Ankal habari za kazi
Nipo Kigoma kikazi tangu J4. Jana katika kupiga stori na wenyeji kwenye kijiwe fulani cha nyama choma niliipata hii ya kutisha.
Nipo Kigoma kikazi tangu J4. Jana katika kupiga stori na wenyeji kwenye kijiwe fulani cha nyama choma niliipata hii ya kutisha.
Mji wa Kigoma na vitongoji vyake kwa takribani wiki mbili tatu sasa umevamiwa na kundi la vibaka wa kutisha wanaotumia nondo kujeruhi na kupora watu chochote, simu pesa n.k. Kundi hilo uvinjali kuanzia saa 2 usiku na kuendela.
Mji kwa sasa una matatizo ya umeme na baadhi ya vitongoji vya mji wakazi wamepanda mahindi hivyo giza utawala. Wakazi kwa sasa utembea kwa teksi kutoka sehemu moja kwenda nyingine ifikapo usiku japo jamaa wameshamliza mtu kwa kumwekea jiwe kubwa njiani kisha wakampora wa kumpiga nondo baada ya kumchomoa kwenye gari.
Wametoka wapi vibaka hawa ghafla bin vuu!? Nimejulisha kuwa kutokana na kusitishwa kwa safari za treni kuja Kigoma kundi la wezi wote wa mizigo ya abiria wa treni lipo JOBLESS na ukabaji ndio imekuwa 'kazi' yao mbadala!
Kigoma wafa jamani Polisi wa doria wamezidiwa na vibaka hawa.
Mdau GBK
ILIKUAJE UKAKUBALI TRANSFER YA KIGOMA!!HIYO NI ZAIDI YA ADHABU!!!Huoni ZITO KABWE Anashinda DAR.
ReplyDeleteILA VUMILIA TU,UTA ADJUST LIFESTYLE TU, NAKUANZA KUWA MBISHI!!