Watumishi wa ofisi ya Rais Tume ya Utumishi wa Umma, leo Februari 4, wakiongozwa na Mwenyekiti wa Tume hiyo Jaji Mstaafu Hamisa H. Kalombola, wametembelea  hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro iliyopo mkoani Arusha ikiwa ni sehemu ya utalii wa ndani, mara baada ya kumalizika kwa mkutano wa Baraza la Wafanyakazi, uliofanyika jana Februari 3, 2026.











 

Shule ya Sekondari ya Royal Family iliyopo Manispaa ya Geita imeandika historia mpya katika matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne 2025 yaliyotangazwa rasmi leo Januari 31,2026 na Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA).

Shule hiyo imefanya vizuri kwa kupata wanafunzi 33 wa Daraja la Kwanza na wanafunzi 3 pekee wa Daraja la Pili huku ikivuna rekodi adimu ya kutokuwa na mwanafunzi yeyote wa Daraja la Tatu,Nne wala Sifuri.

Matokeo hayo yameitambulisha Royal Family Sekondari kama miongoni mwa shule bora zaidi katika Manispaa ya Geita na Tanzania kwa ujumla yakidhihirisha ubora wa taaluma, nidhamu na uwekezaji mkubwa katika elimu.

Miongoni mwa wanafunzi waliopata daraja la kwanza na daraja la pili ni wale waliochujwa kwenye shule zingine kwa kigezo cha kutofanya vizuri na wakapokelewa shule ya sekondari ya Royal Family.

Walimu na wanafunzi wameelezwa kufanya kazi kwa bidii,mshikamano na malengo ya pamoja yaliyowezesha ushindi huo mkubwa usio na doa.

Akizungumza kwa furaha Mkurugenzi wa shule hiyo Mhandisi Lazaro Philipo alisema matokeo hayo ni matunda ya mipango thabiti ya kielimu na ushirikiano wa karibu kati ya walimu,wanafunzi na wazazi.

Aliongeza kuwa mafanikio hayo yanatoa motisha ya kuongeza juhudi zaidi ili shule iendelee kuwa kinara wa ufaulu bora na kuandaa wanafunzi wenye maarifa,maadili na ushindani wa kimataifa.






Serikali imetoa wito kwa wadau kutoka sekta ya fedha nchini kuanzisha huduma na bidhaa za kifedha zitakazowezesha ajenda ya nishati safi ya kupikia kusambaa zaidi, hususan kwa kuwawezesha wajasiriamali wadogo katika maeneo ya pembezoni na vijijini pamoja na wabunifu wa teknolojia za matumizi ya nishati hiyo.

Wito huo umetolewa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba tarehe 4 Februari 2026 wakati akimwakilisha Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi katika uzinduzi wa mradi wa nishati safi ya kupikia katika shule ya sekondari Bunge Wasichana iliyopo mkoani Dodoma.

"Tanzania imepiga hatua kubwa katika ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia, matumizi ya nishati hii yameongezeka kutoka asilimia 6.9 mwaka 2021 na kufikia asilimia 23.2 mwaka 2025. Hata hivyo, bado takribani asilimia 77 ya kaya nchini zinatumia nishati isiyo safi ya kupikia, hivyo natoa wito kwa sekta binafsi kuendelea kushirikiana na Serikali katika kusukuma ajenda hii kwa kuwezesha upatikanaji wa nishati mbalimbali safi za kupikia katika maeneo ya pembezoni na yale ya vijijini." Amesema Mhe. Salome

Aidha, Mhe. Salome amewasisitiza Wasambazaji wa gesi za mitungi kuongeza vituo vya usambazaji na ujazaji wa gesi za mitungi ili kurahisisha upatikanaji wake kwa watumiaji wengi zaidi, pia Wabunifu na vijana walioko vyuoni kufanya tafiti na kubuni nyenzo na teknolojia zitakazowezesha ajenda hii kusambaa na kuwafikia watu wengi.

Kuhusu mradi wa nishati safi ya kupikia aliouzindua Mhe. Salome amesema kuwa ni utekelezaji wa agizo la Serikali kwa taasisi zinazolisha watu zaidi ya 100 kutumia nishati safi ya kupikia ili kulinda afya za binadamu na kutunza mazingira.

Ameongeza kuwa mfumo huo uliozinduliwa utawezesha chakula kupikwa kwa usafi, kwa haraka, kwa ufanisi, kwa gharama nafuu na bila madhara ya moshi kwa wapishi na wanafunzi huku mazingira yakiendelea kustawi.

Mhe. Salome ameeleza kuwa kuzinduliwa kwa mradi huo ni sehemu ya juhudi za kitaifa zinazoongozwa na Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuhakikisha asilimia 80 ya watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo 2034 ambapo mpaka sasa tayari asilimia 23.2 ya wananchi wanatumia nishati safi ya kupikia huku taasisi 1,136 zinazolisha zaidi ya watu 100 kwa siku zikihamia katika matumizi ya nishati hiyo.

Akiwa katika shule hiyo ya Wasichana Bunge, Naibu Waziri amezindua pia Klabu ya Nishati Safi ya Kupikia yaani Clean Cooking School Club ambayo ni ya kwanza kuzinduliwa kwa Tanzania ambayo itakuwa mfano wa kuigwa na shule nyingine nchini katika kueneza elimu ya Nishati Safi ya Kupikia.

Wanafunzi watakaojiunga na klabu hiyo watakuwa Vinara wa Nishati Safi ya Kupikia (Clean Cooking Champions) na watashirikiana na Wizara ya Nishati na wadau wengine katika kutoa elimu mashuleni na katika jamii pamoja na kubuni teknolojia za nishati safi ya kupikia zitakazolinda afya na mazingira.

Awali Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Bunge Wasichana, Richard Msana alisema shule hiyo yenye wanafunzi 555 imefanikiwa kupunguza kwa kiasi kikubwa gharama za nishati ya kupikia baada ya kuachana na matumizi ya kuni na kuhamia katika gesi.

Amesema kuanzia Julai 2020 hadi Mei 2022, shule ilikuwa ikitumia takribani shilingi milioni 10.5 kwa kila miezi mitatu kununua kuni. Baadaye walipoanza kutumia mkaa mbadala, gharama zilishuka hadi kufikia shilingi milioni 2.7 na hivi sasa, kupitia mradi wa matumizi ya gesi, shule imenunua tani moja ya gesi iliyotumika kwa miezi miwili, ambapo matumizi ni wastani wa shilingi milioni 1.3 kwa mwezi, kiwango ambacho ni nafuu zaidi kiuchumi.






Na. Joseph Mahumi, WF, Arusha

Tanzania imeihakikishia Jumuiya ya Kimataifa inayojihusisha na ufuatiliaji na udhibiti wa Utakasishaji fedha haramu, ufadhili wa ugaidi na ufadhili wa silaha za maangamizi. Kwamba Serikali itaendelea kuimarisha na kuboresha mifumo yake ya udhibiti wa vitendo hivyo nchini.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi. Mshamu Ali Munde (Mb), kwa niaba ya Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi. Khamis Mussa Omar (Mb), wakati wa Mkutano wa Kimataifa wa Ubadilishaji wa Taarifa za Udhibiti wa Fedha Haramu Duniani (EGMONT Group meeting), uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha (AICC), jijini Arusha.

Alisema Tanzania imepiga hatua kubwa katika kujenga mfumo imara wa kupambana na uhalifu wa kifedha, ikiwa ni pamoja na kuimarisha taasisi za udhibiti na ushirikiano wa kimataifa, hatua ambayo imewezesha Tanzania kuondolewa kwenye orodha ya nchi zenye mapungufu katika udhibiti wa utakasishaji fedha na ufadhili wa ugaidi, baada ya kutekeleza kwa mafanikio mpango wa hatua uliowekwa na Kikosi Kazi cha Kudhibiti Utakatishaji Fedha (FATF).

“Uamuzi wa Umoja wa Ulaya kuiondoa Tanzania kwenye orodha ya nchi zenye hatari kubwa umefungua ukurasa mpya wa uaminifu wa kifedha na kuvutia uwekezaji wa kigeni na Tunajivunia mafanikio haya ambayo ni matokeo ya uongozi thabiti, mageuzi ya kisheria, na ushirikiano wa karibu kati ya taasisi zetu za ndani na washirika wa maendeleo,” alisema Mhe. Mhandisi Munde.

Alisisitiza kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana na nchi wanachama wa Kikundi cha EGMONT na makundi mengine kama Kikundi cha Afrika Mashariki na Kusini cha Kuzuia Utakasishaji Fedha - ESAAMLG, ili kuhakikisha mifumo ya ndani inalingana na viwango vya kimataifa vya uadilifu wa kifedha.

“Uhalifu wa kifedha hauna mipaka nchi moja haiwezi kushinda vita hii peke yake na tunapaswa kushirikiana, kubadilishana taarifa, na kufuatilia alama za fedha popote zinapopita,” aliongeza Mhe. Mhandisi Munde.

Aidha, Mhe. Mhandisi Munde, alizishukuru taasisi za kimataifa ikiwemo Kitengo cha Hazina cha Uingereza (UK Treasury Unit), Shirika la Ujerumani la Ushirikiano wa Kimataifa - GIZ, Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kudhibiti dawa za Kulevya na Uhalifu - UNODC, Mfuko wa Kimataifa wa Umoja wa Ulaya wa Kuzuia Utakasishaji Fedha na Ufadhili wa Ugaidi (EU Global Facility), Shirika la Fedha la Kimataifa - IMF na Benki ya Dunia kwa mchango wao mkubwa katika kutoa msaada wa kitaalamu na mafunzo kwa wataalamu wa uchunguzi na udhibiti wa fedha nchini.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Sekretarieti ya EGMONT, Bi. Elżbieta Franków- Jaśkiewicz, alisema kuwa Tanzania kama mwanachama wa EGMONT, imekua bora hasa katika ushirikiano wa kimataifa ambao ni muhimu zaidi katika kulinda uadilifu wa mfumo wa kifedha wa ndani na duniani kote.

Bi. Jaśkiewicz alisema Kuwa, EGMONT imejizatiti kusaidia wanachama wake kwa kutoa majukwaa salama kwa vitengo, kubadilishana ujuzi na taarifa za kifedha, na kuwasaidia kupambana na Utakasishaji wa fedha, ufadhili wa ugaidi, na uhalifu unaohusiana.

“Tunafurahi sana kukaribishwa hapa Tanzania kwa ukarimu, sehemu ambayo ina nafasi muhimu na ya kuhamasisha katika kuimarisha ushirikiano katika Ukanda wa Afrika Mashariki na Kusini, na inaendelea kuonesha dhamira yake thabiti katika kuimarisha na kuendeleza ushirikiano wa kikanda na kimataifa katika mapambano dhidi ya utakatishaji wa fedha na ufadhili wa ugaidi” alisema Bi. Jaśkiewicz.

Aliongeza kuwa kuwapo na zaidi ya wajumbe 400, katika mkutano huo ni ushahidi wa nguvu ya kimataifa ya Jumuiya ya EGMONT na dhamira ya pamoja inayowaunganisha.

Naye Kamishna wa Kitengo cha Kudhibiti Fedha Haramu (FIU), Bw. Majaba Magana, alisema kuwa safari ya Tanzania katika kupambana na utakasishaji wa fedha na ufadhili wa ugaidi imekuwa ikikua hatua kwa hatua, na inayolenga mageuzi kwa kuanzishwa kwa Kitengo cha Ujasusi wa Kifedha (Financial Intelligence Unit) chini ya Sheria ya Kuzuia Utakasishaji wa Fedha ambapo ni hatua muhimu ya kitaasisi, iliyounda mamlaka ya kati yenye jukumu la kupokea, na kuchambua taarifa za kifedha.

“Tangu kuanzishwa kwake, Tanzania imeendelea kuwa thabiti katika kuzingatia viwango vya kimataifa kwa kutekeleza mageuzi ya kina ya kuimarisha mifumo yetu ya kisheria na kitaasisi” alisema Bw. Magana

Aliongeza kuwa juhudi za Tanzania katika marekebisho muhimu ya kisheria, uimarishaji wa usimamizi unaozingatia tathmini ya hatari, na kuongezwa kwa uwezo wa kiutendaji zimeleta matokeo dhahiri, yanayoonekana kupitia kuboreshwa kwa taarifa za miamala yenye kutiliwa shaka, kuongezeka kwa matumizi ya taarifa za kifedha katika mashtaka ya jinai, na kuimarika kwa ushirikiano wa kimataifa.

Mkutano huo wa EGMONT, ulikutanisha nchi wanachama wa Jumuiya hiyo zaidi ya 182, ambapo wanachama walibadilishana maarifa, utaalamu na taarifa za kifedha, ili kuimarisha mapambano ya kimataifa dhidi ya utakasishaji wa fedha haramu , makosa ya msingi yanayohusiana na hayo, pamoja na ufadhili wa ugaidi.



Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi. Mshamu Ali Munde (Mb), akizungumza wakati akifungua Mkutano wa Kimataifa wa Ubadilishaji wa Taarifa za Udhibiti wa Fedha Haramu Duniani (EGMONT Group meeting), uliozikutanisha nchi wanachama zaidi ya 182, uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha (AICC), jijini Arusha, kwa niaba ya Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb).


Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi. Mshamu Ali Munde (Mb), akiagana na Mwenyekiti wa Sekretarieti ya EGMONT, Bi. Elżbieta Franków- Jaśkiewicz, baada ya kufungua Mkutano wa Kimataifa wa Ubadilishaji wa Taarifa za Udhibiti wa Fedha Haramu Duniani (EGMONT Group meeting) uliozikutanisha nchi wanachama zaidi ya 182, uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha (AICC), jijini Arusha.




Mwenyekiti wa Sekretarieti ya EGMONT, Bi. Elżbieta Franków- Jaśkiewicz, akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Kimataifa wa Ubadilishaji wa Taarifa za Udhibiti wa Fedha Haramu Duniani (EGMONT Group meeting) uliokutanisha nchi wanachama zaidi ya 182, uliofunguliwa na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi. Mshamu Ali Munde (Mb) kwa niaba ya Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha (AICC), jijini Arusha.


Baadhi ya Washiriki wa Mkutano wa Kimataifa wa Ubadilishaji wa Taarifa za Udhibiti wa Fedha Haramu Duniani (EGMONT Group meeting) uliokutanisha nchi wanachama zaidi ya 182, wakimsikiliza Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi. Mshamu Ali Munde (Mb) akihutubia kwa niaba ya Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), wakati akifungua Mkutano huo uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha (AICC), jijini Arusha.




Kamishna wa Kitengo cha Kudhibiti Fedha Haramu (FIU), Bw. Majaba Magana, akizungumza jambo wakati wa Mkutano wa Kimataifa wa Ubadilishaji wa Taarifa za Udhibiti wa Fedha Haramu Duniani (EGMONT Group meeting) uliokutanisha nchi wanachama zaidi ya 182, uliofunguliwa na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi. Mshamu Ali Munde (Mb) akihutubia kwa niaba ya Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha (AICC), jijini Arusha.


Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi. Mshamu Ali Munde (Mb) (Katikati aliyeketi), Mwenyekiti wa Sekretarieti ya EGMONT, Bi. Elżbieta Franków-Jaśkiewicz (kushoto aliyeketi), Kamishna wa Kitengo cha Kudhibiti Fedha Haramu (FIU), Bw. Majaba Magana (wa pili kushoto) aliyeketi, na Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Wataalamu wa Kuzuia Utakasishaji Fedha Haramu ambaye pia ni Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bi. Sauda Msemo (kulia aliyeketi), wakiwa katika picha ya pamoja na Kamati ya Maandalizi wa Mkutano wa Mkutano wa Kimataifa wa Ubadilishaji wa Taarifa za Udhibiti wa Fedha Haramu Duniani (EGMONT Group meeting) uliokutanisha nchi wanachama zaidi ya 182, uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha (AICC), jijini Arusha.



(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Arusha)

Katika kuadhimisha miaka 49 ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa ambaye pia ni Mlezi wa Kichama Mkoa wa Kilimanjaro, Ndugu Rabia Abdalla Hamid, ametembelea na kukagua utoaji huduma katika jengo la Mama na Mtoto katika hospitali ya Rufaa ya Mawenzi iliyopo mkoa wa Kilimanjaro.

Ndugu Rabia amefika hospitalini hapo leo tarehe 4 Februari 2026 ambapo amejionea utoaji wa huduma na kuzungumza na baadhi ya wakina mama wanaopatiwa huduma katika hospitali hiyo ambao wamemueleza namna ambavyo wamekuwa wakipatiwa huduma bora na kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na serikali yake ya awamu ya sita kwa uwekezaji mkubwa unaoendelea kufanywa katika miundombinu ya sekta ya afya nchini.

Ujenzi wa jengo la Mama na Mtoto hospitalini hapo ni moja kati ya utekelezaji kwa vitendo wa maagizo ya Ilani ya Uchaguzi ya CCM.

Aidha, Ndugu Rabia amesisitiza kuwa, kukamilika kwa ujenzi wa jengo hilo unasaidia kupunguza vifo vya mama na mtoto vitokanavyo na uzazi ambapo amesema kuwa jengo hilo litakua na huduma zote zinazohitajika katika kila wodi, na kwa upande wa wagonjwa wa nje, mama na mtoto ataweza kupata huduma zote hapohapo.

Kwa upande mwingine, Ndugu Rabia ametoa vifaa kwa watu wote wanaohudumiwa katika wodi ya wazazi ikiwa kama sehemu ya kuwafariji na kuwatakia afya njema.


#Miaka49YaCCM

#Tumechagua Umoja na Amani kwa Maendeleo ya Taifa Letu

#KaziNaUtuTunasongaMbele.















TUME ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyojitokeza wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, leo Februari 4, 2026, imekutana na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule.

Katika mkutano huo wa Tume ulifanyika katika Ukumbi wa Mkuu wa Mkoa, Senyamule aliongozana na Kamati yake ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa.

Miongoni mwa yaliyojadiliwa ni pamoja na namna matukio hayo yalivyoanza, athari zake kwa watu, mali na miundombinu pia ushauri wa namna ya kuondokana na matukio hayo.

Tume inaendelea kukutana na makundi mbalimbali wakiwemo waathirika wa Matukio hayo ambapo kwa Dodoma tume inaendesha shughuli zake katika Ukumbi wa Takwimu, kwa Mkoa wa Iringa Tume ipo Ukumbi wa Siasa ni Kilimo na kwa Shinyanga Tume ipo katika Ukumbi wa Manisapaa ya Kahama.






 


Meneja wa Utahini na Utunuku wa Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET), Dkt. Obeid Mahenya akizungumza wakati akifungua mafunzo maalum kwa Maafisa Udahili na Maafisa Mitihani kutoka katika Vyuo vya Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi nchini Tanzania katika ukumbi wa NSSF Mjini Shinyanga leo Februari 4,2026
Meneja wa Utahini na Utunuku wa NACTVET, Dkt. Obeid Mahenya akizungumza wakati akifungua mafunzo maalum kwa Maafisa Udahili na Maafisa Mitihani kutoka katika Vyuo vya Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi nchini Tanzania


Na Kadama Malunde - Shinyanga


Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) limeendesha mafunzo maalum kwa Maafisa Udahili na Maafisa Mitihani kutoka katika Vyuo vya Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi nchini Tanzania, kwa lengo la kuimarisha ufanisi wa mifumo ya udahili na mitihani katika vyuo hivyo.


Mafunzo hayo ya siku mbili, yanayofanyika Februari 4 na 5, 2026 katika Ukumbi wa NSSF, Manispaa ya Shinyanga, yamewakutanisha maafisa kutoka vyuo mbalimbali nchini kwa ajili ya kujifunza, kubadilishana uzoefu na kutatua changamoto zinazojitokeza katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.


Akifungua kikao kazi hicho kwa niaba ya Katibu Mtendaji wa NACTVET, Meneja wa Utahini na Utunuku wa Baraza hilo, Dkt. Obeid Mahenya, amesema Serikali inatambua na kuthamini mchango mkubwa wa elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi katika kukuza rasilimali watu wenye ujuzi unaokidhi mahitaji ya soko la ajira la ndani na kimataifa.


Meneja wa Utahini na Utunuku wa NACTVET, Dkt. Obeid Mahenya.

Ameeleza kuwa sekta hiyo ni mhimili muhimu katika kukuza ajira, kujiajiri, uchumi wa viwanda na utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2025–2050.

Amesema NACTVET, kama taasisi iliyoanzishwa kwa mujibu wa Sheria ya Bunge, Sura ya 129, ina dhamana ya kusimamia na kuhakikisha ubora wa elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi yanayotolewa nchini ili kuzalisha wahitimu wenye umahiri unaokidhi mahitaji ya soko la ajira.

Hata hivyo, amebainisha kuwepo kwa changamoto mbalimbali, ikiwemo udahili hafifu unaoonekana katika kanzidata ya Baraza pamoja na ucheleweshaji wa upakiaji wa matokeo ya mitihani.

Ametoa mfano kuwa hadi Januari 20, 2026, kulikuwa na chuo kilichosajili wanafunzi wanne pekee katika mfumo wa Baraza kwa mwaka wa masomo 2025/2026, hali isiyoakisi idadi halisi ya wanafunzi waliopo vyuoni.

Kutokana na hali hiyo, NACTVET ililazimika kuongeza muda wa usajili wa wanafunzi hadi Januari 31, 2026 ili kutoa fursa kwa vyuo vyote kusajili wanafunzi katika kanzidata ya Baraza.

Aidha, amesema vyuo vingi vimekuwa vikichelewa au kushindwa kupakia matokeo ya mitihani kwa wakati kulingana na kalenda ya kitaaluma ya Baraza, jambo linaloleta athari kwa wanafunzi na wadau wengine.

Dkt. Mahenya amesisitiza kuwa vyuo vyote vinapaswa kuwasilisha matokeo ya mitihani kupitia kanda husika kabla ya Februari 15, 2026.

Kwa mujibu wa Dkt. Mahenya , changamoto hizo zimekuwa zikisababisha wanafunzi kukosa mikopo ya elimu, kuchelewesha kuendelea na masomo, kuchelewa kwa utoaji wa vyeti pamoja na kukosa fursa za ajira, hali inayokwamisha maendeleo ya wananchi na Taifa kwa ujumla.


Meneja wa NACTVET Kanda ya Kati – Dodoma, Bw. Ramadhani Samainda.


Akizungumza katika kikao kazi hicho, Meneja wa NACTVET Kanda ya Kati – Dodoma, Bw. Ramadhani Samainda, kwa niaba ya Mkurugenzi wa Udahili, Mitihani na Utunuku wa NACTVET, Dkt. Marcelina Baitilwake, amesema mafunzo hayo yameandaliwa kufuatia changamoto za uelewa mdogo wa mifumo ya udahili na mitihani, kutokuzingatia taratibu na ucheleweshaji wa uthibitishaji wa matokeo, hali inayowaathiri wanafunzi katika kuendelea na masomo, kupata vyeti na fursa za ajira.


Ameeleza kuwa washiriki wanapatiwa mafunzo kuhusu miongozo ya udahili na mitihani, matumizi sahihi ya mifumo ya kielektroniki, ulipaji wa ada za uhakiki wa ubora na upatikanaji wa namba za uthibitisho wa tuzo, kwa lengo la kuongeza ufanisi na ubora wa huduma zinazotolewa vyuoni.


Kupitia mafunzo hayo, amesema Baraza linakusudia kuimarisha uwezo wa maafisa udahili na mitihani, kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao na kuhakikisha huduma zinatolewa kwa wakati kwa kuzingatia miongozo na kanuni zilizopo.


Amewashauri Maafisa Udahili na Maafisa Mitihani kuhakikisha wanakuwa na Kalenda ya Baraza na kuingiza matukio muhimu katika kalenda za vyuo vyao ili kurahisisha utekelezaji wa majukumu na kufikia malengo ya pamoja ya Baraza na taasisi zao.

Meneja wa Utahini na Utunuku wa NACTVET, Dkt. Obeid Mahenya akizungumza wakati akifungua mafunzo maalum kwa Maafisa Udahili na Maafisa Mitihani kutoka katika Vyuo vya Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi nchini Tanzania

Meneja wa Utahini na Utunuku wa NACTVET, Dkt. Obeid Mahenya akizungumza wakati akifungua mafunzo maalum kwa Maafisa Udahili na Maafisa Mitihani kutoka katika Vyuo vya Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi nchini Tanzania

Meneja wa Utahini na Utunuku wa NACTVET, Dkt. Obeid Mahenya akizungumza wakati akifungua mafunzo maalum kwa Maafisa Udahili na Maafisa Mitihani kutoka katika Vyuo vya Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi nchini Tanzania

Meneja wa Utahini na Utunuku wa NACTVET, Dkt. Obeid Mahenya akizungumza wakati akifungua mafunzo maalum kwa Maafisa Udahili na Maafisa Mitihani kutoka katika Vyuo vya Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi nchini Tanzania

Meneja wa NACTVET Kanda ya Kati – Dodoma, Bw. Ramadhani Samainda, akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Udahili, Mitihani na Utunuku wa NACTVET, Dkt. Marcelina Baitilwake kwenye mafunzo maalum kwa Maafisa Udahili na Maafisa Mitihani kutoka katika Vyuo vya Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi nchini Tanzania

























Top News