Asema nchi ina usalama mkubwa wa mafuta hivyo wananchi waendelee kupata huduma muda wote
Timu maalum kuundwa kufuatilia uingizaji wa mafuta nchini
MichuziBlogV2
Most read Swahili blog on earth
Bonyeza play kuangalia Michuzi TV LiVE
BONYEZA PLAY KUANGALIA AZAM TV LIVE
BONYEZA KUANGALIA CHANNEL TEN LIVE
Asema nchi ina usalama mkubwa wa mafuta hivyo wananchi waendelee kupata huduma muda wote
Timu maalum kuundwa kufuatilia uingizaji wa mafuta nchini.jpeg)

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Dkt. Jim Yonazi amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) Dkt. Adam Joseph Mrisho ambaye amefika kujitambulisha baada ya kuteuliwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kikao hicho kimefanyika tarehe 23 Machi, 2026 katika Ofisi ya Waziri Mkuu iliyopo mtaa wa Reli jijini Dodoma na kudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) Dkt. James Kilabuko pamoja na Mratibu wa Masuala ya UKIMWI Bi. Adela Mpina.
Dkt.Yonazi ameahidi kumpa ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu yake ya kila siku. (PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU).
Benki ya NMB imetwaa tuzo tatu katika Tuzo za Euromoney Private Banking 2026 jijini London, ikishinda Benki Bora ya Huduma za Wateja Maalum Tanzania, Benki Salama Zaidi ya Huduma za Wateja Maalum na Benki Bora kwa Uendelevu Tanzania.
Ushindi huo unazidi kuakisi uimara wa benki ya NMB yenye matawi 241 nchini na zaidi ya mawakala 73,000 pamoja na wateja zaidi ya 9.9 millioni, katika kutoa huduma mahususi kwa wateja, kuimarisha usalama wa fedha na kuongoza katika utekelezaji wa mikakati ya fedha endelevu.
Mafanikio haya yanaendelea kuimarisha nafasi ya Benki ya NMB kama kinara wa ubunifu na mshirika wa maendeleo ya uchumi Tanzania.
SERIKALI imetangaza mpango wa kuongeza ndege nane kwa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), hatua itakayofikisha jumla ya ndege 24 ifikapo mwaka 2030, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha usafiri wa anga na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa.
Taarifa hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Uchukuzi, David Kihenzile, kwa niaba ya Waziri wa Uchukuzi, alipokuwa akizungumza na watumishi wa ATCL katika miji ya Cape Town na Johannesburg nchini Afrika Kusini, ambapo ameelezea kuwa shirika hilo lilianza na ndege moja mwaka 2016 na sasa lina ndege 16
Aidha, katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, serikali imeongeza ndege sita kubwa, kwa lengo la muda mfupi ni kufikia ndege 19 ndani ya mwaka wa fedha 2025/2026, kabla ya kufikia ndege 24 ifikapo mwaka 2030.
Ongezeko hilo la ndege limewezesha kupanuka kwa mtandao wa safari za ndani, ambapo kwa sasa ATCL inahudumia miji mbalimbali ikiwemo Dar es Salaam, Dodoma, Mwanza, Kilimanjaro, Arusha, Mbeya, Mtwara, Kigoma, Iringa, Pemba, Unguja, Songea, Mpanda, Tabora na Bukoba. Aidha, mipango ipo ya kuanza safari katika miji ya Sumbawanga, Musoma na Shinyanga hivi karibuni.
Katika ngazi ya kimataifa na kikanda, shirika hilo linaendesha safari zake katika miji ya Nairobi, Entebbe, Bujumbura, Lubumbashi, Lusaka, Harare, Johannesburg, Guangzhou (China), Mumbai (India) na Dubai, pamoja na huduma za usafirishaji mizigo (cargo) zinazochangia kukuza biashara na uchumi wa taifa.
Katika hotuba yake, Kihenzile amewahimiza watumishi wa ATCL kuendelea kufanya kazi kwa weledi, nidhamu na uwajibikaji kwa manufaa ya taifa.
Kwa upande wake, Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, James Bwana, amebainisha kuwa uwepo wa ATCL katika miji ya Johannesburg na Cape Town unachochea ukuaji wa biashara kati ya Tanzania na Afrika Kusini.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM
TAASISI ya Help to Help East Africa imeendesha mafunzo ya siku 14 kwa wasichana 150 kutoka mikoa 20 nchini, ikiwa na lengo la kuwawezesha kupata ujuzi wa matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) ili kuongeza ushindani wao katika soko la ajira.
Mafunzo hayo yanawalenga zaidi wasichana waliopo vyuoni pamoja na waliohitimu masomo yao, ili kuwajengea uwezo wa kitaalamu unaohitajika katika ajira za kisasa.
Tangu kuanzishwa kwa mradi huo mwaka 2015, tayari umewafikia takribani vijana 11,000 nchini, wakiwemo wanafunzi wa vyuo na wahitimu.
Akizungumza katika mafunzo hayo, Meneja wa Mradi wa taasisi hiyo, Epifania Muhagama, amesema mradi huo unalenga kuwasaidia wasichana wasio na ujuzi wa awali wa TEHAMA kwa kuwapatia maarifa muhimu kama uandishi wa ripoti, uchambuzi wa data, matumizi ya barua pepe, akili mnemba (AI), pamoja na matumizi ya kompyuta kwa ujumla.
Amesema tafiti zinaonesha kuwa ushiriki wa wanawake katika soko la ajira bado uko chini, hali inayochangiwa na kukosa kujiamini pamoja na ukosefu wa ujuzi unaohitajika.
“Mradi huu umeanzishwa baada ya tafiti kubaini kuwa wanawake wengi hawajiamini na hawana ujuzi wa kuwasaidia kupata ajira,” amesema Muhagama.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Uendelezaji TEHAMA kutoka Tume ya TEHAMA na Tafiti iliyo chini ya Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Bw. Gerson Ndanguzi, amesema mafunzo hayo ni muhimu katika kuwajengea wanawake fursa za kidijitali na kusaidia maendeleo ya familia na jamii kwa ujumla.
Ameongeza kuwa ujuzi huo unalenga kuwasaidia washiriki kutumia TEHAMA kwa usahihi kwa ajili ya maendeleo endelevu ya kiuchumi.
Aidha, Ndanguzi amewahimiza wadau mbalimbali kujitokeza kusaidia kutoa mafunzo ya TEHAMA kwa watu wengi zaidi, akibainisha kuwa bado kuna idadi kubwa ya wananchi ambao hawajafikiwa.
Pia amewasisitiza washiriki kuendelea kujifunza zaidi hata baada ya mafunzo hayo, badala ya kuridhika na ujuzi walioupata pekee.
Naye mnufaika wa mafunzo hayo, Shalom Kokonyo, amesema anatarajia kujifunza ujuzi wa kompyuta, uongozi pamoja na uwekezaji ili kuleta mabadiliko chanya katika jamii yake.
Mafunzo hayo yanatarajiwa kufanyika kwa siku 14, yakihitimishwa Aprili 1, 2026, ambapo wataalamu kutoka kada mbalimbali za ajira watashiriki kama wazungumzaji.