Serikali Yachochea Ujenzi wa Soko Kubwa la Mazao ya Misitu Mafinga Kukuza Biashara na Kuvutia Wanunuzi wa Kimataifa
Serikali imeeleza kuwa inaendelea na jitihada za kuratibu uanzishwaji wa soko kubwa la mazao ya misitu katika eneo la Mafinga, mkoani Iringa, kwa lengo la kuboresha mfumo wa biashara ya mazao hayo na kuwezesha wanunuzi wa ndani na nje ya nchi kupata bidhaa katika eneo maalumu badala ya kununua moja kwa moja kutoka kwa wakulima vijijini.
Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Mafinga Mjini, Mhe. Dickson Nathan Lutevele, ambaye alitaka kufahamu mpango wa Serikali wa kujenga soko kubwa la mazao ya misitu katika eneo hilo.
Akijibu swali hilo, Mhe. Chande amesema Wizara ya Maliasili na Utalii imekuwa ikiratibu vikao mbalimbali vya wadau vinavyowakutanisha taasisi na mamlaka muhimu zikiwemo Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Mamlaka ya Maeneo Maalum ya Uwekezaji kwa Mauzo ya Nje (EPZA), Taasisi ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade), Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi, Halmashauri ya Mji wa Mafinga, Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), pamoja na vyama vya wavunaji wa misitu na wadau wengine wa sekta hiyo.
Ameeleza kuwa kupitia vikao hivyo, wadau wamekuwa wakijadili masuala mbalimbali muhimu yatakayowezesha kuanzishwa kwa soko hilo, ikiwemo upatikanaji wa eneo litakalotumika, mfumo wa uendeshaji wa soko, ushiriki wa wadau mbalimbali na namna ya kupata rasilimali fedha kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo.
Naibu Waziri huyo amesema kuwa mpango wa kuanzisha soko kubwa la mazao ya misitu Mafinga ni sehemu ya mkakati mpana wa Serikali unaotekelezwa kwa ushirikiano kati ya Halmashauri husika na Wizara yenye dhamana ya Viwanda na Biashara.
Kutokana na hilo, amemshauri Mbunge wa Mafinga Mjini kuendelea kushirikiana na mamlaka za halmashauri husika katika hatua za kutafuta na kutenga eneo litakalotumika kwa ajili ya soko hilo.
Aidha, amesisitiza kuwa Wizara ya Maliasili na Utalii ipo tayari kuendelea kushirikiana na halmashauri, Wizara ya Viwanda na Biashara pamoja na wadau wa maendeleo ili kuhakikisha ndoto ya kuwa na soko kubwa la mazao ya misitu Mafinga inafanikishwa na kuleta manufaa kwa wakulima, wafanyabiashara na uchumi wa eneo hilo kwa ujumla.








.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)



.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)

.jpeg)

Na Mwandishi Wetu


.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)










