Na Oscar Assenga,Muheza, Tanga

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais anayeshughulikia Maendeleo ya Vijana, Joel Nanauka amesema serikali itaendelea kuvipa kipaumbele vikundi vya vijana vinavyoonyesha uwajibikaji kwa kurejesha mikopo wanayopewa ili viweze kukuza shughuli zao za kiuchumi.

Nanauka aliyasema hayo leo wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii iliyotembelea kikundi cha Vijana cha Mali Hai kilichopo wilayani Muheza mkoani Tanga kwa lengo la kukagua shughuli zao za uzalishaji pamoja na miradi iliyopata fedha kupitia mikopo ya halmashauri.

Akiwa kwenye kikundi hicho alionyesha kuridhishwa na juhudi na nidhamu ya kikundio hicho kurejesha mikopo baada ya kufanikiwa kukuza mtaji wake kutoka shilingi milioni 20 hadi kufikia zaidi ya shilingi milioni 50, hatua inayotajwa kuwa mfano bora kwa vikundi vingine vya vijana nchini.

Nanauka alisema kikundi cha Mali Hali ni miongoni mwa vikundi vichache nchini vilivyofanikiwa kurejesha mikopo kwa wakati, jambo ambalo limekifanya kupata nafasi ya kuangaliwa kwa karibu zaidi katika mipango ya kusaidiwa kuongeza mtaji na kupanua shughuli zake.

Alisema katika mchakato unaoendelea wa kusaidia wajasiriamali wadogo na kurasimisha shughuli zao, serikali itaangalia namna ya kukiweka kikundi hicho kwenye orodha ya vikundi vitakavyosaidiwa ili kuimarisha shughuli zao za uzalishaji.

Aidha, alieleza kuwa serikali inatekeleza maelekezo ya Rais ya kuhakikisha vijana wanaochukua hatua ya kufanya kazi na kuonyesha juhudi wanapatiwa mikopo na serikali ili waweze kujikwamua kiuchumi na pia kutoa ajira kwa wengine.

“Vijana hawa wameonyesha mfano mzuri kwa watanzania wengine wameanza na mtaji mdogo mwaka 2008,wakapata msaada wa shilingi milioni tano mwaka 2018 na baadaye mkopo wa shilingi milioni 20 mwaka wa fedha 2020/2021. Leo hii wameongeza mtaji wao hadi kufikia zaidi ya milioni 50. Huu ni ushahidi kwamba ndoto kubwa zinaweza kuanza na mwanzo mdogo,” alisema Nanauka.

Aliongeza kuwa serikali itahakikisha vijana wenye juhudi kama hao wanapata fursa zaidi, ikiwemo mikopo mingine, pamoja na kushirikishwa katika zabuni za serikali ili waweze kukuza biashara zao.

Nanauka pia aliwashauri vijana nchini kutokudharau mwanzo mdogo na kuwa na uvumilivu wanapotekeleza ndoto zao za kimaendeleo.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii, Hawa Mchafu, alisema kamati hiyo ipo katika ziara ya kawaida ya kukagua miradi ya maendeleo kabla ya kuanza kwa Bunge la Bajeti, ambapo wamepita katika maeneo mbalimbali kutathmini miradi iliyopata fedha za serikali.

Alisema kamati hiyo imevutiwa na kazi nzuri inayofanywa na kikundi hicho cha vijana, lakini imebaini changamoto ya eneo la uzalishaji kuwa dogo na huenda lisiweze kukidhi mahitaji yao iwapo wataongeza mtaji zaidi.

Kutokana na hali hiyo, kamati imeitaka wizara husika kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga kuhakikisha vijana hao wanapatiwa eneo kubwa zaidi la kufanyia shughuli zao za uzalishaji ili waweze kupanua biashara zao.

“Eneo walilonalo sasa ni dogo ukilinganisha na malengo yao ya kupanua uzalishaji hivyo tunashauri wapatiwe eneo kubwa zaidi na lililopo sasa likibaki kama sehemu ya maonesho ya bidhaa wanazozalisha,” alisema Mchafu.

Pia aliishauri serikali kuangalia uwezekano wa kukipa kikundi hicho mkopo mwingine wa kifedha ili kiweze kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazokikabili, ikiwemo kununua gari kwa ajili ya shughuli za uzalishaji na usafirishaji wa bidhaa.

Aidha, alitumia nafasi hiyo kuwakumbusha vijana nchini kutumia fursa zilizotolewa na serikali kupitia mifuko mbalimbali ya maendeleo ya vijana badala ya kujikita kwenye mfuko mmoja pekee.

Mchafu alisema kuwa Rais ametoa zaidi ya shilingi bilioni 200 kwa ajili ya kusaidia maendeleo ya vijana kupitia wizara na taasisi mbalimbali, hivyo vijana wanapaswa kuzitumia fursa hizo kujikwamua kiuchumi.

Kamati hiyo pia imeishauri serikali kuhakikisha sheria ya manunuzi ya umma inayotaka asilimia 30 ya zabuni za serikali zitolewe kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu inatekelezwa kikamilifu ili kuwapatia vijana nafasi ya kukua kiuchumi.

Kwa sasa kikundi cha Mali Hali kinadaiwa kuajiri vijana zaidi ya 20 katika shughuli zake za uzalishaji, jambo ambalo limeelezwa kuwa linaunga mkono dhamira ya serikali ya kukuza ajira kwa vijana na kuimarisha uchumi wa wananchi.

Vijana wa kikundi hicho pia wamemshukuru Rais kwa kuendelea kutoa fursa na kuahidi kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kufikia ndoto zao za kuanzisha kampuni kubwa inayoweza kutoa ajira kwa vijana wengi zaidi katika Mkoa wa Tanga na maeneo mengine nchini.















 

-Kamati yaridhishwa na ujenzi Chuo kikuu Mzumbe kampasi ya Tanga


Na Mashaka Mhando, Mkinga


WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amesema Serikali itaendelea kuimarisha miundombinu ya elimu ya juu kupitia miradi ya kimkakati ikiwemo ule wa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET), ili kuchochea utafiti na ubunifu utakaosaidia maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Prof. Mkenda ametoa kauli hiyo wilayani Mkinga wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Michezo na Utamaduni ilipotembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa Kampasi ya Tanga ya Chuo Kikuu Mzumbe.

Alisema serikali itaendelea kuboresha lakini pia alisema kuwa atahakikisha anavuta wawekezaji wengine binafsi kujenga taasisi za elimu katika eneo hilo.

Alisema Wizara itahamasisha taasisi nyingine za elimu na sekta binafsi kuwekeza Mkinga ili kukuza dhana ya mji wa kitaaluma. Alibainisha kuwa mkoa wa Tanga utapewa kipaumbele kwa Chuo hicho kufundisha kozi za kimkakati ikiwemo uchumi wa Buluu (Blue Economy) Madini na Uvuvi ili kuendana na fursa za mkoa huo.

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Prof. William Mwegoha, ameiambia kamati hiyo kuwa ujenzi wa miundombinu hiyo umefikia asilimia 82, ukijumuisha jengo la taaluma, kituo cha afya, mabweni ya wanafunzi, mkahawa, nyumba za wafanyakazi pamoja na mifumo ya maji safi na taka.

Akijibu maswali ya wabunge waliotaka kujua mkandarasi kuongezewa muda Profesa Mwegoha alisema unatarajiwa kukabidhiwa mwezi Mei mwaka huu na utahudumia wanafunzi 1,500 na mradi una thamani ya Shilingi Bilioni 16.

“Eneo hili lina ekari 300 na ujenzi unazingatia Master Plan ya kisasa. Changamoto kubwa iliyotuchelewesha ni mazingira ya kijiografia ikiwemo miamba na ubovu wa barabara wakati wa mvua, lakini mkandarasi Dimetoclasa Real Hope Ltd yupo asilimia 82 ya utekelezaji,” alisema Prof. Mwigoha.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Husna Sekiboko, amesisitiza umuhimu wa mradi huo kukamilika kwa wakati kwa mujibu wa mkataba, huku akibainisha kuwa taarifa za ziara hiyo zitasaidia katika maandalizi ya Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2026/2027.

“Tumeridhishwa na hatua iliyofikiwa na tunatarajia kazi zote zikamilike kwa wakati ili mradi huu uanze kutoa tija iliyokusudiwa na Serikali katika kuimarisha uwekezaji wa elimu ya juu,” amesema Sekiboko.

Kampasi hiyo ya Chuo Kikuu Mzumbe inajengwa katika Kijiji cha Pangarawe, Kata ya Gombero wilayani Mkinga, mwenyekiti wa Kamati alisema kuwa Wizara ya Elimu iweke wazi mahitaji ya kifedha ili kukamilisha miundombinu wezeshi.

Ziara hiyo ya kikazi ililenga kukagua utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2025/2026 na utekelezaji wa Ilani ya CCM.

Mwenyekiti wa Kamati, Mhe. Husna Sekiboko, alipongeza thamani ya fedha (Value for Money) inayoonekana katika majengo hayo, lakini akaonya kuhusu kusuasua kwa huduma za kijamii. “Haiwezekani mwanafunzi wa Chuo Kikuu abebe ndoo kutafuta maji au barabara ishindwe kupitika. Tunataka Wizara iwe wazi katika mtiririko wa fedha za bajeti ya 2026/2027 ili tumalize kero ya barabara ya kilomita 16 kutoka Mabokweni na umeme wa uhakika,” alisisitiza Mhe. Sekiboko.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mkinga, Mhe. Jumaa Kasinya, alitangaza neema kwa wabunge na wawekezaji kwa kusema kuwa Halmashauri imetenga ekari 500 kwa ajili ya "Academic City" na amewahamasisha wajumbe wa Kamati hiyo kufika na wao wawe sehemu ya uwekezaji katika eneo hilo.

Mkuu wa Wilaya ya Mkinga, Mhe. Gilbert Kalima, aliongeza kuwa kufuatia agizo la Waziri Mkuu, TARURA tayari wamefanya tathmini ya ujenzi wa barabara za lami ndani ya chuo hicho, ambapo aliomba ziongezwe hadi kilomita tano ili kuongeza hadhi ya kampasi hiyo.

Wajumbe wa Kamati, akiwemo Baraka Mwamengo, Asha Feruzi, na Yumna Mmanga Omar, walipongeza uamuzi wa Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuweka chuo hicho Mkinga, wakisisitiza kuwa maboresho ya barabara  za ndani zitazamwe ikiwemo kusimamia mkandarasi aweze kumaliza Chuo hicho kwa wakati alioongezewa.

Viongozi wa Mkoa wa Tanga na Wilaya ya Mkinga waliohusika katika ziara hiyo wameeleza kuwa kukamilika kwa kampasi hiyo kutachochea fursa za ajira na kuvutia uwekezaji katika maeneo ya jirani, jambo litakaloinua uchumi wa wananchi wa ukanda huo.







Wabunge kutoka Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakitembelea maeneo mbalimbali walipofanya ziara ya kikazi ya kujionea maendeleo ya Kongani Maalum la Uwekezaji (BSEZ) ya Buzwagi ambayo ipo ndani ya mgodi wa Barrick Buzwagi ambao upo katika hatua za mwisho za ufungaji.

Wabunge kutoka Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakitembelea maeneo mbalimbali walipofanya ziara ya kikazi ya kujionea maendeleo ya Kongani Maalum la Uwekezaji (BSEZ) ya Buzwagi ambayo ipo ndani ya mgodi wa Barrick Buzwagi ambao upo katika hatua za mwisho za ufungaji.

Wabunge kutoka Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakitembelea maeneo mbalimbali walipofanya ziara ya kikazi ya kujionea maendeleo ya Kongani Maalum la Uwekezaji (BSEZ) ya Buzwagi ambayo ipo ndani ya mgodi wa Barrick Buzwagi ambao upo katika hatua za mwisho za ufungaji.


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Utawala , Katiba na Sheria ya Bunge , Dkt Damas Ndumbaro akizugumza na wajumbe wa kamati hiyo , kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya kahama , viongozi wa halmashauri ya Kahama na wafanyakazi na menejimenti ya Barrick Buzwagi wakati wa ziara hiyo ya siku moja ya kutembelea kongani maalum la uwekezaji ya Barrick Buzwagi.

Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji , Dkt. Pius Chaya akiongea na Wabunge wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria walipofanya ziara ya kikazi ya kujionea maendeleo ya Kongani Maalum la Uwekezaji (BSEZ) ya Buzwagi ambayo ipo ndani ya mgodi wa Barrick Buzwagi ambao upo katika hatua za mwisho za ufungaji.

Meneja wa Ufungaji wa Mgodi wa Barrick Buzwagi , Mhandisi Zonnastraal Mumbi akizungumza mbele ya Wabunge wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria walipofanya ziara ya kikazi ya kujionea maendeleo ya Kongani Maalum la Uwekezaji (BSEZ) ambalo lipo ndani ya mgodi wa Barrick Buzwagi ambao upo katika hatua za mwisho za ufungaji.

Mkurugenzi Mkuu wa TISEZA,Gilead Teri akizungumza mbele ya Wabunge wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria walipofanya ziara ya kikazi ya kujionea maendeleo ya Kongani Maalum la Uwekezaji (BSEZ) ambalo lipo ndani ya mgodi wa Barrick Buzwagi ambao upo katika hatua za mwisho za ufungaji.


*
# Kamati ya Bunge ya Sheria yaitaka Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum (TISEZA) kuisimamia Kongani hiyo badala ya Halmashauri ya Manispaa ya Kahama.


Kamati ya kudumu ya Bunge Utawala , Katiba na sheria imeelekeza serikali kupitia Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji kuikabidhi rasmi kwa ajili ya kusimamiwa Kongani Maalum ya Uwekezaji ya Buzwagi (BSEZ) kwa Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum Tanzania (TESIZA) ili kuhakikisha inaendelea kuvutia wawekezaji na kutengeneza mazingira mazuri ya biashara ili kuleta matokeo Chanya pia imepongeza Barrick kwa kufunga mgodi kitaalamu .




Akizungumza kwenye majumuisho ya ziara ya kamati hiyo , Mwenyekiti wake , Dkt. Damas Ndumbaro (MB) amesema kamati imeonelea kwamba ni muhimu kwa mamlaka ya uwekezaji kusimamia kongani hiyo badala ya kuikabidhi kwa halmashauri ya Manispaa ya Kahama.


“Tunachukua fursa hii ya kipekee kwanza kwa kuwashuruku uongozi wa Barrick kwa kazi nzuri ya ufungaji wa mgodi huu wa Buzwagi kitaalamu na kuweka mazingira mazuri ya uanzishwaji wa kongani maalum ya biashara na uwekezaji ni jambo muhimu kwa maslahi ya nchini yetu,”


“Tumetembelea eneo hili mahususi kwa ajili ya uwekezaji tumeona wenyewe kwamba maji, miundombinu ya barabara , umeme vipo ambavyo ni kichochea cha kuvuta uwekezaji wa ndani na wa nje,” amesema Dkt. Ndumbaro.


Ameongeza kwamba kwenye mchakato wa kuvutia wawekezaji nchini moja ya changamoto ni sheria ya fedha ambayo kwa namna fulani si rafiki sana kwa kuvutia wawekezaji tutaendelea na kuishauri serikali na mapendekezo yetu ni baadhi ya vifungu vya sheria ya fedha viondolewe ili kufungua milango zaidi ya uwekezaji.


Dkt. Ndumbaro amesisitiza kuwa ni muhimu kwa Halmashauri ya Kahama kuendelea na shughuli zingine za wananchi na kuiachia Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) kwenye uendelezaji wa kongani hii na kuvutia wawekezaji nchini.


Dkt. Ndumbaro amesema Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) inaelekeza kila wilaya kuwa na kongani ya viwanda ili kuongeza ajira kwa wananchi na kukuza uchumi wa maeneo husika.


Ameitaka pia (TISEZA) kuwa karibu na eneo hilo na kulitangaza zaidi ili kuvutia wawekezaji wengi zaidi ndani ya nchini na nje.


“Kupitia Ilani ya uchaguzi ya chama cha mapinduzi ni lazima serikali iendelee kuutia wawekezaji wa ndani na wa nje ili kupunguza tatizo la ajira na kupanua wigo wa mapato ya serikali nchini,” ameongeza Dkt. Ndumbaro.


Amesema kongani hiyo ni ya kipekee ikilinganishwa na maeneo mengine ya uwekezaji kwa kuwa ina miundombinu muhimu ikiwemo umeme wa uhakika, maji ya kutosha, barabara pamoja na uwanja wa ndege unaorahisisha usafiri wa wawekezaji.


“Tunataka TISEZA wawe karibu na kongani hii ili wawekezaji watakapopatikana wasikumbane na changamoto za kiutaratibu katika hatua za kuanzisha uwekezaji wao,” amesema Dkt. Ndumbaro.


Kwa upande wake , Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji , Dktt. Pius Chaya amesema kuwa, serikali imeyachukua mapendekezo ya kamati ya kudumu ya Bunge kuhusu mamlaka ya uwekezaji kusimamia kongani hiyo badala ya halmashauri ya kahama kwa ajili ya kuongeza ufanisi.


Amefafanua kwamba serikali ya awamu ya sita kwa kushirikiana na sekta binafsi , kama vile Barrick itaendelea na mipango hiyo ambayo ipo kwenye dira ya taifa ya maendeleo 2020-2050 ili kuhakikisha tunaendelea kupunguza umasikini na kukuza uchumi wa nchini.


“Kupitia mpango wa ushirikiano kati ya sekta binafsi na serikali (PPP) tunataka mchango wa sekta binafsi kwenye pato la taifa lifike 70% ili kuendelea kufungua milango zaidi ya ushirikishwaji wa sekta hiyo muhimu kwenye nguzo za uchumi wa nchini yetu,” ameongeza Dkt. Chaya


Amesema serikali inaipongeza Barrick ambayo ina ubia nayo kupitia kampuni ya Twiga Minerals kwa kuendelea kufanikisha miradi mbalimbali ya maendeleo na kuahidi kwamba ushirikiano huo utaendelea ili kufungua fursa zaidi na kupanua mazingira wezeshi ya uwekezaji hapa nchini.


Naye, Meneja wa Ufungaji wa Mgodi wa Buzwagi Zonnastraal Mumbi amesema Barrick itaendelea kushirikiana na serikali katika kuvutia wawekezaji kwa kutengeneza mazingira mazuri ya uwekezaji na kuzingatia viwango vya kimataifa vya ufungaji wa mgodi na weledi.


“Mgodi wa Barrick Buzwagi ulianza mchakato wa ufungaji 2021 kwa kushirikiana na Tume ya Kitaifa ya Ufungaji na baadaye tukaanza rasmi safari ya kubadilisha eneo hili ilikuwa sehemu ya uwekezaji wenye tija baada ya kujiridhisha pamoja na serikali kwamba miundombinu ya hapa ni bora na ya kuvutia uwekezaji,” amesema.


Mhandisi Magige Marwa kutoka Mamlaka ya Maji Safi wa Mazingira Kahama (KUWASA) akizungumza na kamati hiyo ilipotembelea mradi wa ujenzi wa chujio la maji la Mwendakulima ambayo unatazamiwa kuhudumia zaidi ya 66% ya wakazi waishio Manispaa ya Kahama na ina uwezo wa kutoa lita milioni 10 kwa siku.


“Mradi huu unatarajiwa kukamilika Mwezi Juni mwaka huu na mpaka sasa 78% ya mradi mzima umeshakamilika kutoka na kasi ya ujenzi wa mradi huu mkubwa kwenye mji huu wa kahama,” amesisitiza.


Mhandisi Marwa amefafanua kwamba mradi huo wa chujio la maji ya mvua 62% imefadhiliwa na mgodi wa Barrick- Buzwagi na 38% ni Kuwasa kupitia Wizara ya Maji na Serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania.


Kongani ya Barrick Buzwagi ina ukubwa wa hekta 1,333 na ipo katika eneo lililokuwa Mgodi wa Barrick Buzwagi. Hadi sasa jumla ya wawekezaji 35 wameonesha nia ya kuwekeza katika eneo hilo, ambapo mwekezaji mmoja tayari ameanza uzalishaji wa vipuri na vifaa vya migodini, watano wako katika hatua za kufuatilia leseni huku wawekezaji 29 wakiwa katika hatua za awali za uwekezaji.


Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania (TAFORI) kwa kushirikiana na Shirika la ADAP (Association for the Development of Protected Areas) imeongoza hatua za uanzishwaji wa Jukwaa la Wadau wa Uyoga nchini, hatua itakayowezesha wadau wa Sekta ya Uyoga kunufaika kiuchumi na kuongeza kipato kupitia maendeleo ya zao hilo.

Akizungumza leo Machi 13, 2026 katika Makao Makuu ya TAFORI, Morogoro, wakati wa mkutano wa Uanzishwaji wa Jukwaa la Wadau wa Uyoga Tanzania, Mkurugenzi Mkuu wa TAFORI, Dkt. Revocatus Mushumbusi, alisema jukwaa hilo litaratibu juhudi za Wadau wa Sekta ya Uyoga nchini kwa kuwawezesha kubadilishana maarifa na uzoefu pamoja na kuendeleza sekta hiyo.

Alisema kuanzishwa kwa jukwaa hilo kunalenga kuchangia maendeleo ya ustawi wa uhifadhi wa misitu, uchumi wa wananchi na kuongeza mchango wa zao hili katika pato la Taifa.

Aidha, alisema jukwaa hili litakuwa chombo muhimu cha kutoa ushauri wa kisera, kuhamasisha uwekezaji na kuimarisha ushirikiano wa Kitaifa na Kimataifa.

“Ni matumaini yangu kuwa kupitia chombo hiki, Wadau wataibua mawazo mapya, kuimarisha ushirikiano na kuweka mikakati madhubuti itakayosaidia kuendeleza Sekta ya Uyoga, usalama wa chakula, maendeleo ya uchumi yanayoweza kumgusa Mwananchi moja kwa moja na uhifadhi wa mazingira,” alisema.

Dkt. Mushumbusi alisisitiza ni muhimu kuimarisha tafiti za Kisayansi kuhusu aina na thamani ya uyoga ili zao hili liweze kutoa mchango mkubwa zaidi katika uchumi wa Taifa. Aliongeza kuwa hatua hiyo iende sambamba na kujenga uwezo wa jamii katika kutambua uyoga unaoliwa na wenye sumu, pamoja na kuendeleza teknolojia za uongezaji thamani na kuimarisha masoko ya bidhaa za uyoga.

Alisema uyoga una mchango katika utekelezaji wa Sera mbalimbali za Taifa, ikiwemo Sera za Taifa za Kilimo na Lishe kwa kuongeza upatikanaji wa chakula chenye virutubisho muhimu. Pia alieleza kuwa maendeleo ya zao hilo yanaweza kuchochea ukuaji wa viwanda vidogo na vya kati kupitia uongezaji thamani kama ukaushaji, usindikaji na ufungashaji wa uyoga, hali itakayosaidia kuongeza ajira na kipato kwa Wananachi na hasa makundi maalumu ya kijamii wakiwepo Wanawake na Vijana.

Hatua ya kuanzishwa kwa Jukwaa la Uyoga nchini imefuata baada ya kufanyika kwa Warsha ya Wadau wa Uyoga iliyofanyika Mkoa wa Tabora mwezi Februari, 2025.

Mkutano huo umehudhuriwa na Wadau kutoka Shirika la ADAP, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Mamlaka ya Wanyamapori Tanzania (TAWA), Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela(NM-AIST), Wizara ya Mambo ya Ndani, pamoja na Wakusanyaji na Wafanyabiashara wa Uyoga.


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imefanya ziara ya kikazi mkoani Geita kukagua miradi inayosimamiwa na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), ambapo imemwagiwa sifa kwa mapinduzi ya teknolojia kwa wachimbaji wadogo.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo katika eneo la Katente, Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa, ameeleza kuwa serikali kupitia STAMICO imejikita kuhakikisha wachimbaji wadogo wanajifunza kwa nadharia na vitendo.

Dkt. Kiruswa amebainisha kuwa kituo hicho kinahudumia zaidi ya wachimbaji wadogo 1,019, ambao sasa wana uwezo wa kuleta marudio yao (mbare) na kuondoka na dhahabu iliyo safi ndani ya muda mfupi kutokana na matumizi ya teknolojia ya kisasa ya CIP.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Subira Mgalu, ametoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuwezesha vituo vya mfano vinavyowasogezea wataalam karibu na wachimbaji.

"Ni wakati sasa kwa STAMICO na Wizara ya Madini kuona namna ya kuongeza ukubwa wa vituo hivi ili kutoa huduma kwa wachimbaji wengi zaidi na kwa uharaka zaidi," alisisitiza Mhe. Mgalu.

Kaimu Mkurugenzi wa STAMICO, Bw. Deusdedith Magala, ametoa shukrani kwa Kamati hiyo kwa kuridhishwa na uwekezaji wa shirika hilo. Amesema jitihada hizo zinalenga kuhakikisha huduma za serikali zinafika moja kwa moja kwa walengwa katika sekta ya madini.











Na: Mwandishi Wetu

Wanachama wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), tawi la China (Diaspora), limeandaa Kongamano la Siku ya Kimataifa ya Wanawake 2026 kwa njia ya mtandao (Google Meeting) ili kujadili masuala mbalimbali ya kimaendeleo yamuhusuyo mwanamke.

Kongamano hilo linatarajiwa kufanyika Machi 15, 2026, majira ya saa tisa kamili alasiri hadi saa kumi na mbili kamili jioni. Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa (MCC) na Mbunge wa Viti Maalum, Mary Chatanda, anatarajiwa kushiriki Kongamano hilo akiwa Mgeni Rasmi. 

"Nimefurahi kupata mwaliko huu ambao kama wanawake tutajadili masuala mbalimbali ya kumuinua mwanamke kimaendeleo na changamoto zinazomkabili mwanamke kama tunavyojua mwanamke ni nguzo na kiungo muhimu katika maendeleo kuanzia ngazi ya familia hadi Taifa. Kwa kweli tunajivunia kuona mwanamke mwenzetu, Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, akionyesha uwezo mkubwa wa kiuongozi," amesema Chatanda.

Viongozi wengine watakaoshiriki Kongamano hilo la Wanawake ni pamoja na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) anayeshughulikia Masuala ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa - SUKI, Rabia Hamid, Mbunge wa Viti Maalum Vijana, Timida Fyandomo, Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Rebeca Nsemwa na Mkuu wa wilaya ya Lindi, Victoria Mwanziva.

Wanachama wa CCM waishio nchini China wameandaa kongamano hilo ikiwa ni njia ya kuenzi mchango wa mwanamke katika maendeleo ya nchi. Ikumbukwe Siku ya Kimataifa ya Wanawake huadhimishwa kila mwaka ifikapo Tarehe 08 Machi, ambapo kwa mwaka huu 2026, maadhimisho hayo yamechagizwa na kaulimbiu isemayo " Haki na Usawa kwa Wanawake na Wasichana: Msingi Jumuishi Kufikia Dira 2050."



Cameroon-born, LA-raised Afrofusion artist releases her most personal work yet — a mid-tempo empowerment anthem produced by acclaimed producer Mystro Sugar and mixed by Grammy-nominated mixing engineer Giggz

LOS ANGELES, CA — March 6, 2026 — Nella, the Cameroonian-born, Bamiléké Afrofusion artist raising from Los Angeles and Houston, today announces the release of her new single “LUKAKU,” available now on Spotify, Apple Music, Boomplay, Audiomack, and YouTube.

LUKAKU is Nella’s most fully realized statement to date — a mid-tempo empowerment anthem that flips the Afrobeats tradition of pursuit and longing on its head. Where much of the genre celebrates the chase, LUKAKU is the sound of a woman who has stopped running and stopped waiting. Built on a steady 4/4 groove, syncopated bass, plucked electric guitar, and textured percussion, the production balances dancefloor rhythm with emotional restraint — a minor-key progression that gives the record depth while layered harmonies and polished vocals place it firmly in modern Afrobeats.



“I no fi chase. I no be Lukaku,” she declares in West African Pidgin — a language spoken across Nigeria, Cameroon, Ghana and the diaspora, and one that gives the hook its communal, chantable power. The reference is to the striker known for dribbling defenders: Nella refuses to be dribbled, chased, or played. The song moves between English and Pidgin, and the production — crafted by acclaimed producer Mystro Sugar and mixed by Grammy-nominated engineer Giggz — is globally resonant and unmistakably hers. Sonically, it sits at the intersection of Wizkid’s rhythmic subtlety, the unshakeable cool of early Sade, and the melodic confidence of Tems and Ayra Starr.

LUKAKU offers something genuinely underrepresented in music: a mid-tempo groove that empowers without bitterness, detaches without drama, and lets women walk away without asking to be chased. “Now my feelings stuck on rewind” — not moving forward, not chasing, just pausing. It is the strange peace of not caring enough to fast-forward anymore — emotional intelligence delivered with the vulnerability of Jorja Smith and the cool self-possession of Rihanna’s ANTI era. Produced by acclaimed music producer Mystro Sugar and mixed by Grammy-nominated mixing engineer and producer Giggz, LUKAKU arrives as the emotional centrepiece of a catalog that has amassed over 1.5 million total streams and a devoted global following Nella calls the Moonbeams.

“I gave you all my good years, it blew away to the wind. Now I’m gone. Bye bye.”

— Nella, LUKAKU

The song sits at a specific emotional crossroads in Nella’s discography. Her previous single, No Visa — released October 2025 — is, in chronological terms, its prequel: the release that came before LUKAKU. But as a piece of storytelling, No Visa is the sequel. It depicts a woman who has already done the internal work — who now loves fully and without walls. LUKAKU is the earlier chapter: the reckoning of a woman who once did not love herself, named what she gave away, and chose to reclaim it.

LUKAKU will be released via OneRPM distribution and is accompanied by a content strategy rooted entirely in Nella’s authentic story. Her father dancing to the song became one of the most-shared moments of her release campaign. The “good girl turn bad” origin story behind the song’s key lyric generated the highest saves and shares of any post in her career to date.


ABOUT NELLA


Nella is a Bamiléké Afrofusion artist born in Yaoundé, Cameroon, raised between Los Angeles and Houston. A healthcare provider by training, she is the creator of a sound that belongs to no genre and speaks to everyone who has ever had to choose between who they were told to be and who they actually are.

Her father played guitar; her mother danced. These were not influences — they were architecture. Nella founded her high school’s first Hip-Hop club in California, set music aside to build a career in healthcare, and returned to the studio not as a luxury but as a lifeline. Her catalog moves through English, French, West African Pidgin, and Fèfè, fusing Makossa, Bikutsi, Afrobeats, Amapiano, and R&B into a style that is equally celebration and confession.

Inspired by Tems, Tiwa Savage, Charlotte Dipanda, Beyoncé, and Teyana Taylor, Nella has been featured by Fox 21, GQ South Africa, The Guardian, Soundcity, Chop Daily, and Not Just Okay. With over 1.5 million streams, a growing global audience, and a community of Moonbeams who do not just follow her but claim her — Nella is not a rising artist. She is an arrived one.



STREAM LUKAKU


Spotify: open.spotify.com/artist/1srgbcQlCI56byuqb1FphT

Apple Music: music.apple.com/us/artist/nella/1764690030

YouTube: youtube.com/watch?v=LpWPlN68DoI

Boomplay: boomplay.com/artists/101354562

Audiomack: audiomack.com/nella-355


FOLLOW NELLA


Instagram: instagram.com/nellaleen_/

TikTok: tiktok.com/@nellaleen — 358.4K followers

YouTube Channel: youtube.com/@nellaleen

Facebook: facebook.com/nellasongbird/


PRESS CONTACT


Kris Noulaheu

Press / PR — Songbirds Media

nellasongbird@gmail.com


© 2026 Nella Music · Songbirds Media · OneRPM Distribution · All Rights Reserved



-Akemea watumishi wanaowaelekeza wananchi kununua dawa nje ya hospitali

-Aonya utapeli wa ardhi za vijiji

-Akemea wakandarasi wanaolipwa fedha za miradi lakini hawawalipi mafundi


WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba ameagiza kufanyika kwa uchunguzi kuhusu mfumo wa upatikanaji wa dawa katika hospitali na vituo vya kutolea huduma za afya nchini.

Ametoa agizo hilo leo Jumapili (Machi 15, 2026) alipokuwa akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Nsimbo katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Songambele mkoani Katavi, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi mkoani humo.

Amesema Serikali imekuwa ikipeleka fedha kwa ajili ya ununuzi wa dawa katika hospitali na vituo vya afya, lakini bado baadhi ya wananchi wanapofika kutafuta huduma wanaelekezwa kwenda kununua dawa katika maduka binafsi nje ya hospitali.

“Takwimu zinaonesha tuna utoshelevu wa dawa lakini mwananchi akienda hospitalini anaelekezwa mtaani kwenda kununua dawa. Huu mchezo haukubaliki. Duka la mtaani linapata wapi dawa ambayo Serikali haiwezi ikapata?” amesema.

Kutokana na hali hiyo, Waziri Mkuu amesema ni muhimu kufanya uchunguzi wa kina ili kubaini namna fedha za ununuzi wa dawa zinavyotumika pamoja na mfumo wa upatikanaji wa dawa katika vituo vya kutolea huduma za afya.

Katika hatua nyingine, Dkt. Mwigulu ameonya tabia ya baadhi ya viongozi kuuza ardhi ya vijiji kwa njia zisizo halali na kusababisha migogoro ya ardhi katika jamii.

“Hata tukigombana ardhi haiongezeki. Binadamu tunaongezeka lakini ardhi haiongezeki. Hata tukipigana ardhi haiongezeki, kwa hiyo tuepuke kuchukiana kwa misingi hiyo,” amesema.

Amesema Serikali haitavumilia vitendo vya utapeli wa ardhi vinavyofanywa na baadhi ya viongozi wasiowaadilifu.

“Watu wa aina hii wakishagundulika wasidunde mtaani lazima wafike kwenye mkono wa sheria. Wanataka kuvunja undugu wetu kwa tamaa na ubinafsi,” amesema.

Kadhalika, Waziri Mkuu ameonya wakandarasi wanaolipwa fedha za miradi ya Serikali lakini wanashindwa kuwalipa mafundi na wakandarasi wadogo waliotekeleza kazi hizo.

“Mkandarasi anapewa kazi anaajiri mafundi, anatoa subcontract kwa wengine, yeye analipwa fedha yote ya mradi lakini hawalipi wale waliofanya kazi. Watu wa aina hiyo wasakwe popote pale walipo na wasiwe huru mpaka wawalipe watu ambao wameshafanya kazi,” amesema.

Amesema vitendo hivyo vinawanyima haki wananchi waliotekeleza kazi kwa uaminifu na vinaweza kuifanya jamii kuilaumu Serikali wakati fedha za miradi tayari zimeshalipwa kwa wakandarasi.

“Hii kuchukua fedha Serikali imeshalipa halafu wananchi wetu ambao wamefanya kazi hawajalipwa ni kuwasababishia umaskini watu ambao wamefanya kazi kwa uaminifu,” amesema.

Katika mkutano huo, Waziri Mkuu amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuwekeza katika miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo sekta za afya, elimu na miundombinu.

Amesema katika kipindi cha miaka minne iliyopita Serikali imejenga hospitali za wilaya 119, vituo vya afya 649 pamoja na zahanati zaidi ya 2,700 nchini kote kwa lengo la kuboresha huduma za afya kwa wananchi.

Aidha, amesema Serikali imejenga zaidi ya shule za sekondari 1,300 pamoja na shule za ufundi zaidi ya 103 ili kuwawezesha vijana kupata elimu na ujuzi unaowawezesha kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo.







Maafisa wa kulinda walaji kutoka Tume ya Ushindani (FCC) wametoa elimu kwa wananchi wa Halmashauri ya Chalinze mkoani Pwani kuhusu haki na wajibu wa mlaji, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya maadhimisho ya Siku ya Kumlinda Mlaji duniani yanayotarajiwa kufanyika Machi 31, 2026.

Elimu hiyo imelenga kuwajengea wananchi uelewa kuhusu namna ya kutambua bidhaa na huduma zenye ubora, pamoja na hatua wanazopaswa kuchukua pale wanapokutana na udanganyifu au ukiukwaji wa haki zao kama walaji. Wananchi pia wamehimizwa kuhifadhi risiti za manunuzi na kutoa taarifa kwa mamlaka husika wanapobaini vitendo vya biashara visivyozingatia sheria.

Maafisa hao wameeleza kuwa lengo la utoaji wa elimu hiyo ni kuhakikisha walaji wanakuwa na uelewa wa kutosha ili kujilinda dhidi ya bidhaa bandia, bei zisizo halali na huduma zisizokidhi viwango. Aidha, wamesisitiza umuhimu wa wananchi kushiriki kikamilifu katika kulinda maslahi yao kwa kufahamu haki na wajibu wao wanapofanya manunuzi au kutumia huduma mbalimbali.

Maadhimisho ya Siku ya Kumlinda Mlaji hufanyika kila mwaka duniani kote kwa lengo la kuongeza uelewa kuhusu haki za walaji na kuhamasisha biashara kufuata misingi ya haki, uwazi na uwajibikaji katika utoaji wa bidhaa na huduma. Serikali na taasisi mbalimbali nchini huendelea kutumia maadhimisho hayo kutoa elimu kwa jamii ili kujenga mazingira salama na yenye ushindani wa haki sokoni.






 

Kuna methali isemayo “Asiyejua maana haambiwi maana “ lakini Ngorongoro leo itakuambia maana ya Nyayo za Laetoli.

Nyayo hizi ni za kihistoria na ni sehemu pekee duniani ambayo mafundi Viatu ulimwenguni wanaweza kufika na kutengeneza Viatu vya kihistoria vinavyoweza kushinda nishani ya Nobel kutokana na Nyayo za Laetoli zilivyo.

Katika eneo la Laetoli ndani ya hifadhi ya Ngorongoro, tarehe 24, Julai mwaka 1978, Mtafiti maarufu wa masuala ya Akiolojia Dr. Mary Leakey na timu yake iliyomhusisha Dkt. Paul Abell waligundua nyayo za zamadamu katika eneo la Laetoli zilizohifadhika katika mwamba wa jivu la volcano inayoaminika kuwa ililipuka katika mojawapo wa milima ya Ngorongoro miaka milion 3.6 iliyopita. 

Wataalamu hawa wanaamini kuwa nyayo hizo ziliachwa na jamii ya watu wa kale wanaofahamika kama Australopithecus Afarensis.

Nyayo za Zamadamu katika eneo la Laetoli ni ushahidi wa pekee na wa bayana duniani kote usiopingika kwamba zamadamu (Hominin) kwa mara ya kwanza walianza kusimama wima na kutembea kwa miguu miwili katika eneo la Laetoli Ngorongoro Tanzania miaka milioni 3.6 iliyopita.

 Binadamu hawa waliotembea wima kwa miguu miwili wametokana na babu/bibi mmoja aliyeishi miaka takribani millioni 7 iliyopita. 

Mwanadamu aliyepo Tandahimba, Gamboshi kule Bariadi, Tandale kwa mtogole, Mbagala Zakiem na yule aliyepo Jerusalemu, Macca, Dubai, New York, London, Johannesburg, Tehran, Gaza, Misri hadi Sudan na Mumbai wametokana na babu na bibi mmoja.

Katika kuthibitisha uhai, Nyayo za zamadamu ndizo za kustaajabisha katika eneo la Laetoli, zipo nyayo za wanyama wengine wa kale kama vile nyayo za tembo, twiga, faru na wanyama ndogo kama sungura, kanga na aina za wadudu.

Kwa nyayo za Laetoli zilivyo, mafundi Viatu na wamiliki wa viwanda vya Viatu duniani wanaweza kufika katika Eneo  hilo ili kupata  ujuzi zaidi wa namna ya kutengeneza Viatu vya kihistoria.

 Karibu kwetu Ngorongoro ambapo kila ukilala kuna ndoto ya maajabu inakuita


Muonekano wa Nyayo za Laetoli zilizoachwa na jamii za watu wa kale wanaofahamika kama Australopithecus Afarensis

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, amepongeza jitihada za Benki ya NBC za kuendelea kupanua wigo wa ujumuishi wa kifedha kupitia huduma yake ya kibenki isiyo na riba, La Riba (Islamic Banking), akisema huduma hiyo imewafungulia Waislamu milango mipya ya kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi bila kwenda kinyume na misingi ya imani yao.

Bi. Senyamule aliyasema hayo mwishoni mwa wiki jijini Dodoma wakati akiongoza hafla ya futari iliyoandaliwa na NBC kwa ajili ya wateja wake wenye imani ya Kiislamu pamoja na wadau mbalimbali, wakiwemo viongozi wa dini na serikali. Hafla hiyo pia ilihudhuriwa na viongozi na maofisa wa benki hiyo wakiongozwa na Mkurugenzi wa Fedha wa NBC, Rayson Foya, aliyemwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi.

Akizungumza katika hafla hiyo, Bi. Senyamule alisema huduma za kifedha zinazozingatia misingi ya Kiislamu zimekuwa chachu muhimu ya kuwawezesha waumini wa dini hiyo kushiriki kikamilifu katika mfumo rasmi wa kifedha, hivyo kuongeza kasi ya shughuli za kiuchumi katika jamii.

“Huduma ya La Riba imewafungulia wenzetu wenye imani ya Kiislamu milango ya kushiriki kikamilifu katika huduma za kifedha bila hofu ya kwenda kinyume na misingi ya dini yao. Hii ni hatua muhimu sana katika kuimarisha ujumuishi wa kifedha na kuhamasisha maendeleo ya wananchi,” alisema Bi. Senyamule.

Alisema uwepo wa huduma kama hiyo unachochea wananchi wengi zaidi kutumia taasisi rasmi za kifedha katika kukuza biashara, kilimo na shughuli nyingine za kiuchumi, jambo linalochangia kukuza uchumi wa mkoa na taifa kwa ujumla.

Kwa upande wake, Bw. Foya alisema huduma ya La Riba imeendelea kupata mwitikio mkubwa kutoka kwa wateja wenye imani ya Kiislamu nchini, huku ikitoa fursa kwao kupata huduma za kifedha zinazozingatia misingi ya dini yao.

Alisema kupitia dirisha hilo, zaidi ya wateja 24,000 wanahudumiwa kwa sasa, wakiwa na amana zinazozidi shilingi bilioni 90, huku uwezeshaji wa kifedha uliotolewa kupitia mfumo huo ukizidi shilingi bilioni 48.

“Takwimu hizi zinaonesha wazi kuwa huduma za La Riba zimepokelewa vizuri na wateja wetu wenye imani ya Kiislamu. Tutaendelea kuimarisha huduma hizi ili kuwapa wateja wetu suluhisho za kifedha zinazolingana na mahitaji na imani zao,” alisema Bw. Foya.

Aliongeza kuwa katika kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhani, benki hiyo inaona ni muhimu kuimarisha zaidi mahusiano yake na wateja pamoja na wadau kwa kushirikiana nao katika shughuli za kijamii na kiuchumi.

Bw. Foya alibainisha kuwa NBC imefanikiwa kubuni na kutoa huduma mbalimbali za kifedha zinazozingatia misingi ya Kiislamu, zikiwemo akaunti za akiba na biashara, akaunti za uwekezaji wa muda maalum (Fixed Investment Accounts), pamoja na huduma za uwezeshaji wa kifedha kupitia mfumo wa Murabaha.

Katika hatua nyingine, Bi. Senyamule aliipongeza NBC kwa mchango wake katika kuendeleza michezo na ustawi wa jamii kupitia tukio la NBC Dodoma Marathon, ambalo limeendelea kuwa jukwaa muhimu la kuchochea uchumi wa jiji la Dodoma.

Alisema mbio hizo ambazo mwaka uliopita zilivutia zaidi ya washiriki 12,000, zimekuwa zikichochea shughuli za kiuchumi katika sekta mbalimbali zikiwemo biashara, utalii na huduma, huku pia zikisaidia kukusanya fedha kwa ajili ya kuboresha huduma za afya ya mama na mtoto.

Akizungumzia mbio hizo, Bw. Foya alisisitiza kuwa NBC itaendelea kuunga mkono juhudi za maendeleo ya jamii kupitia miradi mbalimbali ya kijamii, ikiwemo kuendeleza mbio hizo ambazo mbali na kukuza michezo pia zinachangia kuokoa maisha kupitia miradi ya afya.




Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule (kushoto) akipokea zawadi maalum ya mwezi Mtukufu wa Ramadhan kutoka kwa Mkurugenzi wa Fedha wa NBC, Rayson Foya (katikati) wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya wateja wake jijini Dodoma mwishoni mwa wiki. Anaeshuhudia ni Mkuu wa Kanda ya Kati wa benki ya NBC, Bw Miraji Msuya. Hafla hiyo ilihusisha uwepo wa wateja na wadau mbalimbali wa benki hiyo wakiwemo viongozi wa serikali na dini.


Mkurugenzi wa Fedha wa NBC, Rayson Foya (mbele) akiwaongoza wageni waalikwa kupata futari wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na benki ya NBC kwa ajili ya wateja wake jijini Dodoma mwishoni mwa wiki. Hafla hiyo ilihusisha uwepo wa wateja na wadau mbalimbali wa benki hiyo wakiwemo viongozi wa serikali na dini.


Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule (katikati) akifuatilia matukio tofauti wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na benki ya NBC kwa ajili ya wateja wake jijini Dodoma mwishoni mwa wiki. Wengine ni pamoja na Meneja wa Benki ya NBC Kanda ya Pwani Bi Zubeider Haroun (kulia) na Meneja wa NBC tawi la Dodoma Bi Happiness Kizigira. Hafla hiyo ilihusisha uwepo wa wateja na wadau mbalimbali wa benki hiyo wakiwemo viongozi wa serikali na dini.


Mkurugenzi wa Fedha wa NBC, Rayson Foya (pichani) akizungumza na wageni waalikwa wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na Benki ya NBC kwa ajili ya wateja wake jijini Dodoma. Hafla hiyo ilihusisha uwepo wa wateja na wadau mbalimbali wa benki hiyo wakiwemo viongozi wa serikali na dini.


Meneja Uhusiano wa Huduma za Kibenki zinazozingatia Sheria za Imani ya Kiislam (Islamic Banking) wa benki ya NBC Bw Ally Abdul (pichani) akizungumza na wageni waalikwa wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na Benki ya NBC kwa ajili ya wateja wake jijini Dodoma. Hafla hiyo ilihusisha uwepo wa wateja na wadau mbalimbali wa benki hiyo wakiwemo viongozi wa serikali na dini.


Mkurugenzi wa Fedha wa NBC, Rayson Foya (pichani) akifuatilia matukio wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na Benki ya NBC kwa ajili ya wateja wake jijini Dodoma. Hafla hiyo ilihusisha uwepo wa wateja na wadau mbalimbali wa benki hiyo wakiwemo viongozi wa serikali na dini.






Hafla hiyo ilihusisha utoaji wa zawadi mbalimbali za mwezi wa Ramadhan kutoka NBC.









Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule (katikati walioketi) akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wateja na maofisa wa benki ya NBC wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya wateja wake jijini Dodoma. Hafla hiyo ilihusisha uwepo wa wateja na wadau mbalimbali wa benki hiyo wakiwemo viongozi wa serikali na dini. Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Fedha wa NBC, Rayson Foya, Mkuu wa Benki ya NBC Kanda ya Pwani Bi Zubeider Haroun (kulia walioketi) na kulia kwake ni Mkuu wa Kanda ya Kati wa benki ya NBC, Bw Miraji Msuya na Mwakilishi wa Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Sheikh Ahmed Saidi (kushoto walioketi)


Top News