Na Karama Kenyunko, Michuzi TV
MKURUGENZI Muendeshaji wa shirika lisilo la kiserikali (MSI) Tanzania, Dkt. Stephen Mutegeki, amesema utekelezaji wa Programu ya Scaling Up Family Planning (SuFP) kwa kipindi cha miaka tisa umechangia kwa kiasi kikubwa kusogeza huduma za afya ya uzazi na uzazi wa mpango karibu na wananchi, hususan wanawake, vijana, watu wenye ulemavu na makundi mengine yaliyokuwa magumu kufikiwa.

Dkt. Mutegeki ameyasema hayo leo jijini Dodoma wakati wa Kongamano la Kujifunza la Programu ya SuFP lililofanyika chini ya kaulimbiu isemayo, “Kudumisha Mafanikio Yaliyopatikana katika Afya ya Uzazi na Uzazi wa Mpango.”

Amesema MSI Tanzania, kama mmoja wa washirika wa utekelezaji wa programu hiyo iliyofadhiliwa na Serikali ya Uingereza kupitia Foreign, Commonwealth and Development Office (FCDO), imejikita katika kuimarisha mifumo ya afya ya umma, kuboresha ubora wa huduma na kujenga uwezo wa wataalamu wa afya ili kuhakikisha huduma bora zinawafikia wananchi wengi zaidi.

Kwa mujibu wa Dkt. Mutegeki, kupitia programu hiyo MSI Tanzania ilipeleka timu 12 za huduma za mkoba katika mikoa 12 ili kufikisha huduma za afya ya uzazi katika maeneo ya pembezoni na magumu kufikika.

Aidha, wauguzi 28 walipangwa katika mikoa 14 kwa ajili ya kutoa ushauri wa kitaalamu na kujenga uwezo wa watumishi wa afya katika vituo vya umma.

Alisema vituo vya afya vya umma 176 vilipatiwa mafunzo na usimamizi wa kitaalamu, huku watoa huduma za afya 469 wakipatiwa mafunzo maalumu ya utoaji wa huduma bora za uzazi wa mpango na afya ya uzazi.

“Zaidi ya wataalamu wa afya 1,180 wamenufaika na programu za uangalizi na ushauri kazini zilizolenga kuimarisha ubora wa huduma,” amesema.

Akizungumzia huduma kwa vijana, Dkt. Mutegeki amesema MSI Tanzania imetekeleza zaidi ya matukio 32 katika taasisi za elimu ya juu pamoja na miradi 32 ya Human-Centred Design iliyolenga kuongeza upatikanaji wa taarifa na huduma za afya ya uzazi kwa vijana na balehe.
Kwa upande wake, Mtaalamu wa Afya ya Mama na Uzazi ambaye pia ni Mkurugenzi Mkazi wa EngenderHealth, Dkt. Moke Magoma, amesema programu hiyo ililenga kuongeza upatikanaji wa huduma jumuishi za uzazi wa mpango kwa makundi mbalimbali ya wananchi.

Amesema huduma hizo pia zilihusisha uchunguzi wa Virusi vya Ukimwi (VVU), utoaji wa msaada kwa waathirika wa ukatili wa kijinsia pamoja na kuwaelekeza kupata huduma stahiki. Aidha, programu hiyo ilisaidia kuboresha vituo vya afya vya serikali ili kuhakikisha vinatoa huduma bora kwa wanawake waliopoteza ujauzito.

“Tulilenga kufikisha huduma za uzazi wa mpango kwa makundi ambayo hayakuwa yakifikiwa kwa urahisi, hususan vijana balehe, watu wenye ulemavu na wananchi wanaoishi katika maeneo ya mbali,” amesema.

Dkt. Magoma amesema pia walihakikisha mifumo ya utoaji wa huduma inaboreshwa, ukusanyaji wa takwimu unafanyika kwa ufasaha na ubora wa huduma unafuatiliwa kwa karibu kwa kuhamia kutoka mfumo wa makaratasi kwenda mfumo wa kidijitali.
Naye Mwakilishi wa UNFPA Tanzania, Mark Bryan Schreiner, amesema zaidi ya watu milioni 5.2 wamefikiwa na huduma za uzazi wa mpango kati ya mwaka 2017 na 2026.

Amesema hatua hiyo imechangia kuzuia mimba zisizotarajiwa milioni 8.3, utoaji mimba usio salama milioni 2.3 na vifo vya wajawazito 6,511.

Kwa mujibu wa takwimu zilizowasilishwa katika kongamano hilo, programu ya SuFP ilitekelezwa katika mikoa 22 ya Tanzania na kusaidia kuimarisha mifumo ya ugavi wa dawa na vifaa tiba, usimamizi wa taarifa za kidijitali na uwezo wa wahudumu wa afya katika kutoa huduma bora za afya ya uzazi.

Mbali na kuimarisha huduma za afya, programu hiyo ilitoa kipaumbele kwa vijana, watu wenye ulemavu na jamii zilizo katika mazingira magumu kupitia ubunifu mbalimbali, ikiwemo mfumo wa kidijitali wa i-Plan uliorahisisha upatikanaji wa taarifa na huduma za afya ya uzazi.

“Kuna umuhimu wa kuongeza uwekezaji wa ndani katika sekta ya afya ili kuhakikisha mafanikio haya yanaendelea kudumu wakati ambapo misaada ya maendeleo kutoka nje inaendelea kupungua duniani,” amesema.

Programu ya SuFP ilitekelezwa kwa ushirikiano wa UNFPA, MSI Tanzania, EngenderHealth, Pathfinder International, CCBRT, DKT na International Rescue Committee (IRC), kwa ufadhili wa Serikali ya Uingereza kupitia FCDO.

Vichwa vingine vya habari unavyoweza kutumia ni:
SuFP Yafikia Zaidi ya Watu Milioni 5.2 kwa Huduma za Uzazi wa Mpango.



Picha ya pamoja.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, amesema Tanzania ni miongoni mwa nchi chache barani Afrika zilizofanikiwa kusambaza huduma ya umeme  vijijini, hatua ambayo imewezesha wananchi wengi kupata huduma hiyo kutoka ngazi za mikoa, wilaya, kata na vijiji, huku sasa juhudi zikielekezwa katika kufikisha umeme kwenye vitongoji.

Akizungumza na wananchi wa Kata ya Hogoro wilayani Kongwa mkoani Dodoma wakati wa ziara ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi, Senyamule alisema serikali inatarajia kupeleka umeme katika vitongoji sita vya kata hiyo katika mwaka ujao wa fedha.

Alieleza kuwa matarajio ya serikali ni kuhakikisha vitongoji vyote vinapata huduma ya umeme ifikapo mwaka 2030, jambo litakalosaidia kuongeza maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa wananchi.

“Zamani wananchi walitegemea chemli na vibatari kwa ajili ya mwanga, lakini sasa serikali imeona umuhimu wa kupeleka umeme karibu na wananchi ili waweze kupata mwanga wa uhakika na kufanya shughuli mbalimbali za kiuchumi zinazowaongezea kipato na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa.”

Katika sekta ya elimu, Mkuu huyo wa Mkoa alisema Serikali ya Awamu ya Sita imefanikisha ujenzi wa shule nyingi zaidi kuliko vipindi vilivyotangulia, huku akiwataka wazazi na walezi kuhakikisha watoto wote wanapata fursa ya elimu.

Alisisitiza kuwa dhamira ya serikali ni kuona kila Mtanzania anajua kusoma na kuandika katika miaka ijayo ili kuwaandaa wananchi kukabiliana na ushindani wa dunia ya sasa inayokua kwa kasi katika nyanja za sayansi na teknolojia.

“Dunia ya leo imekuwa kama kijiji kutokana na maendeleo ya teknolojia. Elimu na ujuzi ni nyenzo muhimu zinazoweza kumpa mtu fursa ya kufanya kazi na kuishi popote duniani”.

Aidha, Senyamule alisema serikali imeendelea kuboresha huduma za afya kwa kujenga na kuimarisha zahanati, vituo vya afya na hospitali pamoja na kuweka mazingira rafiki ya utoaji huduma.

Kutokana na maboresho hayo, alisema hakuna sababu ya wanawake wajawazito kujifungulia nyumbani kwani huduma bora za afya sasa zinapatikana karibu na wananchi, hatua inayolenga kupunguza vifo vya mama na mtoto wakati wa kujifungua.





-Nchi nane wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki zitakutana Bujumbura, Burundi katika kuadhimisha siku ya Kiswahili Duniani pamoja na Kongamano la Kakama.


Na Vero Ignatus

Kamisheni ya Kiswahili ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (Kakama) imetangaza maadhmisho ya Siku Kiswahili kuwakutanisha wananchi kutoka mataifa nane ya Afrika Mashariki mjini Bujumbura, Burundi.

Akizungumza na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali, Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Kiswahili (Kakama), Dk Caroline Asiimwe amesema maadhimisho hayo yatafanyika kuanzia Julai 5-7 Julai, 2026.

Amesema maadhmisho ya Kiswahili yatatanguliwa na Kongamano la Tatu ka Kakama na kufuatiwa na Siku ya Kiswahiki Duniani Julai 7.

Amesema maadhimisho ya kongamano la Kakama yamkuwa yakifanyika kila baada ya miaka miwili na kutoa fursa kwa kila nchi wanachama.

Amesisitiza kwamba kupitia maadhimisho hayo yamewezesha wananchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kunufaika na fursa mbalimbali kupitia Kiswahili.

Dk Asiimwe: Kiswahili chafikia hadhi kimataifa kuchangia maendeleo

Aidha lugha ya Kiswahili imetajwa kufikia hadhi ya kimataifa kiwango cha kuwezesha kuwa na mchango wa maendeleo katika nchi wanachama Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Amesema lugha ya Kiswahili inaweza kumwezesha mwekezaji kuchangamkia fursa mbalimbali zilizopo katika nchi husika kutokana na kutumika na takribani nchi nane wanachama wa jumuiya.

Dk Asiimwe amesema lugha ya Kiswahili inamwezesha hata mjasiriamali na mfanyabiashara aliyepo kijijini kuamua kuchagua lugha atakayo kupitia akili unde ili kumwezesha kuwasiliana kikamilifu.

Amesema kutokana na maendeleo ya teknolojia, yamewasukuma katika maadhimisho ya Kiswahili Duniani na Kongamano la Tatu yatakayoanyika Bujumbura Julai 5-7 mwaka huu kubeba mjadala wa akili unde na wingi lugha.


 

Meneja Miradi wa Benki ya Absa, Bi. Munira Chambuso akizungumza katika semina iliyoandaliwa na benki hiyo kwa  kushirikiana na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) kwa wanawake wajasiriamali wadogo na wa kati, ikihuhusu   elimu ya fedha na  usimamizi wa uwekezaji, jijini Dar es Salaam jana.

Meneja wa Huduma za Jamii na Matukio wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Abigail Lukuvi (wa pili kutoka kushoto),  akizungumza na baadhi ya washiriki, katika semina iliyoandaliwa na benki hiyo kwa  kushirikiana na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) kwa wanawake wajasiriamali wadogo na wa kati ikihusu   elimu ya fedha na  usimamizi wa uwekezaji, jijini Dar es Salaam jana.

Mkurugenzi wa Wanachama wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Bi. Kinanasy Seif akizngumza katika semina iliyoandaliwa na Benki ya Absa Tanzania kwa kushirikiana na taasisi hiyo kwa wanawake wajasiriamali wadogo na wa kati, ikihusu  elimu ya fedha na  usimamizi wa uwekezaji, jijini Dar es Salaam jana.

Meneja Bidhaa Kitengo cha Biashara wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Devroda Kagusa, akizungumza katika semina iliyoandaliwa na benki hiyo kwa  kushirikiana na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), kwa wanawake wajasiriamali wadogo na wa kati, Ikihusu   elimu ya fedha na  usimamizi wa uwekezaji, jijini Dar es Salaam jana.


 Ofisa Elimu kwa Mlipa Kodi na Mawasiliano wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Zephania Mange, akitoa elimu kuhusu wajibu wa mlipa kodi katika semina iliyoandaliwa na Benki ya Absa Tanzania kwa  kushirikiana na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), kwa wanawake wajasiriamali wadogo na wa kati, Ikihusu   elimu ya fedha na  usimamizi wa uwekezaji, jijini Dar es Salaam jana

Wawakilishi kutoka Benki ya Absa na TPSF, wakipiga picha ya kumbukumbu pamoja na washiriki wa semina hiyo pamoja na wawezeshaji wengine, mara baada ya kumalizika kwa semina hiyo, jijini Dar es Salaam jana.


📍 Chinangali Park, Dodoma

TAWIRI  imeendelea kutoa elimu  kwa wadau wakiwepo  wananchi ambapo wakulima wamepata elimu ya umuhimu wa wadudu katika  uhifadhi endelevu wa wanyamapori sambamba na mchango wa wadudu katika kilimo ikiwa ni pamoja na uchavushaji.

Vilevile wananchi wamepata uelewa  juu ya juhudi zinazofanywa na TAWIRI chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii za kuwahifadhi wanyamapori kwa kutumia taarifa sahihi za kisayansi.

“tunashukuru kwa elimu nzuri, kabla ya elimu hii nilijua wanyamapori wanakaa porini wanajihudumia lakini leo nimepata uelewa  wanyamapori wanatibiwa, wanahesabiwa, wanafuatiliwa mienendo yao kwa kutumia teknolojia” 

amesema  Enderesa Salla miongoni mwa wananchi waliotembelea banda la TAWIRI

TAWIRI tunawakaribisha wananchi na wadau mbalimbali kuja kupata elimu ya sayansi ya wanyamapori  kwa ustawi wa uhifadhi na kukuza Utalii.



Na Said Mwishehe,Michuzi TV


RAIS wa Jamhuri ya Namibia, Dkt. Netumbo Nandi-Ndaitwah amewasili nchini Tanzania kwa ziara ya Kitaifa ya siku tatu kwa mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Akiwa nchini Rais Dkt. Nandi-Ndaitwah anatarajiwa kufanya mazungumzo ya uwili na mwenyeji wake, Rais Dkt. Samia kwa lengo la kuimarisha zaidi ushirikiano katika sekta mbalimbali zenye manufaa kwa Wananchi wa Tanzania na Namibia.

Pia Rais Ndaitwah na mwenyeji wake Rais Dk.Samia wanatarajiwa kushuhudia utiaji saini wa hati mbalimbali za makubaliano ya ushirikiano kati ya Nchi hizo mbili.

Aidha pamoja na mambo mengine inaelezwa kwamba ziara hiyo inakwenda kufungua fursa zaidi za kiuchumi kati ya nchi hizo ambazo zimekuwa na urafiki wa kindugu na wa kihistoria kwa muda mrefu.

Akizungumzia ziara hiyo alipokuwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam wakati wa mapokezi ya Rais Ndaitwah, Balozi wa Tanzania nchini Namibia, Caesar Waitara, amesema ziara hiyo ni ishara ya uhusiano wa muda mrefu na wa kihistoria uliopo kati ya mataifa hayo mawili, huku akisisitiza kuwa ziara hiyo inaleta manufaa makubwa katika utekelezaji wa diplomasia ya uchumi.

Balozi Waitara anasema Rais wa Namibia anaitazama Tanzania kama nyumbani kwake kutokana na historia yake ya kuishi nchini kwa miaka sita alipokuwa mwakilishi wa chama cha SWAPO katika nchi za Afrika Mashariki.

Anabainisha kuwa makao yake yalikuwa katika eneo la Magomeni jijini Dar es Salaam, jambo linaloimarisha zaidi uhusiano wake binafsi na Tanzania.

“Ujio wake unaonyesha jinsi uhusiano kati ya Tanzania na Namibia ulivyo imara na wa muda mrefu. Kila mara anapokuja Tanzania anajisikia kama yuko nyumbani,” anasema Waitara.

Anaeleza kuwa Namibia inaendelea kuthamini mchango wa Tanzania katika harakati za ukombozi wa taifa hilo, hususan kupitia kambi za wapigania uhuru zilizokuwa Kongwa pamoja na msaada wa mafunzo ya kijeshi uliotolewa kwa wapigania uhuru wa Namibia.

Kwa mujibu wa balozi huyo, pamoja na historia ya ukombozi, mataifa hayo sasa yamejikita zaidi katika kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi kupitia biashara, uwekezaji na kubadilishana uzoefu katika sekta mbalimbali za maendeleo.

Waitara anasema Tanzania inaendelea kusukuma mbele ajenda ya diplomasia ya uchumi kupitia balozi zake nje ya nchi kwa lengo la kuvutia uwekezaji na kufungua fursa za biashara.

Anataja uwekezaji wa Watanzania nchini Namibia kuwa ni mfano wa mafanikio ya ushirikiano huo, ambapo baadhi ya Watanzania wameanzisha biashara na taasisi za elimu.

Anabainisha kuwa kuna chuo kikuu nchini Namibia kinachomilikiwa kwa asilimia 100 na Mtanzania, ambacho kinatoa elimu ya shahada, shahada za uzamili na uzamivu, huku kikiwa na zaidi ya wanafunzi 10,000.

Aidha, Watanzania wengine wanaendelea kufanya biashara mbalimbali nchini humo, wakati WanaNamibia wamewekeza Tanzania katika sekta za utalii na mawasiliano.

Katika kuimarisha mahusiano ya kitamaduni, Waitara anasema ubalozi wa Tanzania kwa kushirikiana na Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) umeanza kutoa mafunzo ya lugha ya Kiswahili kwa njia ya mtandao nchini Namibia.

Anafafanua wanafunzi 26 walihitimu mafunzo ya awali mwaka jana, huku kundi jipya la wanafunzi 40 likitarajiwa kuanza masomo hivi karibuni.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, akizungumzia ziara ya Rais wa Namibia anasisitiza ni uthibitisho kuwa mahusiano ya kihistoria kati ya mataifa hayo sasa yamepanuka na kuwa ushirikiano mkubwa wa kiuchumi.

Anasema maboresho makubwa yaliyofanyika katika Bandari ya Dar es Salaam yanaifanya Tanzania kuwa lango muhimu la biashara kwa nchi nyingi za ukanda wa Kusini mwa Afrika, jambo linaloweza kuongeza ushirikiano wa kibiashara kati ya Tanzania na Namibia.

Wakati Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro, anasema mafanikio ya diplomasia ya uchumi hayawezi kupatikana bila kuwepo kwa usalama.

Ananasisitiza kuwa amani na utulivu wa Tanzania ndiyo msingi unaowezesha viongozi wa kimataifa kutembelea nchi na wawekezaji kuendelea kuwekeza.

“Usalama ni mtaji muhimu wa uchumi. Bila usalama hakuna biashara, hakuna uwekezaji wala maendeleo. Ni jukumu la kila mwananchi kuendelea kuilinda amani ya nchi yetu,” anasema Kamanda Muliro.

Ziara ya Rais wa Namibia nchini Tanzania inatarajiwa kuimarisha zaidi ushirikiano wa kihistoria, kiuchumi na kitamaduni kati ya mataifa hayo mawili, huku ikifungua fursa mpya za biashara, uwekezaji na maendeleo kwa wananchi wa pande zote mbili.


Na Chalila Kibuda ,Michuzi TV

SERIKALI imeitaka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kujiandaa mapema kukabiliana na mabadiliko makubwa ya kiuchumi na kiteknolojia yanayotarajiwa katika miaka 30 ijayo, ikieleza kuwa zaidi ya asilimia 70 ya shughuli za kiuchumi zitakuwa zikifanyika kwa njia za kidijitali.

Hayo ameyasema na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Nsubili Joshua, kwa niaba ya Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omary, wakati wa Kongamano la Miaka 30 ya TRA tangu kuanzishwa kwake mwaka 1996, lililoandaliwa na TRA kupitia Chuo cha Kodi.

Joshua alisema mabadiliko ya teknolojia yanayoendelea duniani yanahitaji TRA kuwa mbele ya wakati kwa kuandaa mifumo madhubuti ya usimamizi wa kodi itakayoweza kukusanya mapato kutoka biashara za mtandaoni na huduma zinazovuka mipaka ya nchi.

Alisema pamoja na mafanikio makubwa yaliyopatikana katika kipindi cha miaka 30 ya TRA, bado kuna haja ya kuimarisha mifumo ya kodi ili iendane na kasi ya maendeleo ya uchumi wa kidijitali unaotarajiwa kutawala katika miaka ijayo.

“Katika miaka 30 ijayo zaidi ya asilimia 70 ya shughuli za kiuchumi zitafanyika kwa njia za kidijitali hivyo TRA inapaswa kuwa tayari kuhakikisha mapato ya Serikali yanakusanywa kwa ufanisi bila kuathiri mazingira ya biashara na ubunifu,” amesema Joshua.

Alifafanua kuwa lengo la Serikali si kuzuia maendeleo ya teknolojia, bali kuhakikisha kunakuwa na usawa wa kodi na ulinzi wa mapato ya taifa huku mazingira bora ya uwekezaji na ushindani wa haki yakiendelea kudumishwa.

Aidha, aliitaka TRA kuongeza uwekezaji katika matumizi ya akili mnemba (AI), uchambuzi wa takwimu na mifumo ya ufuatiliaji wa miamala kwa wakati halisi ili kubaini mianya ya ukwepaji kodi na kuimarisha uwazi katika ukusanyaji wa mapato.

Joshua alisema matumizi ya teknolojia hizo yatasaidia kugundua udanganyifu mapema, kupunguza mawasiliano yasiyo ya lazima kati ya walipakodi na maafisa wa kodi pamoja na kuongeza ufanisi wa utoaji huduma.

Pia aliitaka TRA kuendelea kubuni mifumo rahisi ya usajili, ukadiriaji na ulipaji kodi kwa sekta isiyo rasmi ikiwemo wafanyabiashara wadogo na wakulima, ili kupanua wigo wa walipakodi na kuongeza mapato ya ndani.

Alisema mafanikio ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 yatategemea kwa kiasi kikubwa uwezo wa nchi kukusanya mapato ya ndani na kuyasimamia kwa ufanisi, jambo linaloifanya TRA kuwa na jukumu muhimu katika safari ya maendeleo ya taifa.

Joshua alisisitiza kuwa ushirikiano kati ya TRA, wafanyabiashara, watafiti na wadau wengine wa kodi ni muhimu katika kujenga mfumo wa kodi unaoendana na mahitaji ya uchumi wa kisasa na kuhakikisha Tanzania inanufaika kikamilifu na mapinduzi ya teknolojia yanayoendelea duniani.
Kamishina Mkuu wa TRA CPA Yusuph Mwenda akitoa maelezo kuhusiana tangu kuanzishwa mamlaka ya Mapato katika kongamano la miaka 30 tangu Kuanzishwa lililofanyika Ukumbi wa Serena ,jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Nsubili Jushua akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Fedha Balozi Khamis Mussa Omary wakati akizindua Kongamano la Miaka 30 ya Mamlaka ya Mapato (TRA) lililofanyika Ukumbi wa Serena Jijini Dar es Salaam.

Mkuu wa Chuo cha Kodi Profesa Isaya Jairo akizungumza kuhusiana na kuratibu Kongamano hilo kwa lengo kukutanisha wadau kujadiliana miaka 30 ijayo juu utendaji wa TRA.jijini Dar es Salaam.



Picha za pamoja za Makundi katika kongamano la TRA


- Mikopo ya mifugo NMB yavuka Sh180 bilioni.

Ubena Zomozi; Benki ya NMB imetoa zaidi ya Sh180 bilioni kufadhili wafugaji na biashara katika mnyororo wa thamani wa mifugo, ikiwemo unenepeshaji, uzalishaji wa malisho, ununuzi wa mbegu bora na ujenzi wa miundombinu ya kisasa.

Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa NMB, Filbert Mponzi, alisema hayo katika ufunguzi wa Tri-Nations Livestock Expo 2026 uliofanywa na Waziri Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba, katika viwanja vya Mbogo Ranches, Ubena Zomozi, Chalinze. NMB ni mdhamini mkuu kwa mwaka wa nne mfululizo.

Mponzi alisema mikopo hiyo inatolewa kwa riba nafuu ya asilimia tisa, huku mkakati wa NMB wa agribusiness na agri-wholesale ukilenga kufadhili wafugaji, wazalishaji wa malisho, wanunuzi, wasindikaji na biashara kubwa katika sekta hiyo.

Dk. Nchemba aliwataka wafugaji kutumia elimu na teknolojia inayopatikana katika maonesho hayo kukabiliana na uhaba wa malisho na kuongeza tija.

NMB imesema itaendelea kutoa elimu ya fedha, ushauri wa biashara, mikopo na bima kupitia matawi 248, mawakala zaidi ya 75,000 na huduma za kidijitali ili kusogeza huduma karibu zaidi na wafugaji nchini.

Waziri Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba, akisikiliza maelezo kutoka kwa Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa NMB, Filbert Mponzi, kuhusu mikopo, elimu ya fedha na huduma za kibenki kwa wafugaji alipotembelea banda la NMB katika Tri-Nations Livestock Expo 2026, Mbogo Ranches, Ubena Zomozi wilayani Chalinze, mkoani Pwani. 








MECHI ya Leo Juni 20 saa 20:00 usiku katika Uwanja wa NRG, Houston, ni pambano la kilele katika Kundi F. Netherlands wanaanza kwa sare ya 2-2 dhidi ya Japan, huku Sweden wakiongelea kwa ushindi wa 5-1 dhidi ya Tunisia.

Ushindi hapa utaiweka Sweden kwenye pointi sita na kuhakikisha kufuzu, huku Netherlands wakitafuta pointi tatu muhimu baada ya kukosa ushindi katika mechi yao ya kwanza.

Netherlands wana kikosi timamu bila majeruhi wapya, wakiongozwa na nahodha Virgil van Dijk katika safu ya ulinzi pamoja na Frenkie de Jong katika safu ya kati. Hata hivyo, wamepoteza mshambuliaji Xavi Simons kutokana na jeraha, lakini Donyell Malen yuko katika kiwango kizuri akiwa na mabao 14 katika Serie A tangu Januari. Sweden wana jozi ya washambuliaji hatari Viktor Gyökeres na Alexander Isak, ambao wote walifunga katika ushindi dhidi ya Tunisia, pamoja na Yasin Ayari aliyefunga mabao mawili.

Katika historia ya michezo yao kati ya timu hizi, Netherlands wana rekodi nzuri zaidi kwa ushindi 11, sare 6, na kushindwa 8 katika mechi 25 zilizopita. Mechi zao za mwisho katika mashindano makubwa zilimaliza sare 0-0 katika Kombe la Dunia 1974 na michuano ya Ulaya 2004.

Ingia kwenye kasi ya kujishindia pesa kwenye michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Katika mechi ya mwisho kati yao mwaka 2017, Netherlands ilishinda 2-0 katika mechi ya kufuzu michuano hii ya Dunia. Sweden wanakuja na ari kubwa baada ya ushindi wa 5-1, huku Netherlands wakijaribu kurejea baada ya sare yao.

Kocha Ronald Koeman anatakiwa kutatua changamoto ya safu ya ushambuliaji baada ya kuongoza mara mbili dhidi ya Japan lakini kupewa sare. Atategemea wachezaji kama Cody Gakpo na Donyell Malen kuongeza kasi ya mashambulizi.

Kocha Graham Potter wa Sweden atatumia jozi yake ya washambuliaji wenye kasi na nguvu Gyökeres na Isak kuchunguza ulinzi wa Netherlands, ambao ulionyesha udhaifu dhidi ya Japan. Pambano kati ya Van Dijk na Gyökeres litakuwa muhimu sana katika mechi hii.

VIJANA wengi leo wanatafuta fursa za kuongeza kipato huku wakifurahia burudani ya kisasa. Meridianbet imekuja na Aviator, mchezo wa kasino mtandaoni unaovutia maelfu ya wachezaji kwa kasi yake, msisimko wake na nafasi za ushindi mkubwa. Kila raundi ni nafasi mpya ya kujipatia tabasamu na kusogeza malengo yako mbele.

Aviator ni mchezo unaohitaji umakini na maamuzi ya haraka. Unapochagua muda sahihi wa kutoa dau lako kabla kindege hakijapaa mbali, unaweza kujikusanyia ushindi mzuri ndani ya muda mfupi. Hii ndiyo sababu watu wengi wameufanya kuwa mchezo wao wa kwanza kila siku.

Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya MERIDIANBET au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Zaidi ya ushindi wa kawaida, Meridianbet imeongeza hamasa kwa zawadi za kipekee. Kila wiki washindi wawili wanapata nafasi ya kujinyakulia simu mpya ya Samsung Galaxy A26 kwa kucheza Aviator na kukusanya pointi zao kadri wanavyoendelea kufurahia mchezo.

Usikose nafasi hii ya kipekee. Jiunge Meridianbet leo, cheza Aviator na anza safari yako ya ushindi. Kindege kimewashwa, zawadi zipo na nafasi ya kuwa mshindi mkubwa inaweza kuwa yako wakati wowote.

 Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), mdhamini mkuu wa Ligi ya NBC Championship, imejivunia mafanikio yanayoendelea kushuhudiwa katika mchezo wa soka nchini huku ikikabidhi kombe la ubingwa wa msimu wa 2025/2026 kwa Geita Gold FC, timu iliyotwaa taji hilo baada ya kumaliza ligi ikiwa kileleni kwa alama 77.

Ubingwa huo unaipa Geita Gold FC tiketi ya kushiriki Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2026/2027 sambamba na Kagera Sugar FC iliyomaliza nafasi ya pili kwa alama 71 na hivyo nayo kufuzu kushiriki ligi hiyo.

Kombe hilo lilikabidhiwa jana katika Uwanja wa Nyankumbu, Geita, baada ya Geita Gold FC kuhitimisha msimu kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Big Man FC ya Lindi katika mechi iliyoshuhudiwa na mamia ya mashabiki pamoja na viongozi mbalimbali wa soka, serikali na vyama vya siasa.

Katika hafla hiyo, Mkuu wa Biashara wa NBC Kanda ya Ziwa, Mafwimbo Bihemo, aliyemwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi, alisema benki hiyo inafurahishwa na namna uwekezaji wake katika soka unavyoendelea kuzaa matokeo chanya kupitia ongezeko la ushindani, kuibuka kwa vipaji vipya na kuimarika kwa viwango vya ligi za ndani.

Alisema NBC, ambayo imewekeza zaidi ya Shilingi bilioni 32 katika udhamini wa Ligi Kuu ya NBC, NBC Championship na Ligi ya Vijana, itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha soka linaendelea kukua na kutoa mchango mkubwa kwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini.

“Tunawapongeza washiriki wote wa NBC Championship kwa ushindani mkubwa waliouonyesha msimu mzima. Kipekee tunawapongeza Geita Gold FC kwa kutwaa ubingwa na Kagera Sugar FC kwa kufuzu Ligi Kuu ya NBC. Mafanikio haya yanaonyesha kiwango kikubwa cha ushindani kinachoendelea kujengeka katika soka la Tanzania,” alisema Bihemo.

Alisema NBC inaona matokeo ya uwekezaji huo kupitia maendeleo yanayoonekana katika ligi za ndani, kuimarika kwa ushindani wa vilabu na mafanikio yanayozidi kupatikana kwa timu za taifa katika mashindano ya kimataifa.

“Tunajivunia kuona soka la Tanzania likiendelea kupiga hatua. Ushindani unaoanzia ligi za vijana, NBC Championship hadi Ligi Kuu ya NBC umeendelea kuongeza ubora wa mchezo na kuzalisha wachezaji wenye uwezo wa kushindana katika viwango vya juu zaidi. Haya ndiyo matokeo tunayolenga kuyaona kupitia uwekezaji wetu,” aliongeza.

Bihemo alisema NBC itaendelea kuboresha mchango wake kwa wadau wa soka kupitia huduma mbalimbali za kifedha zikiwemo mikopo kwa vilabu, bima za afya kwa wachezaji na benchi la ufundi pamoja na elimu ya fedha inayolenga kuimarisha ustawi wa wadau wa mchezo huo.

Kwa upande wake, Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia, aliipongeza NBC kwa mchango wake mkubwa katika kukuza soka la Tanzania kupitia udhamini wa ligi hizo tatu, akibainisha kuwa ushindani wa sasa katika ligi za ndani ni miongoni mwa matokeo makubwa ya uwekezaji huo.

“Leo tunaona NBC Championship ikiwa na ushindani mkubwa kuanzia mwanzo hadi mwisho wa msimu. Vilabu vinaendesha shughuli zake kwa weledi zaidi, vina uwezo wa kusajili wachezaji bora na kujiandaa vizuri kwa mashindano. Haya ni maendeleo makubwa kwa soka letu,” alisema Karia.

Aliwataka Geita Gold FC na Kagera Sugar FC kutumia fursa ya kupanda Ligi Kuu ya NBC kujiimarisha zaidi ili kuongeza ushindani katika ligi hiyo pamoja na kuwekeza katika miundombinu ya viwanja ili mashabiki wao waweze kufurahia mechi za nyumbani katika mazingira bora.

Akizungumza kwa niaba ya wachezaji wa Geita Gold FC, nahodha wa timu hiyo Yusuph Mhilu aliwashukuru mashabiki, viongozi, benchi la ufundi na wadhamini kwa mchango wao katika kufanikisha ubingwa huo.

Alisema timu hiyo inatambua ushindani mkubwa uliopo katika Ligi Kuu ya NBC na tayari imeanza maandalizi ya kuhakikisha inakwenda kutoa ushindani wa kiwango cha juu msimu ujao.


Mkuu wa Biashara wa NBC Kanda ya Ziwa, Mafwimbo Bihemo (mwenye fulana nyeusi) pamoja na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia (alievaa kofia) wakiwapongeza wachezaji wa timu ya Geita Gold FC ya mkoani Geita baada ya timu hiyo kukabidhiwa rasmi kombe la Ligi Daraja la Kwanza (NBC Championship)msimu wa 2025/2026. Hafla ya kukabidhi kombe hilo ilifanyika jana katika Uwanja wa Nyankumbu, Geita, baada ya Geita Gold FC kuhitimisha msimu kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Big Man FC ya Lindi katika mechi iliyoshuhudiwa na mamia ya mashabiki pamoja na viongozi mbalimbali wa soka, serikali na vyama vya siasa




Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia (katikati alievaa kofia) akiongoza zoezi la uvalishaji wa medali kwa wachezaji wa timu ya Geita Gold FC ya mkoani Geita baada ya timu hiyo kukabidhiwa rasmi kombe la Ligi Daraja la Kwanza (NBC Championship)msimu wa 2025/2026. Hafla ya kukabidhi kombe hilo ilifanyika jana katika Uwanja wa Nyankumbu, Geita, baada ya Geita Gold FC kuhitimisha msimu kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Big Man FC ya Lindi katika mechi iliyoshuhudiwa na mamia ya mashabiki pamoja na viongozi mbalimbali wa soka, serikali na vyama vya siasa



Baadhi ya mashabiki wa Geita Gold FC wakifurafia ubingwa huo.






Haikuwa kazi rahisi! Wachezaji wa Geita Gold FC wakiwa kwenye nyakati tofauti uwanjani.




Vikosi vya Geita Gold FC (juu) na Big Man FC (chini) vilivyokutana kwenye mchezo huo




Muonekano wa kombe la Ligi Daraja la Kwanza (NBC Championship) msimu wa 2025/2026

 


Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) imeungana na Taasisi mbalimbali za umma kushiriki katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma kuanzia, Juni 16, 2026.

Katika maonesho hayo, TCAA inatoa elimu kwa wananchi kuhusu majukumu yake ya msingi, yakiwemo udhibiti wa shughuli zote za usafiri wa anga nchini. Hii inajumuisha pia usimamizi wa matumizi ya droni, ambalo ni eneo linalokua kwa kasi na kuhitaji ufuatiliaji wa karibu siyo tu kwa ajili ya usalama wa anga, bali pia kulinda faragha ya watu na kuepusha matumizi ya vifaa hivyo katika maeneo yasiyoruhusiwa kisheria, kama vile maeneo ya kijeshi, taasisi za serikali, na miundombinu nyeti.

Huduma nyingine zinazotolewa na TCAA ni pamoja na utoaji wa huduma za uongozaji ndege kwa ajili ya kuhakikisha usalama wa safari za anga ndani ya eneo la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Aidha, Mamlaka hiyo inatumia fursa hiyo kuwahamasisha vijana na wadau wa sekta ya usafiri wa anga kuchangamkia fursa za mafunzo zinazotolewa na Chuo cha Usafiri wa Anga Tanzania (CATC), kinachomilikiwa na TCAA. Mafunzo hayo yanalenga kuongeza idadi ya wataalamu wa ndani katika sekta muhimu ya usafiri wa anga.

Maadhimisho ya mwaka huu yanaongozwa na kaulimbiu: “Kuchochea uwajibikaji Jumuishi kwa Huduma Endelevu” ikisisitiza umuhimu wa matumizi ya teknolojia katika kuboresha huduma kwa wananchi na kuimarisha uwajibikaji katika utumishi wa umma.

Wiki ya Utumishi wa Umma huadhimishwa kila mwaka ili kutambua mchango wa watumishi wa umma katika maendeleo ya taifa. Maadhimisho ya mwaka huu yanatarajiwa kufikia kilele chake tarehe 23 Juni 2026.
Meneja wa TCAA Kituo cha Dodoma Aswile Kamendu (katikati) akitoa maelezo kwa Mkurugenzi wa Ufuatiliaji na Tathmini kutoka Wizara ya Uchukuzi Devota  Gabriel aliyefika katika banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma. 
Mkurugenzi wa Huduma za Usafiri kutoka Wizara ya Uchukuzi Biseko Chiganga  akisaini kitabu katika banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma. 
Afisa Rasilimali Watu TCAA Lucy Ngowo (wa pili kulia) akikabidhi zawadi kwa Mkurugenzi wa Huduma za Usafiri Wizara ya Uchukuzi ambaye pia ni Mjumbe wa Bodi Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) Biseko Chiganga
Mkurugenzi wa Huduma za Usafiri kutoka Wizara ya Uchukuzi Biseko Chiganga akiwa kwenye picha pamoja na watumishi wa  Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) alipotembelea banda la Mamlaka hiyo kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma. 

Baadhi ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) wakiendelea kutoa elimu katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika kwenye Viwanja vya Chinangali jijini Dodoma.

Top News