Wafanyabiashara wa Soko Kuu la Jiji la Mwanza wakifanya usafi katika eneo la soko hilo wakati wa zoezi la usafi wa mazingira Mkoani humo Mei 30, 2026 ikiwa ni maandalizi kuelekea Kilele cha Maadhimisho Siku ya Mazingira Duniani, 2026.
Watumishi kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Bi. Sheila Kikula (wa pili kutoka kushoto) na Bw. Lucas Sebida (wa pili kutoka kulia) wakiungana na wafanyabiashara wa Soko Kuu la Jiji la Mwanza Mei 30, 2026 kufanya usafi katika eneo hilo   wakati wa zoezi la usafi wa mazingira Mkoani humo ikiwa ni maandalizi kuelekea Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani, 2026.
Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza, Bw. Balandya Elikana (kulia) akiwa na vitendea kazi mbalimbali kwa ajili ya kuanza zoezi la usafi katika eneo la Soko Kuu la Jiji hilo  wakati wa zoezi la usafi wa mazingira Mkoani humo Mei 30, 2026 ikiwa ni maandalizi kuelekea Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani, 2026.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda amewataka Maafisa Mazingira kuwachukulia hatua za kisheria wafanyabiashara wanaokiuka Sheria Ndogo ya Afya na Usafi wa Mazingira kwa kutupa taka ovyo ndani ya mifereji ya maji taka katika Soko Kuu la Jiji hilo.

Mhe. Mtanda ametoa kauli hiyo Mei 30, 2026 wakati alipoongoza viongozi, watendaji na wananchi Mkoa huo katika zoezi la usafi wa mazingira katika eneo la Soko Kuu la Jiji hilo ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho kuelekea Kilele cha Siku ya Mazingira Duniani mwaka 2026.  

Amesema baadhi ya wafanyabiashara katika soko hilo wamejenga mazoea ya kutupa taka ovyo katika mifereji ya maji taka katika Soko hilo hali inayochangia kukithiri kwa uchafu na hivyo kuchochea kasi ya uharibifu wa mazingira.

“Natoa maelekezo kwa maafisa mazingira wa jiji na meneja wa soko kuhakikisha kunakuwa na utekelezaji wa Sheria ya Afya na Usafi wa mazingira katika Soko hili na kila anayekiuka sheria hakikisheni anatozwa faini” amesema Mtanda.

Aidha Mhe. Mtanda amesema faini hizo zitakazolipwa na wafanyabiashara hao zitatumika katika kulipa gharama za huduma ya usafi inayotolewa na Halmashauri ya Jiji na hivyo kuhimiza watumiaji wa soko kuzingatia taratibu za usafi ili kulinda mazingira.

Mhe. Mtanda pia amewalekeza maafisa mazingira kufanya ukaguzi wa mara kwa mara kwa wafanyabiashara waliopo ndani ya soko ili kuhakikisha wanatekeleza maelekezo, miongozo na ya sheria zilizopo ili huduma za soko hilo ziendelee kuwa endelevu kwa wananchi.

Amesema suala la usafi ni ustaarabu, hivyo ni wajibu wa jamii inayozunguka katika eneo hilo kuhakikisha wanajenga utamaduni wa kupenda na kuthamini usafi wa mazingira yanayowazunguka ili kulinda afya za watumiaji wa bidhaa na huduma zinazopatikana ndani soko hilo.

Katika hatua nyingine, Mhe. Mtanda amewataka wananchi wa Mkoa huo kujenga utamaduni wa kupanda miti katika maeneo yao kwani kwa kufanya ni kutekeleza amri na maelekezo ya mwenyezi mungu aliyoyatoa katika vitabu takatifu.

Awali akitoa taarifa ya tathimini ya hali ya utunzaji na uhifadhi wa mazingira katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Afisa Mazingira wa Jiji hilo, Bw. Daudi Joseph amesema katika mwaka 2025/2026 Jiji hilo limefanikiwa kupanda miti 768,476 ambapo miti 176,750 imepandwa na wananchi na wadau wa mazingira.

Ameongeza pia katika kuchagiza suala la utunzaji na uhifadhi wa mazingira, Jiji hilo limeanzisha na kutekeleza kampeni mbalimbali ikiwemo Tunza Mazingira Ng’arisha Nyamagana na kusimamia shughuli za usafi wa mazingira kwa kushirikiana na viongozi wa Jiji hilo.

“Wilaya ya Nyamagana inaendelea kuchukua hatua mbalimbali katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kwa kushirikiana na wadau ikiwa ni pamoja na kutoa elimu ya uhifadhi na utunzaji wa mazingira katika Kata zote 18” amesema Joseph.

Kwa upande wake Mwakilishi kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Afisa Misitu Mwandamizi Bw. Lucas Sabida ameupongeza Mkoa wa Mwanza kwa juhudi mbalimbali inazoendelea kuzifanya katika kuhamasisha jamii  kuhusu umuhimu wa kuhifadhi na kutunza mazingira.

Amesema Ofisi ya Makamu wa Rais imeendelea kupata ushirikiano wa kutosha kutoka kwa timu ya wataalamu wa Mazingira ya Mkoa huo na kuufanya kuwa ni miongoni mwa Mkoa ya mfano katika uhamasishaji wa jamii kuhusu umuhimu wa kutunza na kuhifadhi mazingira.

Maadhimisho ya Kilele cha Siku ya Mazingira Duniani, 2026 yatafanyika Kitaifa Mkoani Dodoma yakiwa na kauli mbiu isemayo Dira 2050: Tuwajibike Kukijanisha Tanzania.

Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana (kushoto) akiwa na Afisa Utumishi Mwandamizi kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Bi. Sheila Kikula (katikati) wakifanya usafi katika eneo la Soko Kuu la Jiji la Mwanza wakati wa zoezi la usafi wa mazingira Mkoani Mei 30, 2026 ikiwa ni maandalizi kuelekea Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani, 2026
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda (Katikati-traki suti nyekundu) akiongoza viongozi na watendaji Mkoani humo kufanya usafi katika eneo la Soko Kuu la Jiji la Mwanza Mei 30, 2026 wakati wa zoezi la usafi wa mazingira Mkoani humo kuelekea Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani, 2026.
 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda (kulia) akiongoza viongozi na watendaji wa Mkoa huo kufanya usafi katika eneo la Soko Kuu la Jiji la Mwanza Mei 30, 2026 katika zoezi la usafi wa mazingira Mkoani humo kuelekea Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani, 2026.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda (kulia) akiongoza Viongozi na Watendaji wa Mkoa huo kufanya usafi katika eneo la Soko Kuu la Jiji la Mwanza Mei 30, 2026 wakati wa zoezi la usafi wa mazingira Mkoani humo kuelekea Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani mwaka 2026.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda (kulia) akiongoza Viongozi na Watendaji wa Mkoa huo kufanya usafi katika eneo la Soko Kuu la Jiji la Mwanza Mei 30, 2026 wakati wa zoezi la usafi wa mazingira Mkoani humo kuelekea Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani mwaka 2026.
 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda (kulia) akiwa pamoja na Viongozi na Watendaji wa Mkoa huo wakikagua maeneo mbalimbali ya Soko Kuu la Jiji la Mwanza wakati wa zoezi la usafi wa eneo hilo Mei 30, 2026 kuelekea Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani mwaka 2026.  Katikati ni Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Mhe. Amiri Mkalipa.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda (wa pili kushoto) akiwa pamoja na Viongozi na Watendaji wa Mkoa huo wakikagua maeneo mbalimbali ya Soko Kuu la Jiji la Mwanza Mei 30, 2026 wakati wa zoezi la usafi wa eneo hilo kuelekea Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani mwaka 2026.  Kulia ni Katibu Tawala Wilaya ya Nyamagana, Bw. Thomas Salala





Na Janeth Raphael MichuziTv - Bungeni Dodoma

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum imeeleza kuendelea kuimarisha mifumo ya malezi, maadili na ustawi wa watoto na familia kama msingi muhimu wa kujenga Taifa lenye nguvu kazi yenye tija na maendeleo endelevu.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Wizara hiyo, Dkt. Dorothy Gwajima, wakati akiwasilisha hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2026/27 bungeni, ambapo ameeleza kwa kina mikakati inayoendelea kutekelezwa na Serikali katika kuhakikisha watoto wa Tanzania wanalelewa katika misingi bora ya maadili, ulinzi na ustawi wa kijamii.

Dkt. Gwajima amesema Wizara yake ina jukumu la kuratibu na kusimamia masuala yote yanayohusu malezi, maadili, matunzo na ustawi wa watoto pamoja na familia, ambazo ni nguzo muhimu katika maendeleo ya Taifa.

Amefafanua kuwa malezi chanya ya watoto yanayoambatana na maadili mema ni msingi wa kujenga Taifa imara lenye jamii yenye nidhamu, mshikamano na uwezo wa kuchangia maendeleo endelevu ya kiuchumi na kijamii.

Ameongeza kuwa Serikali imeendelea kuratibu utoaji wa elimu ya malezi chanya kwa wazazi, walezi na vijana balehe ikiwa ni sehemu ya juhudi za pamoja za kupunguza na hatimaye kutokomeza vitendo vya ukatili dhidi ya watoto nchini.

Katika hotuba yake hiyo, Waziri Gwajima amesisitiza kuwa watoto ni rasilimali muhimu na mtaji wa Taifa, hivyo wanapaswa kulindwa, kupendwa na kuendelezwa katika misingi ya maadili na tamaduni za Kitanzania.

Amesema mazingira bora ya malezi yanapaswa kuanzia ndani ya familia ambayo ndiyo chimbuko la tabia, nidhamu na maadili ya mtoto, lakini amebainisha kuwa kutokana na changamoto mbalimbali zikiwemo umaskini wa kipato, migogoro ya kifamilia, ukatili na vifo vya wazazi au walezi, baadhi ya watoto hujikuta wakiishi katika mazingira hatarishi yanayowafanya kuhitaji huduma za malezi mbadala na ulinzi wa kijamii.

Ameeleza kuwa Serikali inaendelea kutekeleza Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto ya mwaka 2021/22 hadi 2025/26, ambayo inalenga kuhakikisha kila mtoto mwenye umri wa chini ya miaka minane anapata huduma jumuishi za malezi na makuzi ili kuongeza kiwango cha ukuaji timilifu kutoka asilimia 47 ya sasa hadi asilimia 90 ifikapo mwaka 2050 kama ilivyoainishwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Amesema katika mwaka wa fedha unaoendelea, Wizara imeratibu uandaaji wa mfumo wa kitaifa wa kupima matokeo ya malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto unaojulikana kama Early Childhood Development Scorecard, ambao utasaidia kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa viashiria vya maendeleo ya mtoto nchini.

Aidha, Serikali imeanzisha mfumo wa kukusanya na kuchambua takwimu na taarifa za afua za malezi na makuzi ya awali ya mtoto kupitia mfumo wa ECD Dashboard, unaounganisha mifumo ya sekta mbalimbali za Serikali na taasisi zake.

Mfumo huo unalenga kubaini na kufuatilia utekelezaji wa nguzo tano muhimu za malezi na makuzi ya watoto wadogo ambazo ni afya bora, lishe toshelevu, uchangamshi na ujifunzaji wa awali, malezi yenye mwitikio pamoja na ulinzi na usalama wa watoto. Waziri Gwajima amesema nguzo hizo zina umuhimu sawa katika kuhakikisha mtoto anapata makuzi bora yatakayomwezesha kuwa raia mwenye mchango chanya katika jamii na Taifa kwa ujumla.

Katika hatua nyingine, Dkt. Gwajima amesema Wizara imetoa mafunzo kuhusu mifumo hiyo kwa maafisa 227 kutoka ngazi za mikoa na halmashauri zote nchini, ambapo kati yao maafisa 17 walitoka ngazi ya Wizara, 26 kutoka mikoa na 184 kutoka halmashauri, hatua inayoonesha dhamira ya Serikali ya kuimarisha usimamizi na utekelezaji wa afua za malezi na makuzi kwa karibu zaidi.

Amesema Serikali itaendelea kuhakikisha kila mtoto nchini analindwa, anapata malezi bora na analelewa katika mazingira salama yatakayomuwezesha kukuza vipaji na uwezo wake kikamilifu ili kuchangia maendeleo ya Taifa la kesho.


Na Janeth Raphael MichuziTv - Bungeni Dodoma

Mbunge wa Kigoma Mjini, Clayton Revocatus Chipando maarufu kama Baba Levo, ameibua mjadala bungeni jijini Dodoma baada ya kutoa maoni yanayogusa namna sera na elimu ya kijinsia zinavyotekelezwa nchini, akisisitiza haja ya kuangaliwa kwa usawa wa pande zote mbili za kijinsia bila kuacha kundi lolote nyuma.

Mbunge huyo amezungumza hayo wakati akichangia makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum kwa mwaka wa fedha 2026/27 ambapo ameseleza kuwa maendeleo ya jamii hayawezi kufanikiwa ipasavyo endapo yatabaki yakilenga upande mmoja tu wa jamii.

Katika mchango wake, Baba Levo ameeleza kuwa kumekuwa na mitazamo inayojikita zaidi katika kumuwezesha mwanamke, jambo ambalo kwa mujibu wake ni muhimu, lakini akasisitiza kuwa wanaume nao wanapaswa kuingizwa kikamilifu katika mipango ya elimu na uelimishaji kuhusu masuala ya kijinsia na maendeleo ya familia. 

Alisema kuwa jamii ni mchanganyiko wa wanaume na wanawake hivyo sera zinazohusu maendeleo zinapaswa kuzingatia uhalisia huo kwa usawa ili kuepusha migongano na hisia za upendeleo kwa upande mmoja.

Mbunge huyo pia amegusia changamoto zinazojitokeza ndani ya mahusiano na ndoa, akieleza kuwa baadhi ya migogoro ya kifamilia hutokana na kutoelewana, ukosefu wa uwazi na wakati mwingine madai yanayoibua hisia kali kati ya wanandoa.

 Alisisitiza kuwa mawasiliano ya kweli na uaminifu ni msingi muhimu wa kuimarisha familia, akibainisha kuwa endapo jamii itashindwa kushughulikia changamoto hizo kwa mtazamo mpana, migogoro itaendelea kuathiri ustawi wa familia na jamii kwa ujumla.

Baba Levo amesitiza pia umuhimu wa elimu ya ukatili wa kijinsia kutolewa kwa uwiano, akisema kuwa ingawa wanawake wanapaswa kuendelea kulindwa na kupewa uelewa zaidi kutokana na changamoto wanazokumbana nazo, pia kuna haja ya kuwajengea wanaume uelewa wa namna ya kushughulikia changamoto za kifamilia na kuepuka migogoro inayoweza kusababisha matatizo makubwa katika jamii. 

Aliongeza kuwa baadhi ya matukio ya kifamilia huweza kusababisha hisia kali na migogoro endapo hakuna ukweli na uwazi kati ya pande zinazohusika.

Kauli hizo zimeibua mjadala mpana miongoni mwa wabunge na wananchi, ambapo baadhi wameunga mkono wito wake wa kuangalia usawa wa kijinsia kwa pande zote, huku wengine wakisisitiza kuwa juhudi za sasa bado zinapaswa kuendelea zaidi katika kuwawezesha wanawake kutokana na historia ya changamoto walizopitia. 

Hata hivyo, mjadala huo unaendelea kuonesha umuhimu wa kuangalia upya namna sera na elimu ya kijinsia zinavyotekelezwa ili kuhakikisha zinagusa jamii kwa usawa bila kuacha kundi lolote nyuma.


Na Atley Kuni, WAF-Dar es Salaam 

Washiriki wa Maonesho ya Kimataifa ya Bidhaa za Kinywa na Meno Tanzania kutoka Mataifa mbalimbali duniani wameisifu Tanzania kwa ukarimu, mapokezi mazuri na ushirikiano wa hali ya juu walioupata katika kipindi chote cha maonesho hayo yaliyofanyika nchini.

Washiriki hao wamesema mazingira rafiki yaliyoandaliwa yamechangia mafanikio makubwa ya maonesho na kuimarisha ushirikiano wa kitaaluma na kibiashara kwa sekta ya afya ya kinywa na meno.

Akizungumza wakati wa kufunga maonesho hayo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya anayeshughulikia Dawa na Vifaa Tiba, Ndugu Emmanuel Tayari, amesema mafanikio ya maonesho hayo yanaonesha nafasi ya Tanzania kama kitovu muhimu cha uwekezaji, ubunifu na ushirikiano kwenye huduma za afya barani Afrika, akibainisha kuwa Serikali itaendelea kuweka mazingira wezeshi yatakayochochea maendeleo ya sekta hiyo.

Washiriki kutoka nje ya nchi wameelezea Tanzania kuwa ni taifa lenye watu wenye upendo, heshima na wanaozingatia misingi ya kidiplomasia, jambo ambalo limewavutia wengi wa wageni hao,wengi wameahidi kurejea Tanzania kushiriki katika maonesho yajayo.

"Maonesho haya yametupatia fursa ya kubadilishana uzoefu na kujifunza teknolojia mpya zinazolenga kuboresha huduma za afya ya kinywa na meno kwa wananchi" amesema Mshiriki Mmoja  kutoka nchini Zambia.

Kwa mujibu wa wataalamu wa afya, afya bora ya kinywa na meno ni sehemu muhimu ya afya kwa ujumla kwani huchangia kuzuia magonjwa mbalimbali na kuboresha ustawi wa maisha ya jamii.

Naibu Katibu Mkuu Bw. Tayari amewahakikishia washiriki ushirikiano wa karibu kutoka Serikali kwa maandalizi ya maonesho yajayo yatakayofanyika kuanzia tarehe 27 hadi 29 Mei, 2027.

"Serikali itaendelea kurahisisha taratibu za uingizaji wa bidhaa za kinywa na meno zitakazotumika katika maonesho hayo ili kuhakikisha washiriki wanapata mazingira bora ya kushiriki na kuonesha ubunifu wao", amesema Tayari.

Katika hatua nyingine Naibu Katibu Mkuu Tayari amewataka, washiriki hao kuwa mabalozi wazuri wa Tanzania kwa kuwahamasisha watengenezaji na wadau wengine wa bidhaa za kinywa na meno kutoka mataifa mbalimbali kushiriki kwa wingi katika maonesho yajayo. Hatua inayo tarajiwa kuongeza uwekezaji, kuimarisha ushirikiano wa kimataifa na kuendelea kuboresha huduma za afya ya kinywa na meno kwa manufaa ya wananchi wa Tanzania na dunia kwa ujumla.








MANYARA: KATIBU wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Kenani Kihongosi amesema msingi mkuu wa Chama chao ni kusikiliza wananchi na kuhakikisha changamoto zao zinapatiwa ufumbuzi.

Kihongosi amesema hayo leo Juni Mosi, 2026 wakati akizungumza na wanachama na wananchi wa Shina Namba Moja, Tawi la Masakta, Kata ya Masakta wilayani Hanang, Mkoa wa Manyara, ikiwa ni muendelezo wa ziara yake katika Kanda ya Kaskazini.

Amesema CCM imeendelea kuwa karibu na wananchi kwa sababu imejengwa katika misingi ya kusikiliza maoni yao, kutambua mahitaji yao na kuyafikisha katika mamlaka husika kwa ajili ya kutafutiwa ufumbuzi.

“Kazi hizi zinafanywa na chama kwa sababu chama hiki ndicho kinaunda Serikali. Lakini msingi wa CCM ni kusikiliza watu, kutatua shida za watu na zile changamoto ambazo zinakuwa kubwa basi zipelekwe katika maeneo husika ili zipatiwe ufumbuzi,” amesema Kihongosi.

Katika hatua nyingine, Kihongosi amesema chama kitaendelea kufuatilia suala la kupandisha hadhi zahanati ya Masakta na kuwa kituo cha afya kwa kushirikiana na viongozi wa Serikali ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya.

“Kama vigezo vitakuwa vimekidhi, niwahakikishie chama kitaendelea kusimamia kwa asilimia mia moja. Sote kwa pamoja tutashirikiana kuhakikisha jambo hili linapatiwa ufumbuzi wake,” amesema.

Kihongosi ameeleza hayo akujibu ombi la wananchi wa Kata hiyo ambalo lilihusu kupandishwa kwa hadhi ya Zahanati yao ya Kijiji kuwa Kituo cha Afya kutokana na ongezeko la idadi ya watu wanaohudumiwa katika zahanati hiyo na kuomba kuongeweza madaktari.

Awali akiwasilisha taarifa ya shina, Katibu wa Shina Namba Moja, Dismas Gwasima, aliiomba CCM na Serikali kuangalia uwezekano wa kupandisha hadhi zahanati ya Masakta na kuwa kituo cha afya kutokana na ongezeko la idadi ya wananchi wanaohudumiwa na kituo hicho.

Alisema zahanati hiyo imekuwa ikitoa huduma kwa zaidi ya miaka 20, lakini kwa sasa mahitaji ya huduma za afya yameongezeka sambamba na kukua kwa idadi ya watu, hali inayosababisha wananchi kukosa baadhi ya huduma muhimu zinazopatikana katika vituo vya afya.

Gwasima alisema wananchi wanahitaji kuongezewa huduma za mama na mtoto, huduma za upasuaji, watumishi wa afya pamoja na nyumba za watumishi ili kuboresha utoaji wa huduma katika eneo hilo.
















Meridianbet inaleta burudani ya kiwango kipya kupitia Super Heli Premium, mchezo unaochanganya kasi, ubunifu na msisimko wa kipekee kwa wapenzi wa michezo ya kisasa. Huu ni uzoefu unaobadilisha namna ya kufurahia burudani ya kidijitali kwa mtazamo mpya kabisa.

Kila mzunguko unapoanza, helikopta huonekana ikipaa angani, ikiongeza hamasa ya kuona hadi wapi safari ya ushindi inaweza kufika. Mchezaji anabaki akifuatilia kwa makini mabadiliko ya vizidishi vinavyopanda kwa kasi.

Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya MERIDIANBET au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Ubunifu wa mchezo huu unaruhusu chaguo mbalimbali za kimkakati kama Over/Under na uwezekano wa kusimamia mzunguko kwa njia ya kipekee. Hii inaleta hisia za kuhusika moja kwa moja katika kila hatua ya mchezo.

Mandhari ya safari za helikopta katika maeneo mbalimbali duniani huongeza ladha ya kifahari, ikifanya kila mzunguko kuwa tofauti na wa kuvutia zaidi kuliko uliopita.

Super Heli Premium inabaki kuwa alama ya burudani ya kisasa inayochanganya teknolojia na msisimko wa kipekee wa michezo ya mtandaoni ndani ya Meridianbet. Jisajili sasa uanze kuburudika.
SERIKALI YAFAFANUA JINSI WANAWAKE WA VIJIJINI WANAVYONUFAIKA NA MIKOPO YA ASILIMIA 10 YA HALMASHAURI


Na Janeth Raphael MichuziTv Bungeni - Dodoma 


Serikali imeeleza kuwa imeweka mifumo na taratibu mbalimbali za kuhakikisha wanawake wa vijijini wanapata fursa sawa ya kunufaika na mikopo inayotolewa kupitia asilimia 10 ya mapato ya Halmashauri nchini.

Kauli hiyo imetolewa bungeni na Naibu  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Dkt Festo Ndugange wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Dkt. Neema Peter Majule, aliyetaka kujua mpango wa Serikali wa kuhakikisha fedha hizo zinawafikia wanawake wa vijijini.

DKt Ndugange amesema kuwa kwa sasa utoaji wa mikopo hiyo unafanyika kupitia mfumo wa kielektroniki wa WEZESHA Portal, ambao umeboreshwa ili kutoa nafasi kwa makundi maalumu, ikiwemo wanawake wa vijijini, kuwasilisha maombi yao kwa urahisi na kwa wakati.

Amesema pamoja na matumizi ya mfumo huo wa kidijitali, Serikali imewaelekeza Watendaji wa Kata na Vijiji kuwasaidia wananchi wa maeneo ya vijijini, hususan wanawake, katika mchakato wa usajili na uwasilishaji wa maombi ya mikopo ili kuondoa changamoto kwa wale wasiokuwa na uelewa wa kutosha wa TEHAMA au vifaa vya mawasiliano.

“Lengo ni kuhakikisha hakuna mwanamke anayekosa fursa ya kupata mkopo kutokana na changamoto za matumizi ya teknolojia. Watendaji wa Serikali katika ngazi za chini wamepewa jukumu la kuwawezesha wanawake wa vijijini kufikia huduma hii kwa urahisi,” alisema Waziri huyo.

Aidha, Serikali imeeleza kuwa imeimarisha mfumo wa uhakiki wa waombaji ili kuhakikisha walengwa halisi ndio wanaonufaika na mikopo hiyo. Uhakiki huo unafanyika kuanzia ngazi ya Kamati za Maendeleo ya Kata (WDC), ambazo hupitia maombi yote kabla ya kuidhinishwa.

Hatua hiyo inalenga kuzuia vikundi visivyostahili kutumia anwani za vijijini kwa lengo la kupata mikopo pamoja na kuhakikisha fedha zinawafikia wananchi wa maeneo yaliyokusudiwa.

Kwa upande wa utekelezaji, Serikali imesema mwenendo wa utoaji wa mikopo kwa wanawake umeendelea kuimarika na kuzidi matarajio yaliyowekwa. Takwimu zinaonesha kuwa katika kipindi cha Julai 2024 hadi Machi 2026, Serikali ilipanga kutoa mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni 112.29 kwa wanawake, lakini hadi kufikia Machi 2026 jumla ya shilingi bilioni 136.01 zilikuwa zimetolewa.

Kiasi hicho ni sawa na utekelezaji wa asilimia 121 ya lengo lililowekwa, hali inayoonesha ongezeko kubwa la ushiriki wa wanawake katika kunufaika na mikopo hiyo.

Serikali imefafanua kuwa mafanikio hayo yamechangiwa na maboresho ya kanuni za utoaji mikopo yaliyowezesha fedha ambazo hazijatumika katika kundi moja kuhamishiwa kwenye kundi jingine lenye mahitaji makubwa ndani ya robo husika ya mwaka wa fedha.

Kutokana na hali hiyo, vikundi vya wanawake vimeendelea kupata mikopo kwa kiwango kikubwa zaidi ikilinganishwa na baadhi ya makundi mengine maalumu.

Waziri huyo alisisitiza kuwa Serikali itaendelea kufuatilia na kusimamia kwa karibu utekelezaji wa mpango wa mikopo ya asilimia 10 ili kuhakikisha wanawake wa vijijini wanaendelea kupata fursa za kiuchumi, kuongeza kipato na kuchangia maendeleo ya familia na jamii kwa ujumla.


MCHEZO huu wa kirafiki utakaopigwa leo Juni 1 saa 00:00 usiku una umuhimu mkubwa kwa timu zote mbili zilizofuzu Kombe la Dunia linaloanza mwezi huu. Brazil, anayewemo kundi C, anautumia mchezo huu kujenga kasi na kuirekebisha safu yake ya mwisho kabla ya mashindano.


Panama, ambaye yupo kundi L, anaona fursa ya kupima nguvu zake dhidi ya moja ya timu bora duniani na kujiamini kabla ya safari yake ya Ulimwengu.

Brazil ana safu ya wachezaji wenye vipaji vya kiwango cha juu sana, wakiwemo nyota kutoka Ulaya kama Vinícius Jr., Neymar, na kiungo bora. Uzoefu wao wa mashindano makubwa na kina cha kikosi kinawapa faida kubwa. Hata hivyo, changamoto yao ni kuhakikisha hawajeruhiwi kabla ya kombe la dunia, na wanaweza kucheza kwa mwendo wa polepole ili kuepuka majeraha ya ushindani usio wa lazima. Brazil anategemea mpira wa kuvutia na ubinafsi wa wachezaji wake.

Panama ni timu inayojulikana kwa nidhamu na uwezo wa kukaa imara nyuma, wakiwemo wachezaji wengi wanaocheza katika ligi za Amerika ya Kati na Kusini. Wakiwa ugenini dhidi ya Brazil, watalazimika kujitahidi sana katika safu ya ulinzi na kutumia fursa za mashambulizi ya haraka. Panama ana changamoto ya ukosefu wa kina cha wachezaji wa kiwango cha juu kuliko Brazil, lakini wanapambana kwa moyo wote.

Ingia kwenye kasi ya kujishindia pesa kwenye michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Mpira wa Brazil utategemea kudhibiti kiungo cha kati na kutumia wachezaji wa pembeni kuvunja ulinzi wa Panama. Kipa na safu ya ulinzi ya Panama watakuwa chini ya shinikizo kubwa, na uwezo wao wa kukaba na kudhibiti nafasi utaamua kama wataweza kuzuia magoli mengi. Mabadiliko ya wachezaji yatarajiwa mengi kutoka kwa Brazil katika kipindi cha pili ili kuhifadhi nguvu za wachezaji bora.

Kwa kuwa Brazil na Panama wote wamefuzu kwa Kombe la Dunia linaloanza mwezi huu, Brazil atataka kuondoka na ushindi wa kujiamini na kuwaacha mashabiki wake na furaha. Panama naye atapambana ili kuonesha kuwa anastahili kuwa kundi L licha ya kuwa timu ndogo. Hata hivyo, tofauti ya ubora ni kubwa mno. Jiajili

 

Na Mwandishi Wetu

Waandishi wa Habari watakaoshiriki Tuzo za Uandishi wa Habari na Makala za Maendeleo (Samia Kalamu Awards - SKA) 2026 wamelazimika kukidhi sharti la kuwa na ithibati kutoka Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), hatua inayolenga kuimarisha weledi, uwajibikaji na ushindani wa haki katika taaluma hiyo.

Akizindua rasmi mchakato wa kupokea kazi za kushindanishwa, Jumapili tarehe 31 Mei, 2026, jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa SKA, Mha. Peter Mwasalyanda, amesema maandalizi ya mwaka huu yanazingatia maelekezo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuendelea kutambua mchango wa Waandishi wa Habari za maendeleo nchini.
Mwasalyanda amesema ili kuhakikisha uadilifu, uwazi na ushindani wa haki, maandalizi ya tuzo hizo yanahusisha pia Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) kama mdau muhimu katika kusimamia weledi na maadili ya taaluma ya uandishi wa habari.

“Tuzo hizi zinalenga kutambua, kuthamini na kuhamasisha uzalishaji wa maudhui ya ndani yenye ubora, yanayochangia kuelimisha, kuhabarisha na kuburudisha, na kuimarisha taswira chanya ya Taifa kupitia habari za maendeleo,” amesema.
Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Wakili Patrick Kipangula, amesema tofauti na msimu wa kwanza wa tuzo hizo, mwaka huu washiriki wanapaswa kuhakikisha wamekidhi sharti la ithibati.

“Mtakumbuka Msimu wa kwanza wa Samia Kalamu mambo ya JAB hayakuwepo, kwa hiyo waandishi walishiriki wote bila kujali vigezo vya Ithibati lakini mwaka huu kuna hiki kigezo cha kuwa na ithibati kwa hiyo niwashauri basi wote wanaoshiriki kwenye hizi tuzo wahakikishe wanakuwa na ithibati, wamethibitishwa na Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari.” Amesema Wakili Kipangula na kuongeza;
“Ni muhimu sana kwa sababu ni takwa la kisheria na kitu ambacho hatuwezi kukikwepa. Nawahamasisha tushiriki wote kwa sababu isionekane ni tuzo za watu fulani tu, kila mmoja awasilishe kazi zake,” amesema Kipangula.

Kwa mujibu wa vigezo vya ushiriki vilivyotangazwa, Waandishi wa Habari wa Tanzania Bara wanatakiwa kuwa wamethibitishwa na JAB, huku kwa Zanzibar washiriki wakitakiwa kuwa na kitambulisho cha Mwandishi wa Habari (Press Card).

Tuzo hizo zimeanza kupokea kazi kuanzia Mei 31 hadi Juni 30, 2026 na zinatarajiwa kutolewa kati ya Oktoba na Desemba mwaka huu.

 


Na Mwandishi wetu, Iringa.

Wapiga Kura 222,218 walioandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura watashiriki kwenye uchaguzi mdogo wa Ubunge katika Jimbo la Isimani lililopo Halamashauri ya Wilaya ya Iringa Mkoani Iringa na Kata 12 za Tanzania Bara.
 
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele ameyasema hayo leo Mei 31, 2026 Mkoani Iringa wakati akisoma risala maalum kuhusu uchaguzi katika jimbo na kata husika utakao fanyika kesho Juni 01, 2026 na kusema kuwa jumla ya vituo 628 vya Kupigia Kura vitatumika.
 
“wapiga kura 89,753 wapo kwenye Jimbo la Ismani na wapiga kura 132,465 wapo kwenye kata 12 zitakazofanya uchaguzi mdogo na vituo 277 vipo kwenye Jimbo la Ismani na vituo 351 vipo kwenye kata 12 zitakazofanya uchaguzi mdogo.,”amesema Jaji Mwambegele.
 
Aidha, amesema Katika Uchaguzi huu, jumla ya wagombea 108 kutoka katika vyama vya siasa 17 wanawania nafasi wazi ya ubunge na udiwani katika maeneo niliyoyataja.

“Jimbo la Ismani lina wagombea 17 wa nafasi ya Ubunge ambapo kati ya wagombea hao wagombea nane (08) sawa na asilimia 47.06 ni wanaume na wagombea tisa (09) sawa na asilimia 52.94 ni wanawake. Kata 12 zinazofanya uchaguzi mdogo wa udiwani zina jumla ya wagombea 91 ambapo kati ya hao wagombea 61 sawa na asilimia 67.03 ni wanaume na wagombea 30 sawa na asilimia 32.97 ni wanawake.” alisema Jaji Mwambegele.

“Natumia fursa hii kuvikumbusha Vyama vya Siasa vinavyoshiriki uchaguzi kesho Juni 01, 2026 kuzingatia wajibu wao wa kuweka mawakala katika vituo vyote vya zoezi la kupiga, kuhesabu na kujumlishia kura. Wasimamizi wa uchaguzi katika Jimbo na Kata husika, wamekamilisha taratibu zinazoweka mazingira yanayowawezesha mawakala wa vyama vya siasa kufuatilia mchakato mzima wa uchaguzi,”alisema Jaji Mwambegele.
 
Amesema, mawakala hao, wanawajibika katika kulinda maslahi ya vyama na wagombea wao. Hivyo, wanapaswa kuzingatia Sheria, Kanuni, taratibu za Uchaguzi na maelekezo ya Tume katika utekelezaji wa majukumu yao vituoni.
 
Jaji Mwambegele amesema vituo vitafunguliwa saa 01:00 asubuhi na kufungwa saa 10:00 jioni na kwamba ifikapo muda wa kufunga kituo saa 10:00 kamili jioni, kama wapiga kura bado wapo kwenye mistari, mlinzi wa kituo atasimama nyuma ya mtu wa mwisho na zoezi la upigaji kura litaendelea hadi wapiga kura walio kwenye mstari watakapomalizika.
 
“Baada ya kumaliza kupiga kura, mpiga kura anatakiwa kuondoka eneo la kituo cha kupigia kura; na Mpiga kura awapo kituoni, anatakiwa kufuata maelekezo yote atakayopewa na karani mwongozaji wapiga kura,”amesema Jaji Mwambegele.
 
Kwa mpiga kura ambaye ameandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na taarifa zake zipo katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura lililopo katika kituo husika, lakini amepoteza kadi yake au kadi yake imeharibika, ataruhusiwa kupiga Kura kwa kutumia moja wapo ya vitambulisho cha Taifa NIDA, Leseni ya udereva au Pasi ya kusafiria (Passport).

Kata 12 zitakazo fanya uchaguzi ni Mzimuni iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni; Zongomera, Halmashauri ya Manispaa ya Kahama; Itilo, Halmashauri ya Mji Nzega; Ketare, Halmashauri ya Mji Tarime na Nyumbigwa, Halmashauri ya Mji Kasulu. 

Nyingine ni Kata ya Kala iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi; Ziba, Halmashauri ya Wilaya Igunga; Kamsisi, Halmashauri ya Wilaya ya Mlele; Nyamugali, Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe; Namasakata Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru; Bwongera, Halmashauri ya Wilaya ya Chato na Kibiti, Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti.
Cambridge, Uingereza Mkurugenzi Mtendaji na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna, amesema hatua inayofuata ya ukuaji wa Afrika itategemea taasisi zinazoaminika, mitaji ya muda mrefu na mifumo jumuishi, baada ya kuwasilisha hadithi ya mageuzi ya sekta ya benki Tanzania katika Cambridge Africa Business Conference 2026.

Akizungumza katika kongamano hilo lililoandaliwa na Cambridge Judge Business School, University of Cambridge, chini ya kaulimbiu ya “Kujenga Mustakabali wa Afrika: Mitaji, Ubunifu na Ukuaji wa Pamoja wa Bara la Afrika,” Zaipuna aliitumia safari ya NMB kama mfano wa taasisi ya Afrika inayoweza kuvutia mtaji, kuchochea ubunifu na kujenga uaminifu.

“Mustakabali wa Afrika hautaletwa kwetu na wengine; utajengwa na sisi wenyewe kupitia mifumo jumuishi, taasisi zinazoaminika na nidhamu ya kuleta matokeo chanya na endelevu kwa vizazi vijavyo,” alisema.

Zaipuna alieleza mageuzi ya NMB kutoka matawi 97, wateja takribani 600,000 na amana za Sh bilioni 150 mwaka 1997 hadi zaidi ya wateja milioni 10 leo. Alisema kati ya mwaka 2021 na 2025, NMB imewekeza zaidi ya Sh bilioni 230 katika miundombinu ya kidijitali, usalama wa mifumo, teknolojia za kiotomatiki na uwezo wa matumizi ya takwimu, huku zaidi ya asilimia 98 ya miamala yote sasa ikifanyika nje ya matawi kupitia njia za kidijitali na mbadala.

Katika mjadala huo, Mtaalamu wa Fedha (Structured Finance) kutoka AfDB, Eghosa Giwa Osaige, alisema kuimarisha uaminifu na kupunguza gharama za vihatarishi ni muhimu katika kuongeza mtiririko wa mitaji kuelekea Afrika.

Mkurugenzi wa Uwekezaji wa BII, Jumai Hadiza Mohammed, alisema hati fungani za kijamii na uendelevu za NMB zinatoa mfano imara kwa benki za Afrika kuhusu namna ubunifu, ubia na masoko ya mitaji vinavyoweza kufungua uwekezaji kwa kiwango kikubwa.


Mkurugenzi Mtendaji na Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB Bank Plc, Ruth Zaipuna, akitoa hotuba kuu katika Cambridge Africa Business Conference 2026 katika Chuo Kikuu cha Cambridge, ambako aliwasilisha safari ya mageuzi ya NMB na mchango wake katika uchumi wa Tanzania.







Top News