Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu akitoa ufafanuzi kwa Waheshimiwa Wabunge, wakati akichangia mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Taasisi zake na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2026/2027 katika Bunge la 13, Mkutano wa Tatu, kikao cha Tisa leo Aprili 15, 2026 Jijini Dodoma.

************

Na: OWM (KAM) – Bungeni, Dodoma

Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amepongezwa kwa kuchukua hatua madhubuti katika kuimarisha Mifuko ya Hifadhi ya Jamii nchini kwa lengo la kuhakikisha ustawi wa wananchi, pamoja na kuhakikisha utoaji wa pensheni kwa wakati.

Pongezi hizo zimetolewa Bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mheshimiwa Deus Clement Sangu, leo Aprili 15, 2026 wakati akichangia mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Taasisi zake na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2026/2027.

Aidha, Mhe. Sangu amesema thamani ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii imeendelea kuongezeka ikiwemo Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) thamani yake imeongezeka kutoka Shilingi Trilioni 4.36 hadi Shilingi Trilioni 10.3. Mfuko wa PSSSF thamani yake iliongezeka kutoka Shilingi Trilioni 5.74 hadi Shilingi Trilioni 12.96.

Waziri Sangu amefafanua kuwa deni la Serikali katika mfuko wa PSSSF ilikuwa Trilioni 4.46, mwaka 2022/2023 Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alitoa hati fungani ya shilingi trilioni 2.17 kwa ajili ya kuulipa mfuko wa PSSSF deni lililodumu kwa muda mrefu la shilingi trilioni 4.6 la michango kabla ya 1999. Pia, Serikali imeendelea kulipa Trilioni 2.09 ambayo imesaidia thamani ya Serikali kulipa mfuko huo wa PSSSF kufikia asilimia 95.

Vilevile, Mhe. Sangu amesema kuwa kutokana na mifuko ya hifadhi ya jamii kuwa himilivu imepelekea kwa sasa watumishi wa umma wanaostafu wanalipwa mafao yao ndani ya siku ishirini na tano huku kiwango cha kima cha chini cha pesheni kuongezeka toka shilingi 100,000 hadi kufikia shilingi 250,000 kwa wastaafu.

Kadhalika, Waziri Sangu amesema Mifuko ya hifadhi ya jamii imeendelea kuwekeza katika miradi yenye tija kwa lengo la kuongeza thamani ya michango ya wanachama na kukuza uchumi pamoja na kuongeza ajira kwa wananchi.

Akihitimisha mchango wake, Mheshimiwa Sangu aliwahakikishia wabunge kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano itaendelea kusimamia utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2026/2027 kwa ufanisi, ili kuleta manufaa kwa Watanzania katika sekta zote za kiuchumi na kijamii.

Kwa upande wake, Spika wa Bunge, Mheshimiwa Mussa Azan Zungu, amewapongeza wabunge kwa kupitisha bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu na kusisitiza umuhimu wa wizara na taasisi husika kusimamia utekelezaji wake ili kuchochea maendeleo ya wananchi.


Na. Jacob Kasiri - Moshi.

“Dhamira ya kuurejesha Mlima Kilimanjaro katika usafi wake wa asili imejadiliwa leo Aprili 15, 2026 mjini Moshi katika kikao cha pamoja kilichowahusisha wawakilishi kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii, TANAPA na wamiliki wa Kampuni za utalii.

Uzalishaji wa taka ngumu na laini mlimani na baadae kuzishusha katika malango ya kushukia watalii imeonekana kama ndoto. Lakini ndoto hii itakuwa na matokeo chanya endapo, wenye makampuni ya utalii, waongoza wageni, Watalii na Wapagazi (wagumu) wataungana kwa pamoja kukusanya na kushusha ili kulinda mazingira na mandhari ya mlima huu unaoingiza takribani watalii elfu 65 kwa mwaka.

Akiongea namna ya kudhibiti uchafu, Mwenyekiti wa kikao hicho Bw. Michael Kilawila Mmiliki wa Kampuni ya “Coming to Africa” alisema;

“Sisi wenye Makampuni ndio tunaozalisha uchafu mlimani, hivyo ni jukumu letu kwa kushirikiana na mamlaka (KINAPA) kushusha taka hizo kwa kuwa mlima huo ni ofisi yetu. Hivyo sio vizuri kuichafua ofisi inayotuingizia kipato.”

Aidha, Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Kilimanjaro - Kamishna Msaidizi Mwandamizi Angela Nyaki alisema kuwa jitihada mbalimbali za serikali kudhibiti uchafu mlimani zinaendelea kila siku lakini bado uchafu unazalishwa mwingine.

“Ni wajibu wetu kuungana kuhakikisha uchafu tuonazalisha, tushuke nao ili kuufanya mlima wetu uwe safi, pia kumbukeni Mlima Kilimanjaro ni chanzo cha maji yanayotumika katika mji wa Moshi. Hivyo tunapochafua mlima tutambue madhara makubwa wanayapata wananchi wetu wanaotumia maji hayo.”

Sanjari na hilo pia Kamishna Nyaki aliwaomba wenye makampuni ya utalii wanapounadi mlima Kilimanjaro wauze vilele vitatu ambavyo ni Kibo, Shira na Mawenzi tofauti na sasa hivi wanauza kilele cha Kibo tu chenye urefu wa mita 5895 kutoka usawa wa bahari.

Naye, Simbo Natai - Mkurugenzi wa Kampuni ya “African Scenic” alisema; “Suala la uchafu tusiruhusu kuwa janga kwa sehemu tunayojipatia riziki, hivyo katika kikao hiki nashauri kabla ya kuanza kwa msimu wa utalii mwanzoni mwa mwezi mei, 2026 twende mlimani tukakusanye taka hizo na kuzishusha.”

David Mshana Mkurugenzi wa Kampuni ya “Enjoy Kili Ltd”, alishauri kuwa waongoza watalii(Guides) wapya kabla hawajapewa leseni ya kuongoza watalii wapandishwe mlimani kukusanya taka na kushuka nazo ili anapoongoza wageni pamoja na wapagazi awe ni mlinzi wa timu yake kuhakikisha hawatupi uchafu na kuharibu mazingira.

Mbali na mada ya taka mlimani pia agenda kama uokoaji wa wageni mlimani, waongoza watali na wapagazi kuwa na Kanzi Data na mapendekezo ya utoaji vyeti kwa watalii waliofika kileleni kwa njia ya kielektroniki zilijadiliwa na kupewa kipaumbele.










-Ataka watanzania waache tabia ya kujidogosha.

WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema katika kipindi kifupi cha uongozi wake, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameandika historia ambayo kwa namna yoyote haiwezi kufutika kutokana na magaeuzi makubwa aliyoyafanya.

Amesema historia hiyo inaandikwa kutokana na utekelezaji wa miradi mikubwa, uandishi wa dira mpya ya Taifa ya 2025, kubadilisha mfumo wa elimu, kujenga madarasa mengi na shule za elimu ya amali, kuanzisha Bima ya Afya kwa Wote, kupandisha bajeti ya kilimo na kuongeza upatikanaji wa huduma za umeme na maji kwa wananchi vijijini.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo jioni (Jumatano, Aprili 15, 2026) Bungeni jijini Dodoma, wakati akitoa hoja ya kuhitimisha mjadala wa bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Taasisi zake na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2026/2027.

“Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameingia katika historia ya viongozi wachache wa Taifa letu waliopata heshima na bahati ya kuandika Dira ya Taifa 2050 pamoja na nyaraka nyingine muhimu za utekelezaji wa dira ikiwemo mpango wa maendeleao wa muda mrefu.”

Akielezea mafanikio kwenye sekta ya kilimo, Waziri Mkuu amesema: “Ili kuwezesha mageuzi makubwa katika sekta ya kilimo, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan amewezesha kuongezeka kwa bajeti ya Wizara ya kilimo mara tano kutoka shilingi bilioni 270 mwaka 2020/2021 hadi shilingi trillioni 1.23 mwaka 2025/2026. Tumeshuhudia upatikanaji wa pembejeo za kilimo na ongezeko la matumizi ya mbolea.”

Kuhusu nishati, Waziri Mkuu amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameingia katika rekodi kwa utekelezaji mkubwa wa mradi wa bwawa la umeme ambapo kwa sasa nchini kuna ziada ya umeme. “Alipokea huu mradi ukiwa katika asilimia 27 kwenda 30 ya utekelezaji. Amekamilisha mradi huo na sasa tuna ziada ya megawati zaidi ya 2,000. Tanzania ni nchi ambayo sasa ina ziada ya umeme.”

Amesema Mheshimiwa ametoa zaidi ya trilioni 1.2 za kujenga Mradi wa Gridi Imara ili kuondoa tatizo la kukatikatika kwa umeme katika maeneo mbalimbali nchini.

Amesema kuwa Tanzania imesifiwa kwa weledi katika utafutaji wa rasilmali kwenye utekelezaji wa miradi mikubwa. “Juzi imetolewa tuzo kwa kwa nchi yetu ya kufanya vizuri katika kutafuta fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi. Tanzania ni nchi ya mfano kwenye kutafuta rasilimali kwenye kutekeleza miradi mikubwa ya kimkakati.”

Waziri Mkuu amesema kutokana na hayo, katika mradi wa kimkakati wa reli ya kisasa tayari kipande cha tatu na cha nne kimepata fedha za kuanza ujenzi. “Vilevile, kipande cha tano nacho tayari kimepata fedha na utekelezaji wake unategemea certificates za mtekelezaji kadiri anavyokamilisha.”

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewataka Watanzania waache kujidogosha kwani Tanzania imepiga hatua kubwa za kimaendeleo ikilinganishwa na nchi nyingine barani Afrika.

“Hapa Tanzania tunapenda kujidogosha hasa tusipojilinganisha na nchi nyingine. Tuache kujidogosha. Kwenye suala la umeme, hapa Afrika kuna nchi wameunganisha mikoa na mikoa tu lakini sisi kila kijiji umeme umeshafika. Na kwenye vitongoji 68,000, nusu yake umeme umeshafika na vitongoji zaidi ya 9,000 mikataba imeshasainiwa. Kwingine huko, ni mtu na solar yake au jenereta lake. Tunapaswa tujivunie kuwa tuko kwenye nchi ambayo viongozi wake maisha ya kila mtu na kuhakikisha keki ya Taifa inamfikia kila mtu,” ameongeza.

Kwa mwaka wa fedha 2026/2027, Bunge limeidhinisha sh. trilioni 12.5 ambapo kati ya fedha hizo, sh. trilioni 8.73 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na sh. trilioni 3.76 ni kwa ajili ya matumizi ya maendeleo kwa Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake.

Vilevile, Bunge limeidhinisha sh. bilioni 225 kwa ajili ya Mfuko wa Bunge ambapo kati ya fedha hizo, sh. bilioni 207.99 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na sh. bilioni 17.02 ni kwa ajili ya matumizi ya maendeleo.



Rais w a Jamhuri y a Muungano w a Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo
amepokea ujumbe maalum kutoka kwa Katibu Mkuu w a Jumuiya y a Madola, Bi. Shirley Ayorkor Botchwey, uliowasilishwa kwake n a Mjumbe Maalum, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Malawi, Mhe. Dkt. Lazarus McCarthy Chakwera, Ikulu jijini Dar es Salaam.

Ujumbe huo pia umeainisha maeneo y a kipaumbele yanayofuatiliwa n a Jumuiya y a Madola, ikijumuisha uwazi n a ushirikiano katika tathmini ya matukio yaliyojitokeza wakati na baada y a Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025, pamoja n a kupanua ushiriki wa kisiasa, kuendeleza majadiliano y a vyama n a kuimarisha uwajibikaji w a taasisi.

Katika ujumbe wake, Katibu Mkuu Botchwey amesisitiza dhamira ya Jumuiya ya Madola kuendelea kushirikiana n a Tanzania katika kuimarisha misingi y a demokrasia, utawala bora n a maridhiano y a kitaifa kufuatia matukio yaliyojitokeza wakati n a baada y aUchaguzi Mkuu wa Oktoba, 2025.

Ameeleza kuwa Jumuiya y a Madola inaunga mkono juhudi zinazoendelea nchini na iko tayari kusaidia kujenga mazingira y a kisiasa yenye utulivu, ushirikishwaji n a kuaminiana kupitia mazungumzo na mageuzi ya taasisi.

Akizungumza wakati wa kupokea ujumbe huo, Rais Dkt. Samia amesema Tanzania
inaendelea kushughulikia hali hiyo kupitia taasisi zake, akizitaja hatua mbalimbali
zilizochukuliwa n a Serikali, ikiwemo kuunda Tume Huru ya Uchunguzi, kwa lengo la
kurejesha utulivu, na kuimarisha uwajibikaji nchini.

Amebainisha kuwa matokeo ya Tume hiyo yataongoza hatua zinazofuata, ikiwemo
uwajibikaji, maridhiano na mageuzi y a taasisi, huku Serikali ikiendelea kusimamia
mchakato wa maridhiano ikiwemo majadiliano kupitia majukwaa yaliyopo kisheria na ushirikishwaji wa wadau mbalimbali.

Kwa upande wake, Mhe. Chakwera ameeleza utayari wa Jumuiya ya Madola kuendelea kushirikiana n a Tanzania katika juhudi za kuimarisha utawala w a sheria, ushirikiano wa kisiasa na mshikamano w a kitaifa.

Rais Mstaafu Chakwera amehitimisha ziara yake ya kikazi nchini kama Mjumbe Maalum wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola kwa lengo la kufanya tathmini ya hali ya kisiasa na mchakato w a maridhiano, ambapo tayari amekwishakutana n a wadau mbalimbali wa kisiasa na kitaasisi nchini.












Naibu waziri wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe.Dkt Ngwaru Maghembe (Mb.) amewasili nchini Brazil kwa ziara ya kikazi. Mhe. Naibu Waziri Dkt. Maghembe amepokelewa na Balozi wa Tanzania nchini Brazil, Dr. John Stephen simbachawene katika Ofisi ya Ubalozi. Mhe Naibu waziri alipata nafasi ya kukutana na kujadiliana masuala mbalimbali na Watumishi wa Ubalozi na kusisitiza umuhimu wa utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi kwa kuvutia uwekezaji kutoka Brazili.

Katika ziara hiyo Mhe.Dkt Ngwaru Maghembe (Mb.) ataongoza ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Mkutano wa Pili wa Mashauriano ya kisiasa kati ya Tanzania na Brazil. Mkutano huo unalenga kukuza uhusiano wa Kidiplomasia na Ushirikiano baina ya Tanzania na Brazili katika sekta mbalimbali ikiwemo biashara, Uwekezaji, Kilimo, Mifugo na Utalii







Na Mwandishi wetu


Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imeanza kuweka utaratibu wa kutumia hazina ya maarifa na uzoefu kutoka kwa Mabalozi Wastaafu ili kuimarisha utekelezaji wa mipango mbalimbali ya kuimarisha diplomasia ya nchi.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo , amebainisha utaratibu huo leo Aprili 15, 2026, jijini Dar es Salaam wakati anafungua kikao cha mashauriano kati ya uongozi wa Wizara na Mabalozi Wastafu.

"Wizara tumeanzisha utaratibu wa kuwa na vikao vya mara kwa mara na Mabalozi Wastaafu ili kuvuna maarifa na uzoefu wao kwa lengo la kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia ili ulete nanufaa katika nyanja mbalimbali kama vile, siasa, ulinzi na usalama, uchumi, biashara, uwekezaji na utalii". Balozi Kombo alisema.

Balozi Kombo ametaja mifano ya maeneo ambayo angependa Mabalozi Wastaafu wachangie maarifa na uzoefu walio kuwa nao ili maeneo hayo yaendelee kuwa na manufaa zaidi kwenye nchi.

Maeneo hayo ni pamoja na mwenendo wa ufanyaji wa biashara baina ya Tanzania na nchi nyingine, hususan zilizopo barani Afrika.

Amesema utekelezaji wa Dira 2050 ambayo inalenga uchumi wa dola bilioni moja, ni eneo lingine muhimu ambalo maarifa ya Mabalozi Wastaafu yanahitajika ili kuhakikisha utekelezaji wake unakuwa wa ufanisi.

Waziri Kombo ameongeza kuwa mabadiliko yanayoendelea Duniani hususan, maendeleo ya kidigitali yanahitaji mikakati thabiti ili nchi iweze kunufaika na kuwa na mipango madhubuti ya kukabiliana na athari zake. Haya yote yanahitaji mawazo ya pamoja ili kuyaendeea kwa ufanisi.

Eneo lingine ambalo Waziri Kombo alisisitiza umuhimu wa kupata uzoefu wa Mabalozi Wastaafu ni siasa za ulimwengu ambazo zimekuwa hazitabiriki na zinasababisha madhara mbalimbali, hususan katika nchi zinazoendelea kama Tanzania.

Aidha, uzoefu wa Mabalozi Wastaafu unahitajika katika kuendeleza na kuimarisha taswira nzuri ya nchi na hasa nchi inapopewa dhamana ya majukumu ya kimataifa. Balozi Kombo alisema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika mwaka 2028 na hivyo maarifa yao ni muhimu ili kuhakikisha nchi inatekeleza jukumu hilo kwa ufanisi.

Awali, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo alisema Wizara inaangalia uwezekano wa kuanzisha utaratibu rasmi kupitia Ofisi ya Rais-UTUMISHI ili ushirikishwaji wa Mabalozi Wastaafu uwe unatambulika rasmi.






Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mheshimiwa Paul Christian 

Makonda kwa kushirikiana na Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo wa 
Zanzibar Mhe. Dkt. Riziki Pembe Juma wameteua Wajumbe wa Kamati ya Ndani 
(LOC) ya uratibu wa maandalizi ya Mashindano ya Mpira wa Miguu Barani Afrika
(AFCON 2027).


 




Na; Mwandishi Wetu, Dodoma
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni amesema Mikutano ya Baraza la Wafanyakazi ni nyenzo muhimu ya kujadili utekelezaji wa majukumu, kubaini changamoto na kuweka mikakati ya kuboresha utendaji kwa kuzingatia misingi ya uwajibikaji na weledi.

Amesema ili kuendelea kuboresha utendaji kazi na kuongeza ufanisi na tija katika utekelezaji wa majukumu, ni muhimu kudumisha utamaduni wa kufanya kazi kwa umoja, bidii na weledi. Tunapaswa kujipambanua kwa utendaji wa hali ya juu unaoendana na hadhi ya Ofisi ya Makamu wa Rais katika nchi.

Mhe. Masauni ameyasema hayo wakati akifungua Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi Ofisi ya Makamu wa Rais uliofanyika Dodoma, Aprili 15, 2026 akieleza kuwa Ofisi imeendelea kufanya vizuri katika kudumisha Muungano, hususan kupitia utoaji wa elimu kwa umma kwa makundi mbalimbali.

“Kwa upande wa usimamizi wa mazingira, Ofisi imefanikiwa kufanya marekebisho ya Sheria ya Usimamizi wa Mazingira, Sura 191, hususan kwa kuimarisha vifungu vinavyohusu mabadiliko ya tabianchi na kuanzisha Kituo cha Taifa cha Kuratibu Kaboni (NCMC).

Aidha, ni muhimu kuendelea kuimarisha uwezo wa kitaalam na kitaasisi, upatikanaji wa rasilimali na kuongeza jitihada za uhamasishaji wa rasilimali fedha, ikiwemo kupitia maandalizi bora ya miradi ya uhifadhi wa mazingira.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi Ofisi ya Makamu wa Rais ambaye pia Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi alisema lake kuu tangu kuanzishwa kwake baraza hilo lilikuwa kuimarisha ushirikishwaji wa wafanyakazi katika kupanga, kutekeleza na kutathmini mipangokazi, pamoja na kuboresha uhusiano kati ya Menejimenti na watumishi.

“Madhumuni ya Mkutano huu ni kuwashirikisha wafanyakazi wa Ofisi ya Makamu wa Rais kwa lengo la kupata Taarifa ya utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Ofisi.”
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akiagana na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia anayesimamia Kanda ya Afrika Mashariki na Kusini, Dkt. Ndiame Diop, baada ya kukutana na kufanya mazungumzo katika Ofisi za Benki ya Dunia, jijini Washington D.C Nchini Marekani, katika Mikutano ya Kipupwe ya Benki ya Dunia na IMF (2026 IMF/WBG Spring Meetings) inayofanyika, Jijini humo, ambapo Balozi Omar alishukuru uamuzi wa Benki ya Dunia, Kupitia Bodi yake ya Wakurugenzi, kuidhinishia Tanzania dola za Marekani milioni 550 kwa ajili ya kutekeleza miradi miwili ya kimkakati katika sekta za elimu na kusaidia kaya masikini.


Na Benny Mwaipaja, Washington D.C
BENKI ya Dunia, Kupitia Bodi yake ya Wakurugenzi, imeiidhinishia Tanzania dola za Marekani milioni 550 sawa na zaidi ya shilingi trilioni 1.4 kwa ajili ya kutekeleza miradi miwili ya kimkakati katika sekta za elimu na kusaidia kaya masikini.

Uamuzi huo wa Benki umetangazwa na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia anayesimamia Kanda ya Afrika Mashariki na Kusini, Dkt. Ndiame Diop, alipokutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar, pembezoni mwa Mikutano ya Majira ya Kipupwe ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa IMF, Makao Makuu wa Taasisi hizo Jijini Washington D.C, nchini Marekani.

Kati ya fedha hizo, dola za Marekani milioni 300 zitatumika kusaidia program ya elimu ya kuongeza ujuzi hususana kwa vijana na kiasi kingine cha dola za Marekani milioni 250 kitatumika kwa ajili ya kusaidia program ya kusaidia kaya masikini kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF

Dkt. Diop alisema kuwa uamuzi huo unafuatia uhusiano imara uliopo kati ya Tanzania na Benki hiyo pamoja na utekelezaji mzuri wa miradi inayofadhiliwa na Benki, pamoja na usimamizi mzuri wa sera zake za uchumi na fedha.

Makamu huyo wa Rais wa Benki ya Dunia aliahidi kuwa Benki inaendelea kuchakata miradi mingine ya kimkakati iliyowasiliashwa na Tanzania kwa ajili ya kupata ufadhili wa Benki ikiwemo sekta ya nishati, kilimobiashara, miradi ya afya Zanzibar na mingine ili kuiwezesha Tanzania kufikia malengo iliyojiwekea katika kukuza uchumi na maisha ya wananchi.

Akizungumza baada ya kikao hicho, Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar, aliishukuru Benki ya Dunia kwa kupitisha miradi hiyo miwili ambayo ni muhimu kwa maendeleo ya nchi pamoja na majadiliamo yenye tija kwenye maeneo ya miradi muhimu ya maendeleo kwacnchi.

“Pia tumejadili kuhusu maendeleo ya ushoroba wa usafirishaji ambao ni suala muhimu pia ambapo tumeangazia namna korido ya usafirishaji ambayo nchi imewekeza kiasi kikubwa cha fedha ikiwemo reli ya SGR inavyoweza kuchochea uchumi kujumishi na endelevu” alisema Mhe. Balozi Omar.

Kwa upande wake, Mwakilishi Mkaazi wa Benki ya Dunia anayemaliza muda wake Bw. Nathan Belete, alisema kuwa kikao cha Mhe. Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia, Dkt. Mdiame Diop kilikuwa cha manufaa makubwa na kinaendelea kuonesha namna Benki inavyothamini mageuzi makubwa ya kiuchumi na kijamii yanayoendelea nchini Tanzania.

“Ninaondoka Tanzania nikiwa na furaha kubwa na nimaamini uhusiano wa Benki na Tanzania utaendelea kuwa imara na nchi itaendelea kuwa moja ya nchi kubwa kiuchumi katika bara la Afrika kutokana na rasilimali nyingi ilizonazo” alisema Bw. Belete.

Uwekezaji wa Benki ya Dunia nchini Tanzania Kupitia Dirisha la IDA umefikia dola za Marekani bilioni 8.96 ukihusisha miradi 35 ambapo miradi 32 yenye thamaniya dola za Marekani ni ya kitaifa na miradi mitatu yenye thamani ya dola za Marekani bilioni 0.18 ni ya kikanda.

Kikao hicho kilihudhuriwa pia na Waziri wa Fedha na Mipango kutoka Ofisi ya Rais-Zanzibar, Mhe. Dkt. Juma Malik Akil, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Mipango, ambaye pia ni Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, Dkt. Tausi Kida, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Zanzibar, Bw. Aboud Hassan Mwinyi, na Viongozi wengine waaandamizi wa Taasisi za Serikali.



Farida Mangube Morogoro
KATIKA hatua mpya ya kuimarisha sekta ya utalii nchini, Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja, Mhe. Hamida Mussa Hamis, amebainisha mkakati wa kipekee wa kuendelea kuwavutia watalii wanaotembelea Zanzibar kuongeza safari zao kwa kutembelea vivutio vya Tanzania Bara, hususan Hifadhi ya Taifa ya Mikumi kutokana na upekee wake

Akizungumza baada ya kutembelea hifadhi hiyo iliyopo mkoani Morogoro, Mhe. Hamida alisema ipo haja ya kutumia fursa ya wingi wa watalii wanaoendelea kumimina Zanzibar kama daraja la kuutangaza utalii wa Bara ikiwemo hifadhi za taifa kama Mikumi.

“Zanzibar ni lango kubwa la utalii, lakini tunataka wageni hawa wasiishie visiwani pekee bali wavuke na kuja kuona hazina ya vivutio tulivyonavyo Bara,” alisema.

Katika kile alichokiita uzoefu wa kipekee, Mhe. Hamida alieleza kufurahishwa na tukio la kuona simba ndani ya muda mfupi mara tu baada ya kuingia hifadhini hapo, Tena wakiwa chini ya Ndege zilizoegeshwa ndani ya hifadhi zinazotumika kuleta wageni Mikumi kutokea Zanzibar akisema hali hiyo inaonesha ubora wa vivutio vya Tanzania.

Aliongeza kuwa miundombinu iliyopo ikiwemo reli ya kisasa ya SGR, usafiri wa anga na barabara pamoja na miundo mbinu mizuri ya ndani inayofikika kirahisi licha ya Mvua, imeifanya Mikumi kuwa miongoni mwa hifadhi bora zinazofikika kirahisi kwa watalii wa ndani na nje.

Katika hatua nyingine, aliwahimiza Wazanzibari kubadili mtazamo na kujenga utamaduni wa kutembelea vivutio vya ndani, akisisitiza kuwa utalii si wa wageni pekee bali ni fursa kwa Watanzania wote.

“Ni wakati sasa kwa Watanzania kuwekeza katika kujitambua na kuthamini vivutio vyetu; utalii wa ndani ni msingi imara wa sekta hii,” alisisitiza.

Aidha akawahimiza watanzania kutokea Upande wa Bara kutembelea vivutio vya Utalii wa Zanzibar ikiwemo utalii wa fukwe, kuogelea na dolphins na matamasha mbalimbali likiwemo la Kizimkazi ili kufurahia upekee uliopo.

"Hata Rais wetu Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan, na Rais wa Zanzibar Dkt Husein Ali Mwinyi, wanahimiza utalii wa Ndani, Rais Samia alifanya Kazi kubwa kutangaza Royal Tour, tuwaunge mkono kivitendo viongozi wetu"Alisisitiza.

Kwa upande wake, Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Mikumi, Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi Augustine Masesa, alifichua kuwa idadi kubwa ya watalii wanaotembelea hifadhi hiyo wanatoka Zanzibar.

Alisema hali hiyo inaashiria mafanikio ya juhudi za kuitangaza Tanzania kupitia kampeni mbalimbali ikiwemo Royal Tour, huku akibainisha kuwa bado kuna fursa kubwa zaidi ya kuongeza idadi hiyo kupitia ushirikiano wa pande zote mbili.

Alisisitiza kuwa Mikumi inaendelea kuwa kivutio muhimu kinachochochea utalii wa ndani na wa kimataifa, huku akiwakaribisha Watanzania na wageni kufika kujionea vivutio hivyo kwa macho yao wenyewe hasa kutokana na miundo mbinu Rafiki na inayofikika kirahisi ikiwemo Reli ya SGR, Barabara na ndege ambazo kutoka Zanzibar ni dakika 40 tu kufika.

 

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) ikiongozwa na Mwenyekiti wa Tume, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele leo Aprili 14, 2026 amekutana na kuzungumza na mjumbe maalum Jumuiya ya Madola (Commonwealth) Rais wa zamani wa Malawi Mhe.Lazarus McCarthy Chakwera ambaye alitembelea ofisi za Tume Njedengwa jijini Dodoma. Ziara hiyo maalum ya mjumbe huyo wa Jumuia ya Madola ililenga kuangalia namna Uchaguzi Mkuu wa 2025 ulivyofanyika. (Picha na INEC).








Top News