Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mahmoud Thabit Kombo, amesema Tanzania inaendelea kujizatiti kusawazisha maendeleo ya kiuchumi, uendelevu wa mazingira, na usalama wa bahari.

Waziri Kombo amesema hayo alipozungumza katika Mkutano wa Tisa wa Bahari ya Hindi Aprili 10 2026, jijini Port Louis, Mauritius.

“Tanzania, kupitia juhudi za uhifadhi, ushirikishwaji wa jamii, na ushirikiano wa kikanda, inaendelea kulinda mifumo ya ikolojia ya bahari ya Hindi na kuimarisha usalama katika maji ya eneo lake, Ila mafanikio ya kudumu yatategemea ushirikiano imara zaidi kati ya nchi zinazopakana na bahari ya Hindi”, alisisitiza.

Balozi Kombo alihimiza nchi zinazopakana na bahari ya Hindi kuthibitisha wajibu wa pamoja na kushirikiana kuilinda bahari hiyo ili iendelee kuwa chanzo cha amani, ustawi, na fursa kwa vizazi vya sasa na vizazi vijavyo.

Alieleza kuwa Bahari ya Hindi ni nguzo muhimu ya ukuaji wa uchumi na ushirikiano wa kikanda kwa Tanzania, na ni lango muhimu linalounganisha nchi jirani zisizo na bandari na masoko ya dunia.

Aidha, alieleza kuwa kupitia uwekezaji wa kimkakati katika kuboresha na kuimarisha miundombinu ya bandari na nishati, Tanzania inaendelea kujiweka kama kitovu muhimu cha biashara, usafirishaji na huduma za baharini katika Afrika Mashariki na Kati na kwamba uchumi wa buluu unachangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya taifa, ukisaidia mamilioni ya watu na kukuza sekta za uvuvi, utalii, usafiri wa baharini na biashara za pwani.

Balozi Kombo alisema kaulimbiu ya mkutano huo ya “Uwajibikaji wa Pamoja kwa Usimamizi wa Bahari ya Hindi,” inaendana kikamilifu na hali halisi kwa sasa, na kwamba Bahari ya Hindi inakabiliwa na changamoto za mvutano wa kisiasa, vitisho vya usalama wa baharini vinavyoendelea kubadilika, pamoja na shinikizo la kimazingira.

“Changamoto hizi zinaonyesha umuhimu wa kuimarisha ushirikiano kati ya mataifa husika na kuwa uwajibikaji wa pamoja si hiari tena ni suala la lazima ili kuhakikisha kuwa bahari ya Hindi inakuwa salama, endelevu, na yenye manufaa kwa wote wanaoitegemea,” alisisitiza.













JESHI la Polisi Mkoa wa Rukwa linaendelea na mapambano dhidi ya wahalifu mbalimbali wakiwemo wale wanaosababisha taharuki katika jamii kwa kuzusha kuibiwa sehemu nyeti za miili yao na wale wanaowafanyia ukatili na udhalilishaji watoto.

Katika kuhakikisha jamii ya watu wa Mkoa wa Rukwa wanaishi bila hofu, limewafikisha mahakamani tena vijana watatu waliomzushia bwana Hosea Ngogo (31) mkazi wa Soweto Mbeya kuwaibia nyeti zao katika kijiji cha Kilangawana wilaya ya Sumbawanga kisha kumpiga na kumsababishia jeraha kichwani.

Vijana hao ambao ni Geofrey Milumba Deminic (24), Jafari Nebart Shanjila (25) wakazi wa Kijiji cha Kilangawana pamoja na Huruma Geofrey Kasonso (18) mkazi wa Kijiji cha Kilyamatundu, wametiwa hatiani na mahakama ya mwanzo Kipeta mbele ya Mhe. Hakimu Wilgis Mbunda.

Wote watatu wamepewa adhabu ya kifungo cha miezi sita jela kila mmoja, pia kumlipa fidia ya maumivu na jeraha alilopata bwana Hosea Amani Ngogo kiasi cha Tsh.50,000/= kila mmoja. Adhabu hiyo imetolewa 10 April, 2026 na hakimu huyo huku akisema iwe funzo kwa wote wanaozusha mambo ya kishirikina na kuleta hofu katika jamii ya watanzania waliostaarabika.

Kwa upande mwingine, mahakama ya wilaya ya Nkasi tarehe 09 Aprili 2026, imemhukumu Wandu Frolian Chimukole (30) mkazi wa kijiji cha Mbwendi wilayani Nkasi kutumikia kifungo cha miaka 30 jela baada ya kupatika na hatia ya kumbaka binti mwenye umri wa miaka 13. Mshitakiwa huyu alitenda kosa hilo tarehe 20 Januari 2026 huko kijiji cha Kakoma Wilaya ya Nkasi. Wakati akitoa adhabu hiyo Mhe. Hakimu Denis Luwungo alisema adhabu hiyo iwe onyo kwa wanaume wenye tabia ya kuwafanyia ukatili watoto wadogo.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Rukwa linatoa wito kwa wananchi wote kuendelea kutii sheria za nchi, pia wazazi kuendeleza ulinzi wa watoto ili wasifanyiwe ukatili.

Imetolewa na:
Kamanda wa Polisi,

Mkoa wa Rukwa.


Na Mwandishi Wetu

TANZANIA imeendelea kung’ara katika anga la kimataifa baada ya kuingiza vipengele 41 katika Tuzo za Utalii na Usafirishaji Duniani (World Travel Awards), hatua inayoimarisha nafasi yake kama moja ya vinara wa utalii barani Afrika.

Akizungumza, Aprili 11,2026 jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Paulina Mkama, amesema tuzo hizo zinahusisha jumla ya washindani 85 kutoka sekta za umma na binafsi, zikilenga kutambua na kusherehekea ubora wa huduma, kuhamasisha ushindani na kutoa fursa kwa wadau na watalii kupigia kura vivutio bora duniani.

Paulina  ameeleza kuwa ushiriki wa Tanzania katika tuzo hizo ni fursa adhimu ya kuitangaza nchi kimataifa na kuiweka katika ramani ya dunia kama kitovu cha utalii. 

Ameongeza kuwa taasisi za serikali, ikiwemo TFS na TAWA, zimefanikiwa kuwasilisha vivutio vyake katika kinyang’anyiro hicho.

Kwenye kinyang’anyiro hicho , Tanzania imewania nafasi katika vipengele mbalimbali barani Afrika, huku vivutio vikubwa kama Hifadhi ya Taifa ya Serengeti vikitajwa kuwania tuzo za juu. Aidha, katika baadhi ya vipengele, washindani saba kati ya 14 wanatoka Tanzania, hali inayoonesha uimara na ushindani wa sekta ya utalii nchini.

Amebainisha kuwa sekta ya utalii inachangia zaidi ya ajira milioni moja kila mwaka, na mafanikio katika tuzo hizi yataongeza fursa za uwekezaji, ajira pamoja na kukuza pato la taifa.

Kwa sasa, kampeni ya “Kura Moja, Tiketi Moja kwa Tanzania” inaendelea, huku Watanzania na wadau wa utalii wakihamasishwa kushiriki kikamilifu kupigia kura nchi ili kuongeza nafasi ya ushindi.

“Mbali na kuimarisha ushindani wa ubora wa huduma, tuzo hizo pia huchochea ukuaji wa sekta ya utalii kupitia ubunifu, uwekezaji na kuongeza mvuto wa vivutio katika soko la kimataifa,” amesema Paulina.

Ameongeza kuwa  kwa mara ya kwanza, baadhi ya vivutio vinavyosimamiwa na taasisi za serikali kama TAWA na TFS ikiwemo Mpanga Kipengere, Aman Forest Reserve, Selous Game Reserve, Pugu Kazimzumbwi na Kilwa Kisiwani, vimeingia kwenye ushindani huo, jambo linaloashiria kukua kwa sekta ya utalii nchini.





Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi INEC ambaye pia ni Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume, Ndg. Ramadhani Kailima akizungumza katika kikao hicho cha Baraza.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na wenye Ulemavu), Dkt. James Henry Kilabuko (wapili kulia) akishiriki kuimba Wimbo wa Wafanyakazi wakati wa ufunguzi wa Barala la Wafanyakazi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi lililokutana leo Aprili 11, 2026 mkoani Morogoro. Wengine pichani ni Mwenyekiti wa Baraza hilo na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa INEC, Ramadhani Kailima (wapili kushoto), Katibu wa Baraza, Livini Avith (kulia) na Kulia ni mtumishi wa Tume, Rose Tengu.
Sehemu ya wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi wakishiriki kuimba Wimbo wa Wafanyakazi wakati wa ufunguzi wa Kikao cha Barala la Wafanyakazi INEC lililokutana leo Aprili 11, 2026 mkoani Morogoro.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na wenye Ulemavu), Dkt. James Henry Kilabuko akizungumza wakati wa kufungua baraza la Wafanyakazi la INEC.

Na Mwandishi Wetu, Morogoro
WATUMISHI wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi wametakiwa kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia katiba, sheria, kanuni na taratibu na kuepuka lugha zozote za uchochezi zinazoweza kuleta uvunjifu wa amani na kuhatarisha maisha ya Watanzania.

Hayo yamesemwa leo Aprili 11, 2026 na Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na wenye Ulemavu), Dkt. James Henry Kilabuko kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt Jimmy Yonaz wakati akifungua kikao cha Baraza la Wafanyakazi la Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, katika kikao kilichoketi Mkoani Morogoro.

“Napenda kuwaasa, kuzingatia katiba, sheria, kanuni na taratibu mnapotekeleza majukumu ya Tume na kuepuka lugha zozote za uchochezi zinazoweza kuleta uvunjifu wa amani na kuhatarisha maisha ya Watanzania,”alisema Dkt Kilabuko.

Dkt. Kilabuko amesema, taasisi ina malengo yake, upo uwezakano wa kuepusha migogoro ya ndani na nje ya taasisi inayoweza kuathiri utekelezaji wa majukumu ya Tume kwa ufanisi.

Mapema akimkaribisha Mgeni Rasmi, Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi INEC ambaye pia ni Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume, Ndg. Ramadhani Kailima alisema kwa sasa Tume inaendelea na zoezi la uandishi wa Taarifa ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani ya Mwaka 2025.

“Tume imekamilisha Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 ambao ulifanyika tarehe 29 Oktoba, 2025. Kwa sasa Tume inaendelea na zoezi la uandishi wa Taarifa ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani ya Mwaka 2025. Taarifa hiyo baada ya kukamilika, itawasilishwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,”alisema Kailima.

Aidha, amesema Tume ipo katika maandalizi ya uchaguzi mdogo wa Ubunge katika Jimbo la Isimani mkoani Iringa kufuatia kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo, Mhe. William Lukuvi pamoja na uchaguzi wa udiwani katika Kata mbalimbali nchini ambazo madiwani wake walifariki.

Katika Kikao hicho cha siku moja pia kilitumika kwa kufanya uchaguzi wa Katibu wa Baraza hilo ambapo wajumbe walimchagua Ndg. Mwitaru Keboya kuwa Katibu mpya wa Baraza akichukua nafasi ya Ndg. Livini Avith ambaye amemaliza muda wake.
Katibu Mpya wa baraza la Wafanyakazi INEC, Ndg. Mwitaru Keboya akizungumza.

Katibu wa Baraza aliyemaliza muda wake, Ndg. Livini Avith akizungumza.


Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi INEC wakifuatilia agenda mbalimbali katika mkutano huo.


Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi INEC wakifuatilia agenda mbalimbali katika mkutano huo.

Mwenyekiti wa TUGHE tawi la INEC, Ndg. Juvenile Kaiza akizungumza.


Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi INEC wakifuatilia agenda mbalimbali katika mkutano huo.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Paulina Mkama akizungumza, leo Aprili 11,2026 jijini Dar es Salaam wakati w kutangaza vipengele vya kuwania tuzo za utalii na usafirishaji duniani.

Na Mwandishi Wetu
TANZANIA imeendelea kung’ara katika anga la kimataifa baada ya kuingiza vipengele 41 katika Tuzo za Utalii na Usafirishaji Duniani (World Travel Awards), hatua inayoimarisha nafasi yake kama moja ya vinara wa utalii barani Afrika.

Akizungumza, Aprili 11,2026 jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Paulina Mkama, amesema tuzo hizo zinahusisha jumla ya washindani 85 kutoka sekta za umma na binafsi, zikilenga kutambua na kusherehekea ubora wa huduma, kuhamasisha ushindani na kutoa fursa kwa wadau na watalii kupigia kura vivutio bora duniani.

Paulina ameeleza kuwa ushiriki wa Tanzania katika tuzo hizo ni fursa adhimu ya kuitangaza nchi kimataifa na kuiweka katika ramani ya dunia kama kitovu cha utalii.

Ameongeza kuwa taasisi za serikali, ikiwemo TFS na TAWA, zimefanikiwa kuwasilisha vivutio vyake katika kinyang’anyiro hicho.

Kwenye kinyang’anyiro hicho , Tanzania imewania nafasi katika vipengele mbalimbali barani Afrika, huku vivutio vikubwa kama Hifadhi ya Taifa ya Serengeti vikitajwa kuwania tuzo za juu. Aidha, katika baadhi ya vipengele, washindani saba kati ya 14 wanatoka Tanzania, hali inayoonesha uimara na ushindani wa sekta ya utalii nchini.

Amebainisha kuwa sekta ya utalii inachangia zaidi ya ajira milioni moja kila mwaka, na mafanikio katika tuzo hizi yataongeza fursa za uwekezaji, ajira pamoja na kukuza pato la taifa.

Kwa sasa, kampeni ya “Kura Moja, Tiketi Moja kwa Tanzania” inaendelea, huku Watanzania na wadau wa utalii wakihamasishwa kushiriki kikamilifu kupigia kura nchi ili kuongeza nafasi ya ushindi.

“Mbali na kuimarisha ushindani wa ubora wa huduma, tuzo hizo pia huchochea ukuaji wa sekta ya utalii kupitia ubunifu, uwekezaji na kuongeza mvuto wa vivutio katika soko la kimataifa,” amesema Paulina.

Ameongeza kuwa kwa mara ya kwanza, baadhi ya vivutio vinavyosimamiwa na taasisi za serikali kama TAWA na TFS ikiwemo Mpanga Kipengere, Aman Forest Reserve, Selous Game Reserve, Pugu Kazimzumbwi na Kilwa Kisiwani, vimeingia kwenye ushindani huo, jambo linaloashiria kukua kwa sekta ya utalii nchini.



Picha za matukio mbalimbali.

Na Mwandishi Wetu

MWAKILISHI wa Sekretarieti ya Jumuiya ya Madola na Rais Mstaafu wa Malawi, Dk.Lazarus Chakwera, amekutana na kufanya mazungumzo na Tume ya Rais ya Kuchunguza Matukio ya Uvunjifu wa Amani wakati na baada ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025.

Ujumbe huo wa Jumuiya ya Madola ulikutana na Tume hiyo leo Aprili 11,2026 katika Jengo la Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Jijini Dar es Salaam. 

Rais Chakwela amesema ujumbe wake umekuja Tanzania lengo kuu likiwa ni kutafuta suluhisho la kutafuta Suluhu la Matukio ya Uvunjifu wa Amani wakati na baada ya uchaguzi mkuu.

“Ujumbe wangu umekuja Tanzania kwa lengo la kila mmoja kutafuta Suluhu ya yaliyotokea wakati na baada ya uchaguzi hilo ndilo muhimu kwa sasa mengine nitazungumza baada ya kuhitimisha ziara yangu ya Tanzania,” amesema Chakwera.

Akizungumzia ziara hiyo, Mwenyekiti wa Tume hiyo Jaji Othuman Chande, alisema mazungumzo yao yalijikita zaidi kueleza shughuli za Tume hiyo na hadidu za rejea za Tume huku akiwataka waandishi kusubiri taarifa za mjumbe huyo baada ya kukamilisha ziara yake nchini Tanzania.

 Mjumbe huyo jana alikutana na Msajili wa Vyama vya Siasa na viongozi wa vyama mbalimbali. Bado anaendelea na ziara yake ya kikazi ambayo anataraji kuhitimisha Aprili 16,2026 baada ya kutembelea Zanzibar na Dodoma.







Na Mwandishi Wetu, Morogoro.

Watumishi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi wametakiwa kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia katiba, sheria, kanuni  na taratibu na kuepuka lugha zozote za uchochezi zinazoweza kuleta uvunjifu wa amani na kuhatarisha maisha ya Watanzania.

Hayo yamesemwa leo Aprili 11, 2026 na Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na wenye Ulemavu), Dkt. James Henry Kilabuko kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt Jimmy Yonaz wakati akifungua kikao cha Baraza la Wafanyakazi la Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, katika kikao kilichoketi Mkoani Morogoro. 

“Napenda kuwaasa, kuzingatia katiba, sheria, kanuni  na taratibu mnapotekeleza majukumu ya Tume na kuepuka lugha zozote za uchochezi zinazoweza kuleta uvunjifu wa amani na kuhatarisha maisha ya Watanzania,”alisema Dkt Kilabuko.
 
Dkt. Kilabuko amesema, taasisi ina malengo yake, upo uwezakano wa kuepusha migogoro ya ndani na nje ya taasisi inayoweza kuathiri utekelezaji wa majukumu ya Tume kwa ufanisi.

Mapema akimkaribisha Mgeni Rasmi, Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi INEC ambaye pia ni Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume, Ndg. Ramadhani Kailima alisema kwa sasa Tume inaendelea na zoezi la uandishi wa Taarifa ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani ya Mwaka 2025.

“Tume imekamilisha Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 ambao ulifanyika tarehe 29 Oktoba, 2025.  Kwa sasa Tume inaendelea na zoezi la uandishi wa Taarifa ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani ya Mwaka 2025. Taarifa hiyo baada ya kukamilika, itawasilishwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,”alisema Kailima.

Aidha, amesema Tume ipo katika maandalizi ya uchaguzi mdogo wa Ubunge katika Jimbo la Isimani mkoani Iringa kufuatia kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo, Mhe. William Lukuvi pamoja na uchaguzi wa udiwani katika Kata mbalimbali nchini ambazo madiwani wake walifariki.

Katika Kikao hicho cha siku moja pia kilitumika kwa kufanya uchaguzi wa Katibu wa Baraza hilo ambapo wajumbe walimchagua Ndg. Mwitaru Keboya kuwa Katibu mpya wa Baraza akichukua nafasi ya Ndg. Livini Avith ambaye amemaliza muda wake. 








 


Top News