

Na Farida Mangube Morogoro
Wakazi wa Kitongoji cha Kichangani, Kijiji cha Mamboya katika Kata ya Gairo, Wilaya ya Gairo, wameondokana na changamoto ya muda mrefu ya mafuriko na kukatika kwa mawasiliano baada ya kukamilika kwa mradi wa ujenzi wa daraja na mtaro wa maji wenye thamani ya zaidi ya Shilingi milioni 455.
Mradi huo uliotekelezwa na wakala ya Barabara za vijjini na mjini TARURA umezinduliwa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2026, Ndugu Wazo Michael Mwang’onda, umeleta matumaini mapya kwa wakazi wa Kata hiyo waliokuwa wakikabiliwa na adha ya mafuriko yaliyokuwa yanakatiza mawasiliano na kuathiri shughuli mbalimbali za kijamii na kiuchumi, hususani wakati wa masika.
Akisoma taarifa ya Mradi kwa mkimbiza Mwenge wa Uhuru kitaifa Mhandisi Happnes Mbuge kutoka TARURA WIlaya ya Gairo amesema mradi huo umehusisha ujenzi wa daraja moja, mtaro wa maji wenye urefu wa mita 330 pamoja na gabioni za kuimarisha kingo za mtaro.
Akizungumza mara baada ya kukagua na kulidhishwa na mradi huo kiongozi wa Mbio za Mwenge wa uhuru kitaifa Ndugu Wazo Michael Mwang’onda amesema mradi huo ni sehemu ya jitihada za kuhakikisha wananchi wanapata miundombinu bora inayowezesha maendeleo na kuboresha maisha yao.
“Mwenge wa Uhuru umejionea kazi kubwa iliyofanyika hapa Kichangani. Huu ni mradi wenye manufaa makubwa kwa wananchi kwa kuwa umeondoa changamoto ya mafuriko na kukatika kwa mawasiliano iliyokuwa ikikwamisha shughuli za maendeleo katika eneo hili. Tunawapongeza wote walioshiriki kufanikisha utekelezaji wake,” alisema Mwang’onda.
Ameongeza kuwa maendeleo ya kweli hujengwa kupitia miradi inayogusa maisha ya wananchi moja kwa moja, huku akisisitiza umuhimu wa wananchi kuendelea kuilinda na kuitunza miundombinu hiyo ili iweze kudumu kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.
“Tunapozindua mradi kama huu tunatarajia kuona ongezeko la shughuli za kiuchumi, urahisi wa upatikanaji wa huduma za kijamii na maendeleo ya wananchi kwa ujumla. Jukumu la kuutunza sasa ni la wananchi wenyewe,” alisema.
Mhandisi Simon Masala ni Meneja wa TARURA Wilaya ya Gairo amesema Mradi huo unatarajiwa kuongeza usalama wa makazi ya wananchi, kuboresha huduma za usafiri na usafirishaji, kurahisisha upatikanaji wa huduma za kijamii na kuchochea ukuaji wa shughuli za kiuchumi katika Kitongoji cha Kichangani, Kijiji cha Mamboya na Wilaya ya Gairo kwa ujumla.
Kwa upande wao, wananchi wa Kichangani wameeleza furaha yao baada ya kukamilika kwa mradi huo wakisema umemaliza tatizo ambalo kwa miaka mingi lilikuwa likiwasababishia hasara na usumbufu mkubwa.
Othuma Yusuf ni Mmoja wa wakazi wa Kata hiyo amesema kabla ya ujenzi wa daraja na mtaro huo, mafuriko yalikuwa yakikatiza mawasiliano kati ya Kichangani na maeneo mengine ya Wilaya ya Gairo, hali iliyokuwa ikiathiri biashara, elimu na huduma za afya.
“Tulikuwa tunapata shida kubwa sana wakati wa mvua. Maji yalifurika na kufanya usafiri kuwa mgumu au kukatika kabisa. Wakulima walishindwa kusafirisha mazao yao kwenda sokoni, wafanyabiashara walikosa wateja na hata wagonjwa walipata changamoto ya kufikishwa hospitali kwa wakati. Kwa kweli tulikuwa tunaumia sana,” alisema Othuma.
Naye Jane Joseph amesema changamoto hiyo ilikuwa ikisababisha wananchi wengi kupoteza fursa za kiuchumi kutokana na kushindwa kufikia masoko na maeneo ya biashara kwa wakati.
“Kipindi cha masika kilikuwa kigumu sana kwetu. Wakati mwingine mazao yaliharibika kwa kuchelewa kufikishwa sokoni na biashara nyingi zilisimama kwa sababu ya kukosekana kwa mawasiliano ya uhakika. Mradi huu umetufungua njia mpya ya maendeleo na tunaamini utaongeza kipato cha wananchi wengi,” alisema Jane.
Aliongeza kuwa pamoja na kuimarisha shughuli za kiuchumi, daraja hilo litasaidia wanafunzi kufika shule kwa urahisi na wananchi kupata huduma za afya bila vikwazo vinavyotokana na mafuriko.
Wananchi hao walitoa shukrani kwa Serikali kwa kupeleka fedha zilizowezesha utekelezaji wa mradi huo, wakisema umekuwa mkombozi mkubwa kwa jamii ya Kichangani na maeneo jirani.
Na Diana Byera.
Vijana wa timu 20 wanaotokea Tarafa ya Kamachumu, wilayani Muleba mkoani Kagera, wanatarajia kushindania jumla ya shilingi milioni 6 kupitia mashindano ya Kamachumu Paul Mwijage Cup ambayo yatatimua vumbi kuanzia Juni 10 hadi Julai 15 mwaka huu.
Mkurugenzi wa mashindano hayo, Paul Mwijage, alisema kuwa katika kuhakikisha anaunga mkono serikali katika masuala ya kuibua vipaji vya vijana kupitia michezo, ameamua kuanzisha mashindano hayo ambayo yanalenga kuibua vipaji, kuimarisha mshikamano na kukutanisha vijana pamoja kwa ajili ya agenda zao za michezo.
Alisema kuwa mshindi wa kwanza atajinyakulia shilingi milioni 3, mshindi wa pili milioni 2 na mshindi wa tatu shilingi milioni 1, Pia vifaa vya michezo kama mipira na jezi vitatolewa kwa kila timu, ambapo ameahidi kuwa ligi hiyo itaendelea kuibua vipaji kwa miaka 10 mfululizo.
Ametoa wito kwa wawekezaji kuwekeza katika viwanja kwani tarafa hiyo inakabiliwa na changamoto ya uwanja. Hivyo, anaamini mashindano hayo yatawavutia wawekezaji mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi wanaozaliwa katika wilaya ya Muleba na nje ya wilaya hiyo.
“Mashindano haya ni kivutio kikubwa cha uwekezaji, Wakati mashindano yanaendelea, tunapaswa kuwa na sehemu za migahawa mizuri, tunapaswa kuwa na sehemu za kulala nzuri, chakula, na kutangaza utamaduni wetu na asili zetu kupitia mashindano haya, Ni muda sasa wa wadau wa michezo, wazaliwa wa Wilaya ya Muleba na wakazi wa Mkoa wa Kagera, kuunganisha nguvu na kudumisha michezo katika ukanda huu na kufanya uwekezaji pia”.
Katika uzinduzi wa ligi hiyo, mgeni rasmi alikuwa msemaji wa Timu ya Simba Sports Club, Ahmed Ally, ambaye amesema kuna umuhimu mkubwa mno wa kuanzisha mashindano mengi ngazi ya kata, tarafa na wilaya ili kuibua vipaji vya kweli kutoka maeneo mbalimbali nchini.
Alisema moja ya mambo yanayoweza kuleta radha mpya katika ligi za ndani nchini na nje ya nchi ni kuhakikisha vijana wanajitokeza kwa wingi wakati mashindano haya yanapotangazwa ili kuonyesha vipaji vyao, na kwa namna hiyo watajikuta wanajulikana katika timu mbalimbali zinazoshiriki Ligi Kuu.
Alitoa wito kwa washiriki kuhakikisha wanaonyesha vipaji na kucheza kwa moyo ili waweze kupata muunganisho wa kuendeleza vipaji vyao na kujipatia kipato.
Mechi ya ufunguzi wa mashindano hayo imezishirikisha timu za Kamachumu Stars na Bulembo katika viwanja vya Kamachumu, ambapo timu ya Bulembo imeshinda kwa mikwaju ya penalti na kujinyakulia medali na shilingi 500,000 kama sehemu ya ufunguzi wa michuano hiyo.

NA Mwandsihi Wetu – Chato
Wataalamu kutoka katika Sekta zinazotekeleza Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP ) inayoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na wenye Ulemavu wamekutana Mjini Chato Mkoani Geita tarehe 8 Juni 2026 kwa lengo la kufanyia mapitio mpango kazi wa Programu hiyo.
Akizungumza katika ufunguzi wa kikao kazi hicho, Mhandisi Enock Nyanda, Mkurugenzi Msaidizi sehemu ya Sekta za Uchumi na Uzalishaji Idara ya Tawala za Mikoa Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI alisema lengo la wataalam hao kukutana ni sehemu ya utekelezaji wa maagizo ya kikao cha Mawaziri kilichofanyika mapema mwezi Mei mwaka huu.

Aidha timu hiyo ya wataalam pia itaandaa shughuli zitakazotekelezwa na program kwa mwaka 2027 ilikuweza kufikia malengo pamoja na kutembelea maeneo ya utekelezaji wa Mradi ya Rubambagwe Wilayani Chato pamoja na Kilimi Wilayani Nzega Mkoani Tabora.

Sekta zinazotekeleza Progreamu ya kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) ni Pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Wizara ya Kilimo, Shirika la Uvuvi nchini TAFICO, Shirika la Uvuvi Zanzibar ZAFICO, Wizara ya uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar, Wakala wa Mbegu Nchini ASA, Taasisi ya Uthibiti wa Ubora wa Mbengu Nchini TOSCI na Taasisi ya utafiti wa Mbegu za Kilimo Nchini TARI
-Asisitiza Tsh Trilioni 1.2 zimewekezwa Kilimanjaro, sasa ni zamu ya mfumo wa Usambazaji.
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Baraa, Stephen Wasira, ameiagiza Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Same (SAUWASA) kuhakikisha inatatua kwa haraka changamoto ya upatikanaji maji inayowakabili wananchi wa mji wa Same.
Wasira alitoa agizo hilo leo Juni 8, 2026 alipokuwa akizungumza na wanachama wa CCM wa Shina Namba 9, Tawi la Same, Kata ya Same, wilayani Same mkoani Kilimanjaro.
Akijibu malalamiko ya wananchi kuhusu ukosefu wa maji, alisema haikubaliki kwa wakazi wa Same kuendelea kukosa huduma hiyo muhimu wakati maji yanapatikana kwa wingi kupitia miradi iliyotekelezwa na serikali.
“Ninaiagiza SAUWASA kuhakikisha wananchi wa Same wanapata maji. Haiwezekani watu wa Same waendelee kuyasikia au kuyaona maji bila kuyapata kwa matumizi yao ya kila siku, mfumo wa usambazaji uharakishwe ili wananchi wanufaike na huduma hiyo muhimu,” alisema Wasira.
Alibainisha kuwa, serikali imewekeza fedha nyingi kutekeleza mradi wa maji wa Same–Mwanga–Korogwe, hivyo hakuna sababu ya wananchi kuendelea kukosa huduma hiyo kutokana na changamoto za usambazaji.
NA MWANDISHI WETU
KAMATI ya Kudumu ya Bunge Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) imempongeza Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, kwa ujenzi wa shule za kisasa za ghorofa wilayani Ilala na kueleza kwa mara ya kwanza kamat hiyo imeshuhudia jengo la shule ya sekondari ya kata yenye lifti.
Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa kamati hiyo Florent Kyombo, katika ziara ya wajumbe wa kamati hiyo kukagua miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaa, hususan ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Bonyokwa itakayo chukua wanafunzi wa kidato cha tano na sita.
Kyombo amesema kamati yake imezunguka mikoa mingi Tanzania lakini haijawahi kukutana na jengo la shule lenye hadhi kama hilo la Shule ya Sekondari Bonyokwa lenye lifti.
"Jiji la Dar es Salaam wameupiga mwingi. Msione vinaelea viumeundwa. Tumezunguka mikoa mingi lakini hatujakutana na jengo lenye hadhi kama hii,"ameeleza Mbunge Kyombo.
Amesema kamati hiyo inamshukuru Rais Dk. Samia, kwa uwekezaji mkubwa katika sekta ya elimu hususan ujenzi wa shule za ghorofa ambao utaondoa adha kwa wanafunzi.
"Kamati inawaomba wanafunzi kumlipa Rais Dk. Samia, kwa kufanya vizuri darasani na kutunza mundombinu hii,"amebainisha Kyombo.
Ameongeza licha ya kutembelea na kukagua jengo hilo la shule lakini maelezo ya awali ya viongozi wa wilaya ya Ilala na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam yanadhihirisha ujenzi wa majengo mengi ya ghorofa hivyo kupongeza viongozi kwa utekelezaji wa miradi hiyo .
Hata hivyo kamati hiyo ilielekeza halmashauri hiyo kuboresha majengo ya Shule ya Msingi Bonyokwa na Shule ya Sekondari Bonyokwa ya kiadato cha kwanza na cha nne, yawiane kidogo na hadhi ya jengo hilo la kissa.
Mbali na mradi huo, kamati hiyo mekagua ujenzi wa Barabara ya Kwa mpalange (Buza) Temeke-Kitunda unaogharimu kilometa 6.2, ujenzi wa Kituo cha Afya Mchikichini unaotekelezwa katika Kata ya Mchikichini unaogharimu sh. bilioni 7.4.
Awali Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo, alimshukuru Rais Dk. Samia, kwa kuelekeza fedha nyingi za miradi wilayani humo na kwamba wataendelea kusimamia kikamilifu kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati
Mpogolo, ameeleza ujenzi wa shule za ghorofa ni mkakati uliwekwa kuelekea utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na kusimamia maono ya Rais Dk. Samia, wanafunzi wanasoma katika mazingira rafiki.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam,Elihuruma Mabelya, amesema katika mwaka wa fedha 2026-27 wametenga sh. bilioni 19 kuboresha mundombinu ya elimu.
Mabelya amesema mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari Bonyokwa umegharimu sh. bilioni 2.07 na ina madarasa 20, matundu ya vyoo 45 yakijumuisha matundu ya vyoo vya kawaida 30, matundu ya watu wennye mahitaji maalum 10, sehemu za kujisaidia haja ndogo tano kwa wavulana, vyumba vitano maaluma kwa wasichana vyenye choo ndani yake
"Shule hii inatarajia kuchukua wanafunzi 1400 mwaka 2026/27 na mwaka mwaka 2028 shule itachukua wanafunzi 3100,"amesema Mabelya.
Mbali na jengo la Shule ya Sekondari Bonyokwa kuwa na lifti shule nyingine ambayo jengo lake lina lifti wilayani humo ni Shule ya Sekondari Kipunguni B.
Wanafunzi wanaojiandaa kushiriki mashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma kwa Shule za Sekondari Tanzania (UMMISETA) ngazi ya mkoa wamepata hamasa mpya baada ya kupokea vifaa vya michezo vilivyotolewa na Mbunge wa Jimbo la Mtumba, Anthony Peter Mavunde.
Vifaa hivyo vilikabidhiwa katika Shule ya Sekondari Dodoma kwa niaba ya Mbunge huyo kupitia Katibu wake, Silas Makanyaga, ambae alisema kuwa Jiji la Dodoma kupitia Ofisi ya Afisa Elimu Sekondari liliwasilisha ombi la vifaa vya michezo kwa ajili ya mashindano ya UMMISETA ngazi ya wilaya na mkoa, ambapo Mbunge amejitoa kusaidia kwa kununua jezi kwa kila mchezo.
“Tunawaomba vijana wetu kucheza kwa nidhamu, kuwasikiliza walimu wao na kuendelea kufanya vizuri kama ilivyo desturi ya Jiji la Dodoma ambalo limeendelea kuwa kinara kwa ushindi wa makombe mbalimbali” alisema Makanyaga.
Kwa upande, Afisa Elimu Sekondari Jiji la Dodoma, Mwl. Daniel Mapilya alisema kuwa tayari wanafunzi 120 kutoka shule mbalimbali za sekondari wamewasili kambini tangu Juni 5 kwa ajili ya maandalizi ya mashindano ya ngazi ya mkoa yaliyotarajiwa kuanza rasmi Juni 8.
Sambamba na hilo, Afisa Michezo wa Jiji la Dodoma, Peter Ititi alisema kuwa vifaa vilivyotolewa vimeongeza morali na hamasa kwa wanamichezo, akibainisha kuwa kwa miaka minne mfululizo mbunge huyo amekuwa akiwaunga mkono kwa kutoa vifaa vya michezo jambo lililosaidia kuongeza ushindani na mafanikio.
Nae, mchezaji wa mchezo wa kurusha tufe na Mpira wa Pete, Munira Mohamed alisema kuwa vifaa walivyopokea kutoka kwa mbunge vimeongeza hamasa na kuwapa nguvu ya kupambana kwa ushindi.
Hata hivyo, Nahodha wa timu ya mpira wa miguu, Gabriel Peter alisema kuwa timu ipo katika maandalizi mazuri na watapeperusha vizuri bendera ya Jiji la Dodoma kwa kurudi na ushindi mnono wa makombe kama zawadi ya shukurani kwa mbunge.
Mashindano ya UMISETA ngazi ya mkoa kwa Jiji la Dodoma yanashirikisha michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu (football), mpira wa pete (Netball), mpira wa kikapu (Basketball), mpira wa mikono (Handball), mpira wa wavu (Volleyball), riadha, sanaa za ndani, muziki wa kizazi kipya, tenisi ya mezani (Table Tennis), Goalball, kwaya na ngoma za asili.



.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)




.jpeg)



.jpeg)
.jpeg)








.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)






.jpeg)





