Gwiji wa mashairi nchini HAMIS HIYANA almaarufu kama  "Mkembebwenzi au Gendaheka" hatunaye tena.  Marehemu Hamisi alifariki juzi (02.Desemba.2012) katika ajali ya gari iliyotokea Kibamba shule na amesafirishwa leo (04.Desemba.2012) kwenda kijijini kwao Mdaula, Bagamoyo. kwa mazishi.
Watanzania tunaungana na familia ya marehemu Hamisi Hiayana katika kipindi hiki cha kuomboleza msiba huu mkubwa wa mpendwa wetu.
"SISI SOTE NI WAJA, NA HAKIKA KWAKE TUTAREJEA".


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. Mungu amlaze pema.

    ReplyDelete
  2. INNALILAH WAINA ILAYHI RAJIUN

    ReplyDelete
  3. "INNA LILLAHI WAINNA ILAYHI RAJIUN"

    MOLA pema akulaze, kwake umetangulia,
    Nuruye akuangaze, lokosa kughufiria,
    "Jannatu" akutembeze, milele humo bakia,
    Hatunapo tujibanze, kifo yetu khatamia.

    Mwenyeez Mungu akughufirie kwa yote na akupumzishe katika yake FIRDAUS - AMEN.

    ReplyDelete
  4. Inna Lillahi wa Ina Ilayhi Rajiuuuuuunnnnn !

    ReplyDelete
  5. Raha ya milele ampe EE Bwana, na Mwanga wa milele amuangazie, apumzike kwa Amani, Amen.

    ReplyDelete
  6. Poleni wafiwa.

    Ajali zinatumaliza jamani japo zaweza kuepukwa. Tuziepuke kwa juhudi za mtu mmoja mmoja ama kwa juhudi za pamoja. Endesha taratibu. Ikibidi kulala sehemu, lala halafu kesho yake endelea. Kawia lakini ufike. Wasiwasi wangu huwa ni wale walevi wanao-overtake milimani, kwenye madaraja... Hawa wanaweza kukuua hata pale unapokuwa katika upande wako na ukiwa katika mwendo mdogo.

    Serikali pia ina wajibu wa kutoa adhabu kali kwa ama wenye kuvunja sheria za barabarani ama wenye kusababisha vifo barabarani. Hii ya kulipa 20,000/= na kuondoka, si deterrant hata kidogo.

    Tanzania ni nchi yangu lakini naogopa kuishi Tz. Sababu za kufa ni nyingi mno. Ukiweka pembeni stress za mgao wa umeme/giza, mfumo mbovu wa majitaka, kukatika kwa maji, rushwa sehemu za huduma, madereva wasio heshimu sheria barabarani, mishahara midogo nk nk. Kwa kweli hata kama una utajiri Tanzania, sioni unavyoufaidi katika mazingira haya.

    ReplyDelete
  7. Mdau wa Wed Dec 05, 11.23.00AM 2012,
    nakuunga mkono kwa asilimia mia moja, kuna mengi zaidi ya hayo uliyoyaorodhesha yanayonifanya nichelee kurejea TZ risk ni nyingi mno na maisha ya watu yanapotea kiurahisi mno kama wanyama inatia huzuni mno.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...