Na Oscar Assenga, Handeni.
WATU 11 wamefariki dunia wa Kijiji cha Chang’ombe kilichopo Kata ya Segera wilayani Handeni Mkoani Tanga baada ya kugongwa na lori lililokuwa limebeba saruji baada ya kupoteza uelekeo wakati walipojitokeza barabarani walipokuwa wakishanga ajali ya gari dogo aina ya tata .
Watu hao walijitokeza barabarani ili kuweza kutoa msaada kufuatia ajali ya barabarani ya gari dogo aina ya Tata ndipo walipokumbana na ajali hiyo iliyopelekea kupoteza maisha..
Kwa mujibu wa Taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian lori hilo liliwagonga watu hao usiku wa kuamkia Januari 14,2025 na kusababisha vifo hivyo pamoja na majeruhi.
Lori hilo lenye namba za usajili T.680 BQW likiwa linatokea Tanga lilifeli breki na kuwagonga watu waliokuwepo pembezoni mwa barabara na kusababisha vifo vya watu 11 papo hapo na kujeruhi wengine 11.
Miili ya marehemu hao imehifadhiwa katika Hospitali ya wilaya ya Korogwe Magunga na majeruhi wanaendelea kupatiwa matibabu katika hospitali hiyo .
Hata hivyo Mkuu wa Mkoa huyo alitoa pole kwa familia za marehemu na kuwatakia nafuu ya haraka majeruhi wote .
Mkuu huyo wa Mkoa alitoa wito kwa madereva na wamiliki wa vyombo vya moto kuhakikisha magari yao yanakuwa katika hali nzuri ya kiufundi ili kuepusha ajali za namna hiyo.
Alitoa wito huo wakati akiongoza utoaji wa elimu ya hifadhi ya jamii kwa viongozi wa masoko na baadaye wafanyakazi wa NSSF waliweka kambi kwenye masoko ya Kawe na Tegeta Nyuki kwa ajili ya kutoa elimu ya hifadhi ya jamii, kuandikisha wanachama wapya, kuhamasisha uchangiaji ambapo hamasa ya wajasiriamali kupata elimu na kujiunga imekuwa kubwa.
“Napenda kutoa wito kwa wajasiriamali wote wakiwemo mama lishe, bodaboda, wakulima, wafugaji, wavuvi kuwa NSSF ndio Mfuko wao, hivyo waendelee kujiunga na kujiwekea akiba ili waweze kunufaika na mafao yote kama vile ya uzee, urithi, uzazi na matibabu,” alisema.
Bw. Materu alisema NSSF imeweka utaratibu mzuri wa wajasiriamali kujiunga na kuchangia ambapo mwanachama baada ya kujiandikisha anapewa namba ya kumbukumbu ya malipo na anapaswa kuchangia kuanzia shilingi 30,000 au 52,200 au zaidi kwa mwezi na anaweza kuchangia kidogo kidogo kwa siku, wiki au mwezi ili aweze kunufaika na mafao hayo.
Aidha, alisema NSSF imepiga hatua kubwa katika utoaji wa huduma kwa wanachama na wananchi kwa kutumia mifumo ya TEHAMA ambayo inarahisisha huduma. "Tunaishukuru Menejimenti ya NSSF kwa kuweka nguvu kubwa sana katika kubadilisha mwelekeo wa utendaji kazi kuwa wa kidijitali zaidi ambapo imepelekea wanachama na wananchi kwa ujumla kupata huduma hukohuko waliko bila ya kulazimika kufika katika ofisi za NSSF," alisema Bw. Materu.
Alisema hayo ni mafanikio makubwa na kuwa lengo la NSSF ni kuendelea kufanya maboresho zaidi ya mifumo ili kumuwezesha mwanachama aweze kufungua madai ya mafao yake kwa njia ya mtandao bila ya kulazimika kufika kwenye ofisi za Mfuko.
Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Kundo Methew amemtaka Mkandarasi STC CO LTD anaejenga chanzo cha maji katika Mto nyangao -Chiuwe kukamilisha kazi ndani ya miezi miwili.
Mhandisi Kundo ametoa agizo hilo wakati wa ziara yake Wilayani Lindi kwenye mradi wa maji Nyangao- Mtama na mradi mkubwa wa vijiji 56 kwa kutumia chanzo hicho cha Mto Nyangao/Chiuwe Lindi kwenda Wilaya za Ruangwa na Nachingwea unaogharimu takribani Shilingi Bilioni 119.
Baada ya kukagua ametumia nafasi hiyo kuagiza hadi kufikia mwezi Machi,2025 wananchi wa mtama na Nyangao waanze kupata huduma ya maji kupitia mradi wao mpya ambao unatekelezwa na mkandarasi Halem Co Ltd.
Pia amemtaka Meneja wa RUWASA MKOA, Meneja wa Wilaya kukaa na mkandarasi Halem Co Ltd kwa ajili ya kufanya majadiliano kwa kazi inayoongezeka ili kazi hiyo ifanyike ndani ya mwezi mmoja
Kwa upande wake,Mkuu wa Wilaya ya Lindi Victoria Mwanziva amesema Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan ameidhinisha fedha nyingi za miradi ya maji Wilayani humo kiasi cha Shilingi 4.577Billion na mradi wa kutoka Lindi kwenda Ruangwa na Nachingwea kwa 119.1Billion, naye jukumu lake ni kusimamia na kuhakikisha miradi inajengwa kwa ubora ili idumu vizazi na vizazi na kuondoa kabisa adha ya maji kwa kumtua mama ndoo kichwani.
Na Ashrack Miraji,
Halmashauri ya Wilaya ya Same,Mkoani Kilimanjaro, imewajengea uwezo kuhusu Mtaala wa Elimu ulioboreshwa Wakuu wa shule na walimu wa taaluma 165 kutoka shule 46 za Serikali na 19 za binafsi ili kuwawezesha walimu hao kutekeleza Mtaala huo kwa ufanisi.
Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Wilaya ya Same, Mwalimu Neema Lemunge, amesema baada ya mtaala wa elimu kuboreshwa Wilaya imeona kuna umuhimu wa kuwajengea uwezo wakuu wa shule na walimu ili waweze kuelewa na kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.
“Mbali na kuwajengea uwezo kuhusu mtaala mpya, tumefanya tathmini ya matokeo ya kidato cha pili, tumejipima, tukaona tulipo hivyo tumekubaliana na kuwekeana mikakati ya kuboresha utendaji na kuondoa matokeo duni kama division zero na division four,” alisema Mwalimu Neema Lemunge.
Afisa Elimu huyo aliishukuru serikali ya awamu ya sita kwa juhudi zake za kuboresha sekta ya elimu. Alisema Serikali imejizatiti katika kujenga miundombinu ya shule ili kuhakikisha watoto wanapata elimu bora.
Awali akufungua kikao hicho Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Same Dkt.Cainan Kiswaga aliwataka walimu kutumia muda vizuri wawapo shuleni.
"Lengo letu ni kuongeza ufaulu hivyo lazima tuhakikishe kuwa tunatumia muda vizuri na tusipoteze kipindi hata kimoja"alisema Dkt.Cainan
Akifafanua kuhusu Mtaala ulioboreshwa, Mthibiti ubora wa Shule Wilaya ya Same Bw.Furahini Lubua alisema kidato cha I hadi IV kutakuwa na masomo 27 ambapo haitamlazimu mwanafunzi kusoma masomo yote hayo kwani kutakuwa na uchaguzi (option) kwa baadhi ya masomo.
Aliyataja masomo ya lazima kidato cha I hadi IV yanakuwa sita na sio Saba kama ilivyokuwa mwanzo,Masomo hayo ya lazima ni:
1. Mathematics
2. Kiswahili
3. English Language
4. Business Studies
5. Geography
6. Historia ya Tanzania na Maadili
Alisema somo la Bailojia na Historia yameongezwa kuwa masomo chaguzi (optional). yakiungana na yale ya zamani ya Fizikia na Kemia.
"Zamani Masomo chaguzi (option) yalifanyika kwa wanafunzi wa kidato cha tatu na cha nne lakini kwa sasa wanafunzi wanachagua toka kidato cha kwanza" alifafanua Mthibiti Ubora.
Jumla mwanafunzi anatakiwa asome masomo yasiyo pungua 8 na yasiyozidi 10.
Mtaala huo mpya utaanza Utekelezaji Januari 2025.
Na Muhidin Amri,Songea
WAKALA wa barabara za vijijini na mijini Tanzania(TARURA)Mkoa wa Ruvuma,kwa mwaka wa fedha 2024/2025 umehidhinishiwa Sh.bilioni 38.394 kwa ajili ya kufanya matengenezo na ujenzi wa barabara zenye urefu wa kilometa 1,145,madaraja madogo 50 na makalavati 57.
Kati ya hizo Sh.bilioni 7.8 bajeti ya barabara kuu,Sh.bilioni 9.8 zinatokana na tozo ya mafuta,Sh.bilioni 4.5 fedha kutoka mfuko wa Jimbo na Sh.bilioni 16.2 ni fedha za mradi wa Agricconect chini ya Umoja wa Ulaya(EU).
Hayo yamesemwa na Meneja wa TARURA Mkoani hapa Mhandisi Silvester Chinengo,wakati akitambulisha barabara mpya mbili ya Muungano-Majengo na barabara ya Kilimo Mseto-Pm House zenye urefu wa kilometa 1.5 kwa gharama ya Sh.milioni 949 pamoja na barabara ya Mjimwema-Mkuzo yenye urefu wa kilometa 1.1 ambayo ujenzi wake umegharimu Sh.milioni 426.
“Barabara hizi zimejengwa kutokana na fedha za tozo ya mafuta na zimeleta mabadiliko makubwa kwenye mitaa kwa sababu wakati wa mvua wananchi waliathirika na mafuriko pamoja na matope, kwa sasa ni msaada mkubwa kwa wakazi wa mitaa hiyo na mali zao,pia zitarahisisha sana shughuli za usafiri na usafirisha kwa wananchi wa maeneo hayo.”alisema Chinengo.
Alisema,TARURA mkoa wa Ruvuma inahudumia mtandao wa barabara wa kilometa 71,146.21,madaraja 306,makalavati 531,drifti 14 na mitaro yenye urefu wa kilometa 6.91 ambapo kilometa 2,312 sawa na asilimia 32.36 ni za mjazio,kilometa 3,873.85 sawa na asilimia 54.12 ni za mkusanyo na kilometa 959.52 sawa na asilimia 13.43 ni za jamii.
Chinengo alieleza,katika barabara hizo kilometa 128.66 sawa na asilimia 1.8 ni za lami na zege,kilometa 1,429 sawa na asilimia 20 za changarawe na kilometa 5,588 sawa na asilimia 78.2 za udongo.
Akizungumzia miradi viporo alisema,kuna mradi mmoja wa kuondoa vikwazo vya usafirishaji(RISE)unaotekelezwa kwenye Halmashauri ya Madaba,Mbinga Mji,Halmashauri ya wilaya Mbinga,Nyasa,Namtumbo na Tunduru.
Aidha alisema,Serikali imetenga Sh.bilioni 2.28 kwa ajili ya kuondoa vikwazo barabarani ikiwemo kujenga madaraja na barabara za changarawe ambapo utekelezaji wake umefikia asilimia zaidi ya 70.
Chinengo,ameishukuru Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan,kuongeza bajeti ya barabara kwa kuingizwa vyanzo vipya vya mfuko wa Jimbo na Tozo,kwani awali walikuwa na bajeti moja kutoka Bodi ya Mfuko wa Barabara.
“vyanzo vipya vimewezesha kuongezeka kwa mtandao wa barabara ambapo zaidi ya asilimia 65 zinapitika majira yote ya mwaka,kuongeza mtandao wa barabara za lami na ufungaji wa taa katika makao makuu ya Halmashauri zote za mkoa wa Ruvuma”alisema.
Kwa upande wake Kaimu meneja wa Tarura wilaya ya Songea Godfrey Mngale alieleza kuwa,katika barabara ya Mjimwema-Mkuzo kazi zilizofanyika hadi sasa ni kuweka tabaka la lami,kujenga mitaro ya kupitisha maji kwa kutumia mawe pande zote mbili.
Alisema,ujenzi wa barabara hiyo umewezesha kubadilisha mazingira ya maeneo hayo pamoja na kupandisha thamani ya viwanja na vyumba na awali wananchi wa maeneo hayo walipata adha kubwa hasa wakati wa mvua kutokana na utelezi kwa kuwa eneo hilo lina mteremko mkali.
Amewataka wananchi waliopitiwa na barabara hiyo, kuhakikisha wanalinda miundombinu ili iweze kudumu kwa muda mrefu kwa kuwa waliteseka kwa muda mrefu kabla Serikali kupitia TARURA kuimarisha barabara kwa kiwango cha lami.
Denis Timoth Mkazi wa mtaa wa Matogoro,ameipongeza Serikali ya awamu ya sita kwa kuendelea kutekeleza miradi ya mingi ya barabara ili kuwaondolea wananchi kero ya kusafiri wanapotoka eneo moja kwenda lingine kwa ajili ya shughuli zao za kiuchumi.
Agnes Komba mkazi wa mtaa wa Makambi alisema,ujenzi wa barabara za lami umewasaidia wananchi kujikomboa na umaskini na kuimarika kwa uchumi wa mtu mmoja mmoja na wilaya ya Songea, kwani hivi sasa mitaa maeneo mengi hakuna adha ya usafiri na usafirishaji.
Baadhi ya waendesha pikipiki na watumiaji wengine wakipita kwenye barabara ya Mjimwema-Mkuzo yenye urefu wa kilometa 1.1 iliyojengwa kwa kiwango cha lami kwa gharama ya Sh.milioni 426.
Jumla ya wasichana 10,239 waliokuwa wamekatisha masomo wamenufaika na Mradi wa Kuimarisha Ubora wa Elimu ya Sekondari (SEQUIP), unaotekelezwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (MoEST) na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), kwa kushirikiana na Benki ya Dunia.
Akizungumza mjini Morogoro, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amesema lengo kuu la SEQUIP ni kuimarisha ubora wa elimu kwa wanafunzi walioshindwa kuendelea na masomo yao, hususani wasichana waliopata changamoto kama ujauzito, ndoa za utotoni, au mazingira magumu.
"Mpango huu umelenga kuwafikia wasichana 12,000 wenye umri wa miaka 13 hadi 21. Pia tunajipanga kuwarejesha wavulana wengi zaidi mashuleni kabla na hata baada ya mradi huu kumalizika," ameeleza Waziri Mkenda
Aliongeza kuwa kupitia SEQUIP, wasichana wapatao 351 wamesajiliwa kujiunga na kidato cha tano, huku 218 wakijiunga na vyuo vya kati.
Silvia Diskon ni mmoja wa wanafunzi waliopata habati ya kurudi shule kupitia mpango huo amesema hakubahatika kumaliza masomo yake kutokana na changamoto za kifamilia hivyo anaishukuru serikali kupitia SEQUIP ataweza kutimiza ndoto yake ya kuwa mwalimu baada ya kurudi shule.
Kamishna wa Elimu, Dk. Lyabwene Mtahabwa, amesema kuwa walaka wa Serikali wa mwaka 2021 kuhusu urejeshwaji wa wanafunzi mashuleni umechangia kwa kiasi kikubwa kufanikisha lengo la kuwapa wanafunzi nafasi ya pili ya kuendelea na masomo.
Kwa upande wake, Mkuu wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW), Prof. Muchaeli Ng’umbi, alisema mradi wa SEQUIP umeleta mafanikio makubwa, ikiwa ni pamoja na kuimarisha elimu ya sekondari kwa njia mbadala na kuongeza nafasi za masomo kwa wasichana.
Na Mwandishi Wetu
MWANAMUZIKI maarufu katika Muziki wa Injili nchini Rehema Simfukwe amevunja ukimya kwa mara ya kwanza kwa kuamua kutoa sababu za kutunga wimbo wa Chanzo ambao umekuwa ukipendwa na kuvuta hisia za watu wengi kutokana na mashairi yaliyoandikwa katika wimbo huo.
Rehema Simfukwe tangu alipotoa wimbo huo miaka minne iliyopita hakuwahi kutoa sababu za kutunga na kuimba wimbo huo lakini ameona sasa ni wakati muafuaka kuwaambia Watanzania kuhusu wimbo Chanzo.
Akizungumza jijini Dar es Salaam Januari 12,2024 wakati wa hafla ya kuelezea sababu za kuimba wimbo wa Chanzo sambamba na kusherehekea kumbukizi ya kuzaliwa kwa mtoto wake wa kwanza Dorcas ambaye ametimiza miaka sita tangu kuzaliwa kwake.
Amemetumia nafasi hiyo kueleza kuwa Dorcas ndio sababu iliyomfanya yeye kuimba wimbo wa Chanzo kwani ni mtoto ambaye alimzaa na amekuwa na changamoto ya kupooza kwa ubongo au mtindio wa ubongo.
“Mungu amenijaalia watoto watatu lakini duniani huku watu wengi wanajua nina watoto wawili. Mtoto wangu wa kwanza anaitwa Dorcas ambaye alizaliwa na changamoto ya kupooza ubongo au mtindio wa ubongo kwa hiyo alikuwa na changamoto sana katika maisha yake.
“Changamoto hiyo kwa Dorcas ilisababisha tangu alipozaliwa tukawa na maisha ya hosipitali siku hadi siku. Nimekuwa nikiimba nyimbo za injili, nafanya mahojiano na vyombo vya habari kuhusu wimbo wa Chanzo lakini sijawahi kueleza upande wa pili kuhusu wimbo huu,” amesema mwanamuziki Rehema Simfukwe.
Amesema amekuwa kimya muda wote kwasababu alikuwa anasubiri apate kibali kutoka kwa Mungu kuzungumzia wimbo huo na hiyo ndio sababu ya kutunga na kuimba wimbo huo ambao unazungumzia maisha halisi ya Mtoto Dorcas.
“Ukiusikiliza wimbo huu utaona ndani yake kuna ujumbe uliobeba maumivu ya Dorcas na ndio sababu ya kuimba wimbo huo, nafahamu tangu ulipotoka watu wameuopokea, na wamekuwa wakiuimba na kuufurahia na nimekuwa nikiulizwa sababu za kuimba wimbo huu.
“ Nilimuahidi Mungu kuwa sitasema hili mpaka pale atakaponiruhusu na nimekaa na hii siri kwa miaka kadhaa na ninaamini Mungu amenipa mtoto Dorcas ili niwe mfano kwa wengine, ili nisaidie wengine wenye watoto wenye changamoto kama za Dorcas.
Hata hivyo amesema wakati wakisherehekea kumbukizi ya kuzaliwa kwa mtoto Dorcas pia ameamua kutangaza kufungua kituo cha kuelea watoto ambao wanachangamoto ya mtindio wa ubongo. Kituo hicho kitafahamika kwa jina la Dorcas Home Care Initiative kilichopo Madale jijini Dar es Salaam.
“Wakati leo tunafurahia miaka sita ya Dorcas naomba nitangaze uwepo wa Dorcas Homecare Initiative, lengo la kituo hiki ni kupokea watoto wenye changamoto ya mtindio wa ubongo, na hakutakuwa na gharama yoyote kwani nimeamua kutoa huduma ya kulea watoto hao na nimeanza na watoto nane.
“Kwa wale ambao wataguswa basi wanaweza kutuchangia kupitia akaunti ya NBC 074172000439TZS na 074173000101 wakati namba ya benki ya CRDB ni 015C0005PQW00 TZS na namba ya M-pesa ni 0768571613(Dorcas Home Care.”
Wametoa elimu kwa kuwatembelea kila banda wajasiriamali hao walioshiriki kwenye Maonesho hayo ambayo yameanza Januari 1 na yanatarajiwa kufungwa Januari 15, 2025.
RAIS wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Wakili Boniface Mwabukusi, amekemea tabia za wanasiasa na viongozi wanotumia lugha za kebehi, udini, jinsia na ukabila, kubeza wagombea kwasababu zinaligawa Taifa na badala yake wajenge hoja zenye mashiko.
Aidha, alitolea mfano wa kauli alizotolewa dhodi ya Rais Samia Sukuhu Hassan na mmoja wa wanasiasa wa upinzani na kudai zina lengo la kuligawa Taifa na si kujenga umoja na mshikamano.
Mwambukusi ameyasema hayo leo Januari 13, 2024 jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu masuala yanayoihusu nchi katika kuelekea uchaguzi mkuu ujao.
Amesema “Kulekea kipindi cha uchaguzi ni muhimu kuelewa kwamba sheria na katiba yetu ni nyenzo za kulinda demokrasia. "Tumeshuhudia changamoto zinazohusiana na kauli na vitendo vyenye mwelekeo wa kibaguzi kutoka kwa baadhi ya viongozi wa kisiasa, hii inapaswa kukomeshwa mara moja."
Amesema amepokea malalamiko kutoka kwa watu mbalimbali na ushahidi wa kauli mabazo hazitamkiki zenye nia ovu ya kuwagawa Watanzania.
Amewataka viongozi wote wa kisiasa kuzingatia misingi ya sheria, kuepuka kugawanya wananchi na kujenga mazingira ya umoja wa utaifa.
Aidha, amewataka viongozi wastaafu, wa dini na mila kukemea kauli hizo bila kujali itikadi zao kwasababu hazijengi umoja na mshikamano wa Taifa.
Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Mhe. Hamis Mwinjuma na Naibu Waziri wa Uchukuzi Mhe. David Kihenzile, wameshuhudia utiaji saini makubaliano ya matumizi ya asilimia 80 ya muziki wa wasanii wa kitanzania, kupigwa katika viwanja vya ndege nchini, ili kuwawezesha kufaidi matunda ya kazi zao yatokanayo na malipo ya mirabaha.
Makubaliano hayo yamesainiwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa na Msimamizi wa Haki Miliki (COSOTA) Bi. Doreen Sinare, na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) Bw. Abdul Mombokaleo, ambapo Katika makubaliano hayo, imependekezwa muziki wa wasanii wa kitanzania kusikilizwa zaidi, lengo likiwa ni kulinda kazi za sanaa za watanzania pamoja na kuutangaza muziki huo ndani ya nchi na nje kwa wageni wanaoingia na kutoka nchini kila siku.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe.Mwinjuma amesema kusainiwa kwa mkataba huo ni nia ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kuboresha mazingira ya wasanii.
"Rais alionyesha nia ya kuboresha mazingira ya wasanii kwa kutambua mchango wa sanaa katika Taifa letu na umuhimu wa kazi zao, na pia kutafuta njia za ziada za kukuza kipato chao pamoja na uchumi, leo tumefikia hatua muhimu ambapo COSOTA imefikia Makubaliano ya Ushirikiano na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) kuhusu suala la kulipia leseni (mirabaha) kwa matumizi ya muziki katika viwanja vya ndege. Makubaliano haya, ambayo ni sehemu ya Mkataba kati ya TAA na COSOTA, yatasaidia wasanii wa muziki wanapata haki yao ya malipo kutokana na matumizi ya muziki katika maeneo ya viwanja vya ndege nchini." Amesema Mhe. Mwinjuma.
Amesema hiyo ni hatua kubwa katika kuhakikisha kuwa wasanii wanapata masoko ya kazi zao, na kupata mapato kutokana na vyanzo mbalimbali vya kazi zao, na kwamba haki zao zinaheshimiwa kikamilifu.
Aidha ameongeza kuwa katika kipindi cha Septemba 2023 hadi Novemba 2024, COSOTA kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ilikusanya zaidi ya shilingi Bil. 1.1
"Itakua vema pia nikisema kuwa katika kipindi cha Septemba 2023 hadi Novemba 2024, COSOTA kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imekusanya jumla ya shilingi bil. 1.1 ambazo zitagawanywa kwa wanufaika ambao ni Wasanii, Waandishi wa muziki, filamu, sanaa za maonesho, na sanaa za ufundi.
Nae Naibu Waziri wa Uchukuzi Mhe. David Kihenzile amesema taasisi za COSOTA na TAA zimekuwa za kwanza kuingia makubaliano ya namna hiyo na kutoa wito kwa taasisi zingine za usafirishaji zilizopo kwenye wizara yake, kuiga mfano huo ili kuwanufaisha wasanii kupitia kazi zao.
"Kwa taarifa nilizonazo katika taasisi zetu zote za wizara ya uchukuzi, TAA inakuwa ya kwanza kuingia makubaliano haya, natoa wito kwa taasisi zingine hususan Shirika la Reli Tanzania (TRC), Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA), na Kampuni ya Meli Tanzania (TASHIKO) kuwasiliana na COSOTA na kuiga mfano mzuri uliowekwa na TAA" amesema Mhe. Kihenzile.