WAKALA Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imeendelea kusisitiza umuhimu wa ulinzi wa Miliki Ubunifu kupitia ushirikiano na wanawake wa fani za Sayansi, Teknolojia, Uhandisi na Hisabati hatua inayolenga kuongeza uelewa kuhusu haki za Miliki Ubunifu ili kuhakikisha bunifu za watanzania zinalindwa, zinathaminiwa na zinachangia kikamilifu katika maendeleo ya jamii na kutatua changamoto zilizoizunguka jamii kwenye maisha yao ya kila siku.
Hayo yamebainishwa na Ofisa Mtendaji Mkuu wa BRELA, Godfrey Nyaisa alipokuwa akifungua warsha ya Miliki Ubunifu kwa wanawake katika fani za Sayansi, Teknolojia, Uhandisi pamoja na Hisabati (STEM) iliyofanyika katika ukumbi wa Tume ya Ushindani jijini Dar es salaam.
Nyaisa amesema warsha hiyo ni muendelezo wa utekelezaji wa mkakati wa BRELA kuwafikia wabunifu waka kada na fani zote ili kuwaelezea umuhimu wa ulinzi na ubiasharishaji wa bunifu zao.
“Kwa kutambua umuhimu wa fani za Sayansi, Teknolojia, Uhandisi na Hisabati katika uvumbuzi BRELA imeona ni vyema kuandaa warsha hii ili kuwapa ninyi nafasi ya kujifunza masuala ya Miliki Ubunifu pamoja na urasimishaji wa biashara zinazotokana na bunifu mnazozifanya,” amesema Nyaisa.
Awali akimkaribisha Ofisa Mtendaji Mkuu Godfrey Nyaisa, Kaimu Mkurugenzi wa Miliki Ubunifu Bw. Seka Kasera amesema idadi ya wanawake katika fani za Sayansi, Teknolojia, Uandisi na Hisabati kwa sasa imezidi kuongezeka na kwamba warsha hiyo itasaidia wanawake wengi kwenye fani ya Sayansi, Teknolojia, Uhandisi na Hisabati kulinda bunifu zao.
Kwa upande wao baadhi ya washiriki wa warsha hiyo walieleza kuwa warsha hiyo imebadilisha kwa kiasi kikubwa mtazamo wao kuhusu masuala ya Miliki Ubunifu hasa kwenye kulinda kazi ambazo wanabuni kwenye kada yao ya STEM.
“Temekuwa tukitengeneza bunifu mbalimbali na tunaishi nazo, unakuta mwingine hajasajili popote wala kulinda bunifu yake ambayo inamsaidia kutambulika, mtu anaweza akabuni leo na mtu mwingine akaja akabuni kitu kinachofanana na chako na akakisajili na wewe ukakosa mahali pakwenda kulalamika hata kama lilikuwa wazo lako,” alieleza Bi. Tanjana Mgonja.
Warsha hiyo yenye kauli mbiu isemayo ‘Bunifu zetu, Nguvu yetu kwa Maendeleo ya Jamii na Taifa Letu’ imewakutanisha kundi la wanawake wenye fani mbalimbali kutoka idara za Sayansi, Teknolojia, Uhandishi na Hisabati ambapo washiriki walipata fursa ya kujadili mada kuhusu Miliki Ubunifu na kutoa mapendekezo yao namna ya kuboresha bunifu zao.
Mikopo hiyo imetolewa katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ambapo jumla ya Shilingi milioni 359 zilitolewa kwa vikundi 17 vya wanawake, Shilingi milioni 557 kwa vikundi 25 vya vijana na Shilingi milioni 75 kwa vikundi tisa vya watu wenye ulemavu.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini, Mhe. Silvestry F. Koka, amesema mikopo ni nyenzo muhimu ya kuwawezesha wananchi kujikwamua kiuchumi, hasa kwa kuzingatia kuwa wengi hukosa mitaji kutokana na masharti magumu ya taasisi za kifedha.
Amesema Halmashauri inapaswa kuendelea kutoa mafunzo ya ujasiriamali na usimamizi wa fedha ili kuhakikisha walengwa wanatumia mikopo hiyo kwa tija na kurejesha kwa wakati.
“Wapo wananchi wenye uwezo wa kufanya biashara lakini wanakosa mtaji kutokana na kutotimiza vigezo vya mikopo ya taasisi za fedha. Kupitia mikopo hii ya Halmashauri tunaendelea kufungua milango ya fursa na kupunguza umaskini kwa wananchi wetu,” alisema Mhe. Koka.
Mbunge huyo amebainisha kuwa zaidi ya Shilingi bilioni 4.5 ziko katika mzunguko wa mikopo iliyotolewa na Halmashauri, hali inayochochea ukuaji wa biashara, kuongeza ajira na kupanua wigo wa mapato ya ndani ya Manispaa.
Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Mhe. Nickson Simon John, aliwataka wanufaika kuwa na nidhamu ya matumizi ya fedha na kuhakikisha mikopo hiyo inatumika kwa malengo yaliyokusudiwa.
“Fedha ni kama damu katika uchumi. Zinapozunguka kwa usahihi huleta uhai wa biashara, huongeza uzalishaji na kuinua maisha ya wananchi. Ni muhimu mikopo hii ikatumike kwa shughuli za maendeleo badala ya matumizi yasiyo na tija,” alisema.
Awali, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha, Dkt. Rogers Shemwelekwa, amesema kuwa katika mwaka wa fedha 2025/2026 Halmashauri tayari imetoa jumla ya Shilingi bilioni 2.1 kwa vikundi 457 vya makundi maalum.
Amefafanua kuwa kati ya fedha hizo, Shilingi bilioni 1.09 zimetolewa kwa vikundi 275 vya wanawake, Shilingi milioni 904.5 kwa vikundi 161 vya vijana na Shilingi milioni 158.8 kwa vikundi vya watu wenye ulemavu.
Utoaji wa mikopo hiyo unaendelea kuthibitisha dhamira ya Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha ya kutumia mapato ya ndani kuwawezesha wananchi kiuchumi, kuongeza ushiriki wao katika shughuli za uzalishaji na kujenga msingi wa maendeleo jumuishi yanayowanufaisha makundi mbalimbali ya jamii.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Zanzibar inakusudia kuimarisha uhusiano na ushirikiano na Jamhuri ya Singapore kwa kuelekeza nguvu zaidi katika diplomasia ya uchumi, biashara na uwekezaji.
Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 10 Juni, 2026 Ikulu alipofanya mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Singapore, Mhe. Tharman Shanmugaratnam, Ikulu Zanzibar ambapo alizikaribisha kampuni na wawekezaji wa Singapore kuwekeza Zanzibar katika sekta za uchumi wa buluu, utalii, nishati, teknolojia na kuongeza thamani ya mazao ya baharini na mwani.
Kwa upande wake, Rais Tharman Shanmugaratnam amepongeza hatua kubwa za maendeleo zinazofanywa Zanzibar na kuahidi kuhamasisha wawekezaji wa Singapore kuja kuwekeza Zanzibar.
Baada ya mazungumzo hayo, Rais Dkt. Mwinyi, alimwandalia mgeni wake, Rais Tharman dhifa ya chakula cha mchana iliyofanyika Ikulu Zanzibar.
.jpeg)

Kongamano hilo la siku mbili lililozinduliwa rasmi na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, ambapo wadau walijadili fursa na mikakati ya kuharakisha matumizi ya nishati safi ya kupikia ili kufikia lengo la asilimia 80 ya kaya kutumia nishati hiyo ifikapo mwaka 2034.
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Umoja wa Ulaya, UNCDF na wadau mbalimbali inaendelea kuimarisha jitihada za kuongeza upatikanaji wa nishati safi ya kupikia kupitia maboresho ya sera na mifumo ya udhibiti, kutafuta rasilimali fedha, kutoa elimu kwa jamii na kuimarisha ushiriki wa sekta binafsi.
Licha ya mafanikio yaliyopatikana, matumizi ya kuni na mkaa bado ndiyo chanzo kikuu cha nishati ya kupikia kwa kaya nyingi nchini. Kuongeza matumizi ya nishati safi ni muhimu katika kuboresha afya za wananchi, kulinda mazingira na kuwawezesha wanawake na vijana ambao huathirika zaidi na athari za matumizi ya nishati za asili.
Chini ya kaulimbiu "Kuendeleza Mustakabali wa Nishati Safi ya Kupikia Tanzania: Mafanikio, Ushirikiano na Njia za Kufikia Asilimia 80 ya Matumizi ifikapo 2034," mkutano huo ulionesha mafanikio yaliyofikiwa, kubaini changamoto zilizopo na kuweka mikakati mipya ya kuongeza matumizi ya nishati safi nchini. Wadau walisisitiza umuhimu wa uratibu na ushirikiano katika utekelezaji, pamoja na kuwepo kwa mifumo madhubuti ya ufuatiliaji na uwajibikaji ili kuhakikisha uwazi na matokeo yanayopimika.
Akizungumza katika mkutano huo, Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, alisisitiza dhamira ya Serikali akisema Serikali ya Tanzania imejipanga kikamilifu kuhakikisha inafikia lengo la asilimia 80 ya matumizi ya nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.
“Mkutano huu umetuwezesha kuoanisha sera, mifumo ya ufadhili na mikakati ya ushirikishwaji wa jamii ili kuharakisha utekelezaji, nishati safi ya kupikia ni muhimu katika kulinda afya za wananchi, kuwawezesha wanawake na vijana, pamoja na kuhifadhi mazingira yetu," alisema.
Aidha, alieleza kuwa juhudi za Mheshimiwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi zimekuwa chachu ya mabadiliko, huku kampeni za kitaifa zinazosimamiwa na UNCDF zikisaidia kuongeza uelewa wa wananchi na kubadili mitazamo kuhusu matumizi ya teknolojia za kisasa za kupikia.
Naye Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania na Jumuiya ya Afrika Mashariki, Bi. Christine Grau, alisisitiza umuhimu wa ushirikiano, akibainisha kuwa, Umoja wa Ulaya umetenga euro milioni 30, sawa na zaidi ya shilingi bilioni 92 za Kitanzania, kwa ajili ya kupanua upatikanaji wa nishati safi ya kupikia, kuimarisha masoko ya nishati endelevu, kulinda rasilimali asili na kuzalisha fursa za kiuchumi.
“Huu ndio ufadhili mkubwa zaidi wa Umoja wa Ulaya katika sekta ya nishati safi ya kupikia katika nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara, ukiendana na mkakati wa Global Gateway unaolenga kuchochea uwekezaji wa sekta binafsi, kuhimiza ubunifu na kuleta matokeo yenye tija”, akiongeza kuwa msaada huo ni sehemu ya mkakati mpana wa kikanda wa kukuza maendeleo ya sekta binafsi na kupanua matumizi ya nishati safi ya kupikia barani Afrika.
Mkutano huo umefanyika wakati Tanzania ikiendelea kushuhudia mafanikio katika utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia (2024–2034). Kwa mujibu wa ripoti ya mkakati huo, matumizi ya nishati safi ya kupikia yameongezeka kutoka asilimia 16 mwaka 2022 hadi asilimia 28.6 kufikia Machi 2026. Mafanikio hayo yamechangiwa na ruzuku ya mitungi ya gesi ya LPG, kupunguzwa kwa gharama za umeme, kuondolewa kwa baadhi ya kodi kwenye vifaa vya nishati safi ya kupikia pamoja na uwekezaji wa sekta binafsi na washirika wa maendeleo.
Kwa mujibu wa Shirika la Kimataifa la Nishati (IEA), zaidi ya watu bilioni 2.3 duniani bado hawana huduma za nishati safi ya kupikia, huku Bara la Afrika likiwa na idadi kubwa zaidi. Hivyo, juhudi za Tanzania zinachangia si tu katika kufikia malengo ya maendeleo ya taifa, bali pia katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, kuboresha afya za jamii na kuimarisha usawa wa kijinsia duniani.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mshauri Mkuu wa Masuala ya Ufundi wa UNCDF, Bw. Peter Malika alisema, UNCDF ina jukumu la kuwezesha upatikanaji wa mitaji kwa ajili ya maendeleo ya jamii kwa kuondoa vikwazo vinavyokwamisha uwezo wa wananchi kumudu gharama, usambazaji wa bidhaa na upatikanaji wa mitaji kwa biashara.
“Kupitia programu ya CookFund, tunawezesha upatikanaji wa fedha, kujenga ushirikiano na kusaidia biashara na wabunifu kuhakikisha suluhisho za nishati safi ya kupikia zinawafikia Watanzania wote."
“Kupitia programu hii UNCDF imeendelea kutoa mitaji kwa biashara ndogo na za kati ili kusaidia upanuzi wa teknolojia za nishati safi ya kupikia, kuchochea ubunifu na kuongeza ajira”, aliongeza Bw. Malika.
Tangu kuanzishwa kwake, programu hiyo imetoa zaidi ya dola za Marekani milioni 11.2 kupitia ruzuku 102 kwa biashara ndogo na za kati, na kusaidia ajira takribani 27,000 nchini.
Programu hiyo imewezesha zaidi ya kaya 413,000 kupata huduma za nishati safi ya kupikia, zikiwanufaisha karibu watu milioni 1.94 nchini kote. Aidha, imeziwezesha biashara 961 na taasisi za umma 45, ikiwemo shule zinazotumia briketi, majiko ya umeme ya shinikizo (EPC), gesi ya LPG na nishati nyingine endelevu. Hatua hizi zimechangia kupunguza utegemezi wa kuni na mkaa huku zikiboresha ufanisi, usalama na ubora wa huduma za upishi katika taasisi.
Katika sekta ya elimu pekee, wanafunzi 62,105 kutoka wilaya 14 katika mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Morogoro, Dodoma na Mwanza wamenufaika na programu hiyo, hatua iliyobooresha mazingira ya kujifunzia na kupunguza madhara yatokanayo na moshi. Kwa ujumla, utekelezaji wa CookFund umechangia kupunguza zaidi ya tani milioni 3.8 za hewa ukaa (CO₂e), na hivyo kusaidia Tanzania kufikia malengo yake ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na kuonesha nguvu ya ushirikiano kati ya sekta ya umma na binafsi.
Mkutano huo umehitimishwa kwa Serikali, wafadhili na sekta binafsi kuthibitisha upya dhamira yao ya kuharakisha matumizi ya nishati safi ya kupikia ili kuhakikisha kila kaya nchini inanufaika na suluhisho salama, nafuu na endelevu za kupikia.
Naibu Waziri wa Nishati, Mheshimiwa Salome Makamba (kushoto), akipokewa na Mshauri Mkuu wa Kiufundi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Mitaji (UNCDF), Bw. Peter Malika, kabla hajazindua Kongamano la Kitaifa siku mbili la Nishati Safi ya Kupikia, lililoanza jijini Arusha leo. Kongamano hilo likiwa na kauli mbiu, "Kuendeleza Mustakabali wa Nishati Safi ya Kupikia Tanzania: Mafanikio, Ushirikiano na Njia za Kufikia Asilimia 80 ya Matumizi ifikapo 2034," linaangazia umuhimu wa kuoanisha sera, ufadhili na mikakati ya ushirikishwaji wa jamii ili kuharakisha maendeleo. Kongamano hilo limeandaliwa na UNCDF kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania, kupitia Wizara ya Nishati, kwa msaada wa Umoja wa Ulaya (EU). Wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Nishati Safi ya Kupikia, Wizara ya Nishati, Nolasco Mlay na kulia ni Mwakilishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Polycarp Nkuyumba
Mshauri Mkuu wa Kiufundi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Mitaji (UNCDF), Bw. Peter Malika (wa pili kuia), akizungumza wakati wa Kongamano la Kitaifa la siku mbili la Nishati Safi ya Kupikia, lililoanza leo jijini Arusha. Kongamano hilo likiwa na kauli mbiu, "Kuendeleza Mustakabali wa Nishati Safi ya Kupikia Tanzania: Mafanikio, Ushirikiano na Njia za Kufikia Asilimia 80 ya Matumizi ifikapo 2034," linaangazia umuhimu wa kuoanisha sera, ufadhili na mikakati ya ushirikishwaji wa jamii ili kuharakisha maendeleo. Katikati ni Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba na wa pili kushoto ni Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU), nchini Tanzania na Jumuiya ya Afrika Mashariki, Bi. Christine Grau.
Naibu Waziri wa Nishati, Mheshimiwa Salome Makamba, akizindua Kongamano la Kitaifa la siku mbili la Nishati Safi ya Kupikia, lililoanza leo jijini Arusha. Kongamano hilo likiwa na kauli mbiu, "Kuendeleza Mustakabali wa Nishati Safi ya Kupikia Tanzania: Mafanikio, Ushirikiano na Njia za Kufikia Asilimia 80 ya Matumizi ifikapo 2034," linaangazia umuhimu wa kuoanisha sera, ufadhili na mikakati ya ushirikishwaji wa jamii ili kuharakisha maendeleo.
Na Mwandishi Wetu
UJUMBE wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania umeungana na mataifa mengine katika Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Kupinga Utumikishwaji wa Mtoto yaliyofanyika Juni 9, 2026 katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, Geneva, Uswisi.
Aidha, ujumbe huo wa Tanzania uliongozwa na Kamishna wa Kazi, Suzan Mkangwa ambaye aliambatana na Jaji wa Mahakama ya Rufani, Dkt. Yose Joseph Mlyambina, Kamishna wa Kazi Zanzibar, Rashid Khamis Othman, Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, Wataalamu na Wawakilishi wa Waajiri (ATE) pamoja na Wawakilishi kutoka Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA).
Akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi wa maadhimisho hayo, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Kazi Duniani (ILO), Gilbert F. Houngbo ametoa wito kwa jamii ya Kimataifa na Wadau wa Utatu kutekeleza kwa vitendo Mipango na Maadhimio ya Mkutano wa Marrakesh uliofanyika nchini Morocco, Februari 2026 kwa lengo la kupinga utumikishwaji wa Mtoto.
Pia alisisitiza juu ya jitihada za makusudi zinazotakiwa kuchukuliwa na nchi wanachama wa ILO, katika kukuza kazi za staha na utekelezaji wa sera ya elimu bure.
Kwa upande wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe. Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano imeendelea kudhihirisha mafanikio yaliyopatikana katika sekta ya kazi na ajira, hasa hatua madhubuti zilizochukuliwa katika kutokomeza ajira za watoto nchini ni kama zifuatazo:- Utekelezaji wa Mradi wa pamoja kati ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Brazil kwa kushirikiana na ILO mradi huo umefanikiwa kwa kiasi kikubwa kutoa elimu kuhusu utumikishwaji wa mtoto na madhara yake.
Pia, kuhuishwa kwa Mkakati wa Taifa wa Kutokomeza Utumikishwaji wa Mtoto 2024/25–2028/29, unaolenga kuunganisha nguvu za wadau wote wa maendeleo, mashirika ya kiraia na jamii kwa ujumla. Kadhalika, Serikali imeendelea kuimarisha mifumo ya Haki Kazini kupitia Mahakama Kuu, Divisheni ya Kazi, na Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA).
Vyombo hivi vimekuwa vikitimiza vyema wajibu wake wa kutafsiri sheria na kutoa haki, hususani ulinzi kwa mtoto; Kuadhimisha Siku ya Kupinga Utumikishwaji wa Mtoto Kitaifa kila tarehe 12 Juni. Wadau kutoka Tanzania Bara na Zanzibar hushiriki na kupokea mikakati ya Serikali ya kukabiliana na tatizo hili; pamoja na Kutoa elimu kwa Umma kwa kuwa utumikishwaji wa mtoto ni jukumu la jamii nzima,
Hivyo ushirikiano baina ya Wizara, wadau wa maendeleo, kaya, na kila mwananchi unahitajika ili kufafanua tafsiri ya utumikishwaji wa mtoto, kazi za shuruti, na kazi hatarishi kwa afya na maendeleo ya mtoto.
Siku ya Kupinga Utumikishwaji wa Mtoto uadhimishwa kila mwaka tarehe 12 Juni na Shirika la Kazi Duniani (ILO) pamoja na nchi wanachama kwa lengo la kuhamasisha nguvu ya pamoja baina ya Serikali, Vyama vya Waajiri, na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi katika kukuza ajira zenye staha na kutokomeza utumikishwaji wa watoto unaowanyima fursa za kijamii, hususan haki ya elimu.
Maadhimisho hayo kwa mwaka huu 2026 yataongozwa na Kaulimbiu isemayo: “Red Card to Child Labour” ikimaanisha wito kwa wadau wote wa maendeleo kutoonesha uvumilivu wowote kwa vitendo vinavyochochea au kusababisha utumikishwaji wa mtoto katika sekta zote za kijamii na kiuchumi.
Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya Kitanzania ya Ngoteya Wild, inayoongozwa na muandaaji wa makala zenye maudhui ya uhifadhi na wanyamapori @Hans_Cosmas_Ngoteya, imetangaza kuwa filamu yao mpya ya Sentinels of Engaruka ambayo wamefanya kwa kushirikiana na African people and wildlife itaoneshwa rasmi kupitia YouTube channel yao Juni 21, 2026.
Filamu hiyo imechukua zaidi ya miaka mitatu kuandaliwa, ikihusisha utafiti wa kina, upigaji picha wa mazingira ya asili na simulizi inayoonesha uhusiano wa kipekee kati ya jamii ya Kimasai, twiga na mazingira ya Engaruka mkoani Arusha.
Toleo la Kiswahili la filamu hiyo limesimuliwa na mtangazaji maarufu Meena Ally, ambaye sauti yake itaongeza mguso wa kipekee katika kuifikisha hadithi hiyo kwa watazamaji wa Tanzania na Afrika Mashariki.
Kwa mujibu wa Hans Ngoteya, filamu hiyo inalenga kuhamasisha uhifadhi wa maliasili, kuonesha utajiri wa urithi wa Tanzania na kuifikisha hadithi ya Engaruka kwa hadhira ya kimataifa kupitia jukwaa la YouTube.
Sentinels of Engaruka ni moja ya miradi mikubwa ya filamu za uhifadhi iliyotayarishwa nchini Tanzania, ikiwa na lengo la kuonesha namna jamii na wanyamapori wanavyoweza kuishi kwa maelewano huku wakilinda mazingira kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.
Tume ya Utumishi wa Umma inatarajia kufanya Mkutano wake Na. 4 wa mwaka wa fedha 2025/2026 kuanzia tarehe 15 Juni hadi 3 Julai 2026 jijini Mwanza, ambapo itajadili na kutoa maamuzi kuhusu rufaa na malalamiko mbalimbali yaliyowasilishwa na watumishi wa umma.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma tarehe 10 Juni 2026, Kaimu Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. John C. Mbisso, amesema kuwa kupitia mkutano huo, Tume itatoa fursa kwa warufani na warufaniwa walioomba kufika mbele ya Tume ili kutoa ufafanuzi wa ziada kuhusu hoja zilizowasilishwa katika rufaa zao.
Bw. Mbisso amesema hatua hiyo inatekelezwa kwa mujibu wa Kanuni ya 62(1) ya Kanuni za Utumishi wa Umma za mwaka 2022, aidha Tume itapitia taarifa mbalimbali za utekelezaji wa majukumu yake katika kipindi cha robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2025/2026.
Pamoja na shughuli za mkutano, amesema Tume itafanya ziara katika baadhi ya taasisi za serikali zilizopo jijini Mwanza kwa lengo la kutoa elimu kwa waajiri, mamlaka za ajira na mamlaka za nidhamu kuhusu umuhimu wa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu katika usimamizi wa rasilimali watu.
Vilevile ameeleza kuwa Tume itatoa elimu kwa watumishi wa umma katika taasisi hizo kuhusu haki na wajibu wao katika utekelezaji wa majukumu ya utumishi wa umma Sambamba na hilo, itapokea na kushughulikia malalamiko ya watumishi wa umma ambao hawakuridhika na maamuzi yaliyotolewa na waajiri, mamlaka za ajira au mamlaka za nidhamu.
Kwa mujibu wa Kifungu cha 12(1)(d) kikisomwa pamoja na Kifungu cha 27(1)(b) cha Sheria ya Utumishi wa Umma, Sura ya 298, Marejeo ya Mwaka 2023, Tume ya Utumishi wa Umma imepewa mamlaka ya kupokea na kushughulikia rufaa na malalamiko ya watumishi wa umma wasiokubaliana na maamuzi yaliyotolewa na waajiri, mamlaka za ajira na mamlaka za nidhamu katika utumishi wa umma.
Na Karama Kenyunko Michuzi Tv
KAMPUNI za Singapore zimeendelea kuimarisha uwekezaji wake nchini Tanzania huku kampuni ya Wilmar Rice iliyopo Morogoro ikitajwa kuwa kiwanda kikubwa zaidi cha kusindika mpunga na kuzalisha mchele si Tanzania pekee wala Afrika Mashariki, bali katika bara lote la Afrika.
Akizungumza katika Jukwaa la Biashara la Tanzania na Singapore, Juni 9, 2026 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo amesema uwepo wa wawekezaji wa Singapore nchini unaonyesha namna ushirikiano wa kiuchumi kati ya mataifa hayo mawili unavyoendelea kukua.
"Wilmar Rice Morogoro ni kiwanda kikubwa zaidi cha kusindika mpunga na kuzalisha mchele si Tanzania pekee, si Afrika Mashariki pekee, bali kikubwa zaidi Afrika, na tunajivunia sana kampuni hii iliyopo Morogoro," amesema.
Profesa Mkumbo amesema pamoja na Wilmar Rice, kampuni ya Norman Gohines imekuwa mwekezaji muhimu Zanzibar kwa zaidi ya miaka 100 ikijikita katika uzalishaji wa viungo na shughuli za mashamba ya viungo.
Amesema kampuni hizo ni sehemu ya uwekezaji wa Singapore nchini Tanzania, huku kampuni nyingine nyingi kutoka taifa hilo zikiendelea kufanya shughuli zake nchini.
Profesa Mkumbo amesema Singapore imepitia safari ya maendeleo inayovutia dunia, ikitoka kuwa nchi ndogo yenye kipato cha chini na pato la mtu mmoja mmoja la dola 565 hadi kufikia zaidi ya dola 100,000 kwa sasa.
Amesema mafanikio hayo yameifanya Singapore kuwa na sauti muhimu katika uchumi, diplomasia na siasa za dunia.
Kwa mujibu wa Profesa Mkumbo, kampuni za Singapore ni miongoni mwa wawekezaji wakubwa duniani zikiwa zimewekeza takribani dola trilioni 1.5 katika maeneo mbalimbali duniani, hasa Asia, huku uwekezaji wake barani Afrika ukifikia kati ya dola bilioni 26 na 32 kupitia kampuni takribani 100 zinazofanya shughuli katika nchi 40.
Amesema ziara ya Rais wa Singapore, Tharman Shanmugaratnam, nchini Tanzania itasaidia kupeleka ushirikiano wa kiuchumi kati ya nchi hizo mbili katika hatua nyingine.
Profesa Mkumbo amesema mwelekeo wa kiuchumi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuimarisha ushirikiano wa kimataifa kwa kuvutia biashara na uwekezaji.
"Ametuelekeza tushirikiane na dunia nzima, tusiende kutafuta misaada bali kutafuta washirika wa biashara na uwekezaji," ameisema.
Ameongeza kuwa historia ya maendeleo ya Singapore inatoa mafunzo muhimu ambayo Tanzania inaweza kujifunza na kuyatumia kwa kuzingatia mazingira yake katika safari ya maendeleo.





.jpeg)
.jpeg)











.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)



