MBUNGE wa Morogoro Mjini, Aziz Abood atafungua mafunzo ya waandishi wa habari za michezo yatakayofanyika kwa siku mbili Morogoro Hoteli mkoani Morogoro.

Washiriki wataondoka Dar es Salaam Ijumaa Septemba 30, 2011, eneo la Ubungo Maji saa tisa alasiri, ambapo Mkuu wa Msafara atakuwa Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), Maulid Kitenge.

Viongozi wengine wa TASWA ambayo ndiyo imeandaa mafunzo hayo yakidhaminiwa na Vodacom na Kampuni ya mabasi ya Al Saedy watakuwa ni Mhazini Sultani Sikilo na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji, Salum Jaba.

Mafunzo hayo yatakayoshirikisha waandishi 40 kutoka mikoa ya Morogoro, Pwani na Dar es Salaam yatafungwa Jumapili Oktoba 2, 2011 alasiri na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera.

Mafunzo yatakuwa katika sehemu mbili, ambayo ni taalum ya habari itakayofanyika Jumamosi na masuala yahusiyo sheria za michezo ya wavu na netiboli ambayo itafanyika Jumapili.

TASWA inawatakia kila la heri washiriki wote, huku ikiamini mafunzo hayo yatakuwa na manufaa makubwa kwao na kufanya vizuri kwao itakuwa ni fursa nzuri ya kuandaa mafunzo mengine kwa kadri itakavyowezekana.

Nawasilisha.
Amir Mhando
Katibu Mkuu TASWA
29/09/2011.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...