Taasisi ya LALJI FOUNDATION kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo Kigoma Hilltop Hotel, Ahlulybayt Academic Center, Vision 4 All Eye Centre pamoja na Supa Foam imeendesha kambi maalumu ya siku nne ya matibabu ya macho bure kwa wakazi wa mkoa wa Kigoma.

Kambi hiyo ilifanyika kuanzia tarehe 03 hadi 06 Aprili 2026 katika viwanja vya shule za Ahlulbayt Islamic Center Manispaa ya Kigoma Ujiji, ilitoa huduma mbalimbali muhimu ikiwemo uchunguzi wa macho, ushauri wa kitaalamu, utolewaji wa miwani, huduma za dawa pamoja na upasuaji wa mtoto wa jicho bila malipo.

Akizumza baada ya kukamilika kwa kambi hiyo mlezi wa Taasisi ya LALJI FOUNDATION Mohsen Lalji amesema Zaidi ya wananchi 6000 walijiotokeza kupata huduma ambapo watu 5079 walifanyiwa uchunguzi wa macho, 2218 walipatiwa miwani ya macho, 518 walifanyiwa upasuaji wa mtoto wa jicho na watu 3215 walipatiwa dawa za macho huku huduma zote zikitolewa bure bila malipo.

Amesema lengo la kambi hiyo ni kuunga mkono juhudi za serikali na kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na endelevu kwa wakati na ukaribu zaidi.

Akizindua rasmi kambi hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mh Balozi Simon Sirro aliipongeza LALJI FOUNDATION na washirika wake kwa jitihada hizo za kuwafikia wananchi na kuwapatia huduma muhimu za matibabu ya macho, hususan kwa wale wasio na uwezo wa kumudu gharama za matibabu.

Aidha, aliwataka wananchi kujitokeza kwa wingi ili kunufaika na huduma hizo, huku akisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya serikali na taasisi zisizo za kiserikali katika kuboresha huduma za kijamii na kutatua changamoto zinazowakabili wananchi.

Wakizungumza baada ya kupatiwa huduma, wananchi wengi walieleza kuwa walikuwa hawana uwezo wa kumudu gharama za matibabu ya macho, ikiwemo upasuaji na ununuzi wa miwani, hali iliyowafanya kuendelea kuishi na matatizo ya macho kwa muda mrefu.

Wananchi hao pia waliomba juhudi kama hizi ziendelee kudumishwa ili kuwasaidia watu wengi zaidi, hasa wale wa kipato cha chini ambao bado wanakabiliwa na changamoto ya kumudu gharama za huduma za afya.

Kambi hiyo imeelezwa kuwa ni sehemu ya juhudi za wadau wa maendeleo katika kuhakikisha jamii inapata huduma bora za matibabu ya macho hususan katika maeneo yenye uhitaji mkubwa kama Kigoma.




Baraza la Wafanyakazi la Nne la Tume ya Ushindani (FCC) limehitimisha kikao chake cha siku mbili kwa kuazimia kuunga mkono rasimu ya Mpango Mkakati Mpya wa Miaka Mitano 2026/27-2030/31 unaolenga kutekeleza moja kwa moja Dira ya Taifa ya 2050.

Kikao hicho kilichofanyika tarehe 9 na 10 Aprili, 2026 katika ukumbi wa Hoteli ya Sunset, Manispaa ya Morogoro kiliwakutanisha wajumbe wa Menejimenti na Wawakilishi wa Watumishi kujadili ajenda kuu mbili : Rasimu ya Mpango Mkakati na Rasimu ya Bajeti ya 2026/27

Akifunga baraza hilo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza Bi. Khadija Ngasongwa alisema Mpango Mkakati huo umeandaliwa kwa kuzingatia maono ya Dira ya 2050 ya kuwa na “Uchumi shindani, jumuishi na himilivu unaochochea ustawi wa Watanzania wote”

“Baraza la Wafanyakazi ni jukwaa muhimu la ushirikishwaji. Mpango Mkakati huu tuliojadili ni nyaraka muhimu inayoonesha ramani ya safari ya Tume na unaakisi dhamira yetu ya pamoja ya kuiunga mkono Dira ya 2050 kupitia soko huru, salama kwa mlaji na linalochochea ukuaji wa uchumi shindani ,” alisema Bi. Khadija

Kupitia Azimio la Baraza, watumishi wa FCC wamekubaliana kuunga mkono kikamilifu rasimu ya Mpango Mkakati huo na kushiriki katika utekelezaji wake utakaoanza tarehe 01 Julai, 2026. Maeneo yaliyopewa kipaumbele ni pamoja na kukuza ushindani huru na wa haki, kupambana na bidhaa bandia na kuimarisha ulinzi wa mlaji.

Baraza hilo ambalo hukutana mara mbili kwa mwaka kwa mujibu wa sheria, limeelezwa kuwa chombo muhimu cha kuimarisha mshikamano, uwajibikaji na mawasiliano ya wazi kati ya Menejimenti na Watumishi.

“Kupitia mshikamano huu, tutaongeza ufanisi katika kusimamia ushindani wa haki na kulinda maslahi ya walaji kama sehemu ya mchango wa Tume katika kufanikisha Dira ya Taifa ya 2050,” ilisomeka sehemu ya azimio la baraza.

Uongozi wa Tume umedumisha utamaduni shirikishi katika kujadili masuala ya taasisi kimkakati. Watumishi wote hushirikishwa kupitia ngazi mbalimbali ndani ya Tume kabla ya rasimu kuidhinishwa na Bodi ya Tume ya Ushindani.

FCC itaendelea kuthamini mchango wa Baraza la Wafanyakazi katika maamuzi ya kimkakati sambamba na azma ya kujenga mazingira bora ya kazi na kutoa huduma bora kwa umma.





















Leo tarehe 13 Aprili saa 22:00, Uwanja wa Old Trafford utakuwa mwenyeji wa pambano la Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) kati ya Manchester United na Leeds United. Mechi hii inajulikana kwa jina la "War of the Roses" kutokana na uhasama wa kihistoria kati ya mikoa ya Lancashire (Manchester) na Yorkshire (Leeds).

Kwenye msimamo, Manchester United wako nafasi ya 3 wakiwa na pointi 55 baada ya mechi 31, wakiwa na rekodi ya ushindi 15, sare 10 na kupoteza 6 . Kwa upande wa Leeds United, wako nafasi ya 15 wakiwa na pointi 33 baada ya mechi 31, wakiwa na ushindi 7, sare 12 na kushindwa 12 .

Hii ni mechi muhimu kwa United kujiimarisha kwenye nafasi ya kuwania Kombe la Ulaya, na kwa Leeds ni muhimu kukimbia eneo la kushuka daraja kwani wana pointi 3 tu juu ya Tottenham iliyopo nafasi ya 17 .

Mechi hii itasimamiwa na mwamuzi mkuu Paul Tierney anajulikana kuwa mwamuzi mkali, na kwa kuzingatia umuhimu wa mechi hii, nidhamu itakuwa muhimu sana.
a
Kwa upande wa Manchester United, kocha Michael Carrick ndiye anayeongoza timu. Carrick ameweza kujenga timu yenye nguvu ya kushambulia kwa njia mbalimbali. Wachezaji hatari wa United ni pamoja na Benjamin Sesko (mshambuliaji), Bryan Mbeumo (winga), na Bruno Fernandes (kiungo mshambuliaji) . United wana nguvu kubwa katika kuunda nafasi za kufunga, kushambulia kwa mbavu, na kumaliza nafasi .

Kwa upande wa Leeds United, kocha Daniel Farke ndiye anayeongoza. Leeds wana nguvu katika mikondo ya adhabu za moja kwa moja (direct free kicks) na mashambulizi ya mpira wa kona . Wachezaji hatari ni pamoja na Dominic Calvert-Lewin (mshambuliaji) aliye katika kiwango kizuri baada ya kufunga kwenye michezo ya kombe .

Ingia kwenye kasi ya kujishindia pesa kwenye michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Manchester United wamepokea habari njema ya kurudi kwa Lisandro Martinez ambaye amekosa mechi 5 za mwisho kutokana na jeraha na anatarajiwa kucheza leo . Hii ni nyongeza muhimu hasa akizingatiwa kuwa Harry Maguire hayupo kwa sababu ya kusimikwa kwa kadi nyekundu aliyopata dhidi ya Bournemouth .

Majeruhi wengine wa United ni Matthijs De Ligt (mgongo) ambaye hajacheza tangu Novemba, na Patrick Dorgu (hamstring) ambaye bado hajajiandaa kikamilifu . Benjamin Sesko na Bryan Mbeumo wanatarajiwa kuwa fiti licha ya kukosa mazoezi

Kwa upande wa Leeds, wana wasiwasi wa majeruhi wakiwemo Anton Stach (kiungo) anayekisiwa kuwa na jeraha la ligament kwenye kifundo cha mguu, na Joe Rodon (beki) aliyeumia kwa kuanguka vibaya . Pia, Daniel James anatarajiwa kukosa kutokana na jeraha la adductor . jisajili sasa

Kihistoria, timu hizi zimekutana mara 117, huku Manchester United ikishinda mara 52, Leeds mara 26, na sare 39 . Walipo kutana mwanzoni mwa msimu huu (Januari 2026) ulimalizika kwa sare ya 1-1 kwenye Dimba la Elland Road. United wamekuwa wakitawala kwenye michezo ya hivi karibuni, huku Leeds wakishindwa kufunga katika mechi zao 4 za mwisho za ligi .


Bahati imekuwa ikicheza mchezo wa kujificha, lakini sasa Meridianbet wameleta Leprechaun Wish, mchezo wa sloti unaomlipa kila mtu anayecheza. Hii sio sloti ya kawaida, ni safari ya kwenda Ireland kwenye milima ya kijani kibichi, sarafu za kuvutia, karafuu zilizojaa bahati na kofia za kichawi. Ukicheza, unahisi kama uko kwenye hadithi halisi za Irish.

Kila raundi ina msisimko, maana ndani ya mchezo kuna chungu cha dhahabu kinachokupa scatter, sarafu na alama zingine za kushangaza. Mistari 20 ya kubashiri inakuwezesha kucheza kwa mtindo yako, ukijua kila mchezo unaweza kuleta jackpot. Hapa, hakuna mtu anayechelewa, kila dakika ni nafasi ya kushinda pesa halisi.

Meridianbet wanakupa jukwaa pana la kubashiri, mechi kali za kimataifa hadi michezo ya kasino mtandaoni iliyojaa burudani. Ukiwa na odds zenye ushindani mkubwa, kila tiketi inakuwa na thamani zaidi. Jiunge sasa kupitia tovuti yao au piga *149*10#.

Na kwa wale wanaopenda mambo ya haraka, kuna kipengele cha kununua bonasi. Hii inakupa nguvu ya kuingia moja kwa moja kwenye mchezo wa ushindi. Sasa si lazima usubiri, unaweza kujaribu kila njia na kujaribu bahati yako mara moja. Hii ni nafasi ya kujaribu ushindi mkubwa.

Huu mchezo siyo tu cheza cheza, ni stori ya kushinda, kusherehekea na kujaribu bahati yako. Ireland iko mkononi mwako, na pesa ziko karibu tu. Mchezo mmoja tu, na unaweza kuwa bosi.

Hivyo, usichelewe, ingia Meridianbet, cheza mizunguko yako kadhaa, ufurahie Leprechaun Wish huku bahati ikikufanyia kazi. Hii ni safari ya raha, msisimko na pesa, yote kwa upande wako.



Na Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, amesema kuwa ni jambo la kawaida kwa baadhi ya watu kupinga hatua za Serikali, hasa pale maamuzi hayo yanapogusa maslahi yao binafsi—hususan kwa wale waliokuwa wakinufaika kwa njia zisizo halali.

Akizungumza leo jijini Dodoma mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami ya Ntyuka–Mvumi–Kikombo yenye urefu wa kilomita 76, pamoja na kipande cha barabara ya Chololo–Mapinduzi (Makao Makuu ya TPDF) chenye kilomita 5, Dkt. Mwigulu alisema Serikali haitayumbishwa na kelele za wachache wanaopinga mabadiliko yenye manufaa kwa taifa.

Alieleza kuwa mara nyingi watu wanaoguswa na hatua hizo hujipanga kwa kuajiri wengine ili kuishambulia Serikali na viongozi wake kupitia mitandao au majukwaa mbalimbali ya kijamii.

“Watanzania msitishike na hao watu, kwa sababu wanafugwa huko waliko. Ili mikataba yao iendelee, ni lazima waendelee kutukana,” alisisitiza.

Dkt. Mwigulu amesema kuwa mwenendo huo si wa sasa pekee, bali umekuwepo hata katika awamu zilizopita za uongozi, ambapo baadhi ya watu walikuwa wakitoa kauli za kejeli na mashambulizi dhidi ya viongozi wanaochukua hatua thabiti.

Aidha, amebainisha kuwa hata yeye binafsi amekuwa mhanga wa mashambulizi hayo, akifananisha hali hiyo na mapambano ya kiimani, ambapo wanaosimama kupinga maovu hukumbana na upinzani mkali.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewataka Watanzania kuendelea kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan, akisisitiza kuwa juhudi za Serikali ya awamu ya sita zinalenga kulinda rasilimali za taifa na kuhakikisha zinawanufaisha wananchi wote.

Amesisitiza kuwa miradi ya maendeleo kama ujenzi wa barabara hizo ni ushahidi wa dhamira ya dhati ya Serikali katika kuboresha miundombinu na kukuza uchumi wa nchi.





Na Mwandishi Wetu, Michuzi TV

BANK of Africa Tanzania imezindua programu ya masuluhisho na huduma mahususi za kifedha pamoja na ushauri kwa Wafanyabiashara Wadogo na wa Kati (SMEs), ikiwa ni jitihada za kuboresha upatikanaji wa mikopo, elimu ya biashara na kukuza ushindani wa biashara nchini.

Uzinduzi wa programu hiyo ulipongezwa na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Emmanuel Tutuba, aliyesema kuwa hatua hiyo inalenga kuboresha mahitaji ya kifedha ya wajasiriamali kupitia huduma, mikopo na elimu ya biashara.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi iliyofanyika katika Tawi la Lumumba jijini Dar es Salaam, Tutuba alisema tukio hilo linaashiria hatua muhimu katika kuimarisha masuluhisho ya kifedha kwa SMEs na kukuza sekta binafsi.

“Mpango huu unaonyesha mabadiliko chanya katika sekta ya benki, kutoka mfumo wa ukopeshaji wa jumla kwenda kwenye huduma jumuishi za kifedha zinazolenga mahitaji maalum ya wateja,” alisema.

Aliongeza kuwa SMEs ni uti wa mgongo wa uchumi wa Tanzania, zikichangia takribani asilimia 95 ya biashara zote na asilimia 35 ya Pato la Taifa (GDP), huku zikitoa ajira kwa zaidi ya watu milioni tano.

Aidha, alisema mpango huo unaendana na Mkakati wa Taifa wa Huduma Jumuishi za Fedha (2023–2028) unaolenga kuhakikisha Watanzania wanapata huduma za kifedha nafuu na za kuaminika. Alitaja makundi ya kipaumbele kuwa ni pamoja na wanawake, vijana, watu wenye ulemavu, wakulima na wavuvi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Bank of Africa Tanzania, Esther Cecil Maruma, alisema mkakati huo umejengwa katika uelewa wa kina wa mahitaji ya SMEs.

“Tunataka kuwezesha biashara kukua kwa kasi, kushindana vyema na kudumu kwa muda mrefu kupitia masuluhisho yanayojibu changamoto zao moja kwa moja,” alisema.

Alieleza kuwa huduma mpya zilizozinduliwa ni pamoja na ufadhili wa ankara (invoice discounting), overdraft, mikopo ya muda mfupi na mrefu, ufadhili wa mali na magari, dhamana, pamoja na huduma za biashara za kimataifa.

Maruma alisisitiza kuwa benki inalenga kuwa mshirika wa kweli wa ukuaji wa biashara, si mtoaji wa mikopo pekee.

Naibu Mkurugenzi Mtendaji – Biashara, Hamza Cherkaoui, alisema wameboresha huduma ili ziwe rahisi, zenye unyumbufu na zinazoendana na mahitaji halisi ya biashara.

Naye Mjumbe wa Bodi, Waziri Kindamba, aliipongeza benki hiyo kwa ubunifu huo unaolenga kutatua changamoto za wajasiriamali.

Kwa upande wake, mteja wa muda mrefu wa benki hiyo, Mohammed Bahasawan, alisema mpango huo ni fursa muhimu kwa wafanyabiashara kukuza mitaji na biashara zao.

“Nimekuwa mteja wa benki hii kwa miaka mingi, na ninaamini huu ni mwanzo wa suluhisho la changamoto nyingi za wajasiriamali nchini,” alisema.
Gavana wa Benki kuu ya Tanzania (BOT), Emmanuel Tutuba (katikati), akikata utepe kuzindua Programu ya masuluhisho na huduma mahususi za kifedha na ushauri kwa wafanyabiashara wa kati na wadogo (SMEs)wa Bank of Africa, jijini Dar es Salaam juzi. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji - Bank of Africa, Esther Cecil Maruma, Mjumbe wa Bodi - Bank of Africa - Mkurugenzi, Waziri Kindamba (kulia), Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Biashara wa benki hiyo, Hamza Cherkaoui (kushoto) na Naibu Mkurugenzi Mtendaji Uendeshaji wa Bank of Africa, Wasia Mushi.
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha SME wa Bank of Africa, Beatrice Richard, akielezea jambo kwa Mgeni rasimi, Gavana wa Emmanuel Tutupa na Viongozi wa benki hiyo, alipotembelea eneo jipya maalum kwa wateja wa SME wakati wa uzinduzi juzi.
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Emmanuel Tutupa na Mjumbe wa Bodi wa Bank of Africa, Waziri Kindamba na Mkurugenzi Mtendaji - Bank of Africa, Esther Cecil Maruma (kulia walio kaa) wakiwa katika picha ya pamoja na wateja wa benki hiyo, wakati wa uzinduzi wa masuluhisho na huduma mahususi za kifedha na ushauri kwa Wafanyabiashara Wadogo na wa Kati (SMEs).
Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro, amekutana na Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kiarabu ya Sahara (SADR), Mhe. Brahim Ghali. Katika mazungumzo hayo, aliwasilisha salaam za Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Mazungumzo hayo yalifanyika tarehe 9 Aprili 2026 katika makazi rasmi ya Mhe. Ghali, Kambi ya Ausserd, Tindouf, Algeria. Balozi Migiro alisisitiza kuwa msimamo wa Tanzania na CCM wa kuunga mkono haki ya watu wa Saharawi kujitawala ni wa muda mrefu. Alieleza kuwa msingi wake uliwekwa tangu enzi za Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere.

Kwa upande wake, Mhe. Ghali alimshukuru Rais Dkt. Samia kwa salaam na kwa kutuma uwakilishi kwenye maadhimisho ya miaka 50 ya SADR yaliyofanyika tarehe 8 Aprili 2026 katika Kambi ya Ausserd. Pia aliomba salamu zake zifikishwe kwa Rais, CCM na Watanzania.

Aliongeza kuwa watu wa Saharawi wanathamini mchango wa Mwalimu Nyerere katika kuhamasisha mshikamano wa Afrika na dunia. Alisema mshikamano huo umeendelea kuimarisha harakati za SADR, chini ya uongozi wa Chama cha Polisario, katika kudai haki ya kujitawala.





NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

Waziri wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga, amesema Serikali itaendelea kuweka mazingira rafiki kwa wanawake wajasiriamali kwa kuwaondolea vikwazo na kurahisisha taratibu za urasimishaji wa biashara ili waweze kushiriki kikamilifu katika uchumi wa taifa.

Dkt. Kapinga ameyasema hayo leo Aprili 12, 2026 Jijini Dar es Salaam wakati akizungumza katika Maadhimisho ya Women In Balance Kitchen Party Gala 2026, akieleza kufurahishwa kwake kushiriki kwa mara ya kwanza katika jukwaa hilo linalowaunganisha wanawake wajasiriamali kutoka ngazi mbalimbali.

Amebainisha kuwa jukwaa hilo limekuwa na mchango mkubwa kwa zaidi ya miaka 16 kwa kuwaunganisha wanawake wenye mitaji midogo, ya kati na hata wanaojihusisha na biashara za ndani na nje ya nchi, hali inayochochea maendeleo yao kijamii na kiuchumi.

“Jukwaa hili ni muhimu sana kwa maendeleo ya wanawake kijamii na kiuchumi. Limekuwa mstari wa mbele katika kuwaunganisha na kuwawezesha wanawake kuinuana,” amesema Waziri Kapinga.

Akizungumzia changamoto zinazowakabili wanawake, Waziri Kapinga amesema bado wapo wanaohofia kurasimisha biashara zao kutokana na mtazamo wa ugumu wa taratibu. Hata hivyo, alisisitiza kuwa Serikali imebadili mwelekeo na sasa inalenga kuwawezesha wafanyabiashara badala ya kuwaadhibu.

“Zama za kufungia biashara zimekwisha. Tukimkuta mama anafanya biashara bila leseni, tutamwelekeza na kumsaidia kupata vibali vinavyohitajika. Lengo letu ni kuwawezesha, si kuwaadhibu,” amesisitiza.

Aidha, ameeleza kuwa Serikali inaendelea kuboresha utoaji wa huduma kwa kusogeza karibu taasisi zinazohusika na biashara, hatua inayolenga kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa wafanyabiashara, hususan wanawake na vijana.

Katika hatua nyingine, Waziri Kapinga amewahimiza wanawake kuchangamkia fursa zilizopo katika sekta ya viwanda vidogo, vya kati na vikubwa, akisisitiza kuwa wao ni sehemu muhimu ya utekelezaji wa maono ya taifa ya kujenga uchumi imara.

Ameongeza kuwa sekta binafsi ina mchango mkubwa katika ukuaji wa uchumi, huku akiwahamasisha wanawake kuwa mstari wa mbele katika biashara na uwekezaji.

“Wanawake ni jeshi kubwa. Tukiamua, tunaweza. Mafanikio ya mwanamke yako mikononi mwake kupitia ushirikiano na kujituma,” amesema.

Aidha, amepongeza waandaaji wa jukwaa hilo kwa kuendelea kuwa chachu ya kuwawezesha wanawake kiuchumi na kijamii, na kuahidi kuwa Serikali itaendelea kushirikiana nao katika juhudi za kuinua wanawake.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Women In Balance Kitchen Party Gala 2026Vida Nasari, amesema washiriki 200 walihudhuria tukio hilo na wengi wao ni wanawake wenye ushawishi katika jamii.

Amesema washiriki hao wako tayari kushirikiana na taasisi zilizo chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara, ikiwemo BRELASIDOTANTRADECBETBS na FCC, ili kupata elimu na taarifa sahihi zitakazowawezesha kusonga mbele.

Amesisitiza kuwa ushirikiano huo utakuwa mwanzo wa safari ya kuwajengea wanawake uwezo zaidi kiuchumi na kijamii.















Top News