @serengeti.apple
Elegant women + premium vibes + unforgettable toasts.#SerengetiApple #SophisticationBottled #ToastToMoms @serengeti.apple
Weekend ya fashion, vibes na celebrating moms the sophisticated way ikisindikizwa na Serengeti Apple.#SerengetiApple #SophisticationBottled #ToastToMoms @serengeti.apple
Wanawake wa Dar walijitokeza kwa confidence, elegance na premium energy kusherehekea Siku ya Mama Duniani na Serengeti Apple.#SerengetiApple #SophisticationBottled #ToastToMoms @serengeti.apple
Katika hatua muhimu kwa sekta ya benki nchini na uongozi wa taasisi za kibiashara barani Afrika, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB Plc, Ruth Zaipuna, anatarajiwa kuzungumza katika Cambridge Africa Business Conference 2026, utakaofanyika Mei 30, 2026 katika Chou cha Biashara cha Cambridge Judge chini ya Chuo Kikuu cha Cambridge Uingereza.
Katika jukwaa hilo, Zaipuna anatarajiwa kutoa hotuba kuu kuhusu safari ya mageuzi ya NMB na mchango wake katika uchumi wa Tanzania, akieleza namna benki hiyo ilivyokua kutoka katika mizizi ya huduma ndogo za fedha hadi kuwa moja ya taasisi zinazoongoza katika sekta ya fedha nchini.
Mkutano huo wenye kaulimbiu ya “Kujenga Mustakabali wa Afrika: Mitaji, Ubunifu na Ukuaji wa Kiwango cha Bara,” unalenga kujadili nafasi ya Afrika katika kuchochea ukuaji kupitia mitaji, ubunifu na uwezo wa taasisi za Afrika kufanya kazi kwa kiwango cha bara, hususan katika mazingira ya AfCFTA.
Akizungumzia mwaliko huo, Zaipuna alisema ni heshima kwa NMB na Tanzania, akibainisha kuwa safari ya benki hiyo inaonesha kuwa taasisi zinazoongozwa na Waafrika zinaweza kujenga ubora wa kiwango cha dunia huku zikibaki karibu na mahitaji ya wananchi, biashara na vipaumbele vya taifa.
Msimamizi
Mkuu wa Zoezi la 14 la Vikosi vya Ulinzi na Usalama vya Uamrishaji vya
Jumuiya ya Afrika Mashariki “Ushirikiano Imara 2026” Balozi Lindsay
Kiptiness akiwakaribisha viongozi na maafisa wa kijeshi kutoka nchi za
Kenya, Tanzania, Burundi, Uganda, Rwanda, Somalia na Sudani Kusini
wanaoshiriki zoezi hilo Jijini Nairobi leo Mei 11, 2026. Zoezi hilo
linalenga kuimarisha ushirikiano wa kikanda pamoja na kuongeza uwezo wa
pamoja wa kukabiliana na changamoto za kiusalama zinazoikabili kanda
hiyo.
Zoezi hilo limewakutanisha viongozi na maafisa wa kijeshi kutoka nchi za Kenya, Tanzania, Burundi, Uganda, Rwanda, Somalia na Sudani Kusini kwa lengo la kuimarisha ushirikiano wa kikanda pamoja na kuongeza uwezo wa pamoja wa kukabiliana na changamoto za kiusalama zinazoikabili kanda hiyo.
Akizungumza katika hafla hiyo, Balozi amesema kuwa kufanyika kwa zoezi hilo kuna umuhimu mkubwa katika kuimarisha mfumo wa usalama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, akibainisha kuwa mabadiliko ya hali ya usalama duniani yanahitaji nchi wanachama kushirikiana kwa karibu zaidi katika kulinda amani, utulivu na ustawi wa wananchi wake.
Aidha, amesema migogoro na hali ya kutokuwa na utulivu katika maeneo mbalimbali duniani, hususani Mashariki ya Kati pamoja na maeneo mengine yenye migogoro, inaendelea kuathiri kwa namna mbalimbali uchumi, usalama na maisha ya wananchi wa nchi za EAC. Amesema hali hiyo inaonesha umuhimu wa kuendelea kuimarisha mshikamano wa kikanda, kubadilishana taarifa za kiusalama na kuwa na mikakati ya pamoja ya kukabiliana na changamoto hizo.












.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)




.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)