Watumishi wanawake wa Mamlaaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) wameungana na wanawake wengine kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani 2026 katika maadhimisho ya kimkoa yaliyofanyika Viwanja vya Barafu Mburahati, Wilaya ya Ubungo jijini Dar es Salaam.

Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Albert Chalamila, ambaye aliwahimiza wanawake kuendelea kutumia fursa zilizopo kujiendeleza kiuchumi na kuchangia maendeleo ya taifa.

Akizungumza katika hafla hiyo alisema, “Wanawake wana mchango mkubwa katika maendeleo ya jamii na taifa, hivyo ni muhimu waendelee kupewa na kutumia kikamilifu fursa zilizopo ili kufikia maendeleo jumuishi.”

Maadhimisho ya mwaka huu yanaongozwa na kaulimbiu isemayo: “Haki na Usawa kwa Wanawake na Wasichana: Msingi Jumuishi kuifikia Dira 2050.”

Siku ya Wanawake Duniani huadhimishwa kila mwaka tarehe 8 Machi.




Picha mbalimbali za matukio ya wafanyazi wanawake wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) katika maadhimisho ya Siku ya wanawake duniani yaliyofanyika leo Machi 08, 2026 leo katika viwanja vya Barafu Mburahati, Wilaya ya Ubungo jijini Dar es Salaam.

ACI FMA Tanzania has reaffirmed its commitment to supporting the sustainable growth of Tanzania’s financial markets and contributing meaningfully to the broader development of the national economy.

This was revealed by the Association’s President, Mr. Farid Yahya Ally, during an iftar gala held in Dar es Salaam over the weekend. The event featured a panel discussion on the progress and challenges facing Tanzania’s financial markets and brought together market participants, policymakers, and regulators.

“Through continued collaboration with regulators, policymakers, and industry participants, the Association will continue to support initiatives aligned with Tanzania’s long-term development objectives, including the aspirations of DIRA 2050, which aims to build a one-trillion-dollar economy,” said Mr. Ally.

Addressing distinguished representatives from the Bank of Tanzania, the Dar es Salaam Stock Exchange, and Heads of Global Markets from leading banking institutions, Mr. Ally noted that as a professional body representing financial markets practitioners, ACI FMA Tanzania recognises its critical role in strengthening the development and integrity of Tanzania’s financial markets.

“Strengthening partnerships with policymakers and regulators remains central to our mission of promoting best market practices and ensuring that Tanzania continues to provide a conducive environment for both local and international investors,” he said.

The iftar served as an important platform for dialogue and engagement among market participants, policymakers, and regulators. The discussions focused on identifying ways to bridge existing institutional gaps and enhance collaboration in shaping a well-functioning and resilient financial market environment.

During the discussions, participants highlighted several challenges affecting the financial markets sector, including limited product diversification, complex regulatory onboarding processes, and the dominance of bank-led financing.

Responding to the concerns, Mr. Peter Nalitolela, Chief Executive Officer of the Dar es Salaam Stock Exchange, acknowledged that while Tanzania’s capital markets continue to grow, retail investor awareness remains limited.

He noted that although the number of Central Depository System (CDS) accounts remains relatively low, the market has recently seen an increase in new investors entering the bourse.

“While more investors are showing interest in the market, persistent challenges remain, including limited product diversity and market preparedness to accommodate growing investor participation,” he said.

Mr. Nalitolela also observed that initial public offerings (IPOs) have slowed not only in Tanzania but also globally, reflecting broader market trends.

However, he emphasised that Tanzania is gradually transitioning from a government-led economic model towards a stronger public-private sector-driven economy, a shift that is beginning to yield positive momentum in both capital and equity markets.

Meanwhile, Mr. Rui Correia, President of ACI FMA Global, announced that the association will introduce a scholarship programme for women in Africa, aimed at supporting female professionals in the financial markets sector.

“This is something we want to do particularly as we approach International Women’s Day. For this year, we will focus on scholarships for women in Africa, and next year we will introduce another initiative,” Mr. Correia said.

He emphasised that the association places strong value on knowledge sharing and professional development within the financial markets community.

“For us, education is not just about obtaining certificates. It is about sharing expertise, knowledge, and experiences across different areas of the financial markets,” he added.
seb

ACI FMA Tanzania is a non-profit organisation operating under the umbrella of ACI FMA Global. The association promotes best market practices by providing financial markets practitioners with access to training, professional engagement opportunities, and internationally recognised certifications.
Dar es Salaam Stock Exchange (DSE), Chief Executive Officer, Mr. Peter Nalitolela (right), ACI FMA Global President, Mr. Rui Correia and ACI FMA Tanzania President, Mr. Farid Yahya Ally, serving iftar dinner at an occasion hosted by ACI FMA Tanzania in Dar es Salaam yesterday.   The gathering brought together market participants, policymakers, and regulators to strengthen collaboration and promote a resilient financial market environment in the country. ACI FMA Tanzania is a non-profit organisation that promotes best market practices by providing financial markets practitioners with training, professional engagement, and certifications.
ACI FMA Tanzania President, Mr. Farid Yahya Ally, addresses participants during an iftar dinner in Dar es Salaam yesterday. The gathering brought together market participants, policymakers, and regulators to strengthen collaboration and promote a resilient financial market environment in the country. ACI FMA Tanzania is a non-profit organisation that promotes best market practices by providing financial markets practitioners with training, professional engagement, and certifications.
ACI FMA Tanzania President, Mr. Farid Yahya Ally (right), exchanges views with ACI FMA Global President, Mr. Rui Correia (left), and Bank of Tanzania Senior Financial Analyst, Mr. Stanslaus Shenyali, during an iftar dinner hosted by ACI FMA Tanzania in Dar es Salaam yesterday. The gathering brought together market participants, policymakers, and regulators to strengthen collaboration and promote a resilient financial market environment in the country. ACI FMA Tanzania is a non-profit organisation that promotes best market practices by providing financial markets practitioners with training, professional engagement, and certifications.
Dar es Salaam Stock Exchange Chief Executive Officer, Mr. Peter Nalitolela (right), speaks during a dialogue session held alongside the iftar dinner hosted by ACI FMA Tanzania in Dar es Salaam yesterday. The gathering brought together market participants, policymakers, and regulators to strengthen collaboration and promote a resilient financial market environment in the country. ACI FMA Tanzania is a non-profit organisation that promotes best market practices by providing financial markets practitioners with training, professional engagement, and certifications.
A cross-section of invited guests during the iftar dinner hosted by ACI FMA Tanzania in Dar es Salaam yesterday. The gathering brought together market participants, policymakers, and regulators to strengthen collaboration and promote a resilient financial market environment in the country. ACI FMA Tanzania is a non-profit organisation that promotes best market practices by providing financial markets practitioners with training, professional engagement, and certifications.
ACI FMA Tanzania President, Mr. Farid Yahya Ally (eighth from left), ACI FMA Global President, Mr. Rui Correia (sixth from left), ACI officials and other invited dignitaries pose for a group photograph after an iftar dinner hosted by ACI FMA Tanzania in Dar es Salaam yesterday. The gathering brought together market participants, policymakers, and regulators to strengthen collaboration and promote a resilient financial market environment in the country. ACI FMA Tanzania is a non-profit organisation that promotes best market practices by providing financial markets practitioners with training, professional engagement, and certifications.


Na Munir Shemweta, Masasi


Mbunge wa Jimbo la Masasi ambaye pia ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo amekabidhi baiskeli kumi kwa watu wenye ulemavu wilayani Masasi mkoani Mtwara, ikiwa ni sehemu ya juhudi zake za kusaidia watu wenye mahitaji maalum katika jimbo hilo.

Dkt. Akwilapo amekabidhi baiskeli hizo Machi 8, 2026 wakati wa ziara yake mkoani Mtwara, akieleza kuwa hatua hiyo inalenga kurahisisha usafiri na shughuli za kila siku kwa watu wenye ulemavu ili waweze kujitegemea kiuchumi.

Amesema ari yake ya kusaidia watu wenye ulemavu imetokana na uzoefu wake wa maisha ya kulea mtoto mwenye ulemavu, jambo lililompa uelewa wa karibu kuhusu changamoto wanazokabiliana nazo na umuhimu wa kuwasaidia.

Amebainisha kuwa, kusaidia watu wenye uhitaji ni jukumu la kila mwenye uwezo katika jamii, na kwamba ataendelea kuwahamasisha marafiki na ndugu kushiriki katika kutoa msaada kwa watu wenye uhitaji ili kuwapa furaha na matumaini.

“Mheshimiwa Rais Mama Samia alishatuambia kuwa katika kazi tunazofanya tuhakikishe tunawapa wananchi furaha.’’ amesema Dkt. Akwilapo.

Kwa mujibu wa Mbunge huyo wa Masasi, msaada kwa watu wenye uhitaji unaweza kuwa mdogo au mkubwa kulingana na uwezo wa mtu, lakini jambo muhimu ni kushirikiana katika kuleta mabadiliko chanya kwa jamii.

“Tutawaangalia watu wa madaraja yote, rika zote na wenye uwezo wowote ili kuwainua wale wenye uhitaji. Kimsingi tunataka wote tufikie hatua ya kuweza kuona fursa zilizo mbele yetu,” ameongeza.

Kwa upande wake, mmoja wa wanufaika wa msaada huo, Bw. Teophil Liundi, amemshukuru Mbunge huyo kwa kuwapatia baiskeli ambazo amesema zitawasaidia kurahisisha usafiri na kuwawezesha kufanya shughuli zao za kujipatia kipato kwa urahisi zaidi.
Amesema, baiskeli hiyo itamwezesha kufanya mizunguko ya shughuli zake kwa ufanisi zaidi na hivyo kumsaidia kufikia malengo yake ya kujiongezea kipato.

Mbunge wa jimbo la Masasi na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo akijaribu kumsaidia msichana mwenye ulemavu Samia Hamad mkazi wa Masasi kuendesha Baiskeli mara baada ya kumkabidhi tarehe 8 Machi 2026 mkoani Mtwara.

Mbunge wa jimbo la Masasi na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo (wa pili kulia) akiwa katika picha na baadhi ya watu wenye ulemavu mara baada ya kuwakabidhi Baiskeli wilayani Masasi mkoani Mtwara tarehe 8 Machi 2026 mkoani Mtwara. Kulia ni Mkuu wa wilaya ya Masasi Rachel Kasanda.

Mbunge wa Jimbo la Masasi na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo akimsaidia Bw. Teophil Liundi mwenye ulemavu wa miguu kuweka magongo yake ya kutembelea vizuri mara baada ya kumkabidhi Baiskeli wilayani Masasi mkoani Mtwara tarehe 8 Machi 2026 mkoani Mtwara. (PICHA ZOTE NA MUNIR SHEMWETA)

Na Mwandishi wetu

OFISI ya Mkuu wa Wilaya ya Chemba Mkoani Dodoma imezindua mfumo wa kusikiliza kero za wananchi kidigitali kupitia namba maalumu WhatsApp ijulikanayo kama Chemba konektedi.

Kupitia namba hiyo maalum ya 0771400500 itakayotumika kwa mfumo wa WhatsApp wananchi wataweza kuwasilisha kero na changamoto zao moja kwa moja bila kutumia muda, nauli kwa kusafiri kwenda katika ofisi ya mkuu wa Wilaya, idara na taasisi za Umma katika Halmashauri ya Chemba.

Akizungumzia kuhusiana na hatua hiyo Mkuu wa Wilaya ya Chemba Halima Okash amesema kupitia Chemba Connect WhatsApp chatbot mwananchi ana uwezo wa kutuma malalamiko yake, kero na changamoto mbalimbali na kujibiwa ndani ya saa 24.

Pia Okash amesema kupitia Chemba Konektedi ya whatsapp wananchi na wadau wa ndani na nje ya wilaya hiyo wana uwezo wa kupata taarifa ya fursa mbalimbali zinazopatikana katika Wilaya hiyo zikiwemo za kilimo,utalii, uwekezaji na pia kujua idara zinazopatikana na huduma zinazotolewa katika Halmashauri ya Wilaya hiyo.

Kwa mujibu wa Mkuu huyo wa Wilaya namba hiyo maalumu ambayo ofisi yake imeipata yeyote atakayepiga ataunganishwa moja kwa moja na ofisi yake pia mwananchi anaweza kuingia whatsapp moja kwa moja na kuandika ujumbe wake kuhusiana na kero inayomkabili.

"Mpango huu Mhe. Rais alikua anatamani sana ufanyike kuwarahisishia wananchi namna ya kuwasilisha kero zao kwa wakati ili ziweze kushughulikiwa na hii itarahisisha pia kujua kazi zinazofanywa na Wilaya hiyo moja kwa moja kupitia njia ya kidigitali," amesema

Okash, amewasisitiza wananchi kutumia mfumo huo rahisi na haraka katika utatuzi wa kero, changamoto na fursa mbalimbali zinazohusu Wilaya ya Chemba.

Wakizungumzia kuhusiana na mpango huo wa chemba konektedi baadhi ya wakazi wa Wilaya hiyo akiwemo Jamali Juma kutoka Kijiji cha Magandi amemshukuru Mkuu huyo wa Wilaya kwa kuanzisha utaratibu mpya wa kuwasilisha kero zao kupitia namba maalumu.

Juma amesema utaratibu huo utawarahisishia kufikisha taarifa kwa mkuu wa wilaya kuhusiana na mambo mbalimbali yanayotokea kwenye maeneo yao ikiwemo kero zilizopo ndani ya jamii ziweze kufika kwa wakati na kushughulikiwa bila kusubiri mikutano na ziara za viongozi

Mmoja wa Vijana kutoka kijiji cha Magandi Joshua Vicent naye amemshukuru Okash kwa kuanzisha mfumo wa kidigitali ambao unakwenda kuwarahisishia kufikisha kero zao jambo ambao litaokoa muda na gharama waliyokuwa wakiitumia awali kuifikia ofisi ya Mkuu wa Wilaya na idara mbalimbali katika ofisi ya Mkurugenzi. .

Kadhalika Sakina Juma amesema wapo wananchi ambao kuzungumza kwenye mikutano kwao ni shida lakini kupitia mfumo huo watawasilisha kero zao sehemu husika kwa wakati.

Wananchi hao wamesema kupitia mfumo huo popote mwananchi alipo atawasilisha kero zake bila kusubiri mikutano ama ziara ya mkuu wa wilaya na viongozi wengine kwenye kijiji chao na hiyo itawapa nafasi ya kufanya shughuli zao za Maendeleo kwa kuokoa muda na gharama.

Mpango huo wa Chemba Connect WhatsApp chatbot kupitia namba maalumu unapatikana kwa saa 24 siku 7 zote za wiki.
Na Said Mwishehe,Michuzi TV

MAISHA yamekuwa rahisi sana huku kwetu! Hivyo ndivyo anavyoanza kuelezea Mkazi wa Kisevule Center katika Kata ya Vikindu mkoani Pwani Mariam Mohamed ambaye kwa sasa anapika chakula kwa gesi asilia iliyofungwa nyumbani kwake kwa ufadhili wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

REA imetoa Kiasi cha fedha Sh.bilioni 6.8 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya gesi asilia ikiwemo ujenzi wa bomba kutoa gesi Mtwara hadi Pwani na kisha kupeleka gesi hiyo kwa kaya 1000 ikiwemo kaya ya Mariam mjane wa watoto watano.

Wakati akizungumza na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari walioko katika ziara iliyoandaliwa na REA kwa ajili ya kuangalia mradi huo wa usambazaji gesi asilia kwa wananchi wa Kisuvule wilayani Mkuranga mkoani Pwani ,Mkazi huyo amesema tangu aanze kutumia gesi ya REA maisha kwake yamekuwa marahisi sana hasa katika kuandaa mlo wa familia yake.

“Nashukuru sana kwani mradi huu umetusaidia sana yaani umetuokoa na hasa huu mwezi huu wa Ramadhani… kuna wepesi nauona kwanza nalala mapema na tunapika vyakula kwa wakati

“Namshukuru sana Mungu ,namshukuru sana mama yetu Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kwani katuokoa sana sana yaani kila nikipika siachi kumtaja Mama Samia kwa kutuletea gesi hii bure majumbani kwetu.”

Ameendelea kueleza kuwa kwa sasa hana wasawasi anapotaka kupika kwani hata gesi ikiisha ananunua kwa Sh.1000 tu na kuendelea na mapishi hivyo maisha yamekuwa rahisi .

“Siku za nyuma nilikuwa napika daku nahangaika lakini sasa hivi naweza kwanza kufanya shughuli zangu kisha nikalala na ikifika saa saba nikaamka nawasha gesi naandaa chakula changu na saa nane nakula maisha yanaenda.Kwa kusema mkweli maisha yamekuwa mepesi sana.”

Aidha amesema wakati mradi huo unataka kuanza baadhi ya wananchi hawakuwa tayari kuwekewa gesi hiyo katika nyumba zao kwa madai nyumba zitalipuka kwa gesi lakini kwa sasa wananchi hao wameanza kuomba namba za simu za REA ili wafungiwe mfumo huo wa gesi asilia unaotekelezwa na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC).

“Kwangu walivyokuja nikawaambia niko tayari kwani niliamini Rais wetu hawezi kuleta kitu kibaya kwa raia wake au wananchi wake lazıma ataleta kitu cha kutuokoa.”

Akiendelea kuelezea gesi hiyo iliyofungwa nyumbani kwake anasema hivi sasa hata watoto wake wanakimbilia jikoni kupika wakati alipokuwa akitumia mkaa walikuwa hawataki kupika.

“Tumewekewa gesi hii bure kabisa na ukweli Mwenyezi Mungu amjalie Mama Samia yaani ampe maisha marefu apate kuwasaidia wengine,”amesema Mariam na kusisitiza akinunua gesi ya Sh.1000 anapika kwa siku tatu.

Kwa upande wake Hussein Shemndolwa ambaye ni Mwenyekiti wa Kitongoji cha Kitangwi katika kijiii cha Kisimvule kata ya vikindu wilayani Mkuranga amesema wanaishukuru Serikali inayoongozwa na Rais Samia kwa kuwapatia mradi huo kwani wananchi wanafaidika na mradi huo.

“Kwasababu viwango ambavyo vinatumika kwa siku kama walivyosema ni Sh. 1, 000 kwa siku na wananchi ambao wameingiziwa huduma hiyo wamekuwa ni mashahidi.Hata hivyo nitoe ombi kwa REA na TPDC kuhakikisha mradi huu unakwenda katika nyumba nyingi zaidi ,tunazo Kaya 12000 hapa kwetu hivyo tunauhitaji mradi huu sana.”

Awali Kaimu Meneja Usaidizi wa Kiufundi kwa Waendelezaji wa Mradi kutoka REA, Mhandisi Emmanuel Yessaya amesema Wakala huo ulitenga fedha kwa ajili ya kufadhili mradi wa usambazaji wa gesi asilia kupitia Mfuko wa REF ambapo takribani kaya 1000 na taasisi moja zimenufaika kwa kusambaziwa miundombinu ya gesi asilia kwa ajili ya kupikia majumbani katika mkoa wa Lindi na Pwani.

“Mradi huo ni wa kimkakati kwa ajili ya kupunguza gharama za nishati ya kupikia, kulinda afya za wananchi na kupunguza athari za kimazingira zitokanazo na ukataji wa misitu kwa ajili ya nishati ya kupikia kwa wananchi wanaoishi Vijijini na kwenye vijiji miji.”

Kwa upande wake Mhandisi wa mradi huo kutoka Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Mha. Anthony Karomba, amesema mradi huo wa kuunganisha wateja wa majumbani kwenye mtandao wa gesi asilia umegharamikiwa kwa fedha nyingi na Serikali kupitia REA na hivyo amewasihi wananchi kuendelea kuilinda miundombinu hiyo.








Na Mwandishi Wetu

KATIBU wa NEC Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kenani Kihongosi amemsifia na kumpongeza Mbunge wa Jimbo la Itilima mkoani Simiyu Njalu Silanga kwa namna anavyowasilisha bungeni hoja zenye mashiko na zenye kulenga kuwaletea maendeleo wananchi wa jimbo hilo.

Kihongosi amesema mbunge huyo ameonesha dhamira ya dhati ya kuwatumikia wananchi wake kwa kusimamia masuala muhimu ya maendeleo na kuyapeleka kwa nguvu bungeni ili kupata ufumbuzi.

Ametoa pongezi hizo Machi 8 wakati Kenani Kihongosi alipotembeleq na kukagua miradi ya maendeleo katika Jimbo la Itilima mkoani Simiyu, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi katika Kanda ya Ziwa.

Kutokana na juhudi hizo, Kihongosi amewataka wananchi wa Jimbo la Itilima kuendelea kumuamini na kumuunga mkono mbunge wao ili aweze kuendelea kupigania maendeleo yao kwa ufanisi zaidi.

Kwa upande wao, wananchi wa Jimbo hilo wameonesha furahiq na kuridhishwa na kazi inayofanywa na mbunge wao, wakimpongeza kwa kuwaletea maendeleo mbalimbali jimboni humo ikiwemo ujenzi wa shule, vituo vya afya pamoja na kusambazwa kwa huduma ya umeme katika maeneo tofauti ya jimbo hilo.

Pia wamemshukuru mbunge huyo kwa kujali ustawi wa jimbo lao na kumuombea aendelee kuwa na nguvu na moyo wa kuwatumikia ili maendeleo yaendelee kuongezeka katika Jimbo la Itilima.

NA FARIDA MANGUBE , MOROGORO

Katika kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani, mamlaka ya mapatao Tanzania (TRA) Mkoa wa Morogoro imetumia maadhimisho hayo kutoka elimu ya masuala ya kodi pamoja na huduma ya usajili wa namba za utambulisho wa mlipa kodi (TIN).

Maadhimisho hayo kimkoa yameyofanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro ambapo yamewakutanisha wanawake kutoka sehemu mbalimbali walioungana kwa pamoja kusherehekea siku hiyo huku wakipata huduma na elimu kutoka kwa taasisi za serikali ikiwemo TRA

Katika banda la TRA, wananchi walipatiwa elimu kuhusu umuhimu wa kulipa kodi kwa maendeleo ya taifa pamoja na kufahamu taratibu za usajili wa namba ya TIN, hususani kwa wafanyabiashara wanawake ambao wengi wao wanajishughulisha na shughuli ndogo ndogo za kiuchumi.

Afsa Mwandamizi wa Huduma na Elimu Mawasiliano Bi Immaculate Chagguaakitoa elimu katika maadhimisho hayo amesema kuwa namba ya TIN ni hatua muhimu kwa mfanyabiashara kwani humwezesha kufanya shughuli zake kwa mujibu wa sheria pamoja na kupata fursa mbalimbali za kiuchumi.

Mbali na kutoa elimu, mamlaka hiyo pia ilitoa huduma ya usajili wa namba za TIN papo kwa papo kwa wananchi waliojitokeza katika viunga vya maadhimisho hayo.

Huduma hiyo imepokelewa kwa furaha na wanawake pamoja na wananchi kutoka maeneo mbalimbali ikiwemo Mwajuma Omary mkazi wa Kijiji cha Fulwa, ambapo amesema kuwa hatua ya TRA kusogeza huduma karibu na wananchi imewasaidia kuokoa muda na gharama ambazo wangetumia kufuata huduma hiyo ofisini.

Nae Mwajabu Othuman kutoka Malinyi amesema kuwa upatikanaji wa huduma hiyo katika maadhimisho hayo umewapa hamasa zaidi ya kujiunga katika mfumo rasmi wa ulipaji kodi na kuendesha biashara zao kwa kufuata taratibu za kisheria.

Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani hufanyika kila mwaka Machi 8 duniani kote yakilenga kutambua mchango wa wanawake katika maendeleo ya jamii pamoja na kuhamasisha usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake katika nyanja mbalimbali za maisha.









Wanawake wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) mkoa wa Dodoma leo Machi 8, 2026 wameungana na wanawake wenzao wa mkoa wa Dodoma, Tanzania na ulimwenguni kuadhimisha Siku ya Mwanamke Duniani, ambapo maadhimisho ya kimkoa yamefanyika katika wilaya ya Kongwa.

Maadhimisho hayo yalipambwa na shamrashamra mbalimbali zikiwemo burudani za ngoma za asili, matarumbeta pamoja na Brass Band ya JKT Makutupora. Mgeni rasmi katika hafla hiyo alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule.

Mapema asubuhi ya leo, wanawake walikusanyika katika viwanja vya maadhimisho kabla ya kuanza kwa maandamano rasmi. Walionekana kuwa na uchangamfu na kujiamini, hali iliyoonesha ari kubwa ya kushiriki katika maadhimisho hayo muhimu.

Baadhi ya wanawake wa TBA waliozungumza katika maadhimisho hayo wamesema kuwa maadhimisho ya mwaka huu yamekuwa ya kuvutia na yenye kuhamasisha ushiriki wa wanawake katika nyanja mbalimbali za maendeleo.

Akizungumzia maendeleo ya wanawake ndani ya TBA, Afisa Rasilimali Watu wa TBA, Bi. Nashila Iddi amesema kuwa wanawake ndani ya taasisi wamepiga hatua kubwa kitaaluma na kiutendaji.

Amesema kuwa idadi ya wanawake wataalamu kama wahandisi, wakadiriaji majengo (QS) pamoja na wabunifu wa majengo inaendelea kuongezeka kila mwaka, jambo linaloonesha maendeleo chanya katika ushiriki wa wanawake katika taaluma za ujenzi.

“Ndani ya TBA tuna wanawake wengi katika nafasi za uongozi. Yupo Mkurugenzi, wapo mameneja wa mikoa, wakuu wa vitengo pamoja na wasimamizi wa miradi, na wote wanafanya kazi zao kwa ufanisi mkubwa,” amesema Bi. Nashila.

Kwa upande wake, Afisa Manunuzi wa TBA, Bi. Ruth Mwakalinga amesema wanawake wanazidi kujiamini kadri wanavyopata fursa katika maeneo mbalimbali ya kazi.

“Wanawake wanazidi kujiamini kila mwaka, na kila wanapopata nafasi wanaonyesha uwezo mkubwa walionao katika kuleta maendeleo,” amesema.

Naye Maria Paulo, ambaye anafanya kazi katika mradi wa ujenzi wa nyumba 3,500 unaotekelezwa na TBA katika eneo la Nzuguni, amesema wanawake kwa sasa wanajituma zaidi katika utekelezaji wa miradi.

“Wanawake kwa sasa wanajituma sana. Hata hapa kwenye mradi wetu tunaona namna wanavyofanya kazi kwa bidii na kujituma,” amesema.

Siku ya Mwanamke Duniani huadhimishwa kila mwaka Machi 8 ikiwa na ujumbe maalum wa kuhamasisha haki, usawa na maendeleo ya wanawake. Kaulimbiu ya mwaka huu inasema: “Haki na Usawa kwa Wanawake na Wasichana ni Msingi Jumuishi wa Kufikia Dira ya Maendeleo 2050.”

 

Kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani mkoani Geita kimepambwa na ujumbe mzito wa kuwataka wanawake nchini kuzingatia mila na desturi zinazojenga jamii, huku wakizidi kupiga hatua kubwa za kiuchumi.

Akizungumza katika maadhimisho hayo Machi 8, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima, amesema mafanikio ya kiuchumi hayapaswi kuwa chanzo cha kubomoa misingi ya familia.

Dkt. Gwajima amebainisha kuwa Serikali imekuwa ikiunda majukwaa mbalimbali kama mpango mkakati wa kuimarisha kipato cha mwanamke ili kupunguza ukatili majumbani. 

Hata hivyo, amesisitiza kuwa wanawake wanapaswa kulinda kizazi kijacho kwa kuzingatia mila bora.

"Serikali inaimarisha uchumi wa mwanamke mmoja mmoja ili kupunguza ukatili, lakini hatupaswi kusahau mila na desturi zinazojenga ili kulinda kizazi chetu," alisema Dkt. Gwajima".

Naye Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Wazee kutoka Zanzibar, Mhe. Zawadi Amour Nassor, ametoa rai kwa wanawake kutodharau nafasi ya mwanaume ndani ya familia wakati wakidai haki zao.

Amesema kuwa pamoja na mapambano ya usawa, mwanamke hapaswi kusahau kuwa mwanaume ni kiongozi wa familia na anapaswa kupewa utii unaostahili. Aliwaasa wanawake kutokuwa chanzo cha kuvunjika kwa ndoa zao kwa kisingizio cha kusaka haki.

Katika hatua nyingine ya kihistoria, Mkoa wa Geita umezindua mradi wa mpango wa kutokomeza vitendo vya ukatili kwa wanawake na watoto ujulikanao kama PAMOJA.

Mradi wa PAMOJA unatekelezwa katika mikoa 10 na halmashauri 40 nchini, chini ya ufadhili wa Benki ya Dunia (WB) kwa thamani ya dola za kimarekani milioni 104 sawa na sh bilioni 262 za kitanzania.

Mkuu wa mkoa wa Geita Martin Shigela amesisitiza kuwa mradio huo unaenda kumaliza Hali ya ukatili katika jamii ya mkoa wa Geita ambapo kupitia mradi huo wanawake na watoto watasaidika.














Top News