Wakati wakongwe wa Redio Tanzania wakiadhimisha miaka 75 ya utangazaji Tanzania Bara na miaka 61 ya Redio Tanzania wamewataka waandishi na watangazaji vijana kuendelea kulinda misingi ya uandishi bora kwa kuzingatia maadili, utafiti, Kiswahili sanifu na matumizi sahihi ya teknolojia.

Katika kongamano la kuwakutanisha wakongwe wa Radio Tanzania (RTD), lililofanyika Dar es Salaam leo Julai 18,2026 wadau mbalimbali wa habari wameeleza kuwa pamoja na mabadiliko makubwa yaliyotokana na maendeleo ya teknolojia, msingi wa taaluma ya habari bado unabaki kuwa ukweli, weledi na uwajibikaji kwa jamii.

Mwenyekiti wa wakongwe wa RTD Suleiman Kumchaya amesema vijana wanaochipukia wamekuwa hawana matumizi sahihi ya lugha ya Kiswahili wanapokuwa wakiwasilisha kazi za kihabari na kuwahimiza kuwa pamoja na maendeleo ya teknolojia, bado kuna umuhimu wa kulinda ubora wa lugha ya Kiswahili katika uandishi na utangazaji.

Amesema: " Tunaona na kusikia sasa hivi watangazaji wanakibananga sana kiswahili. Tumeweka msingi wa kuendelea kushirikiana na vijana ili kuhakikisha maadili, weledi na ubora wa kazi vinaendelea kuwa nguzo ya tasnia ya habari,"

Mkongwe wa utangazaji Rose Mwalimu, amesema tofauti kubwa kati ya utangazaji wa zamani na wa sasa ipo katika kiwango cha utafiti, ubunifu na maandalizi ya maudhui.

Amesema enzi zao waandishi walitumia muda mwingi kutafuta taarifa, kufanya utafiti, kuandika script na kutengeneza vipindi vyenye kugusa maisha ya watu, tofauti na baadhi ya maudhui ya sasa ambayo hayana uzito kutokana na kukosa utafiti wa kutosha.

Alisisitiza kuwa utangazaji bora unahitaji ubunifu, hasa kwenye redio ambayo inahitaji mtangazaji kutumia lugha na sauti kujenga picha kwa msikilizaji.

Kwa upande wake, Mary Kafyome, mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), amesema wakongwe wa RTD wameacha alama kubwa katika maendeleo ya taifa kwa kutumia vipawa vyao na weledi katika kipindi ambacho teknolojia haikuwa imeendelea kama ilivyo sasa.

Amesema vijana wanapaswa kujifunza kutoka kwa wakongwe hao kwa kuzingatia kujituma, kuipenda kazi, kuwa waadilifu na kutumia teknolojia kama nyenzo ya kuboresha kazi zao.

“Teknolojia inapaswa kutusaidia kufanya kazi vizuri zaidi, lakini tusiruhusu ichukue nafasi ya ubunifu na misingi ya taaluma,” amesema.

Kwa upande wake, Meneja wa Huduma za Utangazaji wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Kadaya Baluhye, amesema teknolojia imebadili namna habari zinavyotengenezwa na kusambazwa, lakini haiwezi kuchukua nafasi ya maadili ya mwandishi wa habari.

Amesema waandishi wanapaswa kutumia teknolojia kwa ubunifu ili kuelimisha, kuburudisha na kuhabarisha jamii kuhusu masuala muhimu ikiwemo afya, maendeleo ya serikali na maandalizi ya Tanzania kuwa mwenyeji wa mashindano ya AFCON 2027.

Naye mtangazaji wa Bongo FM Radio, Emmy Jovin, amesema jambo kubwa alilojifunza kutoka kwa wakongwe ni umuhimu wa maadili na uzalendo katika utoaji wa taarifa.

Amesema kasi ya mitandao ya kijamii na teknolojia imekuwa ikiwafanya baadhi ya wanahabari kukimbilia kupata watazamaji wengi bila kuzingatia misingi ya taaluma.

Aliongeza kuwa matumizi ya Akili Mnemba (AI) yanapaswa kufanyika kwa umakini huku mwandishi akibaki na jukumu la kuhakiki taarifa na kuhakikisha maudhui yanayowasilishwa yana ukweli na yanazingatia maadili.









Na Mwandishi Wetu.

KATIBU wa Chama cha Mapinduzi (CCM)Wilaya ya Kilosa,Mkoani Morogoro, Janus Mfaume, anatuhumiwa kumdhalilisha na kumtishia maisha mwanachama wa Chama hicho Egon Haule, baada ya kumfukuza ofisini bila sababu za msingi huku akimtolea kauli za vitisho.

Tukio hilo limetokea Julai 17 mwaka huu katika ofisi za Wilaya za Chama hicho ambapo Haule alikwenda kuitikia wito wa Katibu wa Jumuiya ya Wazazi aliyemwita kwa ajili ya kumpa majukumu.

Akizungumza kwa masikitiko makubwa Haule,alisema,hii ni mara ya tatu anafanyiwa udhalilishaji na kutishiwa maisha na Mfaume huku akitishia kumfanyia kitu kibaya ambacho hata kisahau katika maisha yake.

Haule alisema,hana ugomvi wowote na Katibu wake huyo lakini anashangazwa kuona kila siku amekua akimtishia maisha sambamba na kumfukuza kufika katika ofisi za Chama hicho Wilaya.

"Mimi ni mwanachama halali ambaye nimekua nikijitolea majukumu mbalimbali ya Chama kwa mwamvuli wa UVCCM Wilaya lakini napitia manyanyaso na udhalilishaji kwa kufukuzwa kila ninapofika ofsini na nimejaribu mara kadhaa kumuomba Katibu Mfaume anieleze kuna tatizo gani kauli zake amekua akisema hataki kuniona nikifika pale,"

"Kabla ya tukio la juzi nilishamuandikia ujumbe mfupi wa maandishi kumuomba tuonane anieleze nina tatizo gani la kuzuiwa kufika ofsini lakini hajawahi kunijibu,"alisema Haule.

"Kwa masikitiko makubwa huku moyo wangu ukiwa umeelemewa na huzuni na shinikizo kubwa la kukata tamaa katika kuendelea kujifunza uongozi, Itikadi na misingi ya Chama Cha Mapinduzi Ili baadae nami niwe kiongozi sahihi wa UVCCM na hatimaye chama Cha Mapinduzi,'

"Nawasilisha kwenu kitendo cha aibu na udhalilishaji na vitisho alivyo nitendea Ndugu Janus Mfaume Katibu wa CCM Wilaya ya Kilosa Julai 17 mwaka huu nilipofika ofisi ya CCM Wilaya kwa lengo la kumsaidia kazi Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya ambaye alinihitaji nifike hapo," aliandika Haule kupitia kundi sogozi la Chama hicho.

"Nimeamua kuwashirikisha kuhusu changamoto ninayopitia. Katibu wa CCM Wilaya amenieleza nisiende ofisini, na katika mawasiliano yetu kuna kauli nilizozielewa kama vitisho. Nina rekodi ya sauti ya mawasiliano hayo, ambayo niko tayari kuiwasilisha kwa mamlaka husika endapo itahitajika.

Lengo langu si kumhukumu mtu yeyote kupitia kundi hili, bali kuomba suala hili lipatiwe ufumbuzi kwa kuzingatia haki, taratibu za Chama, na misingi ya uongozi wenye uwajibikaji.

"Naomba viongozi mlipokee jambo hili na kulifanyia kazi kwa busara na haki alieleza Haule"

Alipotafutwa Katibu wa CCM Wilaya ya Kilosa, Mfaume kuhusiana na tuhuma hizo alikiri kumfukuza Haule akifafanua kuwa ni kijana ambaye ana mienendo ya kihalifu na taarifa zake zipo ndani ya Jeshi la Polisi.

Alisema,Haule ameshafanya matukio kadhaa ya uhalifu ndani ya ofisi za CCM na ushahidi upo wazi ndiyo maana amechukua jukumu la kumpiga marufuku kufika hapo.

" Huyu kijana amekua akifanya mambo mbalimbali yanayokichafua Chama ikiwemo kujifanya mmoja ya maofisa wa CCM Wilaya kwa maslahi yake binafsi," alisema Mfaume.

"Mimi ndiye Katibu wa CCM Wilaya ninawajibu wa kulinda maslahi ya ofisi za Chama na mali zake siwezi kukubali kuona mtu anafanya vitendo visivyo na maadili nikafumbia macho, nimemfukuza Haule kwa sababu hana jukumu lolote ndani ya ofisi zetu lakini pia tabia zake za kihalifu zinajulikana kila mahali ikiwemo ndani ya vyombo vya dola,"alisema Mfaume.

Kuhusu suala la kumtishia maisha alisema,ni jukumu la mlalamikaji kwenda Polisi kufungua kesi kama ana uthibitisho wa kutosha na yuko tayari kujibu tuhuma hizo.



Mkuu wa Wilaya ya Moshi Godfrey Mnzava amefanya ziara katika Kijiji cha Umbwe Kati, Kata ya Kibosho Magharibi, Tarafa ya Kibosho, na kutatua mgogoro wa muda mrefu uliohusiana na ubainishaji wa barabara.

Mgogoro huo ulitokana na baadhi ya wananchi kutokubaliana na ubainishaji wa barabara uliofanywa na Kamati ya Maendeleo ya Kata. Kutokana na hilo palitokea kutokuelewana kuhusu mipaka halisi ya barabara hiyo.

Katika ziara hiyo Mnzava alisikiliza pande zote zinazohusika. Kwa kushirikiana na wananchi na viongozi wa eneo hilo alisimamia zoezi la ubainishaji wa mipaka ya barabara. Uamuzi huo ulikubaliwa na wananchi wenye maeneo yanayopitiwa na barabara, ambao walikubali kuachia eneo hilo kwa ajili ya matumizi ya umma.

Barabara hiyo inatumika na wananchi kufika Kituo cha Afya cha Umbwe. Inasaidia pia katika shughuli nyingine za kiuchumi na kijamii katika eneo hilo.

Akizungumza na wananchi baada ya zoezi hilo, Mnzava amewataka kuendelea kudumisha umoja, amani na mshikamano. Amesema maendeleo ya jamii yanategemea wananchi kuweka mbele maslahi ya pamoja.

Wananchi wa Umbwe Kati wamesema wameridhika na jinsi mgogoro huo umetatuliwa na wameahidi kushirikiana na viongozi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.





Na Janeth Raphael - MichuziTv

Tanzania na Misri zimefikia makubaliano ya kuimarisha ushirikiano katika sekta za kilimo na mifugo, hatua inayotarajiwa kufungua ukurasa mpya wa uwekezaji kupitia maendeleo ya Ranchi ya Ruvu na matumizi ya teknolojia za kisasa katika uzalishaji wa chakula.

Akizungumza Ikulu jijini Dar es Salaam, Julai 18, 2026, baada ya mazungumzo rasmi na Rais wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, Abdel Fattah El-Sisi, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, alisema nchi hizo mbili zimekubaliana kuongeza ushirikiano ili kuinua uzalishaji wa mazao na mifugo na kuimarisha usalama wa chakula.

Rais Samia amesema mazungumzo yao yalijikita katika namna ya kutumia teknolojia za kisasa za umwagiliaji na ufugaji ili kuongeza tija, huku yakifungua fursa mpya za uwekezaji katika sekta hizo muhimu kwa uchumi wa nchi.

Ameeleza kuwa bara la Afrika bado linatumia fedha nyingi kuagiza chakula kutoka nje, jambo linalosisitiza umuhimu wa kuongeza uzalishaji wa ndani kwa kutumia rasilimali zilizopo na kuwekeza katika kilimo chenye tija.

Aidha, Rais Samia amesema Tanzania ina zaidi ya hekta milioni 29 zinazofaa kwa kilimo cha umwagiliaji, hali inayoweka mazingira mazuri kwa uwekezaji mkubwa katika uzalishaji wa chakula kwa ajili ya soko la ndani na nje ya nchi.

Katika hatua nyingine, amesema Serikali ya Misri imeonesha nia ya kushirikiana na Tanzania kuendeleza Ranchi ya Ruvu, ambayo kwa sasa haijatumika kikamilifu, kwa lengo la kuifanya kuwa kitovu cha uzalishaji wa kisasa wa mifugo na uwekezaji wa pamoja.

Rais Samia pia amewahamasisha wawekezaji kutoka Misri kushirikiana na taasisi za Serikali zenye maeneo makubwa ya uzalishaji, ikiwemo Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Magereza, Shirika la Taifa la Ranchi (NARCO), pamoja na miradi ya kilimo inayotekelezwa Zanzibar.

Amesisitiza kuwa ushirikiano huo unalenga kuongeza uzalishaji wa chakula, kuvutia uwekezaji, kuzalisha ajira kwa Watanzania na kuiwezesha Tanzania kuwa kitovu cha uzalishaji wa mazao na mifugo kwa soko la Afrika na masoko mengine ya kimataifa.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, Mhe. Abdel Fattah El-Sisi, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 18 Julai Juni, 2026.


Na Janeth Raphael - MichuziTv

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Misri zimefikia makubaliano ya kuimarisha ushirikiano katika sekta ya usafirishaji wa baharini kwa kuunganisha bandari za mataifa hayo mawili, hatua inayolenga kuongeza biashara, kuvutia uwekezaji na kupanua masoko ndani ya Afrika na ukanda wa Ghuba.

Akizungumza Ikulu, Dar es Salaam, Julai 18, 2026, baada ya mazungumzo rasmi na Rais wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, Abdel Fattah El-Sisi, Rais Samia alisema ushirikiano huo utahusisha maendeleo ya Bandari ya Dar es Salaam pamoja na ujenzi wa eneo maalumu la kuhifadhi bidhaa na makontena ya Misri katika Bandari ya Bagamoyo, ambalo litaunganishwa na reli hadi Kwala ili kuongeza ufanisi wa usafirishaji wa mizigo.

Amesema pande zote mbili zimekubaliana kuendeleza mazungumzo ya kuunganisha Bandari za Dar es Salaam, Bagamoyo, Safaga pamoja na bandari nyingine za Misri, jambo litakalorahisisha usafirishaji wa bidhaa, kupunguza gharama za biashara na kuongeza ushindani wa mataifa hayo katika soko la kimataifa.

Kwa mujibu wa Rais Samia, mpango huo utafungua njia kwa bidhaa za Tanzania kuingia kwa urahisi zaidi katika masoko ya nchi za Ghuba, huku bidhaa kutoka Misri zikipata fursa ya kufikia nchi za Afrika Mashariki na Kusini kupitia bandari za Tanzania.

Katika kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi, Rais Samia amesema Rais El-Sisi ameambatana na ujumbe wa wafanyabiashara wakubwa 35 wanaoshiriki Jukwaa la Biashara Tanzania na Misri, hatua inayotarajiwa kuongeza kiwango cha biashara na uwekezaji kati ya mataifa hayo mawili.

Aidha, amesema Shirika la Ndege la EgyptAir tayari linaendesha safari tatu kwa wiki kati ya Misri na Tanzania, huku akiihimiza Air Tanzania kuanzisha safari za moja kwa moja kuelekea Misri ili kurahisisha usafiri wa abiria, kukuza utalii na kuongeza fursa za biashara.

Rais Samia amesisitiza kuwa ushirikiano huo unaipa Tanzania nafasi ya kuendelea kuwa kitovu muhimu cha biashara na usafirishaji kwa ukanda wa Afrika Mashariki na Kusini, huku ukiimarisha zaidi uhusiano wa kiuchumi na kibiashara kati ya Tanzania na Misri.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, Mhe. Abdel Fattah El-Sisi wakati wakishuhudia utiaji saini wa Mikataba na Hati za Makubaliano katika sekta ya umeme, nishati jadidifu, pamoja na masuala ya mbalimbali za Uchukuzi baina ya Tanzania na Misri. Hafla hiyo ilifanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 18 Julai, 2026.






Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiongoza Ujumbe wa Tanzania kwenye mazungumzo rasmi na Ujumbe wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, uliongozwa na Rais wa nchi hiyo, Mhe. Abdel Fattah El-Sisi, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 18 Julai Juni, 2026.

Na Victor  Masangu, Pwani

Hatimaye Chama cha wafanyakazi wa serikali na afya  (TUGHE) Mkoa wa Pwani kimefanya uchaguzi wake mkuu na kuweza kumchangua kwa kishindo Mwenyekiti  aliyekuwa anatetea  kiti  chake  Catherine Katele ambaye ameweza kuibuka na ushindi baada ya   kupata kura 33 dhidi ya mpinzani wake ambaye amejinyakulia kura zipatazo 18 kati ya kura halali 51 ambazo zimepigwa.

Katika uchaguzi huo ambao  ulifanyika  katika ukumbi wa Mkuu  wa Mkoa wa Pwani ulihudhuliwa na wajumbe mbali mbali kutoka Wilaya zote saba za Mkoa wa Pwani zikiwemo, Kibaha, Rufuji, Bagamoyo , Mkuranga, Mafia,Kisarawe, pamoja na Kibiti ulikuwa na amani na utulivu katika kipindi chote cha uendeshaji wa  zoezi  zima la upigaji wa kura.    

Akitangaza matokeo hayo msimamizi wa uchaguzi ambaye pia ni  Afisa kazi   Mkoa wa Pwani Metta Nahonyo  amesema kwamba uchaguzi umekwanda vizuri bila ya kuwa na dosari ya aina yoyote na kwamba wagombea wote wamekubalina na matokeo ambayo yametokea na kuongeza kuwa  fomu zote wameweza kuzisahi  bila shaka ya yoyote ikiwa ni ishara tosha ya kuridhika na matokeo hayo.

Msimamizi huyo  amebainisha kwamba katika kinyang'anyiro cha uchaguzi huo Mwenyekiti ambaye ambaye alikuwa anapambana kukitetea kiti chake Catherine Katele ameweza kuibuka mshindi kwa  kupata kura za halali zipatazo 33 huku mpinzani wake Ivo Ndukeki ameweza kupata kura za halali zipatazo 18.

"Nikiwa kama msimamizi wa uchaguzi huu wa Tughe Mkoa wa Pwani nimeweza kusimamia vizuri mwenendo mzima wa zoezi hili  la uchaguzi na ninashukuru Mungu kwamba zoezi hili limemalizika salama bila ya kuwa na kosaro ya aina yoyote ile na wagombea wotte wamekubaliana na matokeo ambayo yametokea kwani uchaguzi ulikwenda vizuri  na kila mgombea  ameridhika na ameweza kusaini fomu ,"amebainisha Msimamizi huyo.

Kwa upande wake  Mwenyekiti wa TUGHE Mkoa wa Pwani ambaye  ndiye alikuwa akitetea kiti hicho kwa mara nyingine amewashukuru kwa dhati wajumbe wote wa Mkutano mkuu wa kuweza kumuanmini kumchagua tena kwa mara nyingine na kwamba ataendelea kuwapa ushirikiano wa hali na mali katika  kukijenga chama bila kuwa na ubaguzi wowote,

Mwenyekiti huyo amesema kwamba kwa sasa mikakti ambayo amejiwekea ni kuweza kuimarisha  nguvu kazi katika sula zima la kuwatetea wafanyakazi katika kulinda maslahi yao na kwamba atakuwa nao bega kwa bega ili kuweza kuleta chachu ya maendelea katika nyanja mabali mbali mbali,

Pia hakusita kuelezea jinsi gani atakavyoweza kuwa na mipango madhubuti ya kuendelea kukiimarisha chama kuanzia ngazi za chini hadi Mkoa ikiwa pamoja na kutafuta fursa za kiuchumi  katika Wilaza zote za Mkoa wa Pwani na kuahidi kuwasaidia watu wenye ulemavu ili waweze kujikomboa.\

Mwenyekiti huyo amemshukuru na kumpa pomgeza Rais wa awamu ya Sita Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kusimama imara kwa kutenga fedga nyingi ambazo zimeleta matokeo chanya katika kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo .  

Katibu wa TUGHE Mkoa wa Pwani Jonas Rwegoshora amewapongeza viongozi wote ambao wamemeza kuchaguliwa katika mkutano huo na kwamba ataendelea kushirikiana nao bega kwa bega kwa ajili ya mashali mapana ya chama hicho.

Nao baadhi ya wagombea katika uchaguzi huo wamesema kwamba kwa sasa wataweza tofauti zao pembeni na kuungana kwa pamoja na viongozi wote ambao wamechaguliwa kwa lengo la kudumisha upendo amani na na kuleta chachu ya maendelea kwa maslahi ya watu wote hususan wanachama wa Tughe Mkoa wa Pwani na Taifa kwa ujumla.

 Katika uchaguzi mbali na kumchagua Mwenyekiti wameteuliwa wajumbe wa  nafasi mbali mbali ikiwemo nafasi za wawakilishi wa vijana, wawakilishi wa walemavu, pamoja na wajumbe wengine ambao wataweza kuwakilisha  katika ngazi za  Mkoa na Taifa katika mikutano mbali mbali.





Na George Maziku, Kahama
 
DIWANI wa Kata ya Majengo, Halmashauri ya Manispaa ya Kahama, wilayani Kahama, mkoa wa Shinyanga Shida Zacharia Soko amechangia chakula chenye thamani ya zaidi ya milioni 6 kwa ajili ya wanafunzi wanaosoma kwenye shule tatu zilizopo kwenye kata yake.
 
Chakula hicho amekitoa juzi katika mkutano wa wazazi wa wanafunzi wanaosoma katikà shule tatu za Mama Samia Sekondari, shule ya msingi Anderson Msumba na shule ya msingi Majengo.
 
Mkutano huo aliuitisha yeye mwenyewe kwa lengo la kuwahasisha wazazi kuchangia chakula kwa ajili ya watoto wao, ambapo mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa wilaya ya Kahama Frank Nkinda. 
 
Diwani huyo alitoa gunia 45 za mahindi yenye thamani ya milioni 2925000, maharage kilogramu 600 zenye thamani ya Sh. milioni 1200000, Mchele kilogramu 600 zenye thamani ya 12000, na sukari kilogramu 600  zenye thamani ya Sh. 1200000.

Akitoa mchanganuo wa mchango huo wakati akiukabidhi kwa Mkuu wa Wilaya, diwani Soko alisema kila shule itapata gunia 15 za mahindi, kilogramu 200 za maharage, kilogramu 200 za mchele na kilogramu 75 za sukari.

"Mheshimiwa mkuu wetu wa wilaya hapa mbele yako kuna pakeji (package) tatu ya chakula kwa ajili ya watoto wa shule ya sekondari ya Mama Samia, mimi ni mzee wa pakeji tu, hayo ndio mapigo yangu. Pakeji kama hii nimetoa kwa shule mbili za msingi za Anderson Msumba na Majengo", alifafanua Soko.

Akipokea mchango huo, mkuu wa wilaya Nkinda alimpongeza diwani  Soko kwa moyo wake wa kujitolea na kumtaka aendelee na moyo huo wa huruma na kujali wanyonge.

"Nakupongeza sana mheshimiwa diwani kwa moyo wako wa kutoa kwa wanyonge, wewe unaweza kufikiri haya unayofanya kuwa mambo madogo lakini nataka nikuambie kuwa haya ni mambo makubwa sana, ninakuomba uendelee na moyo huo na Mungu atakulipa", alisema mkuu wa wilaya Nkinda.

Aliongeza kuwa, " Nami nakuunga mkono kwa kuchangia kilogramu 500 za mahindi ambazo nitazitoa leo hii baada ya zoezi hili la kupokea mchango wako", alibainisha Nkinda.

Mkuu huyo wa wilaya alitoa wito kwa wazazi na wadau wengine wa maendeleo kuunga mkono juhudi za diwani Soko kwa kuchangia kwa wingi chakula cha watoto wao wanaosoma katikà shule hizo.

Diwani Soko amekuwa na utaratibu wa kuchangia chakula kwa wanafunzi wanaosoma katika shule tatu za kata yake tangu achaguliwe kushika wadhifa huo katika uchaguzi mkuu wa Oktoba, 2025.

Wakitoa maoni yao baadhi ya wazazi waliohudhuria mkutano huo waliunga mkono mpango wa kuchangia chakula cha wanafunzi ili kuwasaidia watoto kufuatilia vizuri masomo kutoka kwa walimu wao.
" Ni jambo zuri sana kwasababu itawasaidia watoto wetu kusoma kwa utulivu na kuelewa wanachofundishwa na walimu wao. Mimi nitachangia na ninawashauri wazazi wenzangu kuchangia kwa ajili ya ustawi wa watoto wetu", alisema Zuhura Rashid Salum ambaye ni mzazi wa mwanafunzi anaesoma shule ya msingi Majengo.

Naye Diana James aliyejitambulisha kuwa mzazi wa mwanafunzi anaesoma shule ya msingi Anderson Msumba alikubaliana na Mpango huo na kuahidi kuchangia.

"Mpango huu ni mzuri na muhimu sana kwasababu njaa ni mbaya, mtoto mwenye njaa hawezi kuzingatia kikamilifu masomo yake, hata sisi watu wazima hatuwezi kufanya kazi tukiwa na njaa, Mimi nipo tayari kuchangia chakula kwa mtoto wangu", alisema mzazi huyo.

Mkuu Wa Wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga Frank Nkinda akiwa katikà mkutano wa  hadhara wa wazazi ulioitishwa na diwani Wa Kata ya Majengo Zacharia shida Soko
Magunia 15 ya Mahindi yaliyotolewa na diwani Soko kwaajili ya Chakula katikà shule ya Sekondari Samia iliyopo Kata ya Majengo Manispaa ya kahama

Wazazi Wa wanafunzi Wa shule tatu zilizopo katikà Kata ya Majengo
Diwani Wa kata ya Majengo Zacharia SOKO akifuatilia hotuba ya mkuu Wa wilaya
 



Na Mwandishi Wetu
TAASISI ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), imezindua mfumo wa kidijitali wa usajili wa wagonjwa na teknolojia mpya ya kisasa ya Dozee ya kufuatilia hali ya mgonjwa hata kiwa nyumbani.

Uzinduzi huo ulifanyika jana jijini Arushwa ambapo mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini,Paul Makonda.

Alisema uwekezaji huo unaifanya Tanzania kuwa miongoni mwa nchi zinazoendelea kupiga hatua barani Afrika katika matumizi ya ubunifu wa kidijitali kuboresha huduma za matibabu na kutekeleza malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Makonda alisema matumizi ya teknolojia katika usajili wa wagonjwa, utunzaji wa kumbukumbu za kitabibu na ufuatiliaji wa wagonjwa baada ya matibabu ni sehemu ya maono ya Serikali ya kujenga taifa lenye uchumi unaotegemea maarifa, sayansi na teknolojia.

Katika kambi hiyo, Taasisi ya Moyo Mfumo wa teknolojia unaojulikana kitaalamu kama Dozee, una uwezo wa kufuatilia hali ya mgonjwa kwa wakati halisi akiwa amelazwa hospitalini au baada ya kuruhusiwa kurejea nyumbani.

Dozee ni mfumo unaotumia kifaa maalumu kinachowekwa chini ya godoro la mgonjwa na kufuatilia viashiria muhimu vya afya bila kulazimika kuunganisha vifaa vingi moja kwa moja kwenye mwili wake.

Dkt. Kisenge alisema mfumo huo una uwezo wa kufuatilia viashiria muhimu vya afya vya mgonjwa, vinavyojulikana kitaalamu kama vital signs, ikiwemo mapigo ya moyo, kiwango cha oksijeni kwenye damu na shinikizo la damu.

Alisema taarifa zinazokusanywa kupitia mfumo huo zinaweza kumfikia daktari kwa njia ya kidijitali, ikiwemo kupitia simu ya mkononi, hivyo kumwezesha kufuatilia mwenendo wa afya ya mgonjwa hata akiwa nje ya hospitali au anaendelea na shughuli nyingine.

Alifafanua kuwa teknolojia hiyo imelenga kusaidia kupunguza vifo vinavyoweza kuzuilika, hususan vinavyotokea baada ya hali ya mgonjwa kubadilika ghafla akiwa nyumbani baada ya kuruhusiwa kutoka hospitalini.

“Mara nyingi wagonjwa wanaporuhusiwa kwenda nyumbani, hali zao zinaweza kubadilika ghafla. Shinikizo la damu linaweza kushuka, mapigo ya moyo yanaweza kwenda kwa kasi sana au kiwango cha oksijeni kwenye damu kikapungua. Kupitia teknolojia hii, daktari anaweza kupata taarifa kwa wakati na kuchukua hatua mapema kabla hali ya mgonjwa haijawa mbaya,” alisema Dkt. Kisenge.

Alisema mfumo huo hautawanufaisha wagonjwa wa moyo na waliopata huduma za upasuaji pekee, bali unaweza pia kutumika kuwafuatilia wagonjwa wenye matatizo mengine ya kiafya.

Alitolea mfano wagonjwa wenye malaria kali, ambao wanaweza kupata mabadiliko ya ghafla ya mapigo ya moyo, shinikizo la damu na kiwango cha oksijeni kwenye damu.

Kwa mujibu wa Dkt. Kisenge, kufuatiliwa kwa viashiria hivyo kwa wakati kunaweza kuwasaidia wataalamu wa afya kubaini hatari mapema, kumfuata mgonjwa alipo, kumrudisha hospitalini inapohitajika na kumpatia matibabu sahihi.

Alisema uwekezaji katika mfumo huo unaifanya JKCI kuwa miongoni mwa taasisi zinazoongoza katika matumizi ya teknolojia za kisasa za kufuatilia wagonjwa, huku akieleza kuwa teknolojia ya aina hiyo inatumika pia katika nchi zikiwemo India na Marekani.

Dkt. Kisenge alisema mafanikio hayo yametokana na uwekezaji mkubwa unaofanywa na Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuimarisha huduma za afya za kibingwa na ubingwa bobezi nchini.


 SUBIRA IMEKWISHA! 😱⚽

Fainali ya FIFA WORLD CUP 2026 inakuja na Oryx Energies tuko tayari kuitazama pamoja nawe! 

Tukutane Mbagala Zakhem

Jumapili | 19 July 2026 

Tunayo kwa ajili yako: 

🎉 Screen kubwa 

🎧 Live DJ & Burudani 

🍔 Vyakula na vinywaji 

💯 Hakuna kiingilio 


Wacha mpira unoge! Tujaze uwanja tucheke, tupige kelele na tushangilie pamoja 🇹🇿

Tag rafiki zako wa mpira hapa chini 👇

#OryxEnergies #FIFAWorldCup2026 #Fainali #MpiraNiFursa #Mbagala #Tanzania #WorldCupFinal



By TBN Staff Writer, London


Swahili Ambassador for Africa and former First Lady of Tanzania, Her Excellency Salma Kikwete, has underscored the vital role of the Kiswahili language in promoting unity, preserving culture and advancing social and economic development across Africa and the wider world.


She said Kiswahili has evolved far beyond its East African roots to become a language of regional integration and international dialogue, bringing together people from diverse cultures, backgrounds and nations. According to her, the language continues to serve as a powerful tool for fostering mutual understanding, strengthening cooperation and encouraging peaceful coexistence among communities.


Mrs Kikwete further noted that the growing use of Kiswahili on international platforms is clear evidence of its expanding global significance. She said its increasing adoption by international organisations, educational institutions and diplomatic forums demonstrates the language’s unique ability to bridge cultures while showcasing Africa’s rich linguistic and cultural heritage.


She made the remarks during a special celebration marking World Kiswahili Language Day, held at the House of Lords in London. The event was hosted following an invitation from Lord Paul Boateng, a Member of the House of Lords and a long-time supporter of stronger relations between the United Kingdom and Africa.


The celebration brought together diplomats, parliamentarians, academics, cultural leaders and members of the African diaspora to recognise the remarkable growth of Kiswahili from a regional lingua franca into one of the world’s fastest-growing international languages. Discussions focused on its contribution to education, diplomacy, trade, literature, media and cultural exchange, as well as opportunities to further expand its teaching and use worldwide.


Mrs Kikwete called upon governments, universities and cultural institutions to continue investing in the promotion of Kiswahili, describing it as an important vehicle for advancing African identity and strengthening international partnerships. She observed that as Africa assumes an increasingly influential role in global affairs, Kiswahili is well positioned to become a leading language of diplomacy, commerce, innovation and intercultural communication.


She also commended initiatives aimed at encouraging young people, both across Africa and within the diaspora, to embrace and preserve the language for future generations, saying such efforts are essential in safeguarding one of the continent’s greatest cultural assets.


The event at the House of Lords further reflected the growing international recognition of Kiswahili since UNESCO established World Kiswahili Language Day, celebrated annually on 7 July, making it the first African language to be officially recognised with a dedicated international day by the United Nations system.










 

Na Vero Ignatus, Michuzi TV-Arusha

Serikali imeeleza kuwa ina matarajio makubwa kwa Mawakili wa Serikali katika kuhakikisha utekelezaji wa miradi ya kimkakati inayolenga kufanikisha Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050,

Matarajio hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Zainab Katimba, wakati akifunga mafunzo ya siku tatu ya Mawakili wa Serikali yaliyofanyika jijini Arusha kuanzia Julai 15 hadi 17, 2026.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Katimba amewataka Mawakili wa Serikali kuyatumia mafunzo hayo kuboresha utendaji wao wa kazi, ikiwemo kutoa ushauri wa kisheria, kuandaa na kupitia mikataba, kusimamia majadiliano ya kimkakati pamoja na kushughulikia mashauri kwa weledi na ufanisi.

Amesema Serikali inahitaji Mawakili wa Serikali wenye uwezo wa kuona mbali, kufikiri kimkakati na kutumia sheria kama nyenzo ya maendeleo ili kuhakikisha kila uamuzi wa Serikali unalinda maslahi ya Taifa, unakuza uchumi na kuchochea utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

"Imani yangu kwenu ni kubwa kuwa ninyi mliohudhuria mafunzo haya mtakuwa sehemu ya kizazi cha Mawakili wa Serikali kitakachoiwezesha Taifa kufikia matarajio makubwa ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050," amesisitiza Mhe. Katimba.

Awali akimkaribisha mgeni rasmi, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Samwel M. Maneno, alisema mafunzo hayo yamewapa washiriki fursa ya kujadili na kujifunza masuala mbalimbali ya kimkakati yatakayowawezesha kutekeleza majukumu yao kwa weledi, ubunifu na ufanisi zaidi katika kulinda na kutetea maslahi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mhe. Maneno alieleza kuwa mafunzo hayo yalijikita katika usimamizi wa majadiliano na mikataba ya kimkakati, usuluhishi wa migogoro, ubia kati ya sekta ya umma na binafsi (PPP), usimamizi wa vihatarishi vya kisheria (Legal Risk Management), pamoja na matumizi ya Akili Unde (AI) katika taaluma ya sheria.

Aidha, aliwataka Mawakili wa Serikali kuendelea kutekeleza maelekezo yaliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Mawakili wa Serikali (TPBA) 2026. 

Pia aliwasisitiza kusoma na kutafakari kwa kina kitabu cha Mama Samia Doctrine of Law ili kuelewa falsafa ya uongozi wa Rais na kuongeza kasi pamoja na ubora katika uchakataji wa masuala ya kisheria, hususan upekuzi na uandaaji wa mikataba kwa kuzingatia sheria, kanuni, miongozo na maslahi ya Taifa.

Mafunzo hayo ya Bespoke 2026 yalifanyika chini ya kaulimbiu "Repositioning State Attorneys for Strategic Legal Leadership in Realizing Tanzania Development Vision 2050," yakihusisha Mawakili wa Serikali kutoka Wizara, Idara Zinazojitegemea, Wakala za Serikali pamoja na Mamlaka za Serikali za Mitaa (RS na LGAs) kwa lengo la kuimarisha uongozi wa kisheria katika kufanikisha Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.








Na Seif Mangwangi, Michuzi TV Arusha

SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar imesema ina mikakati ya kuleta madereva kutoka visiwani humo kuja katika chuo cha ufundi Arusha (ATC), kujifunza ujuzi wa kuendesha magari tofauti ikiwemo ya viongozi na kuepusha ajali zinazotokea mara kwa mara.

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa wizara ya ujenzi na uchukuzi Zanzibar, Badria Atai Masoud, Julai16, 2026 alipofanya ziara katika chuo cha ufundi Arusha na kujionea mitambo mbalimbali inayotumika kufundishia wanafunzi chuoni hapo ikiwemo karakana ya magari.

Amesema katika ziara hiyo amegundua chuo cha ufundi Arusha kina ujuzi na uwezo mkubwa wa teknolojia ikiwemo matumizi ya umeme jua kuendeshea mitambo hivyo wataona namna ya kufanya ushirikiano na chuo hicho Ili kutoa msaada kwa madereva visiwani humo.

Aidha amesema amefurahishwa na ushirikiano unaoendelea kati ya chuo cha ufundi Arusha (ATC), na kampuni ya usafirishaji ya Abnan Transport and Logistic Ltd ambapo chuo hicho kinafundisha walimu wa madereva kupitia kampuni hiyo.

“ Zanzibar tumekuwa na ongezeko la ajali za barabarani ambazo zimekuwa zikisababisha vifo na ulemavu kwa watu wengi, tunaamini ushirikiano huu unaoendelea na ule ambao tutaufanya hapo baadae utasaidia kuepusha ajali,” amesema.

Wakati huo huo, Naibu Waziri Badria amesema Serikali visiwani humo  imeanza mchakato wa kuondoa matumizi ya magari ya mafuta ndani ya Serikali yake na  kuanza kutumia magari ya umeme.

Amesema Serikali ya Zanzibar imeanza kubadilisha mfumo wa injinia za magari yake na kutumia umeme, na kwamba mfumo huo umeanzia kwenye magari ya umma ya usafirishaji na baadae wataendelea kwa magari ndani ya Serikali.

“ Chini ya Rais Dkt Hussein Alli Mwinyi, tumeanza kutumia magari ya umeme hasa kwa magari ya usafiri wa umma, na tutaendelea hadi kwenye magari ndani ya Serikali, naamini tutawatumia sana chuo hiki,” amesema.

Awali Mkuu wa Chuo cha ufundi Arusha, Profesa Mussa Chacha alisema chuo chake kimeingia ushirikiano na taasisi ya Abnan Transport and Logistic Limited ambapo walimu kutoka ATC wako visiwani humo wakiwafundisha walimu na madereva kozinya udereva.

Profesa Chacha amesema chuo cha ufundi ATC kimeshaanza utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050 Kwa kuanzisha vitengo vitakavyotumiwa na wanafunzi kujifunza ujuzi mbalimbali kutokana na bunifu wanazozifanya chuoni hapo.

“ Tumeshaanza utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050, hivi sasa tunajenga karakana ambayo itatumika kutengeneza vipuri vya magari na mitambo na hapa wanafunzi wetu ndio watakuwa wakitumia mitambo hiyo kuzalisha, pia jengo hilo litakuwa na karakana ya kutengeneza fenicha mbalimbali, tutakuwa tunatengeneza na kuuza,” amesema na kuongeza:

“ Pia tunakamilisha jengo la hospitali ambalo mbali ya kutoa huduma Kwa wagonjwa wanafunzi na wengine kutoka, nje pia wale wanafunzi wanaotengeneza bidhaa za hospital watatumia nafasi hiyo kujifunza badala ya kusubiri Hadi waendesha field,” .






Top News