Na Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma
Wizara ya Kilimo imeendelea kuratibu upatikanaji wa mbolea nchini kwa lengo la kuwawezesha wakulima kuongeza uzalishaji na tija ya mazao. Hadi kufikia Machi 2026, kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA), jumla ya tani 1,254,203 za mbolea zimepatikana, sawa na asilimia 83.61 ya lengo la tani 1,500,000 kwa mwaka wa fedha 2025/2026.
Kati ya kiasi hicho, tani 150,686 zimezalishwa ndani ya nchi, tani 869,840 zimeagizwa kutoka nje, huku tani 233,677 zikiwa ni akiba iliyosalia kutoka msimu uliopita.
Aidha, serikali imesambaza tani 674,686.24 za mbolea zenye thamani ya shilingi trilioni 1.21 kwa wakulima kupitia mpango wa ruzuku unaotekelezwa katika mikoa yote nchini. Kati ya fedha hizo, shilingi bilioni 929.16 ni mchango wa wakulima, wakati shilingi bilioni 281.58 zimetolewa na serikali kama ruzuku.
Hatua hiyo imechangia kuongezeka kwa matumizi ya mbolea, ambapo kiwango kimepanda kutoka kilo 19 za virutubisho kwa hekta mwaka 2021/2022 hadi kufikia wastani wa kilo 27 kwa hekta mwaka 2025/2026. Hii ni sawa na asilimia 54 ya lengo la kilo 50 kwa hekta, kama ilivyoainishwa katika azimio la CAADP.
Akizungumza Bungeni jijini Dodoma, Waziri wa Kilimo, Daniel Godfrey Chongolo ameeleza mafanikio hayo wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Kilimo kwa mwaka wa fedha 2026/2027.
Ameongeza kuwa Serikali itaendelea kuboresha mifumo ya usambazaji wa pembejeo, kuimarisha uzalishaji wa mbolea ndani ya nchi, pamoja na kuhakikisha upatikanaji wa mbolea kwa wakati na kwa bei nafuu ili kuwafikia wakulima wengi zaidi. Hatua hizi zinatarajiwa kuongeza zaidi tija katika sekta ya kilimo, kuimarisha usalama wa chakula na kukuza uchumi wa nchi kwa ujumla, hasa kwa kuzingatia kuwa kilimo kinaendelea kuwa mhimili muhimu wa ajira na maendeleo ya Watanzania wengi.



.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)


.jpeg)



.jpeg)















.jpeg)



.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
