Kesho tarehe 7 Disemba 2012 kuanzia saa 3 asubuhi,rufaa ya kupinga ushindi wa Ubunge Jimbo la Ubungo,dhidi ya Mbunbe wa Jimbo hilo kupitia tiketi ya CHADEMA,John Mnyika itaanza kusikilizwa na jopo la majaji watatu wa mahakama ya rufani.
Mbunge wa Jimbo hilo la Ubungo,John Mnyika anawaomba wanachana na wampenzi wa chama hicho kufika Mahakamani hapo kwa wingi ili kusikiliza Rufaa hiyo,Kama alivyonukuliwa akisema "tulivyotafuta kura tulikuwa pamoja, tukapanga mstari kupiga kura pamoja na tukakesha kuzilinda pamoja tujumuike pamoja kujua hatma ya kura zetu".
ndugu yangu Mnyika acha kupiga siasa kila mahali...hivi kweli unataka mimi nifunge duka langu hiyo kesho ili nije tu kukuangalia hapo mahakamani??Je hela ya kula kesho utanipa wewe kutoka kwenye mshahara wako mnono wa ubunge? Je kuwepo kwangu mahakamani kutabadilisha matokeo ya majaji??
ReplyDeleteIfike mahali wanasiasa wetu muwe mnatufikiria wananchi wenu tunavyoteseka na maisha na hata huo muda kidogo wa kupoteza ni gharama sana kwetu jamani.
Jose - Kimara mwisho
Jose,
ReplyDeleteSisi hapa Kimara mwisho tutafika kwa wingi kesho, tulikuwa na kikao hapa kijiweni.
Hivi kwanini wanamsumbua mbunge wetu kwa kesi za mara kwa mara?
Mushi
Nilipoteza muda kupanga foleni kupiga kura yangu, lazima kesho niende kujua hatma yake.
ReplyDeleteHawa CCM waliokata rufaa wanatupotezea muda
Duh Hakika siasa ni inshu.... Bw Jose acha hizooo. W ewe kama hutaenda eti hiyo duka yako itafungwa basi baki siye tutakwenda!Hiyo shuhuli gani One man show!! Sasa uk*+a ndiyo basi tena!!
ReplyDeleteWewe Jose huna lolote, hata kama uchaguzi utarudiwa wa kuitoa CHADEMA Ubungo hajazaliwa! hata wakiweka JIWE litashinda TU!
ReplyDeleteNa huu ndio ukweli wa Jimbo la Ubungo! chezea wana Ubungo weye? wana msimamo kama SIMBA dume