Rogers Mtagwa
Bondia Rogers Mtagwa anayeishi Marekani atapanda ulingoni Januari 23, 2010 na kupambana na bondia Yuriorkis Gamboa katika piagno la raundi 12 litakalofanyika Madison Square Garden jijini New York katika pambano la ubingwa linalotambuliwa na HBO katika uzito wa Unyoya (Feather weight).
Rekodi ya Mtagwa inaonesha keshazipiga mapambano 26, kashinda kushinda 13 kwa pointi, kupoteza mawili na kushinda kwa KO 18.

Gamboa amecheza mapambano 16 na kushinda kwa KO 14, mawili kwa pointi na hajapoteza hata pambano moja.

Aidha, mbali ya pambano hilo pia kutakuwa na pambano la uzito kama huo ambalo litamshirikisha Juan Manuel Lopez atakayezichapa na Steven Luevano.
Pambano jingine linalotarajiwa kufanyika siku hiyo jijini Pasay nchini Philippines, Donnie Nietes atazipiga na Ivan Meneses.
mpinzani Yuriorkis Gamboa
Chanzo cha habari hii


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. mwaha alikosa techniques tu mpambano uliopita na kama ingeongezwa raundi 1 nyingine basi mtagwa alikuwa anamaliza kwa ko.
    natumai sasa ameshapata techns na atashinda. kila laheri/lakheri/raheli/rakheli? kiswahili kigumu jamani

    ReplyDelete
  2. Mcuba with Olympic gold medal basi iko kazi. Technically Roger hataweza kumshinda Mcuba huyu kama ni ushindi itakuwa ni kumvizia achoke round za mwisho. Natabiri Mcuba atashinda kwa knockout!

    ReplyDelete
  3. Watuchungie tuu kijana wetu wasimpambanishe na mijitu iliomzidi uwezo kwa Tamaa zao za madola!Youtube mapambano ya Roger utagundua jamaa ni kama boxing bag anauwezo mkumbwa wakuvumilia makonde mazito raundi zote kumi na mbili lakini side effect za hao makonde hasa kichwani ni kubwa..

    ReplyDelete
  4. Bwana Michuzi nimecheki fights kama tano za Mtagwa, this Guy is a piece of boxing art!!jamaa anaongeza maujuzi kila fight, kuna promoter maarufu wa Philly alikiri kwamba amekuwa kwenye bizness hiyo kwa miaka mingi,anaamini Rogers yupo Top Ten yake ya vifaa!!ukicheki mpambano alioupiga Madison na ya nyuma,ni tofauti kabisa, anazidi kuwa mzuri,tumuombee ndugu yetu huyu!!

    ReplyDelete
  5. feather weight= uzito wa unyoya hahaha kweli kiswahili kitamu....hiyo nimeipenda sana mie....anyway GOODLUCK KAKA MTAGWA

    ReplyDelete
  6. Jana niliangalia ngumi kati ya kijana wa kitanzania(obote umeme) na veto sijui wa wapi.yaniii,nimesikitika sana mtanzania alivyokuwa anapigwa masumbwi,pia nilijisikia huruma sanaa kwani alijiona inferior sana kwenye ulingo,anakinga ngumi saba anarusha moja,sita zinamtandika.huruma sanaa,hakuna techniques,pia hata water bottle,wanatumia chupa ya kawaida nyumbani na kikombe cha plastiki.poa baada,Watanzania jamani,msitusikitishe
    mdau uk

    ReplyDelete
  7. Wewe mwandishi wa hii stori hesabu yako haiko sawasawa, amecheza 26, ameshinda 13 na kupoteza 2, what happened to the other 11 fights? Niliwahi kuona enzi za GTV Mtagwa ana record mbaya sana, idadi ya mapambano aliyoshindwa ni kubwa sana, sio kama hivyo unavyosema. Kama alivyosema mdau mmoja hapo, wasimtumie tu kama njia ya kuwapandisha mabondia wao, mi namuonaga picha zake ni kama analazimishwa vile kupigana halafu kama hatibiwi majeraha anayoyapata, anagalia tofauti ya sura kati yake na bondia atakayepambana nae, uso wake umevimba chini ya macho kabla hata ya pambano, ni nani sijui anaangalia maslahi ya Rogers huko!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...