Mojawapo kati ya vipaumbele muhimu vya Marekani nchini Tanzania ni kukuza maendeleo ya kiuchumi na kujenga uwezo (empowerment) wa raia wote kwa ubia na Watanzania kutoka sekta zote. Nchi hii imejaaliwa neema ya kuwa na maliasili nyingi na utajiri mkubwa, mbali na kuwa na vivutio vingi vya dunia kama vile Mlima Kilimanjaro, mbuga za wanyama za Taifa na maeneo ya urithi wa Dunia yanayotambuliwa na UNESCO kuanzia Kilwa Kisiwani hadi Zanzibar. Wakati dunia ikitambua hazina hizi kuwa na thamani kwa dunia nzima, bado ukweli ni kuwa, kwa njia ya kipekee kabisa hazina hizi ni za Kitanzania. Pamoja na hali hii, baadhi ya raia wanajiuliza ni kwa namna gani uchumi wa Tanzania utabadilika na kuwa ule wenye kuleta ustawi.
Mustakabali wa maendeleo ya Tanzania utategemea mawazo na maono ya uongozi wa Watanzania wenyewe. Nimevutiwa sana na jitihada za Watanzania kutoka serikalini na taasisi huru za kiraia kutafuta njia mpya zenye uwazi, uwajibikaji na uadilifu zaidi katika kusimamia na kutumia utajiri mkubwa wa asili ambao nchi hii imejaliwa kwa manufaa ya wote. Mpango wa Kimataifa wa Uhamasishaji Uwazi na Uwajibikaji katika Tasnia zinazohusika na Uvunaji Maliasili (Extractive Industry Transparency Initiative - EITI) ni nyenzo inayoweza kusaidia katika kufikia azma hii adhimu na inayostahili kufikiwa kwa haraka .
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
nimefurahi sana kusoma huu ujumbe wako inaleta matumaini.
ReplyDelete