Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akiwasili kwenye kijiji cha Mswakini Wilayani Monduli tayari kwa hafla fupi ya uzinduzi wa vikoba katika kijiji hicho.Katikati ni Mkewe Mama Regina Lowassa aliefatana nae kwenye hafla hiyo ya Uzinduzi wa Vikoba.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa na Mkewe Mama Regina Lowassa wakiwasalimia wananchi wa kijiji cha Mswakini Wilayani Monduli walipowasili tayari kwa hafla fupi ya uzinduzi wa Vikoba katika kijiji hicho.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akitoa hotuba yake kwa wananchi wa kijiji cha Mswakini Wilayani Monduli wakati wa hafla ya uzinduzi wa VIKOBA kijijini hapo.Mh. Lowassa katika hotuba yake,amesema kuwa ushirika wa VIKOBA ni sawa na mshipa wa damu kwa sera ya maisha bora kwa kila Mtanzania,pia alisema kuwa kutokana na kutambua hivyo ushirika wa Vikoba utaanzishwa katika wilaya nzima ya Monduli.Miasha bora kwa kila Mtanzania ni sera aliyoingia nayo madarakani Rais Jakaya Kikwete.
Afisa Maendeleo ya Jamii Wilaya ya Monduli,Bi Judith (kulia) akikabidhi kwa Mhe. Edward Lowassa hati maalumu ya uzinduzi wa Vikoba ili ikabidhiwe kwa Wananchi Mswakini Monduli.
Baadhi ya wanachama wa Vikoba wa kijiji cha Mswakini Wilayani Monduli.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Lowasa alitangaza hawanii tena mbio za uraisi, nampongeza sana kwa uamuzi huu mzuri!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...